Monday, September 18, 2017

Salafist cleric says fathers can marry off their newborn daughters



Last week, Egyptian Salafist preacher Muftah Mohammad Maarouf, also known as "Abu Yahya," stated that it's absolutely okay for a newborn girl to be married off by her father - even at such a young age. 
Yes, you heard that right. 
The statement was made during a live TV interview on a show that was discussing a controversial draft law aimed at lowering marital age in Egypt to 16. 
According to the preacher, if no harm will be done to a female, then nothing should prevent her from getting married, regardless of her age. 
"I am not the one saying this, in Islamic Sharia there is no set age for marriage when it comes to females," Maarouf said. 
When the show's presenter pressed on with: "If this is true, then any age would be fine for marriage, 2 months, 1 year," the preacher shockingly responded: 
"Even if she's just 1-day-old." 

People on social media were just not having it

A video of the interview that saw "Abu Yahya" drop his statement went viral on social media shortly after the show aired, sparking outrage. 
Here's a little of what people had to say: 

Many were understandably outraged

"Our religion is clear and straightforward... even a child would denounce such statements... these kinds of 'preachers' only represent themselves and have nothing to do with true Islam." 

"Regression, ignorance and stupidity"

Many raised this point

"He's a liar. Prophet Mohammad said that the consent of a female and her guardian are two conditions that any union must be based on. How will an infant or a young girl consent to a marriage when she doesn't even understand what it means?" 

Some were left speechless

"There are no more words to be said."  

"These fatwas from so called religious figures are defaming Islam"

Others felt that action must be taken against this type of "preaching"

"I am wondering, aren't there laws to punish such germs (preachers)? One that could prevent them from using media outlets to spread their agendas, one that would stop them from preaching in mosques?" 

Lowering marital age for females still up for debate in Egypt

While Abu Yahya's statements are shocking, they're not quite surprising given that the preacher previously voiced out his support for a draft law aimed at lowering marital age for females in Egypt from the current 18 to 16. 
Proposed by Egyptian Ahmed Samih, an independent MP representing the Giza district of Al-Talbiya, the controversial draft law has sparked controversy and debate across the country in recent months. 
Since it was proposed, Samih's legislation has faced intense backlash from fellow MPs, women's rights activists and several others who have labeled it 'regressive.' 
Egypt's government has yet to vote on the draft law, but with a number of MPs who have already taken a stand against it, it seems unlikely for it to pass. 

Sunday, September 10, 2017

JE, UNAYO NEEMA YA YESU KRISTO, MUNGU MKUU?

Image may contain: food
Nini basi maana ya neema? Watu wengi wamekuwa wakiimba ,”Neema, neema imefunuliwa” na kukariri na kuisema Neema ya Bwana (2 WAKORINTHO 13:14) kama Kasuku huku hawajui wayasemayo. Nini basi maana ya neema?
Neema, ni upendeleo wa kuchaguliwa, bila kustahili kutokana na matendo yoyote aliyoyafanya mtu au sifa aliyonayo mtu.
Neema pia, ni uwezo wa kushinda katika tabia na utumishi wa Mungu sawasawa na mapenzi yake, tunaopewa na Mungu bila gharama yoyote au nguvuzetu au kufanyia kazi yoyote.
1. Upendeleo wa kuchaguliwa bila kustahili- Kutokana na matendo yake, hakuna mwanadamu yeyote mwenye haki mbele za Mungu (WARUMI 3:20). Tangu kabisa amekuwa akimhuzunisha Mungu (MWANZO 6:5-7). Wakati wa Nuhu, watu waliangamizwa kwa Gharika. Wakati wa Musa, Mungu alitaka pia kufuta kabisa kizazi cha Wausraeli na kubaki na Musa tu kama siyo maombi ya Musa (HESABU 14:11-20). Wakati wote, wanadamu wote wamepotoka na kuoza (WARUMI 3:12). Ni Yesu peke yake tu ambaye siku zote alifanya yanayompendeza Mungu (YOHANA8:29).Alijaribiwa sawasawa na sisi lakini hakutenda dhambi (WAEBRANIA 4:14-15). Yesu huyu anayempendeza Mungu ndiye aliyekufa msalabani na Baraba aliyekuwa mhalifu mkubwa akafunguliwa. Kama Baraba alivyofunguliwa pamoja na ukosaji wake, kila mwanadamu amefunguliwa, akiamini tu. Mbele za Mungu kila mtu amepimwa na kuonekana amepungua (DANIELI 5:27). Sasa kwa kuamini tu kwamba Yesu alizichukua dhambi zetu pale msalabani, sisi tunaokolewa. Watu wengi hawaokolewi kwa sababu hawajui tunaokolewa kwa neema tu kwa njia ya imani peke yake (WAEFESO 2:5). Kazi aliyoifanya Yesu msalabani imetupa kuirithi mbingu aliyokwenda bila sisi kuifanya. Ni kama ambavyo bondia anavyopigana ulingoni kwa shida kubwa na kasha akishinda na kupewa mamilioni ya fedha, mke wake aliyebaki nyumbani bila kupigana naye atakuwa milionea. Hii ndiyo neema.
2. Uwezo wa kushinda bila kutumia nguvu zetu- Neema ni uwezo wa kushinda dhambi na kumtumikia Mungu apendavyo. Neema ndiyo inayotufundisha (inayotuwezesha) kukataa ubaya na tama za kidunia na kuishi kwa kiasi na haki na utakatifu (TITO 2:11-12; WAGALATIA 2:8). Maisha ya wokovu siyo ya kutumia nguvu zetu au kujitahidi. Uweza wa Mungu unatimilika kwetu katika udhaifu wetu yaani kutokuweza kwetu. Hatupaswi kujitumainia wenyewe katika kufanya lolote (2 WAKORINTHO 1:8-9).
Shalom,
Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

UNAYAJUA MADHARA YA KUANGALIA PICHA ZA UTUPU "PONOGRAFIA"? (SEHEMU YA SABA)


Madhara ya Kiroho unapo angalia ponografia:
Ponografia husababisha madhara mabaya ya kiroho. Inaweza kuwa kizuizi kikubwa kwa mtu anayetaka kuwa na uhusiano na Mungu.

Biblia huhusianisha hamu ya ngono na tamaa na ibada ya sanamu. (Wakolosai 3:5) Mtu anayetamani kitu huwa na hamu kubwa sana ya kukipata hivi kwamba kinakuwa jambo kuu maishani mwake kuliko vitu vingine vyote. Kwa kweli, wale ambao wamezoea ponografia hutanguliza tamaa zao za ngono badala ya Mungu. Kwa hiyo wanazifanya kuwa sanamu yao. Amri ya Mungu inasema: “Usiwe na miungu mingine ila mimi.”—Kutoka 20:3.
Ponografia huharibu mahusiano yenye upendo. Mtume Petro, ambaye alikuwa amefunga ndoa, aliwahimiza waume Wakristo wawaheshimu wake zao. Mungu hatasikiliza sala za mume anayekosa kufanya hivyo. (1 Petro 3:7) Je, mtu anayetazama picha chafu za wanawake faraghani anamheshimu mke wake? Mke angehisije akigundua? Na Mungu ambaye “ataleta hukumuni kila kazi” na ambaye “huzipima roho” angeonaje? (Mhubiri 12:14; Mithali 16:2) Je, mtu anayetazama ponografia anaweza kumtarajia Mungu asikilize sala zake?
Ponografia hukazia kutosheleza tamaa za mtu binafsi kwa vyovyote vile. Kwa hiyo, kutazama ponografia ni kukosa upendo. Hudhoofisha uwezo wa Mkristo wa kudumu akiwa safi kiadili na kuwa mwadilifu mbele za Mungu. “Haya ndiyo mapenzi ya Mungu,” akaandika mtume Paulo, “kwamba mjiepushe na uasherati; kwamba kila mmoja wenu apaswe kujua jinsi ya kupata umiliki wa chombo chake mwenyewe katika utakaso na heshima, si katika hamu yenye tamaa ya ngono . . . , kwamba yeyote asifikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake.”—1 Wathesalonike 4:3-7.
Ponografia huwatumia vibaya hasa wanawake na watoto. Huwavunjia heshima na pia huwashushia hadhi na kuwanyima haki zao. Yule anayetazama ponografia hushiriki na kuunga mkono matumizi hayo mabaya ya wanawake na watoto. ‘Hata mtu akijiona kuwa mwema kadiri gani,’ wasema watafiti Steven Hill na Nina Silver, ‘anapotazama au kukubali ponografia, anakuwa asiyejali au hata mwenye chuki kuelekea mtu anayedai eti anamjali.’
USIKOSE SEHEMU YA NANE
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi Wetu

NINI MAANA YA KUUMBWA KWA MFANO WA MUNGU?

Image may contain: cloud, sky, ocean, text, nature and outdoor
Mungu ni Roho. Je wewe ni nani?
Katika somo hili la uumbaji wa binadamu, nitajibu hoja na maswali mbali mbali ambayo yanaulizwa zaidi na waumini wa dini ya Kiislam katika Mihadhara mbalimbali ya kidini, kupitia wahadhiri wao wa Dini, Waislamu wamekuwa wakipinga kuwa Mungu hana Mfano kama ilivyo andikwa katika kitabu cha Mwanzo Sura ya Kwanza na aya ya 26.
Ndugu msomaji, nakusihi ufuatilie somo hili kwa makini ili ujue ukweli kuhusu kuumbwa kwa Binadamu kwa Mfano wa Mungu na nini maana yake:
Katika siku ya mwisho ya uumbaji, Mungu alisema, "Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu" (Mwanzo 1:26). Mungu alimuumba Mtu kutoka vumbi na akampa uhai kwa kumpulizia pumzi yake mwenyewe (Mwanzo 2:07). Binadamu ni kiumbe cha kipekee ambacho Mungu alikiumba na baada ya kukiumba, akatumia pumzi yake kukipa uhai, zaidi ya hapo, binadamu ni kiumbe pekee chenye Mwili, Roho na Nafsi.
Kuwa "mfano" wa Mungu maana yake, katika suala rahisi ni kwamba sisi hatufanani na Mungu katika maana ya mwili na sura na/au mwonekano wetu, bali sisi tunafanana na Mungu katika Roho. Maandiko yanasema kwamba "Mungu ni roho" (Yohana 4:24). Binadamu tuna Mwili, Roho, na Nafsi. Unaweza kuniuliza, ni kivipi ninaweza kuthibitisha hayo? Ngoja nikupe mfano mdogo. Mtu anapo kufa, huwa tunasema hivi: Huu ni Mwili wa Marehemu “Fulani”. Kwanini tunauita “MWILI WA MAREHEMU”…Fulani? Kwa kifupi ni kwamba, Yule ambaye alikuwa anaishi katika huo MWILI amesha ondoka na/au toka katika huo MWILI na kwenda sehemu nyingine. Kumbe basi Binadamu si Mwili, bali kuna zaidi ya MWILI.
Biblia inasema kuwa, Mungu alipo pulizia pumzi ya uhai ule udongo ambao aliuumba, huo udongo ukafanyika na ukawa kiumbe chenye uhai. Kumbe basi, kilicho fanya huo udongo kuwa kiumbe chenye uhai ni ile pumzi ambayo Mungu alipulizia ule udongo alio ufanya katika umbo la mtu. Hiyo pumzi ndio Roho ya Binadamu. Hiyo Roho ndio mfano halisi wa Mungu.
Sasa tuagalie zaidi maana ya Sura ya Mungu na inahusiana kivipi na sisi Wanadamu. Mtu ni tofauti na hafanani na Wanyama amboa hawana mamlaka juu ya vilivyo umbwa, nikimaanisha kuwa Binadamu alipewa Mamlaka katika kila kitu ambacho kipo hapa duniani (Mwanzo 1:28), na zaidi ya hapo, binadamu alikuwa na uwezo wa kuzungumza na Muumba wake, kitu ambacho Wanyama wote hawana.
Hebu, tumtazame Binadamu kiakili, kimaadili, na kijamii.
Kiakili, mtu ameumbwa kama wakala wa busara. Kwa maneno mengine, mtu anaweza kuchagua nini anataka kufanya kwa kutumia fikra yakinifu na/au pevu. Kwa kufanya hivyo, mtu ameonyesha uhuru wa akili ambayo Mungu anao. Mfano, mtu anapo tengeneza mashine, anapoandika kitabu, fanya mambo mbalimbali, huko ndiko kuna ashiria neno la kufanana na Mungu, maana Mungu aliumba vitu vyote na sasa binadamu anaonyesha ustadi wa akili pevu kwa kufanya mambo ya uvumbuzi katika sura ya Mungu.
Kimaadili, mtu aliumbwa kwa uadilifu na kutokuwa na hatia ya dhambi, huo ni mwaonekano wa utakatifu wa Mungu. Mungu akaona kila alichokifanya ( pamoja na uumbaji wa Mwanadamu) alikiita kuwa ni "kazi nzuri sana" (Mwanzo 1:31). Dhamiri zetu au "dira ya maadili yetu" ni alama ya awali ya hali tuliyo kuwa nayo. Binadamu tumetunga na kuandika sheria za kutuongoza na uovu, sifa na tabia nzuri , nk, hayo yote ni kuthibitisha ukweli kwamba sisi tulifanywa na/au umbwa katika mfano wa Mungu mwenyewe.
Kijamii, mtu aliumbwa kwa ajili ya ushirika na/au kushirikiana. Huu ni uthibitisho kuwa Mungu ni Utatu ambao ni asili ya upendo wake. Katika Bustani ya Edeni, Mtu alikuwa na uhusiano na Mungu (Mwanzo 3:08 ina maana ushirika na Mungu ), na Mungu alifanya mwanamke wa kwanza kwa sababu "si vema huyo mtu awe peke yake " (Mwanzo 2:18). Kila wakati mtu anapo oa, hufanya urafiki na huyo aliye muoa, huzaa watoto na kuwa na familia hayo yote ni kutuonyesha ukweli kwamba sisi ni tulifanywa katika mfano wa Mungu.
Sehemu ya kuumbwa kwa mfano wa Mungu ni kwamba Adam alikuwa na uwezo wa kufanya uchaguzi kwa huru. Adam alipewa haki ya kuchangua mema au mabaya, uhuru huo ni sehemu ya mfano wa Mungu.
Ndugu msomaji, nategemea leo umefahamu kidogo maana ya kuumbwa kwa mfano wa Mungu ni katika Roho na si Mwili au mwonekano wetu. Mungu ni Roho. Je wewe ni nani?
Katika Huduma yake
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

ROHO MTAKATIFU ROHO AWAFUFUAYE WATU WALIOKUFA KIROHO

Image may contain: cloud and text
Kurudi nyuma na kuacha wokovu kunaitwa pia kufa kiroho (Ufunuo 3:1;Waefeso 2:1). Kwa kila aliyerudi nyuma na kuacha wokovu, hii ni saa ya kuamka usingizini na kuanza upya (Warumi 13:11-12).
Lakini, je, inawezekana kuanza upya tena katika hali hii?
Ndiyo, kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Hii ni kazi yake nyingine. Roho Mtakatifu ndiye aliyemfufua Yesu, alipokufa
(Warumi 13:11).
Kwa jinsi hiyo hiyo, Roho Mtakatifu anaweza kutufufua kiroho na kutupa uhai tena wa kiroho (Waefeso 2:1,4-6). Mwambie Roho Mtakatifu kwamba unataka kufufuliwa kiroho, naye atafanya.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

YESU ALIUMBA KILA KITU

Image may contain: text
Sifa ya kuumba niya Mungu peke yake (Yohana 1:3,14 ) “vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakukufanyika chochote kilichofanyika. Naye Neno alifanyika mwili; nasi tukauona utukufu wake kama utukufu wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli”.
Yesu aitwa Neno la Mungu (Ufunuo 19:13) “Kwahiyo Neno ni Mungu “(Yohana 1:1).. na huyo ndiye aliyevifanya kuwako vitu vyote.
Aliyeshuka kutoka juu na kufanyika mwili ni Yesu pekee aliyezaliwa na bikira Mariamu bila mbegu ya kiume kama inavyotokea kwa wanadamu wengine..
Katika yeye vtu vyote viliumbwa (Wakolosai 1:13-16) vinavyoonekana na visivyoonekana;vya mbinguni na vya duniani. Maandiko yako wazi kabisa kwa mtu mwenye Roho wa Mungu anaelewa kwa urahisi.
YESU NI MUNGU
YESU ALIUMBA KILA KITU
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo

UNAYAJUA MADHARA YA KUANGALIA PICHA ZA UTUPU "PONOGRAFIA"? (SEHEMU YA NANE)

Image may contain: one or more people and text
Kuacha zoea la kutazama Ponografia
Vipi ikiwa unapambana na zoea la kutazama ponografia?
Je, kuna lolote unaloweza kufanya ili kuacha zoea hilo? Biblia hutoa tumaini! Kabla ya kumjua Kristo, baadhi ya Wakristo wa awali walikuwa waasherati, wazinzi, na wenye pupa. Hata hivyo, Paulo alisema, “lakini mmeoshwa mkawa safi.” Hilo liliwezekanaje? Paulo ajibu: “Mmetakaswa . . . kwa roho ya Mungu wetu.”—1 Wakorintho 6:9-11.
Usipuuze kamwe nguvu za roho takatifu ya Mungu. “Mungu ni mwaminifu,” yasema Biblia, “naye hatawaacha nyinyi mshawishwe kupita vile mwezavyo kuhimili.” Kwa kweli, ataandaa njia ya kutokea. (1 Wakorintho 10:13) Kusali kwa bidii—kumwambia Mungu shida zako daima—kutakuwa na matokeo mazuri. Neno lake hutia moyo hivi: “Umtwike BWANA mzigo wako naye atakutegemeza.”—Zaburi 55:22.
Bila shaka, lazima utende kupatana na sala zako. Unahitaji kuazimia kutoka moyoni kukataa ponografia. Rafiki unayemtumaini au mshiriki wa familia anaweza kukusaidia sana, akikupa utegemezo na kitia-moyo unachohitaji ili kushikamana na azimio lako. Kukumbuka kwamba hatua hiyo itampendeza Mungu kwaweza kukusaidia uendelee kushikamana na azimio lako. (Mithali 27:11) Kwa kuongezea, kujua kwamba kutazama ponografia kunamchukiza Mungu kwaweza pia kukuchochea uache zoea hilo. (Mwanzo 6:5, 6) Haitakuwa rahisi, lakini unaweza kufaulu. Unaweza kuacha zoea la ponografia!
Kwa kweli, ni hatari kutazama ponografia. Inadhuru na kuharibu. Inawapotosha wale wanaoitayarisha na pia wale wanaoitazama. Huwashushia heshima wanaume na wanawake, ni hatari kwa watoto, na ni zoea ambalo linapasa kupingwa.
USIKOSE SEHEMU YA TISA
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi Wetu.

ROHO MTAKATIFU, ROHO AWATIAYE UZIMA WATU

Image may contain: text
Kabla ya kufa kiroho, hutangulia kuzimia kiroho. Shetani hutupeleka hatua kwa hatua, kama upepo katika tairi unavyotolewa kidogo kidogo kutokana na pancha ndogo.
Tukizimia kiroho, upendo wa kwanza unatoweka. Ingawa bado hatujafikia hali ya kufanya dhambi za uzinzi, uasherati, ulevi n.k kama mataifa, hata hivyo, mambo ya rohoni yanakuwa hayana mvuto kwetu kama mwanzo. Kuomba, kushuhudia, kuhudhuria ibada n.k, yanakuwa mzigo kwetu. Tunaanza kuvutwa zaidi na mambo ya dunia. Katika hali hii tunahitaji nguvu mpya, uzima mpya (Isaya 40:28-31). Anayefanya kazi hii pia ni Roho Mtakatifu, Roho wa uzima (Warumi 8:2). Pepo wa udhaifu wanatolewa kwa Roho wa Mungu (Mathayo12:28), na vivyo hivyo udhaifu wetu kiroho unatolewa na Roho wa Mungu.
Je umezimia kiroho, Mwambie Roho Mtakatifu akuzindue, naye atafanya.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

UNAYAJUA MADHARA YA KUANGALIA PICHA ZA UTUPU "PONOGRAFIA"? (SEHEMU YA TISA)

Image may contain: night and text
Vijana Huuliza . . .
Ninaweza kuepukaje Ponografia?
 Elewa ponografia ni nini? Ni mbinu ya kishetani ya kushushia heshima kitu ambacho Yehova aliumba ili kiheshimike. Kuelewa ponografia kwa njia hiyo kutakusaidia ‘kuchukia yaliyo mabaya.’—Zaburi 97:10.
 Fikiria madhara yake. Ponografia huharibu ndoa. Inawashushia heshima wanawake na wanaume. Inamshushia heshima mtu anayeitazama. Kwa sababu nzuri Biblia inasema: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha.” (Methali 22:3) Andika hapa chini mfano mmoja wa msiba unaoweza kukupata ukiwa na zoea la kutazama ponografia.
“Mvulana mmoja shuleni kwetu alikuwa amebandika picha ya msichana aliye uchi kwenye mlango wa kabati lake. Kabati hilo lilikuwa karibu na langu.”—Robert.*
“Nilikuwa nikifanya utafiti kwenye Intaneti kwa ajili ya ripoti ya shule nilipopata kituo cha ponografia.”—Annette.
WAZAZI wako walipokuwa na umri kama wako, mtu aliyetaka kutazama ponografia alihitaji kuitafuta sana. Siku hizi ni kana kwamba ponografia inakutafuta. Kama vile Robert, aliyenukuliwa hapo juu, huenda umejikuta ukitazama ponografia ya mwanafunzi mwenzako. Au kama Annette, huenda ukaipata bila kukusudia kwenye Intaneti. Msichana mmoja mwenye umri wa miaka 19 anasema, “Nyakati nyingine ninapitia-pitia Intaneti tu au kununua vitu kwenye Intaneti au hata kuchunguza tu habari za akaunti yangu ya benki kisha ghafula ponografia inajitokeza!”*
Hilo si jambo la kushangaza. Katika uchunguzi mmoja, asilimia 90 ya vijana walio kati ya umri wa miaka 8 na 16 walisema kwamba walipata ponografia kwenye Intaneti bila kukusudia, mara nyingi walipokuwa wakifanya kazi za shuleni! Ukweli ni kwamba, kukiwa na mamilioni ya vituo vya Intaneti vilivyo na mamia ya mamilioni ya sehemu zenye habari za wazi kuhusu ngono, ponografia inapatikana kwa urahisi sana. Inaweza pia kupatikana kupitia simu ya mkononi. Denise mwenye umri wa miaka 16 anasema, “Shuleni kwetu ni jambo la kujisifu. Jumatatu mazungumzo huwa kuhusu, ‘Una picha gani kwenye simu yako ulizotoa kwenye Intaneti mwishoni mwa juma?’”
Kwa kuwa unajua watu wengi sana wanatazama ponografia, huenda ukajiuliza, ‘Je, ponografia ina madhara?’ Sababu kadhaa zinaonyesha kwamba jibu ni ndiyo. Fikiria sababu tatu tu:
 Ponografia huwashushia heshima wale wanaoitayarisha na wale wanaoitazama.—1 Wathesalonike 4:3-5.
 Kupendezwa na ponografia ni kama kuiga mapendezi ya ngono yasiyo ya asili ambayo roho waovu wa siku za Noa walikuwa nayo.—Mwanzo 6:2; Yuda 6, 7.
 Mara nyingi kutazama ponografia huwa hatua ya kwanza inayomwongoza mtu kufanya dhambi zinazohusu ngono.—Yakobo 1:14, 15.
Ponografia huwaathiri vibaya wale wanaonaswa nayo. Fikiria mifano miwili tu:
“Niliona ponografia kwa mara ya kwanza nilipokuwa mdogo, na imekuwa vigumu sana kuachana nayo. Miaka mingi sana imepita, lakini picha hizo zimebaki katika kumbukumbu langu. Ni kana kwamba mawazo hayo huwa tu katika akili, na hakuna wakati dhamiri inakuwa safi. Ponografia inakufanya usijiheshimu na inaweza kukufanya ujihisi mchafu na mtu asiyefaa. Nyakati zote unakuwa na mzigo wa siri ambao lazima ubebe.”—Erica.
“Nilikuwa mraibu wa ponografia kwa miaka 10, na sasa miaka 14 imepita tangu nilipoacha kuitazama. Lakini hata sasa, lazima nipambane kila siku. Ingawa tamaa imepungua sana, bado ipo. Udadisi bado upo. Picha bado zimo akilini. Ninajuta kwa nini nilianza kufanya jambo hilo. Mwanzoni ilionekana kama haina madhara. Lakini sasa ninaelewa ukweli wa mambo. Ponografia inadhuru, ni potovu, na inawashushia heshima watu wote wanaohusika. Hata wale wanaoitetea waseme nini, hakuna kitu chochote kizuri kuhusu ponografia.”—Jeff.
INAWEZEKANA NA MWAMBIE TATIZO LAKO YESU NA ATAKUKOMBOA.
BARIKIWA SANA NA TUENDELEE KUMTUMIKIA YESU MUNGU MKUU.
Tumefikia tamati ya somo letu, lakini endelea mwenyewe kumtafuta Yesu na atakufunulia mengi.
Shalom,
Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi Wetu.

ROHO MTAKATIFU ROHO ATUPAYE UTAKASO

Image may contain: one or more people and text
Baada ya kuokolewa, tunahitaji pia kutakaswa. Bila utakaso, tutajikuta bado hatuna ushindi dhidi ya dhambi za ndani katika mawazo, na moyoni, ingawa tayari tuna ushindi dhidi ya dhambi za kutenda. Dhambi za ndani , ni kama hasira, wivu ,chuki, masengenyo, kugombania ukubwa, kiburi, majivuno, kutokusamehe, kinyongo, kupenda udunia n.k.
Hivi vinaweza vikaonekana kwa watu waliookoka ambao hawajatakaswa: Mawazo yasiyo ya ki Mungu (Mathayo 16:21-23), kugombania ukubwa (Luka 22:24-26; Mathayo 20:20-22,25-28; Marko 9:30-37), hasira (Mathayo 20:24) wivu, fitina, ugomvi (Marko 9:38-39; Luka 9:49-50; 1Wakorintho 3:3-5), faraka na matengano (1Wakorintho1:10-13), umimi (Mathayo 28:6-13), kutokusamehe (Mathayo 18:21-35), chuki,kushindwa kuvumilia maudhi,kushtakiana wapendwa mahakamani (Luka 9:51-56; 1Wakorintho 6:1-8); Warumi 7:15 n.k . Mambo haya huondolewa kwa utakaso.
Ndiyo maana Yesu aliwaombea Utakaso wanafunzi wake waliokuwa tayari wameokoka (Yohana 17:14-19).
Roho mtakatifu ndiye atupaye Utakaso (1Wakorintho 6:11; 1Petro1:2)
Je, hujatakaswa, mwambie Roho Mtakatifu akutakase, yeye ni waminifu, atafanya (1Thesalonike 5:23-24)
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

ROHO MTAKATIFU, ROHO ATUPAYE TUNDA LA ROHO

Image may contain: fruit, text and food
Katika Wagalatia 5:22-23, tunajifunza juu ya tunda la Roho. Katika lugha ya asili, yote katika mistari hii yanamaanisha kwamba Tunda la Roho ni moja tu, Upendo. Hata hivyo,upendo huo unadhihirishwa kwetu katika tabia na matendo kama furaha, amani, uvumilivu, utu wema,f adhili, imani, upole, na kiasi. Ni pale tu tunapokuwa na maisha yaliyojaa upendo, ndipo tunapokuwa tunatimiza mapenzi ya Mungu katika maisha yetu.
Pasipo upendo, tunakuwa shaba iliayo na upatu uvumao, tunakuwa si kitu. Lolote jingine tunalolifanya linakuwa halina faida (1Wakorintho 13:3). Hatuwi wanafunzi wa Yesu (Yohana 15:8) Sasa basi , ni muhimu kufahamu kwamba upendo ni tunda la Roho, tunalolipokea kutoka kwa Roho Mtakatifu.
Tukilipokea tunda hili, na kukua kila siku katika upendo (1Wathesalonike 3:12), Kama matunda yanavyokua, ndipo tunapokuwa wanafunzi wa Yesu kwelikweli. Tukiwa na tunda la Roho la upendo, tunakuwa na Furaha ya wokovu ambayo haiwezi kuondoka kwetu kwa sababu ya majaribu yoyote au kukosekana kwa lolote la kimwili (Yakobo1:2). Tutakuwa na amani ipitayo fahamu zote (Wafilipi 4:7) inayotuwezesha kuwa na amani na watu ambao tusingeweza kuwa na amani nao.
Tutakuwa na lengo la kutafuta amani na watu wote wakati wote (Waebrania 12:14) Tutakuwa na uvumilivu wa kipekee katika mateso, makwazo kutoka kwa watu n.k Tutakuwa na utu wema kwa watu wengine hata wale ambao hawajaokoka (Marko 10:17). Tutakuwa na fadhili yaani hali ya kutaka wakati wote watu wanaotuzunguka wawe na furaha.
Tutakuwa watu tuliojaa imani,tusiotetereka kirahisi.Tutakuwana upole yaani unyenyekevu (Mathayo 11:29; Wafilipi2:5-8) Na pili tutakuwa na kiasi (self-control) yaani uwezo wa kukataa kufanya lile ambalo Yesu hataki, kwa gharama yoyote.
Je, unataka kuwa na tunda la Roho katika maisha yako?Mwambie Roho Mtakatifu, naye atafanya.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

JE, KUJICHUA SEHEMU ZAKO ZA SIRI (PUNYETO) NI DHAMBI? (SEHEMU YA KWANZA)

Image may contain: one or more people and text
Hili ni somo linalo tatanisha na kuwewesesha watu wengi, na labda naweza hata kuhukumiwa kuwa natumia lugha chafu, la hasha. Nilazima tujifunze kila kitu, maana msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
KUJICHUA NI NINI HASA?
Kwa Kiingereza tendo hili linaitwa ‘masturbation’ likiwa na maana ya kupiga punyeto. Hapa nimetumia kwa ulaini kabisa; kujichua. Lugha nyepesi na rahisi kufikika kwa wengi ni kujiridhisha! Ni kitendo cha mtu kujichezea kimahaba huku akivuta hisia za mapenzi kwa mtu ambaye yupo mbali naye hadi anapomaliza haja zake.
Namna ya ufanywaji inategemea zaidi na jinsi ya mazoea. Wapo wanaotumia vifaa bandia (artificial) na wengine vifaa halisi kama aina mbalimbali za matunda ambazo zinafanana na sehemu pacha!
Wengine wanatumia njia wanazojua wenyewe, lakini wanaume wengi wanatumia sabuni lengo hapa ni moja tu, unatakiwa kufahamu kwamba namaanisha kujiridhisha
Unapoanza kubalehe, tamaa za ngono zinaweza kuwa zenye nguvu sana. Kwa sababu hiyo, huenda ukaangukia mazoea ya kupiga punyeto. Wengi husema kwamba si neno kufanya hivyo. “Hakuna mtu anayeumia,” wanasema. Hata hivyo, kuna sababu nzuri ya kuepuka mazoea hayo. Mtume Paulo aliandika: “Kwa hiyo, viueni viungo vya mwili wenu . . . kwa habari ya . . . hamu ya ngono.” (Wakolosai 3:5-Toleo la Ulimwengu Mpya) Kupiga punyeto hakuui hamu ya ngono bali kunaichochea. Isitoshe, fikiria yafuatayo:
Kupiga punyeto humfanya mtu kuwa mwenye ubinafsi. Kwa mfano, mtu anapopiga punyeto, anakazia fikira hisia zake mwenyewe za kimwili.
Kupiga punyeto humfanya mtu kuwaona watu wa jinsia tofauti kuwa vitu au vifaa vya kujitosheleza tu.
Badala ya kuamua kupiga punyeto ili kuzima tamaa za ngono, jitahidi kukuza sifa ya kujizuia. (1 Wathesalonike 4:4, 5) Ili ufaulu, kwanza kabisa Biblia inapendekeza ujiepushe na hali zinazoweza kuamsha tamaa ya ngono. (Methali 5:8, 9) Namna gani ikiwa umekuwa mtumwa wa zoea la kupiga punyeto?
Labda umejaribu kuacha lakini hujafanikiwa. Ni rahisi kukata kauli kwamba huwezi kubadilika, na kwamba huwezi kuishi kulingana na viwango vya Mungu. Hivyo ndivyo mvulana anayeitwa Pedro alivyojiona. “Niliporudia zoea hilo, nilihisi vibaya sana,” anasema. “Nilifikiri kwamba siwezi kamwe kusamehewa. Nilishindwa kusali.”
Ikiwa hivyo ndivyo unavyohisi, jipe moyo. Kuna tumaini. Vijana wengi, na watu wazima pia, wamefaulu kushinda mazoea hayo ya kupiga punyeto. Wewe pia unaweza kufaulu!
INAWEZEKANAJE KUJIRIDHISHA?
Ni rahisi sana kumaliza tendo la huba kwa kujifanyisha mwenyewe. Silaha kubwa inayotumiwa na waathirika ni
kuwavutia hisia watu wa jinsi pacha wakati tendo husika likiendelea kufanyika. Habari mbaya kwa watu wenye mchezo huu ni kwamba, kwanza wakishaanza, inakuwa vigumu sana kuacha.
Inashindikana kwa sababu ni jambo la aibu. Si rahisi kupata ushauri kutoka kwa watu maana ni aibu pia kumweleza rafiki yako juu ya mchezo huo. Kutokana na hilo sasa, kinachotokea ni kwamba ‘waumini’ wa mchezo huu wanaendelea kuwa watumwa kwa maisha yao yote. Hapa chini tutaona kwa undani jinsi tatizo hili linavyoumiza vichwa vya wengi.
Ni kweli hutaki kuwa mtumwa wa mchezo huu hatari? Zipo athari nyingi sana rafiki yangu ambazo nitazieleza
USIKOSE SEHEMU YA PILI
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

ROHO MTAKATIFU, ROHO ATUSAIDIAYE KUOMBA.

Image may contain: cloud, sky, bird and text
Kila Mkristo au mtu aliyeokoka, hana budi kuwa na lengo la kufikia kimo na cheo cha utimilifu wa Kristo katika tabia na Utumishi wa Mungu (Waefeso 4:11-15 ). Kufikia kiwango cha Yesu Kristo katika tabia ni jambo linalowezekana, Kama siyo, tusingetakiwa kuwa wakamilifu na watakatifu kama Baba wa mbinguni alivyo Mtakatifu (Mathayo 5:48;1`Petro 1:15-16) Neno la Mungu pia, linatufundisha uwezekano wa kuwa na viwango vya utumishi vya Yesu alipokuwa duniani, na hata kuzidi (Yohana 14:12).
Hata hivyo haya yote hayawezekani kama sisi siyo waombaji kama Yesu alikuwa mwombaji namba moja. Alifanya maombi alfajiri na mapema (Marko 1:35). Alijitenga na shughuli mchana na kufanya maombi (Luka 5:15-16) Aliomba jioni (Mathayo 14:23) Wakati mwingine alifanya maombi usiku kucha (Luka 6:12).
Je,sisi tunaweza kuwa waombaji kiasi hiki? Kwa nguvu na jitihada zetu hatuwezi.
Tunaweza tu, tukisaidiwa na Roho Mtakatifu. Ndiyo maana tunajifunza somo hili muhimu leo katika mfululizo wa masomo haya ya Roho Mtakatifu, na kichwa cha somo la sasa ni
”ROHO MTAKATIFU, ATUSAIDIAYE KUOMBA”, NA TUTAJIFUNZA SOMO HILI KATIKA VIPENGERE VINNE:-
A. UMUHIMU WA MAOMBI KATIKA MAISHA YA KIROHO
B. KUSHUKA KWA MUNGU BAADA YA MAOMBI YA KUUGUA NA KULIA
C. MAFUNDISHO TUNAYOYAPATA KUTOKANA NA MAOMBI YA YESU
D. ROHO MTAKATIFU,MSAIDIZI ATUSAIDIAYE KUOMBA
A. UMUHIMU WA MAOMBI KATIKA MAISHA YA KIROHO
Shetani ndiye adui yetu mkuu. Kazi yake ni kuiba chochote kizuri cha kiroho tulicho nacho, na tena kuchinja au kuua na kuharibu yote mema kwetu kiroho na kimwili.Tukiwa peke yetu, kamwe hatuwezi kupambana na shetani na kumshinda. Hatuna budi kuwa na Mungu katika maisha yetu ili tumshinde ibilisi. Daudi alimshinda Goliathi kwa Jina la Bwana.
Hakumshinda kwa nguvu zake. Kwa maana nyingine hatuwezi kuzaa matunda yoyote mema ya kiroho kama hatuko ndani ya Yesu. Usalama wetu na ushindi wetu wa kiroho, unategemeana sana na sisis kukaa ndani yake Yesu, yaani sisi kuwa na uhusiano au ushirika na Kristo. Pasipo yeye, sisi hatuwezi kufanya neno lolote. (Yohana 15:4-5). Kukaa ndani ya Yesu, kunafananishwa na tawi lililounganishwa na shina.
Kuunganishwa huko ndiyo uhai wa tawi.
Tawi likijitenga na shina, linanyauka na kufa. Sasa basi, tunaunganisha na Mungu na Mungu tunapokuwa tunawasiliana naye katika maombi. Tukiwa hatuna maisha ya maombi, kimsingi ni kwamba tunakuwa ni tawi lililojenga na shina, na hivyo tunanyauka na hatimaye kufa kiroho. Hatuwezi kuwa na kitu tusipoomba (Yakobo 4:2)
Tutaingia majaribuni tusipoomba (Mathayo 26:41).
Tutapepetwa kama ngano na ibilisi na mazuri yote ya kiroho yataondoshwa, na imani yetu itatoweka (Luka 22:31-32).
Shetani atatumeza na kuturudisha katika ufalme wake (1Petro 5:8).
Hatuwezi kuwaleta watu kwa Yesu, tusipokuwa waombaji, maana Shetani hatawaachia (Zaburi 2:8).
Hatuwezi kuona watu wakifunguliwa katika vifungo vya shetani vya kimwili (Luka 13:16) na vile vinavyotokana na mambo ya rohoni (Matendo 12:5-17). Kwa ufupi tutachukuliwa na mafuriko ya Shetani (Zaburi 32:6).
B. KUSHUKA KWA MUNGU BAADA YA MAOMBI YA KUUGUA NA KULIA
Maandiko yanatufahamisha kwamba makao ya Mungu mbinguni, ni Mahali palipoinuka, na Mlimani kwenye kiti cha enzi cha Mungu (Isaya 57:15; Kutoka 24:12-13 ; Ufunuo 7:9-10). Ingawa Mungu wetu yuko mlimani, maandiko yanasema tukimwomba, yeye husikia huko mbinguni na kutujibu maombi yetu kwa kuyatenda tunayoyataka (1Wafalme 8:32; Zaburi 76:8;1 02:19).
Hata hivyo, hatuna budi kufahamu pia kwamba katika mazingira fulani Mungu hushuka kutoka mlimani na kuja duniani katika hali isiyo ya kawaida. Mungu anaposhuka kwa jinsi hii, hutenda mambo ya kutisha, na ya kushangaza, yasiyo ya kawaida na hivyo kuwavuta wengi mno kwake (Waamuzi 4:12-16,5:13; Isaya 31:4; Hesabu 11:23-25,31-32).
Uamsho hutokea Mungu anaposhuka, na watu wagumu wa mioyo huvutwa kwa Yesu, walio vuguvugu huwa moto, mambo mengine makubwa ya kuitikisa jamii kama mamia ya wenye ukimwi kupona kwa mpigo, hutokea, Mungu akishuka.
Hata hivyo kushuka kwa Mungu hutokea baada ya maombi ya kuugua na kulia kwa uchungu mkubwa (Kutoka 2:23-24;3:7-8;
Matendo 7:32-34). Wakati wote Yesu Kristo alimfanya Mungu kushuka katika huduma yake kwa kuwa aliomba kwa kulia sana
na machozi (Waebrania 5:7), na wengine walimuombolezea kwa kilio na uchungu mkubwa (Luka 23:27).
Kulia kwa kuugua katika maombi hushusha majibu ya maombi namna ya kipekee (2Nyakati 34:27; Zaburi 34:17;39:12;51:1-2,17;72:12;12;88:1-2; Isaya 58:9; Yeremia 31:9; Luka 18:7).
Sasa basi ni rahisi kuomba maombi kwa kulia na kuugua?
Jibu ni la ,bila msaada wa Roho Mtakatifu, itakuwa kama tunaigiza tu.
C. MAFUNDISHO TUNAYOYAPATA KUTOKANA NA MAOMBI YA YESU.
Tunajifunza mambo mengi zaidi kuhusiana na maombi kwa kuyaangalia maisha ya maombi ya Yesu, na mafundisho yake kuhusu maombi:-
§ Yesu Kristo alikuwa na wakati wa kuomba pamoja na wanafunzi wake (Luka 9:18), Lakini pia alikuwa na muda mrefu wa maombi ya peke yake (Luka 5:16; Marko 6:45-46). Ni muhimu kujiunga na kikosi cha maombi cha Kanisa na kushiriki maombi ya pamoja na wengine, lakini ni lazima kila mmoja kuwa na muda wa kuomba mwenyewe.
§ Yesu hakukubali kuchukuliwa na huduma za kushauri watu, kuwaombea watu n.k na kuziruhusu zimkoseshe kuomba.
Alijua bila maombi, huduma hizo zitakuwa hazina nguvu. Aliziacha huduma, akafanya maombi (Luka 5:15-16). Kabla ya kuzungumza na watu, alizungumza na Mungu KWANZA. Alifanya maombi ya alfajiri na mapema sana na baadaye alipokutana na watu ilikuwa rahisi mno kwake kuponya ukoma na kutoa pepo. (Marko 1:35-42).
§ Kabla ya Yesu kutembea juu ya maji, na kukomesha upepo, alikuwa na kipindi kirefu cha maombi (Marko 6:46-51). Vipindi virefu vya maombi vinaweza kutupa uwezo wa kuona yasiyowezekana yakiwezekana!
§ Utukufu wa Yesu ulitokana na maombi! (Luka 9:28-29) Hatuna utukufu wa Mungu kwa kuwa siyo waombaji! Mwombaji, utukufu wake humwogopesha shetani
§ Alipokuwa na huzuni aliomba hakunung'unika tu na kulalamika, na ghafla alipata ujasiri wa kukabili lolote lile (Mathayo 26:36-39; 47-49). Hatuna ujasiri na tumejaa woga kwa kuwa hatuombi
§ Maombi yake yalikuwa ni vita hasa. Alipokuwa akiomba, alitoka jasho (hari) kama matone ya damu (Luka 22:44).
Maombi ni mapambano dhidi ya shetani anayezuia majibu yetu (Danieli 10:12-13). Ni lazima iwe ni vita. Mwili ni lazima tuushughulishe kama wapiganaji hasa, tukiwa katika roho Maombi yenye matokeo makubwa, ni yale ya kutoka jasho! Ni lazima tumkabili shetani katika vita ya maombi kabla hata hajatushambulia.Katika vita ya siku sita kati ya waisraeli na wamisri, miaka kadha iliyopita; Waisraeli walishinda Wamisri ingawa walikuwa na ndege nyingi zaidi za kivita kuliko wao,kwa kuwa walizipiga KABLA hazijaondoka katika vituo vyao.
Tusingoje matatizo ndio tuombe!
§ Imani yetu na ya ndugu zetu,inaweza kutokutindika,ikiwa tu tutakuwa waombaji;kinyume cha hapo ni rahisi kumezwa na
shetani (Luka 22:31-32;1Petro 5:8-9)
§ Maombi ndiyo yanafanya tuutunze utakatifu wetu,na kuwa mbali na dunia. Bila maombi ni rahisi kuvutwa na masumbufu
ya dunia (Luka 21:34-36).
§ Yesu aliliombea Kanisa (Yohana 17:14-15). Ni muhimu kuliombea kanisa na siyo kujiombea wenyewe tu wakati wote.
Je tunaweza kuyatendea kazi yote haya kwa nguvu zetu? Jibu ni la kwa nguvu zetu hatuwezi ,bila msaada wa Roho Mtakatifu.
D. ROHO MTAKATIFU MSAIDIZI ATUSAIDIAYE KUOMBA
Shetani anafahamu sana umuhimu wa maombi, na hivyo atatuzuia sana kufanya maombi kuliko yote mengine, ili tubaki kama matawi ambayo hayajaunganishwa na shina. Anajua pasipo Mungu, sisi hatuwezi neon lolote. Kwa kujifunza tu juu ya maombi,bado hatuwezi kuwa na maisha ya maombi. Tunaweza kuomba sisi hatuwezi neno lolote. Kwa kujifunza tu juu ya maombi, bado hatuwezi kuwa na maisha ya maombi. Tunaweza kuomba siku mbili, tatu, halafu basi. Pamoja na wanafunzi wa Yesu kuhimizwa kuomba na Yesu mwenyewe, bado walishindwa kuwa waombaji (Mathayo 26:37-43).
Ndipo hatimaye akawaambia atakuja Msaidizi ambaye kazi yake mojawapo, ni kutusaidia kuomba (Yohana 16:7; Warumi 8:26-28). Yeye Roho, kwa kuwa hutuombea kwa kuugua, na tena ni Roho ya neema na kuomba, huweza kutupa msaada wa kutuwezesha kuomba kwa kuugua na kulia (Zakaria 12:10) Baada ya Roho Mtakatifu kuja na kuwasaidia wanafunzi wa
Yesu, maisha yao ya maombi yalibadilika (Matendo 10:9). Siri ni hii, usitumie nguvu zako kuomba. Kabla ya kuingia katika maombi, mwombe Msaidizi akusaidie kuomba.
Shalom,
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

JE, KUJICHUA SEHEMU ZAKO ZA SIRI (PUNYETO) NI DHAMBI? (SEHEMU YA PILI)

Image may contain: 1 person, text


CHANZO NI NINI HASA?
Wenye umri mkubwa au wa kati, huanza tabia hii mbaya hasa baada ya kuanza mchezo wa kuangalia video za kikubwa wakiwa peke yao. Kwa sababu wanachotazama kinahusisha msisimko wa mapenzi, basi bila kutarajia hujikuta ayari!
Hii inafanana pia na kwa watoto wa kike, vyanzo nilivyoeleza hapo juu pia husababisha kwa karibu sana.
Jambo la kushangaza ni kwamba, hakuna mdau wa mchezo huo ambaye amefundishwa jinsi unavyofanywa. Wengi wameanza wenyewe, tena wengine bila kujua nini kitakachotokea, lakini baada ya matokeo kuonekana, ndiyo
mwanzo wa kutopea huko.
Kwa vijana wa kiume, wengi huanza tabia hii wakiwa kwenye umri wa kubalehe. Mara nyingi hutokea asubuhi wakati wa kuamka, usiku wakati wa kulala au bafuni wakati wa kuoga.
Kwa kawaida, mtu anapokuwa katika sehemu ya utulivu kwa maana ya kupumzika, wakati mwingine mkono unaweza kutembea huku na huko kwenye mwili na mwisho wake bila kutegemea mhusika anajikuta ameshaingia kwenye mchezo huo.
Kama ilivyotajwa mapema, wale walio na mazoea ya kupiga punyeto mara nyingi hujiona kuwa wenye hatia. Bila shaka, ‘kuhuzunishwa kwa njia ya kimungu’ kunaweza kukuchochea ushinde mazoea hayo. (2 Wakorintho 7:11) Lakini kujiona kuwa mwenye hatia kupita kiasi kunaweza kuwa na matokeo mabaya. Kunaweza kukuvunja moyo sana mpaka utake kukata tamaa.—Methali 24:10.
Kwa hiyo, jaribu kuwa na usawaziko. Kupiga punyeto ni uchafu. Mazoea hayo yanaweza kukufanya uwe ‘mtumwa wa tamaa na raha za namna mbalimbali’ na kukufanya uwe na maoni yasiyofaa. (Tito 3:3) Hata hivyo, kupiga punyeto si upotovu wa kingono, kama vile uasherati. (Yuda 7) Ikiwa una tatizo la kupiga punyeto, usikate kauli kwamba umefanya dhambi isiyoweza kusamehewa. Siri ni kupinga tamaa ya kufanya hivyo na kutokubali kamwe kushindwa!
Ni rahisi kuvunjika moyo baada ya kurudia zoea hilo. Ukirudia, kumbuka maneno ya Methali 24:16: “Huenda mwadilifu akaanguka hata mara saba, naye hakika atasimama; lakini waovu watakwazwa na msiba.” Kujikwaa hakumaanishi kwamba wewe ni mwovu. Kwa hiyo, usikate tamaa. Badala yake, chunguza jambo lililofanya urudie zoea hilo, kisha ujaribu kuliepuka.
Tafakari kuhusu upendo na rehema za Mungu. Mtunga-zaburi Daudi, ambaye pia nyakati fulani alifanya dhambi kwa sababu ya udhaifu wake, alisema: “Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema, ndivyo ambavyo Mungu amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa. Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.” (Zaburi 103:13, 14) Ndiyo, Mungu hukumbuka hali yetu ya kutokamilika na ‘yuko tayari kusamehe.’ (Zaburi 86:5) Kwa upande mwingine, anataka tujitahidi na kufanya marekebisho. Hivyo basi, unaweza kuchukua hatua gani ili kushinda zoea hilo?
USIKOSE SEHEMU YA TATU
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU








Ili tuweze kuwa mashahidi wa Mungu,tunahitajika kubatizwa kwa Roho Mtakatifu baada ya kuokoka na kutakaswa. Ili tumtendee Mungu kazi kikamilifu, ni lazima tupokee nguvu ya Roho Mtakatifu (Matendo 1:8;Luka 24:49). Kwa sababu hili, somo hili, ni la muhimu sana kwa mtu yeyote anayetaka kuwa mtendakazi mzuri wa Mungu. Tutaligawa somo hili katika vipengere vinne:-
A. MAANA YA UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU
B. UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU,UWEZA WA KUTUWEZESHA KUWA MASHAHIDI WA MUNGU
C. ALAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA JINSI ZINAVYOTUPA UFAHAMU KUHUSU UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU
D. JINSI YA KUBATIZWA KWA ROHO MTAKATIFU
E. ISHARA YA KWANZA YA KUBATIZWA KWA ROHO MTAKATIFU NA NIDHAMU INAYOAMBATANA
F. UMUHIMU WA KUUCHOCHEA MOTO WA ROHO MTAKATIFU
A. MAANA YA UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU
Baada ya mtu kuokolewa,inambidi kubatizwa kwa maji kwa jina la baba,Mwana na Roho Mtakatifu (Mathayo 28:19). Hata hivyo,huo siyo ubatizo wa mwisho.Baada ya mtu kutakaswa,anahitajika kubatizwa kwa Roho Mtakatifu (Mathayo 3:11) Ubatizo wa maji, unamfanya mtu azamishwe ndani ya maji na kuzungukwa na maji pande zote. Vivyo hivyo, Ubatizo wa Roho Mtakatifu unamfanya mtu aliyeokoka,kuzamishwa ndani ya Roho Mtakatifu na kuzungukwa na Roho Mtakatifu pande zake zote.Roho Mtakatifu,anakuwa msaidizi wake (Yohana 15:26). Ubatizo wa maji,tunabatizwa na wanadamu waliopewa Agizo la Mungu lakini Ubatizo wa Roho Mtakatifu, tunabatizwa na Yesu mwenyewe (Mathayo 3:11).
B. UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU, UWEZA WA KUTUWEZESHA KUWA MASHAHIDI WA MUNGU
Neno “mashahidi” katika (Matendo 1:8), linatokana na neno la lugha ya Kiyunani “Martus” ambalo linatafsiriwa katika Kiingereza" Martyr” ambalo maana yake ni “Mtu anayekuwa tayari kuteswa sana au hata kuuawa kwa sababu ya imani yake,pamoja na hayo, hawezi kuiacha imani yake”.Bila ubatizo wa Roho Mtakatifu, hatuwezi kuwa mashahidi kama walivyokuwa Stefano na Antipa (Matendo 22:20; Ufunuo 2:13). Kabla ya kubatizwa kwa Roho Mtakatifu,Petro alisema asingemkana Yesu hata ikibidi kuuawa, lakini kinyume chake alimkana mara tatu,na yeye pamoja na wanafunzi wenzake walipoyaona mateso yanakuja,walimwacha na
kumkimbia Yesu (Mathayo 26:31-35,56) Lakini baada ya ubatizo walikuwa na ujasiri mkubwa. Matendo 4:13
C. ALAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA JINSI ZINAVYOTUPA UFAHAMU KUHUSU UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU
§ Maji (Yohana 7:37-39)Hakuna maisha bila ya maji.Mwanadamu ni asilimia 60%maji.Kuharisha na kutapika sana humfanya mtu kupoteza maji mengi na huweza kusababisha mtu kupoteza uhai. Vilevile sisi tunaosema tumeokoka, hatuwezi kabisakuwa na maisha ya kiroho yaliyo hai yenye nguvu, bila Ubatizo wa Roho Mtakatifu.Ni lazima tunyweshwe Roho (1Wakorintho 12:13).
Jambo jingine, maji ni muhimu katika usafi wa miili yetu hutuondolea kunuka n.k Roho Mtakatifu hutumulikia dhambi au uchafu wowote.
§ Moto (Mathayo 3:11).Kuwepo kwa moto ni alama ya uwepo wa Mungu (Kutoka 3:1-5; Matendo 2:2-3). Moto vilevile,unangarisha madini kama dhahabu na fedha (Malaki 3:2-3). Ubatizo wa Roho Mtakatifu hufanya uwepo wa Mungu uwe dhahiri kwa mtu na pia humng’arisha mtu na kuwa mtumishi wa Mungu anayeng’aa . Siyo hayo tu, moto huleta mwanga.Ubatizo wa Roho Mtakatifu hutupa mwanga mkubwa wa maandiko yaani Biblia na kutupa mwanga wa uzuri wa mbinguni na ubaya wa Jehenam.Ukiwa na mwanga huo hakutakuwa na gharama kubwa yoyote ya kukufanya ushindwe kufanya mapenzi ya Mungu. Moto pia huleta nguvu ya kuendesha, magari, treni, Ndege n.k vifaa vyote hivyo huendeshwa kutokana na moto unaotokea baada ya cheche za umeme kuunguza mafuta.
Kazi ya Mungu inaendeshwa kwa nguvu ya moto, ubatizo wa Roho Mtakatifu na kwa moto. Mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu, moto unawake ndani yake na hawezi kuacha kushuhudia au kuhubiri na kufundisha (Yeremia 20:9; Isaya 62:1; Matendo4:20). Mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu,maneno yake huwa moto unaoteketeza kila ugumu wa mioyo ya watu kwa kuwa Roho Mtakatifu hushuhudia pamoja naye na hivyo matokeo yake ya utumishi wake huwa makubwa. Ni nguvu kwa ajili ya Utumishi (Yeremia 5:14; Yohana 15:26-27;16:6-8;Mika 3:8).
§ Upepo (Yohana 3:8) Upepo wakati wote unatembea, na uko mahali pote. Roho Mtakatifu hakufanya kazi wakati wa mitume tu, hata sasa anatembea na yuko kwetu tayari, ni wajibu wetu kumpokea tu. Upepo huvuma upendako.
Ni vigumu kuubadilisha mkondo wa upepo tunavyotaka sisi,jahazi hufuata mkondo wa upepo. Ni muhimu kutakaswa kwanza kabla ya Ubatizo huu.
Utakaso humfanya mtu kuwa mtii mno katika yote na Roho Mtakatifu ni mshirika wa wale wamtiio(Matendo 5:32) Upepo pia hutuletea hewa safi inayotuburudisha wakati wa joto, moshi n.k Mazingira yoyote magumu tukiyakabili katika utumishi wa Mungu, Roho Mtakatifu huwa hewa safi kwetu inayorekebisha mazingira.
§ Mafuta (Luka 4:16-21) Roho Mtakatifu hututia mafuta au kutuweka katika utumishi wa Mungu (1Samweli 16:13; Kutoka 30:30; 1Wafalme 19:16;Yohana 2:27) Rais kabla hajaapishwa huitwa Rais mteule na hana mamlaka sana wakati huo kisheria.
Kuapishwa kwa leo ndiyo kutiwa mafuta kwa zamani.Bila ubatizo huu,mamlaka yetu huwa hafifu. Mafuta yanalainisha na kuzuia msuguano.Ubatizo wa Roho Mtakatifu hutupa hekima ya kuvuta roho za watu(Mithali 11:30) mafuta huufanya mwili uwe laini.
Ubatizo wa Roho Mtakatifu hulainisha ukavu wa maombi yetu (Warumi 8:26).
§ Mvua (Zaburi 72:6;Hosea 6:3) Nchi haiwezi kutoa matunda bila mvua.Mtu aliyeokoka hawezi kuwa na matunda mengi bila mvua yaani ubatizo wa Roho Mtakatifu (Yohana 15:16).
§ Mvinyo (Waefeso 5:18;Matendo 2:12-13) mvinyo kwa walevi unasahaulisha shida. Ubatizo wa Roho Mtakatifu, humwezesha mtu kudharau majaribu na kuondoa wasiwasi na kubabaishwa na mambo madogo madogo tu. Mvinyo kwa walevi, pia unawapa ujasiri wa kufanya lolote lile, aibu, woga vinatoweka. Ubatizo wa Roho Mtakatifu humfanya mtu kuwa jasiri kama simba na mtu aliye kuwa mwoga kama Petro, kuwa jasiri (Mithali 28:1; Mathayo 26:31-35,56; Matendo 4:13).
§ Hua (njiwa)- (Yohana 1:32) Ubatizo wa Roho Mtakatifu haufanyiki kwa mtu wa ulimwengu huu yaani ambaye
hajaokoka. Njiwa hakutua kwenye ulimwengu,alirudi safinani kwa waliookoka (Mwanzo 8:8-9)Roho Mtakatifu ni mweupe, kama hua.Ni Mtakatifu,huja kwa watakatifu waliotakaswa.
§ Muhuri (Waefeso 1:13) Muhuri ni alama ya mamlaka.Bila muhuri barua hupungua mamlaka yake. Ubatizo wa Roho Mtakatifu humfanya mtu kuwa na mamlaka ya Yesu kwake na shetani husema “ Yesu namjua na Paulo namfahamu (Matendo 19:15) Ubatizo wa Roho Mtakatifu ni mamlaka au uwezo kutoka juu wa kuzifanya kazi za Yesu.
§ Arabuni (2Wakorintho 1:21-22)Neno arabuni maana yake- Uhakikisho au uthibitisho wa Uimara.Ubatizo wa Roho Mtakatifu, hutufanya kuwa na uthibitisho wa uimara wa Neno la Mungu, hutuongezea imani ya kufanya maajabu.Shetani hawezi kumpeperusha huku na kule mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu.
D. JINSI YA KUBATIZWA KWA ROHO MTAKATIFU
Kuokoka au kuzaliwa mara ya pili.Mafuta haya hayatiwi kwa mtu mgeni ambaye jina lake haliko katika kitabu cha Uzima mbinguni (Kutoka 30:31-33)
Kutakaswa (Yohana 17:17;1Wathesalonike 5:23) Wanafunzi 120 orofani,walitakaswa kabla ya Ubatizo wa Roho Mtakatifu.
Kuwa na Imani kama Roho Mtakatifu yuko kwetu tayari na kwamba ni ahadi ya Mungu kwetu(Matendo 2:38-39); Luka 11:10-13)
Kuwa na kiu ya kumtumikia Mungu (Isaya 44:3)
Kuomba kwa kufumbua sana kinywa na kutokuruhusu kutumia akili,wala kuwaza kwambatutasema lugha ya mapepo. (Luka 11:10-13; Zaburi 81:10).
E. ISHARA YA KWANZA YA KUBATIZWA KWA ROHO MTAKATIFU NA NIDHAMU INAYOAMBATANA
Mtu akibatizwa kwa Roho Mtakatifu,kutakuwa na mambo ya kusikia kwake na ya kuyaona kwake(Mathayo 3:16-17).
Ishara ya kwanza ni kusikia kutoka kwake kabla ya kuona mengine. Atasema au ananena kwa lugha mpya asiyoifahamu
ambayo siyo ya dunia hii (Matendo 2:4;10:44-46;19:6). Ni muhimu mno kwa mtu aliyeokoka kuomba kwa kunena kwa lugha hii (1Wakorintho 14:2,4-5,15). Hata hivyo hatupaswi kunena kwa lugha mbele ya mataifa wasioelewa kitu. Watadhani sisi ni wendawazimu (1Wakorintho14:18-25)
Kunena kwa lugha mbele ya mataifa wasiojua kitu nikuwapa mbwa kilicho kitakatifu na kutupa lulu zetu mbele ya nguruwe matokeo yake watatudhihaki kwa kuwa hawajui maana (Mathayo 7:6).
F. UMUHIMU WA KUUCHOCHEA MOTO WA ROHO MTAKATIFU
Moto bila kuchochewa huzimika (Mithali 26:20). Hatuna budi kuwa waombaji na kuomba kwa Roho, yaani kunena kwa lugha katika maombi mara kwa mara katika maombi yetu binafsi (1Wakorintho 14:14-15; Yuda 1:20) Vile vile hatuna budi kudumu katika usafi kwa Neno (Zaburi 51:4,11;119:11; Yohana 15:3).
Hatuna budi pia kujihusisha katika kushuhudia na kuwaleta watu kwa Yesu (Mika 3:8).
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

JE, KUJICHUA SEHEMU ZAKO ZA SIRI (PUNYETO) NI DHAMBI? (SEHEMU YA TATU)

Image may contain: one or more people and text
Chunguza burudani yako. Je, wewe hutazama sinema au programu za televisheni au hutembelea vituo vya Intaneti vyenye kusisimua kingono? Kwa hekima, mtunga-zaburi alisali kwa Mungu: “Uyafanye macho yangu yapite ili yasione jambo lisilofaa.”*—Zaburi 119:37.
Sali kuhusu jambo hilo. Mtunga-zaburi alisali hivi kwa Yehova: “Uyafanye macho yangu yapite ili yasione jambo lisilofaa.” (Zaburi 119:37) Yehova Mungu anataka ufaulu, naye anaweza kukupa nguvu za kufanya yaliyo sawa!—Wafilipi 4:13.
Zungumza na mtu. Mara nyingi kuchagua mtu unayeweza kumfunulia moyo wako husaidia sana kushinda zoea hilo. (Methali 17:17) Andika hapa chini jina la mtu mkomavu ambaye unaona ni rahisi kumweleza jambo hilo.
ATHARI ZA KUJICHUA "PUNYETO"
Zipo athari nyingi sana ambazo mwathirika anaweza kuzipata kwa kuendekeza mchezo huu. Hapa nataka nizungumze kwa herufi kubwa kabisa kwamba, ndugu zangu usidanganyike kwamba hakuna madhara kwa kufanya mchezo huu.
Yapo MADHARA makubwa sana ambayo yanapatikana kwa mchezo huo. Achana na propaganda za mitaani, zenye utafiti hewa.
Sikia nikuambie rafiki yangu, hasa wewe ambaye unafanya mchezo huo. Upo kwenye hatari kubwa ya kushindwa
kufurahia mapenzi, kwa vile mazoea ya kiungo siri chako ni kwenye vitu ‘artificial’ zaidi ya ‘natural’.
Mwanaume aliyezoea kujiridhisha mwenyewe, akikutana na mwanamke, hana muda mrefu sana, kila kitu kinamalizika.
Siyo hivyo tu, uwezo wa kurudia tendo unakuwa mdogo au unakosekana kabisa. Kinachotokea ni kwamba, kiungo siri chake kinakuwa kimeshazoea, aina nyingine ya ‘hali ya hewa’ hivyo kinapokutana na sehemu siri za kike, ambazo ni laini na zenye ute mwepesi, inakuwa rahisi kumaliza ‘biashara’ mapema wakati wateja bado wanahitaji!
Kiungo siri cha mwanaume huwa kigumu, hivyo kusababisha maumivu kwa mwanamke kutokana na sugu aliyoitengeneza bila kujua. Kwa kawaida viungo siri vyote ni laini sana na vinatakiwa kubaki katika hali hiyo ili kuleta msisimko wenye usawa.
Mazoea yoyote tofauti na yale ambayo yanatakiwa hupunguza msisiko na kusababisha mmoja wa washiriki wa tendo la ndoa kubaki na kiu na mwenzake.
“Najuta kuufahamu huu mchezo, kila siku ninapokutana na mume wangu, ananiacha nikiwa sijatosheka. Kiukweli tangu amenioa, sijawahi kufurahia tendo la ndoa. Nilianza huu mchezo zamani sana, tangu nikiwa kidato cha tano.
USIKOSE SEHEMU TA NNE
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW