Wednesday, August 16, 2017

IPO WAPI AYA KUTOKA QURAN INAYO SEMA KUVUTA SIGARA NI DHAMBI? (SEHEMU YA PILI)

Image may contain: one or more people, people sitting, people playing musical instruments and smoking
KUVUTA SIGARA HUHARIBU MWILI
Jarida The Tobacco Atlas linasema hivi: “Kuvuta sigara . . . kumethibitishwa kisayansi kwamba kunadhuru karibu viungo vyote mwilini na husababisha magonjwa na kifo.” Inajulikana kwamba kuvuta sigara husababisha magonjwa kama vile kansa, ugonjwa wa moyo, na wa mapafu. Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, kuvuta sigara ni chanzo kikuu cha vifo vitokanavyo na magonjwa ya kuambukiza kama vile kifua kikuu.
Kupitia Neno lake, Biblia, Mungu anatufundisha jinsi ya kuwa na maoni yanayofaa kuhusu uhai, mwili na uwezo wetu. Mwanaye, Yesu, alikazia jambo hilo aliposema hivi: “Lazima umpende Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.” (Mathayo 22:37) Bila shaka, Mungu anataka tutumie vizuri na kuthamini uhai na mwili wetu. Tunapoendelea kujifunza kumhusu Mungu na ahadi zake, tutapendezwa na kuthamini wema wake. Hilo litatuchochea kuepuka jambo lolote linalochafua mwili wetu.
Jayavanth, ambaye ni daktari nchini India, alivuta sigara kwa miaka 38. Anasema hivi: “Nilisoma kuhusu madhara ya kuvuta sigara kwenye majarida mbalimbali ya afya. Nilijua ubaya wa kuvuta sigara na niliwashauri wagonjwa waache sigara. Hata hivyo, nilishindwa kuacha licha ya kujaribu mara tano au sita.” Ni nini kilichomsaidia afaulu? Anasema: “Niliacha kuvuta sigara baada ya kujifunza Biblia. Tamaa ya kumpendeza Mungu ilinichochea kuacha kabisa tabia hiyo.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
==== USIKOSE SEHEMU YA TATU ====
KUVUTA SIGARA HUWADHURU WENGINE
Moshi wa sigara una madhara sana. Kupumua moshi unaotoka kwa mtu anayevuta sigara kunaweza kusababisha kansa na magonjwa mengine, na kila mwaka watu 600,000 wasiovuta sigara hufa, hasa wanawake na watoto. Shirika la Afya Ulimwenguni linaonya hivi: “Moshi wa sigara unaweza kumdhuru mtu asiyevuta bila kujali kiwango cha moshi anachopumua.”

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW