JE, MUHAMMAD AU JIBRIL NI ROHO YA KWELI/ROHO MTAKATIFU?
Leo nitawajibu Waislam wote duniani kwa kutumia Biblia Takatifu kuwa Muhammad hakuwa Roho ya Kweli kama alivyo ahidiwa na Yesu Kristo ambaye ni Bwana na Mwokozi wetu.
Mara nyingi Waislam wanauliza, "Roho ya Kweli ni nani ambaye Yesu alimuhadi katika Yohana 16 aya ya 12 mpaka 14.
Nimekuwa nikiwauliza Waislam, hivi wao wanafikiri huyu Roho wa Kweli ni nani? Na wakanijibu kuwa huyo Roho wa Kweli ni Malaika Jibril.
Yohana 16:13 inasema: Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
Zaidi ya hapo, Waislam wengi wanadai kuwa, Yesu alikuwa anamtabiri Muhammad, na wakati huo huo, wengine wanasema kuwa alikuwa anatabiriwa Jibril. KINYUME CHAKE, kama ilivyo shahidiwa katika Yohana 16 aya 13, Yesu alikuwa anamzungumzia Roho Mtakatifu. Tunafahamu hili kwasababu Yesu anamzungunzia Roho ambaye atawaongoza Wanafunzi wake kuanzia wakati huo na sio miaka mamia baadae.
Zaidi ya hapo, Waislam wengi wanadai kuwa, Yesu alikuwa anamtabiri Muhammad, na wakati huo huo, wengine wanasema kuwa alikuwa anatabiriwa Jibril. KINYUME CHAKE, kama ilivyo shahidiwa katika Yohana 16 aya 13, Yesu alikuwa anamzungumzia Roho Mtakatifu. Tunafahamu hili kwasababu Yesu anamzungunzia Roho ambaye atawaongoza Wanafunzi wake kuanzia wakati huo na sio miaka mamia baadae.
Ukiisoma Biblia kwa makini kuanzia Yohana 16 aya ya 5 mpaka 15 utagundua hapo hapo kuwa Waislam wote pamoja na Allah wao ni waongo.
Lakini, kuna njia nyingi tunaweza kuzitumia kufahamu kama Waislam wako sahihi katika ufafanuzi wao kwa kuangalia na au soma kila wakati Yesu alipo sema "ROHO" katika Injili hiyo hiyo ya Yohana na tuone kama kweli alikuwa anamtabiri Muhammad wa Waislam katika aya mojawapo.
UTHIBITISHO WA KWANZA:
Yohana 1 aya ya 32 inasema: Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake "YESU".
Wote tunafahamu kuwa Muhammad hakuwa Mtakatifu na vile vile hakuwa anapaa kama ndege na alikuja miaka 600 baada ya Kristo, hivyo basi, ni dhahiri kuwa Roho Mtakatifu sio Muhammad ambaye alikuja miaka 600 baadae. Yohana hakuwai mwona Muhammad.
UTHIBITISHO WA PILI:
Yohana 1:33, [ Yohana Mbatizaji anaendelea kusema] "Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu."
Yohana anaweka kiuwazi zaidi aya hiyo hapo juu kuwa Yesu ndie atakaye kuwa anabatiza kwa Roho Mtakatifu.
Kwa kifupi Yesu atamtuma ROHO ambaye ni Mwenye Nguvu ya Mungu na ni Mungu.
Je, Muhammad ni huyo Roho? HAPANA KABISA, kwasababu Yesu aliwabatiza Wanafunzi wake na zaidi ya hapo, wafuasi wake walibatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku ya Pentekoste. Mda mchache baada ya Yesu kupaa kwenda kwa Baba yake Mbinguni, hivyo basi, na narudia tena, hii ilifanyika Miaka mia sita 600 kabla ya Muhammad kuzaliwa. Wanafunzi wa Yesu hawakubatizwa kwa kupitia Muhammad wala Waislam hawabatizi au batizwa.
UTHIBITISHO WA TATU:











