Tuesday, August 22, 2017

UNAYAJUA MADHARA YA KUANGALIA PICHA ZA UTUPU "PONOGRAFIA"? (SEHEMU YA NNE)

No automatic alt text available.
YOSEFU ALIUKIMBIA UASHERATI
Yosefu alishawishiwa jinsi gani, naye alifanya nini?
Yosefu, ndugu-nusu ya Dina, aliyekuwa kijana mzuri aliyempenda Mungu, aliukimbia uasherati. (Mwanzo 30:20-24) Alipokuwa mtoto, Yosefu aliona matokeo mabaya ya upumbavu wa dada yake. Inaonekana kukumbuka mambo hayo, na vilevile kutamani kukaa katika upendo wa Mungu, kulimlinda Yosefu miaka mingi baadaye huko Misri wakati mke wa bwana wake alipokuwa akijaribu kumshawishi “siku baada ya siku.” Bila shaka, kwa sababu Yosefu alikuwa mtumwa, hangeweza kuacha kazi na kuondoka! Ilimbidi ashughulikie hali hiyo kwa hekima na uhodari. Alifanya hivyo kwa kukataa tena na tena vishawishi vya mke wa Potifa, na mwishowe, kwa kumkimbia.—Mwanzo 39:7-12.
Fikiria hili: Ikiwa Yosefu angetumia muda mwingi akiwaza kuhusu mwanamke huyo au kuwaza-waza juu ya ngono, je, angeendelea kuwa mtimilifu? Haielekei angeweza. Badala ya kuwazia daima mambo yasiyofaa, Yosefu alithamini uhusiano wake pamoja na Yehova, jambo ambalo lilionekana wazi katika maneno ambayo alimwambia mke wa Potifa. Alisema: “Bwana wangu . . . hakunizuilia chochote ila wewe, kwa sababu wewe ni mke wake. Basi ninawezaje kufanya ubaya huu mkubwa na kwa kweli nimtendee Mungu dhambi?”—Mwanzo 39:8, 9.
Mungu alielekeza mambo jinsi gani katika kisa cha Yosefu?
Wazia shangwe ambayo Mungu alikuwa nayo alipomwona kijana Yosefu akiendelea kuwa mtimilifu siku baada ya siku, ingawa alikuwa mbali na familia yao. (Methali 27:11) Baadaye Mungu alielekeza mambo ili Yosefu afunguliwe kutoka gerezani na vilevile kuwa waziri mkuu wa Misri na msimamizi wa chakula! (Mwanzo 41:39-49) Jinsi yalivyo kweli maneno haya ya Zaburi 97:10: “Enyi mnaompenda Mungu, chukieni yaliyo mabaya. Yeye anazilinda nafsi za washikamanifu wake; huwakomboa kutoka katika mkono wa waovu”!
USIKOSE SEHEMU YA TANO
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi Wetu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW