Tuesday, August 1, 2017

JE’ BWANA YESU ANAPATAJE KUWA MUNGU? (SEHEMU YA TANO)

Image may contain: one or more people, meme and text


Qur an 57:3
Yeye ndiye wa Mwanzo na ndiye wa Mwisho, Naye ndiye wa Dhahiri na wa Siri, naye ndiye Mjuzi wa kilakitu.
Andiko hilo linataja sifa hizo za msingi za Mungu ambapo moja ya sifa hizo ni ile Dhahiri na Siri, kupitia sifa hizi tunapata uthibitisho wa dhana nzima ya utendaji wa Mwenyezi Mungu katika hali mbalimbali yaani kwanza katika hali yake ya kutoonekana (Siri) na ile ya kujifunua Dhahiri na jambo la kufurahisha zaidi ni kuwa maandiko ya Qur an tukufu yameweka mifano muhimu juu ya aina zote hizi za mifumo ya utendaji wa Mwenyezi Mungu ambapo kwa mfano ile hali ya dhahiri inaonekana katika kisa cha nabii Musa kama tunavyosoma:-
Qur an 20:9-12
Na je imekujia hadithi ya Musa? 10’alipouona moto, akawaambia watu wake (aliokuwa nao) “Ngojeni, hakika nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga katika huo (moto)au nitapata mwongozaji katika moto huo (wakutuonyesha njia).11’ Basi alipofika akaitwa “Ewe Musa! 12’”Bilashaka Mimi ndiye Mola wako.Basi vua viatu vyako.hakika wewe uko katika bonde takatifu la Tuwa.
Hapo tunaona katika kisa hicho cha Nabii Musa kutokewa Mungu anajifunua kwa Musa kupitia kichaka cha moto ambapo Musa kwa kutojua anadhani hicho ni kichaka cha moto wa kawaidia tu na kumbe kichaka hicho kilikuja na uwepo wa Mungu, hivyo Musa kwa kukiona kichaka hicho alipaswa kukubali kuwa hapo alikutana na Mungu bayana. Rejea tamko la Mungu mwenyewe’ “Bilashaka mimi ndiye Mola wako”.
Je Mungu anazaliwa ikiwa alikuja kama mwanadamu?
Kimsingi Mungu yeye kama Mungu hazaliwi na hakuwahi kuzaliwa kamwe, ila kile kinachotajwa kuzaliwa na Mariam ni ubinadamu wa Yesu tu ambao ulizaliwa ili kufunika Uungu ambao kuwepo kwake ni tangu milele. Na kwa hivyo Mariam hakuzaa Uungu bali alizaa ubinadamu uliobeba Uungu, kwakuwa kusema kwamba Mariam alizaa Uungu wenyewe ni sawa na kusema kuwa Mungu ana mwanzo wa kuwepo kwake yaani alianza kuwako mara tu baada ya kuzaliwa na Mariam na kwa hali hiyo Mungu ana umri maalumu na mwanzo wa kuwepo kwake tendo ambalo linapingana na maelekezo tunayoyapata katika maandiko matakatifu:-
Zaburi 102:24-27
Nitasema, Ee Mungu wangu, usiniondoe katikati ya siku zangu; Miaka yako ni tangu kizazi hata kizazi.25 Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako.26 Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumu Naam, hizi zitachakaa kama nguo; Na kama mavazi utazibadilisha, Nazo zitabadilika.27 Lakini Wewe U Yeye yule; Na miaka yako haitakoma.
Na ili kukaza uelewa wa hili tunaweza kuona maelezo ya Yesu mwenyewe juu ya hili katika mjadala wake na Wayahudi pindi walipopingana na tamko la Yesu kujihusianisha na Ibrahimu ambapo Wayahudi walimkumbusha umri wake tangu alipozaliwa na Mariam na kutumia kigezo hicho kukosoa madai ya Yesu juu ya mahusiano yake na Ibrahimu hebu tusome majibu ya Yesu:-
Yohana 8:55
Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.57 Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Hilo ndilo tamko la Bwana Yesu akibainisha kuwa uwepo wake katika nyanja ya Kiuungu usingepaswa kuwekwa katika vipimo vya miaka ya kibinadamu maana kwa hali halisi yeye alikuwapo hata kabla ya Ibrahimu.
Hivyo kwa muktaza huu haitakuwa sahihi kusema kuwa Mariam ni mama wa Mungu kwakuwa neno lenyewe mama tu humaanisha mzazi (mlezi) hivyo ni kusema kwamba Mariam ni mzazi au mlezi wa Mungu tendo ambalo ni kufuru na ni kosa la wazi la kutotendea haki maandiko matakatifu.
Mifano michache juu ya uwezekano wa Mungu kutwaa ubinadamu.
Ni jambo linalonishangaza sana ninapoona hali ya upinzani juu ya ukweli huu ili hali ziko simulizi mbalimbali ambazo zingeweza kutumika kama vielelezo muhimu vya kurahisisha uelewa wa jambo hili, hebu ona mfano wa kisa hiki kinachosimuliwa na watu wengi majini dare s salaam:
Kijana mmoja alikuwa akipita njiani na kukutana na binti mzuri aliyetokea kumpenda, na ndipo baada ya maongezi binti huyo alikubali kwenda kupafahamu nyumbani kwa kijana huyo’ baada ya kufika na wakiwa wameketi ukumbini ndipo kijana huyo akamuomba yule binti ampatie rimoti ya TV iliyokuwa mbele kidogo upande wake na kwa namna ya kutisha binti huyo badala ya kuinuka na kwenda kuchukua rimoti hiyo alifyatua tu mkono wake ulioonekana kurefuka kupita kiasi na kuichukua rimoti hiyo. Kwa hali hiyo upendo uliishia hapo na kijana huyo kupiga kichwa mlango na kutoka nje kwa hofu na hatimaye kuzimia mlangoni.
Watu wengi wanaosimulia kisa hicho huonekana kufanya hivyo wakiamini kabisa kuwa huyo alikuwa ni jini aliyebeba taswira ya kibinadamu,na hivyo kile kinachonishangaza ni namna watu wanavyoweza kuamini kuwa shetani anaweza kujibadili ili kutesa watu lakini kwa nguvu zote hupingana na swala la Mungu kuvaa ubinadamu ili kutukomboa’ tafakari upya na badili mtazamo.
Bwana Yesu alichukua ubinadamu ili kumkaribia mwanadamu na hatimaye kusaidia ili aweze kuokolewa, Mtume Yohana alitamka:-
Yohana 1:14
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.
Hivyo kusudi la yesu kufanyika mwili na kukaa kwetu ndilo lingepaswa kupokelewa kwa shukrani zaidi maana lilileta utukufu kwa wanadamu tofauti na matukio tunayoshabikia juu ya viumbe vibaya. Tendo hilo la yesu kukaa kwetu (baada ya kuvaa mwili huo) linatajwa katika lugha ya Kigiriki kama:
Eskenosen’ ambayo maana yake ni kupiga kambi ( English – ‘Tent’/ dwelt among us).
Pamoja na uchambuzi wa Biblia ni jambo lililonifurahisha sana kuona katika vitabu vingine vinavyoaminiwa sana katika ulimwengu wa imani hususani msahafu wa Qur an kuona kielelezo muhimu juu ya dhana nzima ya mabadiliko yanayoweza kufanyika kwa hali moja kuchukua hali nyingine kwa lengo Fulani muhimu, mfano wa hili ni kisa cha Malaika aliyemtokea Mariam kwa nia ya kutotaka kumwogofya Mariam aliamua kubadili maumbile yake alipomtokea. Hebu tusome katika maandiko:-
Qur an 19:17
Na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea muhuisha Sharia Yetu (Jibrili) akajimithilisha kwake (kwa sura ya ) binaadamu aliyekamili .
Kama nilivyotangulia kueleza kuwa hicho ni kisa cha Malaika Jibril ambaye alimtokea Mariam kadri inavyoelezwa na kuaminiwa na ndugu zetu wa Kiislam yakuwa Malaika huyo alimtokea kwa umbile la kibinadamu, hivyo swali la kutafakari hapo ni kuwa kama Malaika tu aliweza kubadili umbile na kuja katika hali hiyo je Mungu anawezaje kushindwa?
Hivyo ukweli nikuwa Bwana Yesu alitwaa umbile hilo kwa lengo la kufunika utukufu wake ambao mwanadamu asingeweza kuukabili , andiko la mtume Paulo la Wakoritho linatuhitimishia sehemu hii ya uchambuzi.
2Wakoritho 5:18-19
Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho;19 yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.
Hivyo ieleweke kuwa umbile la kibinadamu la Yesu ndani yake lilibeba mamlaka kamili ya Uungu, mamlaka ambayo ilikuwepo tangu milele na hata kabla ya kuzaliwa kwa ubinadamu wa Yesu na Mariam.
Kama ni Mungu mbona alisema anaenda kwa Baba yake?
Hii nayo ni miongoni mwa hoja tete katika Ulimwengu wa imani ambapo kile kinachohojiwa hapo ni tendo la Yesu kuonekana mara kadhaa akitaja habari ya Baba katika mazungumzo yake kwa nyakati na matukio tofauti na hivyo kuibua hoja hii kuwa kama Yesu ni Mungu inakuwaje basi aseme anaenda kwa Baba yake na je kuna uhusiano gani baina ya Yesu na Baba?
Jibu la msingi la hoja hiyo”
Kimsingi kama nilivyokwishafafanua kwa kina juu ya utatu mtakatifu tuliona juu ya uwepo wa nafsi tatu za Mungu mmoja ambapo Baba ni mojawapo ya nafsi hizo, hivyo jambo la msingi katika hoja hii ni kuangalia tu sababu ya Yesu kuitamka nafsi hiyo ya Baba kama mamlaka tofauti wakati Fulani na ndipo tuangalie uhusiano uliyopo baina ya Baba na Neno-Yesu.
Yohana 16:25
Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa yaja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba.
Katika maelezo yake hayo Bwana Yesu anaeleza kuwa wakati fulani amekuwa akitumia mithali (mafumbo) kueleza juu ya habari ya Baba na sasa anaahidi kuwa hatimaye ipo siku ambapo atatamka wazi wazi juu ya habari ya Baba.
USIKOSE SEHEMU YA SITA
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW