Kwa tafsiri kutoka kamusi ya Webster Mkristo ni “mtu mwenye kukiri imani ndani ya Yesu kama Kristo au Imani yenye msingi wa mafundisho na ufunuo wa Yesu.” Ijapokuwa huu ni mwanzo mwema wa kufahamu Mkristo ni mtu gani, kama maelezo mengi ya kidunia yalivyo, inapungukiwa na uhalisi wa kibiblia juu ya Maana kamili ya Ukristo au Mkristo.
Neno Mkristo limetumika mara tatu katika agano jipya (Matendo 11:26; Matendo 26:28; Petero Wa Kwanza 4:16). Wafuasi wa Yesu Kristo waliitwa kwa mara ya kwanza “Wakristo” antiokia (Matendo 11:26) kwa sababu tabia zao, matendo yao na hotuba zao zilikuwa kama za Kristo. Ilitumika kiasili na watu wasiookoka wa Antiokia kama jina la kimajazi kuwadhihaki wakristo hao. Ina maana sawa na “Kuwa mmoja wa kundi la kristo” au “mfuasi wa Kristo,” ambayo imefanana na tafsiri ya Neno hili katika kamusi ya Webster.
Kwa bahati mbaya, neno Mkristo limepoteza kwa kiwango kikubwa usawa wa matumizi yake na Linatumika mara kwa mara kumaanisha tu mtu mwenye dini au pengine muadilifu kinyume cha Mfuasi halisi wa Yesu Kristo aliyezaliwa mara ya pili. Watu wengi wasioamini na kuwa na tumaini ndani ya Yesu Kristo hujichukulia tu kuwa ni wakristo kwa sababu wanahudhuria ibada za Kanisa ama wanaishi katika taifa la kikristo. Lakini, kuenda kanisani, kuwahudumia wale wasiobahatika maishani au kuwa mtu mzuri haviwezi kukufanya kuwa mkristo. Kama Muinjilisti mmoja alivyosema, “kuenda Kanisani hakufanyi mtu kuwa Mkristo sawa na mtu kuenda gereji hakumfanyi kuwa gari.” Kuwa mshirika wa kanisa anayehudhuria ibada kila mara na kutoa kwa ajili ya kazi za kanisa hakuwezi kukufanya wewe kuwa Mkristo.
.jpg)