Tuesday, April 30, 2013

Mpango Wa Wokovu ni nini?


Una njaa? Si njaa ya chakula, lakini je, una njaa ya kitu Fulani zaidi maishani? Je, kuna hali Fulani ya kutotosheka ndani yako? Ikiwa iko basi Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi mkate wa kweli. Kila ajaye kwangu hatahisi njaa na aniaminiye hataona kiu” (Yohana 6:35).

Je, umechanganyikiwa? Je, huoni mbele ya maishani mwako? Je, unajihisi kama umeachwa kwenye giza na huoni pa kutokea? Ikiwa hali yako ni kama hiyo basi Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi nuru ya ulimwengu. Anifuataye hatatembea gizani, bali atakuwa na nuru ya uzima” (Yohana 8:12).

Je, unajisikia kama umefungiwa nje ya maisha yako? Je, umejaribu njia nyingi na kutambua ya kwamba kile ulichokitarajia hakipo ndani yake? Je, unatafuta njia ya kufikia maisha makamilifu? Ikiwa haya ndiyo uyatafutayo, Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi mlango wa kondoo; aingiaye kupitia mimi ataokolewa. Ataingia na kutoka na kupata malisho” (Yohana 10:9).

Je, watu wengine husababisha kushindwa kwako? Je, uhusiano wako nao umekuwa si wa kina na bila muelekeo? Je, ni kama watu wanakutumia tu kwa manufaa yao? Ikiwa ndiyo hali unayopitia Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema hutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo……. Mimi ndimi mchungaji mwema; Ninajua kondoo wangu na kondoo wangu wananijua” (Yohana 10: 11,14).

Je, unashangazwa na kinachotendeka baada ya maisha haya? Je, umechoshwa na maisha ya kupigania tu vitu vinavyooza na kushika kutu? Je, wakati mwingine maana ya maisha yako huionea shaka? Je, unataka kuishi hata baadaya kufa? Ikiwa haya ndiyo uliyonayo basi Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi huo ufufuo na uzima. Aniaminiye ataishi, hata ajapokufa; na aishiye na kuniamini hata kufa kamwe” (Yohana11:25-26).

Njia ni nini? Ukweli ni nini? Uzima ni nini? Yesu akajibu, “Mimi ndimi njia kweli na uzima.Hakuna afikaye kwa baba bila kupitia kwangu” (Yohana 14:6). 

Monday, April 29, 2013

Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga? Je, Ushoga ni dhambi?


Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.

Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.

Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).

Biblia inasema nini juu ya kushirikiana katika ngono kabla kuoana?


Pamoja na matendo mengine ya uchafu, kufanya kitendo cha mapenzi kabla kuoana kumekatazwa katika maandiko (matendo 15:20; warumi 1:29; wakorintho wa kwanza 5:1; 6:13, 7:2; 10;8; wakorintho wa pili 12:21; wagalatia 5:19; waefeso 5:3; wakolosai 3:5; wathesalonike 4:3; yuda7). Biblia inasisitiza kuepuka kitendo hicho kabla ya ndoa.hii ina maana ya kuwa ni dhambi kama ya uzinifu kwa kuwa hujaunganishwa na unayefanya naye kitendo hicho. Mapenzi baina ya mume na mke waliooana ndiyo mapenzi yanayokubalika mbele za Mungu (waebrania 13:4).

Kushirikiana katika ngono kabla ndoa kumeenea sana kwa sababu nyingi. Mapenzi yanastarehesha. Mungu aliyaumba hivyo. Anawataka wanaume na wanawake wafurahie kitendo cha ngono (ndani ya ndoa). Hata hivyo, lengo la msingi la ngono si starehe bali kuzaana tukaongezeke. Hivyo tunazuiwa kufanya kitendo cha ngono kabla ndoa ili tusijipatie watoto tusiowatarajia. Kama jambo hili lingezingatiwa, magonjwa ya zinaa na wamama wasioolewa na kuavya mimba na kadhalika kungepungua. Kujizuia kunaokoa maisha, kunalinda watoto wachanga na kuleta ladha halisi ya ngono pamoja na heshima kwa Mungu.

Biblia inasema nini juu ya kunywa kileo? Je, ni dhambi kwa mkristo kunywa kileo?


Maandiko yana ilani nyingi juu ya kunywa kileo (mambo ya walawi 10:9; hesabu6:3; kumbukumbu la torati 29:6; waamuzi 13:4,7,14; samueli wa kwanza 1:15; methali 20:1; 31:4,6; isaya 5:11;22; 24:9; 28:7; 29:9; 56:12; mika 2:11; luka 1:15). Maandiko hayakatazi mkristo kunywa pombe, divai wala kinywaji chochote chenye kileo ndani. Maana maandiko mengine huzungumzia kileo kwa kuhalalisha matumizi yake. Mhubiri 9:7 inaamuru, “ kunywa kileo na moyo mkunjufu.” Zaburi 104:14-15 inaeleza Mungu hutoa divai “ inayofurahisha mioyo ya wanadamu.” Amosi 9:14 inazungumzia juu ya kunywa divai kutoka kwa shamba lako kama alama ya baraka za Mungu. Isaya 55;11 inapongeza “ naam, njoo ununue divai na maziwa…”

Kile Mungu anachowaamuru wakristo juu ya kileo ni wajizuie na ulevi (waefeso 5:18). Biblia inakataza ulevi na athari zake (methali 23:29-35). Wakristo wanakatazwa kuachilia miili yao itawalwe na vitu vinginevyo. (wakorintho wa kwanza 6:12; petro wa pili 2:19). Kunywa kileo kingi kunaathiri mtu. Maandiko yanakataza chochote kile ambacho kwa kukifanya unasababisha wengine kujikwaa( wakorintho wa kwanza 8:9-13). Kwa mujibu wa haya ni vigumu mkristo kukiri kuwa anakunywa kileo kwa utukufu wa Mungu ( wakorintho wa kwanza 10;31). 

Yesu aligeuza maji kuwa Divai. Huenda ikawa Yesu alikuwa akinywa divai katika karamu Fulani Fulani (Yohana 2:1-11; Mathayo 26: 29). Katika nyakati za agano jipya, maji yalikuwa yakijawa na vidudu na uchafu kama hali ilivyo sasa katika mataifamengine ya ulimwengu wa tatu. Hii ndiyo sababu watu walipendelea kunywa divai kutoka kwa zabibu ili kuepukana na taka taka hizi. Katika timotheo wa kwanza 5:23, Paulo alimkataza timotheo kunywa maji yaliyokuwa yakimtatiza tumbo lake na mahali pake anywe divai. Divai ilikuwa na asili ya kileo ndani lakini haikuwa na kiwango cha kilevi sawa na cha leo. Haikuwa maji ya mzabibu moja kwa moja wala kileo sawa na cha leo. Maandiko hayakatazi mkristo kunywa kileo cha aina yoyote bali yanakataza ulevi na utumwa wa kileo (waefeso 5:18; wakorintho wa kwanza 6:12).

Kileo, kinapotumiwa kwa uchache hakina athari kwa mwenye kukitumia. Kutumia kiasi kichache cha kileo ni jambo linaloruhusiwa mkristo. Ulevi na utumwa wa kunywa kileo ni dhambi. Kwa sababu ya kushindwa kujizuia katika viwango vya matumizi ya kileo, kukwaza wengine na hata kupatikana na hatia mbali mbali, ni vizuri mkristo aepukane kabisa na matumizi ya kileo cha aina yoyote.

Je! Mkristo anaweza pagagwa na Mapepo?


Bibilia kwa ukamilifu haitaji kama Mkristo anaweza shikwa na pepo. Ingagwa, kwa vile Mkristo amejazwa na Roho Mtakatifu (Warumi 8:9-11; 1 Wakorintho 3:16; 6:19), inaweza ooneka kinyume kwamba Roho Mtakatifu anaweza kumuruhus pepo kushika mtu ambaye Roho Mtakatifu anakaa ndani yake. Hii mara nyingine ni jambo la kutatanisha; ingawa, tunaamini sana kuwa Mkristo hawezi shikwa na pepo. Tunaamini kuwa kuna tofauti kubwa kati ya kushikwa na pepo na kukandamizwa na pepo au kushawishika na pepo. Kupagagwa na pepo yahuzisha,pepo kuwa na uhusika wa Karibu au kuongoza mawazo yako/mafikirio yako/matendo ya mtu (Luka 4:33-35; 8:27-33; Mathayo 17:14-18). Kukandamizwa na pepo au kushawishiwa na pepo inahuzisha pepo kumkabili mtu kiroho na kumtia moyo kwa matendo ya dhambi (1 Petero 5:8-0; Yakobo 4:7). Tambua kwamba kurasa zote za Agano Jipya zashugulikia vita vya kiroho, kamwe hatwambiwi kutoa pepo kutoka kwa mkristo (Waefeso 6:10-18). Wakristo wameambiwa kumtoroka shetani (1 Petero 5:8-9; Yakobo 4:7), si kutoa mapepo.


Ni jambo lisilofikirika kuwa Mungu anaweza kumruhus mwanawe, ambaye alimununua kwa dhamani, kwa damu ya Yesu Kristo (1 Petero 1:18-19), na kufanywa viumbe vipya (2 Wakorintho 5:17), kupagagwa na kutawaliwa na mapepo. Naam, mkristo twafanya vita na shetani na mapepo yake, lakini si kutoka ndani yetu. Mtume Yohana anasema, “Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mtungu; ninyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko aliye katika dunia” (1 Yohana 4:4). Ni nani aliye ndani yetu? Roho Mtakatifu. Ni nani aliye katika dunia? Ni shetani na mapepo yake. Kwa hivyo, mkristo ameushinda ulimwengu wa mapepo, na hali ya kupagagwa na pepo halitafanywa kuwa la kibilia.

Ubatizo wa Rohoho Mtakatifu ni nini?





Ubatizo wa Roho mtakatifu unaweza kufafanuliwa/kuelezwa kuwa ile kazi ambayo Roho Mtakatifu wa Mungu unamweka muumini kuwa na ushirika na Kristo na kwa ushirika na waumini wengine katika mwili wa Kristo wakati wa kuokolewa. Wakorintho wa kwanza 12:12-13 ni ukurasa wa katikati katika Bibilia kuhusu ubatizo wa Roho Mtakatifu, “Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.” (1Wakorintho 12:13). Bali Warumi 6:1-4 haitaji roho wa Mungu, bali yaelezea sehemu ya wakristo mbele za Mungu kwa lugha sawa na ile ya ujumbe wa kwanza Wakorintho: “Tusema nini basi? Tudumu kaitka dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.”

Hoja zifuatazo zatosha kudumisha uelefu wetu juu ya ubatizo wa Roho Mtakatifu. Kwanza, 1Wakorintho 12:13 yataja wazi kwamba wale wote waliobatizwa wananyweshwa Roho mmoja (kuwepo kwa Roho mtakatifu). Pili, hamna mahali katika Bibilia Wakristo wameelezwa wabatizwe, ndani ya, au kwa Roho au kwa vyovyote vile watafute ubatizo wa Roho Mtakatifu. Hii yaonyesha kuwa Wakrisot walikuwa na uzoevu. Tatu, Waefeso 4:5 yaonekana kuashiria ubatizo wa Roho. Kama hii ndio hali, ubatizo wa Roho Mtakatifu ni kitu cha kweli kwa kila Mkristo, kama vile “Imani mija” na “Baba mmoja” viko.

Kwa kumalizia, ubatizo wa Roho Mtakatifu wafanya mambo mawili, 1) Watuunganisha na mwili wa Kristo, na 2) Waambatanisha kusulubiwa kwetu na Yesu. Kuwa na mwili wake, yamaanisha, tumefufuliwa naye kwa upya wa uzima (Warumi 6:4). Kwa hivyo lazima tuviweka katika matendo vipawa vyetu vya Roho ili tuuweke mwili wa Kristo kuendelea kufanya kazi kulingana na 1Wakorintho 12:13. Kushuhudia ubatizo wa roho mmoja huwa mzingi wa kuwa na umoja wa Kanisa, kulingana na mkudhatha wa Waefeso 4:5. Kuwa na ushirika wa karibu na Kristo katika mauti yake, kuzikwa kwake na ufufuo wake kupitia kwa ubatizo wa Roho waweka mzingi wa kutenganishwa na nguvu za dhambi na kutembea katika maisha mapya. (Warumi 6:1-10; Wakolosai 2:12).

Nawezaje kujazwa na Roho Mtakatifu?


Kifungu cha maana katika kuelewa juu ya kujazwa na Roho Mtakatifu in Yohana 14:16, mahali ampapo Yesu anaahidi kukaa kwa Roho Mtakatifu kwa wakristo, na huyo atadumu si kwa muda. Ni kitu cha maana kutofautisha kati ya kukaa kwa Roho Mtakatifu na kujazwa na Roho Mtakatifu. Kudumu kwa Roho Mtakatifu aupo kwa baadhi ya wakristo, bali ni kwa Wakristo wote. Kuna sehemu nyingi katika Bibilia zinazo pongeza huu msimamo wetu. Kwanza, Roho Mtakatifu ni zawadi iliyopewa Wakristo wote katika Kristo Yesu bila kupagua, na hakuna sheria za kutimiza ila tu ni kuwa na imani katika Kristo Yesu (Yohona 7:37-39). Pili, Roho Mtakatifu unapokewa wakati wa kuokoka (Waefeso 1:13). Wagalatia 3:2 inasisitiza ukweli huu pia, kwa kusema kwamba kutiwa muhuri na kujazwa na Roho Mtakatifu ulitokea wakati wa kuokoka. Tatu, Roho Mtakatifu unakaa kwa Wakristo milele. Wakristo wamepewa Roho Mtakatifu kama mtaji ama tibitisho la utukufu wao katika siku zijazo katika Kristo (2 Wakorintho 1:22; Waefeso 4:30).

Hili ni linganisho la kujazwa kwa Roho Mtakatifu ambao Waefeso 5:18 yazungumzia. Kikamilifu ni lazima tuzame katika Roho Mtakatifu ili atumiliki na katika hali hiyo atujaze. Warumi 8:9 na Waefeso 1:13-14 za sema kwamba anakaa kwa kila Mkristo, lakini anaweza kuhusunishwa (4:30), na kazi yake ndani yetu unaweza poa (1Wathesalonike 5:19). Wakati tunaruhusu haya kutokea hatuwezi kuhisi kikamilifu Roho Mtakatifu ukifanya kazi na nguvu zake ndani yetu. Kujazwa na Roho Mtakatifu haimaanishi tendo la nche pekee; pia yamaanisha tendo la kimawazo ambalo latutia moyo kwa kila tendo tutendalo. Zaburi 19:14 yasema, “Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee BWANA, Mwamba wangu, na mwokozi wnagu.”

Dhambi ndiyo huzuia kujazwa kwa Roho Mtakatifu, na kumtii Mungu ndio njia pekee Roho anaweza kutunzwa. Waefeso 5:18 yatwaamuru kwamba tujazwe na Roho Mtakatifu; bali si kwa kuomba ili tujazwe na Roho Mtakatifu ambayo itawezesha kukamilisha kujazwa kwa Roho. Ni utiifu wetu wa sheria za Mungu wawezesha Roho kufanya kazi kwa huru ndani yetu. Kwa sababu tumeadhirika kwa dhambi, ni vigumu kujazwa na Roho wakati wote. Wakati twatenda dhambi ni lazima tutubu papo hapo kwa Mungu na tufanye upya mkataba wa kujazwa na Roho and kuongozwa na Roho Mtakatifu.

Yamaaninisha nini kumkufuru Roho Mtakatifu?


Wazo la “kumkufuru Roho” limetajwa katika Mariko 3:22-30 na katika Mathayo 12:22-32. neno kufuru linaweza kuelezwa kwa ujumla kama, “tabia iliyo kando”. Hilo neno laweza kutumika kwa dhambi kama zile za kumlaani Mungu au kwa makusudi ya kutotambua mambo yanohusiana na Mungu. Pia ni kumhuzisha Mungu na dhambi, ama kukana yale mazuri tunayostahili kumhusisha nayo. Hii hatia ya kukufuru ingawa ni pekee inaitwa “kukufuru Roho Mtakatifu” katika Mathayo 12:31. katika Mathayo 12:1-32, Wafarisayo baada ya kushuhudia matendo makuu yasiyopingika ya Yesu alikuwa akitenda miujiza kwa nguvu za Roho Mtakatifu, na wakadai kuwa alikuwa amepagagwa na pepo “Beelzebuli” (Mathayo 12:24) unaweza gundua kwamba katika Mariko 3:30 Yesu analengo kuhusu kwa kile ambacho hawakukifanya “kumkufuru Roho Mtakatifu.

Huku kukufuru na kuhusu na mtu kumtusi Yesu Kristo kuwa amepagagwa na mapepo badala ya kujazwa na Roho Mtakatifu. Kwa sababu hiyo kwa matukio haya ya kukufuru Roho Mtakatifu hauwezi kuongezeka hii leo. Yesu Kristo hayumo duniani leo hii, bali ameketi katika mkono wa kulia wa Mungu. Hamna mtu atakaye shuhudia Yesu Kristo akitenda miujiza na kudai kwamba nguvu hizo ni za Shetani badala ya Roho Mtakatifu. Mfano wa karibu sana leo hii utakuwa ule wa mtu akikombolewa na kubadilisha maisha yake kwa nguvu za Shetani na badala ya kujazwa na Roho Mtakatifu. Kukufuru Roho Mtakatifu leo hii, ambayo ni sawa na dhambi isiyo samehewa ni hali ya kuendelea kutokua na imani. Hakuna msamaha kwa mtu yule akufaye bila imani. Kuendelea kukataa Roho Mtakatifu ambao watusukuma kuwa na imani katika Yeus Kristo ni kufuru isiyosamehewa. Kumbuka chenye kimesemwa katika Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele” mbele yake kuna aya ingine, “Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia” (Yohana 3:36). Hali pekee ambayo mtu hawezi kuwa na msamaha ni ikiwa ako kati ya wale, “yeyote atakaye mwamini” kwa maana ni yule amemkataa Mwana.”

Roho Mtakatifu ni nani?


Kuna utatanishi mwingi juu ya kumtambua Roho Mtakatifu. Wengine humchukulia kama nguvu Fulani zisizoonekana. Wengine huamini kwamba ni uwezo wa Mungu ambao Mungu huuachilia maishani mwa wale ambao ni waumini wa kristo. Je, biblia inasemaje juu ya Roho Mtakatifu? Kwa kifupi biblia inasema kwamba Roho mtakatifu ni Mungu. Pia biblia inasema kuwa Roho mtakatifu ni mtu, mwenye akili, hisia na mapenzi yake.

Swala la kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu limo ndani ya aya nyingi za biblia kama vile Matendo 5:3-4. Katika ayah ii petro anapambana na anania aliyemdanganya Roho Mtakatifu na nasisitiza yakuwa “hukumdanya mtu bali Mungu.” Hili ni tangazo la wazi kwamba kumdanganya Roho Mtakatifu ni kumdanganya Mungu. Tunaweza pia kujua Roho Mtakatifu ni Mungu kwa kuwa ana tajwa na hali sawa na za Mungu. Roho Mtakatifu yuko kila mahali katika Zaburi 139:7-8, “nitaenda wapi nijifiche na Roho? ama nitakimbilia wapi mbali na uwepo wako? Nikipanda juu mbinguni, huko uko; nikifanya malazi yangu kuzimu, tazama uko huko,” tena katika wakorintho wa Kwanza 2:10 tunaona hali yakuwepo kila mahali kwa Roho Mtakatifu “Lakini Mungu ameyajulisha kwetu kupitia Roho wake Mtakatifu. Kwa kuwa Roho huyachunguza mambo yote, naam, mambo ya siri ya Mungu. Kwa maana ni nani ayajuaye ya mwanadamu isipokuwa roho ya mwanadamu inayokaa ndani yake? Vivyo hivyo, hakuna ajuaye mambo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.”

Tunaweza kujua kweli kwamba Roho Mtakatifu ni Mungu kwa kuwa ana akili, hisia na mapenzi yake. Roho Mtakatifu hufikiri na hujua (Wakorintho wa kwanza 2:10). Roho mtakatifu anaweza kuugua (Waefeso 4:30). Roho hutuombea (Warumi 8:26-27). Roho Mtakatifu hufanya maamuzi kutokana na mapenzi yake mwenyewe (Wakorintho wa kwanza 12:7-11). Roho mtakatifu ni Mungu, sehemu ya tatu ya utatu wa Mungu. Kama Mungu, Roho Mtakatifu anaweza kufanya kazi ya msaidizi na mshauri kama vile Yesu kristo aliyevyoahidi kuwa atakuja kufanya (Yohana 14:16,26; 15:26).

Saturday, April 27, 2013

Back to Basics: Dealing with demonic dreams

 
Ugh.
While I totally understand the despair, I would like to offer an alternative response: embrace these dreams as the gifts they are.
This may seem crazy—but let me tell you a story I just heard which may give you a new perspective.
The story  (heard on a Plumbline Ministries video)  goes something like this: a man and his son were driving together. The son looked up and was disturbed to see a number of vultures circling in the sky. “There must be a dead animal somewhere,” he sadly exclaimed. His father wisely pointed out that if the animal were, in fact, dead, then the vultures would have landed. Then the dad asked the child what he thought they could do if they were going to help the wounded animal. The son pondered this, then said, “Well, I guess we wouldn’t want to kill the vultures—because they are our marker for where the wounded animal is.”
Exactly.
The demonic is the marker for the wounding.
So let me give you a strategy for leveraging demonic harassment in your dreams to greater healing and spiritual dominion.
(1)   Choose to put things in proper perspective. If dark spiritual influences could kill you- believe me–you would already be dead! If the worst thing they  can do is give you a bad dream—yes, it is annoying, but seriously, it is just a bad dream!  Don’t put too much weight on it—instead leverage it for change.
(2)   “Dream forward!” (leverage the dream). This requires an action plan. Here are some suggestions—
  • Interpret the dream- in general, what is the main essence of the dream? (i.e. let’s say that a witch is stabbing you in you on the couch in your livingroom, and you tell her to leave in the name of Jesus, but she doesn’t . The essence of this dream is that witchcraft – perhaps word curses are preventing you from finding rest/peace in your day to day life and that you do not have the authority to deal with it at this time.
  • Look for clues as to the arena—is this occurring at work, home, spiritual community, in your friendships? Drilling down to the specifics is essential to putting this all to an end!
  • Note the feelings in the dream- (likely the big 6–fear, anger, shame, disgust, sadness and hopeless) These feelings are the manifestation of the wounding, sin , or generational issues – and succumbing to them often throws the door wide open to further harassment.
  • Pay particular attention to “proclamations” made in the dream—by yourself or others. These can give you strategies for dealing with the situation/issues opening you up to such dreams.

MUHAMMAD WAS UNAWARE OF RELIGION

MUHAMMAD WAS UNAWARE OF RELIGION By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute Abstract This article explores the controversial cl...

TRENDING NOW