Wednesday, August 16, 2017

IPO WAPI AYA KUTOKA QURAN INAYO SEMA KUVUTA SIGARA NI DHAMBI? (SEHEMU YA TATU)

Image may contain: 1 person
KUVUTA SIGARA HUWADHURU WENGINE
Moshi wa sigara una madhara sana. Kupumua moshi unaotoka kwa mtu anayevuta sigara kunaweza kusababisha kansa na magonjwa mengine, na kila mwaka watu 600,000 wasiovuta sigara hufa, hasa wanawake na watoto. Shirika la Afya Ulimwenguni linaonya hivi: “Moshi wa sigara unaweza kumdhuru mtu asiyevuta bila kujali kiwango cha moshi anachopumua.”
Kulingana na Yesu, kumpenda jirani, yaani, familia yetu, rafiki zetu, na wengine ni amri ya pili, ya kwanza ikiwa ni kumpenda Mungu. Yesu alisema hivi: “Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Mathayo 22:39) Tukiwa na tabia inayowadhuru wengine, hatuwezi kusema tunampenda jirani. Upendo wa kweli unatuchochea kufuata ushauri huu wa Biblia: “Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali ile ya yule mtu mwingine.”—1 Wakorintho 10:24.
Armen, anayeishi Armenia anakumbuka hivi: “Watu wa familia yangu walinisihi niache kuvuta sigara kwa sababu iliwaathiri. Hata hivyo, sikukubali kwamba kuvuta sigara kuliwasababishia matatizo.” Anasema hivi kuhusu kilichomsaidia: “Mambo niliyojifunza katika Biblia na kumpenda Yehova kulinisaidia niache kuvuta sigara na kukubali kwamba kuvuta sigara kuliniathiri mimi na wengine pia.”
KUVUTA SIGARA KUTAKOMESHWA MILELE!
Kujifunza Biblia kuliwasaidia Olaf, Jayavanth, na Armen kuacha tabia iliyowadhuru wao wenyewe na pia watu wengine. Waliacha kuvuta sigara si kwa sababu tu walijua madhara yake, bali pia kwa kuwa walimpenda Mungu walitamani kumfurahisha. Upendo unakaziwa kwenye andiko 1 Yohana 5:3, linalosema: “Kwa maana kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si mzigo mzito.” Huenda ikawa vigumu kufuata kanuni za Biblia, lakini ukimpenda Mungu kwa moyo wote, ni rahisi kumtii.
Kupitia mpango wa elimu wa ulimwenguni pote, Mungu anawaweka watu huru kutoka kwenye utumwa wa tumbaku. (1 Timotheo 2:3, 4) Hivi karibuni, Mungu kupitia Ufalme wake, yaani, serikali ya mbinguni inayoongozwa na Mwanawe, Yesu Kristo, ataondoa mfumo wa kibiashara wenye pupa ambao umesababisha mamilioni ya watu kuwa watumwa wa tumbaku. Ataondoa janga la kuvuta sigara na kuwasaidia wanadamu kuwa wakamilifu kimwili na kiakili.—Isaya 33:24; Ufunuo 19:11, 15.
Ikiwa unatamani kuacha kuvuta sigara, usikate tamaa. Ukijifunza kumpenda Mungu na kukubali maoni yake, wewe pia unaweza kufanikiwa kuacha kuvuta sigara.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi weyu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW