Thursday, September 22, 2016

ALLAH NA UISLAM NI DINI YA WAFU

Ndugu msomaji,
Ukisoma Biblia takatifu ambayo ndio NENO la Mungu, inasema: Mungu ni Mungu wa walio hai na sio wa wafu. Soma Mathayo 22 aya ya 32 ..... Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai."
Marko 12:27 Mungu si Mungu wa wafu bali ni Mungu wa walio hai.
Kama Biblia ilivyo tuhakikishia kuwa Mungu si Mungu wa Wafu kama ambavyo Marehemu Muhammad wa kwenye Quran ambaye anaombewa kila siku na Allah na Malaika wake. Hebu tusome aya kutoka Quran.
Surat Al Ahzab 56. Hakika Mwenyezi Mungu na Malaika wake wanamsalia Nabii. Enyi mlio amini! Msalieni na mumsalimu kwa salamu.http://www.quranitukufu.net/033.html
Waislam wameamrishwa kuombea Marehemu Muhammad ambaye mpaka hivi leo yupo kaburini akisubiri hukumu kutoka kwa Yesu muumba wake.
Imam Amirul Mu’minin Ali (a) alisema:
Watembeleeni wafu Makaburini, maana wanajisikia furaha mnapo watembelea. Omba unacho taka katika kaburi la Baba yako na mama yako baada ya kuwaombea. Al-Akhlaq wa al-Aadab al-Islamiyyah compiled by Hay’at Muhammad al-Amin, Qum:
Imam al-Sadiq (a) anawataka Waislam watembelee makaburi, kwasababu hao wafu kwa kupitia Allah wanafahamu mnapo watembelea makaburini na wanasikia furaha mnapo kwenda kuwatembelea. Abu Muhammad Zaynu’l ‘Abidin, Manifestations of the All-Merciful:
Wafu wanashukuru mnapo watembelea makaburini, na wanajisikia upweke unapo ondoka. http://www.alseraj.net/3/index2.shtml?91&100&92&1&15
Ushuhuda hapo juu unathibitsiha kuwa, UISLAMU ni dini ya wafu na wanaamini kuwa Wafu walio oza na kuliwa na Mchwa makaburini wanawasikia na wapo kwenye hayo makaburi. Lakini, nini hutokea usiku wa kwanza unapo zikwa, soma hiki kisa cha ajabu sana kutoka Sahihi hadith.
USIKU WA KWANZA WA MUISLAM KABURINI:
[Hasan: At-Tirmidhee from Abu Hurairah.]
Nabii wa Allah (sallAllahu 'alaihi wa sallam) anasema, mtu aliye kufa anapo zikwa, Malaika wawili mmoja wa Mweusi na mwengine wa Bluu, mmoja anaitwa Al Munkar na mwengine an Makeer, na wanamsemesha maiti na kumuuliza; Nini ulikuwa unasema kuhusu huyu mtu? Hivyo husema alicho kuwa ansema, Mtume wa Allahm nashuhudia kuwa mwenye haki ya kuabudiwa ni Allah na Muhammad ni mtume wake. Na wale Malaika watasea, hakika tulijua utasema hivyo, hivyo kaburi lake litaongezwa na kufikia upana wa Sabini kwa Sabini, na anafanyiwa nuru kwake, na litasema lala. Na yeye atasema nitakwenda kwa familia yako na kuwafahamisha..........
Muhammad anasema; Marehemu anapozikwa kaburini, husikia sauti za nyayo za ndugu zake ........ [Saheeh: Al-Bukhaaree (2/422), Muslim, Ahmad, Abu Daud, an-Nasaa.ee: from Anas.],
Al-Baraa b. 'Azib anasema, tulenda Makaburini na tulikuta mmtu moja wa Nasar hajazikwa, basi Nabii wa Allah akamuuliza maiti, asema najisalimisha kwa Allah.....[Saheeh: Ahmad, Abu Dawud (3/4735) Ibn Khuzaimah, al-Haakim, al-Baihaqee in 'Shu'ab ul-Imaan', ad-Diyaa: from al-Baraa.]
Hadithi hapo juu zinatuthibitishia kuwa Uislam ni DINI YA WAFU wakati Biblia inasema kuwa Mungu si Mungu wa wafu bali ni Mungu wa walio hai.
ENDELEA:
Ada ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipomaliza kuzika alikuwa anasimama kaburini na husema: “Muombeeni msamaha ndugu yenu kwa Allaah na amfanye thabiti kwani hivi sasa anahojiwa” (Abu Daawuud).
SASA WAISLAM WANAMSWALIA MAITI QURAN
Maiti huswaliwa kwa kufuata utaratibu huu:
Atasimama Imaam (kiongozi wa Swalah) upande wa kichwa, kama maiti ni mwanaume, na hii imethibiti katika Hadiyth ya Abu Ghaalibi al-Khayyaat, amesema:
“Nimemshuhudia Anas bin Maalik akiswalia maiti ya kiume akasimama usawa wa kichwa chake.”
Pia Imaam atasimama usawa wa katikati wa ikiwa maiti ni mwanamke, kama ilivyothibiti katika Hadiyth ya Samurah bin Jundub, anasema:
“Nimeswali nyuma ya Mtume (Rehma na amani ya Allaah ziwe juu yake) naye akimswalia mama wa Ka’ab….akasimama katikati yake.”
Kisha, Imaam ataleta takbira kwa kusema, ‘Allaahu Akbar’, (Allaah ni mkubwa) mara nne au tano au tisa, kwani aina zote hizi zimethibiti kutoka kwa Mtume (Rehma na amani ya Allaah ziwe juu yake). Lakini mara nyingi Mtume (Rehma na amani ya Allaah ziwe juu yake) alileta takbira nne.
Allah na Muhammad wanaendelea kusema kuwa eti Muombeeni MSAMAHA MAITI ...............“Muombeeni msamaha ndugu yenu na mumuombee uthabiti, kwani hakika sasa hivi anaulizwa maswali”[36] kama ilivyokuja katika Hadiyth ya ‘Uthmaan bin ‘Affaan.

Inamaanisha kuwa, wewe Muislam endelea kutenda dhambi, bila wasiwasi wowote ule, maana ukifa tu NDUGU ZAKO Watakuombea msamaha, huu jamani ni UONGO MKUBWA SANA.
Kuombea wafu huwafanya wenye dhambi kuendelea kutenda dhambi wakiamini kwamba baada ya kufa kanisa litaomba ili wao waingie mbinguni. Ndugu nakuambia tena WOKOVU NI SASA.
Katika Luka 16:26…Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.'' Biblia inatuonyesha watu waliokufa wengine wako pema peponi na wengine wako kuzimu,’’ ’’
BIBLIA INASEMA NINI KUHUSU WAFU?
MUNGU humpokea mwenye dhambi ambaye hutubu kwa woyo na kujitakasa kwa msingi wa imani peke yake katika damu ya YESU KRISTO. Hivyo humpa uzima wa milele. 2 Kor 6:2’’(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa) ‘’
Biblia inatuambia ya kuwa baada ya mtu kufa, hupelekwa Mbinguni au Jehanamu kulengana na hoja ya kuwa alikuwa amemkubali ama kumkataa Kristo kama mwokozi. Kwa walioamini, kufa ni kuondoka katika mwili na kuenda kukaa na Bwana (wakorintho wa pili 5:6-8; wafilipi 1:23). Kwa wasioamini, kufa ina maana ya hukumu ya milele jehanamu (Luka 16:22-23).
Hapa ndipo kwenye utata juu ya ni nini hufanyika baada ya kifo. Ufunuo wa Yohana 20:11-15 inaeleza juu ya wale walio kuzimu wakitupwa katika ziwa la moto. Ufunuo wa Yohana 21 na 22 inazungumzia juu ya mbingu mpya na dunia mpya. Kwa hivyo ina maana ya kuwa mpaka wakati wa ufufuo wa mwisho, baada ya kufa mtu hubaki katika mahali Fulani kwenye mfano wa mbinguni na kuzimu. Mahali pa mtu anapofaa kukaa milele hapatabadilika ila makazi ya muda yatabadilika. Muda Fulani baada ya kufa, waumini watapelekwa katika mbingu mpya na nchi mpya (ufunuo wa Yohana 21:1) na wasioamini katika ziwa la moto (ufunuo wa Yohana 20:11-15). Haya ndiyo makao ya milele ya watu yanayotegemea kama mtu alimwamini Yesu Kristo pekee kwa wokovu kutokana na dhambi zake.
Waislam, baada ya kifo ni hukumu na hakuna kuombea maiti msamaha. Muda thabiti wa kutengeneza maisha yako ni huu ulio nao sasa na sio kusubiri kuombewa rehemea baada ya kifo. Huo ni mtego wa Shetani aliye iketia njia iliyo nyooka ya Allah.
Vipi mwenzangu? Umejitayarishaje kwa ajili ya kifo?
Maisha ya hapa duniani hayana uhakika kwamba tutaishi na kuiona kesho. Kifo huja ghafla, Biblia inatuonya “Haya basi, ninyi msemao, leo au kesho tutaingia mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; walakini hamjui yatakayokuwako kesho.
Uzima wenu nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, na kisha hutoweka,” Yak. 4:13-14. Biblia tena inasema, “Kwa maana asema wakati uliokubalika nalikusikia, siku ya wokovu nalikusaidia; tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa,” 2 Kor. 6:2. Anza leo, wakati kuna nafasi, mwamini Yesu Kristo Mwana wa Mungu, Yoh. 8:24. Yeye ni njia ya kweli na uzima, Yoh. 14:6. Kwa jina la Yesu Kristo pekee ndilo tunaloweza kuokolewa kwalo, Mdo. 4:11-12. Tubu dhambi zako zote, Mdo. 17:30-31. Mkiri Yesu Kristo kuwa ni Mwana wa Mungu, Mdo. 8:37. Uzikwe pamoja naye katika ili upate ondoleo la dhambi, Rum. 6:4; Mdo. 22:16. Kisha mtumikie Kristo katika Kanisa lake kwa maisha yako yote yaliyosalia na utabarikiwa.
Leo tumejifunza tofauti ya KIFO katika Uislam na UKRISTO. Waislam wanaamini kuombea maiti msamaha na Wakristo wanaamini kuwa, wokovu ni sasa.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 11, 2016

1 comment:

Unknown said...

Asalam Alykum/ Amani iwe nawe/ Shalom (maana Ni moja)

Ama baada ya Salam:
Nikushauri ndugu mtunzi wa tungo hiyo yenye upotoshi wa Hali ya juu
Sina hakika unapata ujira gani kwa kuandaa makala hiyo
Ila Mungu mwenye ndio anajua atakurudi vipi.

Kazi njema.

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW