Friday, May 4, 2018

MAREHEMU MUHAMMAD NI ALLAH

Image result for MUHAMMAD IS ALLAH
Quran inasema mambo mengi sana kuhusu Allah. Na inadai kuwa hakuna anaye fanana na Allah. Lakini Quran hiyo hiyo inaleta utata kwa kusema Allah na Muhammad lazima wafuatwe. Inamaanisha kuwa Muhammad na Allah wapo sawa na wana heshima moja.

Maswali la kujiuliza:
1. Kwanini Waislam wanalazimishwa kumtii Muhammad na sio Allah?

2. Hivi unawezaje kumtii mtu aliye kufa (Marehemu/hayati)?

3. Kwanini Muhammad alipo kufa; Allah hakusikika tena? Ndio utafahamu kwanini nasema Muhammad ni Allah.

UTHIBITISHO:

Surat Al Imran 31. Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu.

32. Sema: Mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume. Na wakigeuka basi Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.

50. Na ninasadikisha yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati, na ili nikuhalalishieni baadhi ya yale mlio harimishiwa, na nimekujieni na Ishara kutokana na Mola Mlezi wenu. Kwa hivyo mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.

132. Na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpate kurehemewa.

Muhammad anawaambia Waislam WAMTII YEYE. Hivi kwanini tumtii mtenda dhambi na kuachana na Mwenyezi Mungu? Kwanini Muhammad asingesema tuzitii sheria za Mwenyezi Mungu na akajiweka yeye? KUMBE MUHAMMAD NI SAWA NA ALLAH. KUMBE MUHAMMAD NI ALLAH.


Surat AL Baqara 285. Mtume ameamini yaliyo teremshwa kwake kutoka kwa Mola Mlezi wake, na Waumini vile vile. Wote wamemuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake na Mitume wake. Hatutafautishi baina ya yeyote katika Mitume wake, na (Waumini) husema: Tumesikia na tumet'ii. Tunakutaka maghfira Mola Mlezi wetu! Na marejeo ni kwako.

MUHAMAMD ANAENDELEA KUSEMA MCHENI MWENYEZI MUNGU NA MTIINI YEYE "MUHAMMAD" NA SIO MWENYEZI MUNGU.

Surat Ash Shuaraa 108. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
109. Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
110. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

125. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
126. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
127. Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

131. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
132. Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.

141. Kina Thamud waliwakanusha Mitume.
142. Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
143. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
144. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
145. Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

150. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

160. Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.
161. Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?
162. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
163. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.

176. Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
177. Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
178. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
179. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

KUMBE USIPO MTII MUHAMMAD NA UKAMTII MWENYEZI MUNGU NA KUMWABUDU MWENYEZI MUNGU, KAMWE HUTO ENDA AKHERA, NDIO MAANA WAISLAM WAPO TAYARI KUFA, PALE UNAPO MUUMBUA MUHAMMAD.

Muhammad ni Allah maana alipo kufa Muhammad, na Allah hakusikika tena. Nikimaanisha Muhammad alipo kufa na Allah naye alikufa.

Swali la mwisho: Msemaji wa hizo aya hapo juu ni nani? Maana Waislam wanadai Allah ndie msemaji wa aya za Quran huku leo hii tunamsoma Muhammad akisema NITIINI MIMI ndani ya Quran?

UISLAM KWISHA HABARI YAKE HAPA.

Shalom,

Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Titon 2:13

Islam is not a religion proof # 121

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW