Wednesday, November 16, 2016

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA KWANZA)


Ndugu msomaji,
Mwezi huu nitaweka mada kadhaa zitakazo fundisha kuwa, Isa wa Quran na Yesu wa Biblia ni wawili na tofauti:
MAANA YA JINA LA ISA
Ni jambo la kawaida sana jina au majina kuwa na maana. Mfano majina haya ya kiarabu yana maana hizi: Muhammad, linamaanisha mwenye kushukuriwa, Abdalla ni Mtumwa wa Allah; Abu-Bakar maana yake ni Baba wa bikira; Abu Huraira ni baba wa Mapaka. Aidha majina ya Kiebrania nayo pie yana maana. Malaki ni mtumishi au Mjumbe wa Yehova, Isaya ni Wokovu wa Yehova; Ezekiel inamaanisha Mungu hutia nguvu, Daniel – Mungu ni hakimu wangu.
JINA LA ISA MAANA YAKE NINI?
Katika Qurani yenye jumla ya juzuu 30; Surah 114; aya 6236; maneno yenye kutamkia 76,440; herufi 322,373; jina Isa linatamkwa lisa au Aysi limetajwa mara 25. Isa pia ameitwa masihi mara 93. Lakini tunaposoma Qurani iliofarsiriwa/tafsiriwa na Imam Baidawi Vol 1 Ukurasa 160 ameeleza kuwa Isa jina la Kiarabu maana yake ni Wekundu unaozidiana na weupe "ZERUZERU". Hii ndio maana ya Jina la Isa wa Quran. Je, Yesu wa Biblia maana yake nini?
JINA LA YESU MAANA YAKE NINI?
JINA Yesu linatokana na lugha ya Kiebrania ‘Yehoshua’ katika lugha ya Kigiriki wanasema ‘lesous’ inatamka ‘Yesous’ yaani Yesu. Katika lugha ya Kiarabu wanasema ‘Yasu’, kwa kiingereza ni “Jesus” maana yake ‘Bwana anaokoa au Bwana ni Mwokozi’ Isaya 43:6, 10-11.
Katika Biblia ambayo ina jumla ya Sura 1189; aya 31,102; vitabu 66 – Agano la kale vitabu 39 na agano Jipya vitabu 27; Neno Mwokozi kwa Kiingereza wanasema ‘Saviour’ limetajwa mara 55. Ikumbukwe kwamba katika agano jiypa jina Yesu au Yehoshua (kwa Kiebrania) limetajwa mara 1275 katika aya zipatazo 1226.
Zingatia pia kuwa agano jipya lina jumla ya aya 7930 na sura 260 hivyo hapa tunaona jina Yesu maana yake ni Mwokozi na jina Isa ni wekundu uliozidiana na weupe. Kwa kuwa maana ya haya majina tofauti bila shaka Isa sio Bwana Yesu.
Leo tumejifunza kwa kifupi tu kuwa, Jina la ISA lenye maana ya Wekundu unao zidiana na weupe ni TOFAUTI KABISA NA Jina la Yesu lenye maana ya MWOKOZI katika Biblia. Zaidi ya hapo, tafsir ya Jina la Yesu kwa Kiarabu ni Yasu na sio Isa kama ambavyo Waislam wanadai katika vitabu vyao.
Mungu awabariki sana na tuendele kujifunza Neno lake bila ya kuchoka.
Katika huduma Yake,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Max Shimba Ministries Org.

YESU ALIMAANISHA NINI ALIPO SEMA MSIDHANI NALIKUJA KUTANGUA TORATI?


Baadhi ya watu wameshindwa kuelewa kuwa torati imeondolewa kwa sababu ya maneno ya Yesu aliposema “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amini, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie” (Mathayo 5:17-18). Watu hawa hutumia andiko hili kujenga hoja kuwa Torati haikuondolewa.
Maana ya neno tangua:
Kulingana na kamusi ya Kiswahili Sanifu, neno “tangua” maana yake ni vunja kanuni au maafikiano; batilisha.
Maana ya neno “hata”:
Neno “hata” maana yake ni “mpaka”
Kwanza kabisa naomba nitoe mifano kadhaa ya mambo yaliyokuwa ni lazima muumini wa Agano la Kale afuate ili ahesabiwe haki ambayo leo hii ukiyafuata hauwezi kuhesabiwa haki mbele za Mungu:
1. Kutahiriwa; Katika Agano la Kale muumini asiyetahiriwa hangeweza kuhesabiwa haki hata kidogo. Katika Agano Jipya kutahiriwa siyo lazima ili uhesabiwe haki na Mungu (Mwanzo 17:9-10, Galatia 6:15).
2. Katika Agano Jipya tunaweza kula vyakula vyote isipokuwa vilivyotolewa sadaka kwa sanamu au vilivyonyongwa bila kuchinjwa, lakini wakati wa Agano la Kale kulikuwa na kuzuiliwa kula baadhi ya vyakula hasa baadhi ya wanyama kama vile sungura, nguruwe, samaki wasio na magamba, nk. (Matendo 26:12-18).
3. Katika Agano la Kale kulikuwa na utaratibu wa kutoa sadaka za wanyama ili mtu aweze kuhesabiwa haki. Hii ilikuwa sheria. Katika Agano Jipya Yesu amelitangua kabisa hilo halipo tena. Damu yake iliyomwagika inatosha kuondoa dhambi ya kila amwaminiye Yesu.
4. Katika Agano Jipya Kuhani alipaswa kuwa mtu mmoja tu amabaye alipaswa kuendesha ibada yote na kutoa sadaka za kuteketezwa. Hilo nalo Yesu alilitangua baada ya Kifo chake Msalabani kila amwaminiye anakuwa kuhani wa Mungu na anaweza kufanya ibada ya kuongea na Mungu moja kwa moja bila kupitia kwa mtu mwingine.

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA PILI)


Je, kuzaliwa kwa Bwana Yesu ni sawa na Isa?
Taarfa za Malaika kabla ya kuzaliwa kwao, kadiri ya Qurani na Biblia.
Jibrili alivyomtokea Mama wa Isa == Gabrieli alivyomtokea mama wa Yesu:
WAISLAM-JIBRIL Alienda kwa Mariamu aliyekuwa Msikitini Qurani 19:16-17
WAKRISTO-GABRIEL Alienda kwa Mariamu aliyekuwa nyumbani kwake - Lk 1:26-28
WAISLAM-Mariamu Mama wa Isa haijulikani aliishi kijiji kipi wala mji gani wala hata nchi haijulikani. Isitoshe Quran inasema kuwa Jibril ndiye aliyemletea utume Muhammad asiwapelekee Mayahudi (hana kosa) Sura 2:97
WAKRISTO-Lakini Mariamu Mama yake Yesu alitokewa na Malaika Gabriel akiwa katika kijiji cha Nazareti mji wa Galilaya nchi ya Israeli (Lk 1:26) Mariamu Mama wa Yesu ni Myahudi.
WAISLAM-Jibrili hakutoa salamu kwa Mariamu mama wa Isa ila alijimithilisha kwa umbo la binadamu aliye kamili - Sura 19-17
WAKRISTO-Malaika Gabrieli alimsalimia Mariamu Mama wa Yesu – Luka 1:28
WAISLAM-Jibril alimwambia Mariamu kwamba mimi ni mjumbe wa mola wako ili nikupe mwana mtakatifu - Sura 19-19
WAKRISTO-Lakini malaika Gabrieli alimwambia mama wa Yesu kuwa utachukua mimba – Luka1: 31
WAISLAM-Jibrili alisema kwa Mariamu kuwa ili tumfanye mtoto muujiza kwa wanadamu – Sura 19: 21. Isitoshe Jibrili hakutaja jina la mwana kwa Mariamu. Bali alisema ili nikupe mwana mtakatifu.
WAKRISTO-Malaika Gabrieli alisema kwa Mariamu mama ya Yesu kuwa mtoto jina lake utamwita Yesu (Luka 1:31; 2:21) Gabrieli hakusema kuwa atampa mwana Mariamu. Bali alisema, Roho mtakatifu atakujilia juu yako, yaani motto atazaliwa kwa uwezo wa Mungu.
TOFAUTI YA KUZALIWA KWA ISA NA YESU

QURAN NI SAWA NA GAZETI LA UDAKU


WAPAGANI WANASEMA QURAN NI SAWA NA HADITHI ZA KALE.
Hapa ni ushahidi wa baadhi ya mistari ya kuchaguliwa kutoka Quran kutuambia kwamba wapagani walikuwa na ufahamu kwamba Muhammad alikuwa anawaambia hadithi ya kale walizokuwa wamesikia kabla ya-Muhammad:
Wasioamini walisema kuwa Quran ni kama hadithi za watu wa kale wa Kipagani ... 08:31
Wasioamini walisema kwamba Aya za Muhammad zilinakiliwa kutoka hadithi za kale ... 16:24
Wapagani wengi walishasiikia hadithi za ufufuo kutoka katika hadithi zamani za Kipagani... 23:83
Makafiri walisema kuwa 'Qur'ani ni hadithi za kale ambazo walisikia kabla ya Muhammad' ... 25:5
Wasioamini walisisitiza kwamba Qur'ani ni hadithi kutoka vitabu vya kale ... 27:68
Wakasema makafiri Quran imejaa visa vya watu wa kale ... 46:17
Wasioamini wanaliziita na kuzifananisha aya za Muhammad na hadithi za kale ... 68:15
Quran ni sawa na gazeti la udaku tu.
Max Shimba Ministries

MUHAMMAD NI ADUI WA WAKRISTO


Quran 4:51 na 57 (Surat Al Maida)
Enyi mlioamini! Msiwafanye mayahudi na wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika hao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu.
Ndio maana huwa nasema Uislam ni dini ya mashetani.

UISLAM NI DINI YA JEHANNAM


Quran 50 au Surat Qaf 30 (kuapa)
Siku tutakayoiambia Jahanamu, ‘Je! Umejaa?’ Nayo itasema ‘Je kuna ziada (zaidi? Naije tu!
Imesimuliwa na Anas kuwa: mtume alisema watu watatupwa jahanamu, Naye Allah ataiuliza jahanamu akisema je umejaa nayo jahanamu itasema kwani kuna nyingine zaidi na ije tu? Mpaka Allah atakapo ingiza mguu wake nayo jahanamu itasema inatosha! Inatosha

SABABU TANO KWANINI WAKRISTO WANAABUDU JUMAPILI


Ndugu msomaji,
Katika kijarida hiki kifupi, nitakuwekea sababu tano (5) kwanini Wakristo wanaabudu siku ya Jumapili.
Siku ya JUMAPILI, ambayo ndiyo siku ya kwanza ya juma, SIKU YA BWANA aliyoshinda mauti na kufufuka [UFUNUO1:10] Tunaitenga maalum kumwabudu Bwana kwa sababu:-
1) Ni sikukuu ya malimbuko ya mavuno ambayo ilifanywa katika Agano la Kale, SIKU YA PILI baada ya Sabato; Ikiwa ni utabiri wa Kristo ambao ni LIMBUKO lao waliolala [WALAWI23:9-14;1WAKORINTHO15:20].
2) Ni siku ya ushindi ya Bwana wetu Yesu aliyofufuka, na kujidhihirisha kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka kwa Yesu [YOHANA 20:1,19,26 WARUMI 10:9].
3) Siku ya kuja Roho Mtakatifu, Mwangalizi mkuu wa kazi yote ya Mungu katika kanisa, ilikuwa siku ya Pentekoste ambayo ni Jumapili, siku ya pili baada ya sabato [MATENDO 2:1]
4) Siku ya Pentekoste, Jumapili ndiyo siku ya kwanza ambayo kanisa la kwanza lilianza mahubiri na watu 3,000 wakaokoka na kuanza kusanyiko la kwanza la Ibada kanisani [MATENDO 2].
5) Wakristo wa kanisa la kwanza walikusanyika Jumapili [MATENDO 20:6-12;1WAKORINTHO 16:1-2].
Sababu hizi, zinadhihirisha pia wazi wazi kwamba kuabudu Jumapili hakukuanzishwa na mfalme CONSTANTINE wala kanisa Katoliki.
Hakuna andiko lolote linalosema mtu yeyote anayeabudu Jumapili ana alama ya 666 ya mnyama. Huo ni uzushi. Biblia inatupa uhuru wote katika kuchagua siku ya kumwadhimisha Bwana [WARUMI14:5-6]. Vilevile ni muhimu kufahamu kuwa siku zote ni siku za kujifunza Neno [MATENDO 17:11;2:46].
KUSHIKA SIKU, SIYO NJIA YA KUOKOKA
Kushika siku yoyote hata iwe Jumapili, sio njia ya kuokoka.Tunaokolewa kwa kumuamini Yesu kuwa ni BWANA na MWOKOZI na sio kwa kushika siku yoyote [WARUMI 10:9-10,13].
Wokovu wetu siku hizi uko ndani ya Kristo, siyo kwa kushika Torati ya Musa. Kuna watu wasiijua Biblia tena hawaelewi hata Agano Jipya. Hawaelewi KWA NINI Yesu alikufa. Kwa mfano wanaposema, ‘Imeandikwa katika Kutoka 20:8-11 lazima tushiike sabato!’ Je! ina maana mtume Paulo alifundisha uongo? Au alitaka kutudanganya? Au Unafikiri Biblia inajipinga yenyewe? Je! Unaamini Biblia siyo neno la Mungu? Au kwa nini watu wanapenda kujizika katika Agano la Kale?
Najua kuwa narejea kwenye mambo yale yale ambayo tayari nimekwisha yaandika hapo juu. Lakini mambo hayo ni ya kimsingi. Ni lazima tuyaelewe mambo hayo pale tunapoyaangalia maisha ya watu wa Agano la Kale! Kwa kupitia Biblia nzima tunajifunza sasa juu ya Yesu Kristo na wokovu wake. Lakini kama Biblia ni neno la Mungu (na ndivyo lilivyo) kwa nini basi waopo watu wanaopinga mpango wa Mungu kupitia mwanae Yesu Kristo ili waweze kubakia katika mpango wa kale ambaop Mungu mwenyewe ameuondoa?
“Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo… Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.”
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 16, 2016

NENO "MUNGU" KWA KIARABU NI "ILAHA"


USHAHIDI UPO NDANI YA QURAN NA AYA ALIITEREMSHA ALLAH MWEYEWE.
Shahada: LA ILAHA ILLALLAH Muhammadur Rasulullah, Quran 3:18 na soma hapa pia (Sahih Al-Bukhari, Volume 4, Book 56, Number 725)
Hakuna Mungu ila Allah na Muhammad ni Mtume wa Allah. Hii ni Shahada wanayo sema Waislam au mtu anaye taka kuwa Muislam.
Kwasababu Waislam ni wabishi, basi leo nawawekea maana ya hiyo SHAHADA neno kwa neno:
Maneno hayo manne "lâ ilâha illâ allâh" yana maanisha hivi:
:
lâ = HAKUNA, no, not, none, neither
ilâha = MUNGU, a god, deity, object of worship
illâ = ISIPOKUWA but, except (illâ is a contraction of in-lâ, literally if not)
allâh = ALLAH, allâh
Kama tulivyo soma hapo juu maana ya hayo maneno Manne. Utangundua kuwa Neno ILAHA maana yake ni MUNGU na Neno ALLAH halina Tafsir na kubakia ALLAH (Thibitisha kupitia Al Tafsir Kitengo cha Tafsir cha Serikali ya Saudi Arabia/ http://www.altafsir.com/).
Kumbuka Allah hana wa kufananishwa na au linganishwa. Hivyo Kumfananisha Allah na Mwenyezi Mungu wa Wakristo ambaye ni Yesu au mungu Buddah, au mungu wa Rasta Fari au na mungu wa Wabantu ni KUKUFUR. Allah yeye kasema hana wa kufananishwa wala linganishwa. Kumbe basi Allah sio Mwenyezi Mungu.
NARUDIA TENA, TAFSIR YA NENO:
ILAHA ==> MUNGU
ALLAH ==> ALLAH
Hakuma wa kubisah sasa kuwa Allah sio Mungu.
LEO KWA MARA NYINGINE TENA TUMEJIFUNZA KUWA ALLAH SIO MUNGU.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo

IBADA YA VIATU NA SHUTUMA ZA WAISLAMU KWA WAKRISTO


“IBADA YA VIATU NA SHUTUMA ZA WAISLAMU KWA WAKRISTO”
Kumekuwepo na shutuma nyingi sana kutoka kwa jirani zenu walio kushoto (Waislamu) wakitushutumu sisi Wakristo kwa kuingia kwetu Ibadani hali ya kuwa tumevaa Viatu, wakati wao wanapoenda kuswali msikitini, huingia bila viatu, kuonesha kwamba wao ndiyo wenye kufanya Ibada sahihi kuliko watu wa imani zingine zote Ulimwenguni, shutuma hizo huambatanishwa na baadhi ya maandiko ndani ya Biblia, ambayo kwa sehemu kubwa sana yametumika kuwasilimisha Wakristo (Kuwaingiza kwenye uislamu) wakidhani kwamba, kuingia kwao huko wataenda kufanya Ibada sahihi inayodhaniwa na jamaa zetu waislamu, ibada ya kuvua Viatu, maandiko ambayo huyatumia ni haya:
Kutoka 3:4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.
5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.
Yoshua 5:15 Huyo amiri wa jeshi la Bwana akamwambia Yoshua, Vua viatu vyako miguuni mwako; kwa kuwa mahali hapo usimamapo ni patakatifu. Yoshua akafanya vivyo.
Mandiko haya ndiyo ambayo huwafanya waislamu wavue viatu vyao msikitini, hata wengine kuzifunga YEBO YEBO, au Kandambili zao kwa kutumia kamba, au Kufuri, ili tu kuzuia wezi wasiwezi kuiba yebo yebo zao, hata kama zimetoboka, na maandiko hayo pia yametumika kuwasilimisha Wakristo wengi bila wao kujua kuwa walipotoshwa, sasa fuatana nami katika somo hili ili uweze kujifunza juu ya Ibada hii ya kusali na Viatu, au kusali bila viatu:
1. MUSA NA KUVUA VIATU KATIKA NCHI TAKATIFU
Musu huyu yeye mwanzo alilelewa katika ngome ya Farao, baada ya kunusurika kuuawa akiwa mdogo,wenzie Waebarania ambao walikuwa wanatumikishwa, alijisikia vibaya kuona wakiteswa wakati yeye anaishi vizuri, siku moja baada ya kumona Mmisri mmoja anampiga nduguye Mwebrania, ikabidi Musa amuue Yule Mmisri
Kutoka 2:11 Hata siku zile, Musa alipokuwa mtu mzima, akatoka kuwaendea ndugu zake, akatazama mizigo yao. Akamwona Mmisri anampiga Mwebrania, mmojawapo wa ndugu zake.
12 Basi akatazama huko na huko, na alipoona ya kuwa hapana mtu, akampiga Mmisri yule, akamficha ndani ya mchanga.
Baada ya kumuua huyo Mmisri, habari zile zikawafikia Waebrania wengine bila Musa kujua kama taarifa zile zimeshaenea, siku moja walipokuwa wanagombana Waebrania wao kwa wao, Mussa akaona siyo vema, akaenda kuwaamulia, mmoja wao akadhani Mussa anataka kumuua.
Kutoka 2:13 Akatoka siku ya pili, na tazama, watu wawili wa Waebrania walikuwa wakipigana. Akamwambia yule aliyemdhulumu mwenzake, Mbona unampiga mwenzako?
14 Yule akasema, Ni nani aliyekuweka wewe kuwa mkuu wetu, na mwamuzi juu yetu? Je! Wataka kuniua mimi kama ulivyomwua yule Mmisri? Musa akaogopa, akasema, Kumbe! Jambo lile limejulikana.
15 Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani; akaketi karibu na kisima.

MUHAMMAD ALIKUWA ANAVAA VIATU MSIKITINI


Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujikumbushe na kujifunza kuhusu kusali na viatu katika nyumba za ibada. Hususan Msikitini.
Waislam mara nyingi wamekuwa wakiwashutumu Wakristo na kuwakejeli kuwa, eti wanasali na viatu Kanisani.
Je, Mtume wa Allah aitwaye Muhammad alivaa viatu alipo kuwa anaswali Msikitini?
Hebu tuangalie ushahidi huu hapa:
Ukisoma kitabu cha Al-u-lu wal-marjan Uk. 179
14. Mlango:
Ruhusa ya kusali na Viatu.
325. Hadithi ya Anas Bin Malik (R.a) kutoka kwa Said Bin Yazid Al-Azid (r.a) amesema, Nilimuuliza Anas Bin Malik (r.a) “Hivi Mtume (s.a.w) alisali huku amevaa viatu vyake?” Akanijibu, “Ndiyo” (Bukhari, Hadithi N. 383, Juzuu ya 1)
Hapo tunamuona Muhammad akisali na Viatu, na mlango hapo umesema, Ruhusa ya kusali na Viatu, maana yake waislamu hapo wameruhusiwa kusali na Viatu, pia haikuishia hapo, Muhammad akasema tena kuwaambia Waislamu.
Ukisoma kitabu kinachoitwa “TAFSIRI YA BULUGH AL-MARAM MIN JAM’I ADILLATIL AHKAM
Ukurasa wa 101 Hadithi Na. 171
Abu Said (r.a) amesimulia: Mtume (S.a.w) amesema: “Ye yote miongoni mwenu atakapoenda msikitini kusali, basi atizame, akiona uchafu au najisi katika viatu vyake aondoe kisha aswali navyo”. Abu Dawud Ibnu Khuzaimah ameipa daraja ya Sahih.
*Murad wa kutwaharisha viatu:
Iwapo mtu amekanyaga najisi kwa kiatu, atakitwaharisha kwa kusugua chini mchangani*
Hapo kwa mtu mwenye akili zake timilifu, hawezi kukomaa na kuanza kuwalaumu Wakristo, eti kwa nini wana Sali na viatu? Wakati Muhammad mwenyewe, alisali huku amevaa viatu, na pia akawaambia waislamu wanapoenda kusali, basi watazame viatu vyao kama kuna najisi, basi wavisugue chini mchangani, labda waislamu watuambie wao kusali na viatu, ni Uviviu wa kusugua viatu mchangani? Au mazingira yao wanayoishi hayana mchanga?
Tena Muhammad akakazia zaidi kuhusu Viatu, aliponukuliwa katika Hadithi hii.
Kasema Mtume (S.a.w) “Atakaepata (ona) nge nae anasali, basi amuue kwa kiatu cha kushoto” (Mkweli Mwaminifu, Juzuu ya 1-2, Hadithi Na. 188, Uk, 88)
Muhammad anawataka Waislamu wakimuona Nge basi wamuue kwa kiatu cha kushoto, sasa jiulize, wewe umevua viatu, unaswali peku peku (kama bata) Halafu amekatiza nge, unaweza kweli kumkanyaga kwa mguu? Nachoweza kusema ni uvivu tu wa waislamu katika kusugua mchangani viatu vyao vilivyo na najisi, kwani wameshapewa ruhusa ya kusali navyo.
Kumbe Mtume Muhammad alikuwa anavaa viatu alipo kuwa ndani ya Msikiti.
Kumbe Mtume Muhammad alisali na viatu Msikitini.
Hakika Uislam ni dini bandia.
Max Shimba Ministries Org

Jesus is good because He is God

 

TRENDING NOW