Tuesday, October 22, 2019

YESU NI NENO

No photo description available.
Kwa kawaida, maneno “Neno la Mungu” yanawakilisha ujumbe kutoka kwa Mungu au mkusanyo wa ujumbe huo au Yesu ambaye ni Neno. (Luka 11:28) Katika sehemu chache, “Neno la Mungu” au “Neno” hutumiwa kumwakilisha Yesu.​—Ufunuo 19:13; Yohana 1:​14.
Yohana 1:1 inasema “Neno alikuwa Mungu”. Yohana 1:14 inasema “Neno akafanyika mwili.” Hii inaonyesha wazi ya kwamba Yesu ni Mungu katika mwili. Matendo 20:28 inatuambia, “…Muwe wachungaji wa kanisa la Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe,” Ni nani aliyelinunua kanisa kwa damu yake mwenyewe? Yesu kristo. Matendo 20:28 inasema ya kwamba Mungu alilinunua kanisa kwa damu yake mwenyewe. Kwa hivyo Yesu ni Mungu!
Ujumbe kutoka kwa Mungu. Mara nyingi manabii walisema kwamba ujumbe ambao walitoa ulikuwa Neno la Mungu. Kwa mfano, Yeremia alianza ujumbe wake wa kinabii kwa kusema “Neno la Yehova likaanza kunijia.” (Yeremia 1:4, 11, 13; 2:1) Kabla ya kumwambia Sauli kwamba Mungu alikuwa amemchagua kuwa mfalme, nabii Samweli alisema hivi: “Simama tuli sasa ili nikuambie Neno la Mungu.”​—1 Samweli 9:27.
Pia “Neno” linaonekana katika Biblia likiwa ni Yesu Kristo, akiwa Roho mbinguni na pia akiwa Mwanadamu duniani. Fikiria sababu kadhaa za kufikia mkataa huo:
Neno aliishi kabla ya vitu vingine vyote kuumbwa. “Hapo mwanzo Neno alikuwako . . . Hapo mwanzo huyo alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.” (Yohana 1:1, 2,3).
Neno alikuja duniani. “Neno akawa mwili, akakaa katikati yetu.” (Yohana 1:14) Kristo Yesu “alijiondolea mwenyewe hali yake na kuchukua umbo la mtumwa na kuwa kama wanadamu.”​—Wafilipi 2:5-7.
Neno ni Mungu. Baada ya kusema kwamba “Neno akawa mwili,” kama ilivyonukuliwa hapo juu, mtume Yohana aliendelea kusema hivi: “Nasi tukautazama utukufu wake, utukufu kama ule ulio wa Mwana mzaliwa-pekee kutoka kwa Baba.” (Yohana 1:14) Pia, Yohana aliandika hivi: “Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”​—1 Yohana 4:15.
Neno ana sifa za Mungu. “Neno alikuwa Mungu.” (Yohana 1:1) Yesu “ndiye mng’ao wa utukufu [wa Mungu] na mwakilisho sawasawa wa utu wake wenyewe.”​—Waebrania 1:2, 3.
Neno anatawala akiwa mfalme. Biblia inasema kwamba kwenye kichwa cha Neno la Mungu “kuna vilemba vingi.” (Ufunuo 19:12, 13) Neno anaitwa pia “Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.” (Ufunuo 19:16) Yesu anaitwa “Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.”​—1 Timotheo 6:14, 15.
Neno ni Mungu. Inaonekana kwamba jina “Neno” linamtambulisha Yesu. Yesu alisema kwamba alitimiza jukumu hilo: “Baba mwenyewe aliyenituma amenipa amri kuhusu jambo la kutangaza na la kusema. . . . Kwa hiyo mambo ninayosema, kama vile Baba alivyoniambia, ndivyo ninavyoyasema.”​—Yohana 12:49, 50.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW