Saturday, March 5, 2016

YESU AKUBALI KUITWA MUNGU


Ndugu msomaji,
Kwenye somo letu la leo ninakuletea uthibitisho Saba (7) wa Yesu kuitwa Mungu.
Bila ya kupoteza muda tuanze kusoma aya za Biblia.

1. THOMASO ANAMWITA YESU MUNGU
Tomaso mwanafunzi wa Yesu alisema kuhusu Yesu, “Bwana na Mungu wangu” (Yohana 20:28). 28 Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu! 29 Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki.
Baada ya Thomaso kumwita Yesu "Bwana na Mungu wangu", tunasoma kuwa Yesu anakubali na kumwabia, wewe Thomaso unameniona ndio unasadiki. Sasa Thomaso anasadiki nini? Kumbe Thomaso sasa anasadiki aliyo sema kuwa Yesu ni Bwana na Mungu.

2. YESU ANAITWA MUNGU MKUU NA WAFUASI WAKE
Tito 2:13 tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;
KUMBE HATA WANAFUNZI NA WAFUASI WA YESU WALIMWITA YESU MUNGU tena MKUU. Tumesoma katika Tito Mlango wa 2 na aya ya 13 kuwa, Kristo Yesu ni Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Sasa wapi Yesu alikataa kuitwa Mungu Mkuu?
3. PETRO ANAKIRI KUWA YEYE NI MTUMWA WA YESU AMBAYE NI MUNGU WETU NA MWOKOZI WETU
2 Petro 1:1 Simoni Petro, mtumwa na mtume wa Yesu Kristo, kwa wale waliopata imani moja na sisi, yenye thamani, katika hali ya Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo.
Petro anajitambulisha kuwa yeye ni mtumwa wa Yesu Kristo ambaye ni Mungu wetu na Mwokozi wetu.
Kumbuka Petro aliishi WAKATI WA YESU NA ALIKUWA MMOJA WA WANAFUNZI WAKE. Kama Petro aliye kuwa na Yesu anamwita Yesu Mungu, je, wewe ni nani kupinga ukweli huu?
4. MUNGU BABA ANAMWITA MWANA - YESU "MUNGU"
Waebrania 1:8-9 8 Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.
Baba asema juu ya Yesu, “Lakini juu ya mwana asema haya, “Na Kiti chako cha enzi, MUNGU, Kitadumu milele, na haki itakuwa fimbo ya ufalme wako.” ==> Baba anasema kuwa kiti cha Enzi ni cha Yesu, na zaidi ya hapo anaongeza kwa kumwita "MUNGU"
KUMBE HATA Baba aliye Mbinguni anamwita Yesu ni Mungu. Hatusomi na wala hakuna aya ambayo Yesu anamwambia Baba yake asimwite Mungu.
AYA YA 9, Mungu Baba anamaliza kabisaa kwa kusema yafuatayo "KWAHIYO MUNGU, MUNGU WAKO". Hapo teyari Mungu Baba anasisitiza kuwa MWANA NI MUNGU NA YEYE BABA NI MUNGU.
5. MALAIKA WANAMWABUDU YESU: KUMBE YESU NI MUNGU
Katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana, Malaika alimwamuru Mtume Yohana kumuabudu Mungu tu (Ufunuo wa Yohana 19: 10). Mara nyingi Yesu katika maandiko aabudiwa (Mathayo 2;11; 14:33; 28:9,17; Luka 24:52; Yohana 9:38). Hakemei watu kwa kumuabudu. Kama Yesu hakuwa Mungu, angewaambia watu wasimuabudu, kama vile Malaika alivyofanya. Kuna aya nyingi za maandiko zinazoshuhudia ya kwamba Yesu ni Mungu.
6. VIONGOZI WA KIYAHUDI WASEMA YESU AMEKUFURU BAADA YA KUKUBALI KUWA YEYE NI MWANA WA MUNGU
Wakati wa kujaribiwa kwake mbele ya viongozi wa Kiyahudi, kuhani mkuu alimtaka Yesu, “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu” (Mathayo 26:63). “Yesu akamwambia wewe umesema,’ Yesu akamwambia, wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni” (Mathayo 26:64) viongozi wa Kiyahudi walimdhania kwa kukufuru (Mathayo 26:65-66).
7. WAYAHUDU WANAZIDI KUSISITIZA KUWA YESU NI MWANA WA MUNGUBaadaye mbele ya Pilato, “Wayahudi wakamjibu, Sisi tunayo sheria, na kwa sheria hiyo amestahili kufa, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu” Yohana 19:7) ni kwa nini makisio yake kuwa Mwana wa Mungu yachukuliwe kuwa kufuru na astahili hukumu ya kifo?
Wayahudi wilielewa vizuri sana chenye Yesu alimaanisha kwa maneno haya “Mwana wa Mungu” kuwa Mwana wa Mungu ni kuwa hali moja na Mungu. Mwana wa Mungu “wa Mungu” kusema uko katika hali sawa na Mungu-hakika kuwa Mungu- kulikuwa sawa na kukufuru kwa viongozi wa Kiyahudi; kwa hivyo walimtaka Yesu auwawe, kulingana na Mambo ya Nyakati 24:15. Waebrania 1:3 inadhihirisha haya wazi, “Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu.”
Tumesoma tena kwa ushahidi wa aya kadhaa kuwa Mungu Baba anamwita MWANA NI MUNGU, Wanafunzi wake wanamwita Yesu ni Mungu, Malaika wanasema tumwabudu Yesu ambaye ni Mungu, na Wayahudi wanasema Yesu alikufuru alipo kubali kuitwa Mwana wa Mungu na Pilato.
Kwakuwa inafahamika Yesu hakuwa na dhambi wala hakuwai tenda dhambi:
1. Je, kukubali kwake kuitwa Mungu kunamaanisha nini?
2. Kwanini Yesu hakumkatalia Thomaso pale alipomwitwa "Bwana na Mungu wangu?
3. Kwanini Petro anamwita Yesu ni Mungu wetu na Mwokozi wetu?
4. Kwanini Mungu Baba anamwita Mwana ambaye ni Yesu KUWA NI "MUNGU"
5. Kwanini Malaika wanasema tumwabudu Yesu, huku wakisisitiza kuwa anaye abudiwa ni Mungu pekee?
6. Kwanini Kuhani Mkuu alimtaka Yesu kukiri kuwa ni Mwana wa Mjungu? Je, jinu la yesu lilisababisha nini kwa Wayahudi?
7. Kwanini Wayahudi walimshataki Yesu mbele ya Pilato kuwa kajiita Mwana wa Mungu, na kufanya hivyo ni kukufuru?
Ni maombi yangu kuwa, hizi aya chache tulizo ziweka hapa zitakufungua macho na uelewe Uungu wa Yesu na kwanini Yesu hakukana kuitwa Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Friday, March 4, 2016

QURAN, ALLAH, MUHAMMAD, NA JIBRIL WANAKIRI KUWA YESU NI MUNGU KWASABABU ANASAMEHE DHAMBI

Ndugu msomaji,
Tunaendelea kujifunza kuhusu Uungu wa Yesu. Quran, Allah, Muhammad na Jibril kwa mara nyingine tena wanakiri kuwa Yesu ni Mungu.
Hii ni sifa nyingine ya Mungu pekee na wala si ya mwanadamu.
Quran 40:2-3
Uteremsho wa Kitabu umetoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu, Mwenye kujua. Anaye samehe dhambi na anaye pokea toba, Mkali wa kuadhibu, Mwenye ukarimu, hakuna mungu ila Yeye; marejeo ni kwake.
Je, Bwana Yesu alikuwa na sifa hii? Katika tukio moja ambalo Yesu alionesha mamlaka yake ya Uungu kwa kusamehe dhambi na wakuu wa dini walioina hiyo kama kufuru kwani mwenye uwezo wa kusamehe dhambi ni Mungu pekee kwa vile hata wao hawakufahamu mamlaka ya Yesu ni Mungu
Marko.2:5-11
Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao, Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu? Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu? Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende? Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza), Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako.
Hili ni mojawapo ya matendo ya Yesu kusamehe dhambi aliyotenda kuonesha Uungu wake na mamlaka yake.
Sura ya 4
Ubinadamu wa Yesu na sababu ya kuitwa Mwana wa Mungu toka mamlaka ya Uungu.
Ndugu mpendwa msomaji tutakubaliana kuwa hilo ni moja kati ya maswali nyeti yanayoulizwa na watu wengi wanao hoji na kutafiti mamlaka haswa ya Bwana Yesu.
“Ubinadamu wake”
Chanzo cha maswali yote yanayo ulizwa juu ya Bwana Yesu kinaanzia mara tu Yesu alipovaa mwili wa kibinadamu tendo hilo kwa fikra za haraka tu linaweza kudhaniwa kuwa ndilo linaloshusha mamlaka yake ya asili kama Mungu. Pamoja na hayo mimi binafsi nichoelewa ni kuwa tendo hilo kamwe halishushi mamlaka bali linafunika mamlaka aliyokuwa nayo kwa kadri ya sababu…………
Ifuatayo:-
Mungu aliwahi kujifunua wazi katika nyakati za nyuma na wanadamu wakaangamia
Fuatilia:- kutoka 19:20-21 Bwana akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; Bwana akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu. Ndipo Bwana akamwambia Musa, Shuka chini, uwaonye watu wasije wakapasua njia waje kwa Bwana kutazama, kisha wengi miongoni mwao wakaangamia.
“swali la kujiuliza”
Je! Mungu aje katika hali gani ili mwanadamu aweze kuikabili?
“Jibu”
Ni lazima aje katika hali inayofunika uwazi wa mamlaka yake iliyo ya utisho kwa mwanadamu mdhambi.
Na anapokuwa katika hali ya ubinadamu ndipo anapoona njaa, kulia, kutembea, kusinzia na hali zote za ubinadamu anakuwa nazo na ndo maana Yesu ni Mungu 100% na mwanadamu 100%
Fuatilia kutoka 33:18,20 (Musa) Akasema, Nakusihi unionyeshe utukufu wako…. Kisha akasema, Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi
Sababu hiyo ya kimsingi ndiyo inayofanya Bwana Yesu kuchukua mwili wa kibinadamu kupitia Mariam kama tulivyo kwishaona. Hivyo mwili ya Bwana Yesu ulisitiri mamlaka kuu ya Uungu wake ambayo hainge kuwa busara kuufunua na kufanya binadamu kuangamia badala ya kuokolewa naye. Kwa kauli nyingine ni kuwa Mungu (Yesu) alitumia mwili huo ili kuwafikia waja wake kama tulivyoona hapo nyuma jinsi Mungu alivyojifunua hata kwa kichaka kwa kadri ya Qur-an tukufu. “Ubinadamu ni njia ya Mungu kusema na waja wake:”
Qur-an 42:51 ……….. Mungu husema na wajawake kwa njia ya:-
Ilhamu – sauti ya ndani ya moyo ya Mungu
Nyuma ya pazia – ishara ya kufunika mamlaka.
Kwa kadri ya Aya hiyo tunaona Qur-an ikitaja “Pazia” kama chombo cha mawasiliano ya Mungu kwa wanadamu, pazia hii umaanisha ni kitu kinachofunika ili kuzuia kuonekana kwa uhalisi wa jambo kwa lugha nyingine Mungu wakati Fulani huamua kufunika uhalisi wake kwa kujifunua nyuma ya “Pazia”.
“Pazia ni nini Kibiblia?”
Waebrania 10:20 ……….. ipitayo katika “Pazia” yaani mwili wake.
Katika Biblia Pazia huashiria mwili wa Bwana Yesu, hivyo hiyo ni njia ya kimawasiliano kati yake na binadamu inayofunika mamlaka yake ya Asili ya Uungu ili binadamu kumudu kukutana naye.
1Timotheo 3:16 Mungu alidhihirishwa katika mwili
Ebrania 10:5 Mwili uliniwekea tayari
Filipi 2:7 alijifanya hana utukufu …….. akawa na mfano wa mwanadamu.
Kwanini aitwe Mwana naye ni Mungu?
Tendo la Bwana Yesu kuitwa Mwana wa Mungu linaanzia kwenye chanzo cha kutwaa mwili.
Yohana 1:14 naye neno akafanyika mwili akakaa kwetu nasi tukaona utukufu wake utukufu
kama wa Mwana pekee atokae kwa baba …………..
Andiko hii linaonyesha hatua kuu mbili yaani:-
Kufanyika mwili
Kuitwa mwana atokae Mbinguni.
Sababu kuu
Tendo la Yesu kuamua kuchukua jukumu la kutuokoa lilimladhimu siyo kufunika Utukufu wake (Uungu ) tu kwa mwili bali pia kubadili kitambulisho chake cha mamlaka
“Fatilia mfano huu”
Maji yanaweza kugeuka katika hali mbalimbali katika kile ninachojua maji hayo mara yanapo badiri hali tu pia tendo hilo huambatana na kubadilli jina, yaani mfano maji yanapoganda hayaitwi tena maji bali huitwa barafu
Swali:- Je barafu si maji?
Jibu:- la barafu ni maji ila yamebadili asili kwa muda na baadae hurejea.
Sababu ya Bwana Yesu kuitwa mwana inatokana na kusudi lake tu la kuja Duniani Kutukomboa hivyo alifanyika barafu toka asili ya maji (alifaninyika mwana toka asili ya Uungu kama njia ya Ukombozi) lakini asili yake ya Uungu inabaki palepale.
Fuatilia ushauri mwingine juu ya Uungu wa bwana Yesu katika mafungu yafuatayo:-
Yohana 14:7-10……… aliyeniona mimi amemwona Baba
Tito 2:13 ……. Yesu Mungu mkuu na mwokozi wetu.
Yohana 20:28 Bwana wangu (Yesu) na Mungu wangu.
Ndugu mpendwa ninaamini hofu na mashaka ya moyo wako juu ya mada hii yamepingwa na uondolewa kupitia uchambuzi huu, fanya maamuzi yako leo kwa kujenga upya imani yako juu ya mamlaka ya Bwana Yesu kama tulivyo jifunza.
Hitimisho
Yesu ni Mungu na hivyo yeyote anayehitaji kwenda mbinguni, njia pekee na pekee tu ni Kristo Yesu-‘Matendo 4:12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

QURAN, ALLAH, MUHAMMAD, NA JIBRIL WANAKIRI KUWA YESU NI MUNGU KWASABABU ANAUMBA

ALLAH ANAULIZA KUWA, JE ALIYEUMBA NI KAMA ASIYE UMBA?
Surat An Nahl 17. Ati anaye umba ni kama asiye umba? Basi hebu, hamkumbuki?
Ndugu msomaji, hilo ni swali kutoka kwa Allah wa Waislam. Allah anataka ajibiwe, Je, aliye umba unaweza mlinganisha na asiye umba?
Ndugu zanguni, huu ni MSIBA MKUBWA sana kwa Waislam, maana Allah sasa anakiri kuwa, aliye umba hawezi kuwa sawa na asiye umba.
JE, ISA ALIWAI KUUMBA?
Ndugu msomaji wangu bilashaka umeanza kufunguka masikio kupitia Aya hiyo ya Quran katika Aya hiyo inaonekana orodha ya matendo makuu ambayo Bwana (Isa) anatangaza kuwa na uwezo wa kuyatenda bila shaka matendo hayo ikiwa umeyachunguza kwa makini, yanaonekana kuhusika na uwezo wa kiutendaji wa Mungu Mwenyezi, sasa hebu tufuatilie kwa makini.
Nukuu kwa muktasari Qur-an 3:49 Na ni Mtume kwa Wana wa Israili kuwaambia: Mimi nimekujieni na Ishara kutoka kwa Mola Mlezi wenu, ya kwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege. Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma, na ninawafufua maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ninakwambieni mnacho kila na mnacho weka akiba katika nyumba zenu. Hakika katika haya ipo Ishara kwenu ikiwi nyinyi ni wenye kuamini.
a) Nakuumbieni katika udongo kama sura ya ndege.
Bila shaka tendo hili hufanana fikiri na kile alichofanya Mungu pindi alipokuwa akimuumba Adamu maandiko yanaonyesha kuwa Mungu alifinyanga udongo na kumuumba Adamu vivyo hivyo Isa (Yesu) nae anafanya Uumbaji kwa kufinyanga udongo kwa sura ya ndege.
Ref: Mwanzo 2:7 Bwana Mungu akamuumba mwanadamu kutoka katika udongo wa ardhi
Qur-an 22:5…… tulikuumbeni kwa udongo mzee wenu Nabii Adamu ………
Hivyo Yesu anafanya tendo la Uumbaji kwa hatua zinazo fanana fika na kile alichofanya Mungu (kufinyanga udongo).
b) Kisha nampulizia mara anakuwa ndege.
Ndugu mpendwa yawezekana liletendo la kufinyanga udongo lisiwe na nguvu sana kwa wajenga hoja , lakini hapa ndipo panapo nishangaza zaidi Qur-an inapoonyesha wazi kuwa Isa aliweza kupulizia udongo nao ukapata uzima na kuwa kiumbe hai.
Wanasayansi huu ndio uumbaji na wanabaiolojia wamejitahidi kuumba na kutengeneza mtu lakini wamegonga mwamba inapofikia hatua ya kumfanya kuwa kiumbe hai, aweze Kutembea, Kunusa, kuona n.k
Lakini maandiko ya Qur-an ufunua siri hii ya ajabu, bilashaka tendo hili la kupuliza pumzi na kitu kikawa hai ndiyo uleta maana halisi ya Uumbaji na hili ndilo tendo linaloleta maana na uzito haswa unaofanya tendo hilo kuwa rasmi na kumhusu Mungu pekee.
Mafunuo ya Qur-an huonyesha kuwa tendo hilo haswa ndilo alilotenda Mungu alipokuwa akimuomba Adamu nalo ni tendo la kutoa uhai (Maisha) kwa kuomba.
Qur-an surat 15:28 Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
Tunajua fika juu ya tabia ambazo Mungu umshirikisha mwanadamu na pamoja na ha yo zipo zile ambazo Mungu kamwe hawezi kumshirikisha mwanadamu, lakini katika andiko hilo tunaona Yesu akitenda kazi hiyo kuu yenye uhusiano kwa asilimia miamoja na uwezo wa Kiuungu bilashaka huyo Yesu anayo asili inayopita ubinadamu aliokuwa nao na siyo asili ya kawaida.
Je! Mbona Qur-an inasema aliumba kwa idhini ya Mungu?
Inawezekana ndugu msomaji wangu ukawa na swali la namna hiyo ndani ya moyo wako hebu niruhusu sasa niweze kuondoa mashaka uliyonayo.
Je! Neno kwa idhini humaanisha nini?
Katika tafsiri ya kawaida Neno “Idhini” humaanisha “ruhusa” au “Ukubali”
Hivyo Qur-an inapomnukuu Nabii Isa akisema kwa “idhini” inaleta maana tu ya ukubali, ruhusa toka kwa Mungu.
Swali:- je kwanini apewe ruhusa na hali yeye ni Mungu? Au Je kuna miungu wangapi?
Jibu:- katika mafunuo ya Biblia mara kadhaa Bwana Yesu ametumia kauli hiyo ya kuruhusiwa au kukubaliwa na Mungu (eg: Yohana 5:30) mara kadhaa Yesu alisema “ninenalo si neni yaliyoyangu nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo”
Kwanini aseme hivyo (kwa idhini)?
Kwa msingi ujio wa Yesu hapa Duniani ulimlazimu kufunika uwezo na mamlaka yake ya asili ya Kimungu, ilimpasa kumwelekeza mwanadamu kwa vielelezo hai vya kimwenendo, hali na mazingira hayo yalimfanya kujipa cheo cha chini mara kadhaa alipozumngumza na watu.
Rejea Qur-an 20:9-11 Mungu alijifunua kwa Musa kupitia kichaka cha moto bila shaka alichukua ufinyu huo ili kuwa Asili na mwanadamu.
Pamoja na hayo Bwana Yesu akuadhimu mara chache kufunua taratibu mamlaka aliyonayo kiasili, mfano ni pale aliposema.
Yohana 10:30 mimi na Baba tu umoja.
Kauli hiyo iliwafunulia mafarisayo juu ya mamlaka ya Yesu ya Kimungu, lakini haikuwa jambo rahisi kwao kukubaliana na hilo
na katika aya hiyo tunaona wakiadhimu kumpiga mawe kwa kujiita yeye ni Mungu.
Bilashaka Yesu alitambua saikolojia ya imani ya watu hao anaowajua hata mioyo, hivyo Yesu aliamua kushuka kwa kumtaja Mungu wanayemdhani kama Mungu aliye ng’ang’ana Mbinguni tu lakini kwa hakika hiyo ndiyo asili yake binafsi.
Ndiyo maana alisema kwa Idhini.
Katika wazo hilohilo ndiyo maana Yesu Utumia neno kwa “Idhini”alipenda watu watambue mamlaka yake katika utendaji wake zaidi kuliko katika maneno yake
Hata hivyo neno kwa “Idhini” halimaanishi kwa “uwezo” Idhini na uwezo ni mambo mawili yanayo tofautiana sana
Mfano:- wewe unaweza kupewa Idhini ya kuhubiri lakini usiweze (usiwe na uwezo ) wa kuhubiri hivyo idhini( ruhusa ) na uwezo nitofauti kulingana na maandiko tabia ya Yesu ihusuyo Uumbaji uonekana akiwa nayo katika asili (Yohana 1:1-3) hivyo ni tabia ya kiuwezo na mamlaka yake ya Kimbinguni kabla ya kujishusha na kuvaa ubinadamu (nitalieleza mbele kwaupana ) na kuja hapa duniani.
Neno idhini Isa (Yesu) analitumia anapo kuwa hapa Duniani kama sehemu ya hatua yake ya kujishusha na kutwaa ubinadamu kwaajili ya kuokoa, lakini bado tendo la uumbaji linarejea asili na mamlaka yake kama Muumbaji na si wa ndege tu bali Dunia kwa ujumla (Yohana 1:1-3)
Qur-an inampa cheo gani (Isa) kwa tendo la Kuumba?
Uandishi au kuchapaji mwandishi na mengineyo ya kimsingi.
Qur-an 16:17 …….Ati yeye aliyeumba (naye ni Mwenyezi Mungu) atakuwa sawa na wale wasio umba je hamkumbuki?
Andiko hilo la Qur-an linasema kuwa
– “Ati yeye aliyeumba (Mungu) atakuwa sawa na wasio umba”?
Jibu :- la” aliyeumba hawezi kuwa sawa wasioumba bali aliye umba anakuwa sawa na aliyeumba hivyo ikiwa Yesu aliumba je yeye ni nani?
Qur-an kamwe haimpi sifa au usawa kiumbe yeyote asiye na sifa inayohusika na Mungu, maana sifa inayomhusu Mungu haswa ile ya kuumba ndiyo humfanya Mungu kuitwa Mungu kamwe hawezi kupewa Mwanadamu.
Pamoja na hayo jambo la kushangaza ni pale Qur-an inapoo nekana kuweka wazi kuwa Nabii “Isa Ibn Mariam” naye alikuwa na sifa hiyo inayo mhusu Mungu maana naye aliweza kuumba
(rejea neno nakuumieni Qur-an 3:49)
Na kutokana na kile kichosemwa na aya tuliyoisoma punde Nabii Isa anaonekana kuwa sawa na Mungu au kwa lugha rahisi naya ufupi yeye ni Mungu Muumbaji aliye adhimu kuvaa ubinadamu, lakini ana mamlaka inapita huo ubinadamu (yeye ni neno, muumbaji).
Ndugu msomaji, leo tumejifunza kwa mara nyingine tena kuwa Yesu ni Mungu kwasababu aliumba Quran Sura 16 aya ya 17.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Thursday, March 3, 2016

ALLAH ASEMA ISRAEL NI TAIFA BORA NA LA NEEMA KULIKO WALIMWENGU WOTE

1. Allah asema Israel ndio taifa la Mungu, Surat Al Baqara 47
2. Allah asema ardhi ya Israel ni ya Waisraeli, Soma Quran Surat Al Maida aya ya 21
3. Palestina yakatwa na haipo kwenye Quran
Ndugu wasomaji,
Huu ni Msiba kwa Waislam wanao pigia debe Wapalestina. Hivi kwanini Allah hakuitaja Palestina kwenye Quran yake? Lakini ameitaja Israel na Wairaeli?
Surat Al Jaathiya 16. Na hakika tuliwapa Wana wa Israili Kitabu na hukumu na Unabii, na tukawaruzuku vitu vizuri vizuri, na tukawafadhilisha kuliko walimwengu wote.
ALLAH ANASEMA KWA WAYAHUDI KUWA ARDHI YA ISRAEL IMETAKASWA NA IMEANDALIWA KWA AJILI YAO:
Allah (s.w.t.) amesema: Enyi watu wangu! Ingieni katika hiyo ardhi iliyotakaswa ambayo Allah amekuandikieni. Wala msirudi nyuma, msije mkawa wenye kukhasirika.(5:21)
Katika aya hapo juu, Allah anawaita Wayahudi kupitia Musa "WATU WANGU" zaidi ya hapo anawaambia kuwa Waende Israel kwenye ARDHI ILIYOTAKASWA, kumbe ata Allah anafahamu kuwa ardhi ya Israeli si ya Wapalestina. Ndugu msomaji, kwanini Allah anaiita ardhi ya Israel kuwa imetakaswa lakini hakuwai sema hivyo kwa Makka?
Ardhi hii imebarikiwa kiroho na kirutba. Ni jambo hili ndilo lililowafanya watu na staarabu tofauti kuigombania. Agano la Kale inatuhadithia ya kuwa ardhi hii ilibubujika asali na maziwa.(Hesabu, 13:27) Na katika kitabu cha Hesabu Sura ya 13 inatueleza kuwa WAISRAEL walipo kuwa wakitoka Misri walipata humo matunda ya makudhumani, tini na zaituni ambayo yalikuwa makubwa na kila tunda kubebwa na watu wawili.
Swali lamsingi: KWANINI ALLAH HAKUITAJA PALESTINA KWENYE QURAN YAKE?
Waislam, Allah kasema kwa Waisrel kuwa, WAINGIE KATIKA ARDHI ILIYOTAKASWA, sasa, kwanini nyie mnataka Wapalestina ambao hata Allah hawajui, wavamie ardhi ya Israeli?
Waislam wanawivu mkubwa sana kwa Israel kwasababu Allah amesema kuwa Israel ni ardhi iliyotakasika na hakusema kuwa Uarabuni kumetakasika. Huu ni MSIBA kwa Waislam.
ALLAH ANASEMA:
SURAT AL BAQARA 40. Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni neema yangu niliyo kuneemesheni, na timizeni ahadi yangu, na Mimi nitatimiza ahadi yenu, na niogopeni Mimi tu.
Allah anaendelea kusema kuwa Israel wana neema ya Mwenyezi Mungu, lakini hatusomi Palestina ikitajwa hata sekunde moja, wala hatusomi kuwa Waarabu wameneemika.
ALLAH ANASEMA KUWA ISRAEL NI ZAIDI YA WAARABU WOTE
Surat Al Baqara 47. Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni zile neema zangu nilizo kuneemesheni, na nikakuteuweni kuliko wote wengineo.
ALLAH ANAKIRI KUWA AMEWATEUWA WAISRAELI KULIKO WATU WENGIENEO, IKIWEPO WAARABU, KUMBE NDIO MAANA WAARABU WANA CHUKI KUBWA KWA WAISRAELI KWASABABU WAO HAWAKUTEULIWA
Kama ulivyo soma hapo juu, Israel ina neema na ni zaidi ya wengine wote, pamoja na Palestina. Kumbe ndio maana Waarabu hawana ubavu kwa Israel.
Leo ningependa muelewe kuwa, Israel ni nchi iliyo barikiwa na hata Waarabu wafanye nini, hata Allah wao amekiri kuwa Waarabu wataendelea kufuata mkia kwa Israel mpaka Kiyama.
ALLAH KAWAPA ISRAEL KITABU, HUKUMU NA UNABII NA KUWAFADHILISHA KULIKO WALIMWENGU WOTE
Surat Al Jaathiya 16. Na hakika tuliwapa Wana wa Israili Kitabu na hukumu na Unabii, na tukawaruzuku vitu vizuri vizuri, na tukawafadhilisha kuliko walimwengu wote.
Kumbe Israel wamepewa Unabii, Kitabu na Hukumu. Hii ndio sababu Waraabu wanaendelea kusaliti amri kwa Israel.
Kwanini Allah hakuitaja Palestina kwenye Quran?
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

MUHAMMAD AKIRI KUPATA UTUME KWA KUCHEZEWA NAFSI YAKE NA SHETANI

Ndugu msomaji,
Kwanza ningependa tujifunze maana ya neno Nabii:
Nabii ni mtu gani?
Nabii ni mtu aliyeteuliwa rasmi kwa vigezo vya Kiungu ili kuleta ujumbe wa Mungu kwa wanadamu, kwa maneno mengine nabii ni msemaji wa siri za Mungu.
Mitume wote na manabii wote wa Biblia waliwai ongea na Mungu. Lakini, Mtume wa Allah "Muhammad" hakuwai ongea na Mungu HATA MARA MOJA. Je, utume wake tutauamini vipi maana hakuwai ongea na aliye mtuma?
Kama Muhammad alikuwa Mtume wa Mungu, kwanini hakuongea na Mungu aliye Mtuma? Maana ya neno Mtume kwa kifupi: Ni Mtu aliye tumwa.
HEBU TUANGALIE, HUYU MUHAMMAD ALIZALIWAJE NA KUUPATAJE UTUME WAKE?
1. MUHAMMAD ALIKUWA NA SHETANI TANGU KUZALIWA KWAKE,
Abu Huraira (r.a) amesimulia kuwa "Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa na shetani tangu alipozaliwa, (Fat'hul Baary Juzuu ya 6 Uk. 389).
Je, kuna ushahid wowote ule kuwa Muhammad alitolewa Shetani ALIYE KUWA NALO TANGU KUZALIWA KWAKE? Kama upo Basi Waislam, tuleteeni tuuone.
2. MUHAMMAD AKIRI KUPINGWA NA KUBANWA MBAVU ZAKE NA KIUMBE AKIWA PANGONI,
Katika kitabu kiitwacho: Maisha Ya Nabii Muhammad s.a.w uk 16-17 kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al-Farsy, tunasoma kama ifuatavyo;-
Hata siku moja- katika mwezi wa Ramadhani mwezi 17, Jumatatu katika mwaka wa 40 ½ wa umri wake- mtume alimwona mtu kamsimamia mbele yake bila ya kumwona wapi katokea, akamwambia; “soma”. Mtume akamjibu; “Mimi sijui kusoma kwani sijapata kujifundisha kusoma.” Akaja akamkamata akambana, akamwambia tena; “soma,” Mtume akamjibu jawabu yake ileile. Hata mara ya tau akamwambia; “soma- Iqraa Bismi Rabbik.” Akamsomea sura hiyo ya 96 mpaka kati yake. Kisha mtume akaisoma kama alivyosomewa. Hii ndiyo sura ya kwanza kushuka katika Qur’an, ingawa haijawekwa mwanzo.
Mara, yule mtu (Malaika) akaondoka machoni mwake- asimwone kenda wapi. Na mtume naye akarejea kwake-khofu imemshika. Alipofika nyumbani, Bibi Kadhija alidhani ana homa, akamfunika maguo gubigubi na akakaa mbele yake akimsikiliza anavyoweweseka. Hata homa ilipomwachia alimweleza Bibi Kadhija yote yaliyomtokea; na Bibi Kadhija akamtuliza moyo wake, akamyakinishia ya kuwa hapana lolote baya litakalomzukia. Mara bibi huyu akaondoka akenda kwa jamaa yake – Bwana Waraqa bin Naufal- akampa habari yote iliyompata mumewe. Naye akamwamrisha amwite. Na mtume akenda akamweleza habari yake yote. Bwana Waraqa akamwambia; “ Huyo ndiye Jibril aliyemshukia Nabii Musa na Nabii Isa. Basi jibashirie kuwa wewe ni mtume wa umma huu, nami natamani kuwa hai nikuone unavyosimama kuwatengeneza jamaa zako; Inshaallah nitakuwa mkono wako wa kulia” Wakarejea kwao na khofu yote imemtoka”.
Alipokuwa pangoni alichezewa na Shetani: Katika kitabu kiitwacho “ Wakeze Mtume Wakubwa Na Wanawe” kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al Farsy uk.12 tunasoma maneno haya
3. MUHAMMAD AKIRI KUCHEZEWA NAFSI YAKE NA SHETANI
“Basi Mtume akafanya hofu akarejea kwa mkewe akamhadithia; na pale pale homa kubwa kabisa ikampanda akataka afunikwe maguo. Mara akawa anatetemeka kwa nderema na anaweweseka na kusema “Najikhofia nafsi yangu kuchezewa na Shetani na kuniharibu akili yangu na kunizuga”. Bibi Khadija palepale alimdakiza akamwambia; “ Wacha hayo; Siyo yatakayokuwa hayo. Wewe huwezi kuchezewa na mashetani. Shetani hawezi kumchezea mtu mwenye sifa zako. Wewe unatazama vyema jamaa zako, unachukuwa mizigo ya hata watu wasiokuwa wako, unawadhihirishia watu sifa zako nzuri ambazo hakuna mwenye nazo. Unafanya hivi na unafanya hivi. Furahi ndugu yangu. Tua moyo wako, Wallahi! Mimi naona umekwishakuwa mtume”.
Katika tukio hili lililompata Muhammad akiwa pangoni , ndipo Waislamu wote ulimwenguni wanapolieleza kuwa hapo ndipo Muhammad s.a.w alipoletewa wahyi (ufunuo) na kupewa unabii na utume. Lakini unapotafakari juu ya ujumbe huo utaona kuwa hata yeye mwenyewe hajui nini kilichokuwa kimemtokea kule pangoni. Ndiyo maana tunasoma kuwa alipofika nyumbani kwake mkewe Bi. Khadija alimfunika nguo mumewe akidhani ana homa. Muhammad alimweleza mkewe kilichomtokea kuwa ni “Shetani” hakumsema malaika yeyote kama Waislamu wanavyotaka kutuaminisha leo. Kwa sababu kama angekuwa ni malaika kama tunavyosoma ndani ya Biblia ,asingesita kujitambulisha kwa Muhammad kuwa yeye ni nani.
KUFUATANA KITABU CHA MAISHA YA NABII MUHAMMAD, tunajifunza kuwa Muhammad kwa mara ya kwanza kabisa alipata utume wake pangoni baada ya NAFSI YAKE KUCHEZEWA NA MASHETANI.
Wahyi (ufunuo) uliokuja kwa Muhammad alisikia makengele, uso kuwa mwekundu, jasho kumtoka. Katika Bukhar, Hadithi na 2, Juzuu na 1,Al-Lu’lu Kitabu cha 3.Uk. Na.874 Hadithi na 1505 “Hadithi ya Aisha r.a mama wa waumini amesema, kuwa Al Harith ibn Hisham r.a alimuuliza mtume wa Allah s.a.w ‘ Ewe mtume wa Allah hivi wahyi (ufunuo) hukujia vipi?’ Mtume wa Allah s.a.w akajibu, “ Wakati mwingine hunijia kama mlio wa kengele, na aina hiyo ndiyo ngumu zaidi kwangu, inaondolewa hali hiyo kwangu wakati tayari nimeshapata wahyi. Na nyakati nyengine malaika anakuja kwangu akiwa katika mfano wa mtu, kwa hiyo ananieleza na ninayazingatia aliyoyasema.” Aisha r.a alisema , Na hakika nilimwona unamshukia wahyi siku ya baridi kali na ilipomuondoka hali hiyo, paji lake la uso lilichuruzika jasho.”
Muhammad akiwa Medina aliulizwa na Wayahudi ikiwa ufunuo wake umetoka kwa Mungu wa Kweli kwa kumtaka atoe sifa za manabii. Akijibu swali hilo alisema:
Mkweli Mwaminifu Juzuu 3-4 Uk.63.Hadithi Na. 880. “Kasema Mtume (s.a.w):- (Mambo) mane ya sheria za mitume (Kuwa na) na haya,na kujipaka mafuta mazuri,na kuowa (wake),na kupiga mswaki.
Hizi si sifa za Ki-Mungu kwa nabii na mtume bali ni za kibinadamu tu.
4. QURAN INASEMA KUWA, NABII LAZIMA AFANYE MIUJIZA; MUHAMAMD AKIRI KUWA YEYE NI MTUME BANDIA NA HAKUFANYA MIUJIZA
Qur’an nayo inathibitisha kuwa manabii na mitume ni lazima wafanye miujiza.
Qurani 40:78 Suratul Al-Muumini [Waumini] inasomeka “Na kwa yakini tumewatuma mitume kabla yako wengime katika wao tumekusimulia (majina yao na habari zao) na wengine hatukukusimulia na haikuwa kwa mtume yoyote kuleta muujiza wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu”
Muhammad hakupewa kufanya muujiza wowote ili kuthibitisha madai ya unabii na utume wake.
Qur’an 29:50 Suratul Al-Ankabuut (Buibui). “Na walisema “Mbona hakuteremshiwa miujiza kutoka kwa Mola wake? Sema miujiza iko kwa Mwenyezi Mungu tu (akitaka atakuteremshieni na kama hataki basi),nami hakika ni mwonyaji mbainishaji (dhahiri tu).” (Taz. Qur,an 6:35-37 13:7,)
MASWALI:
(i). Kama Jibril ndie alitumwa na Allah, na huyo Allah ni Mungu, kwanini Muhammad alisema kuwa nafsi yake imechezewa na MASHETANI baada ya kukutana na Jibril?
(ii). Kama Jibril alitoka kwa Allah, kwanini Muhammad alipo toka pangoni alisema kuwa Jibril AMEMZUGA AKILI YAKE?
(iii) Je, wapi katika Injili au Taurat au Zaburi tunasoma kuwa Manabii na Mitume katika Biblia walipata kwa njia ya homa na kukiri kuchezewa na mashetani kama Muhammad wa kwenye Quran?
(iv) Kama Muhammad alikuwa Mtume wa Mungu, kwanini hakuongea na Mungu aliye Mtuma? Maana ya neno Mtume kwa kifupi: Ni Mtu aliye tumwa.
3. KUROGWA KWAKE MUHAMMAD
Zaidi ya hayo tunaona Muhammad alirogwa. Kurogwa ni hali ya mtu kuathirika na nguvu za giza yaani uchawi. Je nabii au mtume wa Mwenyezi Mungu wa Kweli anaweza kurogwa?
Amesema Mwanaisha Mkewe Mtume kuwa "Yahudi Mmoja aitwaye Labiid bin Al'answan alimroga Mtume Muhammad, ikawa Mtume baadhi ya Nyakati huchanganyikiwa na kuanza kuita Ovyo ovyo na kupiga makelele. (Sahih Muslim J. 4 uk. 38-39)
Hii ni uthibitisho mwingine mzito unaoonesha kuwa utume wa Muhammad una utata.
MASWALI:
(a) Hivi, kuna Mtume au Nabii yeyote yule ambaye alikiri kurogwa kama Muhammad?
(b) Hivi Allah alikuwa wapi wakati Muhammad anarogwa? [Ingawa Quran inakiri kuwa aliye teremsha uchawi/urogi ni Allah]
(c) Wapi tunasoma kuwa Muhammad aliombewa na kutoa huo uchawi/urogi aliofanyiwa na Labiid bin Al'answan?
YAANI INA MAANA MUNGU ALIKOSA MTU WA KUTUMA MPAKA ATUME MTU ALIYECHEWA NA MASHETANI KAMA HUYU?
Ndugu msomaji,
Muhammad hakuwa Mtume wa Mungu na wala hana sifa za KITUME.
1. Muhammad hakuwai ongea na Allah aliye mtuma.
2. Muhammad alikuwa na Shetani tokea kuzaliwa kwake.
3. Muhammad alikiri kuchezewa na Shetani wakati wa kusimikwa utume wake Pangoni.
4. Muhammad alikiri kuwa Shetani amechezea akili na nafsi yake.
5. Muhammad alikiri kuwa alirogwa na Labiid bin Al'answan.
SASA WAISLAM, NIONYESHENI, wapi kwenye Taurat, au Zaburi au Injili kama kuna Mtume aliye na sifa za ajabu kama za Muhammad.
Karibuni kwa Yesu ambaye ndie Njia Pekee ya Kwenda Mbinguni.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

MASHAHIDI WA YEHOVA WANAPINGA WOKOVU KWA KUMKIRI YESU KRISTO

i. Wanadai kuwa kuna Nafasi ya Pili Kuokolewa.
ii. Wanadai kuwa si nia ya Mungu kuwaokoa watu sasa.
iii. Wanadai kuwa Mavuno ya Injili yamekwisha.
Ndugu msomaji,
NINI MAANA YA KUOKOKA?
KUOKOKA ni lugha ya kawaida kabisa, yenye maana ya;
Kunusurika, kusalimika, kupona, kukombolewa, kufunguliwa au kutoka katika janga au hatari fulani. Ambavyo jamii yetu maneno haya tunayatumia sana,
NINI MAANA YA WOKOVU?
Watu wengi neno hili wamelitafsiri vile wa pendavyo au waonavyo sasa Swali hili acha lijibiwe na maandiko matakatifu, na maneno haya yasibadilishwe kwamba ni wakati gani wa kuokoka kitendo kikishamalizika cha kukiri kifuatacho ni uwokovu kwa mjibu wa neno, fuatilia hapa chini, “Kwasababu ukimkiri Yesu Kristo kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, UTAOKOKA. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa mtu hukiri hata KUPATA WOKOVU”. (Warumi 10:9-10.)
LAKINI, MASHAHIDI WA YEHOVA WANASEMA KUWA ILE FIDIA ALIYOTOA YESU KWA WANADAMU WOTE HAITHIBITISHI UZIMA WA MILELE WALA HAIWEZI KUKUOKOA:
Kitabu chao cha “Studies in the Scriptures” Vol. 1, uk. 150, cha Mashahidi wa Yehova kinasema, “Ile ‘fidia kwa watu wote’ aliyoitoa yule ‘mwanadamu Kristo Yesu’ haitoi wala kuthibitisha uzima wa milele wala baraka kwa mtu ye yote; bali inamthibitishia kila mtu nafasi nyingine au jaribu la kupata uzima wa milele.”
MASHAHIDI WA YEHOVA WANADAI KUWA KUNA NAFASI YA PILI YA KUOKOLEWA
Katika uk. 143, wanasema, “Nafasi ya pili itakuwa bora kuliko nafasi ya kwanza kwa sababu ya mazoezi yaliyopatikana katika matokeo ya jaribu la kwanza.” Tena, katika uk. 130, 131 wamesema: “Wote walihukumiwa mauti kwa sababu ya kuasi kwake Adamu, na wote watafurahia (katika maisha hayo au yanayokuja) na nafasi kamili kupata uzima wa milele kwa masharti mema ya Agano Jipya.”
LAKINI, MAFUNDISHO YA BIBLIA YANASEMA NINI KUHUSU WOKOVU?
HAKUNA NAFASI YA PILI KUOKOLEWA KAMA WANVYODAI MASHAHIDI WA YEHOVA!!!!!
Soma Waebrania. 9:27, “Kufa mara moja na baada ya kufa hukumu.”
Luka. 9:59-60, “Akamwambia Waache wafu wawazike wafu wao.”
Matendo. 13:44-46 “Kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa milele.” Je, alisema hapa kwamba wata pata nafasi ya pili! Hata siku moja!
Waebrania. 10:26, “......haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.”
Kwa hiyo tumeona kwa urahisi kwamba Biblia inatufundisha kwamba tutaishi na tutakufa mara moja tu na bada ya kufa hukumu!!
Lini unatakiwa ufanye uamuzi huu muhimu?
Hebu MUNGU na aseme nawe kupitia maneno yake ambayo ni amina na kweli anasema:
Warumi 13:11 Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
2Wakorintho 6:2 "Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa"
Biblia inaonya kuwa "tazama, wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa" yaani wakati huu unaposoma hapa ndio wakati wako wa kutubu na kumgeukia Mungu kwa njia ya kristo kama bado haujafanya hivyo kwani huu ni uamuzi ambao kila mwanadamu lazima aufanye.Mungu ana kalenda yenye miaka mingi lakini kwenye swala la kuukiri wokovu wa kristo wakati ni sasa..Ninakuomba umpe kristo maisha yako,ili hata kama ukifa muda wowote akupokee na uishi naye milele.
MASHAHIDI WA YEHOVA WANAENDELEA KUFUNDISHA KUWA SI NIA YA MUNGU KUWAOKOA WATU KATIKA KIPINDI CHA INJILI BALI ULIMWENGU UTAOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA UTAWALA WA MIAKA 1000.
Mafundisho ya Biblia yanasema nini kuhusu Wokovu:
Yesu mwenyewe alifundisha katika Marko. 16:15-16, kwamba tuhubiri Injili ili watu waokolewe. Na tangu siku ya Pentekoste wakovu umehubiriwa, Matendo. 2:38, 40; 13:26, 47. Pia Paulo alisema, “LEO NI SIKU YA WOKOVU”, katika 2 WaKorintho. 6:2; Wafilipi. 2:12. Na katika Waebrania. 2:3-4, mwandishi anatuambia kwa urahisi kama tunakataa wokovu hatuwezi kukwepa adhabu!!! Kwa hiyo ina maana tunaweza kukosa wokovu leo!
Na tunakosa kwa kutotii injili, katika kipindi cha Injili.
LAKINI, MASHAHIDI WA YEHOVA WANADAI KUWA, “MAVUNO” YA INJILI YAMEKWISHA.
Katika kitabu chao, “Studies in the Scriptures,” Vol 2, uk. 245, Mashahidi walisema: “Miaka arobaini ya mavuno ya kipindi cha Injili itakoma Oktoba 1914, na vivyo hivyo, upenduzi wa Ukristo, kama unavyoitwa, lazima tutegemee kuuona mara.” Hivyo wanasema kuwa hakuna mtu awezaye kuokolewa baada ya Oktoba 1914, BK. Tena, Ukristo (maana yake madhebehu yote isipokuwa kanisa lao) utapinduliwa mara baada ya mwake ule.
BIBLIA INAWAJIBU MASHAHIDI WA YEHOVA KUWA:
Mwaka 1914 umekwisha kupita zamani; mbona madhehebu bado yapo? Isitoshe, ikiwa mavuno ya kipindi cha Injili yalikwisha mwaka 1914, basi Mashahidi wenyewe walio hai leo wamechelewa!
Imekuwaje wao kudai kuwa wamejua tareje na majira hali Yesu amesema hakuna ajuaye mambo hayo?
(Marko. 13:32; Matendo. 1:7).
WOKOVU NI HAPA DUNIANI
Usikubali uongo wowote wokovu ni hapa duniani na baada ya kufa ni hukumu na hukumu hii itategemea uliishije hapa duniani.” Na Kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, baada ya kufa hukumu, Waebrania 9:27”
“Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo Watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima na wale waliofanya mabaya kwa ufufuo wa hukumu Yohana 5:28-29”
Kwa hiyo maisha yetu ya hapa duniani ndiyo yatakayoamua hukumu yetu itakavyokuwa.
Mungu amezibitisha mwenyewe kuwa kuna Watakatifu Duniani.”Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora, Nao ndio nliopendezwa nao, Zaburi 16:3”
Kataa uongo wowote tunaokoka hapa duniani na tunaishi Maisha ya utakatifu yanayompendeza Mungu.
SALA YA TOBA
Inawezekana kabisa ya kuwa wewe unayesoma ujumbe huu hujaokoka - yaani hujampokea Yesu Kristo ndani ya moyo wako kama Bwana na Mwokozi wako. Lakini sasa umeona umuhimu wa kumpokea Yesu Kristo katika maisha yako.
Naamini Roho Mtakatifu ameweka fursa hii mikononi mwako kwa mpango maalum wa Mungu ili ufike mahali pa kutubu na kuokoka. Inawezekana kabisa, pia ya kuwa hujawahi kuambiwa juu ya umuhimu wa wewe kuokoka. Lakini napenda kukuambia ya kuwa ni mpango wa Mungu uokoke. Soma Wakolosai 1:13,14 na Yohana 1:12-14 na 1 Timotheo 2:3-6 na Warumi 1:16,17 na Yohana 3:7. Ni vigumu kuona baraka za Damu ya Yesu bila ya kuokoka.
Kwa hiyo kama unataka kuokoka - tafuta mahali palipo na utulivu, na usome kwa sauti sala ifuatayo: (ukiweza unaweza kupiga magoti unapoomba sala hii)
“Ee Mungu wangu ulie Mtakatifu. Ninakuja mbele zako. Mimi ni mwenye dhambi. Naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizokukosea katika maisha yangu. Ninatubu kweli. Naomba damu ya Yesu Kristo iliyomwagika msalabani kwa ajili yangu initakase sasa katika roho yangu na nafsi yangu na mwili wangu. Nimefungua moyo wangu. Bwana Yesu Kristo nakukaribisha ndani yangu. Ingia kwa uwezo wa Roho wako – uwe Bwana na Mwokozi wangu kuanzia sasa na siku zote. Ahsante kwa kunisamehe na kwa kuniokoa. Nimejitoa kwako nikutumikie katika siku zote za maisha yangu. Shetani hana mamlaka tena juu yangu katika jina la Yesu Kristo. Amina.
Ikiwa umesoma sala hii kwa kukusudia kabisa na kwa imani, basi wewe umeokoka na dhambi zako zimesamehewa na kusahauliwa na Mungu sawasawa na alivyoandika katika neno lake. Damu ya Yesu iko juu yako sasa.
Baada ya kuokoka
Unapoanza maisha haya mapya katika Yesu Kristo nakushauri mambo yafuatayo:
1.Zungumza na Mungu kwa maombi kila siku (Yohana 15:7)
2. Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku (Matendo ya Mitume 17:11)
3.Mruhusu Roho Mtakatifu akutawale (Wagalatia 5:16-25; Warumi 8:14-17)
4.Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako (1Petro 5:7; Zekaria 4:6)
5.Usiache kukusanyika na kushirikiana na wengine waliompokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao kama wewe ili uimarike zaidi (Waebrania 10:25)
Ukipenda unaweza kuniandikia kwa anwani hii hapa chini juu ya uamuzi uliofikia leo wa kuokoka, ili tumshukuru Mungu pamoja, na tuzidi kukuombea; na pia, tukutumie maandiko mengine ya kukusaidia: maxshimbaministries@gmail.com.
Ni maombi yangu Mungu ayafungue macho ya Mashahidi wa Yehova kwa ukweli wa injili na mafundisho ya kweli ya neno la Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Tuesday, March 1, 2016

MUHAMMAD AKIRI KUWA ALLAH NI MUNGU WA KIPAGANI

Je, Wakristo na Waislam, wanaabudu Mungu mmoja?
Je, Allah ni Mungu wa Kipagani?
Ndugu wasomaji, kwa mara nyingine tena, Nabii wa Allah amekiri kuwa Wakristo na Waislam hawaabudu Mungu mmoja na Allah ni mungu wa Kipagani.
Katika hiki kijarida tunaangalia ushahidi mbalimbali kuwa, Allah sio Mungu wa Adam, Musa na Mitume wote walio tajwa kwenye Biblia Takatifu.
Kutokana na Surat Al Kafirun iliyoteremka Makka, Nabii Muhammad anakiri kwa mdomo wake kuwa Wakristo na Wayahudi hawaabudu Mungu mbaye anaabudiwa na Waislamu.
Sura 109 1. Sema: Enyi makafiri! 2. Siabudu mnacho kiabudu;
3. Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu. 4. Wala sitaabudu mnacho abudu. 5. Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu. 6. Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.
Surah hii inamatatizo mengi sana ambayo ypo wazi kuwa, madai ya Wiaslam ya Mungu wa Wakrist na Mungu wao ni mmoja, ni batili na hayana ushahid.
TATIZO LA KWANZA: Hivi, hii Surah inamzungumzia nani?
(a) Watu wa Kitabu (Wayahudi, Wakristo na labda Wasebia)?
(b) Makafir wa Makkah?
Quran hapa imeshindwa kutueleza kuwa, Muhammad alikuwa anaongelea ummah upi.
TATIZO LA PILI: Hata kama ni moja ya dai la (a) au (b) hapo juu, hii Surah ya 109 imejaa utata na kupinga aya mbaimbali za Quran ambazo zinadai kuwa Wakristo, Wayahudi na wengine wote wanaabudu Mungu mmoja ambaye anaabudiwa na Waislamu.
Surat Al Baqara 62. Hakika Walio amini, na Mayahudi na Wakristo, na Wasabai; yeyote atakaye muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akatenda mema basi watapata malipwa yao kwa Mola wao Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.
2: 139. Sema: Mnahojiana nasi juu ya Mwenyezi Mungu, naye ni Mola wetu Mlezi na Mola wenu Mlezi, na sisi tuna vitendo vyetu na nyinyi mna vitendo vyenu? Nasi tunamsafia Yeye tu
Surah 3: 64. Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka basi semeni: Shuhudieni ya kwamba sisi ni Waislamu.
KWENYE Surat Al Ankabut 46. Wala msijadiliane na Watu wa Kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa, isipo kuwa wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni: Tumeyaamini yaliyo teremshwa kwetu na yaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu kwake.
Kwenye hiyo aya hapo juu, Muhammad anadai kuwa Mungu wa Wakristo, Wayahudi na Waislam ni mmoja.
Hivyo basi, kwenye ushahidi tulio sona unaonyesha kuwa kikundi cha (b) nacho kinaabud Mungu wa Waislam ingawa vilevile kinaabudu miungu mingine na mbalimbali.
Surah 29: 61. Na ukiwauliza; Nani aliye umba mbingu na ardhi na akafanya jua na mwezi kuti'ii amri yake? Bila ya shaka, watasema: Mwenyezi Mungu. Wapi basi wanako geuzwa? ***
62. Mwenyezi Mungu humkunjulia, na humdhikishia, riziki amtakaye katika waja wake. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu. ***
63. Na ukiwauliza: Ni nani anaye teremsha maji kutoka mbinguni, na akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake? Bila ya shaka watasema: Ni Mwenyezi Mungu. Sema: Alhamdu Lillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Bali wengi katika wao hawafahamu. ***
Surat An Nahl 35. Na washirikina wanasema: Mwenyezi Mungu angeli taka tusingeli abudu chochote badala yake, sisi wala baba zetu, wala tusingeli harimisha chochote bila ya Yeye. Kama hivyo walifanya walio kuwa kabla yao. Basi lipo lolote juu ya Mitume isipo kuwa kubalighisha kwa uwazi? ***
Wapagani tulio wasoma hapo juu, walikuwa wanarudia na au sema maneno ambayo Allah aliyasema kwa Muhammad.
Surat Al Ana’am 107. Na lau Mwenyezi Mungu angeli penda, wasingeli shiriki. Na Sisi hatukukufanya wewe uwe mtunzaji wao. Wala wewe si mlinzi juu yao. ***
Mwisho basi:
Surat Azzumar 3. Hakika Dini Safi ni ya Mwenyezi Mungu tu. Na wale wanao wafanya wenginewe kuwa ni walinzi wakisema: Sisi hatuwaabudu ila wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu - Hakika Mwenyezi Mungu atahukumu baina yao katika wanayo khitalifiana. Hakika Mwenyezi Mungu hamwongoi aliye mwongo kafiri. ***
Katika aya hapo juu, tumejifunza kuwa mungu wa Wapagani ni Allah, na hao miungu wao wengine walikuwa ni wasaidizi katika kumwabudu Allah. Hivyo basi, Allah, ndie aliye kuwa MUNGU WA MKUU WA KIPAGANI.
Kuna aya moja katika Quran ambayo inawasema watu ambao wanamwamini Allah kama muumba wa vitu vyote:
Surah Luqman (31:25). Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu. Wewe sema: Alhamdulillahi! Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Lakini wengi wao hawajui kama hii aya inazungumzia kundi la A au B, au yote mawili, hii aya ipo wazi kuwa, Muhamamd alijua ni kuwa anamwamini Allah wa Magani wa Mekkah.
Ngoja niweke kwa kifupi hiyo aya:
1. Wakristo na Wayahudi wanadaiwa kumwabudu Allah.
2. Wapagani na waislam vilevile nao wanamwabudu Allah, ingawa walikuwa na miungu wengine.
Kama hii ndio dai letu, ni kivipi Surah 109 idai kuwa Makafiri hawamwabudu mungu wa Muhammad na hawaabudu anacho abudu Muhammad?
Kusema kuwa hii aya inahusu waabudu “idols” ni Wapagani peke yao, ni uongo kwasababu zifuatazo:
1. Waislam wanafahamuje kuwa hii aya iliteremshwa kwa ajili ya Wapagani peke yao?
2. Hata kama hii aya ilikuwa inawaongelea Wapagani peke yao, je, Quran si inasema kuwa Wapagani walijua kuwa wanamwabudu Allah, na hivyobasi walikuwa wanaabudu alicho kuwa anaabudu Muhammad.
Ni kweli kuwa Muhammad hakuabudu miungu wao wote, lakini ukweli unabakia palepale kuwa wote Muhammad na Wapagani waliabudu mungu wa Kipagani aitwaye Allah kama ilivyo semwa kwenye sura 109:3.
Kwa mfano, Quran inadai kuwa Muhammad aabudu ambacho Wapagani waliabudu isipokuwa Allah:
Surat Yunus (10: 104). Sema: Enyi watu! Ikiwa nyinyi mnayo shaka katika Dini yangu, basi mimi siwaabudu mnao waabudu nyinyi badala ya Mwenyezi Mungu. Lakini mimi namuabudu Mwenyezi Mungu anaye kufisheni. Na nimeamrishwa niwe miongoni mwa Waumini.
Surat Ghafir (40:66). Sema: Mimi nimekatazwa kuwaabudu hao mnao waomba badala ya Mwenyezi Mungu, zilipo nijia hoja zilizo dhaahiri kutokana na Mola wangu Mlezi. Na nimeamrishwa nisilimu kwa Mola wa walimwengu wote.
Hizo aya hapo juu zinasema kuwa, Wapagani walikuwa wanamwabudu Allah, pamoja na miungu wengine wa kipagani.
Hivyo basi, leo tumejifunza kwa undani kabisha kuwa Muhammad alikuwa anamwabudu Allah ambaye ni mungu wa kipagani. Jina la Baba yake Muhammad ni Abdallah, likimaanisha slave of allah. Inafahamika kuwa Muhammad ndie muislam wa kwanza, au sio. Kama hayo madai ni kweli, je, baba yake Muhammad alilipata wapi jina la Abdallah kama si yule Allah mungu wa kipagani?
Hakika Allah aabudiwe na Wapagani ni yule yule ambaye aliabudiwa na Muhammad.
Katika Hudma yake
Max Shimba Ministries
@February 9, 2015

MUHAMMAD AKIRI KUWA DHAMBI ZAKE HAZIKUSAMEHEWA

Katika kitabu chake " mwisho mstari wa mbele "anaandika Reza Safa F inasema katika hadith ambapo mke wa Muhammad Khadija kumtaka kusamehe dhambi yake, Muhammad alimjibu kuwa hakuwa na uhakika wa kusamehewa dhambi zake mwenyewe! Angewezaje kusamehe dhambi yake?
YESU HAKUWA NA DHAMBI NA WALA HAKUWAI FANYA DHAMBI
Lakini kwa upande mwingine, Biblia na Quran vinasema kwamba Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, hakuwa na dhambi na wala hakutenda dhambi:
Waebrania 4:15 Kwa maana huyu kuhani wetu mkuu si kuhani ambaye hawezi kutuhurumia katika udhaifu wetu, bali ni kuhani ambaye kwa kila hali amejaribiwa kama sisi, lakini pasipo kutenda dhambi.
Yesu anaweza kuokoa na kusamehe dhambi kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa bila dhambi, na zaidi ya hapo, Yesu ni Mungu! Alikufa kwa ajili ya watu wote ili kuwaokoa. Kwa kifo chake msalabani alichukua dhambi zetu!
Muhammad hawezi kujiokoa na kusamehe kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa mwenye dhambi kubwa kiasi cha kuomba msamaha mara mia kwa siku.
Sasa ndugu msomaji, hivi ni sahihi kumfuata Mtume ambaye alikuwa mtenda dhambi na hisia mbaya kwenye nyoyo yake?
Karibu kwa Yesu aliye hai. Yeye anamamlaka ya kusamehe dhambi na kukuokoa.
Hakika Yesu ni Mungu.
Kwa maana huyu kuhani wetu mkuu si kuhani ambaye hawezi kutuhurumia katika udhaifu wetu, bali ni kuhani ambaye kwa kila hali amejaribiwa kama sisi, lakini pasipo kutenda dhambi.
MUHAMMAD ALIKUWA NA DHAMBI KUBWA KIASI CHA KUOMBA MSAMAHA MARA MIA KWA SIKU
Leo ni leo asemaye kesho ni mungo. Ndugu zanguni, kila ninapo usoma Uislam, nazidi kupata shaka kubwa kubwa, maana hakuna jema kabisa katika hii dini ya Muhammad na Jibri. Hivi mtu anye omba msamaha mara mia kwa siku, unafikiri ametenda dhambi gani kiasi cha kuogopa namna hii?
MUHAMMAD AOMBA MSAMAHA MARA MIA KWA SIKU:Katika "Sahih Muslim, Kitabu 35, 6522 Idadi" inasema kwamba Mtume Muhammad alikuwa mwenye dhambi kubwa sana kiasi cha kuomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu mara mia kila siku. "Nukuu"
"Al-Agharr al-Muzani, ambaye alikuwa mmoja wa (Mtume) wenzake taarifa kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (amani ilikuwa juu yake) alisema: Kuna (wakati mwingine) aina ya kivuli juu ya moyo wangu, na mimi kutafuta msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu mara mia kwa siku. "
Kumbuka kwamba utamaduni si tu anasema kwamba Muhammad alikuwa mwenye dhambi kubwa, lakini kwamba alijisikia kivuli, hisia mbaya, juu ya moyo wake. Katika kesi hii kwa Muhammad, itakuwa vigumu kwa sababu Qur'an inasema kuwa yeye ni kipaji katika maisha yake na vitendo:
Sasa, kivipi Muhammad alikuwa na kivuli ndani ya nyoyo yake?
Hii chuki aliipataje wakati yeye alikuwa anapokea wahyi kutoka kwa Allah?
Je, inawezekana kuwa hiyo wahyi ndio ilikuwa chuki iliyo jaa ndani ya nyoyo yake?
68: 4
Maisha yako na matendo yako ni `aa [mfano]. (Mohammed Knut Bernstöm, Qur'an)
Watu wote wamefanya dhambi
Biblia inasema kwamba watu wote wamefanya dhambi. Hii ni pamoja na Mtume Muhammad alikuwa mwenye dhambi kama watu wengine wote, lakini Muhammad yeye alikiri kuwa dhambi zake hazikusamehewa ingawa aliomba msamaha mara mia kwa siku.
Ndugu msomaji, kwanini tumfuate na sikiliza Muhammad aliye kiri kuwa dhambi zake hazikusamehewa?
Kwanini Allah alishindwa kumsamehe Muhammad dhambi zake?
Je, Allah anauwezo wa kusamehe dhambi?
Muhammad ndio mtume pekee aliye kufa na dhambi na Mshahara wa dhambi ni mauti ya Jehannam. Warumi 6:23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Kwa sababu mwenye dhambi, amehukumiwa kufa.“Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti”(Warumi 6:23). Hii ina maana kutengwa na Mungu katika Jehanum milele.“Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu” (Waebrania 9:27).
Hivyo basi, kwanini ufe na dhambi kama Muhammad na utengwe na Mungu katika Jehannam?
Rafiki yangu:Ninakuuliza swali muhimu maishani mwako. Furaha yako ya milele au huzuni yako ya milele inategemea jibu Ia swali hili. Swali ni hili:Je, umeokolewa? Si swali la jinsi ulivyo mwema, wala si swali la kama u mshiriki wa kanisa, bali:Je, umeokolewa? Una uhakika kwamba utaenda mbinguni utakapokufa?
Hakikisha kwamba umeokoka. Ukipoteza nafsi yako utapoteza mbingu na utapoteza vyote. Tafadhali, mruhusu Mungu akuokoe sasa hivi.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

UTATA MKUBWA KUHUSU KUTEREMSHWA KWA QURAN

Ndugu msomaji,
Leo tutaangalia UTATA kuhusu kuteremshwa kwa Quran. Allah na Muhammad kwa mara nyingine tena, wameshindwa kutuhakikishia kuhusu lini Quran iliteremshwa?
Hapa chini kuna aya kadhaa ambazo zinaendelea kutuonyesha shaka kubwa kubwa iliyo ndani ya Quran.
ALLAH ANASEMA KUWA, QURAN ILITEREMSHWA MWEZI WA RAMADHANISurat Al Baqara 185. Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa ni uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi. Basi ataye kuwa mjini katika mwezi huu naafunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongoeni ili mpate kushukuru.
Lakini nilipo soma aya kutoka Surat Addukhan, Allah alibadilika na kusema kuwa:
QURAN ILITEREMSHWA USIKU MMOJASurat Addukhan 3. Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji. 4. Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima
Nilipo endelea kuisoma Quran kwa makini katika Surat Al Furgan, Allah akabadilika tena na kusema kuwa:
QURAN ILITEREMSHWA KIDOGO KIDOGOSurat Al Furgan
32. Na wakasema walio kufuru: Kwa nini hakuteremshiwa Qur'ani kwa jumla moja? Hayo ni hivyo ili tuuthibitishe moyo wako, na ndio tumeisoma kwa mafungu.
Ndugu zanguni, hivi ni kweli huyu Allah aliteremsha Quran?
Hivi ni kweli kuwa Allah ni mjuzi wa yote?
Hivi, kwanini Allah anashindwa kukumbuka, ni lini aliiteremsha Quran?
Hivi, hata huyo Muhammad, kwanini anashindwa kumkumbsha Allah wake kuhusu kuteresmhwa kwa Quran?
Mbona hata Jibril na yeye ameshindwa kumkumbusha Allah kuhusu lini aliteresmhwa Quran.
WAISLAM, naomba mnijibu kwa aya na bila ya matusi, KURAN ILITERESMHWA LINI?
Watakabahu,
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ

Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction ...

TRENDING NOW