Friday, July 31, 2015

YESU NI MUNGU

(Sehemu ya Nne)
“Marafiki na maadui wa Yesu waligawanyika tena na tena na kile alichosema na alichofanya [Yesu]. Alikuwa alitembea barabarani, dhahiri kama mtu yeyote, kisha akageuka na kusema kitu fulani mfano ‘Kabla ya Abraham kuwako, nipo.’ Au iIkiwa umeniona, basi umemuona baba. Kisha kwa utulivu baada ya kulaumiwa kukufuru, alisema, ‘Mwana wa Adamu ana mamlaka duniani kusamehe dhambi’ Kwa wafu, alisema ‘Njoo mbele’, au, ‘Inuka’ na walitii. Kwa tufani baharini aliweza kusema ‘Tulia’ na kwa kipande cha mkate, alisema ‘Kuwa vipande elfu moja’ na vilifanyika mara moja.”

Baadhi ya watu wanadai hakuwai waziwazi kusema “Mimi ni Mungu”. Je, ni kweli kwamba hakuwai kunena maneno hayo? “Mimi ni Mungu”. Vilevile, Yesu hakuwai waziwazi kusema “Mimi ni binadamu” au “Mimi ni Nabii” Na Yesu alikuwa binadamu bila shaka, na wafuasi wake walimchukulia kama nabii kama Musa na Eliya. Kwa hiyo hatuwezi kuamua kwamba Yesu kuwa mtakatifu ni kwa sababu hakusema maneno hayo, kama ambavyo hatuwezi kusema hakuwa Nabii.

“Wahubiri wa injili” wa Kiislamu huwa wanapinga kuwa Yesu ni Mungu na unapowakatalia wanakwambia, “Lete andiko.” Maandiko yapo mengi sana ndani ya Biblia juu ya ukweli kwamba Yesu ni Mungu. Ni mengi mno!
Ukishawapa andiko, wanabadilika na kusema, “Nataka maneno aliyoongea Yesu mwenyewe.”

Hiki ni kigezo POTOFU na si cha kibiblia hata kidogo. Ukweli ni kwamba, Biblia YOTE ni Neno la Mungu. Haijalishi amezungumza Musa, Isaya, Yohana, Petro au Yesu mwenyewe. Imeandikwa:

Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. (2Petro 1:21).

Hivyo, kudai kwao eti, “Nataka maneno aliyosema Yesu mwenyewe,” ni kigezo batili na kisicho na mantiki hata kidogo.

Ufuatao ni ushahidi wa kibiblia kwamba YESU KRISTO ni Mungu.
Yohana 8:58
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.

NIKO ni jina la Mungu peke yake. Tunakutana na jina hilo pale Musa alipoongea na Mungu na kutumwa kuwakomboa wana wa Israeli kutoka Misri. Imeandikwa:

Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO (Kutoka 3:13-14).

Mwanadamu yuko kwa sababu Mungu alisababisha awepo. Gari liko kwa sababu injinia au mbunifu alisababisha liwepo. Nyumba ipo kwa sababu fundi alisababisha iwepo. Lakini Mungu YEYE YUKO TU!! Hayupo kwa kusababishwa na yeyote! Ndiyo maana akasema MIMI NIKO AMBAYE NIKO! Yesu ni NIKO. Kwa hiyo, Yeye ni Mungu.

Yohana 10:30
Mimi na Baba tu umoja.

Waislamu wana msemo wao kwamba eti, Yesu na Mungu ni wamoja katika malengo, si katika asili yao. Basi huwa nawauliza swali kuhusu aya ifuatayo ya Isaya, nao wanazimika na kukosa jibu:

Thursday, July 30, 2015

UONGO WA DINI YA KIISLAM



Tunaamini unapofuata kwa makini mada hii utatii neno la Mungu wa kweli, kuliishi, na kulitenda.
Mkristo wa kweli hatorudi katika ubishi wa ki dini pamoja na wapagani ambao ni miongoni mwa Anti-Kristo waitwao waislamu.
Huu ni utafiti wa ki maandiko tulioufanya tukilinganisha ujumbe wa Qur’an Tukufu pamoja na Biblia Takatifu pamoja na kwamba mimi nimeishi msikitini nikajaliwa neema kuujuwa ukweli. Karibu na twakutakieni usomaji mwema.
MWANZONI KABISA
Tunakusalimu tena katika jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo,
Ni kwa mara ingine Mungu wetu ambaye jina lake ni YEHOVA ametupa neema yake ili tuweze kuchangia pamoja haya maneno ya uzima yaani ‘UKWELI WA NENO LA MUNGU, BIBLIA’
Kwanza kabisa nataka niendelee kukujulisha kama hii wavuti yetu siyo ya kidini bali ni kwa ajili ya kuipiga tarumbeta ili wana wa Mungu wa pekee na wa kweli waweze kuikimbilia kwa mbali ibada kinyume na mapenzi ya Mungu!
Hatujali wewe wa ni dini gani? taifagani? au lugha gani? sisi tunachokifanya ni kujaribu kuyachnguza maandiko matakatifu pamoja na kugundua ukweli wake!
Bwana Mungu akubariki unapokuwa sehemu ya kuitafuta kweli.
JE, SISI NA WAISLAM TWAENDA NJIA MOJA?

Amosi 3:3
‘Je, Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?’
Yaani hata mtoto wa miaka mitano atakuletea jibu lisemalo APANA!!!

Sababu No.1
WAO NI DINI ILA SISI NI KANISA
Qr. 5 au surat Al Maida 2-3,

Enyi mlioamini! Msivunje hishima ya alama ya dini ya Mwenyezi Mungu wala mwezi mtakatifu, wala wanyama wanaopelekwa Makka kuchinjwa, wala vigwe vyao, wala wanaoelekea kwendea Nyumba Takatifu, wakitafuta fadhila na radhi za Mola wao mlezi. Namkishatoka Hija yenu basi windeni. Wala kuwachukia watu kwa kuwa walikuzuilieni kufika Msikiti mtakatifu kusikupelekeeni kuwafanyia uadui. Na saidianeni katika wema na uchamngu. Wala msisaidiane katika dhambi na uadui. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.
Mmeharimishiwa nyamafu, na damu, na nyama ya nguruwe, na myama aliyechinjwa si kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na aliyekufa kwa kunyongeka koo, na aliyekufa kwa kupigwa, na aliyekufa kwa kuanguka, na aliyekufa kwa kupigwa pembe, aliye liwa na mnyama, ila mkimdiriki kumchinja. Na pia ni haramu kula nyama aliyechinjiwa sanamu. Na ni haramu kupiga ramli. Hayo yote ni upotovu.
Leo waliokufuru wamekata tamaa na DINI yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini. Na mwenye kushurutishwa na njaa, bila ya kupendelea dhambi, basi hakika Mwenyezi Mungu ni msamehevu na Mwenye kurehemu.
Qr. 4 Au surat An Nisaai 171,

Enyi watu wa kitabu! Msipite kiasi katika DINI yenu, wala msiseme Mwenyezi Mungu ila kwa lililo kweli…..
Biblia inasemaje?
Mathayo 16:16, 18,

Simoni Petro akasema akajibu akasema, Wewe ndiwe KRISTO, Mwana wa Mungu aliye hai.
Nami nakwambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
Matendo ya mitume 2:41, 47,

Naowaliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.Wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha KANISA kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.
1Wakorintho 3:23, Nanyi ni WAKRISTO, na Kristo ni wa Mungu
Matendo ya itume 11:26Hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa WAKRISTO kwanza hapo Antiokia.

               Sababu NO.2      MUNGU MMOJA

Ukitazama kwa haraka haraka namna wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu wanavyolinganisha aya za Qurani na Biblia unaweza ukashawishika kuamini hicho wanachokifundisha, lakini ni vyema tukajifundisha kwa undani kadiri ya Qurani na Biblia na kisha tuone kama kuna ukweli juu ya hayo mafundisho yao, ya kusema Allah Sub-hana Wataala ndiye Yehova.tukumbuke kuwa Mungu tunayeabudu alitutahadhalisha sana Wakristo kwa kusema hivi.

Kutoka 20:1-3
Mungu akanena maneno haya yote akasema Mimi ni BWANA Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa usiwe na Miungu mingine ila mimi.
Tahadhari hii Ya Mungu wetu ya kusema usiwe na Miungu inamaanisha kuwa Miungu mingine yenye kuabundiwa na watu ipo. Kwa sababu katika Biblia neno Mungu Kiebrania“Elohim” Kiyunani "Theos" limetanjwa mara 3979 lakini pia miungu ya uongo imetanjwa mara 271. Baadhi ya miungu hiyo ya uongo ni hii:
mungu Dargoni  Waamuzi16:23
mungu Baal  Wafalme 18:21
mungu mke wa Waefeso aitwae Artemi  Matendo 19:24-28.
Aidha tusomapo Qurani pia imetaja miungu mbalimbali iliyokuwa inaabundiwa kule Makka nayo ni hii;
Qurani 53:19-20,23 Suratul An- Najm (Nyota).
Je, mumewaona Lata na Uzza? Na Manata (mungu wenu) mwingine wa tatu (kuwa ndio waungu hao badala ya mwenyenzi mungu)? ayakuwa haya (majina ya Lata mungu mwanamke na Uzza mungu mwanamke mwenye enzi. Na Manata mungu mwanamke anayeneemesha ila ni majina tu mliowapa nyinyi na baba zenu…..
Hivyo basi tunaona kuwa miungu yenyewe kuabudiwa ni mingi na kila mwenye kuabudu humtegemea huyo mungu wake na kusema ni mmoja. Mfano waliyemuabudu Dagoni walisema ni mungu mmoja, waliyemwabudu Baali walisema ni mungu mmoja, waliyemwabudu Artemi walisema Artemi ndiye mungu mkuu. Kadharika Manabii.walimtumikia Mungu mmoja aitwaye Yehova, naye Muhammad alimwabudu mungu mmoja aitwaye Allah. Ninachotaka kukifundisha kwa jamii ijue je, huyo Allah ndiye Yehova?,

Nabii Musa alivyosema:
Kumbukumbu la Torati 6:4
Sikiza ee Israeli; BWANA Mungu wetu BWANA ndiye mmoja.
Nabii Isaya alisema hivi
Isaya 45:18, 21,
Maana BWANA, aliyeumba mbingu, asema hivi, yeye ni Mungu,ndiye aliyeumba Dunia na kuifanya ….. si mimi BWANA? Wala hapana Mungu zaidi ya mimi. Mungu mwenye haki, mwokozi hapana mwingine zaidi ya mimi.
Nabii Daudi Alisema:
Zaburi 86:10Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, wewe ndiwe mfanya miujiza, ndiwe Mungu peke yako.
Yesu alisema hivi:
Yohana 17:3, Na uzima wa milele ndio huu wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliye mtuma
Paulo naye Alisema hivi
1 Wakorintho 8:4
Basi kwa habari ya kuvila vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu; twajua ya kuwa sanamu si kitu katika ulimwengu, na yakuwa hakuna Mungu ila mmoja tu
.
Sababu NO.3
ALLAH WAO SIYE YEHOVA MUNGU

NANI KAMPA UTUME NA UNABII MTUME MUHAMMAD?


           


Twakusalimu kwa mara ingine katika jina tukufu na takatifu la Yesu Kristo Bwana wetu.

Twazidi pia kukushukuru kwa ajili yakuyafuata mafundisho haya ya Biblia Takatifu.

Twaamini mada ile ile lakini ya tatu kuhusu imani ya kiislamu itakusaidia ukiwa mkristo wa kweli kutoishiriki mihadhara ya ubishi kati ya waislamu na wakristo.
Sababu ya pili, ni kwako ndugu na dada ambaye ungali bado katika upotevu wauislamu bila yako kujuwa ukweli kwa wazi.

Katika zile sababu zaidi ya 25 zinazotudhihirishia uongo na upotevu wa dini ya uislamu tumetamani kuchimbua «Utume na unabii wa nabii Muhammad s.a.w» 

Tunazo sababu zaidi ya mia (100) kuwauliza waislamu na kitabu chao qura'n swali tulilolitaja hapo juu na maswali mengine kuhusu UISLAMU na Qura'n! na moja ya hayo maswali ni sababu kitabu chao yaani Qur’ani kinatutaka sisi wakristo kusilimu, lakini kabla tusilimu nakuingia dini ya uislamu ni sherti tumjuwe vyema vilivyo huyu nabii sababu Yesu Kristo anatuonya kwamba manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi yamkini hata wachaguliwa wa Mungu. Mathayo 7 :15-20. Kwa hivi ni sherti Muhammad atumbukizwe ndani ya Biblia iliyokitangulia kitabu alichopewa ijapokuwa baadaye tutajuwa alikipewa na nani ? na akizama ndani ya Biblia hatuna budi kumfwata na kumtumikia Allah subhanahu wa tahalah! Lakini ikimtema kando huyo si nabii na mtume wa Yehova Mungu.

Kama mimi mwenyewe Fred Nguli MWAMBA niliyewahi kunaswa nakujikuta katika wavu wa hiyo imani nilizidi kujiswali maswali mengi huku nikifanya uchumguzi kwakulinganisha maandiko ya kiislamu na yale ya kikristo lakini nisiupate ukweli huko na neema yake Kristo Yesu ikanirudisha kwa mara ingine katika imani ya kweli katika yeye Kristo Yesu na ukristo wake.

Ukweli ambao hatuwezi kuupinga ni kwamba Biblia Takatifu ambayo waislamu pia huitumia kwakuichezea-chezea na isitoshe pia kwakuitumia kuwapiga wakristo waliopofushwa wakidhani kwamba waislamu wanaiamini, hiyo Biblia imekuwapo duniani zaidi ya miaka 2000 kabla ya Qur’ani tukufu kuwepo.
Biblia Takatifu inasema hivi:
Kutoaka 20:1-3
«Mungu akanena maneno haya yote akasema,  Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi
Hapa Mungu alitutahazarisha mapema kumpitia mtumishi wake nabii Musa ya kwamba tuepuke kuwa na miungu mingine ila yeye pekee ambaye jina lake ni Yehova!
Haya maneno sawa na Mathayo 7:15-20 Mungu aliyasema kabla ya Muhammad kuwepo, kabla ya Qur’ani kuwepo na kabla kuwepo kwa wanaume 4 walioiandika Qur’ani tukufu ambao ni:Seidinah Umar, Osman, Abubakar na Ali.

Inamaanisha nini?
Ni kwamba kama Mungu mwenyezi anavyokuwa na watumishi kama vile mitume na manabii, vilevile miungu nayo yaweza kuwa namitume na manabii wake.
Kwa mujibu wa Mathayo 7:15-20, Yesu Kristo anatupatia alama yakuwatambuwa manabii wa uongo akisema katika mstari wa 16 hivi « Mtawatambua kwa matunda yao » 
Basi natujaribu kuliangalia andiko lingine jinsi gani twaweza kuwatambua,
1Yohana 4:1-3, 15
«Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. 
Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. 
Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.»

15 «Kila akiriye ya kuwa Yesu ni mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu
Hiki ni kipimo tunachokitumia kuwapima mitume na manabii! 
Mathayo 7:15-20
Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?
Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazurina mti mwovu huzaa matunda mabaya.
Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.»

Hebu niseme hivi kulingana na tahazari ambayo Mungu ametupatia katika maandiko hayo mawili hapo juu:

‘Muhammad namlinganisha na mti, sasa matunda yake yakiwa mazuri sina ubishi nitamfuata, lakini yakiwa ni matunda kinyume na hayo nitamhesabu kama nabi iwa uongo’.

Je, katika Qurani Allah wa waislamu na Muhammad anasemaje?

Qr. 112 au surat Al-Ikhlas’
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
Hakuzaa wala hakuzaliwa.
Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.

Qr. 19 au surat Maryam 35
Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwa na mwana, Subhanau, Yeye ametakasika! Anapolihukumia jambo basi huliambia tu: Kuwa! Likawa.
Huyu ni mungu tofauti na Mungu wa mbinguni ambaye jina lake ni Yehova! na tukilinganisha na yale maandiko ya Mathayo na waraka wa kwanza wa Yohana ukweli uko wazi kama huyu hatokani na Mungu na kwamba huyu ni Anti-Kristo! Kwani Biblia inasemaje ?
1Yohane 2:22-26,
Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana. Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia. Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba.
Na hii ndiyo ahadi aliyoyuahidia, yaani, uzima wa milele.
Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza.
Wakolosai 1:13-15,
Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi; Naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
Yohane 3:16-17,
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminie asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Kwa maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.

Kwahivi sisi wakristo tunazo sababu zaidi ya 100 kwanini hatumtambui mtume Muhammad, dini yake na mungu wake ambazo Mungu akituwezesha tutaziweka wazi moja kwa moja.

Ila hatuwezi kutosema hii moja ambayo ni hii:

Katika kitabu cha Qura’n tukufu kuanza na surat Al-Faatihah hadi surat Al-Nasmaandishi yake yanampinga Yehova Mungu wa israel.

CHIMBUKO NA UKOO WA UTUME NA UNABII WA MUHAMMAD

Kwanza kabisa, sote twajuwa kama kila mtoto huenda na kabila, lugha na mil aya babaake ila si ya mamaake. Hilo halina shaka hata kidogo!
Ibrahimu babaake Isaka na Ismail kabla aitwe na Mungu alikuwa ni mwarabu wa ki kurdi na baadaye Mungu aliyeviumba vyote akambadilisha na uzao wake wote baadaye ukawa ni waebrania.

Mwanzo 12:1-3
«Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa

Lakini Muhammad, Qur’ani na wafuasi wake huzidi kuhakikisha kuwa Muhammad ni wa ukoo wa Ibrahimu wakati Ibrahimu si mwarabu tena!

Katika kitabu cha «maisha ya mtume Muhammad sw», twahakikishiwa kwamba Muhammad ni mwarabu wa kabila la Makureshi. 

                   KUPEWA UTUME

JE, ISA BIN MARYAM NDIYE YESU KRISTO?



 Utangulizi

SHALOM TENA,

Kwa mara nyingine twamshukuru Yehova Mungu kwa kutupa neema hii tena ili tuweze kukufikishia ujumbe huu wa Biblia na kweli zake.

Kwa muda wa miaka mingi sana pia duniani pote imekuwa ni kawaida kuwasikia waislamu wakifundisha watu wao na kuwadanganya bila ya wao kujuwa ao wengine wakiwa wanakijuwa wanachokifanya kuwa ISA bin Maryam’ Kama Qurani inavyofundisha ndiye “YESU KRISTO”.

Mafundisho haya hivi sasa yanaendeshwa kwa kulinganisha aya za Biblia na Qurani. Ma sheihk, ma Imam na wahubiri wengi wa dini ya kiislamu wanaendesha mihadhara kwa uwingi duniani. Wahadhiri hao pia hutumia mbinu zingine mbali-mbali kama majarida na kurekodi kanda za audio na video, ambazo zimesababisha baadhi ya wakristo nusu au wakristo wajinga waamini kuwa Isa Bin Maryamu ndiye Yesu Kristo. Swali la msingi kwa wakristo wote;Je, ni kweli Isa bin Maryam ndiye Yesu Kristo?

Nakusihi kwa jina lake Bwana wetu Yesu Kristo kufuatilia somo hili kwa umakini wote kama tulivyokuahidi katika lile somo ambalo lilitangulia wiki jana.

SEHEMU KUU ZA SOMO HILI

1. Madai yanayotumika na waislamu kusema Isa ndiye Yesu

2. Je, mama wa Isa ndiye wa Yesu?
3. Maana ya jina Isa
4. Maana ya jina Yesu
5. Je, kuzaliwa kwa Yesu ni sawa na Isa?
6. Je, Isa bin Mariamu ni mwana wa Mungu?
7. Je, mamlaka ya Isa na Yesu ni sawa?
8. Ikiwa Yesu ndiye Isa je, Isa.
9. Ujue umuhimu wa kumwamini Bwana Yesu

1.  Kisingizio N0.1
Waislamu husema Isa ndiye Yesu
Qr.3 au surat I’mran 45
(Kumbukeni) waliposem malaika. ‘Ewe Maryamu Mwenyezi Mungu anakupa habari njema za (kumzaa moto bila mume bali hali kwa kutamka) Neno tu litokalo kwake (la kumwambia zaa ukazaa pasina kuingiliwa) jina lake ni Masihi Isa mwana Maryamu, mwenye hishima kaitka dunia na ahera na miongoni mwa waliopelekwa mbele na Mwenyezi Mungu.
Marko 6:3-4, Huyo si Yule seremala, mwana wa Mariamu na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake. Yesu akawaambia ‘Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamaa zake na nyumbani mwake.
Hapa Waislamu wanasema kana vile Qurani inavyofundisha jina la mama wa Isa ni Mariamu kadhalika Biblia inafundisha jina la mamake Yesu ni Mariamu. Hivyo wanasema kuwa Yesu ndiye Isa.
Soma pia Mathayo 1: 18-21 na Yohana 2:1.
2. Kisingizio N0.2
Isa ni Mtume wa Allah kwa Waisraeli
Qr. 4 au surat An-Nisaai 171
Enyi watu wa kitabu misipindukie mipaka katika dini yenu, wala msiseme juu ya Mwenyezi Mungu ila yaliyo kweli. Masihi Isa bin Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu…
Hapa tunaona kuwa Qurani imemtaja Isa kuwa ni ntume, je, mtume kwa akina nani? Endelea kusoma aya hizi katika Qurani:
Qr.  61 au surat Ass’af 6
Na Isa bin Maryamu aliposema: enyi wana wa Israili! Mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu. Nisadikishaye yaliyo kuwa kabla yangu kaitka Taurati. Na kutoa habari njema ya mtume atakeayewajia nyuma yangu ambaye jina lake litakuwa Ahmad…
Soma pia katika Qr. 3 au surat Al I’mran 49:
Ayah ii inathibitisha kuwa Isa ni mtume kwa Waisraeli. Je, Yesu ni mtume kwa akina nani? Waislamu wanaoendesha mihadhra pia husoma aya hizi za Biblia.
Waebrania 3:1Kwa hiyo ndugu watakatifu wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtakafarini sana mtume na kuhani mkuu wa maungamo yetu Yesu.
Mathayo 15:24Akajibu, akasema, ‘Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
Kwa hivyo kama Qurani inavyofundisha kuwa Isa mwana wa Maryamu ni mtume kwa Waisreali ndivyo Biblia inafundisha kuwa Yesu ni mtume kwa waisraeli hivyo basi Isa ndiye Yesu. Hapa ndipo wahadhiri wa dini ya Uislamu wanavyoifundisha na kuwashika mateka na jamii za wakristo-nusu. Je, madai haya ni sahihi? Biblia itatusaidia kujibu huko mbele.
3. Kisingizio N0.3
Isa bin Maryamu alifanya miujiza
Qr. 5 au surat Al Maida 110
Na pale Mwenyezi Mungu atakaposema, Ewe Isa mwana wa Maryamu kumbuka neema yangu juu yako na juu ya mama yako. Nilipokutia nguvu kwa Roho takatifu (Jibrili), ukazumgumza na watu katika utoto (wako) na katika utuuzima (wako). Na nilipokufundisha kuandika na hikima na Torati na Injili na ulipotengeneza kwa undongo sura za ndege kwa idhini yangu, na ulipo waponesha vipofu na wenye ukoma kwa idhini yangu, na ulipowafufua (baadhi ya) wafu (makaburi mwao) kwa idhini yangu, na nilipokuzuilia wana wa Israeli (wasikudhuru) ulipowafikia kwa joha zilizo wazi; wale walio kufuru miongoni mwao wakasema: Haya si chochote ila ni uchawi dhahiri
Waislamu wanasem huu ni ushahidi wakutosha kwani Allah anasema Isa alifanya miujuza mingi hii.
Isa aliponyesha vipovu ndiye Yesu aliponyesha vipovu Mk 10:46-52, aliyewafufua wafu makaburi ndiye Yesu aliyewafufua pia huu upande, Mk 5:21-43 na aliyewaponyesha wenye ukoma ndiye…Yesu aliponya Ukima  Luka17:1
Walimu wa kiislamu hao wanasema kama vile Qurani invyosimulia kuwa Isa amefanya miujiza mingi, ndiyo Biblia inavyofundisha hivyo Yesu ndiye Isa, isitoshe wanasema hivi pia:
Isa ibin Maryamu ni Nabii, Quran suratul 4:171, kadhalika Biblia inafundisha kuwa Yesu ni Nabii, Yohana 6:14Yohan 7:40Luka 13:3324:19Marko 6:4, na Mathayo 13:57.
Kulingana na watafiti wa Biblia imeelezwa kuwa imerikodiwa kwamba Yesu ni Nabii mara 12. Vile vile wahadhiri wa Kiislamu wanafundisha ya kwamba Isa ni Neno la Kiarabu, katika kiingreza Jesus na kwa Kiswahili ni Yesu. Kupitia ushawishi huu wamara kwa mara baadhi ya Wakristo wameshawishika kuamini kuwa Isa ndiye Yesu. Lakini, lazima tuzichunguze hizi hoja moja kwa moja ili tujue ukweli.

          4. TUFANYE UCHUNGUZI PAMOJA
 
1. Je, Mama wa Isa ndiye yule wa Yesu Kristo?

VIOJA VYA UISLAM KUHUSU KIFO NA KUFUFUKA WAKATI WA KIYAMA

1. Eti Binadamu asili yake ni MBEGU YA "Ajabu Dhanab"
2. Eti Siku ya Kiyama Allah atanyeshea Mvua Ajab Dhanad na itafufuka tena.

Ndugu Msomaji, ebu jiunge nami leo na jifunze kuhusu Sayansi dhaif ya Allah na Muhammad.


MTU ANAPOKUFA, ZILE ASILI TATU KILA MOJA INARUDI MAHALA PAKE PA ASILI
Kwa kifo, udongo ambao kwao ndio mwili ulijengeka, unarudi mahala pake pa asili napo ni ardhini.
Mwenyezi Mungu anasema:
"Kwa hakika tunajua kiasi cha kila kinachopunguzwa na ardhi katika miili yao (wakati wanapooza huko makaburini) Na kwetu kiko kitabu kinachohifadhi (kila kitu)".
Qaf -4

AJABU DHANAB- ETI BINADAMU NDIO KATOKEA HAPO
Kinachobaki katika mwili wa mwanadamu ni kitu kidogo kinachoitwa "Ajabu dhanab" (kilichoingia pamoja na mbegu). Hii ni sehemu ambayo ndani yake mtu aliumbiwa, na kitu hiki asili yake kilikuwa katika uti wa mgongo wa Baba yetu Adamu(AS), kwa vile kitu hiki ni kidogo sana (Hakiwezi kuonekana ila kwa kutumia microscope zenye nguvu sana), ndiyo maana uti wa mgongo wa Baba yetu Adamu(AS) uliweza kuzibeba asili hizi zote za wanawe.
Na sehemu hii iitwayo "Ajabu dhanab" haiozi wala haivurugiki.
Mtume(SAW) amesema:-
<<Mwili wote wa mwanaadamu unaoza isipokuwa "Ajabu dhanab", kutokana nayo ameumbwa na kutokana nayo atakusanywa tena >>.
Bukhari – Muslim – An Nasai, Malik katika Muwata a na Abu Daud.

Ama Roho itarudi mahali anapopataka Mwenyezi Mungu (katika Barzakh) mpaka Siku ya Kiama.

SIKU YA KUFUFULIWA ZILE SEHEMU TATU ZINAKUSANYIKA TENA
Unapofika wakati wa kufufuliwa, Mwenyezi Mungu atateremsha mvua na kuifanya ile mbegu isiyooza "AJABU DHANAB”, imee tena.

Mtume (SAW) amesema:-
<<Kisha inateremshwa mvua na watamea kama imeavyo mboga, na hapana katika mwili wa mwanadamu kisicholiwa na ardhi isipokuwa fupa moja nalo ni "Ajabu dhanab" ndani yake humo watakusanywa viumbe Siku ya Kiama>>.
(Bukhari, Muslim, Imam Malik, Abu Daud na AnNasaiy)

Yaliyofanana na haya yanatokea duniani kila siku. Panapotokea ukame, tunaona miti ikianguka na kufa (na kutoweka). Hauonekani mti wowote wala mmea. Lakini Mwenyezi Mungu amejaalia ndani ya ardhi au ndani ya mawe kuwemo mbegu, na mbegu hizo hazionekani kwa macho, isipokuwa mvua inaponyesha ndipo hupasuka na kuchipua miti na mimea mbali mbali.

Mwenyezi Mungu anasema:-
"Hukitoa kilicho hai katika kilichokufa na hukitoa kilicho kufa katika kilicho hai na huihuisha ardhi baada ya kufa kwake na hivyo ndivyo mtakavyofufuliwa".
(Al - Rum - 19).
Mtu mmoja alimuuliza Mtume (SAW):-
"Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, namna gani MwenyeziMungu atawarudisha tena viumbe, na nini dalili yake?” 

 Mtume (SAW) akamjibu;
"Uliwahi kupita bondeni kijijini kwenu wakati wa ukame (miti yote ikiwa imekufa), kisha ukapita tena wakati miti (imeota tena na) imejaa na ardhi ikageuka (na kuwa) rangi ya kijani?
Akasema:- "Naam".
Mtume(SAW) akamjibu:
"Basi hiyo ndiyo dalili ya Mwenyezi Mungu katika kuumba kwake na hivyo ndivyo atakavyowafufuwa wafu".
(Imam Ahmad )

(Siku ya Kiama), Pale Ajab dhanab itakapochipua na kutoka ndani ya ardhi na mwili ukarudi tena, ndipo zitakapokuja roho na kuingia kila moja katika mwili wake.
Ndio sababu Mwenyezi Mungu akasema:
"Na nafsi zitakapounganishwa (na viwiliwili vyake)."
(At - Takwiyr - 7)
Na hivi ndivyo watakavyorudi viumbe mara ya pili kama walivyoanzishwa hapo mwanzo.

Mwenyezi Mungu anasema:-
"Kama tulivyoanza umbo la awali tutalirudisha tena, ni ahadi ilio juu yetu, bila shaka sisi ni wenye kufanya (tusemavyo).”
(Al - Anbiyaa -104).

Ndugu msomaji, hivi ni kweli Allah wa hii dini ya Kiislam aliumba? Mbona hii imani imejaa shaka na utata kila kona?

Leo Allah kesha jisahau na kusema kuwa eti wewe umetoka katika Ajabu Dhanab na sio tena vumbi.

UHAKIKA WA UFUFUO WA WAFU KWA WAKRISTO

Wednesday, July 29, 2015

YESU YUPO NA ANAKUJUA HATA JINA LAKO

Yesu ni wa kweli, anajua jina lako na kila kitu kinacho kuhusu, pia anakupenda. Hayuko mbali nawe, yuko karibu nawe, anataka ujue kuwa yupo, anaishi, na anataka kukusaidia ikiwa utapenda. Na kama utapenda kumfahamu, unaweza kumfahamu. Ikiwa utahitaji msaada, atakusaidia, kama utaongea nae atakusilikiza, naye ataongea nawe pia.

Yesu ndiye aliyekufanya usome maandishi haya, kwa sababu ametuambia tukuandikie, na amehakikisha kuwa yamekufikia. Anajua kila kitu kinachokuhusu tangu mwanzo wa maisha yako hadi sasa hivi, amejumuika nawe katika huzuni, madhaifu na hata matatizo yako, atakusaidia mara tu utakapo muhitaji. Hakutaka uwe peke yako, mara nyingi ametaka umjue yeye. Ndiyo maana amekufanya kuwa rafiki kwa makusudi hayo. Mwamini yesu, kwani kwa Yesu urafiki ni mzuri tena wa kweli, isitoshe ni wa upendo ule wa ndani. Hatokuacha kamwe, unachotakiwa kufanya ni kumwamini na uongee nae yeye Yesu, naye atakujibu, atakusaidia, na ndipo utakapomfahamu Yesu. Anakutazama sasa unaposoma maandishi haya na amejaa upendo juu yako.

Imeandikwa kuwa, Yesu alikuja duniani, akafa, akatoa uhai wake kwa ajili yetu. Hii inaonyesha kuwa kifo kilikuwa ni cha lazima, ili kulipa deni la dhambi zetu. Kwa nini alichagua kulipa deni la dhambi kwa njia ya kifo? Ni kwa sababu anakupenda sana!

KAFARA: BABA KAMA MTOTO
Hakuna mtu mwingine katika historia ya dunia hii bali Yesu tu. Hakuwa mdhambi, dhambi ilikuwa kwa wengine. Dhambi zote zinakuja zenyewe kwa namna moja ama nyingine alionekana mnyenyekevu. Baba wa mbinguni alituumba ili tupendane sisi kwa sisi, na pia tumpemde yeye, lakini dhambi imekuwa kinyume na upendo huo na imechukua nafasi kubwa katika maisha yetu, hata kusababisha kifo. Hata hivyo, kifo ndio kimekuwa malipo makuu ya dhambi. Dhambi inatembea kutoka kwa mtu mmoja. Kwenda kwa mwingine, nchi moja kwenda nyingine, na inaleta maumivu kwa kila mtu, na ndiyo maana inawatenganisha wanadamu wote na Mungu, na inawapeleka kuzimu. Mungu hatokubali dhambi iingie Mbinguni, na mbingu ziwe kama dunia ilivyo hivi sasa, imejaa maovu na kujiona zaidi. Kwa miaka mingi Mungu aliruhusu wanyama wafe. Kwa njia hiyo wanadamu walikuwa na mahusiano ya karibu zaidi na Mungu wao mpendwa na waliongea nae. Aliwapenda na kuongea nao pia, kwa mfano, Abrahamu, Ayubu, Adamu na wengine wengi. Mungu anataka uhusiano huo leo kwako, lakini hutaki kujitolea kafara wanyama ili kuwa nae.

HEKIMA ZA MWANADAMU
Mwanadamu amejaribu kuwa na ukaribu na Mungu kwa kupitia njia mbali mbali, lakini si kwa njia ile ambayo Mungu alitegemea kutoka kwao. Kaini mtoto wa Adamu alitoa kafara ya mazao yake badala ya mnyama. Hata hivyo, Mungu hakupokea kafara ya Kaini kwa sababu haikuwa na thamani sawa na dhambi iliyokuwa ndani yake. Haijarishi Kaini alikuwa na mawazo mazuri au mabaya juu ya Mungu, bali kafar yake haikuwa na thamani ya kulipa deni la dhambi.

Ukweli ni kwamba watu bado hawajajua dhambi. Kwetu dhambi imekuwa ni neno la kidini. Wengi hawajajua kwa nini jambo lifanyike kwa ajili ya dhambi. Lakini Mungu ameona ni jinsi imekuwa ya kuume na ya kipekee tena yenye nguvu. Na jinsi ambavyo inaleta shida na masumbufu ndani yetu. Huko mbinguni kama siyo dhambi, tungeweza kuonana na Yesu uso kwa uso, tungekuwa huru kutoka dhambini na kuwa huru wenye nguvu zaidi na zaidi, pia tungekuwa mahali ambapo kila mtu awaye binadamu, au
malaika, au kiroho, angependa kuwepo. Wote tungependana na Mungu angeishi maisha ya upendo kwa wengine na siyo ya kibinafsi.

HEKIMA ZA MUNGU

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW