Wednesday, February 10, 2016

JE, NI HAKI KWA MKRISTO KUSALI (KUOMBA) JUMAPILI?

(SEHEMU YA PILI)

Ndugu msomaji:

Katika ujumbe wa leo, nitawaletea ushahidi mbali mbali unao sema na au mruhumsu Mkristo kusali Jumapili kama ulivyo wekwa na shahidiwa katika Agano Jipya.

Ushahidi wa kubadilika kwa siku ya kusali unaweza kuuona mapema sana katika Agano Jipya. Agano Jipya lina ushahid mwingi sana ambao unasema kuwa SIKU YA SABATO haina nguvu tena na au si Sheria tena kusali Siku ya Saba ya Wiki.


SIKU ZOTE NI ZA BWANA MUNGU
Warumi 14: 5-6 inasema: 5 Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.
6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu.

Ni vyema kuisoma Sura nzima ya Warumi 14, ingawa kuna ushahid mkubwa kuanzia aya ya 1 mpaka ya 12. Hata hivyo, maelekezo hapa ni kwa mtu binafsi kuamua katika akili yake ni siku ipi aitunze na au aitumie kusali na kumwabudu Bwana Mungu. Kwasabau hiyo, basi chaguo ni la Mtu na sio Mungu.


SABATO IMESEMWA NI KIVULI. YESU NDIE SABATO
Wakolosai 2: 16-17 inasema: 16 Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.

Angalia kwa makini hapa jinsi siku zilivyo orodheshwa. Sikukuu huwa ni ya Kimwaka, Mwandamo wa Mwezi ni ya Kimwezi, Sabato ni ya Kiwiki. Hakuna mwenye ruhusa ya kuhukumu katika hili. Sabato imesemwa ni KIVULI. Ukweli kamili ni Yesu. Yesu ndie Sabato yetu.


WALIKUTANA SIKU YA KWANZA YA JUMA
Matendo ya Mitume 20 aya 7 Inasema: 7 Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.

Siku ya Kwanza ya Juma ni Jumapili, na hii ni siku ambayo watu walikusanyika na Kumwabudu Bwana Mungu. Hivyo basi, hii aya inaweza kuonyesha kuwa Kanisa lilikutana/kusanyika siku ya Jumapili.

Katika mkusanyiko huu, kuna mambo Mawili Muhimu sana yalifanyika:
1. Walimeka Mkate -Kula Meza ya Bwana. [Communion]
2. Walisoma Neno.

Zaidi ya hapo, Luka hakutumia njia ya Kiyahudi katika kuhesabu siku, yaani kutua kwa jua mpaka kutua kwa jua. Luka alitumia njia ya Kirumi ambayo siku inaanza Saa Sita ya Usiku. [midnight to midnight.] Huu ni ushahidi tosha kuwa Luka hakutumia na au hesabu siku kwa kutumia Njia ya Kiyahudi ya kuhesabu Sabato.


PAULO ANALIAMBIA KANISA LIKUTANE SIKU YA KWANZA YA JUMA
1 Wakorintho 16: 1-2 inasema: 1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo.
2 Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;

Ona hapa Mtume Paulo analiambia Kanisa likutane siku ya kwanza ya Juma ambayo ni Jumapili na aliwataka waweke akiba katika siku hiyo ya kwanza ya Juma.

Hivyo basi, siku ambayo Kanisa liliambiwa likutane ni Jumapili. Je, hii ni siku ya kisheria ya Mkristo kukutana? Jibu ni lako na uchaguzi ni wako.


YOHANA ALIKUWA KATIKA ROHO SIKU YA BWANA
Ufunuo 1 :10-11 inasema: 10 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu,
11 ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia.

Katika Kamusi ya Biblia kuhsu "SIKU YA BWANA" katika Ufunuo 1:10. hii ni tukui la kwanza katika maandishi ya Kikristo kuwa watu wakuna siku ya kwanza τῇ κυριακῇ ἡμέρᾳ, "ta kuriaka hamera." Hii ni uthibitisho kuwa, ilikuwa ni desturi ya Wakristo kukutana katika siku hio. Vile vile, ushahid huu uliweza kuoneka katika Karne ya Pili, Soma (Ignatius, Epistle to the Magnesians, 1. 67).


Katika Makanisa mengi sana ya leo" SIKU YA BWANA" inafahamika kuwa ni Jumapili kama ilivyo kuwa tokea Karne ya Pili

Nategemea huu ushahid unatosha kukuambia kuwa Biblia hamlazimishi mtu kusali siku ya Jumamosi. Kma unashida ya aya angalau moja basi Warumi 14 aya ya 1-12 imetupa haki ya kuchagua siku ya kumwabudu Bwana Mungu ambayo inaweza kuwa Jumatau, Jumanne, Tuma Tano, Alahamisi, Ijumaa, Jumamosi au JUMAPILI. Zote hizo ni siku za Bwana.

Na hakuna mwenye haki ya kukuhukumu unapo amua kusali Jumatatu au siku yoyote ile. Soma Warumi 6 aya 14. KUMBUKA TUPO HURU KATIKA KRISTO.

Hivyo basi, leo nimewapa ushahid kadhaa kuhusu siku halali ya kuwambudu Bwana Mungu. SIKU ZOTE NI ZA BWANA.

Mungu awabariki sana,

Max Shimba

For Max Shimba Ministries Org

MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED

Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Tuesday, February 9, 2016

UTAFITI: BIBLIA NDIO KITABU BORA NA KINACHO SOMWA SANA KULIKO VYOTE DUNIANI


Mtafiti James Chapman ameweka kumi bora ya vitabu vinavyo somwa sana duniani. Kwa taarifa yako, Biblia ndio kitabu kinacho ongoza kusomwa kuliko vitabu vyote hapa duniani. Quran HAIPO hata kwenye 20 bora.

Zaidi ya hapo, Biblia ndio kitabu kilicho chapishwa sana katika kipindi cha miaka 50 iliyo pita.

Biblia inaongoza kwa kuwa na nakala zaidi ya Bilioni 4 zilizo chapishwa katika kipindi cha miaka 50.

Ikifuatiwa na kitabu cha "Works of Mao Tse-tung" chenye nakala Milioni 820. Kitabu cha Harry Potter nakala millioni 400, The lord of the Rings trilogy nakala milioni 103 na kitabu cha Paulo Coelho's the Alchemist chenye nakala millioni 65.

Sunday, February 7, 2016

JE, MUHAMMAD AU JIBRIL NI ROHO YA KWELI/ROHO MTAKATIFU?

Leo nitawajibu Waislam wote duniani kwa kutumia Biblia Takatifu kuwa Muhammad hakuwa Roho ya Kweli kama alivyo ahidiwa na Yesu Kristo ambaye ni Bwana na Mwokozi wetu.

Mara nyingi Waislam wanauliza, "Roho ya Kweli ni nani ambaye Yesu alimuhadi katika Yohana 16 aya ya 12 mpaka 14.
Nimekuwa nikiwauliza Waislam, hivi wao wanafikiri huyu Roho wa Kweli ni nani? Na wakanijibu kuwa huyo Roho wa Kweli ni Malaika Jibril.

Yohana 16:13 inasema: Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Zaidi ya hapo, Waislam wengi wanadai kuwa, Yesu alikuwa anamtabiri Muhammad, na wakati huo huo, wengine wanasema kuwa alikuwa anatabiriwa Jibril. KINYUME CHAKE, kama ilivyo shahidiwa katika Yohana 16 aya 13, Yesu alikuwa anamzungumzia Roho Mtakatifu. Tunafahamu hili kwasababu Yesu anamzungunzia Roho ambaye atawaongoza Wanafunzi wake kuanzia wakati huo na sio miaka mamia baadae.

Ukiisoma Biblia kwa makini kuanzia Yohana 16 aya ya 5 mpaka 15 utagundua hapo hapo kuwa Waislam wote pamoja na Allah wao ni waongo.

Lakini, kuna njia nyingi tunaweza kuzitumia kufahamu kama Waislam wako sahihi katika ufafanuzi wao kwa kuangalia na au soma kila wakati Yesu alipo sema "ROHO" katika Injili hiyo hiyo ya Yohana na tuone kama kweli alikuwa anamtabiri Muhammad wa Waislam katika aya mojawapo.

UTHIBITISHO WA KWANZA:
Yohana 1 aya ya 32 inasema: Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake "YESU".

Wote tunafahamu kuwa Muhammad hakuwa Mtakatifu na vile vile hakuwa anapaa kama ndege na alikuja miaka 600 baada ya Kristo, hivyo basi, ni dhahiri kuwa Roho Mtakatifu sio Muhammad ambaye alikuja miaka 600 baadae. Yohana hakuwai mwona Muhammad.

UTHIBITISHO WA PILI:
Yohana 1:33, [ Yohana Mbatizaji anaendelea kusema] "Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu."

Yohana anaweka kiuwazi zaidi aya hiyo hapo juu kuwa Yesu ndie atakaye kuwa anabatiza kwa Roho Mtakatifu.

Kwa kifupi Yesu atamtuma ROHO ambaye ni Mwenye Nguvu ya Mungu na ni Mungu.

Je, Muhammad ni huyo Roho? HAPANA KABISA, kwasababu Yesu aliwabatiza Wanafunzi wake na zaidi ya hapo, wafuasi wake walibatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku ya Pentekoste. Mda mchache baada ya Yesu kupaa kwenda kwa Baba yake Mbinguni, hivyo basi, na narudia tena, hii ilifanyika Miaka mia sita 600 kabla ya Muhammad kuzaliwa. Wanafunzi wa Yesu hawakubatizwa kwa kupitia Muhammad wala Waislam hawabatizi au batizwa.

UTHIBITISHO WA TATU:
Yohana 3 aya ya 5 inasema: Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

Nauhakika hakuna Muislam duniani pote anayeweza kusema kuwa Muhammad anazaa, maana katika ya hapo juu Yesu anasema Mtu lazima azaliwe kwa Roho, JE, MUHAMMAD ALIZAA/ANAZAA?

UTHIBITISHO WA NNE:
Yohona 3 aya ya 6 inasema: Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

Hapa Muhammad anatupwa nje mara moja kwasababu ya haya maneno ambayo Yesu ameyasema, kwasababu #1 Muhammad alikuwa binadamu, mbaya zaidi hivi sasa amekufa -marehemu. na #2 KwasaMbabu tena, Roho inazaa kwa kutumia Nguvu ya Mungu, ambaye ni Roho Mtakatifu. Huku kuzaliwa kwa Roho kulianza miaka 600 kabla ya Muhammad kuzaliwa.

UTHIBITISHO WA TANO:
Yohana 3 aya ya 8 inasema: Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho.

HAKUNA HATA MMOJA WETU ALIYE ZALIWA KUPITIA MUHAMMAD. Hivyo basi Muhammad anashindwa tena kuwa Roho ya Kweli.

UTHIBITISHO WA SITA:
Yohana 3 aya ya 34 inasema: Kwa kuwa yeye aliyetumwa na Mungu huyanena maneno ya Mungu; kwa sababu hamtoi Roho kwa kipimo.

Je, Muhamamd alikuwa hana kipimo? Hapo tena Muhammad kashindwa maana alikuwa amepimiwa maneno tu na Allah wake. Muhammad alikiri kuwa yeye hajui Mungu atamfanya nini baada ya kifo, pale alipo ulizwa na watu, je, nini kitatokea baada ya kifo. Muhammad hakuwa "omniscient".


UTHIBITISHO WA SABA:
Yohana 4 aya ya 24 inasema: Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Mungu sio Muhammad, asante Mungu, kwa kuweka huu ukweli kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu. Kumbe hata Jibril sio Roho Mtakatifu.

UTHIBITISHO WA NANE:
Yohana 6 aya ya 63 inasema: Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.

Muhammad hawezi kutoa uzima wa milele, ni kitu ambacho Mungu peke yake anaweza kukupa. Ndio maana tunajua kuwa Yesu ni Mungu, kwasababu, Yesu anatoa uzima wa Milele kwa wale wote wamwaminio.

UTHIBITISHO WA TISA:
Yohana 7 aya ya 39 inasema: Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.

Je, Muhammad atapewa kwa kila mtu ambaye anamwamini Yesu? HAPANA KABISA, Quran inasema kuwa Ukimwanini Mwamad/Allah basi umemwamini Allah. Hivyo Muhammad hawezi kuwa Roho ya Kweli, maana tunao Mwamini Yesu tumepewa Roho Mtakatifu na sio Muhammad ambaye amesha kufa.

UTHIBITISHO WA KUMI:
Yohana 14 aya ya 16,17, na 18 inasema: 16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; 17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.
18 Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.

Hizi aya zinapendwa sana na Waislam na wanapenda kuzitumia kama ushahidi wao. Je, Muhammad aliishi na Mitume wa Yesu katika karne/Century ya kwanza? HAPANA KABISA TENA KABISA. Muhammad hakuwepo wakati wa karne/Century ya kwanza pale Wafuasi wa Yesu walipo pewa huyo Roho Mtakatifu. Yesu alisema kwa Wanafunzi wake kuwa hata waacha YATIMA, Je, iweje Muhammad aliye kuja miaka 600 baadae awe na Wanafunzi wa Yesu katika karne/Century ya Kwanza?

UTHIBITISHO WA KUMI NA MOJA:
Yohana 14 aya ya 26. Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.

Hii aya Waislam hawaipendi kabisaa, kwasababu Yesu anasema KIUWAZI KABISA KUWA, ni nani huyu WAKILI wetu, NI WATATU KATIKA MUUNGANO MTAKATIFU. Huyu Roho Mtakatifu ana adhama zote za Baba na Mwana, HIVYO BASI, Muhammad tena ameshindwa vibaya sana hapa. Muhammad alikuwa Mtenda dhambi, huku Yesu hakuwai tenda dhambi hata moja.

UTHIBITISHO WA KUMI NA MBILI:
Yohana 15 aya ya 26 inasema: Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia.

Kwa mara nyingine tena, hii ndio raha ya kufundisha katika context yake. Tumesoma katika aya hapo juu kuwa Yesu alisema nani ni Msaidizi wetu, na kwa undani zaidi, HAPA KWENYE HII AYA YA 26 Yesu anasema kuwa huyo Msaidizi ni Roho Mtakatifu.
Je, Muhammad aliishi wakati wa Mitume wa Yesu na kuwa msaidizi wao, HAPANA KABISA, inafahamika kuwa Muhammad alikuja miaka 600 baadae.

UTHIBITISHO WA KUMI NA TATU:
Yohana 16 aya ya 13 inasema: Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Muhammad tena ameshindwa hapa, maana hakunena na wala hakuwai sikia kutoka kwa Mungu, Yehova, bali kwa Jibril ambaye anadai kuwa alitumwa na Allah. Zaidi ya hapo, Muhammad hakutoa utabiri wa mambo yatakayo kuja. MUHAMMAD AMESHINDWA TENA KWA MARA YA KUMI NA TATU.

UTHIBITISHO WA KUMI NA NNE:
Yohana 16 aya ya 15 inasema: Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari.

Yesu anasema kuwa yote ya Baba ni yangu, je, binadamu wa kawaida anaweza kudai kuwa kila kitu cha Mungu Baba ni chake? Hakika Yesu ni Mungu. ZAIDI YA HAPO, Yesu anasema kuwa huyo Roho Mtakatifu atatufundisha kuhusu YEYE/Yesu, wakati inafahamika kuwa Muhammad hakuwai fundisha kuhusu Yesu na wala Muhammad hakuwai sema kuwa Yesu ana Baba. Kumbe basi Roho Mtakatifu hawezi kuwa Jibril au Muislam bali ni Mungu mwenye adhama zote za Baba na Mwana.

UTHIBITISHO WA KUMI NA TANO:
YESU ANAWAPA ROHO MTAKATIFU WANAFUNZI WAKE
Yohana 20 aya ya 21 na 22 inasema: 21 Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. 22 Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.

AYA HAPO JUU IPO WAZI kabisa kuwa YESU ALIWAPA ROHO MTAKATIFU WANAFUNZI WAKE NA HAKUWAPA MUHAMMAD AMBAYE alikuwa bado HAJAZALIWA.

Hivyo basi, leo nimetoa USHAHIDI ZAIDI YA KUMI NA TAKO KUTOKA INJILI YOAHANA kuwa Muhammad hakuwa Roho ya Kweli, zaidi ya hapo, Jibril hakuwa Roho ya kweli.

LEO NIMEJIBU KUHUSU ROHO WA KWELI AMBAYE YESU ALIKUWA ANAMSEMA kwa kutumia Aya hizo hizo ambazo Yesu alizitumia kumzungumzia huyo Roho wa Kweli.

Katika huduma yake,

Max Shimba,

Max Shimba Ministries 2013
December 26, 2013
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Saturday, February 6, 2016

ALLAH WA WAISLAM AKIRI KUWA YEYE SIO BABA BALI NI BWANA MWENYE WATWANA

1. Uislam ni dini ya yatima na Watwana.
2. Ukristo ni imani pekee yenye Mungu Baba na Wakristo ni watoto wa Mungu.


MUHAMMAD ANASEMA KUWA ALLAH SIO BABA
Surat Al Maida 18. Na Mayahudi na Wakristo wanasema: Sisi ni wana wa Mwenyezi Mungu na vipenzi vyake. Sema: Basi kwa nini anakuadhibuni kwa ajili ya dhambi zenu? Bali nyinyi ni watu tu kama wale wengine alio waumba. Humsamehe amtakaye na humuadhibu amtakaye. Na ni wa Mwenyezi Mungu tu ufalme wa mbingu na ardhi. Na marejeo ni kwake Yeye.

Kama aya inavyo sema hapo juu, Muhamma na Allah wanakana kuwa Wakristo na Wayahudi sio watoto wa Mungu, eti kwasababu ya Allah kuto kuwa na mwana bila ya Mke. Hii aya inapingana na Biblia ambayo inasema kuwa sisi ni watoto wa Mungu.


WAKRISTO NI WATOTO WA MUNGU
Waebrania 12: 7 Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? 8 Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. 9 Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi? 10 Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.

Yeremia 31:
18 Hakika nimemsikia Efraimu, akijililia hivi, Umeniadhibu, nami nikaadhibika, kama ndama asiyeizoelea nira; unigeuze, nami nitageuzwa; kwa maana wewe u Bwana, Mungu wangu.
19 Hakika baada ya kugeuzwa kwangu, nalitubu; na baada ya kufundishwa kwangu, nalijipiga pajani; nalitahayarika, naam, nalifadhaika, kwa sababu naliichukua aibu ya ujana wangu.


Muhammad alikuwa bila ya matunzo na malezi ya Baba na mama yake. Baba yake alikufa kabla ya muhammad kuzaliwa, na Mama yake alikufa alipo kuwa na miaka sita [6] . Huyu Muhammad kwanza aliishi na babu yake na kwa muda mwingi aliishi na wajomba zake. MUHAMMAD ALIKOSA MALEZI BORA YA WAZAZI WAKE NDIO MAANA ANACHUKIA SANA WAKRISTO PALE WANAPO SEMA KUWA MUNGU NI BABA YETU. Hii chuki ilimuingia kwasababu yeye alikuwa hana baba na kuanza chuki kubwa kubwa kwa Mungu.


LAKINI KATIKA BIBLIA TUNASOMA KUWA MUNGU NI BABA YETU:
Kumbukumbu la Torati 32: 6........Je! Yeye siye Baba yako aliyekununua? Amekufanya, na kukuweka imara.

Zaburi 2: 7 Nitaihubiri amri; Bwana aliniambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.

Isaya 63: 16 Maana wewe ndiwe Baba yetu, ijapokuwa Ibrahimu hatujui, wala Israeli hatukiri; wewe, Bwana, ndiwe Baba yetu, mkombozi wetu tangu milele ndilo jina lako.

Mathayo 6: 9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

Yohana 20: 17 Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu.

UISLAM HAUNA BABA, BALI UNA BWANA MWENYE WATWANA. Ngoja nitumbue jipu, Allah ambaye ni mungu wa Waislam SIO YEHOVA ambaye ni Mungu wa Wakristo. Allah yeye ni dhaifu, duni, na yupo chini ya YEHOVAH ambaye ni Mungu Mkuu.

Allah sio baba bali ni roho dhaifu ambayo ipo chini na duni kwa YEHOVAH, ndio maana Allah anapenda WATWANA na kuwafanya Wiaslam wote kuwa ni WATUMWA WAKE - Muslims are SLAVES OF ALLAH.

SASABU inayo mfanya Allah kushindwa kuwapenda binadamu ni jibu tosha kuwa Allah hakuumba binadamu na ndio maana amejaa chuki kubwa kubwa kwa bianadamu. ZAIDI YA HAPO, Allah yeye ni BWANA MWENYE WATWANA.


WAISLAM NI WATUMWA WA ALLAH - SLAVES OF ALLAH
Surat Azzumar 10. Sema: Enyi waja wangu mlio amini! Mcheni Mola wenu Mlezi. Wale wafanyao wema katika dunia hii watapata wema. Na ardhi ya Mwenyezi Mungu ni kunjufu. Hakika wenye subira watapewa ujira wao bila ya hisabu.

Surat Azzumar 36. Je! Mwenyezi Mungu si wa kumtosheleza mja wake? Na ati wanakutishia kwa hao wenginewe wasio kuwa Yeye! Na aliye hukumiwa na Mwenyezi Mungu kupotea hana wa kumwongoa.

Aya hapo juu zinakiri kuwa Allah yeye anawatumwa na ni tofauti na Yehovah wa kwenye Biblia ambaye yeye anatuita sisi ni watoto wake.

Hii roho mbaya iliyomtisha na kumbana mbavu Muhammad, ipo kwa ajili ya kufanyiwa kazi, ndio maana Waislam wao wanapigana kwa ajili ya Allah. Allah hana upendo zaidi ya chuki.

ALLAH YEYE ANAPENDA WATU WANAO PIGANA KWA AJILI YAKE TU.
Surat Assaf 4. Kwa hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wanao pigana katika Njia yake kwa safu kama jengo lilio kamatana. Maelezo

Surat An Nisaai 74. Basi nawapigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanao uza uhai wa dunia kwa Akhera. Na anaye pigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu kisha akauliwa au akashinda basi tutakuja mpa ujira mkubwa.
75. Na mna nini msipigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu na ya wale wanao onewa, wanaume na wanawake na watoto, ambao husema: Mola Mlezi wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhaalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi anaye toka kwako, na tujaalie tuwe na wa kutunusuru anaye toka kwako. Maelezo
76. Walio amini wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na walio kufuru wanapiana katika njia ya upotofu. Basi piganeni na marafiki wa Shet'ani. Hakika hila za Shet'ani ni dhaifu

Hivi Mungu gani huyu anaye penda kuwachinganisha watu? Hakika Allah ahakuumba ndio maana yeye hapendi watu na amewaitwa WATWANA huku yeye akiwa ni BWANA wao. HUU NI MSIBA MKUBWA SANA.


SOMA BIBLIA YENYE UPENDO:

MWENYEZI MUNGU ANAKUPENDA, NAYE ANATAKA KUKUPANGIA MPANGO WA AJABU KWA MAISHA YAKO.
UPENDO WA MUNGU
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:16

MPANGO WA MUNGU KWAKO
Mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. Yohana 10:10

Warumi 5:8 Bali Mungu aonyesha pendo Lake Yeye Mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.

Kulingana na Warumi 5:8, Mungu alionyesha pendo Lake kwetu sisi kwa njia ya mauti ya Mwanawe. Kwa nini ilimpasa Kristo kutufia? Kwa sababu Andiko la tangaza watu wote kuwa wafanya dhambi. Kufanya "dhambi" kuna maanisha kukosa alama. Biblia inatangaza "wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu (utakatifu mkamilifu) wa Mungu" (Rum. 3:23). Katika maneno mengine, dhambi zetu zatufarikisha sisi na Mungu wetu aliye utakatifu mkamilifu (haki na kweli) na kwa hivyo sharti Mungu awahukumu watenda dhambi.

Ndugu msomaji,

Nakukaribishga sana kwa Mungu wa Wakristo ambaye anakupenda sana. Njoo huku kwa Yesu ili upate uzima wa milele. Njoo kwa Yesu ili upate upendo wa Mungu. Ndugu uansubiri nini?

Mungu awabariki sana na Yesu anakupenda,

Max Shimba Ministries Org

MATOLEO 20 TOFAUTI YA QURAN ::::::::20 VERSIONS OF QURAN::::::::::

Je, Kati ya haya Matolea 20 (Ishirini) ya Quran, toleo lipi ni la kweli?
Je, Nabii wa Allah ajulikanaye kwa jina la Muhammad, alisoma toleo lipi?

Ndugu msomaji,
Leo nitaweka ukweli kuhusu Quran ambayo ina Matoleo 20 na kati ya hayo Ishirini (20) Matoleo 7 (Saba) yametajwa katika Hadith Mwaminifu za Muhammad.
Hapa chini ni Wasomaji Saba (7) ambao wote wana Matoleo Mawili mawili. Hawa Wasomaji saba wanapatikana hapa:
Nafi (from Medina; d.169/785)
Ibn Kathir (from Mecca; d.119/737)
Abu `Amr al-'Ala' (from Damascus; d.53/770)
Ibn `Amir (from Basra; d.118/736)
Hamzah (from Kufah; d.156/772)
al-Qisa'i (from Kufah; d.189/804)
Abu Bakr `Asim (from Kufah; d.158/778)
WASOMAJI SABA NA MATOLEO YAO YA QURAN
1. Msomaji : Nafi`
MATOLEO YAKE
Warsh
Qalun
2. Msomaji: Ibn Kathir
MATOLEO YAKE
al-Bazzi
Qunbul
3. Msomaji: Abu `Amr al-'Ala'
MATOLEO YAKE
Al-Duri
al-Suri
4. Msomaji: Ibn `Amir
MATOLEO YAKE
Hisham
Ibn Dhakwan
5. Msomaji: Hamzah
MATOLEO YAKE
Khalaf
Khallad
6. Msomaji: al-Qisa'i
MATOLEO YAKE
al-Duri
Abu'l-Harith
7. Msomaji: Abu Bakr `Asim
MATOLEO YAKE
Hafs
Ibn `Ayyash
HAWA NI WASOMAJI WENGI WATATU NA MATOLEA YAO MAWILI KILA MMOJA
"The Three" readers
1. Msomaji: Abu Ja`far
MATOLEO YAKE
Ibn Wardan
Ibn Jamaz
2. Msomaji: Ya`qub al-Hashimi
MATOLEO YAKE
Ruways
Rawh
3. Msomaji: Khalaf al-Bazzar
MATOLEO YAKE
Ishaq
Idris al-Haddad
Wadhalimu wa dini ya Kiislamu wanakiri kuwa kuna WASOMAJI wengi zaidi, lakini wanasema kuwa hawa walio tajwa hapo juu ndio thabit na sahihi. Kumbe basi kuna VERSIONS ISHIRINI ZA QURAN !!!!!!
SASA MASWALI YAKUJIULIZA NI HAYA:
1. Kati ya hao wasomaji wakurani, ni yupi yupo sahihi?
2. Kama Allah ndie aliteremsha Quran kwa Muhammad, kivipi awe na wasomaji wengine na kumsahahu Muhammad mtume wake kipenzi?
3. Kama Quran ni moja na ipo kwa Kiarabu tu, kivipi isomeke kitofauti kwa mara ISHIRINI [20] katika lugha hiyo hiyo ya Allah?
4. Je, Kati ya haya Matolea 20 (Ishirini) ya Quran, toleo lipi ni la kweli?
5. Je, Nabii wa Allah ajulikanaye kwa jina la Muhammad, alisoma toleo lipi?
Ndugu msomaji, leo tumejifunza kuwa katika Uislam kuna siri nyingi sana ambazo zimefichwa na wanaona aibu kusema ukweli kuwa QURAN INA MATOLEO/VERSIONS 20. HUU NI MSIBA KWA ALLAH NA MTUME WAKE MUHAMMAD.
Mungu awabariki sana na kuendelea kuwafungua macho.
Katika huduma yake
Max Shimba Ministries Org.

Friday, February 5, 2016

MAOMBI YA KUSAMBARATISHA UCHAWI NA NGUVU ZA GIZA

Baba katika Jina la Yesu.
Laana zote nilizo tupiwa na wabaya wangu zimeshindwa kwa jina la Yesu na nazivunja na kuzisambaratisha kwa Damu ya Yesu.
Mshindwe wote mnao tuma laana kwangu katika Jina la La Yesu.
Nawavunja na kuwaharibu na kuwakatakata Wachawi wote kwa damu ya Yesu.
Nasambaratisha kila neno la uovu lililosemwa juu yangu na famila yangu katika jina la Yesu.
Naharibu na kuisambaratisha madhabahu yenu mliyo fanyia kafara kwa damu ya Yesu.
Navunjavunja na kubomoa kila uovu na uchawi mnaonifanyia katika jina la Yesu.
Nairudisha misukule yote na majini yote yawarudie nyie na kuwalipa dhambi zote mnazo fanya katika jina la Yesu.
Naharibu kila uchawi, kila urogi, kila ndumba kila aina ya uovu ambao mnaufanya ili uniumize mimi na familia yangu katika jina la Yesu.
Nawateketeza kupitia damu ya Yesu Wachawi wote walio tumiwa kunitumia uchawi katika jina la Yesu.
Nawateketeza na kuwaharibu majini yote yaliyo tumwa kuja kufanya kazi hiyo waliyo tumwa na Wachawi katika jina la Yesu.
Nawateketeza na kuwauwa Makuhani wote ambao walienda kunishitaki kwa Wachawi ili waniharibie maisha, nawateketeza kupitia damu ya Yesu. Nawachoma kwa Moto wa Roho Mtakatifu katika Jina la Yesu.
Nateketeza aina zote za vyombo vya kichawi vilivyo tumiwa kuja kunichunguza katika jina la Yesu.
Naharibu fikra zao zote ambazo wanazitumia kufanya kazi zao za kichawi katika jina la Yesu.
Nafuta kumbukumbu zoote zangu ambazo wamewapa Mashetani, Majini, Roho chafu, nafuta hizo kumbukumbu kwa kutumia damu ya Yesu, katika jina la Yesu aliye hai.
Nawateketeza waweka kumbukumbu wa kimashetani kupitia damu ya Yesu aliye hai. Naharaibu na kuchoma kupitia moto wa Roho Mtakatifu makabrasha yote yenye kumbukumbu zangu katika jina la Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuharibu maisha yangu na ubomoa kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuniua nauvunja na kuuteketeza kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanywa ili kuja kuiba mali zangu, nauvunja na kuubomoa na kuuharibu kupitia damu ya Yesu.
Kila uchawi ulio fanya kuja kuniharibia familia yangu, nausambaratisha na kuuvunja na kuubomoa katika jina la Yesu.
Kila neno la kichawi lililo tumwa ili kuja kuniharibia, kunidhihaki, kunitendea mabaya nalirudisha kwa aliye lituma katika jina la Yesu.
Kila uovu, uchawi, wanga, ndumba, ramli, yaliyo tumwa kuja kwangu navunja yote hayo kupitia damu ya Yesu na katika Jina la Yesu.
Nyota yangu ambayo wanaita nairudisha kupitia damu ya Yesu. Nyota yangu ya baraka nailinda na kuzungushia na kuizingira na damu ya Mwana Kondoo katika jina la Yesu.
Namteketeza yule mtu aliye kuja kuiba nyota yangu katika jina la Yesu.
Nateketeza mbinu zote wanazo tumia ili kuja kuiba nyota yangu katika jina la Yesu.
Nateketeza wivu wao, chuki yao, laana zao, maovu yao na kila aina ya uchafu ambao wanao kwa ajili yangu katika jina la Yesu.
Naizungushia na kuizingira nyumba yangu na damu ya Yesu.
Naishungushia na kuizingira familia yangu na damu ya Yesu.
Nashungushia na kuzingira maisha yangu yote na damu ya Yesu.
Navunja laana zote zilizo semwa na mabau zangu katika jina la Yesu.
Navunja laana zato ambazo zilisemwa bila ya mimi kufahamu, nazivunja na kuziharibu kupitia damu ya Yesu na katika jina la Yesu.
Narudisha kila mali walizo ziiba kutoka kwangu katika jina la Yesu.
Narudisha kila baraka walizo ziiba kwangu katika jina la Yesu.
Narudisha amani na upendo katika familia yangu.
Damu ya Yesu ipo juu ya Maisha yangu na inasafisha kila uovu, kila uchawi unaaribiwa na damu ya Yesu katika jina la Yesu.
Leo hii mtaiona Nguvu iliyopo katika damu ya Yesu.
Katika Jina la Yesu aliye hai ninaomba.
Amen
Max Shimba Ministries
03/01/2014

Kwanini Mkristo anauhakika wa kwenda Paradiso zaidi ya Muislamu?

1. Je, Kurani inatoa uhakika kwa Waislamu?
Kurani inatengeneza tu mazingira ya mashaka kuhusiana na kuingia Paradiso au hapana. Muislamu hanauhakika wa kuiepuka jehanamu ya moto:
“Hao wanao waomba, wao wenyewe wanatafuta njia ya kwendea kwa Mola wao Mlezi - hata miongoni mwao walio karibu mno - na wanataraji rehema zake na wanaikhofu adhabu yake. Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi yafaa kutahadhari nayo” (Kurani 17:57).
Waislamu hufikiria kwamba hawawezi kuwa na uhakika kuhusiana na kwenda Paradiso, kwa sababu Kurani inasema Mola huamua na mwanadamu hawezi kujua kwamba ameokoka:
"Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? Ni Moto mkali!" (Kurani 101:6-11).
Muislamu hana uhakika ni upande gani anaohusika nao. Mola alimuumba mwanadamu kufanya wema au uovu:
"Hujui ya kwamba Mwenyezi Mungu anao ufalme wa mbingu na ardhi? Humuadhibu amtakaye, na humsamehe amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu." (Kurani 5:40).
Muislamu hajui ni nani atakuwa pamoja na Mola Paradiso. Kwa hiyo Kurani haiwezi kutoa uhakika kwa Muislamu kuhusiana na kwenda Paradiso.
2. Je, Muhammad anatoa uhakika kwa Waislamu?Kurani iko wazi kwamba Muhammad hawezi kumsaidia Muislamu kuingia Paradiso:
"Wala nasaha yangu haikufaini kitu nikitaka kukunasihini, ikiwa Mwenyezi Mungu anataka kukuachieni mpotee. Yeye ndiye Mola wenu Mlezi; na kwake mtarejeshwa" (Kurani 11:34).
"Hata ukiwa na pupa ya kutaka kuwaongoa, lakini Mwenyezi Mungu hamwongoi yule anaye shikilia kupotea. Wala hawatapata wa kuwanusuru" (Kurani 16:37).
"Sema: Uombezi wote uko kwa Mwenyezi Mungu. Ni wake Yeye tu ufalme wa mbingu na ardhi. Kisha mtarejeshwa kwake." (Kurani 39:44).
Kwa hiyo Kurani inakataa kwamba Muhammad aweza kuwa muwezeshaji kwa Muislamu kuingia Paradiso. Angalia pia Kurani 7:188, 4:123 na 9:80. Hivyo ni nini faida yake, ikiwa kila mwanadamu atateseka jehanamu, kabla ya wenye haki kuchaguliwa kutoka hao waendao jehanamu?
Je ni nini basi kwa habari ya Muhammad kuwa mfano kwa Waislamu kuingia Paradiso? Pia hili nalo halina mbadala kwa Muislamu, kwa sababu Muhammad aliona shaka kuhusu kuingia Paradiso:
“Sema: Mimi si kiroja miongoni mwa Mitume. Wala sijui nitakavyo fanywa wala nyinyi. Mimi nafuata niliyo funuliwa tu kwa Wahyi, wala mimi si chochote ila ni mwonyaji mwenye kudhihirisha wazi." (Kurani 46:9).
Pia nyaraka zingine katika uislamu zinasema kwamba Muhammad hakuwa na uhakika wa kwenda Paradiso [1].
3. Are Christians sure about going to Paradise?Wakati Waislamu wanajaribu kutii sheria za Mola, wanabaki kutokuwa na uhakika wa wokovu, Mkristo anauhakika wa kwenda Paradiso. Mkristo atamjibu Muislamu juu ya swali “Bwana zangu, nifanye nini ili nipate kuokoka?” kwa [2]:
“Mwamini Bwana Yesu Kristo, nawe utaokoka” (Matendo ya Mitume 16:31).
Ni lazima Muislamu afahamu kuokoka kwa upendo na neema ya Mungu. Uislamu hauna Mwokozi. Mwamini ndani ya Mwokozi Mkuu Yesu Kristo wakati wote anakuwa na uhakika wa kwenda Paradiso. Wokovu wa pekee kwa mwanadamu umetolewa kupitia Yesu Kristo, Neno la Mungu. Kwa sadaka ya mwenye haki Yesu Kristo kwa ajili ya msamaha wa dhambi, mwamini ana uhakika wa kuingia Paradiso. Kuna mistari kadhaa kwenye Maandiko Matakatifu yanayothibitisha kuingia Paradiso kwa waaminikwenye utukufu wa Yesu Kristo:
“Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye Mimi hata akifa atakuwa anaishi” (Yohana 11:25).
"Nyumbani mwa Baba yangu kuna makao mengi. Kama sivyo, ningeliwaambia. Nakwenda kuwaandalia makao. Nami nikienda na kuwaandalia makao, nitarudi tena na kuwachukua mkae pamoja nami, ili mahali nilipo, nanyi mpate kuwepo. Ninyi mnajua njia ya kufika ninakokwenda.Thomasi akamwambia, “Bwana, sisi hatujui unakokwenda, tutaijuaje njia?" Yesu akawaambia, “Mimi ndimi njia na kweli na uzima. Mtu hawezi kuja kwa Baba isipokuwa kwa kupitia Kwangu" (Yohana 14:2-6).
4. HitimishoMkristo ana uhakika wa kwenda Paradiso. Muislamu huishi na kufa, hana uhakika wa wokovu. Mkristo, kwa upande mwingine, amemkubali Yesu Kristo kwa ajili ya msamaha wa dhambi zake na ana uhakika. Hii ni habari njema kuhusu upendo na neema ya Mungu ni kitu ambacho Mkristo anataka kuwashirikisha rafiki zake wailslamu.
Rejea:
1. Sahih al-Bukhari, Volume 4, Book 51 and Volume 5, Book 58, Number 266.
2. E.M. Hicham, How Shall They Hear? Sharing your Christian faith with Muslims, Ambassador Publications, Belfast, 2009, 88.

SIFA SABA ZA ROHO MTAKATIFU

Yohana 14: 16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine akae nanyi milele. 17Huyo ndiye Roho wa kweli ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa sababu haumwoni wala haumjui. Ninyi mnamjua kwa kuwa yuko pamoja nanyi naye anakaa ndani yenu.

Yesu Kristo ametupa zawadi ya ajabu sana: Zawadi ya Roho Mtakatifu. Katika baadhi ya maeneo, zawadi hiyo inajulikana kama Roho Mtakatifu, na sehemu nyingine ametajwa kama Msaidizi (Msaidizi na Roho Mtakatifu). Roho Mtakatifu ni sehemu ya tatu ya Uungu, sehemu ya tatu ya Utatu wa Mungu Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Yeye ni Msaidizi katumwa na Yesu, baada ya Msaidizi wetu kuja ambaye ni Roho Mtakatifu, Yesu alipaa tena mbinguni. Roho Mtakatifu hutolewa kwa wote ambao wamempokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wao

Kuna mambo saba ambayo tunahitaji kuelewa kuhusu Roho Mtakatifu. Tunajua kwamba, katika Biblia, saba ni namba ya kukamilika/ kukamilisha, au ukamilifu, na sifa saba zote tofauti za Roho Mtakatifu ni kweli kamili na kamilifu. Tunaweza kuzitegemea sifa hizi za ajabu za Roho Mtakatifu, wakati wote, katika kila hali na katika maisha yetu yote.

1. Roho Mtakatifu ni Msaidizi Mwenye Upendo. Tunapokabiliana na mateso katika maisha, mwongozo wa Roho Mtakatifu ni muhimu zaidi na ni faraja katika mioyo yetu: Roho Mtakatifu ni mtu ambaye ana upendo kwetu na anajua kila kitu kuhusu maisha yetu. Roho Mtakatifu alitupenda tangu kabla ya kuumbwa ulimwengu. Yeye alivyotupenda vizuri. Yeye anatupenda milele na anaendelea kutupenda milele yote. Roho Mtakatifu tu ndie mwenye uwezo wa kweli wa kutufariji mioyo yetu, kwa sababu hakuna mtu anaye tupenda sisi kama anavyotupenda Yeye Roho Mtakatifu.
Warumi 5: 5 wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo Lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.

2. Yeye (Roho Mtakatifu) ni Msaidizi Mwaminifu. 

ROHO MTAKATIFU NI MUNGU

Ndugu msomaji,
Watu wengi hawafahamu kuhusu Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu Ni Nani?
Baadhi ya watu wanadhani Roho Mtakatifu ni aina fulani ya nishati, uweza au radi. Lakini wanakosea.
Roho Mtakatifu Ni Mtu-Person, "SIO BINADAMU", nikimmanisha kuwa sio Mtu kwa maantiki ya Binadamu.
Na kwa kweli ni ‘mtu’ muhimu sana; ni Nafsi ya Tatu katika Utatu wa Mungu (Mt 28:19) (2Kor 13:13). Yeye ni mtu roho, kama vile wewe ulivyo ila Yeye hafungwi na mwili. Twaweza kumwomba kila siku tukisema, ‘Roho Mtakatifu, nijaze kwa uweza wako, niongoze, nipe hekima na ujasiri’ kwa sababu ni mtu kweli tunayeweza kuzungumza naye na kujihusisha naye.
Wengine wanasema kuwa ni Nguvu Fulani ya Mungu. Wengine wanasema ni Malaika Jibril. Lakini, Biblia inatumabia nini kuhusu Roho Mtakatifu?
Hebu ungana nami moja kwa moja na tujifunze kwa pamoja kwa kutumia aya za Biblia kuhusu Roho Mtakatifu. Kwa kifupi, ROHO MTAKATIFU ni Mungu.
Swala la kuwa Roho mtakatifu ni Mungu limo ndani ya aya nyingi za biblia kama vile Matendo 5:3-4. Katika ayah ii Petro anapambana na anania aliyemdanganya Roho mtakatifu na nasisitiza yakuwa “hukumdanya mtu bali Mungu.” Hili ni tangazo la wazi kwamba kumdanganya Roho mtakatifu ni kumdanganya Mungu. Tunaweza pia kujua Roho mtakatifu ni Mungu kwa kuwa ana tajwa na hali sawa na za Mungu. Roho mtakatifu yuko kila mahali katika Zaburi 139:7-8, “nitaenda wapi nijifiche na Roho? ama nitakimbilia wapi mbali na uwepo wako? Nikipanda juu mbinguni, huko uko; nikifanya malazi yangu kuzimu, tazama uko huko,” tena katika wakorintho wa Kwanza 2:10 tunaona hali yakuwepo kila mahali kwa Roho mtakatifu “Lakini Mungu ameyajulisha kwetu kupitia Roho wake mtakatifu. Kwa kuwa Roho huyachunguza mambo yote, naam, mambo ya siri ya Mungu. Kwa maana ni nani ayajuaye ya mwanadamu isipokuwa roho ya mwanadamu inayokaa ndani yake? Vivyo hivyo, hakuna ajuaye mambo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.”
Tunaweza kujua kweli kwamba Roho mtakatifu ni Mungu kwa kuwa ana akili, hisia na mapenzi yake. Roho mtakatifu hufikiri na hujua (Wakorintho wa kwanza 2:10). Roho mtakatifu anaweza kuugua (Waefeso 4:30). Roho hutuombea (Warumi 8:26-27). Roho mtakatifu hufanya maamuzi kutokana na mapenzi yake mwenyewe (Wakorintho wa kwanza 12:7-11). Roho mtakatifu ni Mungu, sehemu ya tatu ya utatu wa Mungu. Kama Mungu, Roho mtakatifu anaweza kufanya kazi ya msaidizi na mshauri kama vile Yesu kristo aliyevyoahidi kuwa atakuja kufanya (Yohana 14:16,26; 15:26).
Je, Roho Mtakatifu Ni Nafsi Halisi?
Madaktari husema kwamba nafsi halisi ni sharti iwe na akili, hiari, na hisia. Na Roho Mtakatifu tunampima kwa vigezo hivyohivyo vitatu.
Je, Roho Mtakatifu Ana Akili?
Akili ni uwezo wa kujifunza, kuelewa na kufikiri. Ndiyo, ana akili sana! (Rum 8:27) (1Kor 2:10-13).
Je, Roho Mtakatifu Ana Hiari?
Hiari inahusiana na kusudio, uchaguzi, takwa na azimio. Ndiyo, Roho Mtakatifu ana hiari yake mwenyewe na anakubaliana na Baba na Mwana (1Kor 12:11).
Je, Roho Mtakatifu Ana Hisia?
Je, ana hisia na hisia kali? Anapenda na hiyo ndiyo hisia yenye nguvu sana aliyonayo, na kuna hisia kali katika kuugua kwake awapo kwenye maombezi (Rum 15:30; 8:26,27).
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW