Thursday, September 24, 2015

OVER 700 PEOPLE DEAD IN MECCA: Graphic photos from Mecca stampede


Over 700 people died today in Hajj stampede in Mecca. Thousands were walking to the 'stoning of the devil' ritual when a sudden surge in the crowd caused many to fall. What caused the surge is not known. It's the worse since 1990. AFP just released some gruesome photos from the incident. 


Wednesday, September 23, 2015

Mabinti wa Allah

Mabinti wa Allah


Mara nyingi Waislam wamekuwa wepesi kuwaambia watu wengine kuwa Mungu ameruhusu Biblia kupotoshwa. Kitu wanachodokeza ni kuwa Kurani leo hii ni neno la Mungu lenye kuaminika wakati ambapo Biblia sivyo. Biblia ina maandiko yanayotofautiana mengi yenye tofauti ndogo, lakini ushahidi wa mabadiliko ya mafundisho hauna uzito. Kurani ina ushahidi mkubwa zaidi wa kupotoshwa kwa mujibu wa Ubai, aya zilizobatilishwa‘Uthman, na matatizo mengine ya Kurani. Hata hivyo, tofauti kubwa zaidi ya mafundisho ya Kurani, iliyoletwa na Waislam wenyewe, ni "mabinti wa Allah."

Muhtasari

Tovuti ya Kikristo http://answering-islam.org/Responses/Saifullah/sverses.htm inasema, "Moja ya matukio yenye kuaibisha zaidi kwenye maisha ya Muhammad lilitokea wakati Shetani alipoweka maneno yake kwenye mdomo wa Muhammad. Muhammad alisema maneno ya Shetani kama neno la Mungu. Tukio hili limethibitishwa kwa maandishi na waandishi kadhaa wa Kiislam wa kale na limeongelewa kwenye Hadithi na Kurani. Waislam wa miaka iliyofuata, kwa kujisikia aibu kuwa nabii wao aliyejitangaza mwenyewe amesema maneno ya Shetani, walikana kuwa tukio hili lilitokea. Visingizio na kukana kwingi vimekuwa vikitolewa na hawa Waislam wa miaka iliyofuata ili kulifunika kosa lenye kuhusisha dhambi la Muhammad.
Ni muhimu ikafahamika tena kuwa tukio la ‘Aya za Shetani’ si jambo ambalo limetungwa na watu wasiokuwa Waislam. Tukio hili limerekodiwa na vyazo vya kale zaidi vya Kiislam vilivyokuwepo wakati wa uhai wa Muhammad. Mtu yoyote asifikiri kuwa jambo hili ni hadithi iliyotungwa na watu wenye kuupinga Uislam. Ni kisa kinachopatikana moja kwa moja kwenye rekodi za kale za Kiislam.
Hili moja ya masomo yenye kubishaniwa zaidi kwenye Uislam. Shetani alimsababishia Muhammad kunena maneno yake (Shetani) kama maneno ya Mungu."

Je Kurani Ilisema Nini Mwanzoni?

Sura ya Nyota (Sura 53) mistari ya 19-20 inasema, "Je umemwona Lat, na ‘Uzza, Na mwingine, (mungu mke) wa tata, Manat?"

Allah alikuwa maarufu huko Arabia kabla ya kuja kwa uislam, kama mungu aliyekuwa na mabinti watatu: al-Lat, al-Uzza, na Manat. (Kumbuka kuwa al- inamaanisha ‘yule’, kwa Kiingereza "the".)

Waandishi wanne wa mwanzo wa maisha ya Muhammad waliandika kuwa awali aya hizi zilifuatwa na:

"Hawa ni mawinchi (wasuluhishi) ambao maombi yao yanapaswa kutumainiwa"

Tafsiri: Mabinti wa Allah walifikiriwa kuwa viumbe wa mbinguni wenye kuomba kwa ajili ya wengine. Mawinchi marefu ya Kinumidia ilikuwa ni sitiari yao. Maneno mbadala ya "inatakiwa kutumainiwa" (turtaja) ni "imekubaliwa kwa kuthibitishwa" (turtada). (Kutoka kwenye tafsiri ya Alfred Guillaume ya The Life of Mohammed, iliyoandikwa na Ibn Ishaq, uk.166.

Baadaye, kifungu hiki kiliondolewa na kifungu kifuatacho kiliwekwa badala yake:

"Nini! Kwako wewe mwenye jinsia ya kiume, Na kwake (mwanaume), mwanamke? Tazama, hakika mgawanyo huu hautakuwa wa haki kabisa." (aya za 53:21-22 leo)

Tafsiri: Wale wanaoamini kuwa Allah alikuwa na mabinti watatu hawakuntendea haki Allah, kwa sababu walipendelea watoto wa kiume ingawa walisema kuwa Allah alikuwa na wasichana tu.

Hizi ndizo ambazo zimeitwa "Aya za Shetani." Katika nyakati za sasa Salmon Rushdie alitumia msemo huu tu kwenye kichwa cha riwaya yake ya kubuniwa na isiyohusika na aya hizi, na andiko hili halikiongelei kisa hiki cha kisasa. Kwa upande wa Aya za Sheatani za asili, Muislam au mtu mwingine asiyekuwa Muislam mwenye kutazama jambo hil bila upendeleo anawezaje kujua aya ambazo zilikuwemo toka awali? Sehemu iliyobaki ya andiko hili inatoa ushahidi wa moja kwa moja na ule usio wa moja kwa moja kuwa Aya za Shetani zilikuwemo asilia, na mapingamizi tisa ya Kiislam.

Waandishi Wanne wa Maisha ya Muhammad: Ushahidi wa Moja kwa Moja

Ingawa si kila kitu Waislam wa kale walichosema kuhusu Muhammad kilikuwa kweli, wanazuoni wa kiislam wana uwezekano mkubwa zaidi wa kukubali mambo ambayo Muhammad aliyasema ambayo yameshuhudiwa na vyanzo vitatu au zaidi. Tunajua kuwa Aya za Shetani hazikutokana na vyanzo visivyokuwa vya kiislam, lakini kutoka wanazuoni wanne tofauti wa kale wa kiislam ambao walikuwa waandishi wa maisha ya Muhammad. Kumbuka kuwa watatu kati ya waandishi hawa walisimulia maisha ya Muhammad hata kabla ya mkusanyiko mashuhuri wa Hadithi ambao dhehebu la Kiisuni limejengeka juu yake.

Al-Wahidi/Wakidi (aliyekufa mwaka 207/823 BK) aliandika Asbab al-Nozul. "Kwenye siku fulani, wakuu wa Maka, walikusanyika kwenye kundi pembeni mwa Kaaba, walijadili kama ilivyo kawaida ya mambo ya mji wao; wakati Muhammad alipotokea na, kukaa karibu yao kwa namna ya kirafiki, alianza kusema sura 53 huku wakimsikia…. ‘Na usimwangalie Lat na Ozza, na Manat wa tatu zaidi?’ Alipofika kwenye aya hii, mwovu alipendekeza njia ya kujieleza mawazo yake ambayo iliitawala nafsi yake kwa siku nyingi; na aliweka mdomoni mwake maneno ya upatanisho na masikilizano, ufunuo aliokuwa anausubiri kwa hamu kubwa sana toka kwa Mungu, yaani; ‘Hawa ni wanawake waliotukuka, na hakika maombezi yao yanatakiwa kutumainiwa. ’ Wakoreish walishangazwa na kufurahishwa na kukubaliwa huku kwa miungu yao; na kama Mahomet alivyoimalizia Sura kwa maneno ya hitimisho ‘Kwa hiyo inama mbele ya Mungu, na mtumikie’ kusanyiko zima lilijiinamisha kwa moyo mmoja chini na kuabudu. … Jioni Gabriel alimtembelea; na nabii aliisema Sura hiyo kwake. Na Gabriel alisema, ‘Umefanya kitu gani? Umeyarudia mbele ya watu maneno ambayo sikuwahi kukupa’. Kwa hiyo Muhammad alisononeka zaidi …"

Ibn Sa’ad/Sa’d (aliyekufa mwaka 230/845 BK), aliifahamu kazi ya al-Wahidi lakini yeye mwenyewe alikuwa mwandishi wa habari za maisha ya watu aliyeandika kitabu chenye juzuu 15 kiitwacho Kitab al Tabaqat al Kabir.

Ibn Isaq/Ishaq (aliyekufa mwaka 145/767 au 151/773 BK) alikuwa Msuni wa mlengo wa Kishafi ambaye baadaye alianzisha shule yake mwenyewe iliyodumu kwa muda mfupi. Aliandika kitabu kiitwacho Sirat Rasullallah (Maisha ya Nabii wa Allah). "[Wahamiaji] walibakia sehemu ileile waliyokuwepo [Ethiopia] hadi waliposikia kuwa watu wa Maka wameukubali Uislam na wamejinyenyekeza. Hii ilikuwa ni kwa sababu sura ya Nyota [Sura 53] ilikuwa imetumwa kwa Muhammad na mtume aliinena. Mtu mmoja Muislam na mwenye kuamini miungu wengi alisikiliza kimya hadi alisema maneno haya ‘Je umemwona al-Lat na al-uzza?’ Walimsikiliza kwa uangalifu sana wakati waumini walimwamini [nabii wao]. Baadhi yao waliiasi imani yao walipoisikia ‘saj’ ya Shetani na kusema, ‘Kwa uwezo wa Allah tutawatumikia (mawinchi) ili kwamba watulete karibu na Allah.’ Shetani alifundisha aya hizi mbili kwa kila mtu aliyekuwa anaamini miungu wengi na ndimi zao zilizielewa kwa urahisi. Jambo hili lilimsunbua Mtume hadi Gabriel alipokuja kwake na kulalamika …." (Anaelezea mlolongo wa kuenea kuwa Yazid bin Ziyad-> Muhammad bin Ishaq -> Salama -> Ibn Hamid -> ibn Isaq

Ibn Jarir al-Tabari (aliyekufa mwaka 923 BK) alikuwa Msuni wa mlengo wa Kishati aliyeandika kitabu chenye juzuu 38 cha Kiislam cha Historia ya ulimwengu hadi mwaka 915 BK. Alipewa jina la "shehe wa wafafanuaji." Anaandika kwenye juzuu ya 6 uk.108-110, "Mjumbe wa Mungu alipoona jinsi kabila lake lilivyomkataa na kuhuzunishwa alipowaona wanauacha ujumbe aliowaletea toka kwa Mungu, alitamani moyoni mwake kuwa kitu chochote kimjie toka kwa Mungu ambacho kitampatanisha na kabila lake …. Na alipoyafikia maneno: ‘Je umewafikiria al-Lat na al-Uzza na Manat, wa tatu, Yule mwingine?’ Shetani alimlaumu, kwa sababu ya midahalo yake ya ndani na vitu alivyokusudia kupeleka kwa watu wake, maneno: ‘Haya ni mawinchi yanayopaa juu zaidi; hakika maombezi yao hupokelwa kwa kuthibitishwa [kwa mpokezano: kuhitajiwa au kutegemea].’ Waquraysh waliposikia hili, walifurahi sana na kupendezwa na namna alivyosema kuhusu muingu yao, na walimsikiliza, wakati Waislam, wakiwa wanamwamini kabisa nabii wao kuhusu ujumbe aliouleta kutoka kwa mungu, hawakumshuku kuwa amepotoka, anaota, au kafanya makosa. … Kisha [baadaye] Gabriel alikuja kwa Mjumbe wa Mungu na kusema, ‘Muhammad, umefanya nini? Umenena kwa watu kitu ambacho sikukuletea toka kwa Mungu …’"

Wanazuoni wa Kiislam wa miaka ya mbele waliosema jambo hili:
 Abu Ma’shar kutoka Chorassan (787-885 BH)
 Ibn Abi Hatim
 Ibn al-Mundhir
 Ibn Hajar from Asqalaan (773-852 BH)
 Ibn Mardauyah
 Musa ibn ‘Uqba
 Ufafanuzi mashuhuri sana wa Zamakhshari wa Sura 22:52. (1070-1143 BH)
Wanazuoni sita ni kwa mujibu wa kitabu kiitwacho The Book of the Major Classes, kilichotafsiriwa na S. Moinul ‘Haq.

Ushahidi usiokuwa wa moja kwa moja wa Aya za Shetani:
Kurani na Hadithi

Bukhari alikufa karibu na mwaka 870 BK (hata miaka mitatu baada ya vyanzo vitatu kati ya vinne vilivyoorodheshwa.) Wakati Muhammad alipoisema Sura ya Nyota, wapagani na Waislam walisujudu. (Bukhari juzuu ya 3 kitabu cha 19 na.173, uk.100 juzuu ya 3 kitabu cha 19, na.176, uk.101; juzuu ya 6 kitabu cha 60 na.385-386 uk.364-365; Abu Dawud juzuu ya 1 kitabu cha 2 sura ya 481 na.1401, uk.369). Wapagani hawasemekani kusujudu kwa ajili ya Muhammad kusema maneno mengine yoyote, ni kwa nini wakubaliane kiasi hiki na sura hii, hasa kwa vile Bukhari na Abu Dawud hawasemi kuwa hao wapagani waliwahi kuwa Waislam, na hii ilikuwa kabla ya vita na hawa wapagani wa Maka!

Pia, Sura 22:52 inasema, "Hatukuwahi kumtuma mtume au nabii Kabla yako, lakini, alipoumba nia, Shetani alimtupia (ubatili) kiasi kwenye nia yake: lakini Mungu atafuta kitu chochote (batili) ambacho Shetani anatupia ndani, na Mungu atafanya dhahiri (na kuthibitisha) Ishara Zake…"

Sura 17:73-75 inasema, "Na lengo lao lilikuwa kukujaribu na kukupeleka mbali na jambo tulilolifunua kwako, kuweka badala yake kitu tofauti kabisa kwa kutumia jina letu: (Kwa ajili hiyo), tazama! Watakuwa wamekufanya kuwa rafiki (yao)! Na je hatujakupa wewe, ungeweza kuelekea upande wao kiasi. Katika hali hiyo tulipaswa kukufanya uonje mara mbili (ya adhabu) kwenye maisha haya, na kiasi kama hichohicho mautini: na zaidi ya hapo usingepata mtu wa kukusaidia dhidi yetu!"

Tuesday, September 22, 2015

PICHA 10 TUKIO LA MAKANISA 3 KUCHOMWA MOTO BUKOBA

Makanisa yaliyochomwa moto ni Pentecostal Assemblies of God (PAG) kata bakoba eneo la buyekera,Living Water International na Evangelical Assemblies of God (EAGT) kata ya Kibeta yote ya mjini Bukoba. Chanzo chake hakijafahamika ambapo wachungaji na viongozi wa kiroho wanaomba vyombo vya dola kuwabaini wahusika.

kamanda wa polisi mkoani kagera Augstine Oromi amedhibtisha kutokea kwa tukio hilo na amemweleza mwandishi wa mtandao huu kuwa yupo katika ziara ya kazi wilayani ngara hivyo atatoa taarifa baadaye.

Matukio ya makanisa kuchomwa yameshamiri katika manispaa ya bukoba ambapo hili ni tukio la sita kwa kipindi cha mwaka mmoja










Saturday, September 12, 2015

UTATA: NUHU WA QURAN NI TOFAUTI NA NUHU WA BIBLIA

Ndugu Msomaji:
Siku zote Waislam huwa mnatutambia kuwa, Quran ni kitabu kilichoeleza kila kitu, ni kitabu ambacho kinajitosheleza, kitabu ambacho kimeshuka kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kuikandia BIBLIA, kuwa haitokanani na Mungu, sasa nitatoa aya mbili kutoka Katika BIBLIA, na kisha aya 2 kutoka ndani ya Quran, kisha nitawauliza swali,

GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA BIBLIA:Mwanzo 7:6 Naye Nuhu alikuwa mtu wa miaka mia sita hapo hiyo gharika ya maji ilipokuwa juu ya nchi.
BIBLIA ambayo mnasema haitokani na Mungu, imesema kuwa, Nuhu, alikuwa ni mwenye Umri wa miaka mia sita (600) GHARIKA lilipotokea, pia ikaeleza miaka ya NUHU baada ya Gharika.
Mwanzo 9:28 Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.

