Monday, December 14, 2015

MAOMBI YA USHINDI KWA MAISHA YAKO

Baba katika Jina la Yesu.
Laana zote nilizo tupiwa na wabaya wangu zimeshindwa kwa jina la Yesu na nazivunja na kuzisambaratisha kwa Damu ya Yesu. Mshindwe wote mnao tuma laana kwangu katika Jina la La Yesu.
Nawavunja na kuwaharibu na kuwakatakata Wachawi wote kwa damu ya Yesu.
Nasambaratisha kila neno la uovu lililosemwa juu yangu na familayangu katika jina la Yesu.
Naharibu na kuisambaratisha madhabahu yenu mliyo fanyia kafara kwa damu ya Yesu.
Navunjavunja na kubomoa kila uovu na uchawi mnaonifanyia katika jina la Yesu.
Nairudisha misukule yote na majini yote yawarudie nyie na kuwalipa dhambi zote mnazo fanya katika jina la Yesu.
Naharibu kila uchawi, kila urogi, kila ndumba kila aina ya uovu ambao mnaufanya ili uniumize mimi na familia yangu katika jina la Yesu.
Nawateketeza kupitia damu ya Yesu Wachawi wote walio tumiwa kunitumia uchawi katika jina la Yesu.
Nawateketeza na kuwaharibu majini yote yaliyo tumwa kuja kufanya kazi hiyo waliyo tumwa na Wachawi katika jina la Yesu.
Nawateketeza na kuwauwa Makuhani wote ambao walienda kunishitaki kwa Wachawi ili waniharibie maisha, nawateketeza kupitia damu ya Yesu. Nawachoma kwa Moto wa Roho Mtakatifu katika Jina la Yesu.
Nateketeza aina zote za vyombo vya kichawi vilivyo tumiwa kuja kunichunguza katika jina la Yesu.
Naharibu fikra zao zote ambazo wanazitumia kufanya kazi zao za kichawi katika jina la Yesu.
Nafuta kumbukumbu zoote zangu ambazo wamewapa Mashetani, Majini, Roho chafu, nafuta hizo kumbukumbu kwa kutumia damu ya Yesu, katika jina la Yesu aliye hai.
Nawateketeza waweka kumbukumbu wa kimashetani kupitia damu ya Yesu aliye hai. Naharaibu na kuchoma kupitia moto wa Roho Mtakatifu makabrasha yote yenye kumbukumbu zangu katika jina la Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuharibu maisha yangu na ubomoa kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuniua nauvunja na kuuteketeza kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili kuja kuiba mali zangu, nauvunja na kuubomoa na kuuharibu kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanya kuja kuniharibia familia yangu, nausambaratisha na kuuvunja na kuubomoa katika jina la Yesu.
Kila neno la kichawi lililo tumwa ili kuja kuniharibia, kunidhihaki, kunitendea mabaya nalirudisha kwa aliye lituma katika jina la Yesu.
Kila uovu, uchawi, wanga, ndumba, ramli, yaliyo tumwa kuja kwangu navunja yote hayo kupitia damu ya Yesu na katika Jina la Yesu.
Nyota yangu ambayo wanaita nairudisha kupitia damu ya Yesu. Nyota yangu ya baraka nailinda na kuzungushia na kuizingira na damu ya Mwana Kondoo katika jina la Yesu.
Namteketeza yule mtu aliye kuja kuiba nyota yangu katika jina la Yesu.
Nateketeza mbinu zote wanazo tumia ili kuja kuiba nyota yangu katika jina la Yesu.
Nateketeza wivu wao, chuki yao, laana zao, maovu yao na kila aina ya uchafu ambao wanao kwa ajili yangu katika jina la Yesu.
Naizungushia na kuizingira nyumba yangu na damu ya Yesu.
Naishungushia na kuizingira familia yangu na damu ya Yesu.
Nashungushia na kuzingira maisha yangu yote na damu ya Yesu.
Navunja laana zote zilizo semwa na mabau zangu katika jina la Yesu.
Navunja laana zato ambazo zilisemwa bila ya mimi kufahamu, nazivunja na kuziharibu kupitia damu ya Yesu na katika jina la Yesu.
Narudisha kila mali walizo ziiba kutoka kwangu katika jina la Yesu.
Narudisha kila baraka walizo ziiba kwangu katika jina la Yesu.
Narudisha amani na upendo katika familia yangu.
Damu ya Yesu ipo juu ya Maisha yangu na inasafisha kila uovu, kila uchawi unaaribiwa na damu ya Yesu katika jina la Yesu.
Leo hii mtaiona Nguvu iliyopo katika damu ya Yesu.
Katika Jina la Yesu aliye hai ninaomba.
Amen
Max Shimba Ministries Org

MAOMBI YA KUFUNGA MWAKA NA KUANZA MWAKA MPYA 2016 KWA BARAKA TELE KUTOKA KWA MUNGU MKUU, YESU KRISTO ALIYE HAI

Ndugu msomaji na mpendwa katika Bwana. Bwana Yesu apewe sifa.
Mpendwa, yawezekana umekuwa ukiishi bila kutambua uwezo wa jina la Yesu katika kukuonyesha mwelekeo wa maisha yako.Je, unahitaji mwelekeo mpya katika maisha yako? Je, unahitaji kujua njia ya kutoka katika hali uliyonayo?
KAMA UMECHOKA NA MAISHA YA TABU, KAMA UMECHOKA KUISHI NA MAGONJWA, KAMA UMECHOKA KUWA MASKINI, KAMA UNAHITAJI KAZI, BIASHARA YAKO IFANIKIWE N.K. BASI HUU UJUMBE NI WAKO.
Napenda kukufahamisha kuwa, tupo katika Maombi kila siku mpaka tutakapo maliza mwaka huu wa 2015. Nafahamu wengi mmepata baraka tele katika Mwaka wa 2015 na labda wengi mmlikuwa katika mashindano na vita kubwa na nguvu za giza. Kumbuka USHINDI ni wetu katika Jina la Yesu.
Mpendwa , pengine hali ya maisha uliyonayo imekufanya ukate tamaa na kujiona kwamba hakuna njia ya kukufanya utimize furaha ya ndoto zako. Je, unahitaji njia ya kuishi kwa amani na furaha; njia ya kuwa na mahusiano mazuri katika ndoa yako; njia ya kuwa na mahusiano mazuri na ndugu zako, kazini kwako, kwenye biashara yako; unahitaji njia ya kuacha ulevi wa pombe na madawa ya kulevya, njia ya kuacha kuabudu sanamu, njia ya kuacha uongo, njia ya kuacha uzinzi, njia ya kuacha uchawi, njia ya kuacha tamaa ya mali zisizo halali; njia ya kuponywa maradhi, njia ya kupata utajiri, njia ya kupata kazi, njia ya kupata mtaji , njia ya kutoka kwenye madeni, njia ya kupandishwa cheo, njia ya kutimiza ndoto zako? Yesu ni njia ya kila mahitaji yetu hapa duniani, pia yeye ni njia ya kutufanya tujue kweli ya neno lake na tuweze kuurithi uzima wa milele.
Kama unahitaji lolote lile ambalo unataka upokee jibu kutoka kwa Mungu Mkuu, Yesu aliye hai, basi nakusihi ututumie hilo hitaji lako haraka ili tuwe pamoja katika maombi katika muda huu wa kumaliza mwaka wa 2015. Tuma ombi lako kupitia barua pepe maxshimbaministries@gmail.com
Matayo 7:7-11Neno: Biblia Takatifu (SNT):
7 “Ombeni nanyi mtapewa. Tafuteni nanyi mtapata; bisheni hodi nanyi mtafunguliwa mlango. 8 Kwa sababu kila aombaye hupewa; naye atafutaye hupata; na abishaye hodi atafunguliwa mlango.
9 “Au ni nani kati yenu ambaye kama mwanae akimwomba mkate atampa jiwe? 10 Au akimwomba samaki atampa nyoka? 11 Ikiwa ninyi mlio waovu mnafahamu jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, ni mara ngapi zaidi Baba yenu wa mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
Yesu katika Matayo hapo juu anakwambia "OMBENI NANYI MTAPEWA' Sasa Mpendwa unasubiri nini kumwomba Mungu Mkuu? Au unapenda kuwa katika matatizo na shida? Shetani teyari alisha wekwa chini ya miguu yetu.

YESU KRISTO AMEKUPA UTAJIRI

Watu wengu wanafikiri kuwa, Mungu aliwaumba ili wawe watu wa kawaida tu, la hasha, Mungu amekuumba wewe ukiwa Tajiri. Ukisoma kuhusu Adam katika Kitabu cha Mwanzo, utaona kuwa, Mungu alimuumba Adam na Hawa baada ya kuumba dunia na kila kitu. Baada ya Adam na Hawa kuubwa, walikabidhiwa kila kitu kilichopo hapa duniani. Huo ni Utajiri mkubwa sana. Soma. Mwanzo 1: 28 Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.” 29Kisha Mungu akasema, “Tazama, nawapeni kila mmea duniani uzaao mbegu, na kila mti uzaao matunda yenye mbegu; mbegu zao au matunda yao yatakuwa chakula chenu. 30Nao wanyama wote duniani, ndege wote wa angani, viumbe vyote vitambaavyo, naam, kila kiumbe chenye uhai, chakula chao kitakuwa majani yote ya mimea.” Ikawa hivyo.
UNAONA: Mungu alimpa kila kitu Adam na Mkewe Hawa. KUMBE ADAMA NA HAWA WALIKUWA MATAJIRI. Je, wewe unasubiri na kungoja nini? Muamuru Shetani akurudishie mali zako zote kwa Jina la Yesu.
Mithali 3:16; (Yesu kristo Mnazareti) ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na Heshima katika mkono wake wa kushoto.
MAANA YA TAJIRI:
Tajiri ni yule mtu mwenye mali nyingi na mwenye moyo wa kusaidia wenye uhitaji na anayefaidi mali zake kwa amani kuu na sio tu kumiliki na kutawala mali nyingi. Huyo ndiye Tajiri katika Bwana anayesomeka pajini mwa uso wake hata pasipo kujua utajiri anaomiliki. Lakini ile kuwa na roho mtakatifu ni utajiri unaothihirika hadi mwilini. Kama ilivyokuwa kwa Mfalme Sulemani (2 Mambo ya Nyakati 1:15) inasema; "Mfalme Sulemani alifanya fedha na dhahabu kuwa kama mawe ule wingi wake huko Yerusalemu na mierezi akafanya kuwa kama mikuyu iliyoko shefela kwa kuwa mingi". Hii yote inatokana na kuwa na Bwana Yesu wa Nazareti ya kwamba ni utajiri utajirishao wengi na sio tu muhusika yaani ni utajiri usio binafsi na ndiyo utajiri wa kweli unaomaanishwa.
Biblia katika Waefeso 3:8-11 pia inasema kwa habari ya Mtume Paulo; “Mimi, niliye mdogo kuliko yeye aliye mdogo wa watakatifu wote, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa UTAJIRI WAKE KRISTO USIOPIMIKA; na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote, kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi. Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu."
“Na Mungu wangu atawajazeni KILA MNACHOHITAJI KWA KADIRI YA UTAJIRI WAKE KATIKA UTUKUFU, NDANI YA KRISTO YESU" (Wafilipi 4:9)

Wednesday, December 9, 2015

SHETANI LA ULAFI KATIKA UISLAMU

Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujifunze kidogo kuhusu roho ya ulafi ambayo inawasumbuwa ndugu ztu katika Adam. Hebu tusome Biblia kama ushahidi.
Wafilipi 3: 19 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.
Walafi wao wamesha amua kuabudu chakula na mungu wao ni matumbo yao. Mtu mlafi akiona chakula, basi yeye hula kwa haraka haraka na kujaza tumbo lake mpaka anavimbiwa. Ulafi ni dhambi kama ilivyo sema kwevye Wafilipi hapo juu. Ulafi ni kuabudu tumbo.
Mithali 23: 20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.
Watu wanao kula nyama kwa Pupa mpaka wanavimbiwa na kushindwa kutembea, hao wana roho chafu ya ulafi, na ni dhambi kuabudu chakula au kuwa mtumwa wa chakula au mtumwa wa tumbo lako.
Kuna dini fulani wao wanapo dai kuwa wanafunga siku thelasini, huwa wanabadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha mpaka wanavimbiwa matumbo yao. Hiyo dini ni dini ya walafi na wanatenda dhambi, huku wao wakifikiria kuwa wanafunga kwa Allah wao.
Wagalatia 5: 16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
24 Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
26 Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
Kama Neno la Mungu linavyo sema kuwa, tusiwe na tamaa za mwili, maana mwili wetu ni hekalu la Mungu. Ikimaanisha kuwa Roho Mtakatifu anaishi ndani ya mwili wetu, na hivyo, ni vyema tuutunze. Ulafu ni roho kutoka kwa Shetani na kula mpaka kuvimbiwa ni dhambi na ni kuabudu chakula na matumbo yetu.
1 Wakorintho 6: 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
Basi mpendwa, usiongozwe na tamaa za mwili bali ongozwa na Roho aliye ndani yako.
Leo tumejikumbusha kuwa, Ulafi ni roho kutoka kwa Shetani na ni dhambi.
1. Kwanini Waislam wanakula usku kucha wakati wa mfungo wa Ramadhani?
2. Kwanini Allah amewaruhusu kula usiku kucha na kuwakalisha na njaa mchana kucha, je huko si kubadilisha masaa ya kula?
3. Mbona Yesu wa Biblia alipo funga, yeye hakula Daku?
Hakika kubadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha ni ulafi, na ni dhambi mbele ya Mwenyezi Mungu.
Max Shimba Ministries

JINSI YA KUENENDA KWA ROHO

Wagalatia 5:16 “Basi, nasema enendeni kwa Roho, wala hamtatimiza kamwe tamaa za mwili”Hapa tunaona Paulo anawaagiza wagalatia kwamba waenende kwa Roho na lengo kubwa ni ili wasizitimize tama za mwili.
Lengo la waraka huu mfupi ni kukueleza namna unavyoweza kuenenda kwa Roho, na hii ni kwa sababu Yesu mwenyewe alisema ni heri mimi niondokeili aje mwingine msaidizi huyo Roho wa kweli. Na 
kama tunaye Roho mtakatifu ni lazima tujue ni kwa namna gani tutaenenda kwa roho?Neno la Mungu/ Mungu anaposema, enendeni kwa Roho ana maana hii:-
(a) Kila unalolizungumza, lizungumze chini ya uongozi wa Roho mtakatifu. Yohana 12:49-50. Yesu mwenyewe hakunena neno lolote kwa shauri lake, bali kila ambalo baba alimwambia kupitia Roho mtakatifu. Hivyo hata wewe
kama unafundisha, unahubiri, unaonya hakikisha unachokisema Roho mtakatifu ndiye amekuruhusu ukiseme. Usiseme kitu cha kwako halafu ukasema Roho mtakatifu amekuongoza.
(b) Tii uongozi wake .Yohana 16:13 “ lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli; atawaongoza awatie kwenye kweli yote…….” Moja ya kazi za Roho mtakatifu ni kutuongoza na kututia kwenye kweli yote. Hivyo kuenenda kwa Roho maana yake ni kutii katika yale anayotuambia maana hata yeye haneni kwa ridhaa yake isipokuwa yale anayoyasikia kutoka kwa Mungu.

SOMO: MAOMBI YA CHUMVI YA KUVUNJA LAANA NA MAAGANO YA UKOO


Jinsi ya kuvunja Roho za laana na maagano kwenye ukoo wenu, maana watu wengi wameshindwa kufikia malengo na hata kukata tamaa kwa sababu ya maagano na laana za kabila zao, leo hii Mungu anakwenda kukuvusha, chumvi uliyoishika enaenda kukugeuza na kuangalia familia yako wapi imetoka na wapi inaelekea.
Habari ya ukoo ni sawa na lugha ya kabila bali siyo lugha ya Taifa, Mungu hakuumba msomi aliumba kabila ndio maana hata baadhi ya mapepo hayawezi kutoka mpaka ya sikie lugha ya kabila la kwenu.usiangalie wapi umetoka maana Mungu wetu hahukumu umefanya dhambi ngapi, bali wewe upo kwenye nafasi gani?
UFUNUO WA YOHANA 7:1 ‘’Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya mti wowote.’’
Maandiko yanasema Malaika walisimama pande nne wakizuia upepo usivume kwa ajili ya makabila kumi na mbili na kila pembe alisimama malaika mmoja.
kwa hiyo uwe na uhakika kwenye ukoo wa kwenu, hiyo nafasi ambayo alitakiwa asimame Malaika lakini sasa yamesimama mapepo ambayo yamezuia pande nne za ukoo wenu kusitokee upenyo wa maendeleo ya fedha na uchumi.
Kwa maana nyingine kusimamishwa kwa ukoo wa kwenu halafu tunashuhudia mnazika watu kuanzi miaka themanini na kuendelea na naghafla mkaanza kuzika kuzika chini ya kiwango hicho mjue kuna Roho nyingine zimewaingilia kati na zinauwa mmoja baada ya mwingine, na hata wale walioendelea bado hawajakufa kiroho lakini fedha zao zinaendelea kutumika na wale wanaendelea kifedha na watoto wao wamekufa, jua kuna matatizo kwenye familia nzima na unajaribu kutoa sadaka , kwenda kwenye maombi lakini tatizo bado linaendelea.
Mwanangu maombi ya siku moja hayawezi kubadilisha jahazi lililokuwa limezama, lazima ujipange sawasawa na kanuni ya Bwana inayosema natafuta mtu atakaekuwa mlango wa mimi kupita ili nipige na nisizuru ukoo iliyo baki nyuma.
Tunapo ongelea pepo haimaanishi ukoo wenu umefungwa bali kuna roho ambayo ni mlango unaokaribisha mapepo,maana kama roho ya Yuda ilijiunganisha na shina la Daudi na shina la Daudi likajiunganisha na Yesu, Uwenauhakika roho ya nyumbani kwenu itajiunganisha na mapepo.
UFUNUO 7,9,10 “Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila Taifa, na kabila,na jamaa na lugha wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za mwana –kondoo,wamevikwa mavazi meupe,wana matawi ya mitende mikononi mwao. wakilia kwa sauti wakisema Wokovu una Mungu wetu aketiye katika keti cha enzi, na mwana kondoo.’’
Mungu anayasikia maombi yako usifikili wingi wa dhambi zako, maandiko yana sema, Adamu pamoja nakufanya dhambi lakini alimsikia Mungu alipo mwita Adamu uko wapi? Mungu hajishuhulishi na dhambi ulizo fanya bali atakuuliza nafasi yako ipo wapi? aliyokuweka kama Habakuki , maana atasimama katika zamu yake na atamuona Bwana atakacho mjibu.
UFUNUO 5:2 “Nikaona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu,Ni nani astahiliye kukifungua kitabu, na kuzivunja muhuri zake? Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya nchi,wala chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu,wala kukitazama.’’
Maandiko ya natuambia kisha nikamuona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma,kimetiwa muhuri saba.
Kwa niaba ya F.J Kilawa
Max Shimba Ministries

MAOMBI YA KUPINGA MAGONJWA, VIFO, AJALI NA UHARIBIFU KATIKA MAISHA YAKO

1. Baba, katika jina la Yesu, naangusha kila mbinu za kishetani zinazozuia mafanikio yangu, katika jina la Yesu.
2. Nakataa na kupinga magonjwa ya kila aina katika nyumba yangu na familia yangu, kwa jina la Yesu.
3. Imeandikwa katika Zekaria 2:8 ya kwamba “Yeye anayenigusa mimi anagusa mboni ya jicho la Mungu”, hivyo, ninalisimamia Neno hili na kupinga kila nguvu inayosababisha magonjwa na upotevu wa fedha zangu katika jina la Yesu.
4. Nasimama kinyume na ajali na vifo katika familia yangu na ndugu zangu katika jina la Yesu.
5. Nawafunika watu wa familia yangu, kijiji changu na nje ya kijiji kwa damu ya Yesu. Ninawalinda na kuwaongoza kila mmoja kwa jina la Yesu.
6. Ninaamuru kila kinachoharibu mtaji na biashara yangu kufa mara moja katika jina la Yesu.
7. Ninaificha fedha yangu yote katika damu ya Yesu na kamwe adui hawezi kuigusa.
8. Baba, katika jina la Yesu, nasimama katika Neno kama mtoto wa Mungu niliyeketishwa mahali pa juu pamoja na Kristo, na ninatangaza kuwa mikutano ya kipepo juu ya maisha yangu na fedha yangu haitafanikiwa, katika jina la Yesu.
9. Namfunga kila anayeharibu fedha yangu nyumbani na sehemu yangu ya kazi katika jina la Yesu.
10. Wewe pepo uliyetumwa kuharibu biashara na fedha zangu, ninakufunga na kukutupa kwenye shimo la giza katika jina la Yesu.
11. Ninaamuru moto wa Roho Mtakatifu kumlamba kila mmoja aliyesimama kinyume na biashara na mafanikio yangu katika jina la Yesu.
12. Ewe mlima uharibio, ninakuangusha na nianaamuru usambaratike, katika jina la Yesu. 13. Ninaificha biashara, ofisi, fedha na miradi yangu yote katika damu ya Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliye hai. Amen.
14. Bwana, ninaomba upendeleo wako katika maisha yangu ili niweze kufanikiwa.
15. Upendeleo wako unizunguke kadiri ya Neno lako, katika jina la Yesu.
16. Bwana, naomba kuunganishwa na watu watakaonisaidia kufikia ndoto zangu kwa jina la Yesu.
17. Oh, Bwana, naomba ufanye njia kwa ajili yangu hata pale pasipo na njia katika jina la Yesu.
18. Baba, naomba niunganishe na mtu ambaye atakuwa msaada mkubwa katika kuyafikia mafanikio yangu katika jina la Yesu. 19. Baba ninaamini ya kwamba kila ninapokanyaga ninapamiliki sawasawa na na Neno lako, hivyo naomba univike vazi lako la upendeleo katika jina la Yesu.
20. Asante Bwana Yesu kwa kuwa umefanya sawasawa na nilivyokuomba katika jina la Yesu.
Amen.

MAOMBI YA HATARI


UTANGULIZI
Maombi ya hatari ndiyo ni sahihi. Kichwa cha habari kinaogopesha katika mtazamo wa kwanza, lakini maelezo yake ni matamu, naamini matamu kuliko asali. Huwezi kueeleza kwa undani maana ya maombi ya hatari mpaka utakapokua unafanya. Haya ni maombi ambayo ulimwengu mzima umekuwa ukiyatamani, kila mtoto wa Mungu anapaswa kuomba haya ili kuweza kumweka shetani pamoja na mapepo yake kule wanakostahili.
Unapokuwa umeomba maombi haya katika Roho na kweli, utakuwa unamwambia shetani 'IMEKWISHA'' mimi niko nje ya kambi yako. Hebu turudi kwenye jarada hili la kitabu hiki tuone kwanza nyundo nzito na yenye hatari inavyoharibu kijibanda kwa nguvu isiyo kifani na utaweza kuona kufuli (kitasa) na mlango wa kijibanda vinavunjwa vipande vipande kwa ile nyundo. Ukitazama kwa uangalifu zaidi, utamwona mtu akikimbia kutoka kwenye kibanda akiwa huru kabisa.
Hivi ndivyo maombi haya ya hatari yalivyomweka mtu huru kutoka kwenye vifungo vya shetani na mapepo yake. Maombi ya hatari ni nguvu na uwezo mkuu wa Roho Mtakatifu unaona hivi na kuangamiza nguvu za giza zilizopo dhidi yako. Maombi haya ukiyatumia, utakuwa huru kutokana na vigongo na mashambulizi ya kishetani yanayo kuzunguka. Kamwe usinisifu mimi, baada ya maombi haya, bali mpe Mungu, Yesu na Roho Mtakatifu utukufu wote, ambao ndiyo walioniwezesha kuyafahamu maombi haya.
Kabla ya maombi yako hayajawa na hatari unapaswa kwa mtu wa hatari unapokuwa mtu wa hatari ndipo utakapoweza kuomba maombi ya haraka na utakapoomba maombi ya hatari UPAKO WA HATARI uatanza kutiririka, na mambo ya hatari yataanza kufanyika katika ulimwengu huu na katika ulimwengu wa Roho.
MAPAMBANO YA KIHEKIMA
Kama tutajua nafasi yako ndani ya Kristo, ndipo utakapojua haki yako. Ukijua haki yako unauwezo wa kutumia haki yako, shetani na mapepo yake watakimbia.
Maombi ya hatari yanashambulia kiini cha matatizo yako. Hii ni njia nzuri ya kufanya nashambulizi. Unapokishinda kiini cha matatizo, sehemu nyingine ya hilo tatizo huwa inakufa. Unapotaka kuua mmea, unachotakiwa ni kung'oa shina lake na mti huo utakufa. Ikiwa tu utakata matawi, bila kung'oa shina hilo shina unaweza kuchipua tena. Hivyo inachotakiwa ni kuikata mizizi na mmea utakufa kabisa.
Maombi ya hatari ni aina ya maombi ambayo yanamlazimisha shetani na majeshi yake kuhama kwa nguvu na Roho Mtakatifu, hata kwama hawataki kuhama. Maombi haya yanaangamiza nguvu zote za shetani kuanzia ngazi za chini hadi ngazi za juu. Maombi ya hatari kama yanavyoitwa humfanya mtu wa Mungu kuwa huru kutokana na kutawaliwa na nguvu za shetani. Maombi haya huleta ukombozi kwa kila mtu wa Mungu
Maombi ya hatari huondoa na kuharibu kila laana maagano na makubaliano dhidi ya mtu wa Mungu. Tukitumia ujasiri tunaopata kwa njia ya Roho Mtakatifu, tunaweza kujiletea ukombozi sisi wenyewe tuapoomba maombi haya.
Maombi ya hatari hayampi shetani nafasi ya kuaingilia maisha yetu au maendeleo yetu. Maombi ya hatari ni maombi ya nguvu yanayopaswa kuombwa na watu wa Mungu wenye nguvu. Maombi ya hatari hutangaza VITA dhidi ya nguvu za giza zinakuzunguka na ufalme wa shetani mwenyewe.
Maombi haya yanakufanya kuwa zaidi ya mshindi; kila mtu wa Mungu anahitaji maombi haya ili awe mshindi wakati unaposhindwa kuishi maisha ya ushindi.
Fellowship, vikundi bya Kikristo, Makanisa na huduma zinahitaji aina hii ya maombi kwa ajili ya ushindi na kuwafanya waumini wake kukombolewa kwa jina la Yesu.
i. Biblia inasema utakuwa kiumbe kipya kiroho (2 Wakoritho 5:17)
ii. Ni lazima uwasamehe wote wakikukosea
Kama ulivyokwesha kujulishwa maombi ya hatari ni nini? Inakufahamisha juu ya maombi haya kwa uangalifu, maombi haya siyo ya mkato bali ni maombi yenye nguvu, kwa sababu ufalme wa Mungu hutekwa na wenye nguvu (MATHAYO 11: 12)
JINSI YA KUOMBA MAOMBI HAYA

VUNJA VIFUNGO, MAAGANO, NA MIKATABA YA KISHETANI MAISHANI MWAKO

Kutoka 23:32 ''Usifanye maagano pamoja nao, wala pamoja na miungu yao.''
Agano ni kitu kikubwa sana, Agana la kipepo ni mapatano ya kishetani, ni mikataba ya kishetani na MUNGU hataki tuingie agano lolote na shetani wala mawakala wake.
Kuna watu wanapitia mateso mengi sana, wengine wamefungwa katika vifungo bila wao kujijuwa basi chukua muongozo huu utakusaidia au itasaidia familia yako.
Biblia inapozungumza habari ya watu waliofungwa wapate kufunguliwa, hii ina maana ya kuwa kuna watu wamefungwa chini ya utawala wa nguvu za giza katika ulimwengu wa Roho. Watu hawa wamefungwa kwenye magereza na Ibilisi.
Isaya 57:8 '' Na nyuma ya milango na miimo umeweka kumbukumbu lako; kwa maana umejifunua nafsi yako kwa ajili ya mwingine, si kwa ajili yangu, ukakwea juu; umekipanua kitanda chako, nawe umefanya maagano na hao; ulikipenda kitanda chao hapo ulipokiona. ''
-Maagano mabaya ni jambo baya sana ndugu. kama zamani uliwahi kuingia maagano ya kishetani basi kimbilia kanisani ukaombewe maana maagano ni mkataba na ukiingia mkataba na shetani mwishowe anaweza kukuangamiza tu na uzima wa milele ukaukosa.
Tutambue ya kuwa Yesu aliposema amekuja kutuokoa hii inamaanisha kwamba kuna mahali ambako tusingeweza kujikwamua wenyewe bila nguvu yake yeye mwenywe kuingia kati yetu.
Aliyahidhirisha haya kwenye kitabu cha nabii Isaya 61:1-2 Roho ya Bwana Mungu i juu yangu kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema, amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao”.
Vunja uhusiano wako na hiyo miungu pamoja na kazi zake na agano lililofanyika kati ya familia au ukoo wako na hiyo miungu. Kila unapotamka mwisho wake sema kwa sababu nimesamehewa. Ipo mistari mingi ya kuvunja maagano lakini mimi nitakupa kifungu hiki cha mstari katika kuvunja maagano na mapoozo ya aina yoyote. “Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa kwa sababu ya kutiwa mafuta” Isaya 10:27

JINSI YA KUTOA PEPO WABAYA/CHAFU

Maana ya neno pepo linamaanisha, pepo mbaya, shetani, mwovu, mharibifu na mwangamizi. Hao ni malaika waliomuasi Mungu wakatupwa duniani. “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na Yule joka (Shetani), Yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; Nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, Yule mkubwa, Yule wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.” Ufu 12:7-9.
1. Ili kutoa pepo, kuna mambo ambayo yanapaswa kuzingatiwa:
Ni lazima uwe na nguvu za Roho Mtakatifu.Tunaweza kujifunza kwa Yesu alivyoweza kutoa pepo kwa uwezo na nguvu za Roho. Imeandikwa, “…..awaaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.” Luka 4:36.
2. Kutoa pepo kwa jina la Yesu. Aliye na amri na mamlaka ya kutoa pepo ni mkristo ambaye amemwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake. “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo……” Math 16:17. Wale ambao bado hawajamwamini Yesu na kuokoka, Si vyema kujaribu kutoa Pepo kwa sababu hatatoka, vile vile wanaweza kushambuliwa na hao walio na Pepo, kama wale wana wa Skewa, Kuhani Mkuu.
“.....wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nakuapisha kwa Yesu, Yule anayehubiriwa na Paulo. Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, Kuhani Mkuu, walifanya hivyo..... na yule mtu aliye pagawa na pepo wachafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.” Mdo 19:13-16.

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW