Tuesday, August 1, 2017

YESU ALISEMA: KABLA YA IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NI MUNGU

Image may contain: crowd and text
Msipaniki Waislam. Kaa chonjo na fungua macho yako ya rohoni.
Kwa maneno rahisi, katika Yohana 8:58 Yesu alikuwa anasema “Kabla Ibrahimu asijakuwako mimi ni Mungu”
Yohana 8:58 Yesu aliposema;
“….Amin, Amin, nawambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko” Wayahudi kwanini waliokota mawe? Soma Walawi 24:16. “Na yeye atakayelikufuru jina la BWANA hakika atauawa; mkutano wote watamuua kwa kumpiga kwa mawe;..”
Je Yesu alimaanisha nini aliposema mimi niko hata wakaona amekufuru? Hebu tuone niko ni jina la nani?
Kutoka 3:13-14; “….Tazama, nitakapofika kwa wana wa Waisraeli na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wataniuliza, Jina lake n’nani? Niwambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO…MIMI NIKO amenituma kwenu.”
Kumbe "MIMI NIKO" ni jina la Mungu.
YESU NI MUNGU
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW