Monday, August 10, 2015

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA SABA)

Je, Yesu ni Mwana wa Mungu?
Je, Isa bin Mariam ni Mwana wa Mungu?

Biblia inasema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu. Katika hii mada, tuanze kwa kuangali, Je, Biblia inasema nini kuhusu Yesu? Kumbuka kuwa, Biblia ndio ilikuja kwanza kabla ya Quran. Ushahid unonyesha kuwa Biblia ilikuwepo miaka 632 kabla ya Quran kuandikwa na marafiki zake Muhammad.


YESU NI MWANA WA MUNGU

Tunaona hapa Biblia inatuambia YESU KRISTO ni Mwana wa Mungu (YOHANA 20:30-31) hapa Yesu mwenyewe anasema yeye ni Mwana wa Mungu ( MATHAYO 26:59-64; 16:13-17 ) , Neno Mwana linamzungumzia Yesu Mwana siyo kuwa Mungu anazaa la hasha

Yesu anaitwa mwana wa Mungu kwa sababu alizaliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Hata sisi tumezaliwa kwa mara ya pili kwa Roho tunapo mwamini Yesu Kristo hivyo tunahesabika kuwa ni wana wa Mungu.(WAFILIPI 2:14-15,YOHANA 1:12). Kwahiyo Yesu anapoitwa Mwana wa Mungu maana yake ni chapa ya  Mungu (HUIOS) WAEBRANIA 1:1-3. Ndiyo maana hapa Yesu anawaambia wanafunzi wake, mumeniona mimi ; mumemuona Mungu, maana yake ndiyo hiyo (HUIOS) yaani chapa ya Mungu (YOHANA 14:7-9)

Tunaona hapa Yesu alisema Yeye ni Mwana wa Mungu  (YOHANA 9:35-37)
Shetani naye anajua kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (MARKO 3:11,LUKA 4:41).
Malaika nao wanasema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (LUKA 1:30-35)
Mungu mwenyewe anasema kuwa Yesu ni Mwanangu mpendwa (MATHAYO 3:17,MATHAYO 17:5   )


ISA WA QURAN SIO MWANA WA MUNGU

Kama kuna jambo ambalo Allah Mungu anayeabudiwa na waislamu analikataa sana kupitia Qurani basi jambo hilo si lingine bali ni uwana wa Mungu. Allah anasema hivi.
Quani 6:101 Suratul Al-An-am [Wanyama]
Yeye ndiye Mwumba wa mbingu na ardhi. inamkinikanaje awe na mwana, hali hana mke. Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu.
Qurani 9:30 Suratul At-Tawba [Kutubu]
Na mayahudi wanasema “uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu;”na “Wakristo wanasema Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu” Haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasina na kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyenzi Mungu uwaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa!

Allah anasema katika aya hizo hapo juu kuwa, yeye hana Mwana na kuwa Wakristo na Wayahudi wanamsingizia Allah kuwa na Mwana. Allah anasema kuwa, yeye hana Mwana kwasababu hana MKE. Ikiimanisha kuwa, Allah hana uwezo wa kuwa na Mwana bila ya kufanya tendo la ndo na Mwnamke. Huu ni ushahid tosha kuwa, Allah sio mjuzi wa yote, maana hawezi kuwa na mwana bila ya mke. 

Hebu tuangalie aya zingine za Biblia zinasema nini kuhusu Yesu.
1. Mathayo 17:5 ….Huyu ni mwanangu mpendwa wangu…
2. Malaika wa Mungu alisema hivi.
Luka 1:30-31,35
Malaika akamwambia usiogope Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu.

Hivyo Isa siyo Mwana Mungu lakini Yesu ni mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa.

Leo tumejifuinza kwa mara nyingine tena kuwa Isa wa Quran sio Yesu wa Biblia kwa kuwa Isa wa Quran yeye sio Mwana wa Mungu.
Katika huduma yake,

Max Shimba

Max Shimba Ministries

Copyright © Max Shimba Ministries 2015

Sunday, August 9, 2015

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA TANO)

Je, Isa ni Jina sahihi la Yesu wa Biblia?
Katika somo letu hili tutajifunza kuhusu jina sahihi la Yesu/Yashua na tafsiri yake katika Kiarabu. Je, Isa ni jina la Yesu wa Biblia?

Jibu sahihi la kihistoria na la wataalam wa kutafsiri litatupa ukweli halisi wa Jina la Yesu na kwanini alipewa Jina hilo katika " sherehe ya kumtaja " (Luka 2:21). Jina ambalo aliitwa na Mama yake, Baba yake wa Kambo, Ndugu zake na jamaa wengine, majirani zake , marafiki zake na wanafunzi wake wakati wa maisha yake duniani. Hakuna kutokuelewana kuhusu ukweli kwamba jina la Yeshua halikuwa la Kiarabu bali la Kiyahudi na Yesu/Yeshua mwenyewe aliishi katika Israeli, na alizaliwa katika familia ya Wayahudi wacha Mungu.

Jina la Yesu bila ya shaka yeyote ile ni la Kiyahudi. (Maana yake ni “kweli”). Tafsir ya jina la Yeshua Kiebrania katika Kiingereza itakuwa ni Jesus. Jina la Yesu halikuchaguliwa kiholela na wazazi wake, lakini yeye alipata jina lake moja kwa moja kutoka kwa Mungu (Mathayo 1:21 , Luka 1:31) kwa sababu ya maana ya jina lake na nani alilileta, basi leo hii tunaelewa madhumuni ya Yesu kuzaliwa na kuja hapa duniani (Mathayo 1:21 ).

Katika utamaduni na jadi ya Kiarabu. Jina la Yesu ni Yasu na si Isa kama ilivyo andikwa kwenye Koran ya Kiislam. Na hata leo, jina la Yasu linatumiwa na zaidi ya 99.99% ya Wakristo wote wa Kiarabu. Tembea katika kanisa lolote la Kiarabu huto sikia wanatumia jina la Isa, Sikiliza matangazo ya Wakristo wa Kiarabu katika Radio na Televisheni (za Kiarabu) huto sikiwa Mkristo anatumia jina la Isa, bali wanatumia jina la Yasu. Matangazo yote ya Kikristo katika Uarabu wanatumia jina la Yasu. Kamwe huto ona jina la Isa kama lilivyo kwenye Koran ya Waislamu.

Katika jadi ya Kiarabu na utoaji wa tafsiri wa jina, jina sahihi la Kiebrania (Yeshua) ni Yasu katika Kiarabu. Kila uchaguzi wa tafsiri ya jina la kigeni katika lugha tofauti ni uvumbuzi wa binadamu.
Kiisimu ipo wazi jinsi jina la Yeshua Kiebrania lilivyo tafsiriwa na kuwa Yesu Kiswahili na Jesus Kiingereza:
Yeshua '(Kiebrania) -> Ιησους (Kiyunani) -> Yesu (Kilatini) -> Jesus (Kiingereza) -> Yesu (Kiswahili).
Mpito muhimu ni kutoka Kiyahudi kwenda Kigiriki. Hatua hii ilifanyika miaka 200 kabla ya Yesu kuzaliwa. Watafsiri wa Septuaginta (LXX), classical Kigiriki tafsiri ya maandiko ya Kiyahudi, kutokaa Yeshua Kiebrania jina kama Ιησους katika Kigiriki. Injili ziliandikwa katika lugha ya Kigiriki ilitumia utamaduni huu wa kutafsir kwa muda mrefu.

Kwasababu Kiyahudi na Kiarabu ni lugha mbili za Kisemiti, na zina uhusiano wa karibu, kuna baadhi ya sheria maalumu ambayo sauti/maneno/maandishi ya Kiebrania yanahusiana na ambayo sauti/maneno katika Kiarabu. Hasa, Neno la Kiebrania Shin mara kwa mara linatumika kama Dhambi katika Kiarabu, kwa mfano neno la Kiyahudi la amani, shalom ni sambamba na neno “salam” la Kiarabu. Kulingana na sheria za lugha na mahusiano kati ya Kiyahudi na Kiarabu, Yasu 'ni sahihi kwa Kiarabu na kwa Kiebrania ni Yeshua:
Yeshua '= Yod + + Shin Waw +' Ain
Yasu '= + Ya + Sin Waw +' Ain
Tena, katika lugha sahihi, jina la Yasu ni Kiarabu sawa na Yeshua Kiebrania. Hivyo, katika utamaduni na jadi ya Kiarabu jina la Yasu ndilo sahihi na pekee kutokana na kiisimu. Mpito kutoka Yeshua kwa Yasu inafuata sheria ya kawaida ya mabadiliko fonetiki kutoka Kiyahudi na Kiarabu. Yasu ni jina la Kiarabu la Yesu. Kinyume chake, Yasu ndio jina lenye asili ya Yeshua.

Early Hebrew (long form): Yehoshua' = Yod + He + Shin + Waw + 'Ain
Later Hebrew (short form): Yeshua' = Yod + Shin + Waw + 'Ain
Arabic (Christian): Yasu' = Ya + Sin + Waw + 'Ain
Arabic (Muslim): 'Isa = 'Ain + Ya + Sin + Ya

“Ya” na “Waw” ni maneno dhaifu, katika lugha ya Kiarabu, hufundisha kwamba mtu anaweza kurejea katika maneno mengine kama kuchukua juu ya aina mbalimbali (declension, inflection). Hivyo, mtu anaweza kuona kwamba fomula ya Kiislamu 'Isa kimsingi ni ya bandia/kutungwa na binadamu (inversion) (pamoja na mabadiliko ya Waw ili Ya) kwa Mkristo wa Kiarabu jina la Yesu ni Yasu na si Isa kama ilivyo andikwa kwenye Koran ya Kiislamu.

Nategemea leo umejifunza tofauti iliyopo kati ya Jina la Yesu-Kiswahili, Yasu-Kiarabu na Yeshua-Kiebrani.

Jina la Yesu Libarikiwe Sana

Katika Huduma yake

Max Shimba

Copyright © Max Shimba Ministries 2013

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA SITA)

Waislam kila mara wamekuwa wakisema kuwa Yesu kwao ni Isa na wana mpenda Isa na kwa kuwa Isa wa Quran ni Mtume na au Nabii wa Allah, hivyo basi Isa wa Quran ni yule yule Yesu wa Biblia. Jibu thabiti la hawa Waislam lipo kwenye Biblia katika Marko 15: 5b na aya ya 6. zinasema:

5Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu ye yote asiwadanganye. 6Wengi watakuja kwa Jina Langu wakidai, ‘Mimi ndiye’, nao watawadanganya wengi. 

YESU ANATUAMBIA TUWE WAANGALIFU, kwasababu wengi watakuja kwa Jina lake na kudai kuwa ni Yesu amerudi tena. Huu ushahid ndio ule uliopo kwenye Quran ambayo imetungwa na au umba Yesu mwengine na kumpa jina la Isa. 

Utumiaji wa Jina la Yesu, Yeshua, Isa, au Esah haiimaanishi moja kwa moja kuwa huyo anaye tajwa ni Yesu wa kwenye Biblia. Ushahid halisi unapatika kwenye Biblia peke yake na sio vitabu vingine vilivyo tungwa na kuja baada yake. Yesu alimjibu Pilato katika Yohana 18:37 Yesu akajibu, “Wewe wasema kwamba mimi ni mfalme. Kwa kusudi hili nilizaliwa na kwa ajili ya hili nilikuja ulimwenguni ili niishuhudie kweli. Mtu ye yote aliye wa kweli husikia sauti yangu.’’ na katika Yohana 17: 17 7Uwatakase kwa ile kweli, Neno Lako ndilo
kweli. 

Ili kujua kama Isa wa Quran ni yule yule na au ndie Yesu wa Biblia basi hatuna budi Kumlinganisha Isa wa Quran kwa kutumia aya za Biblia na tuone kama anapita. Katika Biblia, tumeambiwa kuwa Yesu alikufa katika Msalaba, huu ushahidi upo kwenye Matayo 27:50, Marko 15:37, Luka 23:46, Yohana 19:30, 33, Matendo 7:52. Lakini katika Quran tunaambiwa kiuwazi kabisa kuwa Isa hakufa Msalabani bali Simoni wa Cyrene ndie alisulubiwa badala ya Isa.

Ushahid huu upo wazi kabisa kuwa Isa wa Quran na Yesu wa Biblia ni wawili tofauti na YESU WA BIBLIA HAWEZI KUITWA NA AU FANANISHWA NA ISA WA QURAN. Wakristo wa Uarabuni ambao tumesha kutana nao mara nyingi, wao wameniambia kuwa Yesu wa Biblia anaitwa Yasu na hilo jina ndilo lipo kwenye Biblia za Kiarabu na sio ISA . Zaidi ya hapo, Wakristo wa Uarabuni hawatumii jina la Isa kwasababu Isa ni Mtume/Nabii wa Allah ambae sio Mwana wa Mungu. 

Leo tumejifuinza kwa mara nyingine tena kuwa Isa wa Quran sio Yesu wa Biblia kwa kuwa Isa wa Quran yeye sio Mwana wa Mungu.

Katika huduma yake,

Max Shimba

Max Shimba Ministries

Copyright © Max Shimba Ministries 2015

Saturday, August 8, 2015

YESU NI MUNGU KUTOKANA NA QURAN (SEHEMU YA TATU)

Ndugu msomaji,
Quran inasema kuwa Allah ni Al-Malik al-Mulk, ikimaanisha kuwa ni mmiliki wa kila kitu. Je, hii sifa ya Al-Malik al-Mulk inapatikana kwa Yesu aliye hai?

Hebu tuanze utafiti wetu kwa kusoma Quran na tujionee wenyewe kama kweli Yesu ni Mungu au la.
Moja ya sifa au adhama ya Mungu kutokana na Quran: ni Al-Malik al-Mulk, ikimaanisha MMILIKI WA KILA KITU. Hii sifa ya Al-Malik al-Mulkh ni moja ya Majina 99 ya Allah wa Quran.

Je, Yesu anayo hiyo sifa ya MMILIKI WA VYOTE "Al-Malik al-Mulkh"? Haya tusome kwanza Quran na tuone kama Allah anayo hii sifa ya Al-Malik al-Mulkh.

Surat YA-SIN 83. Basi Mtukufu ametakasika na kila kisicho laiki na dhati yake, yule ambaye katika kudra yake upo Ufalme wa kila kitu, kwa kuumba, na kupanga, na kuendesha - Kwake Yeye peke yake mtarejeshwa, akuhisabuni kwa a'mali zenu.

Allah anasema kuwa yeye ni Mmiliki wa vyote kwenye Quran iliyo andikwa miaka mia 632 AD baada ya Yesu. Je, Yesu anayo hii sifa ya Mmilikiwa vyote?

YESU ANASEMA HIVI:Matayo 11: 27“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu:
hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na ye yote ambaye Mwana anapenda kumdhihirisha Baba kwake.’’

Ikimaanisha kuwa Yesu ndie aliye kuwa wa kwanza kukiri haya maneno kuwa yeye ni mmiliki wa vyote kutokana na ushahid wa Biblia iliyo tangulia miaka 632 kabla ya Quran. YESU ANASEMA KUWA "AMEKABIDHIWA VITU VYOTE". Ikimaanisha hata Muhammad sasa yupo chini ya Yesu.

YESU ANAEDELEA KUSEMA katika Yohana 16 aya ya 15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo Yangu na kuwajulisha ninyi.
Yesu anasema kuwa kila kitu ambacho ni cha Baba yake ni chake. Hapo teyari tumemaliza kazi maana hakuna atakaye bisha kuhusu hii aya iliyo kamilika na kuto kuwa na shaka ndani yake. YESU NI MMILIKI WA KILA KITU.

Sasa kati ya Yesu aliye sema haya maneno miaka mia 632 kabla ya Allah, na Allah aliye kuja baadae na Quran iliyo jaa shaka, nani tutamwamini? Wakwanza ambaye ni Yesu au Allah ambae anaigizia kwa Yesu?
Ndugu zanguni, huu ni ushahid tosha kuwa Yesu ni Mungu, maana leo tumejifunza kuwa Yesu alisema na kuitwa MMILIKI WA VYOTE MIAKA 632 kabla ya Kuandikwa kwa Quran.

Sasa kati ya Biblia iliyo kuja kabla ya Quran na Quran iliyo kuja baada ya Biblia, wewe utafuata kitabu kipi? Watafiti wa mambo mbali mbali huwa wanatumia data za awali katika kuhakiki na kuthibitisha jambo. Na data tuliyo nayo kuhusu MMILIKI wa vyote ambayo ni ya awali ipo kwenye Biblia na inasema kuwa MMILIKI WA VYOTE NI YESU.

Leo nimejibu hoja ya Waislam kuwa, Je, Yesu ni Mungu? Koran pamoja na Allah wanasema kuwa Yesu ni Mungu kwa kuwa Yesu anazo adhama zote na/au sifa zote za Mungu na moja ya sifa hizo ni AL-MALIK AL MULK.
Katika huduma yake,
Max Shimba
Copyright © Max Shimba Ministries 2015

ALLAH ATEREMSHA UCHAWI NA KUWALAZIMISHA WAISLAM KUUFANYA

Naam,

Huu ni Msiba Mkubwa sana katika taifa la Mtume Muhammad. Mara nyingi Wakristo wamekuwa wanajiuliza, hivi, uchawi ulitokea wapi na mwanzo wake ni nani?

Leo Quran inakujibu kuwa Uchawi uliteremshwa na Allah na wachawi nambari moja ni Waislam. Nafahamu unafikiri kuwa Max Shimba anawasingizia Waislam au sio?

Hapa inafaa tufahamishane kuwa ushirikina ni jambo ovu linamtia mtu motoni. Kwenda kwa wachawi, wapiga ramli ni katika ukafiri na ushirikina.

Hebu soma Ushahid huu wa Quran: 

SURAT TAHA: 73. Hakika sisi tumemuamini Mola wetu Mlezi ili atusamehe makosa yetu na uchawi ulio tulazimisha kuufanya. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mbora na Mwenye kudumu zaidi. 

Kwenye Surat Taha ayat 73  kama ilivyo teremshwa Makka kwa Muhammad na kutafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani  inasema kuwa ALLAH ANAWALAZIMISHA WAISLAM KUUFANYA UCHAWI. Huu ni msiba ndugu zangu. Swali la kujiuliza, hivi, tokea lini Mungu akawa mchawi? Hivi huu uchawi ulio teremshwa na Allah unafaida gani kwa Wislamu?

Hebu tuingalie tafsir ya pili ya Surat Taha aya 73 kama ilivyo tafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin inasema: 73. Kwani hakika sisi ni wenye kusimama juu ya Imani kumuamini Mola wetu Mlezi wa Haki, ili atufutie madhambi yetu yaliyo pita, na atusamehe huku kushughulikia uchawi ulio tulazimisha tujifunze na tuufanye! Na Mola wetu Mlezi ni Mbora wa malipo kuliko wewe, akit'iiwa; na ufalme wake na uwezo wake kulipa unadumu zaidi kuliko wako. 

1. Inasema kuwa Waislam wanalazimishwa kujifunza Uchawi
2. Inasema kuwa Waislam wanalazimishwa kuufanya Uchawi.

Ndugu msomaji, leo sina mengi ya kusema maana umesoma wenyewe kutoka Quran kuwa Allah aliteremsha uchawi na kawalazimisha Waislam wajifunze na kuufanya uchawi. Nawashauri Wakristo wenye marafiki wa Kiislam wawe makini, maana huyo rafiki yako anaweza kuwa ndiye anaye-kuroga kwasababu kalazimishwa na Allah kufanya hivyo.

MTUME MUHAMMAD ANATUMIA NDUMBA
Muhammad alitumia ndumba [nguvu za kimazingaombwe] dhidi ya jicho ovu na wanyama jamii ya mjusi wenye sumu Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3525 uk.48.

Hivi wapi tunasoma katika Taurat au Zaburi au Injir kuwa Mitume na Manabii wa kwenye Biblia walitumia NDUMBA?

Hivi Allah hana uwezo wa kutibu jicho ovu au Sumu mpaka atumie NDUMBA?

Mungu awarehemu na kuwasamehe ndugu zetu wote wanao fanya Uchawi. Maana Biblia inasema kuwa WACHAWI WOTE WATAINGIA JEHANNAM. 1 Samweli 15 : 23 .......... dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.

Ndugu msomaji, mpokee Yesu aliye hai na upate uzima wa milele. Dini haita kusaidia kitu, maana sasa unaelewa kuwa, ni dini ambayo inakufanya uwe mchawi na kuachana na upendo wa Mungu.

Katika huduma yake,
Max Shimba
Copyright © Max Shimba Ministries 2015

YESU NI MUNGU KUTOKANA NA QURAN (SEHEMU YA PILI)


Ndugu msomaji,

Je Yesu anazo sifa za kipekee za Mungu kutokana na Quran? Hebu tuanze utafiti wetu kwa kusoma Quran na tujionee wenyewe kama kweli Yesu ni Mungu au la.

Moja ya sifa au adhama ya Mungu kutokana na Quran: ni Al-Warith, ikimaanisha MRITHI WA VYOTE. Hii sifa ya Al Warith ni moja ya Majina 99 ya Allah wa Quran.

Je, Yesu anayo hiyo sifa ya MRITHI WA VYOTE "Al Warith"? Haya tusome kwanza Quran na tuone kama Allah anayo hii sifa ya Al Warith.

Surat Maryam 40. Hebu jamani! Nawajue watu kuwa hakika Mwenyezi Mungu ndiye mrithi wa kuurithi ulimwengu wote na kila kiliomo ndani yake. Na hisabu yao wote ni juu ya Mwenyezi Mungu. 

Allah anasema kuwa yeye ni Mrithi wa vyote kwenye Quran iliyo andikwa miaka mia 632 AD baada ya Yesu. Ikimaanisha kuwa Yesu ndie aliye kuwa wa kwanza kukiri haya maneno kuwa yeye ni mrithi wa yote kutokana na ushahid wa Biblia iliyo tangulia kabla ya Quran.

Sasa tuangalie kama kweli Yesu anayo hii sifa ya MRITHI WA VYOTE ambayo ni adhama ya Mungu pekee kutokana na Koran iliyo andikwa miaka 632 baada ya Yesu.

Biblia takatifi inasema yafuatayo kuhusu Yesu Kristo:
Waebrania 1 aya 2 inasema: lakini katika siku hizi za mwisho
amesema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye
amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, ambaye
kwa Yeye aliuumba ulimwengu. 

Katika aya hii tunasoma kuwa Yesu anaitwa “MRITHI WA VITU VYOTE” ambayo ni adhama/sifa ya Mwenyezi Mungu kama ilivyo shaidiwa na Koran Surah ya 19 na aya 40. Hivyo basi , Allah na Koran wamekiri kuwa Yesu ni Mungu kwasababu Biblia imetuthibitishia kuwa Yesu ni MRITHI WA VITU VYOTE miaka 632 kabla ya kuandikwa kwa Quran na uthibitisho huu upo kwenye kitabu cha Waebrania 1 aya ya 2.

Ndugu zanguni, huu ni ushahid tosha kuwa Yesu ni Mungu, maana leo tumejifunza kuwa Yesu alisema na kuitwa MRITHI WA VYOTE MIAKA 632 kabla ya Kuandikwa kwa Quran. Sasa kati ya Biblia iliyo kuja kabla ya Quran na Quran iliyo kuja baada ya Biblia, wewe utafuata kitabu kipi?  Watafiti wa mambo mbali mbali huwa wanatumia data za awali katika kuhakiki jambo. Na data tuliyo nayo kuhusu Mrithi wa vyote ambayo ni ya awali ipo kwenye Biblia na inasema kuwa MRITHI WA VYOTE NI YESU.

Hakuna ubishi hapa kuhusu URITHI WA VYOTE ambao ni wa Yesu, Maana yeye ndie Mwana wa Mungu na alithibitishwa kuwa Mrithi wa vitu vyote miaka 632 kabla ya Quran. 
Leo nimejibu hoja ya Waislam kuwa, Je, Yesu ni Mungu? Koran pamoja na Allah wanasema kuwa Yesu ni Mungu kwa kuwa Yesu anazo adhama zote na/au sifa zote za Mungu na moja ya sifa hizo ni AL-WARITH.

Katika huduma yake,

Max Shimba

Copyright © Max Shimba Ministries 2015

Friday, August 7, 2015

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA KWANZA)


Ndugu msomaji,
Mwezi huu nitaweka mada kadhaa zitakazo fundisha kuwa, Isa wa Quran na Yesu wa Biblia ni wawili na tofauti:

MAANA YA JINA ISANi jambo la kawaida sana jina au majina kuwa na maana. Mfano majina haya ya kiarabu yana maana hizi: Muhammad, linamaanisha mwenye kushukuriwa, Abdalla ni Mtumwa wa Allah; Abu-Bakar maana yake ni Baba wa bikira; Abu Huraira ni baba wa Mapaka. Aidha majina ya Kiebrania nayo pie yana maana. Malaki ni mtumishi au Mjumbe wa Yehova, Isaya ni Wokovu wa Yehova; Ezekiel inamaanisha Mungu hutia nguvu, Daniel – Mungu ni hakimu wangu.

JINA LA ISA MAANA YAKE NINI?Katika Qurani yenye jumla ya juzuu 30; Surah 114; aya 6236; maneno yenye kutamkia 76,440; herufi 322,373; jina Isa linatamkwa lisa au Aysi limetajwa mara 25. Isa pia ameitwa masihi mara 93. Lakini tunaposoma Qurani iliofarsiriwa/tafsiriwa na Imam Baidawi Vol 1 Ukurasa 160 ameeleza kuwa Isa jina la Kiarabu maana yake ni Wekundu unaozidiana na weupe. Hii ndio maana ya Jina la Isa wa Quran. Je, Yesu wa Biblia maana yake nini?

JINA LA YESU MAANA YAKE NINI?JINA Yesu linatokana na lugha ya Kiebrania ‘Yehoshua’ katika lugha ya Kigiriki wanasema ‘lesous’ inatamka ‘Yesous’ yaani Yesu. Katika lugha ya Kiarabu wanasema ‘Yasu’, kwa kiingereza ni “Jesus” maana yake ‘Bwana anaokoa au Bwana ni Mwokozi’ Isaya 43:6, 10-11.
Katika Biblia ambayo ina jumla ya Sura 1189; aya 31,102; vitabu 66 – Agano la kale vitabu 39 na agano Jipya vitabu 27; Neno Mwokozi kwa Kiingereza wanasema ‘Saviour’ limetajwa mara 55. Ikumbukwe kwamba katika agano jiypa jina Yesu au Yehoshua (kwa Kiebrania) limetajwa mara 1275 katika aya zipatazo 1226.

Zingatia pia kuwa agano jipya lina jumla ya aya 7930 na sura 260 hivyo hapa tunaona jina Yesu maana yake ni Mwokozi na jina Isa ni wekundu uliozidiana na weupe. Kwa kuwa maana ya haya majina tofauti bila shaka Isa sio Bwana Yesu.

Leo tumejifunza kwa kifupi tu kuwa, Jina la ISA lenye maana ya Wekundu unao zidiana na weupe ni TOFAUTI KABISA NA Jina la Yesu lenye maana ya MWOKOZI katika Biblia. Zaidi ya hapo, tafsir ya Jina la Yesu kwa Kiarabu ni Yasu na sio Isa kama ambavyo Waislam wanadai katika vitabu vyao.
Mungu awabariki sana na tuendele kujifunza Neno lake bila ya kuchoka.
Katika huduma Yake,

Max Shimba

Max Shimba Ministries

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA PILI)



Je, kuzaliwa kwa Bwana Yesu ni sawa na Isa?
Taarifa za Malaika kabla ya kuzaliwa kwao, kadiri ya Qurani na Biblia.
Jibrili alivyomtokea Mama wa Isa == Gabrieli alivyomtokea mama wa Yesu:
WAISLAM-JIBRIL Alienda kwa Mariamu aliyekuwa Msikitini Qurani 19:16-17
WAKRISTO-GABRIEL Alienda kwa Mariamu aliyekuwa nyumbani kwake - Lk 1:26-28
WAISLAM-Mariamu Mama wa Isa haijulikani aliishi kijiji kipi wala mji gani wala hata nchi haijulikani. Isitoshe Quran inasema kuwa Jibril ndiye aliyemletea utume Muhammad asiwapelekee Mayahudi (hana kosa) Sura 2:97
WAKRISTO-Lakini Mariamu Mama yake Yesu alitokewa na Malaika Gabriel akiwa katika kijiji cha Nazareti mji wa Galilaya nchi ya Israeli (Lk 1:26) Mariamu Mama wa Yesu ni Myahudi.
WAISLAM-Jibrili hakutoa salamu kwa Mariamu mama wa Isa ila alijimithilisha kwa umbo la binadamu aliye kamili - Sura 19-17
WAKRISTO-Malaika Gabrieli alimsalimia Mariamu Mama wa Yesu – Luka 1:28
WAISLAM-Jibril alimwambia Mariamu kwamba mimi ni mjumbe wa mola wako ili nikupe mwana mtakatifu - Sura 19-19
WAKRISTO-Lakini malaika Gabrieli alimwambia mama wa Yesu kuwa utachukua mimba – Luka1: 31
WAISLAM-Jibrili alisema kwa Mariamu kuwa ili tumfanye mtoto muujiza kwa wanadamu – Sura 19: 21. Isitoshe Jibrili hakutaja jina la mwana kwa Mariamu. Bali alisema ili nikupe mwana mtakatifu.
WAKRISTO-Malaika Gabrieli alisema kwa Mariamu mama ya Yesu kuwa mtoto jina lake utamwita Yesu (Luka 1:31; 2:21) Gabrieli hakusema kuwa atampa mwana Mariamu. Bali alisema, Roho mtakatifu atakujilia juu yako, yaani motto atazaliwa kwa uwezo wa Mungu.

TOFAUTI YA KUZALIWA KWA ISA NA YESUIsa bin Mariam Yesu Kristo

WAISLAM-Isa alizaliwa katika shina la Mtemde – 19:23

WAKRISTO-Yesu kazaliwa katika hori la kulishia ng’ombe. Luka 2:7

WAISLAM-Kuzaliwa kwa Isa haijulikani mimba ya mama yake ilichukua muda gani maana malaika Jibrili alisema nikupe mwana mtakatifu mara akachukua mimba na kuzaa. (19: 22-23)

WAKRISTO-Lakini Mariamu Mama wa Yesu siku zake za kuzaa zilitimia. (Luka 2:6-7)

WAISLAM-Qurani haionyeshi kama Isa alitabiriwa na manabii kuwa atazaliwa

WAKRISTO-Lakini Biblia inatuthibitishia kuwa Manabii walitabiri kuzaliwa kwa Yesu, (Isaya 7: 14; 9:6) utabiri huu ulitolewa na Nabii Isaya miaka 750 kabla ya Yesu kuja kuzaliwa nao ulitimia (Mathayo 1:18-23)

WAISLAM-Isa haijulikani alizaliwa katika kijiji gani wala mji, wala nchi aliyozaliwa Qurani haikueleza.

WAKRISTO-Biblia inatujulisha kuwa Yesu alizaliwa Bethelehemu ya Uyahudi katika Mji wa Daudi umbali wa maili 5 toka kusini mwa Yerusalemu nchi ya Israeli (Lk 2:8-16). Kuzaliwa kwake mahali hapo pia ni kutimiza unabii uliotolewa na nabii Mika miaka 750-686 kabla ya kristo kuja wakati wa wafalme hawa wakitawala – Jotham, Ahaz na Hezekia wafalme wa Yuda. Yesu mwenyewe alizaliwa kama mwaka wa 4 wakati wa Mfalme Herode.

WAISLAM-Isa aliongea na watu akiwa mototo mchanga, na kusema kuwa yeye ni mja wa Mungu amepewa kitabu na amefanywa Nabii (Sura 19:30-33)

WAKRISTO-Yesu hakuongea na mtu akiwa mtoto mchanga. Alianza kuwauliza maswali na kutoa majibu akiwa na wazee Hekaluni akiwa na miaka 12. (Luka 2: 42-49)

Hivyo tunaona kwamba tuna tofauti nyingi tu kati ya Bwana Yesu na Isa. Swali kwako mfuatiliaji je, Isa bin Maryamu ndiye Bwana Yesu Mwokozi? Tafakari.

Mungu awabariki sana na tuendelee kujifunza tofauti za Isa wa Quran na Yesu wa Biblia.

Max Shimba

Max Shimba Ministries

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA TATU)

Je, Isa bin Mariamu ni mwana wa Mungu?
Kama kuna jambo ambalo Allah mungu anayeabudiwa na Waislamu analitataa sana kupitia Quran basi jambo hilo si lingine bali ni YESU KUWA MWANA WA MUGU. Allah ansema hivi.

Sura 6:101 – Yeye ndiye muumba wa mbingu na ardhi, inamkinikaje awe na mwana, hali hana mke? Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu.

Quran 9:30 – Na Mayahudi wanasema ‘uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu’ na ‘wakristo wanasema Masihi ni mwana wa Mwenyezi Mungu’ haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasina kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale walilkufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa?

Hili ni agizo la kutisha kwamba Wakristo na Wayahudi tuangamizwe kwa kuwa tunaamini Mungu ana Mwana, au wana, lakini Wakristo tunaoamini hivyo kwa sababu Mungu wetu:-
- Yehova alifundisha kuhusu Bwana Yesu hivi:
Kutoka 4:22…Israeli ni Mwanangu Mimi……
Mathayo 17:5……Huyu ni Mwanangu Mpendwa wangu….

Malaika wa Mungu alisem hivi.Luka 1:30-31, 35 – Malaika akamwambia usiogope Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kuvuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu.

Hivyo basi Isa wa kwenye Quran siyo Mwana wa Mungu lakini Yesu wa kwenye Biblia ni Mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa.

Leo tumejifunza tena kuwa, katika Quran Allah kakiri kuwa yeye hana Mwana, lakini kwenye Biblia Yehovah anasema kuwa Yesu ni Mwana wake.

Mungu awabariki sana na fahamu kuwa Isa wa kwenye Quran sio Yesu wa kwenye Biblia.

Max Shimba

Max Shimba Ministries

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA NNE)



Je, Mama wa Isa ndiye wa Yesu Kristo?
Hapo awali tumeona kuwa mama wa Isa anaitwa Maryamu, Surah 3:45 na pia mama wa Yesu anaitwa Mariamu Mathayo 1: 18-21, Marko 6: 3-4 lakini kufanana kwa majina hakuwezi kamwe kumaanisha kuwa ni mtu mmoja, kwani walio na jina hilo ni wengi. Biblia inatufundisha hivi.

Yohana 19:25 – Na penye Msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama, Mamaye, na ubu la mamaye Mariamu wa Klopa na Mariamu Magdalena.

Hapa tunaona Mariamu watatu. Ili kutambua tofauti baina ya Mariamu mama wa Isa na mama wa Yesu, lazima tulinganishe ujumbe wa Qurani na Biblia. Qurani inasimulia kuhusu baba na kaka wa Mariamu mama wa Isa hivi.

Suratul 66:12 – Na Maryamu mtoto wa Imrani aliyejihifadhi nafsi yake na tukampuliza humo roho yetu, (inayotokana na sisi) na akayasadikisha maneno ya mola wake, na vitabu vyake; na alikuwa miongoni mwa wanyenyekevu (wakubwa).
Surah 19:28 – Ewe dada yake Haruni. Baba yako hakuwa mtu mbaya. Wala mama yako hakuwa hasharati.

Hapa tunaona kuwa Maryamu mama wa Isa, baba yake ni Imrani na kaka yake aliitwa Haruni. Tusomapo Biblia inatueleza kuwa Amrani aliwazaa hawa:-
Hesabu 26:59 – Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi binti wa Lawi, ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amram Haruni, na Musa, na Miriamu umbu lao.
Pia soma 1 Nyakati 6: 1-3 na Kutoka 6:20.

Huyo Amrani aliishi miaka mingi kabla ya Yesu na tena ametokana na kizazi cha Lawi mtoto wa watu wa mzee Yakobo. Mwanzo 29:34; Kutoka2:1-10
Ikiwa Mariamu wa Qurani baba yake ni Imrani basi atakuwa ameishi miaka 1500 kabla mama yake Yesu wa Biblia hajazaliwa!

Je, Mariamu mama wa Yesu ametokana na kizazi gani?Tunaposoma Biblia tunaona kwamba Yesu anaitwa mwana wa Daudi Mathayo 1:1; Marko 10:47 na Luka 1:27, 32, ndiyo maana pia Yesu anaitwa Simba wa Yuda Ufunuo 5:5. Hivyo basi ukoo aliyetoka Yusufu na Mariamu wa Yesu ni mmoja.

Hivyo basi Maryam wa Quran ambaye aliishi miaka 1500 kabla ya Mariam wa Biblia hakuwa mama yake Yesu. Zaidi ya hapo, Maryam wa Quran ni daya ya Musa na Haruni ambao waliishi Misri.
Leo tumeendelea kujifunza kuwa Maryam wa Quran sio na ni tofauti na Mariam wa kwenye Biblia.
Mungu awabariki sana na tuendelee kujifunza tofauti katika ya Isa wa Quran na Yesu wa Biblia.

Max Shimba

Max Shimba Ministries

TRENDING NOW