NUHU ALIKUFA NA MIAKA MINGAPI?29 Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
Tunaambiwa na BIBLIA kuwa, Nuhu aliishi miaka mia tatu na hamsini (350) baada ya gharika ya maji, akafa akiwa na miaka mia tisa na hamsini (950) HIYO NDIYO MIAKA ya maisha yote ya NUHU hakuishi zaidi ya miaka hiyo, sasa twende Quran kisha niulize swali.

GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA QURAN?Quran 29 وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَى قَوْمِهِ فَلَبِثَ فِيهِمْ أَلْفَ سَنَةٍ إِلَّا خَمْسِينَ عَامًا فَأَخَذَهُمُ الطُّوفَانُ وَهُمْ ظَالِمُون
َ14. Na bila shaka tulimpeleka Nuhu kwa watu wake na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka hamsini, basi mafuriko yakawaangamiza hali walikuwa madhalimu.

فَأَنجَيْنَاهُ وَأَصْحَابَ السَّفِينَةِ وَجَعَلْنَاهَا آيَةً لِّلْعَالَمِين
َ15. Na tukamuokoa yeye na watu wa (ndani ya ) safina, na tukaifanya (iwe mazingatio kwa walimwengu).

MADA KAMILI:BIBLIA imesema, Gharika limetokea Nuhu akiwa na miaka 600 Quran inasema, Gharika la Nuhu limetokea akiwa na miaka 950, sawa na miaka ya kufa kwa Nuhu, kwa mujibu wa BIBLIA, Biblia imesema, Nuhu akaishi miaka 350 baada ya Gharika, akafa na miaka 950 sawa na miaka ya gharika la Nuhu wa Ndani wa Quran.

MASWALI:-
1. Kwa kuwa ndani ya Quran, Nuhu alikuwa na miaka 950 Ndipo gharika likaja, na Biblia imesema ni miaka 600 gharika lilipokuja, na akafa akiwa na miaka 950 Sasa kwa mujibu wa Quran, Nuhu aliishi miaka mingapi kutoka katika Miaka hiyo 950 ya gharika?
2. au alikufa mwaka huo huo wa Gharika, akiwa na miaka hiyo 950 tuliyoambiwa alikuwa nayo wakati wa gharika ndani ya Quran?

NB. Majibu yatokane na Quran, tu kitabu ambacho mnatuambia ni cha Mungu, kama hakijitoshelezi, semeni, niwape ruhusa mtumie hata magazeti, na majarida.

Imeratibiwa na Abel Suleiman Shiliwa

For Max Shimba Ministres 

By Permission 2015

TAARIFA KUHUSU AJALI ILIYOTOKEA KWENYE MSIKITI MKUU WA MECCA SAUDI ARABIA

Hii taarifa imegusa Vichwa vya Habari vya Vyombo vingi vya habari Duniani, inahusu ajali ambayo imetokea wakati watu wakiwa ndani ya Msikiti Mtakatifu wa Mecca, Saudi Arabia ambako waumini wengi wa Dini ya Kiislamu huwa wanakwenda kwa ajili ya Hijjah.Ajali hiyo inahusisha winch kubwa ambalo lilikuwa likitumiwa kwenye ujenzi eneo la jirani na Msikiti huo kuangukia Msikiti huo, ambapo kwa wakati huo kulikuwa na watu zaidi ya 800 wakiendelea na sala ndani ya Msikiti.
Mecca II
Kumekuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa watu wanaoenda kwenye Msikiti huo kutokana na maeneo yanayozunguka Msikiti kuna majengo mengi yanayoendelea kujengwa na kukarabatiwa pamoja na Msikiti wenyewe kufanyiwa ukarabati wa upanuzi ili kuweza kungiza watu wengi zaidi.
Mecca
Mpaka sasahivi Ripoti zinaonesha zaidi ya watu 100 wamefariki, wengine zaidi ya 200 wamepata majeraha na Mamlaka za Mji huo wanasema sababu hasa za winch hilo kuanguka inatokana na upepo mkali pamoja na mvua kubwa.

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW