Friday, July 14, 2017

TOA KWANZA BORITI KWENYE JICHO LAKO, KISHA UTATOA KIBANZI KWENYE JICHO LA MWENZAKO.

Image may contain: text


Mathayo 7: 5 Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.
Wakristo watajifunza kutokana na ukosoaji ujengao.
Imeandikwa katika Mithali 9:8-9 " Usimkaripie mwenye dharau, asije akakuchukia; mkaripie mwenye hekima naye atakupenda. mwelimishe mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima; mfundishe mwenye haki naye atazidi kuwa na elimu."
Nimeweka hili somo kuwakumbusha kuwa, unapo mnyooshea mwenzako kidole kimoja, kuna vidole vingine vitatu vinakunyooshea wewe mwenyewe. Je, umesha jiuliza ni kwanini?
Unaposema, fulani ni mzinifu na mtenda dhambi na apigwe mawe, hata wewe ulisha wai zini lakini haukupigwa mawe.
Tuanze kujichunguza wenyewe, je, sisi sio watenda dhambi kama wale?
Kama wewe ulisha wai mwangalia mdada au mvulana kwa matamanio, BASI WEWE NI MZINZI NA MZINIFU.
Kama wewe ulisha iba hata Penseli au chukua karatasi ofisini kwako, wewe ni MWIZI.
Kama wewe ulisha danganya kwa kuomba kazi au ili upate kitu fulani, wewe ni MUONGO.
Kama wewe ulisha mchukia mtu na kukasirika vibaya, basi wewe ni MUUWAJI. N.K
Je, unaweza nusurika na hukumu ya Mungu.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

KWANINI TUNAKULA NGURUWE? (SEHEMU YA TATU)

Image may contain: one or more people

Watu wa imani nyingine wamekuwa wakiwashutumu Wakristo na hata kuwaita makafiri kwa vile eti wanakula nyama ya Nguruwe, kwa madai kuwa eti imekatazwa katika maandiko matakatifu yaani Tourati na ikiwemo Quran.
Leo nataka kuanika wazi ili kama unakula mdudu huyu umle kwa amani bila kuhukumiwa au kushutumiwa na mtu.
Mafundisho ya Agano jipya kuhusu vyakula (Nguruwe).
Biblia inasema mafundisho yoyote yanayokataza mtu kula vitu Fulani ni mafundisho ya Mashetani (1Timotheo 4;1-5).
Ndio maana waganga wa kienyeji mtu anapokwenda kuaguliwa hukatazwa kula baadhi ya vitu Mungu sio Mganga wa kienyeji. Na wanaomwamini hawana sheria ya kuwazuia nini cha kula au kutokula.
Biblia inasema hakuna kitu najisi kwa mtu asiye najisi lakini kitu Fulani ni najisi kwake yeye aliye najisi (Rumi14;14).
Biblia inafundisha kuwa kula au kutokula hakuongezi utakatifu wala hakuzuii tamaa za mwili (Kolosai 2;16-23) hivyo hatupaswi kujitia katika mambo ya kutunga tu ya mtu,au akilizake na maono ya wanao abudu malaika kumuabudu Mungu hakuji kwa kula au kutokula aina fulani ya vyakula bali katika moyo safi (Mathayo 5;8).
Biblia inafundisha kuwa unajisi wa mtu hautoki nje bali ndani ya mtu pia Yesu alitakasa vyakula vyoote (Marko 7;14-16,17-19)
Paulo mtume alifundisha kuwa chakula ni kwa tumbo tu na si mambo ya rohoni.
(1Koritho 6;13).Hoja ya Pepo waliotolewa na Yesu kuwaingia nguruwe je ina maana gani?
Jambo lingine ambalo wanaharakati wa kiislamu hulishikia bango kuwa Nguruwe hawafai ni lile tendo la Pepo waliotolewa kwa mtu aliyeteseka kama kichaa kuomba ruhusa kuwaingia Nguruwe (Marko 5;12-13).
Kwa mujibu wa wachangiaji wa maoni ya kibiblia kama Mathew Henry commentary na wengineo hujaribu kutoa ufafanuzi huu kuhusia na na swala hili.
Nchi ya Wagerasi ilikuwa inakaliwa na Wayahudi wengi walioasi na kufuata mambo ya mataifa, swala la kufuga Nguruwe lisingeweza kufanywa na Wayahudi wa kawaida kwani kwao walikatazwa kula wanyama hao kwa mujibu wa sheria ya Musa.
Hivyo tendo la Yesu kuruhusu pepo kuingia Nguruwe kama walivyojiombea wenyewe lilikuwa ni sehemu ya hukumu kwao kwa kuishi kinyume cha sheria ya Musa, Jambo hili linathibitishwa na maombi ya mapepo “asiwapeleke nje ya nchi ile” maana yake kutokana na uasi uliokuwepo katika nchi ile mapepo bado yalikuwa na kazi katika mji ule, na hivyo waliomba wasihukumiwe kabla ya wakati wala wasifungwe kwani Kristo alikuwa na mamlaka hiyo.
Aidha inaonekana Tendo lile lilifanyika kwa kusudi la kuwafanya wachungaji wa Nguruwe kuingia mjini na kutoa taarifa kwa haraka watu wamtukuze Mungu na kama sehemu ya kutoa Hesabu ya mifugo kupotea hivyo kutokuwa na Kesi. Jambo hili liliwafanya Wagerasi waogope na kumsihi Yesu aondoke mipakani mwao.
Katika eneo hili pia tunaona jinsi thamani ya mwanadamu ilivyo bora nguruwe walikuwa wapata 2000 kwa sasa kilo ya nyama ya Nguruwe ni kati ya 6000/- kwa wastani chukua 6000 zidisha mara 100 yaani kilo za nguruwe mmoja mara 2000 idadi ya nguruwe woote utapata gharama ya 120,000,000/ yaani Bilioni moja na milioniishirini. Hasara waliyoipata wagerasi hailinganishwi na roho moja ya mtu anayepokea wokovu hivyo Kristo alitaka kuonyesha ni jinsi gani Roho ya Mtu ina thamani.
Jambo lingine ni kuonyesha wingi wa pepo ambao walijitaja kuwa ni jeshi legion kwa kawaida kikosi cha askari wa kirumi kilichoitwa legion kilibeba askari 6000 au zaidi.
Pepo hao walikuwa ni wengi na isingeliwezekana watu kujua Mtu huyu anateswa na pepo wengi kiasi gani kama Masihi hangeuliza Maswali na pia kuruhusu Pepo hao kuingia Nguruwe, hii ilisaidia wanafunzi na jamii kujua ni wingi wa mapepo kiasi gani wakati mwingine hutesa watu.bKwa bahati nzuri pia Nguruwe hao walikufa baharini, hii haimaanishi kuwa Nguruwe woote wana mapepo.
Tendo la Masihi hapo halina uhusiano na kula au kutokula Nguruwe bali thamani ya mtu na mateso yanayotokana na Mshetani ambayo waislamu ni rafiki zao.
Kwa kuhitimisha nawaalika watu wote duniani msiwe na wasiwasi wa kula kiti moto na wanyama wengineo mnaojisikia kuwala Karibuni.
Shalom.

MPENDWA SIMAMA IMARA KATIKA KWELI NAYO KWELI ITAKUWEKA HURU

Image may contain: 1 person, text



Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno Yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli. Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.’
Yohana 8:31-32
Inawezekana umechoka na unaogopa kusema jambo fulani kwasababu unaogopa, ndugu zako au jamaa zako au waumini wa imani yako watasema nini. Hakika inatisha na kutetemesha akili unapokuwa katika njia panda ya namna hiyo.
Kukaa na hiyo siri kunaweza kukusababishia mambo mabaya zaidi na kufungua milango mibaya ya shetani maishani mwako. Basi usiogope kusema kweli, maana hata kama watakucheka na kukusimanga, wewe utakuwa huru na moyoni mwako utakuwa na imani.
Basi simama imara leo na mshirikishe jambo nduguyo au muumini mwenzako na sema yote, omba nae na amini kuwa umesha wekwa huru.
HAKIKA Yesu anataka kukuweka huru hii leo. Basi sema kweli nayo kweli itakuweka huru.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

UMESHA MSAMEHE?


Image may contain: 2 people, text

Mpendwa:
(Mathayo 18:21-22"Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.)
Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mungu Mkuu anakwambia samehe saba mara sabini kwa siku. Cha ajabu watu wa siku hizi wamesha lisahau hili Neno la uzima tena lenye nguvu sana. Kama wewe ni Mkristo halisi, basi utakubaliana nami kuwa, NGUVU YA MSAMAHA ni kubwa kuliko HUKUMU unazo zitoa kwa wale walio kukosea au kosa. Haijalishi wamefanya nini, wewe kazi yako ni kusamehe kama ulivyo samehewa na Yesu.
Isaya 43:25 "Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.
Umeona hapo kwenye Isaya? Yesu anafuta makosa yako si kwaajili yako bali kwa ajili yake yeye. Kwakuwa yeye ni Mtakatifu na mwenye huruma. Wewe huwezi fanya lolote lile liweze kukupa msamaha, ni kwa mapenzi yake tu, ndio maana umesamehewa. Lakini leo umeshahu na kuanza kuhumu yule aliye tenda dhambi, au yule aliye zini. Je, wewe hukuwai zini?
Waefeso 4:26-27' Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi.
Wengi wetu tunalala na vinyongo ndani yetu, huku tukijiita ni Wakristo, tena tulio Okoka. Neno linakwambia, "JUA LISICHWE" huku ukiwa na kinyongo ana au uchungu ndani yako. Huko ni kutenda dhambi. Ukifa na uchingu kwenye moyo wako, basi Jehannam inaweza kuwa yako.
Mathayo 6:12"Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
Basi usichoke kuwasamehe deni wadaiwa wako kama mabvyo Yesu ametusamehe.
Luka 17:4 "Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.
Umesha pewa formula ya kusamehe. Je, upo tayari kumsamehe yule aliye kukosea?
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

BAADA YA MFUNGO WA RAMADHAN, WAMERUDIA UTAMADUNI WAO WA KUNYWA KONYAGI

Image may contain: 1 person, sitting and standing


Sahihi Muslim 3753:'' Sisi tulikuwa pamoja na Mtume wa Allah, na Yeye Mtume wa Allah alikuwa na kiu na mtu mmoja akasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, Je, UNATAKA KUNYWA MVINYO? Mtume Muhammad akasema: NDIO. Basi yule Mtu alikwenda kuleta mvinyo. Mtume wa Allah akamwambia: Lete MVINYO ULIO MKALI ILI NINYWE; Basi Mtume wa Allah alipo kunywa ule MVINYO MKALI ALILEWA"
Biblia ishaonya vileo kabla ya muhamad, na muhamad anadai anasadikisha ya manabii waliopita, swali halishindwa kusadikisha ayah ii ifuatayo mpaka akanywa mvinyo mkali? Tazama.
Isaya 5:22 Ole wao walio hodari kunywa kileo chenye nguvu, watu waume wenye nguvu kuchanganya vileo;
Muslim-3721 Mtume wa Allah alikuwa anatumia chombo(bakuri) cha jiwe kunywea mvinyo.
Mithali 23:31,32 Usiitazame mvinyo iwapo ni nyekundu; Iitiapo bilauri rangi yake, ishukapo taratibu.Mwisho wake huuma kama nyoka; Huchoma kama fira.
(Muslim-AlHayd-451). Aisha alikuwa anammiminia mvinyo mtume wa Allah asubuhi na usiku na pia alikuwa anampelekea ndani ya msikiti.

SHETANI LA ULAFI KATIKA UISLAMU

Image may contain: 1 person, standing and indoor


Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujifunze kidogo kuhusu roho ya ulafi ambayo inawasumbuwa ndugu ztu katika Adam. Hebu tusome Biblia kama ushahidi.
Wafilipi 3: 19 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.
Walafi wao wamesha amua kuabudu chakula na mungu wao ni matumbo yao. Mtu mlafi akiona chakula, basi yeye hula kwa haraka haraka na kujaza tumbo lake mpaka anavimbiwa. Ulafi ni dhambi kama ilivyo sema kwevye Wafilipi hapo juu. Ulafi ni kuabudu tumbo.
Mithali 23: 20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa. 21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.
Watu wanao kula nyama kwa Pupa mpaka wanavimbiwa na kushindwa kutembea, hao wana roho chafu ya ulafi, na ni dhambi kuabudu chakula au kuwa mtumwa wa chakula au mtumwa wa tumbo lako.
Kuna dini fulani wao wanapo dai kuwa wanafunga siku thelasini, huwa wanabadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha mpaka wanavimbiwa matumbo yao. Hiyo dini ni dini ya walafi na wanatenda dhambi, huku wao wakifikiria kuwa wanafunga kwa Allah wao.
Wagalatia 5: 16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
24 Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
26 Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
Kama Neno la Mungu linavyo sema kuwa, tusiwe na tamaa za mwili, maana mwili wetu ni hekalu la Mungu. Ikimaanisha kuwa Roho Mtakatifu anaishi ndani ya mwili wetu, na hivyo, ni vyema tuutunze. Ulafu ni roho kutoka kwa Shetani na kula mpaka kuvimbiwa ni dhambi na ni kuabudu chakula na matumbo yetu.
1 Wakorintho 6: 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; 20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
Basi mpendwa, usiongozwe na tamaa za mwili bali ongozwa na Roho aliye ndani yako.
Leo tumejikumbusha kuwa, Ulafi ni roho kutoka kwa Shetani na ni dhambi.
1. Kwanini Waislam wanakula usku kucha wakati wa mfungo wa Ramadhani?
2. Kwanini Allah amewaruhusu kula usiku kucha na kuwakalisha na njaa mchana kucha, je huko si kubadilisha masaa ya kula?
3. Mbona Yesu wa Biblia alipo funga, yeye hakula Daku?
Hakika kubadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha ni ulafi, na ni dhambi mbele ya Mwenyezi Mungu.
Max Shimba Ministries

MUHAMMAD ALIKUWA ANACHUCHUMAA WAKATI WA HAJA NDOGO KAMA WANAWAKE.

Image may contain: one or more people


Aisha Mke Wa Mtume Anasema "Mwenye kukuhadithieni kuwa Mtume Wa Allah (S.a.w) alikwenda haja Nnogo wima musimsadiki, (Mtume) Alikuwa hajisaidii Ila AMECHUCHUMAA"
Al'mugh'niy 1/156 Muhamad Pia Alikuwa Hataki Kuona Muislam Mwanaume Anakojoa Hali Amesimama.
Soma Sunan Ibn Majah 1/112 Hadith Na 309, "Mtume wa Allah aliniona najisaidia wima (Haja Ndogo) akasema: Ewe Umar, Usijisaidie Wima.
MSIBA MZITO SANA HUU.

MUHAMMAD ALIPAKA WANJA KAMA WANAWAKE


Image may contain: 1 person



Sunan Ibn Majah, Hadith Na 309 Muhamad pia alikuwa anatembea Na KIOO Na WANJA,
Ukisoma maisha ya Muhamad kipengele cha Mavazi Na 26 "Muhammad alikuwa na Kitana Cha Pembe Akichania Nywele Zake, alikuwa na Mafuta Na ALIKUWA NA KIOO akijitazama na KICHUPA CHA WANJA ambao akijitia usiku usiku kabla ya kulala na alipenda sana kutumia Manukato..."
Sio Kawaida Mwanaume KUJIPAKA WANJA
MSIBA MZITO SANA HUU KWA MWANAUME KUJIPAKA WANJA NA PODA.

MUHAMMAD ALIVAA MAGAUNI YA AISHA

Image may contain: 1 person, text and outdoor


From the English translation of the Sahih collection of Imam Muslim, Book 031, Number 5984:
Aisha mke wa Muhammad alisema: Nabii wa Mwenyezi Mungu alikuwa anapata ufunuo wakati amevaa nguo zangu au amejifunika ushingi wangu.
The Book Pertaining to the Merits of the Companions of the Holy Prophet (Kitab Al-Fada'il Al-Sahabah) (http://www.usc.edu/…/fund…/hadithsunnah/muslim/031.smt.html…)
************
From the Sahih collection of Imam Muslim, Hadith Number 4472
Volume Title, “From the Virtues of the Companions.”
Chapter Title, “From the Virtues of Aisha.”
Imesimuliwa na al-Hassan ibn Ali al-Hilwani, ikasimuliwa na Abu Bakr ibn Nadir, ikasimuliwa na Abd ibn Hamid, ikapokelewa na Yakun ibn Ibrahim ibn Sa’d Ibn, ikasimuliwa na baba yake, ikasimuliwa na Salih ibn Shihab, ikasimuliwa na Muhammad ibn Abdel Rahman ibn Harith ibn Hisham akasema kuwa Aisha mke wa Nabii Muhammad alisema:
Mke wa Muhammad alimtuma Fatimah, na alipo ingia chumbani alikumkuta Nabii wa Allah amejilaza kitandani huku akiwa amevaa nguo za mkewe.
Source- http://hadith.al-islam.com/Display/Display.asp
MKRISTO MWENYE KUJITAMBUA HAWEZI KUFUATA MWANAUME MWENYE TABIA ZA KIKE.

URITHI WA UISLAM KUTOKA KWENYE DINI ZA KIPAGANI ZA UARABUNI ** SEHEMU YA PILI

Image may contain: sky


Ka’aba
Katika sehemu ya 1 ya makala haya tuliangalia kuhusu asili ya Allah. Katika sehemu hii ya 2 tutaongelea kuhusiana na mji wa Makka na ka'aba, ambayo ni madhabahu kuu ya Uislamu.
Mji wa Makka ndio kitovu cha Uislamu duniani. Kwenye mji huu ndiko iliko Ka’aba, au kama wanavyoamini na kuiita Waislamu Bait – ul- Haram; au Bait – ul- Allah, yaani ‘nyumba ya Allah’ au ‘nyumba ya Mungu’. Na kila Mwislamu kokote duniani anatakiwa kuswali swala 5 kila siku huku akielekeza uso wake Makka iliko hiyo nyumba ya Mungu wao. Vilevile, kila mmoja wao anatakiwa kwenda Makka kuhiji walau mara moja katika maisha yake, maana hija ni moja ya nguzo kuu katika Uislamu. Kwa maana nyingine, Ka’aba ndiyo madhabahu kuu katika Uislamu.
Ka’aba ni nyumba ya umbo la takriban mchemraba ambayo, pamoja na vitu vingine vichache iliyo navyo, kuna kipande cheusi cha jiwe ambacho kimejengewa ukutani kwenye kona mojawapo. Hivyo, Waislamu wanapoenda Makka kuhiji huzunguka Ka’aba na pia kulibusu jiwe hilo, au kuligusa tu, na kama ikishindi kana, basi japo kulinyoshea mkono.
Zamani, Allah anasema, kuwa Muhammad alikuwa akitazama mbinguni wakati anapoomba [nadhani kila mwenye imani juu ya Mungu anaamini kuwa Mungu yuko juu – na huo kusema kweli nadhani ndio mtazamo sahihi kabisa].
Lakini Allah akamwambia mtume wake:
We have certainly seen the turning of your face, [O Muhammad], toward the heaven, and We will surely turn you to a qiblah with which you will be pleased. So turn your face toward al-Masjid al-Haram. And wherever you [believers] are, turn your faces toward it [in prayer]. Indeed, those who have been given the Scripture well know that it is the truth from their Lord. And Allah is not unaware of what they do. (sura Al Baqarah 2:144) – Sahih International Version.
Yaani:
Hakika tumeona jinsi unavyogeuzia uso wako [ewe Muhammad], kuelekea mbinguni, nasi hakika tutakugeuzia kwenye qiblah utakachokifurahia. Hivyo elekeza uso wako kwenye al-Masjid al-Haram. Na kila mtakakokuwa [enyi mnaoamini] geuzieni nyuso zenu kuelekea huko [mswalipo]. Hakika, wale waliopewa Maandiko wanajua vema kuwa ni kweli kutoka kwa Bwana wao. Na Allah anajua kile wafanyacho.
Allah anasema hafurahii sana Muhammad na Waislamu kugeuzia nyuso zao juu mbinguni (aliko Mungu muumba wa vyote – ajabu sana! Ajabu mno!), badala yake akaamuru wageuzie nyuso zao kwenye ka’aba wawapo popote wakati wa kuswali.
Pia anasema kuwa wale waliopewa Maandiko (yaani watu wa kitabu) eti wanajua fika kwamba jambo hilo ni kweli kutoka kwa Bwana wao!
We Allah wewe! Bwana wao yupi tena wakati wewe unasema ndiwe uliyesema na Ibrahimu ili akajenge ka’aba akitokea Kaanani – kilometa zaidi ya 1,000 kutoka Makka? [Tena basi Makka ambayo hata haikuwapo duniani hadi takriban kwenye miaka 400 baada ya Kristo - sasa sijui Ibrahimu alienda kujenga ka'aba porini kusiko hata na mtu mmoja]!! Ina maana kuna Bwana wao ambaye si wewe basi! Basi huyo Bwana wao ana Ibrahimu na Ishmael wa kwake; na wewe una Ibrahimu na Ishmael wa kwako, au siyo?
Kulingana na Quran, ka’aba ilijengwa na Ibrahimu na mwanawe, Ishmael. Quran inasema kwamba:
Remember We made the House a place of assembly for men and a place of safety; and take ye the station of Abraham as a place of prayer; and We covenanted with Abraham and Isma'il, that they should sanctify My House for those who compass it round, or use it as a retreat, or bow, or prostrate themselves (therein in prayer). [Qur'an 2:125].
Yaani:
Kumbukeni, tuliifanya Nyumba ile mahali pa kukusanyikia kwa ajili ya wanadamu na mahali pa usalama; hivyo chukueni ninyi mahali pa Ibrahimu kama mahali pa swala; nasi tulifanya agano na Ibrahimu na Ishmael, kwamba waitakase Nyumba Yangu kwa ajili ya wale wanaoizunguka, au kuitumia kama mahali pa makimbilio, au kuinama, au kusujudu humo (kwa swala).
[Allah anasema kuwa aliifanya nyumba hii kwa ajili ya wanadamu, lakini waislamu hawaruhusu asiye mwislamu, na hasa aliye Mkristo, kwenda kwenye ka’aba; au hata kupita juu kwa ndege!! Inawezekana Allah anaposema ‘mwanadamu’ ana maana ya ‘mwislamu’!]
Kuhusiana na Ibrahimu, hilo ni jambo ambalo tunawaachia Waislamu wenyewe maana sisi wengine tunaamini na hata ushahidi wa kihistoria na kimaandiko unaonyesha wazi kwamba Ibrahimu hajawahi kamwe kukanyaga mguu wake Uarabuni.
Kwa mfano, ufuatao ni ushahidi mmojawapo juu ya jambo hili. Tunasoma kwamba:
Narrated Abu Dhaar: I said, "O Allah's Apostle! Which mosque was built first?" He replied, "Al-Masjid-ul-Haram." I asked, "Which (was built) next?" He replied, "Al-Masjid-ul-Aqs-a." I asked, "What was the period in between them?” He replied, “Forty years.” (Sahih Bukhari 4:55:636).
Yaani:
Imesimuliwa na Abu Dhaar: Nilisema, “Ewe Mtume wa Allah! Ni msikiti upi ulikuwa wa kwanza kujengwa?” Akajibu, "Al-Masjid-ul-Haram." Nikauliza, “Ni upi ulifuata?” Akajibu, “Al-Masjid-ul-Aqs-a.” Nikauliza, “Ulipita muda gani hapo katikati?” Akajibu, “Miaka arobaini.”
Muhammad naye ana mambo! Al-Masjid ul-Aqs-a ndiko hapo penye Ka’aba. Na Al-Masjid-ul-Haram ni hekalu la Mfalme Sulemani kule Uyahudi.
Sasa, hekalu la Yerusalemu lilijengwa na mfalme Sulemani kwenye takriban miaka ya 950 kabla ya Kristo (KK). Hii ni kusema kwamba, kama maneno ya Muhammad ni ya kweli – na ninaamini kwamba hakuna mwislamu ambaye anaweza kukiri kuwa Muhammad ni mwongo – basi, msikiti wa kwenye Ka’aba unatakiwa uwe ilijengwa kwenye 990 KK (ukiongeza hiyo tofauti ya miaka 40).
Hilo sio tatizo. Lakini shida inakuja unapomwingiza Ibrahimu. Ibrahimu aliishi takriban miaka 2000 kabla ya Kristo. Tazama hapa. Hii ni kusema, aliishi miaka takriban 1050 kabla ya kujengwa kwa hekalu la mfalme Sulemani. Sasa, kama Ibrahimu wa Muhammad aliyejenga Ka’aba aliijenga miaka 40 kabla ya hekalu la Sulemani, basi NI LAZIMA awe ni Ibrahimu mwingine na Ishmael mwingine tofauti kabisa na wale wa kwenye Biblia. Vyovyote iwavyo, hilo ni tatizo la Waislamu wenyewe kulitatua. Ni kazi kwao kujiridhisha na kujithibitishia wao wenyewe kwamba, kama wanataka imani yao itokane na Ibrahimu aliyeongea na Mungu wa Israeli, basi hali ndiyo hiyo!
Kutokana na ukweli huo hapo juu, tunabakia na uwezekano wa aina mbili: kwanza, kama Muhammad yuko sahihi juu ya hiyo miaka 40, basi Allah ndiye aliyekosea au aliongopa kusema kuwa Ibrahimu alijenga Ka’aba. Kama Allah yuko sahihi, basi Muhammad ndiye aliyekosea au kuongopa kwamba Ka’aba ilijengwa miaka 40 kabla ya hekalu la Sulemani. [Hata hivyo, kuna uwezekano kabisa huyu ni Ibrahimu mwingine kabisa. Hebu tutafakari yafuatayo:
Hata kama ka’aba ilijengwa na Ibrahimu (wa Biblia au mwingine tofauti), jambo moja ni dhahiri; kwamba wakati Muhammad anatokea na kuanzisha dini yake, ka’aba ilikuwa chini ya wapagani wa Uarabuni huku ndani na nje yake kukiwa na miungu zaidi ya mia tatu.
Ni mwaka 630 baada ya Kristo (BK), ndipo Muhammad na wafuasi wake walitwaa mamlaka ya mji wa Makka na kuifanya ka’aba kuwa sehemu ya kuabudia Mungu mmoja badala ya miungu zaidi ya mia tatu. [lakini usisahau kwenye sehemu ya 1 ya makala haya tulibainisha kwamba allah alikuwa ni mungu wa kipagani tangu maelfu ya miaka nyuma kabla ya kutokea kwa Muhammad. Na unajiuliza; hivi asili ya ‘allah akbar’, yaani ‘allah ni mkuu’ ni nini? Je, si kwa sababu kulikuwa na mamia ya miungu, na allah akiwamo, ndiyo maana Muhammad akawa, kimsingi, anasema, “Hapana. Hiyo miungu yote si kitu. Allah ndiye anayewazidi wote”? Huo ndio muktadha sahihi wa kutamka maneno kama hayo, au siyo? Hilo ni wazo tu ambalo linahitaji utafiti wako wewe unayemwamini Allah; maana mimi wala siamini kwamba Allah ndiye Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.]
Basi turudi kwenye suala la kuwapo kwa mamia ya miungu kwenye ka’aba wakati Muhammad anaingia. Hivi ndivyo tunavyosoma:
Narrated 'Abdullah bin Masud: The Prophet entered Mecca and (at that time) there were three hundred-and-sixty idols around the Ka’aba. He started stabbing the idols with a stick he had in his hand and reciting: "Truth (Islam) has come and Falsehood (disbelief) has vanished." [Sahih Bukhari 3:43:658].
Yaani:
Imesimuliwa na Abdullah bin Masud: Mtume aliingia Makka na (wakati ule) kulikuwa na miungu mia tatu na sitini kuzunguka Ka’aba. Alianza kuichomachoma kwa fimbo aliyokuwa nayo mkononi huku akisema: “Kweli (Uislamu) imeshakuja na Uongo (kutokuamini) kumetoweka.”
Ndugu zangu waislamu, ka’aba wala haina uhusiano na Mungu Mkuu aliyeumba mbingu na nchi. Ilikuwa ni madhabahu tu ya kipagani kwa ajili ya kuabudia mwezi, jua na nyota.
Hivi ndivyo tunavyoambiwa:
Narrated Abu Huraira: “In the year prior to the last Hajj of the Prophet when Allahs Apostle made Abu Bakr the leader of the pilgrims, the latter (Abu Bakr) sent me in the company of a group of people to make a public announcement: 'No pagan is allowed to perform Hajj after this year, and no naked person is allowed to perform Tawaf of the Ka’aba.'” (Bukhari V2, B26, #689 (V1, B8, No 365).
Yaani:
Imesimuliwa na Abu Huraira: “Kwenye mwaka kabla ya Hija ya mwisho ya Mtume pale Mtume wa Allah alipomfanya Abu Bakr kuwa kiongozi wa mahujaji, Abu Bakr alinituma pamoja na kundi la watu wengine ili kutoa tangazo: ‘Hakuna mpagani anayeruhusiwa kufanya Hija baada ya mwaka huu, na hakuna mtu aliye uchi anayeruhusiwa kufanya Tawaf ya Ka’aba.
Sijui ndugu msomaji kama unaiona maana ya maneno haya? Hiki ndicho tunachosoma humu:
1. Waislamu na wapagani walikuwa wakifanya hija pamoja kwenye ka’aba kwa miaka mingi hadi hapo Abu Bakr alipofanywa kiongozi.
2. Wakati wawapo kwenye hija, wapagani walikuwa wakifanya Tawaf (kuzunguka ka’aba) wakiwa uchi.
3. Wapagani walikuwa wakiabudu miungu yao ya kipagani kwenye ka’aba na waislamu wakimwabudu Allah.
Ili uone uzito wa jambo hili vizuri, hebu piga picha ya Hekalu la Sulemani alilojenga Yerusalemu kwa ajili ya Yehova. Yaani humo ndani ya hekalu wawe wanasali Wayahudi wanaomwamini Yehova na pia wapagani wanaoabudu jua, na mwezi na nyota; tena wakiwa uchi!!!!!!!
Kwa kuwa jambo hilo haliingii kamwe akilini; na haliwezekani, jibu ni moja tu: ni Muhammad ndiye aliyeenda kuingilia madhabahu ya wapagani na si kinyume chake!
Na ndiyo maana Muhammad alikuwa na ujasiri wa kutaka kuibomoa ka’aba. Hivi ndivyo tunavyosoma:
Narrated Aswad: Ibn Az-Zubair said to me, "Aisha used to tell you secretly a number of things. What did she tell you about the Ka'ba?" I replied, "She told me that once the Prophet said, 'O 'Aisha! Had not your people been still close to the pre-Islamic period of ignorance (infidelity)! I would have dismantled the Ka'ba and would have made two doors in it; one for entrance and the other for exit." (Sahih Bukhari 1:3:128).
Yaani:
Imesimuliwa na Aswad: Ibn Az-Zubaid aliniambia, “Aisha alikuwa akikusimulia kwa siri mambo kadha wa kadha. Je, alikuambia nini kuhusiana na ka’aba? Nikajibu, “Aliniambia kwamba, kuna wakati Mtume alisema, ‘Ewe Aisha! Kama watu wa kwenu wangekuwa bado hawako karibu na enzi ya ujinga ya kabla ya Uislamu (ukafiri), ningebomoa Ka’aba na ningejenga milango miwili; mmoja wa kuingilia na mwingine wa kutokea.’”
Hebu piga picha hapa pia; kwamba Musa aliambiwa na Yehova atengeneze hema ya kukutania. Akapewa maelekezo kwa undani sana ya namna kila kitu kinavyotakiwa kuwa, na akaambiwa afanye sawasawa na alivyoonyeshwa na Yehova. Halafu anakuja kutokea mtume au nabii miaka mia kadhaa inayofuata anasema, “Mimi naona katika nyumba hii Yehova alikosea kuweka mlango mmoja. Inatakiwa milango miwili hapa.” Hivi inawezekana kweli?
Sasa, kama kweli ni Allah ndiye alimwambia Ibrahimu na Ishmael wajenge ka’aba, inaingia kweli akilini Muhammad kuja kusema angeweza kuibomoa na kuijengea milango miwili?? Mwanadamu anaweza kumsahihisha Mungu?
Lakini hilo linawezekana tu kama nyumba yenyewe haina uhusiano wowote na Mungu; kama ambavyo ka’aba haina kamwe uhusiano wowote na Mungu wa mbinguni.
Duniani leo kuna makanisa na mahekalu mengi, lakini tunapoongelea hema ya kukutania ya Musa au hekalu la mfalme Sulemani, tunakuwa tunaongelea mahali pa pekee sana ambako Mungu mwenyewe kibinafsi ndiye aliyetoa vipimo na kuchagua mahali pa kujenga. Vivyo hivyo, kuna misikiti mingi duniani, lakini unapoongelea msikiti wa kwenye ka’aba, basi ni allah mwenyewe (anayedaiwa kuwa ni Mungu wa Ibrahimu) kujihusisha moja kwa moja na kazi hiyo. Sasa, hebu pia tazama picha hii hapa chini, kisha ujiulize mwenyewe kama Mungu wa mbinguni anaweza kuagiza nyumba yake ijengwe kwenye eneo lenye sifa hizi:
Nimekwambia hapo mwanzo kwamba kwenye ka’aba kuna jiwe jeusi (wanaloliita Al-hajar Al-aswad) ambalo waislamu hulibusu au kuligusa kama sehemu ya ibada yao humo. Lakini tunaambiwa hivi kuhusiana na jiwe hilo:
Later, Umar said to the black stone, "I know that you are a stone, that neither helps nor hurts, and if the messenger of god had not kissed you, I would not kiss you." (Sahih Bukhari, volume 2, #667).
Yaani:
Baadaye, Umar aliliambia lile jiwe jeusi, “Najua kuwa wewe ni jiwe ambalo haumsaidii wala kumdhuru mtu, na kama mjumbe wa mungu asingekubusu wewe, kamwe nisingekubusu.”
Jiwe hilo ni linaloonekana kwa mbele kama doa jeusi
Hiyo ndiyo hali ya Uislamu na waislamu hadi leo. Karibu kila kitu kwenye uislamu kiko kinyume na hali halisi ya maisha; hata mioyo yao inakataa kuvikubali, lakini wafanye nini sasa na wao wameshajiungamanisha na Muhammad? Anachosema Umar, kimsingi, ni kuwa, “Moyoni najisikia kabisa kwamba hii habari ya kubusu jiwe ni ubatili mtupu, lakini sina namna ya kuacha maana mtume amelibusu.”
Naamini Waislamu wengi wanafikiri kuwa ka’aba iliyopo leo ndiyo hiyohiyo ambayo Allah amewaambia kuwa ilijengwa na Ibrahimu na Ishmael. Lakini ukweli ni kwamba, ka’aba ilishavunjwa na kujengwa zaidi ya mara kumi. Tazama hapa. Kwa hiyo, hii iliyopo leo ni ujenzi wa hivi karibuni tu wa serikali ya Saudia.
Hitimisho
Ni kweli kabisa ka’aba ni nyumba ya Allah, lakini KAMWE si nyumba ya Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Wala Ibrahimu wa Israeli hajawahi kwenda Uarabuni kujenga ka’aba. Hii ilikuwa ni madhabahu ya mungu mwezi, jua, nyota na miungu zaidi ya 360 iliyoabudiwa na wapagani wa Uarabuni. Ukweli ni kwamba hii wala haikuwa ka’aba pekee. Zilikuwapo ka’aba nyingi ambamo wapagani wa huko walikuwa wakiabudia miungu yao. Umeona mwenyewe jinsi ambavyo wapagani hao walikuwa wakienda kuhiji Makka kwenye ka’aba tena wakiwa uchi. Iweje leo useme kuwa mambo yaleyale; palepale kuwa ni mambo ya kumwabudu Mungu aliyeumba mbingu na nchi?
Ndiyo maana Yehova aliwaonya Waisraeli akisema: Basi zishikeni amri zangu zote, na hukumu zangu zote, na kuzifanya, .... Nanyi msiende kwa kuziandama desturi za taifa niitoayo mbele yenu; kwa kuwa wao waliyafanya mambo hayo yote, na kwa ajili ya hayo niliwachukia. (Walawi 20: 22-23). Lakini ajabu ni kwamba Allah anasema kinyume kabisa. Kimsingi, anachosema kwa Waislamu ni kwamba: "Enendeni kwa kuzifuata kawaida za watu waliokuwa wanaishi Makka"!!!
Je, Mungu wa mbinguni anahitaji nyumba hapa duniani ili aweze kuishi humo? Hivi kwa ukuu wake wote, Mungu huyu atakaa kwenye kachumba ambacho ndani yake hakuna hata kitu?
Yesu Kristo anakuita akupe uzima wa milele sasa. Muda unakimbia mbio!
Katika ulimwengu wa leo kupata taarifa si tatizo. Tunayo maktaba kubwa kuliko zote tangu kuumbwa kwa ulimwengu yenye kila taarifa uitakayo duniani - yaani Intaneti. Ni wewe tu kujua unataka nini.
Hoji mambo.
Chunguza.
Fanya utafiti.
Chukua hatua.

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW