Monday, December 14, 2015

USIKUBALI KUWA MPUMBAVU KWA KUKATAA KUWA HAKUNA MUNGU NA KUWA YESU NI MUNGU

Kuna imani nyingi sana hapa duniani, zingine zinadai kuwa "Hakuna Mungu" eti, kwasababu wameshindwa kuongea nae na au kumwona; Imani zingine zinadai kuwa "Hakuna Mungu" eti kwasababu Sayansi inashindwa kuhakikisha uwepo wake scientifically; Imani zingine zinadai kuwa, kivipi Yesu awe Mungu na biandamu kwa wakati mmoja, zinadai eti, Mungu halali, wala hali chakula, lakini wakati huo huo wanakiri kuwa Mungu anaweza kufanya jambo lolote lile atakalo; Haya yote ni madai ambayo hawawezi kuyathibitisha.
Hebu tusome Biblia:
2 Samweli 2:31-34 na Zaburi 14:1 ‘Mpumbavu amesema moyoni, mwake hakuna Mungu…..’ Mpenzi msomaji naamini unaendelea vema kwa ujumla kimwili na kiroho. Katika mwezi huu nataka niseme nawe juu ya kifo cha kipumbavu.
Mpumbavu ni nani? Kibiblia ni mtu yoyote aliyekataa kuwa na ufahamu au elimu ya Mungu ndani yake. Mtu aliyekataa uwepo wa Mungu au kuwa na Mungu maishani mwake.
Hivyo basi mpumbavu ni mtu ambaye moyoni mwake amesema hakuna Mungu. Mauti inayomkuta mtu ambaye amekana elimu au ufahamu au uwepo wa Mungu katika maisha yake ni mbaya sana, maana mwisho wake ni Jehannam. Mauti inayommkuta mtu kabla hajakubali uwepo wa Mugu katika maisha yake. Kifo kinachomkuta mtu ambaye hajampa Mungu nafasi ya utawala moyoni mwake mwisho wake ni ziwa la moto. Je wewe unataka kuishi milele yote kwenye ziwa la moto?
YESU ANAKIRI KUWA YEYE NI MUNGU KATIKA KITABU CHA UFUNUO:
Ufunuo 1:17 na Ufunuo 22:13
Mimi ni wa kwanza na wa mwisho
Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
Ni Mungu TU ndiye mwenye uwezo wa kuwa wa kwanza na wa mwisho; Yesu ni Alfa na Omega. Kwa hiyo Yeye ni Mungu.
Ukikataa kuwa Yesu sio Mungu, basi wewe ni mmoja wa lile kundi la Wapumbavu. Katika Zaburi, tumeambiwa kuwa Mpumbavu kasema kuwa Hakuna Mungu.
Tujifunze kwa Abneri. 2 Samweli 2:22-39 ukisoma vema hapa utaona habari za shujaa mmoja aliyeitwa Abneri. Kwa kifupi Abneri alikuwa;
Kiongozi wa majeshi ya Sauli, mpinzani mkubwa wa Daudi, baadaye alipelekea Daudi kuitawala Israeli yote, Alimwua Asaheli shujaa wa Daudi ndugu yake Yoabu, kiongozi wa majeshi wa Daudi. Na mwishowe Yoabu ndiye aliyemwua Abneri ili kulipiza kisasi cha kifo cha nduguye.
Sasa baada ya kifo cha Abneri, ndipo Daudi akamlilia Abneri akasema, ilimpasaje Abneri kufa afavyo mpumbavu?, mikono yako haikufungwa wala miguu yako haikutiwa pingu; aangukavyo mtu mbele ya wana wa uovu, ndivyo ulivyoanguka.
Ukiendelea kusoma habari hii utaona kwamba siku ile Daudi alikataa kula akimliilia Abneri, akisema hamjui ya kuwa mkuu mmoja, naye ni mtu mkubwa ameanguka leo katika Israeli?
Je kwa mazingira ya leo, mtu anawezaje kufa kifo cha kipumbavu?Unaposhindwa kutumia fursa zilizopo kuiponya nafsi yako matokeo yake ni kifo cha kipumbavu. Abneri hakufungwa mikono wala miguu lakini aliuawa. Daudi alikuwa akimuuliza Abneri kwa nini usitumie mikono na miguu yako kuiponya roho yako? .
Katika Zaburi 14;1 TUMEONA MPUMBAVU NI MTU YULE AMBAYE MOYONI MWAKE AMESEMA HAKUNA MUNGU, kwa lugha nyepesi amekataa kuwa na Mungu moyoni mwake na kwa sababu hiyo amekataa uongozi wa Mugu katika maisha yake.

UTHIBITISHO 10 KUWA YESU NI MUNGU

“Wahubiri wa injili” wa Kiislamu huwa wanapinga kuwa Yesu ni Mungu na unapowakatalia wanakwambia, “Lete andiko.” Maandiko yapo mengi sana ndani ya Biblia juu ya ukweli kwamba Yesu ni Mungu. Ni mengi mno!
Ukishawapa andiko, wanabadilika na kusema, “Nataka maneno aliyoongea Yesu mwenyewe.” Kwa madai haya hata kwenye Qurana hawawezi thibitisha kuwa Allah Allah ni mungu, zaidi ya hapo, hata Utume wa Muhammad unakuwa kwenye njia panda, maana hakuna aya kwenye Quran Muhammad anasema mimi Muhammad ni mtume wa Mungu.
Hiki ni kigezo POTOFU na si cha kibiblia hata kidogo. Ukweli ni kwamba, Biblia YOTE ni Neno la Mungu. Haijalishi amezungumza Musa, Isaya, Yohana, Petro au Yesu mwenyewe. Imeandikwa:
Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. (2Petro 1:21).
Hivyo, kudai kwao eti, “Nataka maneno aliyosema Yesu mwenyewe,” ni kigezo batili na kisicho na mantiki hata kidogo.

1. YESU ALIKUWEPO KABLA YA KUZALIWA
Ufuatao ni ushahidi wa kibiblia kwamba YESU KRISTO ni Mungu.
Yohana 8:58
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.
NIKO ni jina la Mungu peke yake. Tunakutana na jina hilo pale Musa alipoongea na Mungu na kutumwa kuwakomboa wana wa Israeli kutoka Misri. Imeandikwa:
Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO (Kutoka 3:13-14).
Mwanadamu yuko kwa sababu Mungu alisababisha awepo. Gari liko kwa sababu injinia au mbunifu alisababisha liwepo. Nyumba ipo kwa sababu fundi alisababisha iwepo. Lakini Mungu YEYE YUKO TU!! Hayupo kwa kusababishwa na yeyote! Ndiyo maana akasema MIMI NIKO AMBAYE NIKO! Yesu ni NIKO. Kwa hiyo, Yeye ni Mungu.
2. YESU NA BABA NI WAMOJA
Yohana 10:30
Mimi na Baba tu umoja.
Waislamu wana msemo wao kwamba eti, Yesu na Mungu ni wamoja katika malengo, si katika asili yao. Basi huwa nawauliza swali kuhusu aya ifuatayo ya Isaya, nao wanazimika na kukosa jibu:
Isaya 9:6
Maana kwa ajili yetu MTOTO amezaliwa, Tumepewa MTOTO MWANAMUME; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE, Mfalme wa amani.
Aya hii iko wazi kabisa. anayetajwa ni Yesu kwamba Yeye ni Mungu mwenye nguvu.
Yohana 14:9
Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?
Maneno haya Yesu aliyasema baada ya kuulizwa swali lililo wazi kabisa, ambalo lilikuwa na lengo la kumjua MUNGU BABA! Imeandikwa: Filipo akamwambia, Bwana, UTUONYESHE BABA, yatutosha. Ndipo Yesu akajibu waziwazi: ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA. Maana yake ni kuwa, “Mimi ndio Baba mwenyewe.”
3. YESU NI MWANZO NA MWISHO
Ufunuo 1:17 na Ufunuo 22:13
Mimi ni wa kwanza na wa mwisho
Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
Ni Mungu TU ndiye mwenye uwezo wa kuwa wa kwanza na wa mwisho; Yesu ni Alfa na Omega. Kwa hiyo Yeye ni Mungu.
4. YESU NI NENO
Yohana 1:1
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye NENO ALIKUWA MUNGU.
Andiko hili Waislamu hawalipendi kabisa. ni kwa sababu liko wazi mno. Yesu ni Neno; na Neno ni Mungu; hivyo, Yesu ni Mungu!
5. THOMASO AKIRI KUWA YESU NI MUNGU, NA YESU HAKUKATAA KUITWA MUNGU
Yohana 20:28
Tomaso akajibu, akamwambia, BWANA WANGU NA MUNGU WANGU!
Tomaso aliposema hivi, Bwana Yesu hakukanusha na kusema, “Mimi sio Mungu.” Badala yake: Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. (Yoh 20:29).
Kama Thomaso alikuwa muongo, kwanini Yesu hakukataa kuitwa Mungu. Imani zote zinakiri kuwa Yesu hakufanya dhambi na hakuwa na dhambi.
6. DAMU YA YESU INAMAMLAKA
Matendo 20:28
Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake MUNGU, ALILOLINUNUA KWA DAMU YAKE MWENYEWE.
Ni Mungu gani mwenye damu huyu? Jibu liko wazi. Huyu ni Yesu Kristo. Huyu ndiye aliyetoa uhai wake na kumwaga damu yake msalabani; na hapo ndipo alipoanzisha Kanisa.
7. KATIKA YESU, KILA KITU KILIUMBWA
Wakolosai 1:16
Kwa kuwa KATIKA YEYE VITU VYOTE VILIUMBWA, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
Katika Yeye Yesu vitu vyote viliumbwa. Ina maana kuwa vitu vyote vilitokana na Yesu; maana Yesu ni Neno la Mungu. Na tunajua kuwa Muumba wa vitu vyote ni Mungu; hivyo, Yesu ni Muumba – Yeye ni Mungu!!
8. KATIKA YESU, UNAKAA UTIMILIFU WA MUNGU
Wakolosai 2:9
Maana KATIKA YEYE UNAKAA UTIMILIFU WOTE WA MUNGU, kwa jinsi ya kimwili.
Sisi sote ni watu wasio wakamilifu. Tunaanguka tena na tena kwenye dhambi. Kwa hiyo, hakuna mwanadamu wa kawaida ambaye anaweza kujigamba kwamba yeye ametimia kama alivyo Mungu. Lakini katika Yesu “utimilifu WOTE wa Mungu unakaa.” Kwa nini? Kwa sababu Yeye ndiye Mungu huyohuyo.
9. YESU NI MUNGU PAMOJA NASI "EMMANUEL"
1Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.
Ni Mungu gani aliyedhihirishwa katika mwili? Jibu liko wazi. Ni Yesu Kristo peke yake.
10. YESU NI MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Tito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Waislamu ni hii: Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yer 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Lakini utakuta Waislamu wanauliza maswali ya ajabu sana. Eti, kama Yesu ni Mungu, wakati amekufa, nani alikuwa anaangalia dunia?
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO!
YESU NI MUNGU MILELE NA MILELE!!
HALELUYA!!
Tafakari
Hoji mambo
Chukua hatua!

UPONYAJI KATIKA JINA LA YESU

Leo ninaweka aya kadhaa zinazo tupa mamlaka ya kuombea wagonjwa.
Mungu akubari mpendwa na pokea uponyaji wako leo katika Jina la Yesu aliye hai.
Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya nayo yote. - [Zaburi 34:19]
Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa. Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii. - [Yakobo 5:14-16]
Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao. - [Zaburi 107:20]
Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa Bwana. - [2 Wafalme 20:5b]
Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye. - [Yeremia 30:17a]
Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. - [Isaya 40:29]
Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote, - [Zaburi 103:3]
Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. - [Isaya 53:5]
akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi Bwana nikuponyaye. - [Kutoka 15:26]
Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika. - [Luka 17:14b]
Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. - [Mathayo 10:1]
Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini. - [Malaki 4:2a]
Petro akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; ondoka, ujitandikie. Mara akaondoka. - [Matendo ya Mitume 9:34]
Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya. - [Marko 16:17-18]
mkaifanyie miguu yenu njia za kunyoka, ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe, bali afadhali kiponywe. - [Waebrania 12:13]
Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. - [2 Wakorintho 12:7-9]
Baada ya kusoa hizo aya, sasa pokea uponyaji wako katika Jina la Yesu alie hai.
Max Shimba Ministries 2015

MAOMBI YA USHINDI KWA MAISHA YAKO

Baba katika Jina la Yesu.
Laana zote nilizo tupiwa na wabaya wangu zimeshindwa kwa jina la Yesu na nazivunja na kuzisambaratisha kwa Damu ya Yesu. Mshindwe wote mnao tuma laana kwangu katika Jina la La Yesu.
Nawavunja na kuwaharibu na kuwakatakata Wachawi wote kwa damu ya Yesu.
Nasambaratisha kila neno la uovu lililosemwa juu yangu na familayangu katika jina la Yesu.
Naharibu na kuisambaratisha madhabahu yenu mliyo fanyia kafara kwa damu ya Yesu.
Navunjavunja na kubomoa kila uovu na uchawi mnaonifanyia katika jina la Yesu.
Nairudisha misukule yote na majini yote yawarudie nyie na kuwalipa dhambi zote mnazo fanya katika jina la Yesu.
Naharibu kila uchawi, kila urogi, kila ndumba kila aina ya uovu ambao mnaufanya ili uniumize mimi na familia yangu katika jina la Yesu.
Nawateketeza kupitia damu ya Yesu Wachawi wote walio tumiwa kunitumia uchawi katika jina la Yesu.
Nawateketeza na kuwaharibu majini yote yaliyo tumwa kuja kufanya kazi hiyo waliyo tumwa na Wachawi katika jina la Yesu.
Nawateketeza na kuwauwa Makuhani wote ambao walienda kunishitaki kwa Wachawi ili waniharibie maisha, nawateketeza kupitia damu ya Yesu. Nawachoma kwa Moto wa Roho Mtakatifu katika Jina la Yesu.
Nateketeza aina zote za vyombo vya kichawi vilivyo tumiwa kuja kunichunguza katika jina la Yesu.
Naharibu fikra zao zote ambazo wanazitumia kufanya kazi zao za kichawi katika jina la Yesu.
Nafuta kumbukumbu zoote zangu ambazo wamewapa Mashetani, Majini, Roho chafu, nafuta hizo kumbukumbu kwa kutumia damu ya Yesu, katika jina la Yesu aliye hai.
Nawateketeza waweka kumbukumbu wa kimashetani kupitia damu ya Yesu aliye hai. Naharaibu na kuchoma kupitia moto wa Roho Mtakatifu makabrasha yote yenye kumbukumbu zangu katika jina la Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuharibu maisha yangu na ubomoa kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuniua nauvunja na kuuteketeza kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili kuja kuiba mali zangu, nauvunja na kuubomoa na kuuharibu kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanya kuja kuniharibia familia yangu, nausambaratisha na kuuvunja na kuubomoa katika jina la Yesu.
Kila neno la kichawi lililo tumwa ili kuja kuniharibia, kunidhihaki, kunitendea mabaya nalirudisha kwa aliye lituma katika jina la Yesu.
Kila uovu, uchawi, wanga, ndumba, ramli, yaliyo tumwa kuja kwangu navunja yote hayo kupitia damu ya Yesu na katika Jina la Yesu.
Nyota yangu ambayo wanaita nairudisha kupitia damu ya Yesu. Nyota yangu ya baraka nailinda na kuzungushia na kuizingira na damu ya Mwana Kondoo katika jina la Yesu.
Namteketeza yule mtu aliye kuja kuiba nyota yangu katika jina la Yesu.
Nateketeza mbinu zote wanazo tumia ili kuja kuiba nyota yangu katika jina la Yesu.
Nateketeza wivu wao, chuki yao, laana zao, maovu yao na kila aina ya uchafu ambao wanao kwa ajili yangu katika jina la Yesu.
Naizungushia na kuizingira nyumba yangu na damu ya Yesu.
Naishungushia na kuizingira familia yangu na damu ya Yesu.
Nashungushia na kuzingira maisha yangu yote na damu ya Yesu.
Navunja laana zote zilizo semwa na mabau zangu katika jina la Yesu.
Navunja laana zato ambazo zilisemwa bila ya mimi kufahamu, nazivunja na kuziharibu kupitia damu ya Yesu na katika jina la Yesu.
Narudisha kila mali walizo ziiba kutoka kwangu katika jina la Yesu.
Narudisha kila baraka walizo ziiba kwangu katika jina la Yesu.
Narudisha amani na upendo katika familia yangu.
Damu ya Yesu ipo juu ya Maisha yangu na inasafisha kila uovu, kila uchawi unaaribiwa na damu ya Yesu katika jina la Yesu.
Leo hii mtaiona Nguvu iliyopo katika damu ya Yesu.
Katika Jina la Yesu aliye hai ninaomba.
Amen
Max Shimba Ministries Org

MAOMBI YA KUFUNGA MWAKA NA KUANZA MWAKA MPYA 2016 KWA BARAKA TELE KUTOKA KWA MUNGU MKUU, YESU KRISTO ALIYE HAI

Ndugu msomaji na mpendwa katika Bwana. Bwana Yesu apewe sifa.
Mpendwa, yawezekana umekuwa ukiishi bila kutambua uwezo wa jina la Yesu katika kukuonyesha mwelekeo wa maisha yako.Je, unahitaji mwelekeo mpya katika maisha yako? Je, unahitaji kujua njia ya kutoka katika hali uliyonayo?
KAMA UMECHOKA NA MAISHA YA TABU, KAMA UMECHOKA KUISHI NA MAGONJWA, KAMA UMECHOKA KUWA MASKINI, KAMA UNAHITAJI KAZI, BIASHARA YAKO IFANIKIWE N.K. BASI HUU UJUMBE NI WAKO.
Napenda kukufahamisha kuwa, tupo katika Maombi kila siku mpaka tutakapo maliza mwaka huu wa 2015. Nafahamu wengi mmepata baraka tele katika Mwaka wa 2015 na labda wengi mmlikuwa katika mashindano na vita kubwa na nguvu za giza. Kumbuka USHINDI ni wetu katika Jina la Yesu.
Mpendwa , pengine hali ya maisha uliyonayo imekufanya ukate tamaa na kujiona kwamba hakuna njia ya kukufanya utimize furaha ya ndoto zako. Je, unahitaji njia ya kuishi kwa amani na furaha; njia ya kuwa na mahusiano mazuri katika ndoa yako; njia ya kuwa na mahusiano mazuri na ndugu zako, kazini kwako, kwenye biashara yako; unahitaji njia ya kuacha ulevi wa pombe na madawa ya kulevya, njia ya kuacha kuabudu sanamu, njia ya kuacha uongo, njia ya kuacha uzinzi, njia ya kuacha uchawi, njia ya kuacha tamaa ya mali zisizo halali; njia ya kuponywa maradhi, njia ya kupata utajiri, njia ya kupata kazi, njia ya kupata mtaji , njia ya kutoka kwenye madeni, njia ya kupandishwa cheo, njia ya kutimiza ndoto zako? Yesu ni njia ya kila mahitaji yetu hapa duniani, pia yeye ni njia ya kutufanya tujue kweli ya neno lake na tuweze kuurithi uzima wa milele.
Kama unahitaji lolote lile ambalo unataka upokee jibu kutoka kwa Mungu Mkuu, Yesu aliye hai, basi nakusihi ututumie hilo hitaji lako haraka ili tuwe pamoja katika maombi katika muda huu wa kumaliza mwaka wa 2015. Tuma ombi lako kupitia barua pepe maxshimbaministries@gmail.com
Matayo 7:7-11Neno: Biblia Takatifu (SNT):
7 “Ombeni nanyi mtapewa. Tafuteni nanyi mtapata; bisheni hodi nanyi mtafunguliwa mlango. 8 Kwa sababu kila aombaye hupewa; naye atafutaye hupata; na abishaye hodi atafunguliwa mlango.
9 “Au ni nani kati yenu ambaye kama mwanae akimwomba mkate atampa jiwe? 10 Au akimwomba samaki atampa nyoka? 11 Ikiwa ninyi mlio waovu mnafahamu jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, ni mara ngapi zaidi Baba yenu wa mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
Yesu katika Matayo hapo juu anakwambia "OMBENI NANYI MTAPEWA' Sasa Mpendwa unasubiri nini kumwomba Mungu Mkuu? Au unapenda kuwa katika matatizo na shida? Shetani teyari alisha wekwa chini ya miguu yetu.

YESU KRISTO AMEKUPA UTAJIRI

Watu wengu wanafikiri kuwa, Mungu aliwaumba ili wawe watu wa kawaida tu, la hasha, Mungu amekuumba wewe ukiwa Tajiri. Ukisoma kuhusu Adam katika Kitabu cha Mwanzo, utaona kuwa, Mungu alimuumba Adam na Hawa baada ya kuumba dunia na kila kitu. Baada ya Adam na Hawa kuubwa, walikabidhiwa kila kitu kilichopo hapa duniani. Huo ni Utajiri mkubwa sana. Soma. Mwanzo 1: 28 Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.” 29Kisha Mungu akasema, “Tazama, nawapeni kila mmea duniani uzaao mbegu, na kila mti uzaao matunda yenye mbegu; mbegu zao au matunda yao yatakuwa chakula chenu. 30Nao wanyama wote duniani, ndege wote wa angani, viumbe vyote vitambaavyo, naam, kila kiumbe chenye uhai, chakula chao kitakuwa majani yote ya mimea.” Ikawa hivyo.
UNAONA: Mungu alimpa kila kitu Adam na Mkewe Hawa. KUMBE ADAMA NA HAWA WALIKUWA MATAJIRI. Je, wewe unasubiri na kungoja nini? Muamuru Shetani akurudishie mali zako zote kwa Jina la Yesu.
Mithali 3:16; (Yesu kristo Mnazareti) ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na Heshima katika mkono wake wa kushoto.
MAANA YA TAJIRI:
Tajiri ni yule mtu mwenye mali nyingi na mwenye moyo wa kusaidia wenye uhitaji na anayefaidi mali zake kwa amani kuu na sio tu kumiliki na kutawala mali nyingi. Huyo ndiye Tajiri katika Bwana anayesomeka pajini mwa uso wake hata pasipo kujua utajiri anaomiliki. Lakini ile kuwa na roho mtakatifu ni utajiri unaothihirika hadi mwilini. Kama ilivyokuwa kwa Mfalme Sulemani (2 Mambo ya Nyakati 1:15) inasema; "Mfalme Sulemani alifanya fedha na dhahabu kuwa kama mawe ule wingi wake huko Yerusalemu na mierezi akafanya kuwa kama mikuyu iliyoko shefela kwa kuwa mingi". Hii yote inatokana na kuwa na Bwana Yesu wa Nazareti ya kwamba ni utajiri utajirishao wengi na sio tu muhusika yaani ni utajiri usio binafsi na ndiyo utajiri wa kweli unaomaanishwa.
Biblia katika Waefeso 3:8-11 pia inasema kwa habari ya Mtume Paulo; “Mimi, niliye mdogo kuliko yeye aliye mdogo wa watakatifu wote, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa UTAJIRI WAKE KRISTO USIOPIMIKA; na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote, kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi. Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu."
“Na Mungu wangu atawajazeni KILA MNACHOHITAJI KWA KADIRI YA UTAJIRI WAKE KATIKA UTUKUFU, NDANI YA KRISTO YESU" (Wafilipi 4:9)

Wednesday, December 9, 2015

SHETANI LA ULAFI KATIKA UISLAMU

Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujifunze kidogo kuhusu roho ya ulafi ambayo inawasumbuwa ndugu ztu katika Adam. Hebu tusome Biblia kama ushahidi.
Wafilipi 3: 19 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.
Walafi wao wamesha amua kuabudu chakula na mungu wao ni matumbo yao. Mtu mlafi akiona chakula, basi yeye hula kwa haraka haraka na kujaza tumbo lake mpaka anavimbiwa. Ulafi ni dhambi kama ilivyo sema kwevye Wafilipi hapo juu. Ulafi ni kuabudu tumbo.
Mithali 23: 20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.
Watu wanao kula nyama kwa Pupa mpaka wanavimbiwa na kushindwa kutembea, hao wana roho chafu ya ulafi, na ni dhambi kuabudu chakula au kuwa mtumwa wa chakula au mtumwa wa tumbo lako.
Kuna dini fulani wao wanapo dai kuwa wanafunga siku thelasini, huwa wanabadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha mpaka wanavimbiwa matumbo yao. Hiyo dini ni dini ya walafi na wanatenda dhambi, huku wao wakifikiria kuwa wanafunga kwa Allah wao.
Wagalatia 5: 16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
24 Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
26 Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
Kama Neno la Mungu linavyo sema kuwa, tusiwe na tamaa za mwili, maana mwili wetu ni hekalu la Mungu. Ikimaanisha kuwa Roho Mtakatifu anaishi ndani ya mwili wetu, na hivyo, ni vyema tuutunze. Ulafu ni roho kutoka kwa Shetani na kula mpaka kuvimbiwa ni dhambi na ni kuabudu chakula na matumbo yetu.
1 Wakorintho 6: 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
Basi mpendwa, usiongozwe na tamaa za mwili bali ongozwa na Roho aliye ndani yako.
Leo tumejikumbusha kuwa, Ulafi ni roho kutoka kwa Shetani na ni dhambi.
1. Kwanini Waislam wanakula usku kucha wakati wa mfungo wa Ramadhani?
2. Kwanini Allah amewaruhusu kula usiku kucha na kuwakalisha na njaa mchana kucha, je huko si kubadilisha masaa ya kula?
3. Mbona Yesu wa Biblia alipo funga, yeye hakula Daku?
Hakika kubadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha ni ulafi, na ni dhambi mbele ya Mwenyezi Mungu.
Max Shimba Ministries

JINSI YA KUENENDA KWA ROHO

Wagalatia 5:16 “Basi, nasema enendeni kwa Roho, wala hamtatimiza kamwe tamaa za mwili”Hapa tunaona Paulo anawaagiza wagalatia kwamba waenende kwa Roho na lengo kubwa ni ili wasizitimize tama za mwili.
Lengo la waraka huu mfupi ni kukueleza namna unavyoweza kuenenda kwa Roho, na hii ni kwa sababu Yesu mwenyewe alisema ni heri mimi niondokeili aje mwingine msaidizi huyo Roho wa kweli. Na 
kama tunaye Roho mtakatifu ni lazima tujue ni kwa namna gani tutaenenda kwa roho?Neno la Mungu/ Mungu anaposema, enendeni kwa Roho ana maana hii:-
(a) Kila unalolizungumza, lizungumze chini ya uongozi wa Roho mtakatifu. Yohana 12:49-50. Yesu mwenyewe hakunena neno lolote kwa shauri lake, bali kila ambalo baba alimwambia kupitia Roho mtakatifu. Hivyo hata wewe
kama unafundisha, unahubiri, unaonya hakikisha unachokisema Roho mtakatifu ndiye amekuruhusu ukiseme. Usiseme kitu cha kwako halafu ukasema Roho mtakatifu amekuongoza.
(b) Tii uongozi wake .Yohana 16:13 “ lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli; atawaongoza awatie kwenye kweli yote…….” Moja ya kazi za Roho mtakatifu ni kutuongoza na kututia kwenye kweli yote. Hivyo kuenenda kwa Roho maana yake ni kutii katika yale anayotuambia maana hata yeye haneni kwa ridhaa yake isipokuwa yale anayoyasikia kutoka kwa Mungu.

SOMO: MAOMBI YA CHUMVI YA KUVUNJA LAANA NA MAAGANO YA UKOO


Jinsi ya kuvunja Roho za laana na maagano kwenye ukoo wenu, maana watu wengi wameshindwa kufikia malengo na hata kukata tamaa kwa sababu ya maagano na laana za kabila zao, leo hii Mungu anakwenda kukuvusha, chumvi uliyoishika enaenda kukugeuza na kuangalia familia yako wapi imetoka na wapi inaelekea.
Habari ya ukoo ni sawa na lugha ya kabila bali siyo lugha ya Taifa, Mungu hakuumba msomi aliumba kabila ndio maana hata baadhi ya mapepo hayawezi kutoka mpaka ya sikie lugha ya kabila la kwenu.usiangalie wapi umetoka maana Mungu wetu hahukumu umefanya dhambi ngapi, bali wewe upo kwenye nafasi gani?
UFUNUO WA YOHANA 7:1 ‘’Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya mti wowote.’’
Maandiko yanasema Malaika walisimama pande nne wakizuia upepo usivume kwa ajili ya makabila kumi na mbili na kila pembe alisimama malaika mmoja.
kwa hiyo uwe na uhakika kwenye ukoo wa kwenu, hiyo nafasi ambayo alitakiwa asimame Malaika lakini sasa yamesimama mapepo ambayo yamezuia pande nne za ukoo wenu kusitokee upenyo wa maendeleo ya fedha na uchumi.
Kwa maana nyingine kusimamishwa kwa ukoo wa kwenu halafu tunashuhudia mnazika watu kuanzi miaka themanini na kuendelea na naghafla mkaanza kuzika kuzika chini ya kiwango hicho mjue kuna Roho nyingine zimewaingilia kati na zinauwa mmoja baada ya mwingine, na hata wale walioendelea bado hawajakufa kiroho lakini fedha zao zinaendelea kutumika na wale wanaendelea kifedha na watoto wao wamekufa, jua kuna matatizo kwenye familia nzima na unajaribu kutoa sadaka , kwenda kwenye maombi lakini tatizo bado linaendelea.
Mwanangu maombi ya siku moja hayawezi kubadilisha jahazi lililokuwa limezama, lazima ujipange sawasawa na kanuni ya Bwana inayosema natafuta mtu atakaekuwa mlango wa mimi kupita ili nipige na nisizuru ukoo iliyo baki nyuma.
Tunapo ongelea pepo haimaanishi ukoo wenu umefungwa bali kuna roho ambayo ni mlango unaokaribisha mapepo,maana kama roho ya Yuda ilijiunganisha na shina la Daudi na shina la Daudi likajiunganisha na Yesu, Uwenauhakika roho ya nyumbani kwenu itajiunganisha na mapepo.
UFUNUO 7,9,10 “Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila Taifa, na kabila,na jamaa na lugha wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za mwana –kondoo,wamevikwa mavazi meupe,wana matawi ya mitende mikononi mwao. wakilia kwa sauti wakisema Wokovu una Mungu wetu aketiye katika keti cha enzi, na mwana kondoo.’’
Mungu anayasikia maombi yako usifikili wingi wa dhambi zako, maandiko yana sema, Adamu pamoja nakufanya dhambi lakini alimsikia Mungu alipo mwita Adamu uko wapi? Mungu hajishuhulishi na dhambi ulizo fanya bali atakuuliza nafasi yako ipo wapi? aliyokuweka kama Habakuki , maana atasimama katika zamu yake na atamuona Bwana atakacho mjibu.
UFUNUO 5:2 “Nikaona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu,Ni nani astahiliye kukifungua kitabu, na kuzivunja muhuri zake? Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya nchi,wala chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu,wala kukitazama.’’
Maandiko ya natuambia kisha nikamuona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma,kimetiwa muhuri saba.
Kwa niaba ya F.J Kilawa
Max Shimba Ministries

MAOMBI YA KUPINGA MAGONJWA, VIFO, AJALI NA UHARIBIFU KATIKA MAISHA YAKO

1. Baba, katika jina la Yesu, naangusha kila mbinu za kishetani zinazozuia mafanikio yangu, katika jina la Yesu.
2. Nakataa na kupinga magonjwa ya kila aina katika nyumba yangu na familia yangu, kwa jina la Yesu.
3. Imeandikwa katika Zekaria 2:8 ya kwamba “Yeye anayenigusa mimi anagusa mboni ya jicho la Mungu”, hivyo, ninalisimamia Neno hili na kupinga kila nguvu inayosababisha magonjwa na upotevu wa fedha zangu katika jina la Yesu.
4. Nasimama kinyume na ajali na vifo katika familia yangu na ndugu zangu katika jina la Yesu.
5. Nawafunika watu wa familia yangu, kijiji changu na nje ya kijiji kwa damu ya Yesu. Ninawalinda na kuwaongoza kila mmoja kwa jina la Yesu.
6. Ninaamuru kila kinachoharibu mtaji na biashara yangu kufa mara moja katika jina la Yesu.
7. Ninaificha fedha yangu yote katika damu ya Yesu na kamwe adui hawezi kuigusa.
8. Baba, katika jina la Yesu, nasimama katika Neno kama mtoto wa Mungu niliyeketishwa mahali pa juu pamoja na Kristo, na ninatangaza kuwa mikutano ya kipepo juu ya maisha yangu na fedha yangu haitafanikiwa, katika jina la Yesu.
9. Namfunga kila anayeharibu fedha yangu nyumbani na sehemu yangu ya kazi katika jina la Yesu.
10. Wewe pepo uliyetumwa kuharibu biashara na fedha zangu, ninakufunga na kukutupa kwenye shimo la giza katika jina la Yesu.
11. Ninaamuru moto wa Roho Mtakatifu kumlamba kila mmoja aliyesimama kinyume na biashara na mafanikio yangu katika jina la Yesu.
12. Ewe mlima uharibio, ninakuangusha na nianaamuru usambaratike, katika jina la Yesu. 13. Ninaificha biashara, ofisi, fedha na miradi yangu yote katika damu ya Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliye hai. Amen.
14. Bwana, ninaomba upendeleo wako katika maisha yangu ili niweze kufanikiwa.
15. Upendeleo wako unizunguke kadiri ya Neno lako, katika jina la Yesu.
16. Bwana, naomba kuunganishwa na watu watakaonisaidia kufikia ndoto zangu kwa jina la Yesu.
17. Oh, Bwana, naomba ufanye njia kwa ajili yangu hata pale pasipo na njia katika jina la Yesu.
18. Baba, naomba niunganishe na mtu ambaye atakuwa msaada mkubwa katika kuyafikia mafanikio yangu katika jina la Yesu. 19. Baba ninaamini ya kwamba kila ninapokanyaga ninapamiliki sawasawa na na Neno lako, hivyo naomba univike vazi lako la upendeleo katika jina la Yesu.
20. Asante Bwana Yesu kwa kuwa umefanya sawasawa na nilivyokuomba katika jina la Yesu.
Amen.

BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds

  BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds. The targets included a Radwan Force training facility used for weapons drills ...

TRENDING NOW