Sunday, August 28, 2016

Je, Kanisa ni Kiti cha Enzi cha Shetani?




Biblia inasema: “Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani…” (Ufunuo 2:13)


Waislamu “WAHUBIRI WA BIBLIA”, kama kawaida ya “injili” yao potofu hawaachi kuzipotosha njia za Bwana zilizonyooka; lakini kama hawataki kutubu, hukumu yao inakimbia mbio kuwajilia. Wahubiri hawa hutumia andiko hilo hapo juu kuonyesha eti Kanisani ni mahali akaapo shetani, wakimaanisha kuwa Wakristo wote tunapoenda kuabudu Kanisa, basi tunakuwa kwa shetani!

Lakini andiko hili maana yake ni nini?


Maneno haya yamo kwenye ujumbe wa Bwana Yesu kwa Kanisa la Pergamo. Kwa kuwa Bwana Yesu anatoa ujumbe kwa Makanisa kadhaa, hebu tuanzie nyuma kidogo ili tuweze kuona MUKTADHA wa matumizi ya maneno haya kwa usahihi. Siku zote nasisitiza umuhimu wa kuangalia maandiko katika MUKTADHA wake kwa kuwa bila kufanya hivyo, utadanganywa, utadanganywa tu na watumishi wa shetani na roho yako itaangamia milele!!

Mstari wa nane wa sura ya pili ya Ufunuo unasema:
“Na kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa, kisha akawa hai.” (Ufunuo 2:8).


Bwana analiambia Kanisa hili:  “Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.”  (Ufunuo 2:9).

Haihitaji ufahamu wowote mkubwa kutambua kuwa hapa kuna pande mbili – tena zinazopingana. Kuna upande wa Kanisa la Smirna linalomwamini Yesu Kristo; na kuna upande unaopingana vikali na Kanisa hilo, yaani upande wa Sinagogi la Shetani.

Urithi wa Uislamu kutoka kwenye dini za kipagani za Uarabuni – Sehemu ya 2




Ka’aba

Katika sehemu ya 1 ya makala haya tuliangalia kuhusu asili ya Allah. Katika sehemu hii ya 2 tutaongelea kuhusiana na mji wa Makka na ka'aba, ambayo ni madhabahu kuu ya Uislamu.

Mji wa Makka ndio kitovu cha Uislamu duniani. Kwenye mji huu ndiko iliko Ka’aba, au kama wanavyoamini na kuiita Waislamu Bait – ul- Haram; au Bait – ul- Allah, yaani ‘nyumba ya Allah’ au ‘nyumba ya Mungu’. Na kila Mwislamu kokote duniani anatakiwa kuswali swala 5 kila siku huku akielekeza uso wake Makka iliko hiyo nyumba ya Mungu wao. Vilevile, kila mmoja wao anatakiwa kwenda Makka kuhiji walau mara moja katika maisha yake, maana hija ni moja ya nguzo kuu katika Uislamu. Kwa maana nyingine, Ka’aba ndiyo madhabahu kuu katika Uislamu.



Ka’aba ni nyumba ya umbo la takriban mchemraba ambayo, pamoja na vitu vingine vichache iliyo navyo, kuna kipande cheusi cha jiwe ambacho kimejengewa ukutani kwenye kona mojawapo. Hivyo, Waislamu wanapoenda Makka kuhiji huzunguka Ka’aba na pia kulibusu  jiwe hilo, au kuligusa tu, na kama ikishindi kana, basi japo kulinyoshea mkono.


Zamani, Allah anasema, kuwa Muhammad alikuwa akitazama mbinguni wakati anapoomba [nadhani kila mwenye imani juu ya Mungu anaamini kuwa Mungu yuko juu – na huo kusema kweli nadhani ndio mtazamo sahihi kabisa].
Lakini Allah akamwambia mtume wake:
We have certainly seen the turning of your face, [O Muhammad], toward the heaven, and We will surely turn you to a qiblah with which you will be pleased. So turn your face toward al-Masjid al-Haram. And wherever you [believers] are, turn your faces toward it [in prayer]. Indeed, those who have been given the Scripture well know that it is the truth from their Lord. And Allah is not unaware of what they do. (sura Al Baqarah 2:144) – Sahih International Version.
Yaani:
Hakika tumeona jinsi unavyogeuzia uso wako [ewe Muhammad], kuelekea mbinguni, nasi hakika tutakugeuzia kwenye qiblah utakachokifurahia. Hivyo elekeza uso wako kwenye al-Masjid al-Haram. Na kila mtakakokuwa [enyi mnaoamini] geuzieni nyuso zenu kuelekea huko [mswalipo]. Hakika, wale waliopewa Maandiko wanajua vema kuwa ni kweli kutoka kwa Bwana wao. Na Allah anajua kile wafanyacho.
Allah anasema hafurahii sana Muhammad na Waislamu kugeuzia nyuso zao juu mbinguni (aliko Mungu muumba wa vyote – ajabu sana! Ajabu mno!), badala yake akaamuru wageuzie nyuso zao kwenye ka’aba wawapo popote wakati wa kuswali.
Pia anasema kuwa wale waliopewa Maandiko (yaani watu wa kitabu) eti wanajua fika kwamba jambo hilo ni kweli kutoka kwa Bwana wao!
We Allah wewe! Bwana wao yupi tena wakati wewe unasema ndiwe uliyesema na Ibrahimu ili akajenge ka’aba akitokea Kaanani – kilometa zaidi ya 1,000 kutoka Makka? [Tena basi Makka ambayo hata haikuwapo duniani hadi takriban kwenye miaka 400 baada ya Kristo - sasa sijui Ibrahimu alienda kujenga ka'aba porini kusiko hata na mtu mmoja]!! Ina maana kuna Bwana wao ambaye si wewe basi! Basi huyoBwana wao ana Ibrahimu na Ishmael wa kwake; na wewe una Ibrahimu na Ishmael wa kwako, au siyo? 
Kulingana na Quran, ka’aba ilijengwa na Ibrahimu na mwanawe, Ishmael. Quran inasema kwamba:

Remember We made the House a place of assembly for men and a place of safety; and take ye the station of Abraham as a place of prayer; and We covenanted with Abraham and Isma'il, that they should sanctify My House for those who compass it round, or use it as a retreat, or bow, or prostrate themselves (therein in prayer). [Qur'an 2:125].

Yaani:
Kumbukeni, tuliifanya Nyumba ile mahali pa kukusanyikia kwa ajili ya wanadamu na mahali pa usalama; hivyo chukueni ninyi mahali pa Ibrahimu kama mahali pa swala; nasi tulifanya agano na Ibrahimu na Ishmael, kwamba waitakase Nyumba Yangu kwa ajili ya wale wanaoizunguka, au kuitumia kama mahali pa makimbilio, au kuinama, au kusujudu humo (kwa swala).

[Allah anasema kuwa aliifanya nyumba hii kwa ajili ya wanadamu, lakini waislamu hawaruhusu asiye mwislamu, na hasa aliye Mkristo, kwenda kwenye ka’aba; au hata kupita juu kwa ndege!! Inawezekana Allah anaposema ‘mwanadamu’ ana maana ya ‘mwislamu’!]

Kuhusiana na Ibrahimu, hilo ni jambo ambalo tunawaachia Waislamu wenyewe maana sisi wengine tunaamini na hata ushahidi wa kihistoria na kimaandiko unaonyesha wazi kwamba Ibrahimu hajawahi kamwe kukanyaga mguu wake Uarabuni.

Kwa mfano, ufuatao ni ushahidi mmojawapo juu ya jambo hili. Tunasoma kwamba:

Narrated Abu Dhaar: I said, "O Allah's Apostle! Which mosque was built first?" He replied, "Al-Masjid-ul-Haram." I asked, "Which (was built) next?" He replied, "Al-Masjid-ul-Aqs-a." I asked, "What was the period in between them?” He replied, “Forty years.” (Sahih Bukhari 4:55:636).

Yaani:
Imesimuliwa na Abu Dhaar: Nilisema, “Ewe Mtume wa Allah! Ni msikiti upi ulikuwa wa kwanza kujengwa?” Akajibu, "Al-Masjid-ul-Haram."  Nikauliza, “Ni upi ulifuata?” Akajibu, “Al-Masjid-ul-Aqs-a.” Nikauliza, “Ulipita muda gani hapo katikati?” Akajibu, “Miaka arobaini.”

Muhammad naye ana mambo! Al-Masjid ul-Aqs-a  ndiko hapo penye Ka’aba. Na Al-Masjid-ul-Haram ni hekalu la Mfalme Sulemani kule Uyahudi.

Sasa, hekalu la Yerusalemu lilijengwa na mfalme Sulemani kwenye takriban miaka ya 950 kabla ya Kristo (KK). Hii ni kusema kwamba, kama maneno ya Muhammad ni ya kweli – na ninaamini kwamba hakuna mwislamu ambaye anaweza kukiri kuwa Muhammad ni mwongo – basi, msikiti wa kwenye Ka’aba unatakiwa uwe ilijengwa kwenye 990 KK (ukiongeza hiyo tofauti ya miaka 40).

Hilo sio tatizo. Lakini shida inakuja unapomwingiza Ibrahimu. Ibrahimu aliishi takriban miaka 2000 kabla ya Kristo. Tazamahapa. Hii ni kusema, aliishi miaka takriban 1050 kabla ya kujengwa kwa hekalu la mfalme Sulemani. Sasa, kama Ibrahimu wa Muhammad aliyejenga Ka’aba aliijenga miaka 40 kabla ya hekalu la Sulemani, basi NI LAZIMA awe ni Ibrahimu mwingine na Ishmael mwingine tofauti kabisa na wale wa kwenye Biblia. Vyovyote iwavyo, hilo ni tatizo la Waislamu wenyewe kulitatua. Ni kazi kwao kujiridhisha na kujithibitishia wao wenyewe kwamba, kama wanataka imani yao itokane na Ibrahimu aliyeongea na Mungu wa Israeli, basi hali ndiyo hiyo!

Kutokana na ukweli huo hapo juu, tunabakia na uwezekano wa aina mbili: kwanza, kama Muhammad yuko sahihi juu ya hiyo miaka 40, basi Allah ndiye aliyekosea au aliongopa kusema kuwa Ibrahimu alijenga Ka’aba.  Kama Allah yuko sahihi, basi Muhammad ndiye aliyekosea au kuongopa kwamba Ka’aba ilijengwa miaka 40 kabla ya hekalu la Sulemani. [Hata hivyo, kuna uwezekano kabisa huyu ni Ibrahimu mwingine kabisa. Hebu tutafakari yafuatayo: 

Hata kama ka’aba ilijengwa na Ibrahimu (wa Biblia au mwingine tofauti), jambo moja ni dhahiri; kwamba wakati Muhammad anatokea na kuanzisha dini yake, ka’aba ilikuwa chini ya wapagani wa Uarabuni huku ndani na nje yake kukiwa na miungu zaidi ya mia tatu.

Ni mwaka 630 baada ya Kristo (BK), ndipo Muhammad na wafuasi wake walitwaa mamlaka ya mji wa Makka na kuifanya ka’aba kuwa sehemu ya kuabudia Mungu mmoja badala ya miungu zaidi ya mia tatu. [lakini usisahau kwenye sehemu ya 1 ya makala haya tulibainisha kwamba allah alikuwa ni mungu wa kipagani tangu maelfu ya miaka nyuma kabla ya kutokea kwa Muhammad. Na unajiuliza; hivi asili ya ‘allah akbar’, yaani ‘allah ni mkuu’ ni nini? Je, si kwa sababu kulikuwa na mamia ya miungu, na allah akiwamo, ndiyo maana Muhammad akawa, kimsingi, anasema, “Hapana. Hiyo miungu yote si kitu. Allah ndiye anayewazidi wote”? Huo ndio muktadha sahihi wa kutamka maneno kama hayo, au siyo? Hilo ni wazo tu ambalo linahitaji utafiti wako wewe unayemwamini Allah; maana mimi wala siamini kwamba Allah ndiye Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.]

Basi turudi kwenye suala la kuwapo kwa mamia ya miungu kwenye ka’aba wakati Muhammad anaingia. Hivi ndivyo tunavyosoma:

Narrated 'Abdullah bin Masud: The Prophet entered Mecca and (at that time) there were three hundred-and-sixty idols around the Ka’aba. He started stabbing the idols with a stick he had in his hand and reciting: "Truth (Islam) has come and Falsehood (disbelief) has vanished." [Sahih Bukhari 3:43:658].

Yaani:
Imesimuliwa na Abdullah bin Masud: Mtume aliingia Makka na (wakati ule) kulikuwa na miungu mia tatu na sitini kuzunguka Ka’aba. Alianza kuichomachoma kwa fimbo aliyokuwa nayo mkononi huku akisema: “Kweli (Uislamu) imeshakuja na Uongo (kutokuamini) kumetoweka.”

Ndugu zangu waislamu, ka’aba wala haina uhusiano na Mungu Mkuu aliyeumba mbingu na nchi. Ilikuwa ni madhabahu tu ya kipagani kwa ajili ya kuabudia mwezi, jua na nyota.

Hivi ndivyo tunavyoambiwa:
Narrated Abu Huraira: “In the year prior to the last Hajj of the Prophet when Allahs Apostle made Abu Bakr the leader of the pilgrims, the latter (Abu Bakr) sent me in the company of a group of people to make a public announcement: 'No pagan is allowed to perform Hajj after this year, and no naked person is allowed to perform Tawaf of the Ka’aba.'” (Bukhari V2, B26, #689 (V1, B8, No 365).

Yaani:
Imesimuliwa na Abu Huraira: “Kwenye mwaka kabla ya Hija ya mwisho ya Mtume pale Mtume wa Allah alipomfanya Abu Bakr kuwa kiongozi wa mahujaji, Abu Bakr alinituma pamoja na kundi la watu wengine ili kutoa tangazo: ‘Hakuna mpagani anayeruhusiwa kufanya Hija baada ya mwaka huu, na hakuna mtu aliye uchi anayeruhusiwa kufanya Tawaf ya Ka’aba.

Sijui ndugu msomaji kama unaiona maana ya maneno haya? Hiki ndicho tunachosoma humu:

1.  Waislamu na wapagani walikuwa wakifanya hija pamoja kwenye ka’aba kwa miaka mingi hadi hapo Abu Bakr alipofanywa kiongozi.
2.  Wakati wawapo kwenye hija, wapagani walikuwa wakifanya Tawaf (kuzunguka ka’aba) wakiwa uchi.
3.  Wapagani walikuwa wakiabudu miungu yao ya kipagani kwenye ka’aba na waislamu wakimwabudu Allah.

Ili uone uzito wa jambo hili vizuri, hebu piga picha ya Hekalu la Sulemani alilojenga Yerusalemu kwa ajili ya Yehova. Yaani humo ndani ya hekalu wawe wanasali Wayahudi wanaomwamini Yehova na pia wapagani wanaoabudu jua, na mwezi na nyota; tena wakiwa uchi!!!!!!!

Kwa kuwa jambo hilo haliingii kamwe akilini; na haliwezekani, jibu ni moja tu: ni Muhammad ndiye aliyeenda kuingilia madhabahu ya wapagani na si kinyume chake!

Na ndiyo maana Muhammad alikuwa na ujasiri wa kutaka kuibomoa ka’aba. Hivi ndivyo tunavyosoma:

Narrated Aswad: Ibn Az-Zubair said to me, "Aisha used to tell you secretly a number of things. What did she tell you about the Ka'ba?" I replied, "She told me that once the Prophet said, 'O 'Aisha! Had not your people been still close to the pre-Islamic period of ignorance (infidelity)! I would have dismantled the Ka'ba and would have made two doors in it; one for entrance and the other for exit." (Sahih Bukhari 1:3:128).

Yaani:
Imesimuliwa na Aswad: Ibn Az-Zubaid aliniambia, “Aisha alikuwa akikusimulia kwa siri mambo kadha wa kadha. Je, alikuambia nini kuhusiana na ka’aba? Nikajibu, “Aliniambia kwamba, kuna wakati Mtume alisema, ‘Ewe Aisha! Kama watu wa kwenu wangekuwa bado hawako karibu na enzi ya ujinga ya kabla ya Uislamu (ukafiri), ningebomoa Ka’aba na ningejenga milango miwili; mmoja wa kuingilia na mwingine wa kutokea.’”

Hebu piga picha hapa pia; kwamba Musa aliambiwa na Yehova atengeneze hema ya kukutania. Akapewa maelekezo kwa undani sana ya namna kila kitu kinavyotakiwa kuwa, na akaambiwa afanye sawasawa na alivyoonyeshwa na Yehova. Halafu anakuja kutokea mtume au nabii miaka mia kadhaa inayofuata anasema, “Mimi naona katika nyumba hii Yehova alikosea kuweka mlango mmoja. Inatakiwa milango miwili hapa.” Hivi inawezekana kweli?

Sasa, kama kweli ni Allah ndiye alimwambia Ibrahimu na Ishmael wajenge ka’aba, inaingia kweli akilini Muhammad kuja kusema angeweza kuibomoa na kuijengea milango miwili?? Mwanadamu anaweza kumsahihisha Mungu?

Lakini hilo linawezekana tu kama nyumba yenyewe haina uhusiano wowote na Mungu; kama ambavyo ka’aba haina kamwe uhusiano wowote na Mungu wa mbinguni.

Duniani leo kuna makanisa na mahekalu mengi, lakini tunapoongelea hema ya kukutania ya Musa au hekalu la mfalme Sulemani, tunakuwa tunaongelea mahali pa pekee sana ambako Mungu mwenyewe kibinafsi ndiye aliyetoa vipimo na kuchagua mahali pa kujenga. Vivyo hivyo, kuna misikiti mingi duniani, lakini unapoongelea msikiti wa kwenye ka’aba, basi ni allah mwenyewe (anayedaiwa kuwa ni Mungu wa Ibrahimu) kujihusisha moja kwa moja na kazi hiyo. Sasa, hebu pia tazama picha hii hapa chini, kisha ujiulize mwenyewe kama Mungu wa mbinguni anaweza kuagiza nyumba yake ijengwe kwenye eneo lenye sifa hizi: 


Nimekwambia hapo mwanzo kwamba kwenye ka’aba kuna jiwe jeusi (wanaloliita Al-hajar Al-aswad) ambalo waislamu hulibusu au kuligusa kama sehemu ya ibada yao humo. Lakini tunaambiwa hivi kuhusiana na jiwe hilo:

Later, Umar said to the black stone, "I know that you are a stone, that neither helps nor hurts, and if the messenger of god had not kissed you, I would not kiss you." (Sahih Bukhari, volume 2, #667).  

Yaani:
Baadaye, Umar aliliambia lile jiwe jeusi, “Najua kuwa wewe ni jiwe ambalo haumsaidii wala kumdhuru mtu, na kama mjumbe wa mungu asingekubusu wewe, kamwe nisingekubusu.”  

Jiwe hilo ni linaloonekana kwa mbele kama doa jeusi
Hiyo ndiyo hali ya Uislamu na waislamu hadi leo. Karibu kila kitu kwenye uislamu kiko kinyume na hali halisi ya maisha; hata mioyo yao inakataa kuvikubali, lakini wafanye nini sasa na wao wameshajiungamanisha na Muhammad? Anachosema Umar, kimsingi, ni kuwa, “Moyoni najisikia kabisa kwamba hii habari ya kubusu jiwe ni ubatili mtupu, lakini sina namna ya kuacha maana mtume amelibusu.”

Naamini Waislamu wengi wanafikiri kuwa ka’aba iliyopo leo ndiyo hiyohiyo ambayo Allah amewaambia kuwa ilijengwa na Ibrahimu na Ishmael. Lakini ukweli ni kwamba, ka’aba ilishavunjwa na kujengwa zaidi ya mara kumi. Tazama hapa. Kwa hiyo, hii iliyopo leo ni ujenzi wa hivi karibuni tu wa serikali ya Saudia.

Hitimisho
Ni kweli kabisa ka’aba ni nyumba ya Allah, lakini KAMWE si nyumba ya Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Wala Ibrahimu wa Israeli hajawahi kwenda Uarabuni kujenga ka’aba. Hii ilikuwa ni madhabahu ya mungu mwezi, jua, nyota na miungu zaidi ya 360 iliyoabudiwa na wapagani wa Uarabuni. Ukweli ni kwamba hii wala haikuwa ka’aba pekee. Zilikuwapo ka’aba nyingi ambamo wapagani wa huko walikuwa wakiabudia miungu yao. Umeona mwenyewe jinsi ambavyo wapagani hao walikuwa wakienda kuhiji Makka kwenye ka’aba tena wakiwa uchi. Iweje leo useme kuwa mambo yaleyale; palepale kuwa ni mambo ya kumwabudu Mungu aliyeumba mbingu na nchi?

Ndiyo maana Yehova aliwaonya Waisraeli akisema: Basi zishikeni amri zangu zote, na hukumu zangu zote, na kuzifanya, .... Nanyi msiende kwa kuziandama desturi za taifa niitoayo mbele yenu; kwa kuwa wao waliyafanya mambo hayo yote, na kwa ajili ya hayo niliwachukia. (Walawi 20: 22-23). Lakini ajabu ni kwamba Allah anasema kinyume kabisa. Kimsingi, anachosema kwa Waislamu ni kwamba: "Enendeni kwa kuzifuata kawaida za watu waliokuwa wanaishi Makka"!!!

Je, Mungu wa mbinguni anahitaji nyumba hapa duniani ili aweze kuishi humo? Hivi kwa ukuu wake wote, Mungu huyu atakaa kwenye kachumba ambacho ndani yake hakuna hata kitu?

Yesu Kristo anakuita akupe uzima wa milele sasa. Muda unakimbia mbio!

Katika ulimwengu wa leo kupata taarifa si tatizo. Tunayo maktaba kubwa kuliko zote tangu kuumbwa kwa ulimwengu yenye kila taarifa uitakayo duniani - yaani Intaneti. Ni wewe tu kujua unataka nini.

Hoji mambo.

Chunguza.

Fanya utafiti.

Chukua hatua.

Friday, August 26, 2016

Je, Nafsi tatu zaweza kuwa Mungu mmoja?

Hili ni swali nyeti sana na huenda ndilo msingi wa sababu hasa za baadhi ya watu katika ulimwengu wa dini kupinga fundisho hili la kweli la Kibiblia juu ya Utatu Mtakatifu na Uuungu wa Bwana Yesu. Hoja kubwa katika sehemu hii inaonekana kuwa ni ya kimahesabu zaidi ambapo jamii ya wale wanaopinga utatu mtakatifu hudai kuwa haiwezekeni Baba, Mwana na Roho mtakatifu yaani mamlaka tatu kuwa Mungu mmoja. Yaani hiyo ni sawa na kusema 1 + 1 + 1 = 3 na siyo 1’ kwa hiyo Baba + Mwana + Roho Mtakatifu = Miungu watatu. 

Kwa mtazamo huu ninalazimika katika sehemu hii kushughulika na dhana ya kimahesabu zaidi ili kuona kama madai hayo ni sahihi na kama yanaweza kupatiwa ufumbuzi wa kifarsafa katika maandiko. Katika kulipatia swala hili ufumbuzi ni vyema tukaongozwa na mtazamo wa kimaandiko kupitia fungu la kitabu cha ISaya… 

Isaya 55:8 Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana Hiyo ni tahadhari ya msingi sana katika kushughulika na mada hii, Mungu mwenyewe katika kitabu hicho cha Isaya anaweka bayana kuwa katika utendaji wake njia anazozitumia hutofautiana sana na njia zetu za kibinadamu na hata mawazo yetu yako tofauti na mawazo yake. Ukweli wa tamko hilo la Isaya tunaweza kushuhudia katika kipengele hiki cha uchambuzi ambapo kama utakumbuka hoja ya msingi ya upinzani juu ya Utatu mtakatifu imejengwa katika kile kinachoonekena kuwa nafsi tatu haziwezi kuwa Mungu mmoja kwa kuwa moja jumlisha moja jumlisha moja jumlisha moja ni sawa na tatu (1+1+1 = 3). 

‘Hebu tuichunguze hesabu hiyo (Nafsi tatu - Mungu Mmoja) katika maandiko’ Baba Mwana/Neno Roho Mtakatifu Mungu mmoja Elohim’ Mafundisho na mifano mbalimbali ya kimaandiko katika Biblia vinaweka bayana juu ya usahihi wa fundisho hili la kweli na la msingi katika Ulimwengu wa imani ambapo kama hatua ya juu zaidi ya uwazi wa fundisho hili maandiko ya Biblia yanaweka bayana usahihi wa jibu la Mungu mmoja toka katika hesabu ya nafsi tatu za Mungu . Fuatilia mifano na uchambuzi huu:

- Umoja katika wingi ‘A’ 
Ushahidi wa kwanza wa msingi juu ya Mungu mmoja katika nafsi tatu ni ule unaotoka katika kimya cha Mungu mwenyewe kama tunavyosoma katika andiko la kitabu cha Mwanzo;- Mwanzo 1:26-27 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 

ETI BIBLIA INATAJA MASHEHE KWAHIYO INAUNGA MKONO UISLAM, THUBUTU

Wahubiri wa ‘injili potofu’ wa Kiislamu wanaendelea kuhaha kuhalalisha Quran kupitia Biblia. Nasema ‘kuhaha’ kwa sababu hakika kabisa wana juhudi kubwa mno lakini inasikitisha kwa sababu hakuna hata siku moja waliyowahi kusema jambo lenye ukweli kibiblia linalounga mkono quran kama wasemavyo wao – Mungu ni shahidi yangu. Mara waseme Muhammad ametabiriwa kwenye Biblia; mara waseme Yesu aliposema kuwa ataletwa Msaidizi basi alimaanisha Muhammad, n.k. Ni kituko kimoja baada ya kingine. Na wanayemdanganya ni wao wenyewe pamoja na Wakristo wachache wasiojua Biblia.
Kwa msingi huohuo, wanasema eti Biblia imewataja Mashehe; na kwa hiyo kwao huo ni ushahidi kuwa uislamu ulikuwapo tangu zamani.
Acha ninukuu hoja ya mmoja wao kama ilivyo, kuhusiana na suala hili, kisha kama kawaida, utaona jinsi hoja hiyo inavyosambaratika mbele za nuru ya Kristo, yaani neno lake.
Mtu huyu anasema:
"Swali kwenu nyinyi ambao hamjabahatika kuwa waislam, yaani Wakristo. Kama uislam uliletwa na muhammad s.a.w, vipi masheikh watajwe ndani ya agano la kale?
“Ndivyo walivyosimama mikutano miwili yao walioshukuru nyumbani mwa mungu, na mimi, na nusu ya mashehe pamoja nami.” (Nehemia 12:40)
Mkristo jiulize mwenyewe hili swali; mashehe ni viongozi wa dini ipi? waislam...!? au wakristo?"
Mwisho wa kunukuu.
Hapa huyu ndugu wa Kiislamu anaongea kwa ujasiri kabisa na kwa kituo. Na unaona kabisa kuwa moyoni mwake anawaza, “Hapa leo nimewapata Wakristo. Lazima waone kuwa Uislamu ndiyo dini ya kweli.”
Na hivi ndivyo ilivyo kwa hoja zao ZOTE kuhusiana na Ukristo. NI UONGO; NI UONGO; NI UONGO!! NI UPOTOVU MTUPU!!

QURAN SIO MANENO YA ALLAH WALA MWENYEZI MUNGU



Ndugu msomaji,
Huu ni MSIBA mkubwa sana kwa Waislam wote duniani. Waislam wamekuwa na tabia ya kusema kuwa, eti Quran yote ni maneno ya Allah. Unapo wauliza, huyo Allah aliwezaje ongea na Muhammad, wanabakia kimya na kuanza kukutukana. Zaidi ya hapo, leo nitawawekea ushahid tosha kuwa Quran sio maneno ya Allah.
Haya ungana nani kwa ushahidi:
SHETANI ANASEMA KWENYE QURAN
Surah Al Hijr 39. Shetani akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
Kwenye Surat Al Hijr, tumesoma kuwa Shetani ndie anazungumza katika hiyo aya ya 39. Kumbe basi, Shetani ni msemaji ndani ya Qurani.
HAPA TUNASOMA KUWA ZAKARIA NA YEYE NI MZUNGUMZAJI KATIKA QURAN
Surat Maryam: Zakaria Akasema: Mola wangu Mlezi! Mafupa yangu yamedhoofika, na kichwa kinameremeta kwa mvi; wala, Mola wangu Mlezi, sikuwa mwenye bahati mbaya kwa kukuomba Wewe.
Waislam, hivi Quran ni maneno ya nani?
Endelea kupata darasa hapa:
MARYAM NA YEYE NI MSEMAJI KATIKA QURAN
Surat Maryam aya 18: Maryamu akasema: Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe, ukiwa ni mchamngu.
Waislam, mbona na Maryam anasema kwenye Quran? Au siku hizi Maryam amekuwa Allah? Huu ni Msiba mkubwa sana kwa Waislam.
MALAIKA NAO WANASEMA KWENYE QURAN
Surat Maryam aya 21: Malaika akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu, na Rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo lilio kwisha hukumiwa.
Ndugu msomaji, kwanini Waislam wanapenda kusema uongo namna hii, eti Quran yote ni Maneno ya Allah? Mbona tunasoma viumbe wengine wakisema ndani ya Quran?
ISSA BIN MARYAM NA YEYE ANASEMA KWENYE QURAN
Surat Maryam aya 36: Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
Issa na yeye alisema kwenye Quran. Lakini Muhammad yeye hakuwai sema chochote kile kwenye Quruani wala kuzaliwa kwake hakukutajwa kwenye Quran. Huu ni Msiba mkubwa sana kwa WAISLAM.
SWALI LANGU KWA WAISLAM NI DOGO SANA:
1. NI NANI MSEMAJI KATIKA QURAN?
2. QURANI NI MANENO YA NANI?
Mkiweza nijibu kwa aya na bila shari, leo hii nitasilimu na kuwa Muislam.
Waislam huwa wanasema kama huamni kuwa Quran ni maneno ya Mungu, basi teremsha aya kama za Quran, huku tukifahamu kuwa kuna aya nyingi ambazo wasemaji wake ni wengine na sio Allah.
Sasa, huu utata tunawaachia waislam waje hapa kutujibu bila ya kuweweseka.
QURAN NI MANENO YA NANI?
Karibu sana kwa Yesu aliye hai ambaye ndie NENO LA UZIMA.
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Max Shimba Ministries Org.

JINA LA ISA BIN MARYAM HALINA NGUVU WALA UWEZO WA KUOKOA AU KUPONYA MAGONJWA

SHALOM TENA,
Kwa mara nyingine twamshukuru Yehova Mungu kwa kutupa neema hii tena ili tuweze kukufikishia ujumbe huu wa Biblia na kweli zake.
Kwa muda wa miaka mingi sana pia duniani pote imekuwa ni kawaida kuwasikia waislamu wakifundisha watu wao na kuwadanganya bila ya wao kujuwa ao wengine wakiwa wanakijuwa wanachokifanya kuwa ISA bin Maryam’ Kama Qurani inavyofundisha ndiye “YESU KRISTO”.
Mafundisho haya hivi sasa yanaendeshwa kwa kulinganisha aya za Biblia na Qurani. Ma sheihk, ma Imam na wahubiri wengi wa dini ya kiislamu wanaendesha mihadhara kwa uwingi duniani. Wahadhiri hao pia hutumia mbinu zingine mbali-mbali kama majarida na kurekodi kanda za audio na video, ambazo zimesababisha baadhi ya wakristo nusu au wakristo wajinga waamini kuwa Isa Bin Maryamu ndiye Yesu Kristo. Swali la msingi kwa wakristo wote;Je, ni kweli Isa bin Maryam ndiye Yesu Kristo?
Katika hadithi Al-Lu’lu’war-Marjani, Juzuu namba 1, Hadithi namba 104 ukurasa 64 “Hadithi ya Ibn Abbas kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema:
“Nilimuona Musa katika usiku wa Al-Isra, niliopelekwa, naye ni mtu mrefu, mwenye nywele za hudhurungi zimejikunjakunja kama mtu wa Shanua. Na nilimuona Isa, naye ni mtu wa wastani wa umbo, unaelekea kwenye wekundu na weupe, ana nywele zilizonyooka……”
Lakini YESU KRISTO: JINA LAKE NI WOKOVU.
Mdo 4:9-10, 12
“kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu, jinsi alivyoponywa, jueni nyinyi nyote na watu wote wa Israel ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye nyinyi mlimsulubisha, na Mungu alimfufua katika wafu kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu…Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”
Baadhi ya aya ndani ya Qur’an zinaeleza kuwa Isa aliwaponya wenye upofu. Ni akina nani hao tutajiwe angalau mmoja? Yesu alimponya vipofu na mmoja wao ni Batromayo.

KWANINI WAISLAM WALITENGENEZA INJILI YA UWONGO YA BARNABAS? (SEHEMU YA PILI)



Mwalimu Chaka
KUHITILAFIANA NA INJILI TAKATIFU
Kuna ushahidi mwingi kwamba Mwandishi wa Injili ya Barnaba alikuwa hana uhusiano wowote na Mitume wa Kristo, au wanafunzi wake ambao waliandika vitabu vyao wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
1.Ushahidi wa kwanza ni kutokufahamu kwa mwandishi JIOGRAFIA ya Palestina ambayo ndiyo nchi na kitovu cha masimulizi ya kidini. Anasema, “Yesu akaenda kando ya ziwa Galilaya na akapanda mashua kusafiri hadi Nazareti, mji wake mwenyewe. Kukawa na dhoruba kubwa na mashua ilikuwa karibu kuzama” (Sura ya 20:1-2). Ni vizuri kujua kwamba Nazareti iko juu ya mlima wa Galilaya, wala sio mji wa pwani, kama mwandishi anavyosema.
2. Mahali pengine anasema, “Kumbuka kwamba Mungu aliamua kuharibu Ninawi kwa sababu hapakuwa na mmoja katika mji huo ambaye alikuwa mcha Mungu. Yeye (Yona) alijaribu kutoroka Tarso, kwa kuwa na hofu ya watu, lakini Mungu akamtupa baharini na samaki akammeza na kumtupa nje karibu Ninawi” (BARNABA Sura 63:4-7). Ni jambo lanalojulikana kwamba mji wa Ninawi ulikuwa mji mkuu wa Dola ya Waashuri na alikuwa umejengwa kando ya ufuo wa mashariki wa Mto Hidekeli, kwenye kijito kinachojulikana kwa jina la al-Khisr. Kwa hiyo, haupo katika eneo la bahari ya Mediterranean kama ilivyoelezwa na mwandishi huyu.
3. Mwandishi alikuwa hana ufahamu juu ya historia ya maisha ya Yesu Kristo. Katika sura ya tatu ya Injili hii ya kughushi, imeandikwa, “Yesu alipozaliwa, Pilato alikuwa Gavana wakati wa uongozi wa Rabi Anania na Kayafa .” ( Sura 3:2).
Hii si kweli kwa sababu Pilato alikuwa liwali kutoka mwaka wa AD 26-36. Anania alikuwa Rabbi mkuu kutoka AD 6, na Kayafa kutoka AD. 8-36.

KWANINI ALLAH ALITEREMSHA SURATUL HIJR AYA 6 NAKUSEMA KUWA NABII WA WAISLAM NI MWENDAWAZIMU?

Ndugu zanguni,
Biblia inasema kuwa, mtawafahamu kwa matunda yao, hayo yalikuwa maneno kutoka Injili ya [Mathayo 7:16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya].
Mtume Muhammad alishindwa kuonyesha uadilifu katika kazi yake. Kazi aliyo dai katumwa na Mungu, ilijaa maswali mengi ambayo yaliwafanya watu wamuite yeye, Muhammad, “Mwendawazimu”. Kitendo cha Mtume kuoa Mtoto wa miaka 6, kulileta kizungumkuti, kwasabau kitendo hicho si cha kibinadamu na hakikufanywa na Mitume walio kuja kabla yake. Hapa chini ni aya kutoka Koran iliyo teremshwa na mungu wa Islam kupitia msaada wa Gibril.
Quran 15: 6. Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu. http://www.quranitukufu.net/015.html
Muhammad anaitwa mwendawazimu mbele ya kadamnasi. Hayo madai ya uwendawazimu hayakukataliwa na mtume wa Allah. Alicho fanya Muhammad ni kukaa kimya, jambo ambalo ni jibu tosha kuwa alikubali kuwa yeye ni Mwendawazimu. Uhakikisho wa uwendawazimu wake upo kimaandishi.
Hebu tusome Simulizi zake kidogo: "Kitab al-Tabaqat al-Kabir", (Kitabu cha Madarasa Meja), na Ibn Sad, kutafsiriwa na S. Moinal Haq, [4], ukurasa wa 225; Muhammad akisema:
O Khadija, Ninaona Mwanga, na nasikia Masautisauti, nina hofu kuwa mimi nina Wazimu.
Kwenye hiyo simulizi yake, hapo juu, Mtume wa Allah anakiri kuwa yeye ni mwendawazimu. Kukiri huko, kunatuletea maswali mengi, ambayo nategemea mengi ya maswali hayo, yatakosa majibu. Lakini ni vyema tujiulize maswali. Kwanini Allah aliteremsha aya inayo muita Mtume wake Mwendawazimu? Kwanini Muhammad hakukataa kuitwa Mwendawazimu? Utume wa huyu Muhammad umejaa shaka, pale alipo kubali kuwa yeye ni mwendawazimu. Rejea kwenye simulizi yake hapo juu. Nita nukuu sehemu fupi ya kukubali kwake “O Khadija, …….nina hofu kuwa mimi nina Wazimu”.
Hatujawai soma kwenye vitabu vingine vitakatifu kuwa Mitume wa Mungu wa Biblia walikubali kuwa wao ni Wendawazimu, lakini leo hii tumejifunza kuwa Muhammad mtume Allah, anakubali kuwa yeye ni Mwendawazimu.
Hivi, kwanini tufuate mtume aliye kubali kuwa yeye ni Mwendawazimu? Hilo ni swali la msingi. Allah anasema kuwa watu wa Kitabu ambao ni Wayahudi na Wakristo ndio wenye elimu na muwaulize wao, mtakapo kuwa na maswali.
Allah amesha jibu. Wakristo ndio wenye majibu katika hii duni.
MUHAM-MAD ANASEMA: "Nina hofu kuwa mimi nina Wazimu"
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

USHUHUDA WA MUISLAMU ALIYEOKOKA ALIKUWA NA MAJINI YA CHUMA ULETE SASA NI MWINJILISTI, COSMAS JUMA HAMIS



Mimi Mwinjilisti Cosmas Juma Hamis nimezaliwa mwaka 1975 Wilaya ya Urambo Mkoani Tabora nikiwa ni mtoto wa kwanza wa mama Mwamini Said Ntembela na Baba Shekh Juma Hamis Mdaki, Baba akiwa msumbwa na mkazi wa Wilaya mpya ya Kaliua na Mama mwenyeji wa tarafa ya Usoke wilaya Urambo akiwa ni wa kabila la watusi wazawa wa mkoa Tabora. Mwaka 1985 nikiwa na umri wa miaka 10 nilianza elimu ya msingi katika shule ya msingi mapinduzi iliyoko tarafa ya Usoke wilaya ya Urambo mkoa wa Tabora pamoja na kuanza elimu ya msingi pia nilijiunga na shule ya kiislamu (yaani nilijiunga na shule ya kiislamu (madrasat) kusoma elimu ya kiislamu na hii ilitokana na Baba yangu na Mama yangu kuwa ni waislamu hivyo nilipelekwa katika madrtasa hiyo ili nisome uislam ambao ndio dini ya wazazi wangu na ndugu zangu wote.
Nikiwa ni mzaliwa wa kwanza kati ya watoto 12 katika tumbo la mama yangu Mwamini Said Ntembela ambapo mimi kwa Baba tumezaliwa watoto 2 mimi na dada yangu Johari Juma Hamis na mimi nikiitwa wakati ule kwa jina la Hamisi Juma Mdaki mama yangu aliachana na Baba yangu shekh Juma Hamisi Mdaki tukiwa tumezaliwa watoto wawili na baada ya kuachana Mama na Baba ambapo ilikuwa mwaka 1979 mimi nikiwa na umri wa miaka minne na dada yangu akiwa na miaka miwili tukaenda kuishi kwao na Mama ambapo ni tarafa ya Usoke wilaya ya Urambo kwani hapo mwanzo tulikuwa tukiishi mwanza na kaliua baada ya kuishi pale usoke mama yangu aliolewa nma mume mwingine ambae anaitwa Shabani bakari amri moja. Waliishi na mume huyo ambapo kisheria alikuwa mume halali kutokana na mafundisho ya dini ya kiislamu kwa kuwa alishapewa taraka, hivyo waliendelea kuzaa watoto ambapo jumla walifika watoto kumi na hivyo kufanya idadi ya watoto wa Mama huyo kufikia 12 na mimi nikiwa mkubwa wa wote.

KWANINI JINA LA ALLAH HALINA UWEZO WA KUPONYA MAGONJWA?

KWANINI HAKUNA NGUVU YA UPONYAJI KATIKA UISLAM? MBONA KATIKA UKRISTO WATU WANAPONA KWA JINA LA YESU?
1. KWANINI JINA LA ALLAH HALINA UWEZO WA KUPONYA MAGONJWA?
2. ALLAH ASHINDWA KUMPONYA MUHAMMAD
3. MAOMBI YA JIBRIL YAGONGA MWAMBA
4. LAKINI JINA LA YESU LINAPONYA MAGONJWA YOTE
5. JE, UMESHA WAI ONA KUNA MKUTANO WA UPONYAJI KATIKA USILAM?
Ndugu msomaji,
Uponyaji ni nini?
Ni tendo la kiimani la kupokea uzima katika roho au mwili kwa njia ya kuombewa,kuwekewa mikono au kulisikia neno sahihi la Kristo Yesu. Tendo hili la kiimani humletea mwamini uzima wa kiroho na afya ya kimwili pale ilipopunguka,kumbuka~wengi walipoponywa udhaifu wa miili yao,waliponywa pia na roho zao.
Hivyobasi, kwanini Allah alipo mtuma Jibril kwenda kumuombea uponyaji Mtume wake Muhammad kwa ugonjwa uliosababishwa na kula sumu, maombi yao hayakufanya kazi?
Hivyo basi, uponyaji haufanywi na mtu awaye yoyote yule isipokuwa Mungu. Hata madaktari bingwa wao hawaponyi bali hutoa tiba tu, mwenye kuponya ni Mungu. Watumishi wa Mungu pekee ndio hufanyika kama daraja au chombo cha kuleta uponyaji ulioachiliwa na Bwana kwa muhusika mwenye kuhitaji.
HEBU SASA TUMSOME ALLAH NA JIBRIL KATIKA JARIBIO LAO LA KUMPONYA MUHAMMAD:
Ibn Sa'd Ukurasa wa 265
Aisha, Mke wa Mtume Muhammad alikuwa akisema, "Wakati Nabii wa Allah alipo kuwa anaumwa, Jibril alikuwa anamwombea Muhammad kwa Allah kwa kusema haya "Katika Jina la Allah ambalo litakuponya kutoka kila magonjwa na maumivu na kutoka kila wenye ubaya nawe na kila wanakuombea ubaya, utapona..
Je, jina la Allah liliweza kumponya Muhammad? Hebu tusome Sahih hadith kama ilivyo letwa na Al Bukhari:

ALLAH ATEREMSHA AYA NA KUKIRI KUWA MUHAMMAD ALIKUWA HAJUI KUSOMA WALA KUANDIKA


HUU NI MSIBA MKUBWA SANA
Je, kuna uhashihidi wowote ule wa aya kusaidia madai ya kuto kujua kusoma kwa Muhammad katika Quran?
Wanadhuoni wa Kiislam, hupenda kusema kuwa, Nabii wa Allah wao, aitwaye Muhammad alikuwa ameelimika, lakini unapo wauliza maswali na kuomba ushahidi wa madai yao, huwa wanaanza kukutishia na kusema kuwa, Muhammad ndie nabii wa mwisho, na kukwepa swali, la msingi. Je, Muhammad alikuwa anajua kusoma na kuandika?
Hebu tuanze moja kwa moja na aya ambazo ziliteremshwa na Allah kwa kupitia msaidizi wake Malaika Jibril kama Quran inavyo dai.
Ushahidi wa Kwanza:
Koran Surat Al A'raaf [7:157]
Ambao kwamba wanamfuata huyo Mtume, Nabii Muhammad, asiye soma wala kuandika,
Ndugu wasomaji, aya tuliyo isoma katika Surat Al A'raaf 157 inatuambia kuwa Nabii pekee wa Allah, Muhammad, alikuwa ngumbaru; hakufahamu kusoma wala kuandika.
Najua waislam, wataanza kubisha na kutupa maneno ya hapa na pale. Ili kuwanyamazisha tusoma ushihidi mwingine kutoka Quran yao.
Ushahidi wa Pili:
Surah Al A'nkabut [29: 48]. Na wewe hukuwa kabla yake unasoma kitabu chochote, wala hukukiandika kwa mkono wako wa kulia. Ingeli kuwa hivyo wangeli fanya shaka wavunjifu.
Allah kaamua kuteremsha aya nyingine ili kutuhakikishia umaah wake kuwa, Nabii wake, Marehemu Muhammad, alikuwa hajui kusoma wala kuandika jina lake.
Je, kuna Mitume wowote wale katika Biblia ambao walikuwa hawajui kusoma wala kuandika?
Kufuatana na ushaihidi wa Biblia, Mitume wote na Manabii wote wa Biblia walikuwa wanafahamu kusoma na kuandika. Na wengine kama Luka, wao walikuwa Madaktari.
Hakika Muhammad alikuwa Mtume Bandia ndio maana hakuwai ongea na Mungu, kinyume na Manabii wote ambao waliongea na Mungua aliye watuma.
Zaidi ya hapo, Mungu muumba wa mbingu na nchi ambaye ndie mwanzilishi wa elimu, hakuwa na sababu ya kumtuma Mtume ambaye alikuwa Ngumbaru.
Kumbe basi, ndio maana Quran yao imejaa shaka na inatumia usaidizi wa Hadith.
Waislam, karibuni kwa Yesu aliye hai, ili muweze kupata uzima wa milele.
Max Shimba Ministries Org.

UPO WAPI UTHIBITISHO WA AYA KUWA MUHAMMAD ALITAIRIWA?

KUMBE MTUME MUHAMMAD HAKUTAIRIWA.
Ndugu msomaji,
KATIKA sehemu nyingi za ulimwengu, watoto wa kiume wanatahiriwa kwa sababu za kiafya. Watu fulani katika nyakati za zamani, kama vile Wamisri, walitahiriwa, yaani, walikatwa magovi ya kiungo chao cha kiume.
Yesu alitahiriwa. Kwa mujibu wa Agano la Kale, mapokeo haya yalianzia na Mtume Ibrahimu, Katika Mwanzo 17:10-13, imeandikwa, “Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa. Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na nyinyi. Mtoto wa siku nane atatahiriwa kwenu, kila mwanamume katika vizazi vyenu, mzaliwa nyumbani, na mnunuliwa kwa fedha, kila mgeni asiyekuwa wa uzao wako. Mzaliwa nyumbani mwako, na mnunuliwa na fedha yako, lazima atahiriwe; na agano langu litakuwa katika mwili wenu, kuwa agano la milele.
Katika Injili kwa mujibu wa Luka 2:21: “Hata zilipotimia siku nane za kumtahiri, aliitwa jina lake Yesu; kama alivyoitwa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.” Kwa hiyo, kutahiriwa ilikuwa ni sehemu ya njia ya Yesu.
LAKINI NILIPO ISOMA QURAN NA KUSOMA VITABU VINGINE VYA KIISLAM KAMA SAHIH AL BUKHARI, NIKAGUNDUA KUWA, NABII WA ALLAH AITWAYE MUHAMMAD YEYE HAKUTAIRIWA NA HAKUNA UTHIBITISHO WA KIMAANDIKO AU HISTORIA KUWA MUHAMMAD ALITAIRIWA.
Waislam bila ya jazba wala kutokwa mapovu. Naomba mnijibu swali langu:
Kwanini mnafuata Muhammad nabii wa Allah ambaye hakutairiwa?
Kumbuka kutuna hakufai na ni ishara kuwa wewe umejambiwa mdomoni na Shetani:
Abu Huraira (r.a) amesimulia kuwa: Mtume (s.a.w) amesema, "Ye yote mwenye kutukana, basi huyo amejambiwa na Shetani katika Mdomo wake." (Fat'hul Baary J. 10, Uk. 176)
NATANGULIZA POLE KWA WAISLAM KWA KUMFUATA MUHAMMAD AMBAYE HAKUTAIRIWA.

POSA SABA (7) ZA MUHAMMAD ZILIZO KATALIWA

1. Kwanini baadhi ya wanawake walikataa posa za Muhammad?
2. Kwanini muhammad aliendelea kuomba/toa posa na huku zikikataliwa?
Ndugu msomaji,
Leo nitakua ushahid kadhaa kuonyesha jinsi Muhammad alivyo penda wanawake lakini wengine walikataa posa zake na kuto jali utume wake alio pewa na Mkewe.
Muhammad alimwomba amuoe Ghaziyyah kwa sababu ya uzuri wake, lakini alikataliwa. Tabari anadai kuwa [Ghaziyyah] hakuwa mwaminifu lakini hatoi ushahidi. al-Tabari juzuu ya 9 uk.136. Hakuna ushahidi kuwa [Ghaziyyah] hakuwa mwaminifu na kwamba Muhammad hakuwa makini kwa kutokumwadhibu, au kwamba hakuwa mwaminifu na Muhammad alimwadhibu.
Layla aligusa bega la Muhammad tokea nyuma na kumuomba amuoe. Muhammad alikubali. Ndugu za Layla walisema, "Ni jambo baya kiasi gani ulilolifanya! Wewe u mwanamke anayejiheshimu, lakini Nabii ni mpenda wanawake. Tafuta kujitengua toka kwake." Layla alikwenda kwa Nabii na kumuomba aikane ndoa hiyo na aliafikianana na hilo [ombi]." al-Tabari juzuu ya 9 uk.139.
Kutoka al-Tabari juzuu ya 9 uk.140-141, Muhammad alimposa lakini aliishia kutokumuoa:
1) Umm Hani’ bin Abi Talib [Hind] kwa sababu alikuwa na mtoto.
2) Duba’ah binti ‘Amir lakini alikuwa mzee sana.
3) Inaripotiwa kuwa alimposa Saffiyah binti Bashshamah, mateka. Alitakiwa achague mmoja kati ya Muhammad na mume wake, na alimchagua mume wake.
4) Umm Habib bint al-‘Abbas lakini kwa kuwa al-‘Abbas alikuwa kaka wa kulelewa pamoja naye kwa hiyo isingeruhusiwa kisheria kwa hiyo Muhammad aliamua kujiondoa.
5) Jamrah binti Al-Harith. Baba yake alida isivyo sahihi kuwa alikuwa anasumbuliwa na kitu Fulani. Aliporudi, alikuta ameisha kumbwa na ukoma.
Haielezwi kwa kauri moja endapo Umm Hani’ alikuwa muislam kabla au baada ya Muhammad kumwomba amuoe. al-Tabari juzuu ya 39 uk.197 na rejeo chini ya ukurasa 857 uk.197.
Ndugu msomaji ambaye ni mfuasi wa dini ya Uislam, je, unaweza tumabia kwanini posa 7 za Muhammad zilikataliwa?
Max Shimba Ministries Org

MUHAMMAD ALIFANYA MAZINGAOMBWE NA KUPIGA RAMLI



1. Mtume Muhammad alitumia Ndumba
2. Mtume Muhammad adai eti Nywele zake zinatibu jicho ovu.
3. Wapi katika Biblia tunasoma kuwa Manabii na Mitume wa Biblia walitumia Ndumba?
Ndugu Msomaji,
Leo ningependa tusome kuhusu Muhammad na Utumiaji wa NDUMBA katika Uislam,
MTUME MUHAMMAD ANATUMIA NDUMBA
Muhammad alitumia ndumba [nguvu za kimazingaombwe] dhidi ya jicho ovu na wanyama jamii ya mjusi wenye sumu Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3525 uk.48.
Hivi wapi tunasoma katika Taurat au Zaburi au Injir kuwa Mitume na Manabii wa kwenye Biblia walitumia NDUMBA?
Hivi Allah hana uwezo wa kutibu jicho ovu au Sumu mpaka atumie NDUMBA?
MUHAMMAD SASA AMPA MKE WAKE AISHA NDUMBA
Muhammad alimpa ‘Aisha ndumba ili kutibu jicho ovu. Sahih Muslim juzuu ya 3 kitabu cha 24 na. 5445,5447-5450 uk.1196.
Hivi Ndumba ina tofauti gani na UCHAWI? Sasa hapo juu tumesoma kuwa Muhammad ametoa NDUMBA kwa mke wake kipenzi.
Wapi tunasoma kuwa Manabii wa Biblia walitumia NDUMBA?
Muhammad aliamini katika jicho ovu, na kulikuwa na hirizi dhidi yake al-Tabari juzuu ya 39 uk.134.
Sura mbili za mwisho (113 and 114) ziliandika juu ya ubaya wa jicho ovu kufuatana na Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3517 uk.41.
Hata hivyo, sura za 113 na 114 hazimo katika toleo la Ibin Mas’ud katika Korani (The Fihrist uk.57). Kuondolewa huko hakukuwa kwa bahati mbaya. Ilitaarifiwa kuwa Ibn Mas’ud alisema, "Hirizi mbili-Sura za [113, 114] si Kitabu cha Mungu."
Ibn Mas’ud alikuwa katibu muhtasi wa Muhammad. Muhammad aliwaambia watu wengine wajifunze kutoka kwa Ibn Mas’ud na wengine watatu. (Bukhari juzuu ys 6 kitabu cha 60 sehemu ya 8 na.521 uk.486-487).

JE, UNAFAHAMU KWANINI AISHA MKE WA MUHAMMAD ALIZINI NA SAFWAN IBN AL MUATTAL?



ZAIDI YA HAPO, KWANINI AISHA ALIKATAA KUZAA WATOTO NA MUHAMMAD?
Utasikia Waislam wakijgamba, Aisha ni mama wa waaminio, ikimaanisha ni Mama wa Waislam.
Swahaba wa Muhammad Amr bin Al-Aas alimuuliza Nabii wa Allah (PBUH): O, Nabii wa Allah, ni Mke yupi unampenda zaidi kuliko wake zako wat? Nabii Muhammad akamjibu "Aisha"
Kama tulivyo soma hapo juu, Muhammad alimpenda Aisha zaidi ya wake zake wote.
LAKINI:
AISHA MWANA WA ABU BAKAR ALIFUMANIWA AKIFANYA NGONO NA SAFWAN BIN AL MUATTAL:
Imesimuliwa na Ibn Hisham, na kusimuliwa na Ibn Ishaq, kuwa Aisha alifumaniwa akifanya ZINAA "ngono" na Safwan Ibn Al Muattal, mmoja wa Maswahiba wa Muhammad "Safwan incident". Haya mambo yalifanyika huko Madina na habarii ilitapakaa Madina yote na kumfanya Nabii wa Allah amrudishe Aisha kwa Wazazi wake.
Ali ambaye alikuwa binamu yake wa karibu na Mume wa binti yake Fatimah, alimsihi Muhammad ampe takala Aisha ili kuficha hii aibu kubwa ya fumanizi la KUZINI.
Hii ni siri kubwa sana kwa Waislam na hawataki ifahamike kuwa Aisha alifanya ZINAA na Safwan Ibn Al Muattal na kumfanya Muhammad amrudishe Aisha kwa Wazazi wake.
KAMA AISHA ALIPENDWA SANA NA MUHAMMAD KULIKO WAKE ZAKE WOTE, KWANINI AISHA ALIAMUA KUZINI NA SAFWAN BIN AL MUATTAL?
Huu ni msiba Mkubwa sana kwa Muhammad na Waislam.
LABDA NDIO MAANA AISHA ALIKATAA KUZAA NA MUHAMMAD AU LABDA NI KWASABABU YA TABIA MBAYA YA MUHAMMAD YA KUZINI NA WATUMWA WAKE WA KIKE. http://www.islam-watch.org/…/Muhammad-Juwairiya-Aisha-Adult…
Waislamu wa Madina wakiongozwa na Abdulla bin Ubai, walitangaza kuwa Bibi Aisha (RAAH) amezini na Safwan. Mtume (SAW) aliposikia haya aliwaita maswahaba zake na kushauriana nao nini la kufanya, kuna waliotowa ushauri amuache. Mtume (SAW) alimzuru na akamwambia: “Ukiwa huna makosa basi Mwenyenzi Mungu atakusamehe, la kama sihivyo basi omba maghufira kwa Mola wako.” Aisha alilia na kuomba msamaha kwa wazazi wake kwa kosa la uzinifu alilo fanya na Safwan, lakini wazazi wake hakuwa na la kusema.
References:
1) Ibn Sa’ad, Al Tabakat Al Kubra, vol.8 (Arabic)
2) Ibn Hisham, sira al nabaweyya(Arabic)
3) Dr. Sami Alrabaa, Karen in Saudi Arabia
4) Sahih al Bukhari, chapter of washing, Narrated by Anas. (Arabic)
5) Al Lulu wa Al Marjan fima ittaffaqa alihi al shaikhan: Muslim and Bukhari, hadith No.168; 173 (Arabic)
Maswali ya kujiuliza ni haya, Kwanini AISHA ALIKATAA KUZAAA NA MUHAMMAD NABII WA ALLAH. HUKU IKIFAHAMIKA KUWA, MUHAMMAD ALIMPENDA SANA TENA SANA AISHA?
Natanguliza pole zangu kwa Waislam wote. Hakika hii dini imejaa vituko na viroja kedekede.

KWANINI MUHAMMAD ALITAKA KUJINYONGA “COMMIT SUICIDE”?



1. MUHAMMAD ALITAKATA KUJINYONGA
2. MUHAMMAD ALIPANDA MLIMANI NA KUJARIBU KUJIRUSHA ILI AFE
3. AISHA ASEMA MUHAMMAD ALIKUWA AMEROGWA
Ndugu msomaji,
Tunaposoma Biblia tunajifunza kuwa Mungu aliwapa Unabii na Utume watu wake kwa njia ya upendo. Lakini nilipo soma vitabu vya Allah nilikutana na mambo ya ajabu sana.
Bila ya kupoteza muda, ngoja niweke vitabu vyake ili na wewe ujisomee mwenyewe. Maana Waislam huwa wanadai eti nawasingizia au namzulia uongo Allah.
KATIKA SAHIHI BUKHARIY TUNASOMA KUWA MUHAMMAD ALIJARIBU KUJINYONGA KWA SABABU YA HUZUNI KWENYE NYOYO YAKE:
Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: Wao watanifukuza? Riwaya inaendelea kwa yanayoshangaza zaidi kuliko hayo Waraqa bin Naufal alipomkuta MTUME AKIJARIBU KUJINYONGA KWASABABU YA HUZUNI yake kwa kukatika Wahyi, kama si Jibril kumtuliza mara hii baada ya kuwa Waraqa bin Naufal akifanya hivyo. Sahihi Bukhariy J:9 uk 93 kita Ta’abiyri
Swali la kujiuliza hapa ni hili: Hivi wapi tunasoma kwenye Taurat au Zaburi au Injili kuwa Mitume wa kwenye Biblia walijaribu kujinyonga kama Muhammad wa kwenye Quran?
Nilipo endelea kusoma vitabu vya Waislam nikagundua kuwa, hilo tukio la kujaribu kujinyonga “commit suicide” halikufanywa mara moja na Muhammad ambaye ni Nabii kipenzi cha Allah.
MUHAMMAD ALIPANDA MLIMANI NA KUJARIBU KUJITUPA ILI AFE, JE HII TABIA YA KUTAKA KUJIUA NI YA KINABII? Soma hiki kisa hapa chini:
Kisha Waraqa hakuchukua muda akafariki na Wahyi ukakatika kwa muda na Nabii (s.a.w.w.) akahuzunika, ambapo katika yaliyo tufikia mara nyingi huzuni ilipelekea kutaka kujirusha kutoka katika vilele vya milima, lakini kila alipopanda mlima ili ajiangushe Jibril alimtokea na akamwambia Ewe Muhammad “Hakika wewe ni Mtume wa kweli wa Mwenyezi Mungu, basi kwa hayo inapoa hasira yake na nafsi yake inatulia na anarudi na unaporefuka muda wa kutopata Wahyi anarudia hayo, na anapofika kwenye kilele cha mlima Jibril anamtokea na kumwambia mfano wa aliyomwambia. J: 8 uk 234 kitabu Daawaati

KWANINI WAISLAM WALITENGENEZA INJILI YA UWONGO YA BARNABAS? (SEHEMU YA TATU)

Mwalimu Chaka
Leo napenda tuangalie baadhi ya mafundisho na upindaji wa maandiko ya Mungu kama tunaona katika Injili hii ya Barnaba.
Utabiri wa Ujio wa Muhammad katika Injili ya Barnaba.
Katika Biblia tunasoma jinsi Yohana Mbatizaji alitangaza ujio wa Bwana Yesu:
"Sasa huu ulikuwa ni ushahidi wa Yohana, Wayahudi wa Yerusalemu walipowatuma makuhani Walawi, na kumwuliza yeye ni nani. naye alikiri, wala hakukana, alikiri kwamba "Mimi siye Kristo." Nao wakamwuliza, " Ni nani basi? U Eliya wewe?" Akasema, "Mimi siye." "Je, wewe u Nabii yule? "Yeye akawajibu, "La" Basi wakamwambia, "Wewe u nani? ili tuwapelekee jibu wale waliotutuma?, Wanenaje juu ya nafsi yako?" Yohana alijibu kwa maneno ya nabii Isaya, "Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Nyoosheni njia ya Bwana.’”
"... siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, "Tazama Mwana-kondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu!" (Yohana 1:19-29)
Katika Injili ya Barnaba tunaona kisa hiki kimebadilishwa na kumfanya Yesu kutabiri kuja kwa Muhammad, kama Qur'an inasema Isa alifanya (Qur'an 7:157, 61:6).
"Waliona wengi ambao walikuwa wanafuata Yesu, kwa ajili hiyo wakuu wa makuhani wakafanya shauri wao kwa wao ili wamtege Yesu kwa maneno yake. Kwa hiyo wao waliwatuwama Walawi, na baadhi ya walimu wa Sheria kumwuliza, wakisema: "Wewe ni nani" Yesu alikiri, alisema ukweli: ". Mimi sio Masihi" Wakasema: "Je, wewe ni Eliya au Yeremia, au mmojawapo wa manabii wa kale?" Yesu akajibu: "Hapana" Nao wakamwambia, "Wewe ni nani Sema, ili tupate kutoa ushuhuda kwa wale waliotutuma?." Kisha Yesu akasema: "Mimi ni sauti ya mtu apitaye kwa njia yote za Yudea, kwa kilio akisema: “Tayarisheni njia ya Mjumbe wa Bwana, kama ilivyoandikwa katika Isaya." (Sura. 42)
"Ndipo kuhani: akamuuliza "Ataitwaje Masihi atakapokuja ... " Yesu akamjibu, "jina la Masihi ni la kupendeza ... Muhammad, ndilo jina lake lenye kheri" (Surah. 97).
Hapa mwandishi wa Injili ya Barnaba anadai Masihi atakeyekuja ni la kupendeza, yaani Muhammad jina lenye kheri" !!! eti Muhammad ndiye Masihi!!!! ili tutalichambua mbeleni
JE YESU NI MWANA WA MUNGU ?

ALLAH HANA UWEZO WA KUSAMEHE DHAMBI WAISLAM WALIO KUFA

Je, Allah anao uwezo wa Kusamehe watu dhambi?
Ndugu zanguni,
Leo ningependa tumuangalie Allah wa dini ya Uislam ambaye wanasema ndie Mungu wao. Je, huyu Allah anayo mamlaka ya kusamehe dhambi zote?
Quran inaendelea kusema kuwa wale walio kuwa katika Umauti kamwe Allah hana uwezo wa kuwasamehe dhambi, ingawa WAISLAM bado wana utamaduni wa kuombea Maiti msamaha ili Allah aipokee roho ya marehemu.
Suratul Muuminum 101. Basi litapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana. ***102. Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa. ***103. Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu. ***104. Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana. ***105. Je! Hazikuwa Aya zangu mkisomewa, na nyinyi mkizikanusha? ***106. Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea. ***107. Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu. 108. Atasema Mwenyezi Mungu: Tokomeeni humo, wala msinisemeze. 109. Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu. ***110. Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka. ***111. Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu. 112. Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka? 113. Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu. ***114. Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua. ***115. Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa? ***
Katika hii suratul Muuminum tunasoma kuwa hawa ni Waislam walio zidiwa na dhanb, Allah atawakana na hato wasamehe ingawa ndugu zao waliwafanyia maombi wakati wa umauti na kuwasafisha ngama. Allah yeye anasema hato wasamehe hawa Waislam. Ushaidi mwingine unaweza upata hapa S. 35:36-37, S. 40:10-12 , S. 43:74-77, S. 67:6-11, S. 4:93
ALLAH HASAMEI MUISLAM ANAPO UA MUISLAM MWENZAKE: MFANO KAMA ULE WA SUNNI WANAPO UANA NA SHIA.

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW