Saturday, May 8, 2021

KALENDA YA KIYAHUDI


Kalenda ya Kiyahudi (pia: Kalenda yaKiebrania) ni kalenda inayotumiwa katika dini ya Uyahudi na pia nchini Israel. Inatumiwa kupanga tarehe za sikukuu za Kiyahudi na utaratibu wa kusoma Torati kwa kila wiki.

Liturgia na sala hufuata pia mpangilio wa kalenda hiyo.

Kanuni za msingi

Kalenda ya Kiebrania ni kalenda jua-mwezi.

  • Hii inasababisha ulazima wa kupatanisha tofauti kati ya muda wa mwaka wa Jua (siku 365) na muda wa mwaka wa Mwezi (takriban siku 354).
  • Hapo kalenda ya Kiebrania inaongeza mwezi wa nyongeza mara saba katika kila kipindi cha miaka 19. Kwa hiyo kuna miaka ya kawaida yenye siku 354 na miezi 12. Lakini kila mwaka wa pili au tatu ni mwaka mrefu wenye miezi 13 na siku 384.
  • Utaratibu huo unahakikisha tarehe ya Pasaka kubaki katika majira ya machipuo ya kaskaziniWastani wa muda wa mwaka katika kipindi cha miaka 19 ni siku 365.

Juma

Nje ya kalenda hiyo kuna utaratibu wa wiki yasiku saba zinazoendelea mfululizo, sawa na kalenda ya kimataifa. Hutumiwa kubaini siku ya Shabbat, ambayo ni siku ya kupumzika. Wiki haitegemei mwaka wa jua wala wa mwezi. Badala yake, inategemea hesabu ya siku saba ambazo zinaaminika kurudi nyakati za zamani za Babeli na kutajwa katika masimulizi ya kuumbwa kwa Dunia katika Biblia.

Siku za juma la Kiyahudi

Siku ya juma 
(Kiebrania)
TafsiriSiku inaanza kutoka kuzama kwa JuaSiku inaendelea mpaka kuzama kwa jua
יום ראשון 
yom rishon
siku ya kwanzaJumamosiJumapili
יום שני
yom sheni
siku ya piliJumapiliJumatatu
יום שלישי
yom shelishi
siku ya tatuJumatatuJumanne
יום רביעי
yom revi'i
siku ya nneJumanneJumatano
יום חמישי
yom hamishi
siku ya tanoJumatanoAlhamisi
יום ששי
yom shishi
siku ya sitaAlhamisiIjumaa
שבת
shabbat
Shabbat
(Sabato)
IjumaaJumamosi

Miezi

Mwezi 
namba
katika Biblia
Jina la mweziJina la mwezi 
kwa Kiebrania
Idadi
ya siku
Wakati wa mwakaMaelezo
1Nisanנִיסָן30Machi - ApriliMwezi wa Pasaka
2Iyarאִייָר29Aprili- Mei
3Sivanסִיוָן30Mei- JuniMwezi wa Shavuot
4Tammuzתַּמּוּז29Juni- Julai
5Avאָב30Julai- AgostiMwezi wa Tisha B'Av
6Elulאֱלוּל29Agosti- Septemba
7Tishreiתִּשְׁרֵי30Septemba- OktobaMwezi wa Rosh Hashanah, 
Yom Kippur na Sukkot
8Heshvan 
(au Marheshvan)
(מַרְ)חֶשְׁוָן29 au 30 [1]Oktoba - Novemba
9Kislevכִּסְלֵו30 au 29Novemba - DesembaMwezi wa Hanukkah
10Tevetכִּסְלֵו29Desemba- Januari
11Shevatשְׁבָט30Januari- Februari
12Adarאֲדָר29Februari-MachiKatika mwaka mrefu, mwezi wa 13 unaongezwa unaoitwa pia Adar, lakini inapewa namba; kwa hiyo katika mwaka mrefu kuna Adar I na Adar II

Siku na wiki

Katika kalenda ya Kiyahudi, siku inafafanuliwa kufuatana na Biblia ya Kiebrania[2] "Na ilikuwa jioni, na ilikuwa asubuhi, siku moja". Kwa sababu "jioni" inakuja kabla ya "asubuhi", siku katika kalenda ya Kiyahudi huanza jioni baada ya machweo . Ni muhimu kuhakikisha kuwa siku iliyopita imekwisha kabisa, hivyo siku mpya huanza wakati wa usiku umeanza. [3]

Katika kalenda zinazochapishwa, tofauti hii haionekani maana hapa tarehe za kalenda ya Kiyahudi na tarehe za Kalenda ya Gregorizinazoanza usiku wa manane huonyeshwa kandokando. Ineleweka kuwa watu wanaotumia kalenda hizi wanajua utaratibu wa kuanza siku baada ya machweo. Wakati wowote sikukuu, siku ya kuzaliwa au ya kumbukumbu ikionekana kwenye kalenda iliyochapishwa, kwa kweli huanza jioni iliyotangulia, baada ya machweo.

Molad

Hesabu ya kalenda ya Kiebrania mwaka na mwezi huanza na molad inayomaanisha hilaliMolad ni neno la Kiebrania linalomaanisha "kuzaliwa". Neno hilo linamaanisha "kuzaliwa" kwa mwezi mpya kila mwezi. Kalenda ya kisasa ya Kiebrania hutumia molad iliyohesabiwa: urefu wa wastani wa muda kutoka mwezi mpya hadi mwezi mpya. Urefu wa Molad ni siku 29, masaa 12, dakika 44, sekunde 3 na nusu. [4]

Tanbihi

  1.  Idadi inaweza kubadilika katika miaka kadhaa
  2.  Genesis 1:5
  3.  The Jewish Day. Chabad.org. Iliwekwa mnamo 11 May 2016.
  4.  Bromberg. Moon and the Molad of the Hebrew Calendar. Iliwekwa mnamo 19 May 2016.

Marejeo

  • Msimbo wa Maimonides (Mishneh Torah), Kitabu cha Tatu, Tolea Nane: Utakaso wa Mwezi Mpya . Ilitafsiriwa na Solomon Gandz. Yale Judaica Series Vol XI, Press University University of Yale, New Haven, Conn., 1956.
  • Bonnie Blackburn na Leofranc Holford-Strevens. Mpenzi wa Oxford kwa Mwaka: Uchunguzi wa Forodha ya Kalenda na Uhesabuji wa wakati . Vyombo vya Habari vya Chuo Kikuu cha Oxford; USA, 2000. pp 723-730.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW