Saturday, May 31, 2014

Saying “KAFFIR” is a punishable offence in South Africa

Extracts from legal and court papers below:
REPORTABLE
IN THE HIGH COURT OF SOUTH AFRICA
(EASTERN CAPE, GRAHAMSTOWN)

CASE NO: CA 165/2008
In the matter between
MIETA M RYAN Appellant

VS
RODWIN PETRUS Respondent
JUDGMENT
PICKERING J:
turn then to consider the words uttered by defendant. It will be convenient to commence with the use of the highly offensive word “kaffir”.
As far back as 1976 James JP in Ciliza v Minister of Police and Another 1976 (4) SA 243 (N), after having referred to various dictionary definitions of the word, stated at 247H:
It follows that in my opinion one of the recognised meanings which the word ‘Kaffir’ now bears in South Africa is that such a person is uncivilised, uncouth and coarse and that if one calls a person a ‘Kaffir’ this will in certain circumstances constitute an iniuria.
In that matter a white policeman had used the word in addressing the plaintiff, who was a black man. Plaintiff was awarded the sum of R150,00 as damages.
In Mbatha v Van Staden 1982 (2) SA 260 (N) the plaintiff, a black man, sued the defendant, a white man, for iniuria after the defendant had repeatedly called him a “kaffir” and assaulted him. At 262 H – 263A Didcott J stated as follows:
The tirade’s worst feature was the use of the epithet ‘kaffer’. Such alone can amount today to an actionable wrong, according to the decision of the Full Bench here in Ciliza v Minister of Police and Another 1976 (4) SA 243 (N). Everything depends, of course, on the context in which the word is uttered. Settings which make it innocuous can no doubt be imagined. Ordinarily, however, that is not the case when, in South Africa nowadays, a Black man or woman is called a ‘kaffer’ by somebody of another race. Then, as a rule, the term is a derogatory and contemptuous one. With much the same ring as the word ‘nigger’ in the United States, it disparages the Black race and the person concerned as a member of that race. It is deeply offensive to blacks. Just about everyone knows that by now. The intention to offend can therefore be taken for granted, on most occasions at any rate.
The plaintiff was awarded the sum of R2 000,00 as damages.

In S v Puluza 1983 (2) P.H. H150 (E) van Rensburg J (with whom Jennett AJ concurred) referred with approval to the Ciliza andMbatha cases, supra and added:
(W)hen a black man is called a ‘kaffir’ by somebody of another race, as a rule the term is one which is disparaging, derogatory and contemptuous and causes humiliation.
See too: S v Steenberg 1999 (1) SACR 594 (N).
In the present case neither party is a black African. It may well be that if the word is uttered pejoratively by a white person to a black person the amount of damages which would be awarded to compensate the latter for the affront would be greater than when the recipient of the insult was not a black African, because of the racial overtones involved. It is, however, not necessary to determine this issue. In the present case it is abundantly clear from the context in which the word was used that defendant intended to give offence and used the word in its injurious sense of uncivilised, uncouth and coarse. As was stated in Ciliza’s case, supra at 248H such a use of the word constitutes an unlawful aggression upon appellant’s dignity.
 ***    ****   ****
The actio injuriarum is a civil claim where a wronged party sues for monetary compensation.
Race based insults that are directed at individuals have traditionally been dealt with under this head. For example, compensation was given to a victim for derogatory use of the word ‘kaffir’ in Mbatha v Van Staden.
Racist insults can also be criminal and result in criminal penalties and a criminal record. ‘[P]rovided the required intention is proved, … calling a person a ‘kaffir’ is a violation of that person’s dignitas and constitutes the crime of crimen injuria’.
  

Sauti ya Kuzimu

Kikundi cha wanajiolojia watafiti

Katika makala haya, tutaangalia jinsi wanasayansi wa kawaida, tena ambao walikuwa hawaamini  kabisa kwamba kuna Mungu au shetani, katika utafiti wao ambao haukuwa na uhusiano wowote na masuala ya rohoni, walijikuta wanagundua mambo ambayo yaliwatia hofu hadi wengine kukimbia kazi. Waliweza kusikia waziwazi sauti za vilio vya mateso kutokea katikati ya dunia! Sauti hizo walizirekodi; na mwisho wa makala haya utaona anwani inayoweza kukupeleka kuzisikia sauti hizo za kutisha na kusikitisha mno, mno!!

Ni nani ambaye hajasikia habari za kwamba wanga huenda baharini, wakatupa mayai viza kisha malango yanafunguka nao wanashuka hadi kuzimu? Bila shaka habari hizi si ngeni masikioni mwa wengi wetu? Ni mambo ambayo ni rahisi kuaminika katika ulimwengu wa kawaida lakini unapoyaongelea kwa mtazamo wa Biblia, hapo watu wanaanza kukosa imani na kudhani kuwa si za kweli.

Makala haya yanatokana na habari ambayo iliandikwa katika gazeti la Ammennusatia la kule Finland katika toleo lake la Julai 1989.

       Sehemu ya gazeti

Kikundi kimoja cha wanajiologia (wana elimu ya miamba) wa Kirusi walikuwa katika mradi wa kutoboa tundu katika eneo la Kola, karibu na Murmansk; maili takriban 150 kaskazini mwa Duara la Aktiki, nchini Siberia. Watafiti hao waliweza kutoboa tundu ardhini lenye urefu wa kilometa 14.4 kwenda chini.

Saturday, May 17, 2014

YESU WA BIBLIA SIO ISSA WA KURUAN

YESU WA WAKRISTO SIO ISSA WA WAISLAM
****************************************************************************************
JE, ISA BIN MARYAM NI JINA SAHIHI LA YESU WA BIBLIA?
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Katika somo letu hili tutajifunza kuhusu jina sahihi la Yesu/Yashua na tafsiri yake katika Kiarabu. Je, Isa ni jina la Yesu wa Biblia?
Jibu sahihi la kihistoria na la wataalam wa kutafsiri litatupa ukweli halisi wa Jina la Yesu na kwanini alipewa Jina hilo katika " sherehe ya kumtaja " (Luka 2:21). Jina ambalo aliitwa na Mama yake, Baba yake wa Kambo, Ndugu zake na jamaa wengine, majirani zake , marafiki zake na wanafunzi wake wakati wa maisha yake duniani. Hakuna kutokuelewana kuhusu ukweli kwamba jina la Yeshua halikuwa la Kiarabu bali la Kiyahudi na Yesu/Yeshua mwenyewe aliishi katika Israeli, na alizaliwa katika familia ya Wayahudi wacha Mungu.

Jina la Yesu bila ya shaka yeyote ile ni la Kiyahudi. (Maana yake ni “kweli”). Tafsir ya jina la Yeshua Kiebrania katika Kiingereza itakuwa ni Jesus. Jina la Yesu halikuchaguliwa kiholela na wazazi wake, lakini yeye alipata jina lake moja kwa moja kutoka kwa Mungu (Mathayo 1:21 , Luka 1:31) kwa sababu ya maana ya jina lake na nani alilileta, basi leo hii tunaelewa madhumuni ya Yesu kuzaliwa na kuja hapa duniani (Mathayo 1:21 ).

Katika utamaduni na jadi ya Kiarabu. Jina la Yesu ni Yasu na si Isa kama ilivyo andikwa kwenye Koran ya Kiislam. Na hata leo, jina la Yasu linatumiwa na zaidi ya 99.99% ya Wakristo wote wa Kiarabu. Tembea katika kanisa lolote la Kiarabu huto sikia wanatumia jina la Isa, Sikiliza matangazo ya Wakristo wa Kiarabu katika Radio na Televisheni (za Kiarabu) huto sikiwa Mkristo anatumia jina la Isa, bali wanatumia jina la Yasu. Matangazo yote ya Kikristo katika Uarabu wanatumia jina la Yasu. Kamwe huto ona jina la Isa kama lilivyo kwenye Koran ya Waislamu.

Katika jadi ya Kiarabu na utoaji wa tafsiri wa jina, jina sahihi la Kiebrania (Yeshua) ni Yasu katika Kiarabu. Kila uchaguzi wa tafsiri ya jina la kigeni katika lugha tofauti ni uvumbuzi wa binadamu.
Kiisimu ipo wazi jinsi jina la Yeshua Kiebrania lilivyo tafsiriwa na kuwa Yesu Kiswahili na Jesus Kiingereza:

Yeshua '(Kiebrania) -> Ιησους (Kiyunani) -> Yesu (Kilatini) -> Jesus (Kiingereza) -> Yesu (Kiswahili).

Tuesday, May 13, 2014

UKANAJI MUNGU NI NINI?

“Ukanaji Mungu wazi,” pia waitwa “theolojia wazi” na uwazi wa Mungu,” ni jaribio la kuelezea ufahamu kuhusu Mungu kulingana chuguo huru la mwanadamu. Pingamizi la ukanaji Mungu wazi hasa ni huu: wanadamu wako huru kabisa; ikiwa Mungu alijua hatima, wanadamu hakika hawangekuwa huru. Kwa hivyo, Mungu kabisa hajui kila kitu kuhusu kesho. Ukanaji Mungu wazi washikilia kuwa kesho haijulikani. Kwa hivyo Mungu anajua kila kitu ambacho kinaweza julikana, lakini hajui kesho.


Ukanaji Mungu wazi waweka imani yao katika misingi ya kurasa za maandiko ambazo zaelezea Mungu “anabadilisha mawazo yake” au “kushangaa” au “kuonekana kupata hekima” (Mwanzo 6:6; 22:12; Kutoka 32:14; Yona 3:10). Kwa mwangaza wa maandiko mengine mengi ambayo yaelezea ufahamu wa Mungu wa kesho, maandiko haya lazima yaeleweke kama Mungu anajielezea kwa njia ambazo hatuwezi kuzielewa. Mungu anajua vile hatua zetu na maamuzi yatakuwa, lakini “Anabadilisha mawazo yake” kulingana na hatua yake ikitegemea hatua yetu. Chukizo la Mungu katika unyonge wa mwanadamu haimanishi kwamba hakujua kuwa hayo yatatokea.

Kwa hitalafiano na ukanaji wa Mungu wa wazi, Zaburi 139:4,16 yasema, “Maana hamna neno ulimini mwangu usilolijua kabisa, BWANA. Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.” Mungu angewezaje kutabiri mambo tatanishi katika Agano La Kale kuhusu Yesu Kristo kama hajui siku za usoni? Ni namna gani Mungu kwa njia yo yote ile anaweza kuruhusu wokovu wetu wa milele kama hajui chenye kesho imetubebea?

Mwisho, ukanaji Mungu wa wazi unaanguka kwa vile unajaribu kuelezea yenye hayawezi kuelezeka- uhusiano kati ya ufahamu wa Mungu na penzi huru la mwanadamu. Vile aina ya Kikalvinisti yakaenda kupita kiwango yalivyoanguka ya kuwa yakataa uwepo wa Mungu kila mahali na uwezo wake. Mungu lazima yaeleweke kupitia kwa imani, kwa maana “bila imani ni vigumu kumpendeza Mungu” (Waebrania 11:6a). ukanaji Mungu wa wazi kwa hivyo si wa kiroho. Ni njia nyingine ya mwanadamu aliye na hatima kujaribu kuelewa Mungu asiye na mwisho. Ukanaji Mungu wazi lazima ukataliwe na wafuasi wa Kristo. Huku ikiwa ukanaji wa Mungu wa wazi ni elezo la uhusiano kati ya ufahamu wa Mungu kabla ya uumbaji na penzi huru la mwanadamu, sio elezo la kibibilia.

Monday, May 12, 2014

USHAIDI WA BIBLIA NA KURUAN (SEHEMU YA PILI)


Ndugu wasomaji: Leo ningependa tujifunze sifa za Mungu kupitia Biblia na Kuruani kama ushaidi zaidi wa Umungu wa Yesu.

Hapa chini nitaziweka sifa na au adhama za Mungu na tutaziangalia kama hizo zote zipo kwa Yesu Kristo.

1 Mungu ni wa milele
2 Mungu ndiye muumbaji,
3 Mungu yupo mahali popote,
4 Mungu ndiye anaye samehe dhambi za watu,
5 Mungu anajuwa na kufahamu yote hata yaliyomo mioyoni mwetu,
6 Mungu ni Nuru ya Mbinguni na Duniani
7 Mungu ndiye anaye watuma Mitume na Manabibii!
8 Mungu anauwezo wa kujidhihilisha (kuonekana) na tena mngu ni wa sili (kuto onekana)

JE, YESU WA KWENYE BIBLIA ANAZO HIZO SIFA?

1 MUNGU NI WA MILELE
Quran 2:255, Sifa ya milele ni ya Mungu pekee Je Yesu hiyo sifa unayo?
Waebrania 13:8 Yesu Kristo ni yeye yule jana na leo na hata milele,
Sifa ya Umilele teyari Yesu amesha inyakuwa.

2 MUNGU NDIE MUUMBAJI
Je, hii sifa ya Uumbaji Yesu wa Biblia anayo?
Quran 5: 110. Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!

Friday, May 9, 2014

KWA NINI NAKATAA KUWA MWISLAMU?

Katika ulimwengu wa leo kuna njia nyingi za kutumaini. Furaha ya milele na Mbinguni vina hubiriwa kila mahali. Hata hivyo kuna dini nyingi tofauti, filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo (furaha ya milele) vinatofautiana. Na kila mmoja katika tofauti hizo za dini na filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo; anaamini ya kuwa amesimama katika ukweli.
Katika Surat Maryam, Kuruan inasema kuwa (19) 71.72. Inasema, wala hapana yoyote ila mwenye kuifikia jehanamu, maana ni wajibu wa Mola wako umekwisha kuhukumiwa, nasi tutawaokoa wale wamchao na kuwaacha madharimu hali wamepiga magoti.
Kuruan inakiri kuwan kila bin-adam amekwisha hukumiwa kuingia Jehannam kwa maana huo ndio wajibu wa Allah kuwaingiza watu Jihannam. Allah anaendelea kusema kuwa, yeye atawaokoa Waislam baada kuingia Jehanam. Je, haya madai ni kweli?
Quran 40: 60. Na Mola wenu Mlezi anasema: Niombeni nitakuitikieni. Kwa hakika wale ambao wanajivuna na kuniabudu Mimi wataingia Jahannamu wadhalilike.
Katika Surat Ghaafir inakiri kuwa Alla anaendelea kusema kuwa Waislam wote wataingia Jehannam. Mimi kama Mkristo siwezi kuipenda dini hii ambayo teyari mungu wake amesha toa hukumu ya kwenda Jehannam kwa wote wanao ufuata Uislam.
Zaidi ya hapo, katika Surat Maryam, Allah ameshindwa kutueleza ni kivipi atawatoa watu Jehannam, bali ameweka madai tu kuwa atakuja huko na kuwatoa Waislam.
Bukhari :: Kitabu 6 :: Juzuu 60 :: Hadith 371
Imeletwa kwenu na Anas:
Nabii wa Allah alisema: Watu watatupwa katika Jihannam, na Jihannam itasema. "Je, hakuna watu zaidi wa kuingia huku Jehannam?" (50.30) Mpaka Allah atakapo weka Mguu wake Jehannam, na Jihannam itasema, Inatosha, inatosha (qat! qat!)

YESU NDIE NJIA NA KWELI NA UZIMA!

Katika ulimwengu wa leo kuna njia nyingi za kutumaini. Furaha ya milele na Mbinguni vina hubiriwa kila mahali. Hata hivyo kuna dini nyingi tofauti, filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo (furaha ya milele) vinatofautiana. Na kila mmoja katika tofauti hizo za dini na filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo; anaamini ya kuwa amesimama katika ukweli.

Na maisha ya mwanadamu yamefikia mawazo ya hali ya juu. Wengi wetu wanapenda kuishi katika dunia hii kwa muda mrefu iwezekanavyo. Baadhi yao wanategemeo la kuishi milele katika dunia hii.

Lakini kuna njia moja tu ya kumuingiza mtu katika furaha ya kweli ya milele. Kuna ukweli mmoja tu, umfanyao mtu kuwa huru. Kuna namna moja ya maisha itakayomfikisha mtu katika uzima wa milele. Yesu Kristo Mwana wa Mungu, ndiyo “Njia, na Kweli na Uzima.” Kumbuka Yesu mwenyewe alisema, “Mimi ndimi njia na kweli na uzima; mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya Mimi,” Yoh. 14:6. 

Na Yesu Kristo ni “Njia na Kweli na Uzima.” Kwa sababu Yeye alikufa kwa ajili ya dhambi zetu. Wote wametenda dhambi kwa kuiasi Sheria ya Mungu (Rum 3:23; 1 Yoh 3:4). “Na mshahara wa dhambi ni mauti,” Rum 6:23. Hii ndiyo mauti ya pili au Jehanamu (Ufu. 21:8; Mat. 10:28). Kwa sababu ya dhambi zetu tulistahili adhabu ya milele katika Jehanamu, lakini kwa sababu ya upendo mkuu wa Mungu na rehema zake alimtoa mwanawe Yesu Kristo akafa msalabani akalipa deni letu la dhambi zetu (Yoh. 3:16-17; Rum. 5:5-10; 6:17-23).

Tuesday, May 6, 2014

JE, NI HAKI KWA MKRISTO KUSALI(KUOMBA) JUMAPILI?

JE, KUNA USHAIDI WOWOTE ULE NDANI YA BIBLIA UNAO MRUHUSU MKRISTO KUSALI(KUOMBA) JUMAPILI?

Tafadhali ungama nami katika somo hili fupi ambalo lina leta utata mwingi sana kwa waaminio katika Kristo na hata wale wanao mfuta Allah.
Sasa rejea na soma hii aya hapa chini:
WALIKUTANA SIKU YA KWANZA YA JUMA:
Matendo 20: 7 Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.
Siku ya kwanza ya Wiki ni Jumapili na hii ni siku ambayo walio mwamini Yesu walikusanyika na kuabudu. Huu ni ushaidi wa kuonekana kwa macho ambao Wakristo wanaabudu Jumapili hivi leo na walifanya hivyo katika Karne ya kwanza.
1 Wakorintho Mlango 16 1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo. 2 Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;
Katika Wakorintho hapo juu tunasoma kuwa Watakatifu walikutana siku ya kwanza ya Juma ambayo ni Jumapili.
Ingawa kutokana na Warumi 14:1-12, tumewekwa huru kutokana na laana ya Sheria, hivyo basi, kusali si lazima iwe Jumamosi au Jumapili. Mungu hana utegemezi wa siku tena bali unaweza kusali siku yeyote ile na Mungu akakusikia na si lazima uwe kwenye Jengo ambalo tunaliita "Kanisa".
Biblia inaendelea kusema kuwa, tupo huru katika Kristo Warumi 6:14. Ndio maana tuanenda Kanisani katikati ya wiki na tunasali Mungu.
Zaidi ya hapo, kutokana na kuesabu masaa kwa kutumia kalenda ya Warumi, Siku huwa inaanza saa 6 za usiku, ndio maana Mwaka huwa unaanza Saa hiyohiyo ya 6 usiku. Hivyo basi kutokana na ushaidi wa aya hizi (Luka 11:5; Matendo ya Mitume 16:25; 20:7; 27:27) ni ushaidi tosha kuwa, Wakristo wa Kwanza walisali Jumapili na wali hesabu siku kuanzia saa 6 Usiku.
Katika agano la Kale tunasoma: Nehemia 8: 2 Naye Ezra, kuhani, akaileta torati mbele ya kusanyiko, la wanaume na wanawake, na wote walioweza kusikia na kufahamu, siku ya kwanza na mwezi wa saba.
Hapo tumesoma kuwa Kuhani alisoma Torati meble ya mkusanyiko katika Siku ya Kwanza.
SIKU ZOKE NI SAWA NA UNA HAKI YA KUABUDU:
Sasa soma aya hizi hapa chini kwa ufasaha:
Warumi 14.5 Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. 6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu.
Nduguzangu, kutokana na Warumi 14, tumewekwa huru kuchagua siku ya kuabudu, na nini tule au tusile, hivyo hivyo ni kuadhimisha kwa Bwana. Hivyo basi, hakuna kosa lolote lile mtu anapo sali Jumamosi au Jumapili au Jumatatu, au siku yeyote ile ya wiki. Mungu wetu yupo kila siku na siku zote alizumba yeye.
WALIKUTANA KILA SIKU HEKALUNI NA KUSALI:
Matendo ya Mitume 2: 46 Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,
Unaona hiyo aya hapo juu inavyo sema? Je, Jumatatu imekosekana kwenye hiyo aya, vipi kuhusu Jumanne? Ndio maana nilisema sisi tumewekwa huru kutokana laana ya sheria na sasa tupo huru kuabudu Mungu siku yeyote ile. Mungu si wa Jumamosi tu au Jumapili tu au Ijumaa tu. Mungu ni wa kila siku.
KWANINI UNAPENDA MAFUNZO AMBAYO NI DHAIFU?:
Wagalatia 4:8 Lakini wakati ule, kwa kuwa hamkumjua Mungu, mliwatumikia wao ambao kwa asili si miungu. 9 Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? 10 Mnashika siku, na miezi, na nyakati, na miaka.
Mtume Paulo anatukumbusha kuwa, mafunzo ambao tulikuwa tunayafuata kabla ya kukombolewa na Yesu yalikuwa dhaifu. Sasa tumejazwa na Roho Mtakatifu ambaye ndie Mwalimu wetu Mkuu.Basi tushikamane naye na tujifunze kutoka kwake.
Ni mategemeo yangu kuwa, somo hili litatufungua macho na tunasoma Biblia zaidi na kumwomba Roho wa Mtakatifu atufundishe yote.
Katika huduma yake,
Max Shimba Ministries Org.
1633 Broadway, 30th Floor, New York, NY 10019

Monday, May 5, 2014

NINI MAANA YA BIBLIA?

Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 vilivyo andikikwa na watu 40 katika lugha tatu kuu, na katika mabara Matatu, takribani miaka 1600 kabla na baada ya kuzaliwa Yesu. Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu na kisicho kuwa na makosa yeyote yale.

Biblia inabeba mambo mbali mbali ikiwa ni pamoja na Mashairi(Zaburi), Historia (Mwanzo), Sheria (Taurat) na unabii. Biblia ndio kitabu kinacho tumiwa na Wakristo na ndio muongozo wa Wakristo katika kumtafuta Mungu. Zaidi ya hapo, Biblia hutumiwa kama njia ya Binadamu kuishi hapa Duniani.

Kimsingi, Biblia inaeleza asili ya mtu katika bustani ya Edeni pamoja na kuanguka kwake katika dhambi na nje ya ushirika na Mungu. Kisha inaeleza jinsi Mungu alivyo waita watu wake maalum kwa mwenyewe, Israeli. Mungu katika Biblia aliahidi Masihi atakuja kwa Israel ili aje kuokoa na kurejesha uhusiano wa mwanadamu na Mungu. Yesu alizaliwa na Bikira, alikufa juu ya msalaba, na kulipwa kwa dhambi, huu unabii upo katika Agano la Kale na kutimizwa katika Agano Jipya. (Yohana 5:39).

Zaidi ya hapo, Biblia inatufundisha kusamehewa dhambi kupo katika Yesu pekee. Matendo ya Mitume 4: 12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Wengine wanasema kuwa Biblia ni kitabu zaidi za vitabu vyote vilivyo wai kuandikwa hapa duniani. Huu ushaidi unaweza kuwa ni kwasabau Biblia imetabiri mengi na mabo yote ambayo imetabiri yaliweza kuhakikisha na Wana Historia na Wanasanyi tulio nao hapa duniani.

Hivyo basi, Biblia ni kitabu kinacho beba maneno ya Mungu ambayo ndio msingu mkuu wa Ukristo.

Agano la Kale kilichoandikwa na manabii kama vile Musa, Daudi, Isaya , nk

Vitabu vya sheria - 5 vitabu:
Mwanzo, Kutoka, Walawi, Hesabu , Kumbukumbu
Vitabu vya Historia - vitabu 12 :
Yoshua, Waamuzi , Ruthu, Samweli , Pili Samuel , Wafalme , Pili Wafalme, Mambo ya Nyakati , Pili Mambo ya Nyakati, Ezra , Nehemia, Esta.
Mashairi - 5 vitabu:
Ayubu, Zaburi , Mithali, Mhubiri , Wimbo wa Sulemani
Kinabii - 17 vitabu:
Manabii kubwa - Isaya, Yeremia , Maombolezo, Ezekieli , Danieli;
Manabii Wadogo - Hosea, Yoeli, Amosi, Obadia, Yona, Mika , Nahumu, Habakuki , Sefania , Hagai, Zekaria , Malaki

Vitabu vya Agano Jipya vimeandikwa na wale ambao walimjua Yesu au walikuwa chini ya uongozi wa wale ambao walifanya kazi nae

Vitabu vya Historia - 5 vitabu:
Mathayo, Marko, Luka, Yohana, Matendo
Paulo Nyaraka - 13 vitabu:
Warumi, 1 Wakorintho, 2 Wakorintho , Wagalatia, Waefeso , Wafilipi, Wakolosai , 1 Wathesalonike, 2 Wathesalonike . 1 Timotheo, 2 Timotheo, Tito, Philemon
Mashirika yasiyo ya Paulo Nyaraka - 9 vitabu:
Waebrania, Yakobo, 1 Petro , 2 Petro, 1 Yohana, 2 Yohana , 3 Yohana, Yuda , Ufunuo
Kumbuka: Baadhi ya waandishi sifa Waebrania Paulo.

Katika Ezekiel 23:1-4 inasema, " neno la Bwana likanijia tena kusema, 2 " Mwana wa Mtu , kulikuwa na wanawake wawili, binti za mama mmoja; . 3 na wao ukahaba katika Misri Walicheza kahaba katika ujana wao; huko vifua vyao walikuwa taabu , na kuna karibu yao bikira alikuwa kubebwa 4 " majina yao , mkubwa aliitwa Ohola na Oholiba dada yake wakawa Mine, wakazaa wana na binti na kama kwa wao. . . majina, Samaria ni Ohola, na Yerusalemu ni Oholiba. "

Katika Huduma yake,

Max Shimba Ministries Org
1633 Broadway, 30th Floor, New York, NY 10019

Thursday, May 1, 2014

ROHO MTAKATIFU NA KAZI ZAKE KWETU


SOMO LA 1

ROHO MTAKATIFU,MTOA UTAKATIFU
Katika somo la kwanza katika mfululizo wa masomo haya yanayohusu Roho Mtakatifu,Tulijifunza kwamba Roho Mtakatifu,ni mtakatifu,hivyo anakuwepo na kudumu mahali palipo na utakatifu tu.Tukiwana maisha ya uchafu,yaani dhambi;humfanya Roho Mtakatifu akose makao kwetu,na hivyo hawezi kuwepo kwetu.Kama alikuwepo mwanzo kwetu,huondoka (1Samweli 16:14;
Zaburi 51:4,10-11).Sasa swali linakuja,tunawezaje kuwa watakatifu katika maisha yetu ili Roho Mtakatifu afanye makao
kwetu?Jibu ni kwamba,Roho Mtakatifu ,ndiye huyohuyo anayetoa utakatifu tunaouhitaji.Sasa tunamwangalia Roho
Mtakatifu kama Mtoa Utakatifu,kwa kutafakari kazi yake hiyo katika vipengere vitano:-
1. ROHO MTAKATIFU,ROHO ATUPAYE KUZALIWA MARA YA PILI
2. ROHO MTAKATIFU ROHO AWAFUFUAYE WATU WALIOKUFA KIROHO
3. ROHO MTAKATIFU, ROHO AWATIAYE UZIMA WATU WALIOZIMIA KIROHO
4. ROHO MTAKATIFU ROHO ATUPAYE UTAKASO
5. ROHO MTAKATIFU, ROHO ATUPAYE TUNDA LA ROHO

1. ROHO MTAKATIFU,ROHO ATUPAYE KUZALIWA MARA YA PILI
Hatupaswi kamwe kudanganyika kwamba utakatifu siyo duniani ni mbinguni,Maandiko yanaeleza waziwazi kwamba watakatifu walioko duniani ndiyo anaopendezwa nao Mungu(Zaburi 16:3). Hatupaswi pia kudanganyika kwamba tunaweza kufanya dhambi hapa duniani,halafu tukasalimika baada ya kufa,kutokana na misa ya wafu n.k(1Wakorintho 6:9-10;Waefeso 5:5-7;Wagalatia 6:7 ;Waebrania 9:27;IYohana 5:16;Kumbukumbu 10:17) la maana hapa ni kufahamu ni jinsi gani tunavyoweza kuwa na ushindi dhidi ya dhambi hapa duniani,na kuokoka kutupwa motoni,maana bila shaka tunatakiwa kuokoka tukiwa hapahapa duniani (Luka 19:8-10);Tito 3:3-4)Tunawezaje kuwa na ushindi dhidi ya dhambi?Ni kwa kuzaliwa mara ya pili,kwa Roho Mtakatifu(Yohana 3:3-10;Tito 3:3-5)Yesu Kristo,alijaribiwa sawasawa na sisi lakini hakutenda dhambi(Waebrania 4:14-15)Ni nini siri ya ushindi wake huo?Ni kwa sababu alizaliwa kwa Roho Mtakatifu,yaani alizaliwa tofauti na kawaida ya kimwili ya mume na mke.Sisi nasi tunapotubu dhambi
zetu kwa kumaanisha kuziacha,tunapata rehema hii kwa imani tu(Mithali 28:13)Tunazaliwa mara ya pili katika ulimwengu wa roho,na hivyo kuwa na uwezo wa kushinda dhambi kwa muujiza mkubwa.Katika hali ya kawaida ya jinsi tulivyozaliwa kimwili,kamwe hatuwezi kushinda dhambi.Ni mpaka tufanyike viumbe vipya kwa Roho Mtakatifu.Mwambie Roho Mtakatifu kwamba unataka kuzaliwa mara ya pili,naye atafanya.

2. ROHO MTAKATIFU ROHO AWAFUFUAYE WATU WALIOKUFA KIROHO
Kurudi nyuma na kuacha wokovu kunaitwa pia kufa kiroho(Ufunuo 3:1;Waefeso 2:1).Kwa kila aliyerudi nyuma na kuacha wokovu,hii ni saa ya kuamka usingizini na kuanza upya(Warumi 13:11-12).Lakini,je,inawezekana kuanza upya tena katika hali hii?Ndiyo,kwa msaada wa Roho Mtakatifu.Hii ni kazi yake nyingine .Roho Mtakatifu ndiye aliyemfufua Yesu,alipokufa(Warumi 13:11). Kwa jinsi hiyo hiyo,Roho Mtakatifu anaweza kutufufua kiroho
na kutupa uhai tena wa kiroho(Waefeso 2:1,4-6).Mwambie Roho Mtakatifu kwamba unataka kufufuliwa kiroho, naye atafanya.

3. ROHO MTAKATIFU, ROHO AWATIAYE UZIMA WATU
Kabla ya kufa kiroho,hutangulia kuzimia kiroho.Shetani hutupeleka hatua kwa hatua,kama upepo katika tairi unavyotolewa kidogo kidogo kutokana na pancha ndogo.Tukizimia kiroho,upendo wa kwanza unatoweka. Ingawa bado hatujafikia hali ya kufanya dhambi za uzinzi,uasherati,ulevi n.k kama mataifa,hata hivyo,mambo ya rohoni yanakuwa hayana mvuto kwetu kama mwanzo.Kuomba,kushuhudia,kuhudhuria ibada n.k,yanakuwa
mzigo kwetu.Tunaanza kuvutwa zaidi na mambo ya dunia.Katika hali hii tunahitaji nguvu mpya,uzima mpya (Isaya 40:28-31). Anayefanya kazi hii pia ni Roho Mtakatifu,Roho wa uzima (Warumi 8:2). Pepo wa udhaifu wanatolewa kwa Roho wa Mungu (Mathayo12:28), na vivyo hivyo udhaifu wetu kiroho unatolewa na Roho wa Mungu.Je umezimia kiroho,Mwambie Roho Mtakatifu akuzindue,naye atafanya.

4. ROHO MTAKATIFU ROHO ATUPAYE UTAKASO
Baada ya kuokolewa,tunahitaji pia kutakaswa.Bila utakaso,tutajikuta bado hatuna ushindi dhidi ya dhambi za ndani katika mawazo,na moyoni,ingawa tayari tuna ushindi dhidi ya dhambi za kutenda. Dhambi za ndani ,ni kama hasira, wivu ,chuki, masengenyo, kugombania ukubwa,kiburi,majivuno,kutokusamehe,kinyongo,
kupenda udunia n.k.Hivi vinaweza vikaonekana kwa watu waliookoka ambao hawajatakaswa: Mawazo yasiyo ya ki Mungu (Mathayo 16:21-23),kugombania ukubwa (Luka 22:24-26;Mathayo 20:20-22,25-28; Marko 9:30-37),hasira (Mathayo 20:24) wivu, fitina, ugomvi (Marko 9:38-39;Luka 9:49-50; 1Wakorintho 3:3-5), faraka na matengano(1Wakorintho1:10-13),umimi(Mathayo 28:6-13), kutokusamehe (Mathayo 18:21-35), chuki,kushindwa kuvumilia maudhi,kushtakiana wapendwa mahakamani (Luka 9:51-56; 1Wakorintho 6:1-8); Warumi 7:15 n.k .Mambo haya huondolewa kwa utakaso.

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW