Sunday, February 28, 2016

KWANINI MASHAHIDI WA YEHOVA WANAPOTOSHA KWA MAKUSUDI KUHUSU UUNGU WA YESU?

Mashahid wa Yehova wanadai kuwa:
1. Yesu alikuwa Malaika aliyeumbwa.
2. Yesu hakuwa Mungu na mwanadamu wakati ule – “God incarnate”.
Mashahidi wa Yehova wanasema kuwa Yesu hakuchanganya au kushiriki tabia za kiungu na za kimwili alipokuwa duniani. Wanadai alipokuwa duniani alikuwa mwanadamu mkamilifu tu, ikimaanisha, hakuwa na adhama ya Uungu. Na tangu kufufuliwa, yeye ni nafsi kamili ya kiroho tu.
3. Yesu alishindwa kuwakomboa wanadamu.
4. Mwili wa Yesu haukufufuliwa.
5. Mwanadamu Yesu amekufa kwa hiyo haishi tena.
6. Kabla ya kufa Yesu alikuwa mwanadamu tu, bali baada ya kufufuliwa alikuwa na hali ya kiungu (malaika).
7. Yesu si mpatanishi wetu.
Je, madai ya hawa Mashahidi wa Yehova ni ya kweli?

LAKINI BIBLIA INATUFUNDISHA NINI KUHUSU YESU?
Biblia inakataa na kuvunja hoja zote dhaifu za Mashahidi wa Yehova kama ifuatavyo:
1. Yesu si malaika kama wanavyo dai hawa Mashahidi wa Yehova. Soma-Waebrania 1:1-8. Yeye ni bora. Pia soma Yohana 1:1-3; 8:58; Ufunuo 1:8; 21:6; 22:13 – Yesu hakuumbwa bali yeye mwenyewe ni mwumbaji aliye wa milele.
WAEBRANIA MLANGO WA 1: 1 Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3 Yeye kwa kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu; 4 amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao. 5 Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana? 6 Hata tena, amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu malaika wote wa Mungu. 7 Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto. 8 Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio. 10 Na tena, Wewe, Bwana, hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi, Na mbingu ni kazi za mikono yako; 11 Hizo zitaharibika, bali wewe unadumu; Nazo zote zitachakaa kama nguo,
1. Aya ya 2: Inakiri kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu.
2. Aya ya 3: Inakiri kuwa Yesu alimaliza deni la dhambi na yupo upande wa Kuume wa Ukuu huko juu.
3. Aya ya 4: Yesu ni Mmbora kupita mailaka, hivyo basi hawezi kuwa ni Malaika Mikaeli kama wanvyo dai Mashahdi wa Yehova.
4. Aya ya 5: Mungu Baba anakataa kuita Malaika Mwanae.
5. Aya ya 6: Malaika wote wanamsujudia Yesu, pamoja na Mikaeli na Gabrieli.
6. Aya ya 7: Inakiri kuwa Yesu ndie aliye umba Malaika.
7. Aya ya 8: Yesu ndie mwenye Kiti cha Enzi, zaidi ya hapo Yesu anaitwa Mungu na Baba yake.
8. Aya ya 9: Yesu kwa mara nyingine tena anaitwa Mungu na Baba yake.
9. Aya ya 10: Yesu anaitwa Bwana na kukiri kuwa yeye ndie aliye weka Misingi ya Nchi na Mbingu. Ni kazi ya mikono ya Yesu.
10. Aya ya 11: Yesu ni wa milele.
2. Isaya alitabiri kwamba Mungu angeishi kimwili-Isaya 7:14; Mathayo 1:23. Mariamu pia alikuwa na mimba kupitia uwezo wa Roho Mtakatifu, mwili wa Yesu alitoka kwa Mariamu lakini Roho kwa Mungu. Kwa hiyo Yesu alikuwa asili zote mbili--kimwili na kiroho, Mathayo 1:18-20. Katika Filipi 2:6-7 tunaona kwamba Yesu alifanyiwa kuwa mfano wa Mwanadamu, Filipi 2:6-7; Waebrania 2:16. Pia tunaweza kusoma katika Ynoha 1:1-2, 14; 16:28; 1 Timotheo 3:16. Pia tunaweza kumwona Petro alikiri katika Mathayo 16:18, Yesu ni nani? Na kama kuna mtu ambaye anatufundisha ya kuwa Yesu hatokani na Mungu, mwambie asome 1 Yohana 4:3 na 2 Yohana 7.
Isaya Mlango 7: 14 Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.
Aya inakiri kuwa Yesu ni Imanueli.
3. Mashahidi wa Yehova wanasema Yesu si mkombozi wetu. Tusome Yohana. 1:29; Mathayo. 10:28; Rum. 5:11; Waebrania 10:3-14.
Yohana 1: 29 Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
Sasa Je, Nani ni mwongo hapa, Mungu au Mashahidi?
4. Wanadai mwili wa Yesu haukufufuliwa. Yesu alisema kwamba atafufuka, Yohana 2:19-22 [Yesu akajibu, akawaambia, Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha] na pia alionyesha mwili wake (uliofufuliwa) kwa Tomaso, Yohana 20:24-28.
5. Wanadai mwanadamu Kristo alikufa asiwe hai tena. Lakini Biblia inasema katika Zaburi 16:10, hapa Daudi alitabiriwa kuwa Yesu atafufuka. Na Petro alidai kwamba Kristo alifufuka, Matendo ya Mitume 2:30-31, wakati alipokuwa anahubiri siku ya Pentikoste alikuwa anaongozwa na Roho Mtakatifu. Na katika Matendo ya Mitume 1:1-3, Yesu alithilibitisha sana kwamba alikuwa hai.
6. Pia Mashahidi wanadai Yesu hakuwa na hali ya kimungu isipokuwa baada ya kufufuliwa. Katika Yoh.
1:1-3; 17:5 tunaona Yesu alikuwa Mungu tangu mwanzo. Katika Flp. 2:6, Yesu alikuwa sawa na Mungu, na Kristo na Mungu ni kitu kimoja, Yohana. 14:11; 17:21.
Kwa hiyo wanasema kuwa Kristo aliyekufa na yule aliyefufuliwa sio mtu yule yule, wale ni watu wawili tofauti. Lakini Biblia inasema ni yule yule kabla ya kufufuka na baada ya kufufuliwa, Matendo ya Mitume 1:11; Waefeso. 4:10; Waebrania 10:12.
7. Mwisho wanadai Yesu siye mpatanishi wetu. Tusoma gazeti lao, “Watch Tower” Toleo 15/9/1909, uk. 283. “Katika toleo lao la 1906, ukarasa wa 26, walisema, ‘Bwana wetu Yesu, kati ya Baba na nyumba ya waaminio, katika kipindi cha Injili.’ Usemi huu si kweli. Hakuna maandishi yanayosema hivyo. Ni sehemu ya mwisho ya kipindi cha giza, ambao tunafurahi kuufuta kutoka machaoni mwetu.”
Mashahidi ni waalimu gani? Wanaobadili mafundisho yao? Nani anaweza kuamini wameongozwa na Mungu ikiwa wanasema wenyewe kuwa wamekosa katika kufundisha kwao? Lakini, ukweli ni kwamba Yesu ndiye mpatanishi wetu, 1 Timotheo 2:5; Waebrania. 9:15; 1 Yohana 2:1.
YESU NI MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Tito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Mashahidi wa Yehova ni hii: Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yeremia 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Hebu tusome Wafilipi 2: 5-11 INASEMA:
5 Tuweni na nia ile ile aliyokuwa nayo Kristo Yesu. 6 Yeye ingawa alikuwa sawa na Mungu, hakuona kule kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho, 7 bali alijifanya si kitu, akajifanya sawa na mtumwa, akazaliwa katika umbo la mwanadamu. 8 Naye akiwa na umbo la mwanadamu, alijinyenyekeza hata mauti, naam, mauti ya msalaba! 9 Kwa hiyo, Mungu alimtukuza sana na kumpa Jina lililo kuu kuliko kila jina, 10ili kwa Jina la Yesu, kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, vya duniani na vya chini ya nchi 11 na kila ulimi ukiri ya kwamba YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.
NENO la "Kuwa sawa na Mungu" kwa Kigiriki ni MORPHE-: Iikimaanisha Yesu alikuwa na adhama zote za Kimungu na Mungu. Hivyo basi katika ushaidi huu wa katika kitabu cha Wafilipi tunasoma kuwa Yesu hakuwa mtu wa kawaida bali alikuwa ni Mungu pamoja nasi yaani Imanueli.
Ni maombi yangu Mungu ayafungue macho ya Mashahidi wa Yehova kwa ukweli wa injili na mafundisho ya kweli ya neno la Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Saturday, February 27, 2016

MAFUNDISHO POTOFU YA MASHAHIDI WA YEHOVA KUHUSU UTATU WA MUNGU

Ndugu msomaji,
Katika somo hili, nitajibu hoja ya Mashahidi wa Yehova kuhusu kupinga kwao Utatu Mtakatifu wa Mungu.
Taasisi ya Mashahidi wa Yehova wanafundisha kuwa kuna nafsi moja tu katika Uungu naye ni Baba tu. Ikimaanisha kuwa, wanapinga Uungu wa Yesu na wanapinga Uungu wa Roho Mtakatifu.
Mafundisho ya Biblia:
1. Je! Yesu ni yule Mungu mmoja?
Musa alisema: “Sikiliza, Ee Israeli: Bwana Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja,” Kumbukumbu ya Torati 6:4
Lakini katika Injili kutokana na Yohana Yesu anasema yafuatayo: Yesu alisema: “Mimi na Baba tu umoja,” Yohana. 10:30.
Mtume Paula alisema, “Maana katika yeye (Yesu) unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili,” Wakolosai 2:9.
Sasa Mashahidi wa Yehova wanafundisha kuwa kuna nafsi moja na ni Yehova.
Lakini hapa kwenye Wakolasai 2: 9 tumeona nini? Tumeona kwamba wako wawili sasa [kuna Mungu Baba na kuna Yesu ambaye kuna utimilifu wote wa Mungu]. Lakini JE, kuna wawili tu? La hasha! Mafundisho ya Biblia yaliyo wazi sana yanasema.
Soma: 1 Yohana 5:8, “Kwa maana WAKO WATATU washuhudiao mbinguni, BABA, na NENO, na ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja.”
Tazama, neno la Mungu lasema kuwa WAKO WATATU MBINGUNI, na nafsi hizi tatu hufanya Uungu ule mmoja. Na maana ya kusema hayo ni sawasawa na maana yake aliposema kuwa duniani kuna “Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja.” mst. 9. Na tunaelewa kwamba roho, maji na damu sio kitu kimoja kiasili. La, bali umoja wao ni ushuhuda wanaotoa kuhusu Yesu. Vivyo hivyo, Baba, Neno, na Roho Mtakatifu ni nafsi tofauti tatu wanaomshuhudia Yesu kuwa Mwana wa Mungu. Kuna Mungu mmoja tu, walakini ana nafsi zake tatu. Yesu aliposema, “Mimi na Baba tu umoja,” hakuwa na maana kuwa Yeye mwenyewe ndiye Baba.
Tena tuangalie 2 Wakorintho. 13:14, maneno hayo ya Biblia yaonyesha kuwa Uungu ni wa nafsi tatu. Sasa tuchunguze kwenye Biblia maana ya “Umoja” walio nao Baba na Mwana.
Waefeso 5:29-32, “Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitndea Kanisa. Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili moja. Siri hiyo ni kubwa; ila mimi na nena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.”
Mst. 30 - “Tu viungo vya mwili wake”.
Mst. 31 - “Hao wawili watakuwa mwili moja.”
Tazama:
1) Kanisa ni mwili ule mmoja wa Kristo. Sasa maana ya maneno hayo ya Waefeso. 5 ni kwamba kanisa ni mtu mmoja tu. Je, Petro, Paulo, Apollo, Barnaba, Timotheo, Tito na Yohana wote walikuwa mtu mmoja tu? La, mtume mwenyewe alisema kuwa ni Viungo vya mwili ule mmoja. Kanisa ni watu mbalimbali tofauti wanaounganishwa washiriki umoja wa kiroho. Wanashirikiana katika baraka na kazi za Yesu. Vivyo hivyo, Yesu na Baba wa umoja, hata ingawa ni wawili.
2) Pia mistari hii inasema mume na mkeo ni mwili mmoja tu! Je, kweli hawa wawili ni mwili mmoja?
Hapana. Lakini wale wawili ni umoja katika kazi na baraka za ndoa? Vivyo hivyo Yesu, Baba na Roho ni mmoja; hata ingawa ni watatu.
Yohana 17:20-21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako: hao nao wawe ndani yetu.”
Je, umoja ambao Yesu alituombea ni kwamba Wakristo wote wawe mtu mmoja tu? Si anaongea habari ya umoja wa matendo, imani, na maneno yetu? Kama vile Yesu na Baba wanao umoja katika kutuumba na kutuletea wokovu, vivyo hivyo Wakristo wawe na lengo moja na juhudi moja. Tuone mfano mwengine wa umoja katika Biblia. 2 Samweli 7:23, “Tena ni taifa lipi duniani lililo kama watu wako, kama Israeli...?”
Waisraeli walikuwa watu wengi na makabila mengi lakini wanaitwa kuwa ni taifa moja tu! Vivyo hivyo, Uungu ni mmoja, lakini una nafsi tatu.
2. Matatizo ya kusema kuna nafsi moja tu.
Yohana 17:1-5, Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Mimi nimekutukuza dunia, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa nifanye. Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.”
Sasa kama Mungu ni nafsi moja tu, na Mungu alikuja ulimwenguni katika mwili na aliitwa Yesu. Sasa huyo Yesu (Kama nafsi pekee) alikuwa ana ongea na nani hapa? Mbona alisema, Wakujue wewe, Mungu wa pekee, na Yesu Kristo uliyemtuma. Akiwa yeye (Yesu) alikuwa nafsi pekee sasa nani alitumwa huyu?
Kwa hiyo tumeona Baba na Mwana ni nafsi mbili tofauti. Na wana umoja katika kazi zao na asili yao ya Uungu.
Soma Yohana 14:9-10, “Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.”
Sasa wakati Yesu alisema “Siyasemi kwa shauri langu”. Sasa ameyasema kwa shauri la nani? Akiwa ninafsi pekee, ni nani aliyempa maneno ayaseme? Yesu tena alisema, “Mimi ni ndani ya Baba na Baba yu ndani yangu.” Sasa hakusema Yeye ni Baba! Lakini alisema Baba yu ndani yake! Kwa hiyo 1 + 1=2!
Kumbe!
Yohana 14:26, “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.”
Tazama 1+1+1=3. Wako Watatu! Roho Mtakatifu atakayepelekwa na Baba kwa jina
la Yesu! Pia angalia mistari hii:
1 Wakorinth 11:3; 1 Wakorintho 15:24-28; 1 Timotheo 2:5; Marko 13:32; Mathayo 27:46; Luka 23:46-47.
HIVYOBASI, TUMEJIFUNZA kuwa kumbe wako Watatu, tena hao watatu wapo Mbinguni: 1 Yohana 5:8, “Kwa maana WAKO WATATU washuhudiao mbinguni, BABA, na NENO, na ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja.”
Baada ya kusoma huu ujumbe, sasa jiulize maswali yafuatayo:
MASWALI YAKINIFU:
Je, Yesu na Baba ni UMOJA – Yohana Mlango wa 10 aya ya 30?
Je, UMOJA maana yake ni MMOJA?
Je, Yesu ni UKAMILIFU WA KIMWILI WA MUNGU – Wakolosai 2”9?
Je, UNAKUBALINA NA: 1 Yohana 5:8, “Kwa maana WAKO WATATU washuhudiao mbinguni, BABA, na NENO, na ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja.”?
Namaliza kwa kusema kuwa, hoja ya Mashahid wa Yehova kupinga UTATU MTAKATIFU wa Mungu ni dhaifu, maana 1 Yohana 5:8, “Kwa maana WAKO WATATU washuhudiao mbinguni, BABA, na NENO, na ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja
Ni maombi yangu Mungu ayafungue macho ya Mashahidi wa Yehova kwa ukweli wa injili na mafundisho ya kweli ya neno la Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Friday, February 26, 2016

MASHAHIDI WA YEHOVA WANAFUNDISHA KUWA HAKUNA JEHANNAM

(i) Wanafundisha kuwa, kifo ndio mwisho wa maisha yako
(ii) Wanafundisha kuwa, hakuna Jehannam.
Ndugu msomaji,
Mashahidi wandai kwamba hakuna Jehannam. Wanasema mwovu anapokufa, basi anapotea moja kwa moja tu! Wanadondoa Mhubiri 3:20-21; 12:7.
Je, haya madai ya Mashahid wa Yehova ni ya kweli?
Je, ni kweli kuwa hakuna maisha baada ya kifo, yaani wewe ukifa ndio unapotea moja kwa moja?
Biblia Yasema Nini kuhusu jambo hili?
1. Ni kweli mwili wa mtu hurudi mavumbini anapokufa, Mwanzo 3:19. Lakini mwanadamu si mtu tu -MWILI NA NYAMA PEKEE!
Mwanadamu ni nafsi ya roho pia, maana tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, (Mwanzo 1:26) naye Mungu hana mwili bali ni roho (Yohana 4:24; Luka 24:39). Miili ya wanadamu wote itarudi mavumbini hata wakiwa wema au waovu. Lakini roho za mwanadamu ndizo zitakazoishi milele ama pamoja na Mungu ama katika Jehannam.
WEWE NI MFANO WA MUNGU
Mwanzo 1: 26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
MUNGU NI ROHO, KUMBE BASI WEWE NI ROHO!
Yohana 4: 24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
Kumbebasi wewe ni roho na sio mwili na nyama.
2. Kifo Cha Roho-Kifo maana yake ni utengano. Ukitenga roho na mwili basi mwili umekufa, Yakobo 2:26. INASEMA: Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.
Vivyo hivyo, ukitenga roho na Mungu aliye uhai wetu, basi roho nayo imekufa. (Mungu hakumwambia Adamu uongo aliposema “Siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika” Mwanzo 2:17. Adamu hakufa kimwili siku ile bali alikufa kiroho maana alitengwa na Mungu, na kufukuzwa katika bustani.
Kifo cha roho hakina maana kwamba roho haitakuwapo tena. Roho ni ya milele. Roho ya mwovu inapotengwa na Mungu, basi tunaweza kusema imekufa hata ingawa ili roho bado ipo, 1 Timotheo 5:6 6 Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai.
Waefeso 2:5; Warumi 8:10. Walakini, mtu akifa katika dhambi zake, basi roho ya mwovu yule itakuwa katika hali ya mateso daima mbali na Mungu, 2 Thesalonike1:7-9; Mathayo 25:41-46. Hii ndiyo inayoitwa MAUTI YA PILI na ndiyo kifo cha kiroho, Ufunuo 21:8; 20:14-15.
3. Ikiwa hakuna mahali pa mateso panapoitwa Jehannam, mbona Yesu hakujua? Maana Yesu ametuonya mara nyingi kuhusu Jehannam, Mathayo 10:28; Luka 12:5; Mathayo 5: 22, 29-30; 23:33.
Yohana 10: 28 Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.
4. Mhubiri 3:20-21; 12:7 haisema kwamba hakuna Jehanum. Mistari hii inaonyesha kwamba mwili unarudi mavumbini mtu anapokufa. Lakini, miili yetu haitakaa mavumbini daima. La! bali Yesu atakapokuja, wafu wote watafufuliwa, Yohana 5:28-29; Ufunuo 20:12-15. Si vigumu kwa Mungu kufufua miili yetu kutoka
mavumbini, Ezekiel 37:1-13. Isitoshe, mara tutakapofufuliwa miili yetu itabadilishwa kama apendavyo Mungu maana nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, 1 Wakorintho. 15:50-54.
5. Mashahidi wanasema kwamba hakuna adhabu ya milele, Soma Daniel 12:2; Mt. 25:46; Yonana 5:28-29; Ufunuo 20:10.
JEHANNAM:
Jehanamu, kama vile mbinguni, si mahali patajwapo kwa utisho tu bali ni mahali dhahiri. Hapa ni mahali ambapo wasiohaki watakutana na ghadhabu isiyokoma ya Mungu. Watavumilia mateso ya kihisia, kiakili, na kimwili wakiwa katika akili zao timamu huku wakijihisi kuaibika na kujuta kwa matendo yao maovu.
Jehanamu inaelezewa kama shimo la giza (Luka 8:31, Ufunuo wa Yohana 9:1), na Ziwa la Moto, liwakalo na kiberiti ambapo watakao kuwemo watateswa usiku na mchana milele na milele (Ufunuo 20:10). Huko kutakuwa na kulia na kusaga meno, ikiashiria machungu makali na hasira (Mathayo 13:42). Hapa ni mahali ambapo mdudu hatakufa wala makaa kuzimika (Marko 9:48). Mungu hafurahishwi na kufa kwa mtu muovu, lakini hutaka wazighairi njia zao mbaya ili waishi (Ezekiel 33:11). Lakini hatatulazimisha kumkubali; tukiamua kumkataa yeye. Hana budi kutupatia tulilolichagua – kuishi mbali naye.
Je unaamini kuwa kunayo maisha baada ya kifo?
Ni nini hufanyika baada ya kufa?
Je, unaamini kuwa hakuna Jehannam kama Mashahid wa Yehova?
Je, unaamini kuwa ukisha kufa wewe ndio umeishia hapo/unapotea moja kwa moja kama ambavyo Mashahid wa Yehova wanavyo kiri?
Mungu awabariki sana,
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wake.
Max Shimba Ministries Org
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Thursday, February 25, 2016

MALAIKA GABRIEL WA BIBLIA NI TOFAUTI NA JIBRIL WA KWENYE QURAN


Ndugu msomaji,
Tokea kuanzishwa Kwa dini ya uislam, waislamu duniani wanaamini na kuifundisha jamii kuwa malaika aitwae ‘Gabriel’ Kama maandiko matakatifu ya Biblia yanavyofundisha ndiye malaika ‘Jibril’ Kama Quran inavyosimulia.
Swali la muhimu je ni kweli kuwa malaika “Gabriel” ndiye “Jibril” nakusihi fuatilia somo hili ili kujua ukweli….
HOJA ZA WAISLAMU ZA KUAMINI KUWA MALAIKA GABRIEL NDIYE JIBRIL
Waislam wanalinganisha kwa kusoma aya za Quran na Biblia na kusema kuwa malaika Gabriel ndiye Jibril wanasoma aya hizi….
QURAN 19:16-17 SURAT MARYAM
16. Na mtaje Mariamu kitabuni (humu) alipojitenga na jamaa zake (akenda) mahali upande wa mashariki (wa msikiti) 17. Na akaweka pazia kujikinga nao.Tukampelekea muhuisha sharia yetu (jibril) - akajimithilisha kwake kwa sura ya Binadamu aliye kamili.
LUKA 1:26-28
26. Mwezi wa sita, malaika Gabriel alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti. 27. Kwa mwana mwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu wa mbari ya Daudi. Na jina lake Bikira huyo ni Mariamu 28 Akaingia nyumbani kwake akasema, salamu uliyepewa Neema, Bwana yu pamoja nawe.
“Mbali na kusoma aya hizi, pia wanaendelea kusoma kitabu cha maisha ya nabii Muhammad kilichotungwa na aliyekuwa kadhi mkuu wa Kenya marehemu sheikh Abdallah Saleh Al-Farsy katika ule ukurasa wa 17 kifungu (A) kuna maneno haya...
NAMNA YA KULETWA WAHYI…
Waislamu wanaitikadi kuwa Quran ni maneno ya Mwenyezi Mungu na vilevile Taurat ya nabii Musa na injili ya nabii Isa, na Zaburi ya nabii Daudi. Vyote pia ni vitabu vyenye maneno ya mwenyezi Mungu. Lakini Mungu haonekani Kwa macho wala hayupo mahali mahsusi. Basi vipi hao mitume wamepata maneno haya? Jawabu yake ni hii wao huyapata ima kwa Jibril malaika mkubwa kuliko malaika wote wa Mwenyezi Mungu.
QU-RAN 53:2-6 SURATUL NAJM (NYOTA)
2. Kwamba mtu wenu huyu Nabii Muhamad (hakupotea Kwa ujinga) na wala hakukosa (na hali ya kuwa anajua) 3. Wala hasemi Kwa matamanio (ya nafsi yake) 4. Hayakuwa haya (anayosema) ila ni wahyi (ufunuo) uliofunuliwa (kwake) 5. Amemfundisha (malaika) mwenye nguvu Sana 6. Mwenye uweza na yeye (huyu jibril) akalingana sawa sawa.

JE, MASHAHIDI WA YEHOVA NI WAKRISTO?

Ndugu msomaji,
Swali la kwanza la kujiuliza hapa ni hili, Je, Mashahidi wa Yehova wanaamini nini?
Tukianza kuutafakari kwa karibu sana msimamo wa kanuni yao kwa masomo ya IMANI YA KIKRISTO kama, Mwili wa Kristo, Wokovu, Utatu wa Mungu, Roho Mtakatifu na upatanisho wa Mungu na mwanadamu yaonyesha bila shauku yoyote kuwa hawashikilii kanunu ya msimamo wa Kikristo katika masomo haya.
Utadungua kuwa:
1. Mashahidi wa Yehova wanaamini kuwa Yesu ndiye Mikaeli malaika mkuu, kiumbe kikuu. Hii inahitilafiana maandiko mengi ambayo wazi yamtaja Yesu kuwa Mungu (Yohana 1:1,14, 8:58, 10:30).
2. Mashahidi wa Yehova wanaamini kuwa wokovu unapatikana kwa ushirika wa imani, matendo mazuri na itiivu. Hii inahitilafiana maandiko mengi yasiyo hesabika ambayo yasema wokovu unapatikana kwa neema kupitia kwa imani (Yohana 3:16; Waefeso 2:8-9; Tito 3:5).
3. Mashahidi wa Yehova wanakataa utatu wa Mungu, wakiamini kuwa Yesu ni kiumbe na Roho Mtakatifu kuwa ni nguvu za Mungu zizokuwa na uhai (active force/energy).
4. Mashahidi wa Yehova wanakataa dhana ya Kristo kuwa thabihu kwa niaba yetu na badala yake wanashikilia kuwa nadharia ya ukombozi, kuwa kifo cha Yesu fidia ya dhambi ya Adamu.
5. Wanakana kwamba Mungu alifanyika mwili (incarnation) ...kinyume na Yohana 1:14;1Timotheo 3:16
6. Wanakana Kifo mbadala cha Kristo kwa ondoleo la dhambi(substitutionary atonement)..kinyume na aya hizi Mathayo 20:28; Marko 10:45.
7. Wanakana fundisho la Utatu Mtakatifu...kinyume na Yohana 1:1-3; 1 Yohana 5:8
8. .Wanakana Uungu wa Yesu na wanafundisha Yesu ni kiumbe si Muumbaji...kinyume na ya hizi Isaya 9:6; Tito 2:13; Wakolosai 1:16-17; Yohana 1:1-3
9. Wanaamini kuwa wanakazi moja ya kubadili aya zote za Biblia ili ziendane na kile wanachodai kuvuviwa!!! Hii ni kinyume na Wagalatia 1:6-9; Ufunuo 22:18,19.
10. Wameunda bodi yao inayofasiri maandiko na mfuasi wao yeyote hatakiwi kupambanua jambo kinyume na tafsiri hizo!! Bodi hiyo inaitwa Watchtower Bible and Tract Society....na Biblia yao inaitwa New world Translation; ama Le monde neauval Tradiction en Francois. Yaani wana injili yao na Biblia yao, Mungu wao!!
11. Wanakana "Umasihi" 'Ukristo" wa Yesu....kwa hiyo hawa ndo wapinga Kristo hasa.1 Yohana 4:3 kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu.Hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
12. 1 Yohana 2:22-23 Ni nani aliye mwongo ila yeye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo,yeye amkanaye Baba na Mwana.Kila amkanaye Mwana hana Baba; amkiriye Mwana ana Baba.
Ndugu msomaji,
Inawezekana vipi kwa mtu kujiita Mikristo bila ya Roho Mtakatifu ambaye ni Mungu na anaye ukamilisha Ukristo ndani yetu -sustaining?
Inawezekana vipi mtu au watu kujiita Wakristo bila ya Yesu ambaye ndie Mungu katika Mwili na ndie KRISTO Mwenyewe?
Biblia inasema:
Kwanza: Biblia inatufundisha kuwa Mpinga Kristo ni yule ANAYEKATAA KUWA YESU KRISTO HAJAJA KATIKA MWILI…YANI SIYE MWANA WA MUNGU, Soma (2 Yohana 1:7) na hapa tunawaona Mashahidi wa Yehova wanafauli kuingia katika hili kundi, sasa je, ni nani ni Mpinga Kristo kama si wewe unaye sema kuwa eti, Yesu ni Malaika Gabrieli?
Pili: Mtu yeyote ambaye hamwamini Bwana Yesu ya kuwa ni Bwana na Mwokozi wa maisha yake huyo tayari ni mpinga Kristo kwa sababu hana ushirika nayeye na wala hamuabudu yeye kabisa. Aliye hivyo huyo anaitwa Mpinga Kristo na ule mwisho Yesu akija kuhukumu ulimwengu hatawachukua hao wasiyo mwabudu yeye, na Nabii huyo Yesu wa Nazareti. Nabii huyu watu wanamjua ni nabii wa Mungu na ndiye atakayekuja kuhukumu ulimwengu siku ile ya kiama. Sasa kama hapa tu sasa hivi unampinga, je jiulize swali nayeye atakukubali uende naye uzimani alipo yeye? Jibu hatakuchukua na ameniambia niuambie ulimwengu wote atakaye sikia na asikie atakayekataa shauri lake. Wote wasiomwabudu yeye 100% ni wapingaji wa kumpinga Yesu Kristo na hao ni wapinga Kristo.
Namaliza kwa kusema kuwa, Mashahid wa Yehova sio Wakristo bali wanampinga Kristo kama ilivyo semwa katika 2 Yohana 1:7. Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea duniani, wasiokiri ya kuwa Yesu Kristo yuaja katika mwili. Huyo ndiye yule mdanganyifu na mpinga Kristo.
Ni maombi yangu Mungu ayafungue macho ya Mashahidi wa Yehova kwa ukweli wa injili na mafundisho ya kweli ya neno la Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Wednesday, February 24, 2016

MAJINA KUMI NA MBILI YA ROHO MTAKATIFU

 
Katika kijarida hiki, tutajikumbusha majina kumi na mbili ya Roho Mtakatifu na kazi zake.

Haya ungana nami moja kwa moja na tujifunze kuhusu Roho Mtakatifu.
Roho Mtakatifu anamajina mengi na wasifa mwingi, mengi yao kama sio yote yanaeleza kazi na huduma yake. Hapa chini ni baadhi ya majina na wasifa wake kama yalivyo semwa katika Biblia kuhusu Roho Mtakatifu.

1.   MWANDISHI WA NENO (Author of Scripture)
2 Petro 1:21; 2 Timotheo 3:16. Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; 
Roho Mtakatifu ndie aliye weka pumzi katika vitabu vyote vya Biblia 66. Hivyo basi, waandishi wa Biblia walipewa nguvu/upako na Roho Mtakatifu na wakaandika Biblia bila ya makosa.

2.   MSAIDIZI/WAKILI/MSHAURI WETU (Comforter / Counselor / Advocate)
Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele.
Isaya 11:2; Yohana 14:16, 15:26; 16:7.
Maneno yote matatu yanatokana na neon la Kigiriki Parakletos, amabalo linatupa Paraclete. Jina linguine la Roho. Yesu alipo ondoka duniani, Wafuasi wake walijisikia vibaya sana kwasababu awalikosa mfariji. LAKINI Yesu aliwapa ahadi ya Roho ambaye atawafariji, Washauri, Wawakilisha na kuwa Msaidizi wao wale ambao wapo katika Kristo. Roho Mtakatifu vile vile yeye Ushuhudia roho zetu kuwa sisi ni watoto wa Mungu na utuhakikishia wokovu wetu.
KUMBE BASI, ROHO MTAKATIFU akama aya zinavyo sema atakuwa nasi MILELE.


3.   MHAKIKISHI WA DHAMBI (Convictor of Sin)
Yohana 16: 7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu. 
8 
Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. 
9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi; 
10 kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena; 
11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. 
Roho Mtakatifu yeye ndio anakuonyesha au kufunulia UKWELI kuhusu Mungu katika akili zetu na roho zetu. Ukweli huu ndio utatuhumu kwa kuwa tutafahamu kuwa sisi ni watenda dhambi na hatuto weza pinga huo ukweli. Hufanya hivi kwa kuweka hatiani Moyo wako kwamba sisi ni watenda dhambi mbele ya Mungu Baba, na kwamba tunahitaji haki yake (righteousness) na kwamba kwahakika siku moja hukumu itakuja kwa watu wote. Wale ambao wanapinga ukweli huu, basi wanapinga ukweli wa Roho Mtakatifu.

        4. AMANA/MHURI/BIDII (Deposit / Seal / Earnest)
2 Wakorintho 1:22; 5:5; Waefeso 1:13-14. Roho Mtakatifu ni Mhuri kwa watu wa Mungu. Yeye hutujali sisi kama watoto wake. Zawadi ya Roho Mtakatifu ni kama malipo ya amana kwetu sisi kwa urithi wa mbinguni, ambao Kristo alituahidi baada ya kazi ya pale Msalabani. Ni kwasababu ya Roho Mtakati ambaye ameweka Mhuri kwetu ndio maana tuna uhakika wa Wokovu. Hakuna mwenye uwezo wa kuvunja hii “SEAL” ya Mungu.

5.   KIONGOZI (Guide)
Yohana 16:13. Kama ambavyo Roho alivyo waongoza waandishi wa Biblia katika kweli yote, vivyo hivyo ametuahidi kutuongoza wote tuaminio katika Kristo. Ukweli kuhusu Mungu ni jambao la mzaha kwa watu wa dunia na Makafiri, kwasababu hawana macho ya rohoni na hawamweli Roho Mtakatifu (1 Wakorintho 2:14)  Wale walio katika Kristo ndani yao wana Roho Mtakatifu ambaye anatuongoza katika yote tunayo hitaji. Wale ambao hawana Roho Mtakati wao ni kama yatima, maana hawana kiongozi na hawata weza elewa maneno ya Mungu, wao baba yao ni Yule muovu, IBILISI.

6.   ANAMAKAZI NDANI YA WAAMINIO (Indweller of Believers)
Warumi 8:9-11; Waefeso 2:21-22; 1 Wakorintho 6:19) Roho Mtakatifu anaishi katika mioyo ya waaminio/watu wa Mungu, na huku kuishi ndani ya kila mtu kwa wakati mmoja (omnipresence) ni sifa mojawapo pekee ya Mungu. Akiwa ndani ya Waaminio, huwaongoza, huwafundisha, kuwafariji, na ni mshawishi na zaidi ya hapo huzalisha matunda ya Roho (Wagalatia 5:22-23) Hutoa uhusiano wa karibu kati ya Mungu na Watoto wake “Intimate connection” Wakristo wote walio okoka wana Roho Mtakatifu ndani yao/katika mioyo yao.


     7. MWOMBEZI (Intercessor)
Warumi 8:26 Kazi na au huduma moja ya muhimu sana ya Roho Mtakatifu kwa walio kombolewa na damu ya Yesu ni kuwaombea “interceding”
Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

    8. MFUNUAJI/ROHO WA KWELI (
Revealer / Spirit of Truth)
Yohana 14:17; 16:13; 1 Wakorintho 2:12-16.
Yohana 14: 16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; 
17 
ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu. 
18 Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. 
Roho Mtakati yeye ndie anatufunulia yote ambayo Yesu aliyafanya na yote ambayo Yesu anataka tuyaelewa. Ndio maana watu ambao hawa Roho Mtakatifu wao huona mambo tunayo funiliwa si ya maana.

1 Wakorintho Mlango wa 2 :12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. 
13 
Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. 
14 Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. 
15 Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu. 
16 Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.

.         9. ROHO YA MUNGU/BWANA/KRISTO (Spirit of God / the Lord / Christ)
Mathayo 3:16; 2 Wakorintho 3:17; 1 Petro 1:11 Katika vitabu hivyo tunahakikishiwa kuwa Hakika Roho Wa Mungu ni sehemu ya Utatu na Hakika yeye Ni Mungu kama alivyo Mungu Baba na Mungu Mwana. Alisemwa kwa mara ya kwanza wakati wa uumbaji, ikifuatiwa na Yesu ambaye aliumba kila kitu. Yohana 1:1-3. Tunaona Utatu huohuo katika Yesu wakati alipo kuwa anabatizwa, wakati Roho alipo shuka na tukasikia sauti ya Mungu Baba.

   10. ROHO YA UZIMA (Spirit of Life)
Warumi 8:2 Neno Roho ya Uzima maana yake kuwa ni Roho Mtakatifu ambaye anatupa na au umba UZIMA, haimaanishi kuwa anasaidia wewe kuoka, bali anakufanya wewe kuwa umeokoka. Bila ya Roho Mtakatifu hakuna wokovu. HAPA VILE VILE tunaona Utatu katika Kazi ya Mungu. Tumeokolewa na Mungu Baba kupitia kazi ya Mwana wake Yesu, na wokovu unaedelezwa “sustained” na Roho Mtakatifu.

11.MWALIMU (Teacher)
Yohana 14:16; 1 Wakorintho 2:13.  Yesu aliahidi kuwa Roho atawafundisha kila kitu na kuwakumbusha yote ambayo aliwafundisha wakati alipo kuwa nao. Waandishi wa Agano Jipya waliongozwa na Roho Mtakatifu ndio maana walikumbuka kila kitu ambacho Yesu alisema na kufanya.
Yohana 14: 26 Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia. 

12.SHAHIDI (Witness)
Warumi 8:16; Waebrania 2:4; 10:15 Roho anaitwa SHAHIDI kwasababu YEYE anatuhakikishia na kutushuhudia kuwa sisi ni watoto wa Mungu, na kwamba Yesu na Wanafunzi wake walitumwa na Mungu Baba na kuwa Biblia ni Neno la Mungu. Zaidi ya hapo, Roho hutupa Zawadi ya Roho Mtakatifu, na utushuhudia sisi na dunia kuwa sisi tulio okolewa na Damu ya Yesu ni watoto wa Mungu.
Warumi Mlango wa 8:16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; 
17 
na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. 

Nakushauri uendelee kumwomba Mungu aliki aendelee kukufulia mambo makuu kupitia Roho Mtakatifu. Kumbu, bila ya Roho Mtakatifu, Wokovu wetu unakuwa wa mashaka. Ndio maana lazima tumfahamu huyu Roho Mtakatifu aliye ahidiwa kuja na Bwana wetu Yesu Kristo aliye kufa kwa ajili ya dhambi zetu.

Basi mpendwa, Mungu aendelee kukubariki.

Ni mimi, Mtumishi wake Max Shimba.

Katika huduma yake

Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED

Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Monday, February 22, 2016

YESU ATABIRI KUWA MUHAMMAD NI MTUME NA NABII WA UONGO


Ndugu msomaji,
Mara nyingi Waislam wamekuwa wakisema kuwa, eti, Yesu alitabiri kuja kwa Muhammad, pale alipo sema kuhusu Roho wa Kweli, la hasha.
Nabii ni mtu gani?
Nabii ni mtu aliyeteuliwa rasmi kwa vigezo vya Kiungu ili kuleta ujumbe wa Mungu kwa wanadamu, kwa maneno mengine nabii ni msemaji wa siri za Mungu.
Nabii: Ni mtu ambaye ni msemaji wa Mungu (a mouthpiece of God) .Husimama kati ya Mungu na binadamu, mwenye jukumu la kupeleka ujumbe wa Mungu kwa watu. Nabii anapokuwa msemaji wa Mungu, huvuviwa na Roho wa Mungu, bila ujumbe wake kuwa na makosa. Nabii hujizuia kabisa utashi wake, nafsi yake, na mawazo yake, anapokuwa anatoa ujumbe wa Kinabii toka kwa Mungu. Wakati mwingine Mungu mwenyewe hutia maneno yake vinywani mwao (Kum 18:18, Yer 1:9). Nabii ni mtumishi wa Mungu (Zekaria 1:6) na mjumbe wa Mungu 2 Nyak 36:15).
Ni kweli kuwa Yesu alitabiri kuja kwa manabii, lakini kamwe hakusema lolote kuhusu utume wa Muhammad zaidi ya kukiri kuwa watu wenye sifa kama za Muhammad ni Mitume na Manabii wa Uongo.
Miongoni mwa wanadamu wanaoitwa nabii na mtume, ni mtu aitwaye Muhammad s.a.w ibn Abdullah, ibn Abdu Mutallib, ambaye ni mtume na nabii katika dini ya Kiislamu.
Pengine wewe msomaji wa somo hili unaweza kushangaa ni kwa vipi sisi ambao si Waislamu bali Wakristo tuanze kuhoji habari za Muhammad s.a.w mtume wa Waislamu? Jibu lake ni kwamba kitabu cha Qur’an kinachotumiwa na Waislamu kimetutaja sisi Wakristo mara 62 kikitutaka kuupokea, kuuamini na hatimaye kuufuata ujumbe wa Muhammad s.a.w kwa madai ya kuwa yeye ni nabii na mtume wa mwisho hata kwetu Wakristo, aliyetumwa na Mungu.
YESU ATABIRI KUHUSU MTUME WA UONGO AMBAYE NI MUHAMMAD
Tahadhari ya Bwana Yesu: Bwana Yesu alipokuwa hapa duniani alituonya kuhusu kuwatambua manabii na mitume wa uongo kabla Muhammad hajazaliwa (amezaliwa 570 B.K), wala kabla Uislamu haujaanzishwa na Muhammad mwaka 610 B.K, wala kabla ya kuwepo kitabu kinachoitwa Qur’an. Tunayasoma maonyo hayo ya Bwana Yesu katika
Mathayo 7:15-16 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali, mtawatambua kwa matunda yao”.
Mathayo 24:11-13 “Na manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi na kwasababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa. Lakini mwenye kuvumilia mpaka mwisho, ndiye atakayeokoka”.
Yesu katika Ufunuo alisema kuwa watakuja Manabii na Mitume wa Uongo.
Ufunuo 2:2 Nayajua matendo yako na taabu yako, subira yako, na kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume nao sio, ukawaona kuwa waongo.
Je, Muhammad ni nabii wa Mungu?
Je, Muhammad anasifa za nabii wa Mungu?
Hebu endelea na somo hapa chini:
JINSI YA KUMFAHAMU NABII WA UONGO:
Kwa hivyo Muhammad ni miongoni mwa hao Mitume ambao ni waongo, ambao sisi kama Wakristo yatupasa kuutambua uwepo wao hapa Duniani, kwani tumeshapewa angalizo la kuwatambua hawa wanaojiita Mitume na Manabii, hali ya kuwa ni waongo
1 Yohana 4:1-3
1 Wapenzi msiamni kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu: kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea duniani. 2 Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; KILA ROHO IKIRIYO KWAMBA YESU KRISTO AMEKUJA KATIKA MWILI, YATOKANA NA MUNGU, 3 Na Kila roho isiyomkiri Yesu, haitokani na Mungu. Na HII NDIO ROHO YA MPINGA KRISTO ambayo mliskia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
Vigezo hivi tulivyopewa na Biblia Takatifu kuwajua manabii na mitume wa uongo ni muhimu sana tukavichunguza katika maisha ya wale wanaoitwa nabii au mtume
Kila nabii na mtume ambaye yeye hakubali kuwa Kristo alikuja katika mwili, kwa maana kuwa Mungu alidhihirishwa katika mwili, hiyo roho yaani huyo nabii si ambaye anatokana na Mungu, huyo ni Nabii anaetokana na shetani, kwa mujibu ya maandiko Matakatifu, Kristo alidhirishwa katika mwili.
1 Timotheo 3:16 Na Bila shaka siri ya utauwa ni kuu, Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulikana kuwa na haki katika roho,
Akaonekana na Malaika, akahubiriwa katika mataifa. akaaminiwa katika ulimwengu, akachukuliwa juu katika utukufu,
SASA KAMA MNATAKA KUAMINI KUWA KWELI Muhammad ni nabii na mtume wa uongo, waulizeni wafuasi wake,
SWALI LA KUPIMA UNABII WA MUHAMMAD:
Je! Kwa mujibu wa uislamu, Wanakubali kuwa Mungu alikuja kwa njia ya mwili wa kibinadamu na kuonekana?
Wakikubali, basi tambueni kuwa Muhammad ni mtume wa kweli, na wakikataa basi mjue kuwa Muhammad ni nabii na mtume wa Uongo.
SIFA ZA NABII WA KWELI:
Nabii wa kweli hupata ufunuo wake kwa njia ya Roho Mtakatifu:- 2Petro 1:20-21.” Mkijua neno hili kwanza,ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu;bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu,wakiongozwa na Roho Mtakatifu”.
LAKINI MUHAMMAD YEYE ALIPATA UNABII KWA NJIA HII, SOMA
Katika kitabu kiitwacho “ Wakeze Mtume Wakubwa Na Wanawe” kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al Farsy uk.12 tunasoma maneno haya
“Basi Mtume akafanya hofu akarejea kwa mkewe akamhadithia; na pale pale homa kubwa kabisa ikampanda akataka afunikwe maguo. Mara akawa anatetemeka kwa nderema na anaweweseka na kusema “Najikhofia nafsi yangu kuchezewa na shetani na kuniharibu akili yangu na kunizuga”. Bibi Khadija palepale alimdakiza akamwambia; “ Wacha hayo; Siyo yatakayokuwa hayo. Wewe huwezi kuchezewa na mashetani. Shetani hawezi kumchezea mtu mwenye sifa zako. Wewe unatazama vyema jamaa zako, unachukuwa mizigo ya hata watu wasiokuwa wako, unawadhihirishia watu sifa zako nzuri ambazo hakuna mwenye nazo. Unafanya hivi na unafanya hivi. Furahi ndugu yangu. Tua moyo wako, Wallahi! Mimi naona umekwishakuwa mtume”.
Je, wapi katika Injili au Taurat au Zaburi tunasoma kuwa Manabii na Mitume katika Biblia walipata kwa njia ya homa na kukiri kuchezewa na mashetani kama Muhammad wa kwenye Quran?
1 Petro1:10-11 “Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta tafuta na kuchunguza chunguza ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi. Wakatafuta ni wakati upi na wakati wa namna gani ulioonywa NA ROHO WA KRISTO ALIYEKUWA NDANI YAO ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaokuwako baada ya hayo…..” (maneno ya msisitizo kwa herufi kubwa ni ya mwandishi)
Ufunuo 19:10 “Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndiyo roho ya unabii”
Biblia Takatifu imetuonya kuwachunguza mitume na manabii. Katika kitabu cha Ufunuo 2:1-2 “ Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu. Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao siyo ukawaona kuwa waongo”
Kwa mujibu wa aya hizi Muhammad s.a.w hastahili kuitwa nabii na mtume wa Mungu wa Kweli, bali anaangukia katika kundi la manabii na mitume wa uongo.
Mungu awabarikisana, na tuendelee kujifunza kweli, na kweli itatuweka huru.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries Org.

ISLAM, QURAN AND 666

"The truth is that This Quran is the 666 , The Book from The Lord of the Universe.
GOD made His Messenger a witness with the letter Qaf and the number 666."

The following links are to more Islamic sites that connect the Quran (Koran Kuran), and Islam's "Messenger", to the number 666. Scroll down (or Ctrl+f) on this link for the following quote:

"This book is the Quran; and the Quran is '666.'"


"They say, '666 is the sign of the Anti Christ, the sign of the Anti Church.' Obviously the Church has recognized the importance of the 666, they believe that the number represents a force that shall rise against them."

Since the false prophet Muhammad denied the whole subject of the Gospel.....

Surah 4:157 That they said (in boast), "We killed Christ Jesus the son of Mary, the Messenger of Allah";- but they killed him not, nor crucified him, but so it was made to appear to them, and those who differ therein are full of doubts, with no (certain) knowledge, but only conjecture to follow, for of a surety they killed him not:-

.....and his followers are commanded to conquer all kingdoms and subjugate all people to denying the Son of God and rejecting the blood He shed for us all, is it really a stretch to consider that Muhammad could be THEfalse prophet of the book of Revelation, and his Islamic kingdom "beast" the final foe of God's people?

Bukhari, V1 B2 #24 Narrated Ibn 'Umar: Allah's Apostle said: "I have been ordered (by Allah) to fight against the people until they testify that none has the right to be worshipped but Allah and that Muhammad is Allah's Apostle, and offer the prayers perfectly and give the obligatory charity, so if they perform a that, then they save their lives an property from me except for Islamic laws and then their reckoning (accounts) will be done by Allah."

Surah 9.29 Fight those who believe not in Allah nor the Last Day, nor hold that forbidden which hath been forbidden by Allah and His Messenger, nor acknowledge the religion of Truth, (even if they are) of the People of the Book, until they pay the Jizya with willing submission, and feel themselves subdued. 30 The Jews call 'Uzair a son of Allah, and the Christians call Christ the son of Allah. That is a saying from their mouth; (in this) they but imitate what the unbelievers of old used to say. Allah's curse be on them: how they are deluded away from the Truth!

Links to sections on this page include The 666 BeastThe Tragedy of the Mark and Saved By the Grace of God.
Here's a link to a 9 minute video regarding that site.
Here's a video of a Muslim that has 666 written on the page edges of his Quran.

"The sum of sura numbers from Sura 1 to Sura 36 is 666 (Table 7)."

Revelation 13:18 Here is wisdom. Let him that hath understanding count the number of the beast: for it is the number of a man; and his number [is] Six hundred threescore [and] six.

Not such a surprise for a Christian to find an association when we learn that the single most egregious and only unforgivable sin in Muhammadanism, is committed if a Muslim were to confess that Jesus is the Son of God or even pray in Jesus' name. As compared to child rape or cold-blooded mass murder, for example, which may be forgiven. (more on Islam's sin of "shirk")
 
"Allah" = 666 (link to this spot)

On the Zola Levitt program, Walid Shoebat, a former PLO terrorist now Christian evangelist, said that when he saw the Greek symbol that is translated in the Bible as 666, he immediately read it as the Arabic character “Bismillah” (some spell Bismilla) which means "in the name of Allah." (Though it looks more like the character for "Allah").

Here's a seven minute video of Walid Shoebat on 666 at a different venue:

Below (left) are photos of Greek symbols translated in the Bible as 666, from Free Jesus.net:  The gold symbol(bottom and right) is Arabic for "Allah" when turned and mirrored.  Additionally, crossed swords are a symbol for Islam.  So in 666 we may find symbols for both "Islam" and "Allah".


If Shoebat's account seems a stretch, even though Arabic was his first language and Islam the religion he was indoctrinated into, consider how this Arabic character is stylized into many different artistic forms.  Consider also how some look for this character in trees, clouds and virtually everywhere, as this search link attests - even in a fish!

Can you make out the word in the picture below?

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW