
“Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.” (Wafilipi 2:9-11)
Kwa mistari hii michache tunaona ya kuwa jina la Yesu kristo lina mamlaka MBINGUNI, DUNIANI na CHINI YA NCHI au KUZIMU.
“Kwa jina la Yesu kila goti lipigwe” maana yake jina la Yesu lipate heshima linavyostahili kila mahali.Likiwa mojawapo ya funguo za ufalme wa mbinguni, jina la Yesu linatupa MAMLAKA mbinguni, duniani na chini ya nchi.
Kwa mfano: tunaokolewa kwa jina la Yesu (matendo ya mitume 4:12). Tunazaliwa mara ya pili kwa jina la Yesu (yohana 1:12). Kwa maneno mengine kwa sababu ya jina lake, Yesu alisema; “Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu. Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu” (yohana 16:23-24)
Mtu anapata furaha iliyo timilifu anapoomba kwa jina la Yesu Kristo! Kwa nini? Kwa sababu akiomba kwa jina la Yesu Kristo – anapata kile alichoomba. Heshima yote hii ya kujibiwa maombi yetu na Mungu Baba inatokana na Jina la Yesu Kristo, aliye Bwana na mwokozi wetu. Yesu Kristo alisema, “Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.” (yohana 12:26)
Hebu tuyatafakari maneno yafuatayo aliyoyasema Kristo juu ya mamlaka iliyomo katika Jina lake.
Biblia inasema, “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu
-watatoa pepo;
-watasema kwa lugha mpya;
-watashika nyoka;
-hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa;
-wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”. (marko 16:17-18).
-watatoa pepo;
-watasema kwa lugha mpya;
-watashika nyoka;
-hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa;
-wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”. (marko 16:17-18).
Hebu na tuangalie kwa undani zaidi baadhi ya ishara alizosema zitatokea tukilitumia Jina la Yesu Kristo.
“Kwa Jina Langu watatoa pepo”
Yesu Kristo alitaka sisi tumwaminio tujue ya kuwa kwa jina lake tuna mamlaka juu ya mapepo. Ni vizuri ufahamu ya kuwa kwa kuwa umemwamini Kristo rohoni mwako kama Bwana na mwokozi wako, basi, una mamlaka yakuwatoa pepo mahali walipo! Ukijua pepo yuko mahali Fulani, una uwezo nanmamlaka ya kumtoa mahali hapo kwa jina la Yesu Kristo, naye atatii!!
Yesu Kristo alitaka sisi tumwaminio tujue ya kuwa kwa jina lake tuna mamlaka juu ya mapepo. Ni vizuri ufahamu ya kuwa kwa kuwa umemwamini Kristo rohoni mwako kama Bwana na mwokozi wako, basi, una mamlaka yakuwatoa pepo mahali walipo! Ukijua pepo yuko mahali Fulani, una uwezo nanmamlaka ya kumtoa mahali hapo kwa jina la Yesu Kristo, naye atatii!!







