Friday, September 2, 2016

MUHAMMAD ALITAMBIKWA KWA MIUNGU YA KIPAGANI NA USHIRIKINA NA BABU YAKE

Huu ni Msiba mkubwa sana.
Tunaposoma kitabu cha maisha ya Muhammad S.A.W. kilichoandikwa na aliyekuwa kadhi mkuu wa Kenya na Zanzibar Sheikh Farsy ukurasa wa 5 kuna maneno haya…
Pale pale alfajiri alipokwisha kuzaliwa mtume alikwenda kuitwa babu yake kuja kumwona mjukuu wake. Babu huyu alifurahi sama na akamfunika maguo mjukuu wake, akajikongoja naye mpaka kwenye Al-ka’ba akafungua mlango akaingia ndani, akasimama, akamwombea dua kwa mashairi mazuri ya kiarabu aliyoyatunga mwenyewe wakati ule ule, kisha akarejea naye na jua bado halikuchomoza.
(1) Imani ya Abdul Muttalib ilikuwa hii:
Katika kitabu " Acha Biblia Iseme" kilichoandikwa na mwanachuoni maarufu wa kiislamu aitwae Ali muhsin Barwani ukurasa wa 153 tunasoma maneno haya; “hapakutokea mwarabu ambaye alipewa jina hilo (Muhammad) na babu yake tangu kuzaliwa kwake, na huyo babu hakuwa Mkristo bali alikuwa akifuata mila za kishirikina.” Na wala hakujua Taurati wala Injili." mwisho wa Nukuu
Ushahidi wa wazi unaothibitisha kuwa babu yake Muhammad Abdul Muttalib pamoja na kuomba miungu haswa mungu Hubaal sanamu kuu ndani ya alkaaba; vilevile aliomba dua kwa Allah; Mungu atakayerithiwa baadaye na mjukuu wake katika uislamu; ushahidi tunaupata tunaposoma utangulizi wa Suratul al-fyl ulio katika juzuu ya ukurada wa 946 Qurani iliyotafsiriwa kwa kiswahili chapa ya nane tunasoma maneno hayo. “chifu mkuu wa Makka zama hizo alikuwa Abdul Muttalib, alikwenda Al ka’ba pamoja na baadhi ya machifu wa kikuraish na akilishika komeo la chuma la mlango wa al-ka’ba, akamwambia Allah (S.W.) kuilinda nyumba yake pamoja na wahudumu wake. Zama hizo kulikuwa na masanamu 360 ndani na kando ya Al- ka’ba.”
(2) Himizo la Muhammad (S.A.W.) kwa makureshi wenzie kuhusu mungu aitwae Allah.
Katika kitabu kiitwacho mkweli mwaminifu kilichotungwa na Sheikh Said Moosa Muhamed al kindy juzuu ya mwanzo na pili chapa ya kumi ukurasa wa 130 tunasoma maneno haya: “katika wakati wa ujaahiliya kabla mtume (S.A.W.) kupata utume alikuwa akiwaambia watu “enyi watu semeni laa ilaha illah laah mtafuzu” yaani hapana mola ila Allah mtafuzu.
Huu ni ushahidi wa wazi kabisa ya kwamba Allah aliabudiwa na makureshi ma waarabu wenzao hao watu walikuwa washikina , wapagni na majahilia (wajinga). Kumbuka Muhammad alikuwa ni mkureshi naye aliposema “hapana mola ila Allah” alikuwa yupo zama za ujahilia na hakuwa anajua kitabu wala imani tazama Qurani 42:52 na alikuwa amepotea njia Qu 93:5-8
Ndio maana nasema Muhammad alikuwa mpagani na alifanya ushirikina. Zaidi ya hapo nasema kuwa Muhammad alikuwa mtume wa Majini na JINI NA ALLAH NI MUNGU WA KIPAGANI.
Courtesy Mwalimu Chaka
For Max Shimba Ministries Org.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW