Tuesday, April 30, 2013

Je ni nini kitawapata watu wale hawajawai pata nafasi ya kusikia kuhusu Yesu?


Je ni nini kitawapata watu wale hawajawai pata nafasi ya kusikia kuhusu Yesu? Je Mungu atawahukumu wale ambao hajawai sikia kuhusu Yesu?"

Jibu: Watu wote wamewajibika kwa Mungu hata kama wamesikia au hawaja “sikia kumhusu” Bibilia yatwambia wazi wazi kuwa Mungu anajidhihirisha mwenyewe kwa uungu (Warumi 1:20) na katika Roho za watu (Mhubiri 3:11). Shida ni kwamba ni uzao wa dhambi wa mwanadamu. Zote twakataa hii hekima ya Mungu na kuasi (Warumi 1:21-23). Kama isingekuwa ni neema ya Mungu, tungejitolea kwa mioyo ya dhambi, kujiruhusu kujigundulia vile maisha ni bure, yakustaajabisha ni sehemu kando naye Mungu. Anafanya haya kwa wale wanaoendelea kumkataa (Warumi 1:24-32).

Ukweli ni, si eti watu wengine hawajasikia juu ya Mungu. Badala, shida ni wamaekataa chenye wamesikia na chenye kinaonekana katika uumbaji. Kumbukumbu La Torati 4:29 yasema, “Lakini huko, kama mkimtatufa BWANA, Mungu wako, utampata, ukimtafuta kwa moyo wako wote, na roho yako yote.” Aya hii yatufunza nguzo muimu. Kila mmoja anayemtafuta Mungu atampta. Kama mtu amenuia kumjua Mungu, Mungu atajudhihirisha kwake.

Shida pekee, “Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu” (Warumi 3:11). Watu wanakataa hekima ya Mungu ambayo ipo katika uumbaji na katika mioyo yao, na badala wanaanza kuabudu “miungu” yao wenyewe wamejitengenezea. Ni ubumpavu kubishana juu ya haki/uungwana wa Mungu kumtuma mtu jahanamu mwenye hakuwa na nafasi ya kuisikia injili ya Kristo. Watu watawajibika kwa Mungu kwa yale yote Mungu ameyafunua kwao. Bibilia inasema watu wanakataa hekima na kwa hivyo Mungu ako haki anapowahukkumu kwenda jahanamu.

Badala ya kujadiliana juu ya mwisho wa wale hawakusikia, sisi kama Wakristo yatupasa kufanya tuwezavyo wao kusikia injili wenye hawajaisikia. Tumeitwa kutangaza injili kwa mataifa yote (Mathayo 28:19-20; Matendo Ya Mitume 1:8). Tunajua kuwa watu wanakataa hekima ya Mungu ambayo imedhihirishwa kwao na hiyo inatusukuma kutangaza injili ya wokovu kupitia Yesu Kristo. Ni kwa kukubali neeme ya Mungu pekee kupitia Yesu Kristo watu wanaweza kuokolewa kutoka dhambini na kuepuka mauti ya milele pasipo na tumaini. Kama tutapuuza kuwa wale wote hawakusikia injili wameokolewa, haina tofauti wakati tunaakikisha kuwa hakuna mtu yeyote amepokea injili. Kitu kibaya zaidi tunaweza kufanya ni kushiriki injili na mtu na kumfanya huyu mtu aikatae hiyo injili. Kama hiyo ingekuwa itendeke, huyo mtu atahukumiwa. Watu wasioisikia injili watahukumiwa, la sivyo hatutakuwa na cha kututia moyo wa kuhiubiri injili. Mbona tujiatarishe watu kuikataa injili na kujihukumu wao wenyewe na hapo mbeleeni walikuwa wameokolewa kwa sababu hawakuwa wameisikia injili?

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW