Tuesday, March 22, 2016

ALLAH AFANYA KOSA KUBWA LA KISAYANSI NA JIOGRAFIA KUHUSU KUTUA/ZAMA KWA JUA



Ndugu msomaji,
Zul-Qarnain na Kutua kwa Jua katika Sura 18:85-86
Je, ni kweli kuwa jua linazama katika chemichemi za maji zenye tope au giza, au Koran ina makosa, au kuna maelezo mengine? Kwanza tutaangalia maana ya wazi Sura ya 18:85-86, na kisha tutaangalia maelezo na majibu ya baadhi ya Waislam kuhusu jambo hili.
Unajimu Kidogo
Inawezekana kuwa haijulikani kwa mapana kwamba watawala wa kislam wa Abbasid, Waarabu na Waajemi waliendelea sana katika unajimu, wakizipa majina nyota nyingi, hata walinukuru na kusahihisha baadhi ya orodha za hesabu za watawala wa Misri (Ptolemy’s tables). Hata hivyo jua ni kubwa mara nyingi zaidi ya dunia nzima, na dunia husafiri ikilizunguka jua. Jua halizami katika chemichemi za maji zenye tope.
Zul-Qarnain ni Nani?
Hatuna ushahidi kama Muhammad alimwambia mtu yeyote kuwa Zul-Qarnain alikuwa nani hasa. Waislam wana mitazamo minne tofauti.
Alexander Mkuu (wa Makedoni) ni mtazamo wa Waislam wengi zaidi. Zul-Qarnain humaanisha kuwa ni "mtu mwenye pembe mbili." Kuna hadithi ya kubuniwa isemayo kuwa Alexander Mkuu alikuwa mungu na alikuwa na pembe mbili za kondoo dume zilizokuwa zinakua pembeni mwa kichwa chake. Licha ya ukweli kwamba hii haikuwa kweli (na ni tatizo kupata kofia ya vita—helimeti inayoweza kutosha), hadithi hii ilijulikana, na waislam wengi hudhani kuwa Allah katika sura ya 18 Alexander alitajwa kwa jina hili, mungu.
Koreshi I Muajemi ni mtizamo mwingine. Ufalme wake hasa ulikuwa ufalme uliohusisha makundi mawili: Wamedi na Waajemi, lakini zaidi ya hayo hakuna uthibitisho kuwa pembe mbili zinamhusu yeye.
Mfalme wa Yemeni ambaye alivaa kofia ya vita yenye pembe mbili za kondoo dume, ni mtazamo walionao baadhi ya Waislam.
Mtu asiyejulikana ni mtizamo wa nne. Hata hivyo inaonekana si vema sana kutoa maelezo juu ya watu ambao msemaji hajawahi kuyasikia.
Hitimisho: Haijalishi kuwa Zul-Qarnain alikuwa nani hasa. Kama aligundua kuwa jua hutua kwenye chemichemi za maji zenye tope, na huwa halizami kwenye chemichemi za maji zenye tope, kwa hiyo huu ni ubatili, bila kujali mtu ambaye Muhammad alimzungumzia.
Sura 18 Mawazo na Majibu

Wazo la I: Jua huzama kwenye chemichemi za maji zenye tope!
Kwa Waislam wa awali, Koran iliwafundisha kuwa jambo hili linatokea hasa. Mwanahistoria wa kiislamu wa awali al-Tabari juzuu ya 1 uk.234 anaonesha hili. Kama mfano wa pili, "[Dhu al-Qarnaiyn] alishuhudia kuzama kwa jua katika sehemu yake ya kupumzika ndani ya bwawa jeusi na tope la kunuka." Kwa mujibu wa al-Tabari juzuu ya 5 uk.173-174. Dul Qarnain [Zul Qarnain] anapatikana pia kwenye al-Tabari juzuu ya 1 uk.371.
Jambo jingine linaloingiliana na hili, dunia hukaa juu ya samaki mkubwa kwa mujibu wa al-Tabari juzuu ya 1 uk.220 (839-923 K.K.).
Wazo la 2: Jua lilionekana kwa Alexander likitua katika ziwa la Ithaca Makedonia
Wazo hili hubashiri kuwa Zul-Qarnain alikuwa Alexander, na kwamba Alexander alikuwa Muislam mzuri. Wazo hili haliendani na ukweli kwamba Alexander alikuwa na hekalu lililotengenezwa kwa ajili yake. Pia Alexander alikwenda kuteka kaskazini na magharibi mwa Ithaca ambayo ni Albania ya sasa.
Kibaya zaidi katika wazo hili, Wayunani walifanya makazi mamia ya maili magharibi mwa Ithaca ambayo ni Hispania, Sicily, n.k. za asa, miaka mia tano kabla ya Alexander. Kitu gani kingemfanya Myunani mwenye akili sana afikiri kuwa jua lilizama katika ziwa la Makedonia wakati meli za kiyunani zilikuwa zinaenda mbali zaidi magharibi mwa nchi ya Alexander? Kwa nyongeza, Tertullian katika Hoja Juu ya Nafsi [A Treatise on the Soul] sura 49 uk.227 anasema kwamba Aristotle, aliyeishi wakati ule ule, anataja shujaa kutoka kisiwa cha Sardinia mbali magharibi mwa Makedoni lakini ni kama kwenye latitudi ile ile.
Wazo la 3: "Chemichemi ya maji yenye tope" ni Bahari ya Atlantic
Bahari ya Atlantic haina tope na si nyeusi, bali ni bluu-kijani. Pia si chemichemi bali ni bahari. Jua huwa halizami katika bahari. Cha muhimu zaidi, Alexander, Koreshi I wa Uajemi na wafalme wa Yemeni hawakuwahi kwenda kwenye Bahari ya Atlantic na Sura ya 18:85-86 inasema kuwa Zul Qarnain aliona au alishuhudia hili.
Sababu yoyote kati ya hizi nne inatosha kulindoa wazo hili, hivyo basi kwa Waislam wanapendekeze hili? Hiki ndicho kiwango ambacho wanajaribu kwenda ili kuonyesha kuwa Sura ya 18:1-2 sio potofu. Ikiwa Allah [Mungu] wa uislam alikuwa na wazo hili katika Koran, na Allah alijua kuwa hili ni wazo potofu, hivyo jambo hili litakuwa uongo. Kama Allah wa uislam hakujua ukweli huu, wasingelikuwa na ufahamu na hakika wasingekuwa na uwezo wa kujua kila kitu. Kama mistari hii isingetoka kwa Allah [Mungu] wa uislam, basi Koran ingekuwa na makosa dhahiri, kwa sababu inathibitisha upotofu huu kutoka kwa Allah wakati sivyo hivyo. Bila shaka, ikiwa kweli si Allah wa uislam, na Mungu wa kweli si mwandikishi wa Koran, basi Allah wa uislamu hakusema uongo kwa sababu hayupo.
Wazo la 4: "Chemichemi ya maji yenye tope" ni Koreshi I alikoangalia Bahari Nyeusi (Black Sea)
Hata kama Koreshi I alikwenda magharibi mwa ufuko wa mashariki mwa Bahari Nyeusi (Black Sea), na jua lingeonekana vipi likitua katika Bahari Nyeusi, ikiwa alikuwa ameshaupita ufuko wa mashariki kuelekea kusini na mashariki? Hatuna ushahidi kuwa Koreshi aliwahi kusafiri kwenda ukanda unaojumuisha Georgia, Amernia, Azerbaijan, n.k. za sasa, zilizo mashariki mwa Bahari Nyeusi. Muislam angekuwa na hoja yenye udhaifu kidogo kama angesema kuwa Koreshi aliliona jua likichomoza kutoka kwenye Bahari Nyeusi, kwa sababu alivuka hadi Uyunani, lakini Koran inaongelea kuzama kwa jua. Hata hivyo Bahari Nyeusi sio chemichemi, kila mtu kuanzia wamisri na wengineo kaskazini ya mbali, walijua kuwa jua halikuzama kwenye Bahari Nyeusi.
Wazo la 5: "Chemichemi ya maji yenye tope" ni Koreshi I alikoangalia Bahari ya Aegean
Lakini Waajemi walikuwa wakiwafahamu vema Waatene, Waspartani, (asili ya Wayunani), na Wayunani wengine. Waajemi wangelijua kuwa Wayunani hawakuwa upande mwingine wa jua.
Wazo la 6: Hakika "Chemichemi ya maji yenye tope" ni mfalme wa alikoangalia Bahari Nyekundu
Wayemeni (Wasaba/Waseba) wakati wote waliwafahamu Waabisinia (Waethiopia) ng’ambo ya mto. Ikiwa walifikiri kuwa jua lilizama katika Bahari Nyekundu (Red Sea) basi Waabisinia wangelikuwa watu waliokuwa upande mwingine jua lilikokuwa.
Wazo la 7: "Chemichemi ya maji yenye tope" ni usemi wa kufananisha na kitu kingine
Ikiwa kitu hiki hakikuwa halisi, bali ni kifananishi cha kitu au vitu vingine, basi Koran imeshindwa kuelezea kuwa hakikuwa kweli, na wazo hili lilikuwa la kupotosha. Zaidi ya yote, hakuna mtu anayeweza kusema kwa hakika kuwa kitu hiki kilifananishwa ni nini hasa.
Hakuna kitu chochote kwenye Koran kinachoonyesha kuwa kitu hiki si halisi, na Waislam wengi wa awali walikichukulia kuwa kitu halisi, yaani ukweli halisi. Kwa kuzingatia kuwa walijua maana hasa ya jambo hili kutoka kwa wafuasi wa Muhammad, kwa hiyo walipotoshwa na Sura ya 18.
Wazo la 8: Muhammad alikuwa akisimulia juu ya ndoto yake
Wazo hili halimfahamu Zul-Qarnain kuwa ni nani hasa. Ikiwa Muhammad alikuwa anasimulia juu ya ndoto yake, jua lingeweza kutua popote alipotaka litue. Hata kama haifahamiki ni muhusika gani dhahania aonaye kitu kilicho potofu kabisa, na watu wanaoamini kuwa ni kitu cha kweli, atatufundishaje sisi juu ya kuiamini kweli.
Hata hivyo, ikiwa mtu atasema kuwa walimwona mtu fulani aitwaye ‘Ali akifanya kitu cha ajabu ajabu, na mamilioni ya watu wakamwamini kwa karne nyingi. Je, mtu huyo ataweza kuwa mwongo ikiwa alisahau kuwaambia watu kwamba, "ilikuwa ndoto yangu tu na sikumwona Ali akifanya hivyo kwa macho yangu."?
Hitimisho
Bila kujali kama Zul-Qarnain alikuwa Alexander Mkuu au mtu mwingine, Korani yaeleza jambo hili kama ukweli kuwa jua huzama katika chemichemi za maji yenye tope. Hata watu wa zamani miaka 1,000 kabla ya Muhammad walijua kuwa jua halikuzama upande huu wa Hispania. Wazo hili halikuwa kifananishi cha kitu kingine kwa sababu hakuna Muislam wa zamani aliyepatikana kuwa hakulichukua jambo hili kuwa halisi au kutoa maana yake kama usemi wa kufananisha na kitu kingine, na Waislam wote wa zamani waliamini kuwa Koran haikutolewa kwa ajili ya kudanganya.
Orodha ya Vitabu vya Tafsiri ya Korani
1. Arberry, Arthur J. The Koran Interpreted. Macmillian Publishing Co., Inc. 1955.
2. Dawood, N.J. The Koran. Penguin Books. 1956-1999.
3. Malik, Farooq-i-Azam. English Translation of the Meaning of AL-QUR’AN : The
Guidance for Mankind. The Institute of Islamic Knowledge. 1997
4. Pickthall, Mohammed Marmaduke. The Meaning of the Glorious Koran. Dar al-
Islamiyya (Kuwait) (no date given)
5. Rodwell, J.M. The Koran. First Edition. Ivy Books, Published by Ballantine
Books. 1993.
6. Shakir, M.H. The Qur’an. Tahrike Tarsile Qur’an, Inc. 12th U.S. Edition 2001.
7. Sher Ali, Maulawi. The Holy Qur’an. Islam International Publications Limited
(Ahmadiyya) 1997
8. Yusuf ‘Ali, Abdullah. The Holy Qur-an : English translation of the meanings
and Commentary. King Fahd Holy Qur-an Printing Complex. (Al Madina
Saudi Arabia) 1410 A.D.
Vitabu Vingine vya Rejea
Encyclopaedia Britannica. Encyclopaedia Britannica, Inc. 1958.
The History of al-Tabari : An Annotated Translation. Ehsan Yar-Shater, General Editor. State University of New York Press 1989-
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 22, 2016

MTUME MUHAMMAD ALIKUWA ANADAI SADAKA - FEDHA KABLA YA KUONGEA NAE


Ndugu msomaji,
Leo nitajibu hoja ambayo Waislam wamekuwa wakiitumia kwa muda mrefu kuwashutumu Wakristo kuwa tunadai Sadaka kutoka waumini, huku wakificha aya kutoka Quran zinazo onyesha kuwa Muhammad alikuwa anapokea Sadaka.
Watu waliokuwa wakiishi katika zama za Mtume walikuwa wanaenda kwa Mtume katika nyakati tofauti, na walikuwa wanamuuliza masuala tofauti yenye faida na yasiyo na faida, na suala hili lilisababisha kumkosesha Mtume wakati wa mapumziko, ndipo ilipokuja Qur-ani na kuwaamrisha watu kuwa kila anayetaka kuuuliza suala basi kwanza anatakiwa kutoa sadaqa, kabla ya kuuliza suala lake. Na Aya hiyo iko katika (Surat Mujadila aya ya 12) inasema hivi:-
يَا اَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نَاجَيْتُمُ الرَّسُولَ فَقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيْ نَجْوَاكُمْ صَدَقَةً ذٰلِكَ خَيْرٌ لَّكُمْ وَاَطْهَرُ فَإِن لَّمْ تَجِدُوا فَإِنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ[1]
Maana ya Aya hiyo ni kama hivi ifuatavyo:-
“Enyi mlioamini! Mnapomsemesha Mtume Muhammad toeni Sadaqa kabla ya kumsemeza; hayo ni bora kwenu na ni ya kukusafisheni sana. Ikiwa hamkupata (cha kutoa), basi Mwenyeezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu”.
Kwa amri hiyo basi, wao wenyewe wakawa ni wenye kurudi nyuma, na ni mtu mmoja tu ndiye aliyekwenda kwa Mtume (s.a.w.w), na kumuuliza masuala baada ya kushuka Aya hii, naye alitoa dirham kumi, kisha akauliza masuala muhimu ya kidini mbele ya Mtume (s.a.w.w). Naye alikuwa ni Dinar ambaye ni Mtumishi wa Imam Ali bin Abi Talib (a.s).
Lakini watu walipo gundua kuwa Muhammad alikuwa mtume bandia na anatumia sadaka kulisha famila yake kubwa, Allah akashusha aya kama ifuatavyo, nayo ni (Aya ya 13 ya Surat Mujadilah) isemayo:-
اَاَشْفَقْتُمْ اَن تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيْ نَجْوَاكُمْ صَدَقَاتٍ فَإِذْ لَمْ تَفْعَلُوا وَتَابَ اللهُ عَلَيْكُمْ فَاَقِيمُوا الصَّلاَةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَاَطِيعُوا اللهَ وَرَسُولَهُ وَاللهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ[2]
Maana ya Aya hiyo ni kama hivi ifuatavyo:-
“ Oh! Mnaona tabu kutanguliza hiyo Sadaqa kabla ya kumsemeza kwenu? Ikiwa hamjafanya haya basi. (Yamekwisha hayo). Na Mwenyeezi Mungu amekusameheni. Basi simamisheni sala na toeni Zaka na Mtiini Mwenyeezi Mungu na Mtume wake. Na Mwenyeezi Mungu anayo habari ya mnayoyatenda yote”.
Kama tulivyo soma hapo kwenye Surat Mujadilah aya ya 13, Muhammad kagonga mwamba, baada ya Waarabu kumshtukia kuwa Muhammad alikuwa anakula fedha zao kwa kuwapa unabii wa uongo.
Hebu soma kwanza:
17. SURA AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
90. Na walisema: Hatutakuamini mpaka ututimbulie chemchem katika ardhi hii.
91. Au uwe na kitalu cha mitende na mizabibu, na utupitishie mito kati yake ikimiminika.
92. Au utuangushie mbingu vipande vipande kama ulivyo dai; au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika uso kwa uso.
93. Au uwe na nyumba ya dhahabu, au upae mbinguni. Wala hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie kitabu tukisome. Sema: Subhana Rabbi, Ametakasika Mola wangu Mlezi! Kwani mimi ni nani isipo kuwa ni mwanaadamu na Mtume?
(Qur-Sura 17:90-93)
Baada ya kuombwa afanye angalau muujiza mmoja tu, Muhammad alishindwa vibaya sana na kuto fanya hata muujiza mmoja.
Swali:
1. Kwanini Muhammad alishindwa kufanya miujiza kama alivyo ombwa afanye?
2. Muhammad ni Nabii peke yake alieshindwa kufanya Miujiza tokea dunia iumbwe, Je, anaa kufuatwa na kuaminiwa?
3. Kwanini Allah nay eye hakumsaidia Nabii wake kufanya muujiza?
HAKIKA MUHAMMAD ALIKUWA NABII WA UONGO
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 22, 2016

Sunday, March 20, 2016

KUMBE FIRAUNI A.K.A FARAO ALINYENYEKEA NA KUWA MUISLAMU



Ndugu msomaji,
Kutokana na ushahid wa Surat Yunus aya ya 90-92, iliyo teremka Makka na kufanyiwa turjuma na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani inakiri kuwa Farao aka Firauni alisilimu na kuwa Muislam.
Surat Yunus 90. Tukawavusha bahari Wana wa Israili, na Firauni na askari wake wakawafuatia kwa dhulma na uadui. Hata Firauni alipo kuwa anataka kuzama akasema: Naamini kuwa hapana mungu ila yule waliye muamini Wana wa Israili, na mimi ni miongoni mwa walio nyenyekea!
91. Ala! Sasa? Na hali uliasi kabla yake na ukawa miongoni mwa mafisadi!
92. Leo, basi, tutakuokoa kwa mwili wako, ili uwe Ishara kwa ajili ya walio nyuma yako. Na hakika watu wengi wameghafilika na Ishara zetu
Aya hizo hapo juu kama zilivyo kwenye Surat Yunus zinatufahamisha kuwa Farao aka Firauni alisilimu na kuwa Muislam, lakini nilipo endelea kuisoma Quran kwa makini, nikakutana na shaka kubwa sana ndani ya Quran. Hebu soma kwanza ......aya kutoka Surat An Nisaai amabazo zinapinga aya kutoka Surat Yunus hapo juu.
Surat An Nisaai 17. Hakika toba inayo kubaliwa na Mwenyezi Mungu ni ya wale wafanyao uovu kwa ujinga, kisha wakatubia kwa haraka. Hao ndio Mwenyezi Mungu huwakubalia toba yao, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na ni Mwenye hikima.
18. Wala hawana toba wale wafanyao maovu mpaka yakamfikia mmoja wao mauti, kisha hapo akasema: Hakika mimi sasa nimetubia. Wala wale wanao kufa na hali wao ni makafiri. Hao tumewaandalia adhabu chungu.
Allah kupitia Surat An Nisaai analeta shaka na utata kwa kusema kuwa, toba inayo kubaliwa ni ile uliyo fanya dhambi kwa ujinga, lakini wote tunafahamu kuwa Farao yeye alikuwa anajua nini anafanya, hivyo hawezi kuingizwa kwenye kundi la wajinga.
ENDELEA KUSOMA UTATA NDANI YA QURAN
Surat Ghaafir 83. Walipo wajia Mitume wao kwa dalili zilizo wazi walijitapa kwa ilimu waliyo kuwa nayo. Basi yakawazunguka waliyo kuwa wakiyafanyia maskhara.
84. Walipo iona adhabu yetu walisema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu kuwa ni wa pekee, na tunaikataa miungu tuliyo kuwa tukiishirikisha naye.
85. Lakini imani yao haikuwa yenye kuwafaa kitu wakati ambao wamekwisha iona adhabu yetu. Huu ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu ulio kuwa kwa waja wake. Na hapo walio kufuru walikhasiri
Allah anaendelea kupinga ya zake mwenye kwa kusisitiza kuwa, yeye huwa hasamehi watu ambao wamekwisha ionja adhabu, lakini cha kushangaza, WAISLAM HAWA HAWA, huwa wanaombea Maiti msamaha wa dhambi, sasa Allah atawasamehe vipi maana teyari wamesha ionja adhabu ya kifo?
Kufuatana na wasomi wa dini ya Uislam, wengi wao nakubali kuwa Allah alimuokoa Farao na kumsamehe dhambi zake na kuwa Muislam. (Muhammad Asad, The Message of the Qur'an [Dar al-Andalus Limited, 3 Library Ramp, Gibraltar 1993], p. 306, fn. 112)
Ndugu zanguni, kila ninapo isoma Quran, huwa napata na kukutana na utata mkubwa sana kiasi cha kujiuliza, hivi ni kweli Allah aliumba na yeye ni mjuzi wa yote? Mbona Quran yake imejaa shaka na utata mkubwa?
Nawasihi Waislam wote duniani, mje kwa Yesu ambaye yeye hana utata wala hana shaka ndani yake. Maana Yesu ni JIBU, NJIA NA YEYE NI MWOKOZI WETU NA MUNGU MKUU.
Je! Unataka kumpa Yesu maisha yako sasa hivi ili akuokoe na kukupatia uzima wa milele? Je! Unajua maana ya kumpokea Yesu maishani mwako?
Kumpokea Yesu maana yake ni KUKIRI kwamba Yesu ni MWOKOZI, na pia hakuna mwingine awezaye kuokoa isipokuwa Yesu pakee. Biblia Takatifu inatuambia kwamba:
“Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.” (Matendo 4:12)
Kama unataka kuokoka sasa hivi; Tafuta mahali palipo na utulivu, na usome kwa kutamka kwa kinywa chako sala ifuatayo: (ukiweza unaweza kupiga magoti unapoomba sala hii)
“Ee Mungu wangu ulie Mtakatifu. Ninakuja mbele zako. Mimi ni mwenye dhambi. Naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizokukosea katika maisha yangu yote. Ninatubu kwa dhati ya kweli kutoka rohoni mwangu. Naomba damu ya Yesu Kristo iliyomwagika msalabani kwa ajili yangu initakase sasa katika roho yangu na nafsi yangu na mwili wangu. Nimefungua moyo wangu. Bwana Yesu Kristo nakukaribisha ndani yangu. Ingia kwa uwezo wa Roho Wako – Uwe Bwana na Mwokozi wangu kuanzia sasa na siku zote. Nakuomba unifanye niwe vile utakavyo mimi niwe. Ahsante kwa kunisamehe na kwa kuniokoa. Nimejitoa kwako nikutumikie katika siku zote za maisha yangu. Shetani hana mamlaka tena juu yangu katika jina la Yesu Kristo. Amina."
Ikiwa umesoma sala hii kwa kukusudia kabisa na kwa imani, basi wewe umeokoka na dhambi zako zote zimesamehewa kabisa. Damu ya Yesu iko juu yako sasa.
Baada ya kuokoka
Unapoanza maisha haya mapya katika Yesu Kristo nakushauri mambo yafuatayo:
(a) Zungumza na Mungu kwa maombi kila siku (Yohana 15:7).
(b) Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku (Matendo ya Mitume 17:11).
(c) Mruhusu Roho Mtakatifu akutawale (Wagalatia 5:16-25; Warumi 8:14-17).
(d) Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako (1Petro 5:7; Zekaria 4:6).
(e) Usiache kukusanyika na kushirikiana na wengine waliompokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao ili uimarike zaidi (Waebrania 10:25).
(f) Ikemee dhambi na ujitenge nayo. Ukiamini, kwa jina la Yesu unaweza kuishi maisha matakatifu (Yakobo 4:7-8).
(g) Jidhihirishe wazi kwa watu kwamba wewe umeokoka na pia shuhudia kwa watu injili (Mathayo 10:32-33; Warumi 1:16).
Hongera kwa kuokoka, tangu sasa umekuwa kiumbe kipya. Nakutakia baraka tele katika jina la Yesu Kristo, amina.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 20, 2016

Saturday, March 19, 2016

ALLAH AUMBA UCHAWI NA KUUTEREMSHA KWA NABII MUHAMMAD




Naam,
Huu ni Msiba Mkubwa sana katika taifa la Muhammad. Mara nyingi Wakristo wamekuwa wanajiuliza, hivi, uchawi ulitokea wapi na mwanzo wake ni nani?
Leo Quran inakujibu kuwa Uchawi ULIUMBWA NA Kuteremshwa na Allah, HIVYO BASI wachawi nambari moja ni Waislam. Nafahamu unafikiri kuwa Max Shimba anawasingizia Waislam au sio?
Hapa inafaa tufahamishane kuwa ushirikina ni jambo ovu linamtia mtu motoni. Kwenda kwa wachawi, wapiga ramli ni katika ukafiri na ushirikina.
Hebu soma Ushahid huu wa Quran:
SURAT TAHA: 73. Hakika sisi tumemuamini Mola wetu Mlezi ili atusamehe makosa yetu na uchawi ulio tulazimisha kuufanya. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mbora na Mwenye kudumu zaidi.
Kwenye Surat Taha ayat 73 kama ilivyo teremshwa Makka kwa Muhammad na kutafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani inasema kuwa ALLAH ANAWALAZIMISHA WAISLAM KUUFANYA UCHAWI. Huu ni msiba ndugu zangu. Swali la kujiuliza, hivi, tokea lini Mungu akawa mchawi? Hivi huu uchawi ulio teremshwa na Allah unafaida gani kwa Wislamu?
Hebu tuingalie tafsir ya pili ya Surat Taha aya 73 kama ilivyo tafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin inasema: 73. Kwani hakika sisi ni wenye kusimama juu ya Imani kumuamini Mola wetu Mlezi wa Haki, ili atufutie madhambi yetu yaliyo pita, na atusamehe huku kushughulikia uchawi ulio tulazimisha tujifunze na tuufanye! Na Mola wetu Mlezi ni Mbora wa malipo kuliko wewe, akit'iiwa; na ufalme wake na uwezo wake kulipa unadumu zaidi kuliko wako.
1. Inasema kuwa Waislam wanalazimishwa kujifunza Uchawi
2. Inasema kuwa Waislam wanalazimishwa kuufanya Uchawi.
Ndugu msomaji, leo sina mengi ya kusema maana umesoma Mwenyewe kutoka Quran kuwa Allah aliteremsha uchawi na kawalazimisha Waislam wajifunze na kuufanya uchawi.
Nawashauri Wakristo wenye marafiki wa Kiislam wawe makini, maana huyo rafiki yako anaweza kuwa ndiye anaye-kuroga kwasababu kalazimishwa na Allah kufanya hivyo.
Nimenukuu quran aya ya 2:102 na maelezo/ufafanuzi wake hapo chini kutoka tafsiri mbili za quran (Tafsiri ya Sheikh Abdullah Saleh Al-Farsy na Tafsiri ya Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani). Aya hii na maelezo/ufafanuzi wake inaonesha mambo yafuatayo:
(a) Uchawi umeteremshwa na malaika wa Allah
(b) Kuna wachawi wa kiislam.
(c) Uchawi ni amali ya ukafiri
Pia, kwa mujibu wa Sahih Bukhari juzuu ya 4, Kitabu cha 54, Hadithi namba 490 na Sahih Bukhari, juzuu ya 7, kitabu cha 71, hadithi namba 658; Muhammad alirogwa na akazurika na uchawi. Kisa cha mtume kurogwa na kuzurika na uchawi pia kinasimuliwa katika quran Tafsiri ya Sheikh Abdullah Saleh Al-Farsy ukurasa wa 977 na 978.
MASWALI
(a) Ikiwa uchawi ni ukafiri, Kuna uhusiano gani kati ya Allah na ukafiri mpaka ateremshe uchawi?
(b)Mtume Muhammad alirogwa na wachawi wa kiislam au wachawi wengine?
(c) Mtume Muhammad alirogwa na uchawi ulioteremshwa na malaika wa Allah au uchawi mwingine?
(d) Mtume au nabii gani mwingine alirogwa na akaathirika na uchawi kama Muhammad?
Quran 2:102 inasema:
Wa Attaba`ū Mā Tatlū Ash-Shayāţīnu `Alá Mulki Sulaymāna Wa Mā Kafara Sulaymānu Wa Lakinna Ash-Shayāţīna Kafarū Yu`allimūna An-Nāsa As-Siĥra Wa Mā 'Unzila `Alá Al-Malakayni Bibābila Hārūta Wa Mārūta Wa Mā Yu`allimāni Min 'Aĥadin Ĥattá Yaqūlā 'Innamā Naĥnu Fitnatun Falā Takfur Fayata`allamūna Minhumā Mā Yufarriqūna Bihi Bayna Al-Mar'i Wa Zawjihi Wa Mā Hum Biđārrīna Bihi Min 'Aĥadin 'Illā Bi'idhni Al-Lahi Wa Yata`allamūna Mā Yađurruhum Wa Lā Yanfa`uhum Wa Laqad `Alimū Lamani Ashtarāhu Mā Lahu Fī Al-'Ākhirati Min Khalāqin Wa Labi'sa Mā Sharaw Bihi 'Anfusahum Law Kānū Ya`lamūna
Quran 2: 102(Tafsiri ya Sheikh Abdullah Saleh Al-Farsy) inasema: Wakafuata yale waliofuata mashetani wakadai kuwa yalikuwa katika ufalme wa (Nabii) Suleiman; na Suleiman hakukufuru, bali mashetani ndio waliokufuru, wakiwafundisha watu uchawi (waliokuwa wakiujua wenyewe tangu zamani na uchawi) ulioteremshwa kwa malaika wawili, Harut na Marut, katika (mji wa) Babil. Wala Malaika hao hawakumfundisha yoyote mpaka wamwambie: “ Hakika sisi ni mtihani (wa kutazamwa kutii kwenu); basi usikufuru.” Wakajifunza kwao ambayo kwa mambo hayo waweza kumfarikisha mtu na mkewe (na mengineyo). Wala hawakuwa wenye kumdhuru yeyote kwa mambo hayo ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza ambayo yatawazuru wala hayatawafaa Na kwa yakini wanajua kwamba aliyehiari haya hatakuwa na sehemu yoyote katika akhera. Na bila shaka ni kibaya kabisa walichouzia (starehe za) nafsi zao (za Akhera). Laiti wangalijua, (hakika wasingefanya hivi). (Tafsiri ya Sheikh Abdullah Saleh Al-Farsy ukurasa 25-26)
Nanukuu Maelezo/ Ufafanuzi wa quran 2: 102
Suleiman aliyetajwa hapa ni nabii, Mayahudi wanamwita Nabii Suleiman kuwa ni mfalme aliyepata ufalme kwa uchawi, si Mtume. Basi na hawa wachawi wa kiislam humnasibishia Nabii Suleiman hizo ilimu zao za uchawi. Basi Mwenyezi Mungu anamkanushia haya. Na aya hii yaonesha wazi kuwa
(a) uchawi ni amali ya ukafiri na
(b) kuwa mchawi hawezi kumdhuru mtu ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na
(c) kuwa mchawi mwenyewe anadhurika kwa uchawi wake. Na anataja hapa Mwenyezi Mungu kuwa nyuma huko kabisa katika zama za mfalme
Qura 2:102.(Tafsiri ya Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani) Inasema:
Na wakafuata yale waliyo zua mashet'ani kuuzulia ufalme wa Su leiman. Na wala Suleiman hakukufuru, bali mashet'ani ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu uchawi, na yaliyo teremshwa kwa Malaika wawili, Haaruta na Maaruta katika Baabil. Wala hao hawakumfundisha yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani; basi usikufuru. Wakajifunza kwa hao wawili yale ya kumfarikisha mtu na mkewe. Wala hawawezi kumdhuru mtu ila kwa kutaka Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza yatayo wadhuru wala hayawanufaishi. Na hakika wanajua kwamba aliye khiari haya hatakuwa na fungu lolote katika Akhera. Na hakika ni kiovu mno walicho jiuzia nafsi zao laiti wangelijua.
Mungu awarehemu na kuwasamehe ndugu zetu wote wanao fanya Uchawi. Maana Biblia inasema kuwa WACHAWI WOTE WATAINGIA JEHANNAM. 1 Samweli 15 : 23 .......... dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.
Ndugu msomaji, mpokee Yesu aliye hai na upate uzima wa milele. Dini haita kusaidia kitu, maana sasa unaelewa kuwa, ni dini ambayo inakufanya uwe mchawi na kuachana na upendo wa Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 19, 2016

Friday, March 18, 2016

MUHAMMAD ALIKUWA ANAVAA VIATU MSIKITINI

Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujikumbushe na kujifunza kuhusu kusali na viatu katika nyumba za ibada. Hususan Msikitini.
Waislam mara nyingi wamekuwa wakiwashutumu Wakristo na kuwakejeli kuwa, eti wanasali na viatu Kanisani.
Je, Mtume wa Allah aitwaye Muhammad alivaa viatu alipo kuwa anaswali Msikitini?
Hebu tuangalie ushahidi huu hapa:
Ukisoma kitabu cha Al-u-lu wal-marjan Uk. 179
14. Mlango:
Ruhusa ya kusali na Viatu.
325. Hadithi ya Anas Bin Malik (R.a) kutoka kwa Said Bin Yazid Al-Azid (r.a) amesema, Nilimuuliza Anas Bin Malik (r.a) “Hivi Mtume (s.a.w) alisali huku amevaa viatu vyake?” Akanijibu, “Ndiyo” (Bukhari, Hadithi N. 383, Juzuu ya 1)
Hapo tunamuona Muhammad akisali na Viatu, na mlango hapo umesema, Ruhusa ya kusali na Viatu, maana yake waislamu hapo wameruhusiwa kusali na Viatu, pia haikuishia hapo, Muhammad akasema tena kuwaambia Waislamu.
Ukisoma kitabu kinachoitwa “TAFSIRI YA BULUGH AL-MARAM MIN JAM’I ADILLATIL AHKAM
Ukurasa wa 101 Hadithi Na. 171
Abu Said (r.a) amesimulia: Mtume (S.a.w) amesema: “Ye yote miongoni mwenu atakapoenda msikitini kusali, basi atizame, akiona uchafu au najisi katika viatu vyake aondoe kisha aswali navyo”. Abu Dawud Ibnu Khuzaimah ameipa daraja ya Sahih.
*Murad wa kutwaharisha viatu:
Iwapo mtu amekanyaga najisi kwa kiatu, atakitwaharisha kwa kusugua chini mchangani*
Hapo kwa mtu mwenye akili zake timilifu, hawezi kukomaa na kuanza kuwalaumu Wakristo, eti kwa nini wana Sali na viatu? Wakati Muhammad mwenyewe, alisali huku amevaa viatu, na pia akawaambia waislamu wanapoenda kusali, basi watazame viatu vyao kama kuna najisi, basi wavisugue chini mchangani, labda waislamu watuambie wao kusali na viatu, ni Uviviu wa kusugua viatu mchangani? Au mazingira yao wanayoishi hayana mchanga?
Tena Muhammad akakazia zaidi kuhusu Viatu, aliponukuliwa katika Hadithi hii.
Kasema Mtume (S.a.w) “Atakaepata (ona) nge nae anasali, basi amuue kwa kiatu cha kushoto” (Mkweli Mwaminifu, Juzuu ya 1-2, Hadithi Na. 188, Uk, 88)
Muhammad anawataka Waislamu wakimuona Nge basi wamuue kwa kiatu cha kushoto, sasa jiulize, wewe umevua viatu, unaswali peku peku (kama bata) Halafu amekatiza nge, unaweza kweli kumkanyaga kwa mguu? Nachoweza kusema ni uvivu tu wa waislamu katika kusugua mchangani viatu vyao vilivyo na najisi, kwani wameshapewa ruhusa ya kusali navyo.
Kumbe Mtume Muhammad alikuwa anavaa viatu alipo kuwa ndani ya Msikiti.
Kumbe Mtume Muhammad alisali na viatu Msikitini.
Hakika Uislam ni dini bandia.
Max Shimba Ministries Org

JE KUSALI NA VIATU KATIKA JENGO LA IBADA NI MAKOSA?



Ndugu msomaji,
Ni kwa muda mrefu sasa kumekuwa na sauti zinazopazwa kila kona ya ncha ya dunia toka kwa ndugu na rafiki zetu wapendwa wa Kiislam, wakihoji juu ya kile wanachokiita kuwa ni tendo la Wakristo kupuuzia au kutotii ukweli wa Biblia kwa madai kwamba maandiko matakatifu ya Biblia kupitia agizo fulani lililotolewa kwa nabii Musa yanaelekeza Wakristo kutekeleza matendo yao ya ibada kwa kuvua viatu vyao waingiapo makanisani.
Katika mada hili tutaangazia mambo muhimu yatakayo saidia kutoa mwangaza na majibu ya msingi juu ya hoja hiyo tete.
Mapitio ya mada:-
Chimbuko la hoja hiyo katika Biblia na Qur an.
Farsafa juu ya tukio Musa kuvua viatu / nini kusudi la tukio hilo?
Je’ Musa alivua viatu katika matendo halisi ya ibada katika utumishi wake?
Je’ mtume Muhammad naye alisali na viatu au bila viatu?
Bwana Yesu / Manabii na Mitume katika farsafa ya ibada na kuvaa viatu.
Kwa kuatilia kwa makini vipengele hivyo vya uchambuzi hadi mwisho ni imani yangu kuwa hautabaki kama ulivyo ikiwa u Muislam au ni Mkristo, ninachokusihi ni kufungua moyo wako ili kweli za maandiko zipate nafasi ndani yako.
Uchambuzi wa mada
Hebu sasa bila ya kupoteza muda tuanze kwa kuangalia kipengele namba moja kama vilivyoainishwa katika muongozo wa mapitio ya mada:-
Chimbuko la hoja hiyo katika Biblia na Qur an.
Kuibuka kwa hoja hii chanzo chake ni matokeo ya ndugu zetu na marafiki wa Kiiislam kugeukia matumizi ya Biblia katika harakati zao mbali mbali za uenezi wa Uislam duniani.
Kuanzia kule Durban - Afrika ya kusini’ mwana mihadhara mashuhuri marehemu Ahmed Deedat ndiye mwanzilishi mkuu wa hoja hizi chini ya shirika lake la uenezi wa Uislam IPC – (Islamic Propagation Centre), bwana Deedat ameandika majarida na vitabu vingi vinavyohoji na kukosoa msingi mzima na misimamo wa mafundisho ya teolojia ya Kikristo, ambapo katika kitabu kimojawapo pia ameibua hoja hii juu ya kile anachodai kutokuwepo kwa uhalali wa mtu kuingia kwenye jengo la ibada akiwa na viatu miguuni mwake.
Katika hoja yake hiyo Deedat kama ilivyo wanaharakati wengine wa uenezi wa Uislam hivi leo ananukuu kile anachokiita kuwa ni ushahidi wa katazo hilo la kusali na viatu katika kitabu hiki cha nabii Musa ndani ya Biblia:-
Kutoka 3:4-5
Bwana alipoona kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa’ Musa’ naye akasema mimi hapa. (5) Naye akasema, usikaribie hapa. Vua viatu vyako miguuni mwako, maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.
Katika maandiko ya kitabu cha msahafu pia maelezo ya kisa hicho cha Musa yamenukuliwa kama tunavyosoma:-
Qur an 20:11
Basi alipofika akaitwa, ewe Musa, bilashaka mimi ndiye Mola wako’ basi vua viatu vyako kwa kuwa wewe huko katika bonde takatifu la tuwa...
Hivyo kupitia maelezo ya maandiko hayo Wanaharakati hao wa uenezi wa dini wamesikika wakifundisha kwa ujasiri kuwa jamii ya Wakristo imepotoka kwa kuingia katika majengo ya ibada na viatu huku wakiacha maelekezo hayo ya Biblia kupitia tukio hilo la Musa maelekezo ambayo kwa mtazamo wao huyaona kuwa ndiyo yanayotoa muongozo wa ibada ya kusali bila ya kuvaa viatu miguuni.
Katika uchambuzi wa mada hii tutaangalia mawazo hayo kwa ulinganifu wa kina ili kuondokana na utata huu uliotawala katika masikio ya watu wengi.
Farsafa juu tukio hilo la Musa kuvua viatu, na je’ nini kusudi lake?
Wazo la wajenga hoja juu ya tukio hilo linaangukia moja kwa moja katika dhana ya fundisho la ibada.
Na kwa kiwango cha usomaji na uchunguzi wao wamejikuta wakihitimisha hoja hiyo kwa kuondoka na wazo hilo kwamba kusudi la andiko hilo lilkuwa ni kuelekeza namna ya kuabudu kwa kutovaa viatu miguuni.
Ukweli halisi
Pamoja na maelezo au niite mapendekezo ya waalimu hao mbalimbali, binafsi kadri ya uchunguzi wa kina nilioufanya ili kuelewa farsafa au muktaza halisi wa tukio hilo, nimegundua kuwa hakuna usahihi au uhalali wowote wa kuhusisha tukio hilo la Musa kuamriwa kuvua viatu machungani ( mlima horebu) na fundisho la mfumo wa ibada makanisani au kwenye majengo mengine ya ibada.
Ili kupata ufumbuzi wa hilo hebu turejee kwanza historia ya maisha ya Musa
Musa alikuwa mtoto wa tatu kati ya watoto wa mzee Amrani na mkewe mcha Mungu aliyeitwa Yokobedi, historia inaonyesha kuwa Musa alizaliwa kwa 593 KK katika bara la Afrika nchini Misri, akiwa mtoto wa miezi mitatu aliokotwa na binti wa Farao na kulelewa katika jumba la kifalme Misri (Matendo 7:20-22).
Musa aliishi katika himaya hiyo ya Kifalme kwa miaka 40’ yaani toka mwaka 593 KK hadi 1553 KK, na baadae alikimbilia Midiani baada ya kumuua Mmisri mmoja aliyemkuta akimpiga Mwebrania alipokuwa ameenda kutazama ndugu zake huko, na huko Midiani aliishi kwa mkwewe Yethro aliyekuwa akifanya kazi ya Ukuhani ambaye ndiye aliyemwolea binti yake mmoja wa mwisho miongoni mwa mabinti 7 aliyeitwa Sipora, Musa aliishi hapo ukweni kwa muda wa miaka 40’ tangu mwaka 1553 KK hadi 1513 KK na ndipo akiwa na umri wa miaka 80’ alitokewa akiwa machungani na kutakiwa kwenda kuwakomboa Israel toka nchi ya Misri (Kutoka 3:1-15).
Mambo machache ya msingi tunajifunza katika historia hiyo ya Musa.
Musa alikwenda kutazama ndugu zake na kukuta Mmisri akimpiga Mwebrania na ndipo akampiga Mmisri yule na kumuua ( Kutoka 2:11).
Kama sehemu ya makimbilio Musa akakimbilia Midiani – ambapo ni mwisho wa magharibi mwa jangwa la Arabu, Ghuba ya Akaba kuingia mkono wan chi ya Sinai kwa mkwewe aliyeitwa ‘ Reueli au Yethro.
Mkwe wa Musa Yethro alikuwa ni kuhani, hivyo Musa aliishi na kuhani kwa miaka “40’.
Mambo ya kiugunduzi
Kadri ya historia ya maisha na mizunguko hiyo ya Musa tunaweza kugundua mambo ya msingi yanayoweza kujenga msingi wa ufumbuzi wa mada hii, lakini kubwa zaidi ni kuwa Musa baada ya kufanya kosa lile la kuua alikimbia na kwenda kuishi kwa kuhani Yethro.
Tendo hilo la Musa kuishi kwa kuhani Yethro’ linatupa msingi wa kuelewa kusudi hasa la Musa kutakiwa kuvua viatu kama lililenga fundisho la mfumo wa ibada au la’_ufumbuzi huo tunaupata kwa kujiuliza maswali yafuatayo;-
Endpo Musa aliishi kwa kuhani’ swali Je’ nini kazi ya kuhani?
Kadri ya Biblia tunagundua kuwa kuhani kazi yake ni:-
- Kusimamia na kuendesha ibada za upatanisho wa dhambi kadri ya mfumo na utaratibu uliowekwa na Mungu katika hekalu la dunia/ kwa kifupi ni msimamizi na mwendeshaji wa ibada.
Hivyo kutokana na jukumu hilo la kuhani tunaweza kupiga picha ifuatayo juu ya maisha ya Musa akiwa kwa kuhani huyo tukilinganisha na tukio la mlima Horebu, kwa kuzingatia mwenendo wa maisha ya makuhani kuwa:-
- Kwa kuishi huko na kuhani’ basi huenda nabii Musa alikuwa akihusishwa au kushiriki katika maisha ya ibada za nyumbani kwa kuhani huyo kwa kuzingatia msimamo wa makuhani katika matendo ya kidini tokea katika ngazi ya familia.
- Kwa hali hiyo kama kuvua viatu ingalikuwa ni sehemu ya mfumo wa ibada basi Musa angekuwa ameshajifunza au kuona kwa kuhani huyo Yethro’ katika ibada za nyumbani na hivyo kusingekuwa na haja ya Mungu kutoa maelekezo tena kwa Musa juu ya kuvua viatu pale Horebu endapo pia kusudi la kuwepo kwake kule porini lingekuwa ni kutekeleza matendo ya ibada.
Lakini pamoja na hoja hizo za msingi bado inapaswa ieleweke kuwa tukio hilo la agizo la kuvua viatu kwa Musa lilitolewa kwa Musa pindi akiwa katika shughuli za kawaida za kimaisha za kuchunga wanyama tena kipindi ambacho bado hakuwa na nafasi yeyote ya utumishi kwakuwa uteuzi wake ulikuwa bado, na kwa hali halisi Musa alikuwa mlimani tena kwenye mapori kwakuwa alikuwa akilisha wanyama na hakuwa kanisani wala katika eneo la mazingira ya kiibada.
Pamoja na hayo kile kinachoonekana kuwachanganya wapendwa wangu na ndugu Waislam ni agizo tu kwa Musa kutakiwa kuvua viatu vyake, na kwa hali hiyo kulichikulia kwamba tendo hilo kuwa ndicho kinapaswa kuwa kielelezo cha mifumo ya ibada zetu za makanisani na katika majengo mengine ya ibada.
Sababu ya kina / kwanini kuvua viatu katika Biblia?
Kile nilichotangulia kusema awali ni swala la uaminifu na moyo wa dhati katika kusoma maandiko, kimsingi Biblia ina majibu kwa kila swali la imani hivyo jukumu letu ni kuichunguza kwa makini tu.
Na katika kufikia kina halisi cha uchunguzi wa neno la Mungu hasa kwa hoja zenye utata kama hii, ni vyema kanuni ya usomaji wa Biblia inayoelekezwa na kitabu cha Mhubiri ikazingatiwa.. rejea:
Mhubiri 7:27
Tazama, asema mhubiri, “mimi nimeyaona hayo kwa kulinganisha na hili, ili kuitafuta jumla.”
Mhubiri anaweka bayana kuwa kanuni ya msingi katika usomaji wa maandiko imejengwa katika mfumo wa kanuni ya kulinganisha maandiko mbalimbali katika harakati za kutafuta fafsiri au maana ya kile ulichosoma, na kwa kutumia kanuni hiyo ya Biblia nitaomba sasa tuungane kusoma nukuu hii ya andiko la kitabu cha nabii Ruthu ili kugundua chimbuko na sababu ya kina juu ya tamaduni hii ya kuvua viatu, na yakuwa ilikuwa na madhumuni gani basi kwa wana wa Israel na hata Mungu amtokee Musa kwa kuanza na agizo hilo hilo la kuvua viatu.
Ruthu 4:7
Basi ilikuwa desturi zamani za kale katika Israel, kwa habari za kukomboa na kubadiliana, ili kuyahakikisha yote; mtu huvua kiatu chake na kumpa mwenziwe; ndivyo walivyohakikisha neno katika Israel.
Pamoja na kwamba kinachoshikiliwa zaidi na wajenga hoja ni utakatifu wa eneo kuwa ndiyo sababu iliyofanya Musa kutakiwa kuvua viatu, lakini kile anachoeleza Ruthu ndiyo sababu ya kiasili na kina hasa, kwakuwa kimsingi Biblia kama tutakavyoona mbele bado tena inaonyesha Mungu akiagiza yeye mwenyewe na wakati mwingine kupitia malaika akiwataka manabii na mitume kuvaa viatu vyao katikati ya utakatifu na uwepo wake.
Katika andiko hilo nabii Ruthu anataja mambo kadhaa yanayolengwa au kukusudiwa katika tendo la kuvua viatu kama ifuatavyo:- Ruthu 4:7.
- Ilikuwa ni utekelezaji wa desturi ya zamani katika Israeli
- Ilikuwa ni uthibisho wa utayari wa kazi ya kukomboa au mambo ya rehani.
- Ilikuwa ndiyo ishara ya kuthibitisha mambo katika Israeli
Kwa kile kinachomaanishwa kupitia tendo hilo la kuvua viatu kwa Waisrael kadri ya ufafanuzi wa andiko hilo la Ruthu, utangundua kuwa wale wanaojenga hoja ya kuwalaumu wale wanaoingia katika majengo ya ibada na viatu hivi leo, wanafanya hivyo ikiwa ni matokeo tu ya kutotumia muda wa kutosha kuchunguza mambo kwa kina kabla ya kuibua hoja au mafundisho.
Hivyo kile alichofanya Musa kwa kutii agizo hilo la kuvua viatu ilikuwa ni kuonyesha utayari wake wa kuwa kiongozi wa njia kwa Wana wa Israel katika harakati za kuwakomboa toka katika utumwa wa Farao. Vinginevyo kama dhana kuu ingekuwa ni utakatifu wa eneo basi tungekuwa na swali la kujiuliza kwamba:-
“Kwakuwa nchi yote ilikuwa ni takatifu je’ Musa alihifadhi viatu hivyo wapi?
Au je ni wapi imeandikwa kuwa Musa alikimbia kutoka nje ya ardhi hiyo ya Horebu kwenda kutupa viatu vyake ili kutonajisi utakatifu wa eneo hilo?”
Na kwa msingi huo basi ni bayana kuwa tendo hilo la kuvua viatu lililenga zaidi kupima utayari wa Musa kwaajili ya kupatiwa jukumu hilo la kuwakomboa wana wa Israel kama ambavyo kitabu cha Ruthu kinaeleza kuwa ilikuwa ni uthibisho pia kwa habari ya kukomboa.
Hata hivyo kwajumla tukio lenyewe halikuwa tukio la Musa kuabudu au kufundishwa mfumo wa ibada badala yake kile kinachoonekana hilo lilikuwa ni tukio la kumtawadha nabii Musa kwa jukumu la kukomboa watu wa Mungu.
Tukio kama hilo linaweza kufanana na kile tunachofanya mara kadhaa tunapokamilisha kuchagua viongozi wetu kwa upande wa uongozi wa Serikali..
Jifunze kwa mfano;
Kwa kawaida huwa baada ya kumchangua raisi wa nchi pamoja na taratibu nyingine, huwa anapoapishwa huonekana pia akivalishwa shuka begani na kushikishwa ngao na mkuki na wazee wa jadi kisha kuketi katika kigoda.
Kimsingi tendo hilo ni tendo linalotendwa kwa siku moja tu likiwa na lengo la kutoa kiashiria kuwa huyo aliyeko mbele sasa ni kiongozi wa nchi. Na baada ya hapo kiongozi huyo huvua mavazi hayo na kuendelea na majukumu yake....
Hivyo kile kilichotendeka kwa Musa kama ilivyo kwa tamaduni zetu hizo, ni tukio la kutawadhwa na kuthibitishwa kuwa sasa ni kiongozi wa umma wa Israel na hivyo matukio hayo ya kumthibitisha maana yake inakomea katika eneo husika la tukio hilo... hivyo kwamaana hiyo tendo hilo lisingepaswa kuhusianishwa na mifumo ya kawaida ya ibada.
Je’ Musa alivua viatu katika matendo halisi ya ibada katika utumishi wake?
Hii ni moja ya sehemu muhimu sana katika uchambuzi wa mada hii, katika sehemu hii ndipo pia tunaweza kukaza wazo la msingi juu ya dhumuni hasa la agizo la Musa kuvua viatu kama tulivyokwishaona hapo nyuma, kwakuwa kimsingi kama agizo hilo lililenga mfumo endelevu wa ibada basi niwazi kwamba hatutarajii kuona Mungu huyo huyo akitoa agizo jingine la kumtaka tena Musa kuvaa viatu katika matendo ya ibada.
Lakini hapa ni kinyume, na ndipo pia tunakuwa bayana na kuona ukweli wa uchambuzi tuliofanya hapo nyuma na kuona jinsi ambavyo tukio hilo halikulenga kuelekeza mfumo wa ibada ya kuvua viatu katika majengo yetu.
Matukio ya mbele yote yanayohusu ibada za nabii Musa yanataja jinsi Musa alivyofanya au kuruhusiwa kuyafanya ibada zake akiwa amevaa viatu vyake, na tukio kubwa maarufu zaidi ni lile la ibada ya kwanza ya pasaka katika nchi ya Misri, kumbuka ibada hiyo ndiyo imefanya msingi wa ibada ya leo ya pasaka kupitia kafara ya damu ya Yesu ambayo inaadhimishwa na Wakristo karibu katika makanisa yote. Ibada hii Musa aliambiwa aifanye akiwa amevaa viatu...
Kutoka 12:11-12
Tena mtamla hivi, mtakuwa mmefungwa viuno vyenu, “mmevaa viatu vyenu miguuni”, na fimbo zenu mikononi mwenu, nanyi mtamla kwa haraka ni pasaka ya Bwana (12) maana nitapita katika nchi ya misri usiku huo.....
Maelezo hayo ya Biblia ni bayana, tena Mungu mwenyewe kwa kinywa chake anamwagiza nabii Musa kuendesha ibada ya pasaka na tena basi ibada hiyo anatakiwa kuifanya yeye na Wana wa Israel wakiwa wamevaa viatu vyao.........
Kwa andiko hilo tungeweza hata kuhitimisha mada hii kwakuwa kila kitu sasa kiko bayana, lakini tunaweza kuendelea kufanya mikazo zaidi ili kwamba ndugu msomaji wangu umalize mashaka yote juu ya hili, na basi kwa kulinganisha agizo lile la kuvua viatu lililodhaniwa kuwa ndiyo fundisho la mfumo wa ibada na tukio hili halisi la ibada tunaweza kujiuliza maswali ya fuatayo:-
- Kama tendo la Musa kuambiwa vua viatu vyako lililenga mambo ya ibada na kumtaka Musa awe akivua viatu katika matendo ya ibada:
Je’ sasa ni Mungu yupi tena anayemtaka Musa kuvaa viatu katika ibada hiyo ya pasaka na tena Mungu huyo akiahidi kupita hapo Misri usiku huo na huku tayari wana wa Israel wakiwa wamevaa viatu vyao?
- Na je’ inaaminisha nini vitabu vyetu vinapomtambulisha Mungu kuwa si mwenye kigeugeu endapo kama maagizo hayo ni ya kujipinga? Rejea; (Qur an 17:77/ Yakobo 1:16-18)
Ndugu msomaji wangu hayo ni maswali ya changamoto na kumsha ufahamu wetu, lakini kama tulivyokwishaona ni kuwa kamwe agizo lile la kuvua viatu halikulenga kuelekeza mfumo wa ibada kwa Wakristo , na badala yake ilikuwa ni tukio la kumtawadha Musa ili kupewa dhamana ya kuwakomboa Israeli toka utumwa wa Farao. (Rejea’ Ruthu 4:7 Basi ilikuwa desturi zamani za kale katika Israel, kwa habari za kukomboa na kubadiliana, ili kuyahakikisha yote; mtu huvua kiatu chake na kumpa mwenziwe; ndivyo walivyohakikisha neno katika Israel.)
Nabii Musa akiwa jangwani
Baada ya kutoka Misri chini ya nabii Musa wana wa Israel walikuwa na mikutaniko mbalmbali ya kiibada Jangwani...
Qur an 7:138
Na tukawavusha wana wa Israil baharini ( wakasalimika na balaa za Firauni) na wakawafikia watu waliokuwa wakiabudu masanamu yao. Wakasema “Ewe Musa! Tufanyie waungu na sisi ( yaani masanamu....(Nabii Musa akasema) Hakika ninyi ni watu mufanyao ujinga...........
Matendo 7:38
Yeye ndiye aliyekuwa katika kanisa jangwani, pamoja na yule malaika aliyemtokea..
Maandiko hayo kimsingi yanaweka bayana juu ya kuwepo kwa matendo ya ibada kwa wana wa Israil baada ya kuvuka bahari ya shamu na kuendelea na msafara jangwani, andiko la Qur an linataja jaribio la watu waasi kuwataka wana wa Israel kujihusisha na ibada ya sanamu tendo linalotajwa na Qur an kuwa lilikataliwa na nabii Musa.
Kwa upande mwingine maandiko ya Biblia nayo yanaonyesha kuwa wana wa Israeli walikuwa katika umoja wa kanisa ambao kimsingi ni umoja wa watu walioitwa kutoka gizani na kujiunganisha pamoja wakimwabudu Mungu.(Greec: Ekllessia)
Habari gani juu ya viatu?
Kumbukumbu 29:4-5
- Lakini Bwana hakuwapa macho ya kuona..
- Name miaka arobaini nimewaongoza jangwani..
- Nguo zenu hazikuchakaa mwilini..
- Viatu vyenu havikuchakaa miguuni mwenu...
Andiko hilo la kumbukumbu linaonyesha muujiza ambao Mungu aliwatendea wana wa Israeli, ambapo miongoni mwa matendo hayo ya miujiza ni tendo la kufanya viatu vya wana wa Israel kutochakaa katika miguu yao, kipindi chote cha miaka arobaini ya jangwani.
Hivyo hoja ya msingi hapo ni kuwa kumbe wana wa Israel wakiwa hapo jangwani bado walikuwa na viatu, swali la msingi ni kuwa:-
je’ ni mahali gani katika maandiko ambapo Mungu aliwalekeza wana wa Israel waingiapo kwenye kanisa la jangwani wawe wanavua viatu hivyo vinavyotajwa?
Na endapo ushahidi huo wa kutakiwa kutovaa viatu hivyo wakati wa ibada basi wale wanaojenga hoja ya kukosoa wanaoingia na viatu hawatakuwa na uhalali wa kujenga hoja hiyo kwakuwa ni hoja isiyo na utetezi wa kimaandiko.
Je’ mtume Muhammad naye alisali na viatu au bila viatu?
Hii ni hoja ya msingi sana katika uchambuzi wote wa mada hii, kwakuwa pamoja na mitazamo yetu juu ya maswala ya kidini lakini tunakubaliana kuwa manabii tunaowaamini kadri ya makundi ya imani zetu ndiyo wanaotoa sura nzima ya kanuni na masharti juu ya mwenendo wa wafuasi katika imani zao hivyo kadri ya vile inavyoaminika kuwa wao hupokea maelekezo kwa Mungu...
Hivyo katika kipengele hiki tutaangalia kwa upana wake juu ya ibada za mtume Muhammad anayeaminiwa na jamii ya ndugu zetu Waislam ili kuona naye anatoa kielelezo gani kitakacho tusaidia kupata suluhisho la utata wa hoja hii katika ulimwengu wetu wa imani.
Maandiko mawili ya msingi katika Qur an ndiyo yatakayotupatia kanuni na njia ya kutafiti hoja hii:-
Qur an 33:21
Bilashaka mnao mfano mwema (riwadha nzuri) kwa mtume wa Mwenyezi Mungu....
Katika andiko hilo la kwanza tunaona kuwa Qur an ikimtaja Muhammad kama ndiye anayepaswa kuwa mfano au kilelezo katika matendo ya kidini na hivyo jamii ya Waislam inapaswa kuiga toka kwake.
Andiko hilo pamoja na mambo mengine linatupatia kibali au uhalali wa kuchunguza ili kuona mwenendo wa ibada za mtume Muhammad mwenyewe ambazo kimsingi ndizo zinapaswa kuigwa na wapendwa wetu Waislam. Hata hivyo ni vyema ieleweke kuwa maandiko ya masahafu wa Qur an hayataji kwa upana mwenendo wa matendo ya ibada ya mtume, lakini yanatoa mwongozo wa kanuni ya kufanya. Hebu soma ayah ii:-
Qur 42:10
Mkihitirafiana katika jambo lolote, rejeeni katika kitabu cha Mwenyezi Mungu na hadithi za mtume.
Hivyo njia inayotajwa na andiko hilo ni kutafuta ufumbuzi juu ya hoja yeyote kwa kurejea katika vitabu vilivyo nje ya Qur an vilivyopitishwa kama vitabu halali vya teolojia ya Uislam, vinavyoitwa vitabu vya hadithi.
Hebu sasa tuandalie katika vitabu hivyo vya hadithi kuelewa ukweli huo:-
Nukuu 1’
Book’ Sahih Al-Bukhari (Arabic English – Dr Muhsin Khan – Islamic University, Al Medina Al Munawwra / Al Maktabat Al Salafiat)
Vol 1’ Chapter 24/ (Hadith) no 383’
Narrated Abu Maslama, Sai’id Yazid Al Azid: I asked Anas bin Malik whether the Prophet had ever prayed with His shoes on. He replied “Yes.”
Tafsiri
Imesimuliwa na Abu Maslama, Sai’id Yazid Al Azid; Nilimuuliza Anas bin Malik endapo mtume alishawahi wakati wowote kusali na viatu vyake. Akajibu“ Ndiyo.”
Simulizi hiyo isiyo na maneno mengi inaweka bayana juu ya namna mtume Muhammad alivyoendesha ibada zake za swala, na yakuwa kumbe Muhammad mwenyewe aliabudu na viatu vyake na hakuwa akivua viatu wakati wa ibada.
Hebu tuone nukuu nyingine:
Book’ Sahih Al-Bukhari (Arabic English – Dr Muhsin Khan – Islamic University, Al Medina Al Munawwra / Al Maktabat Al Salafiat)
Vol 1’ Chapter 25/ (Hadith) no 384 / 385
(384)Narrated Ibrahim: Hammam bin Al Harith said, “I saw Jarir bin ‘Abdullah urinating. Then he performed ablution and passed his (wet) hands over his Khuffs, stood up and prayed. He was asked abaut it. He replied that he had seen the Prophet doing the same.”
Tafsiri
Imesimuliwa na Ibrahimu; Hammam bin Al Harith alisema, nilimuona Jarir bin‘ Abdallah akiungana na wengine na kisha akatawadha na kupitisha mkono uliolowa maji juu ya viatu vyake, kisha akasimama na kuswali. Alipoulizwa juu ya hilo. Alijibu kwamba alimuona mtume akifanya kitendo kama hicho”.....
(385)Narrated Al –Mughira bin Shu’ba: Ihelped the Prophet in perfoming ablusion and passed his wet hands over his kuhuffs and prayed.
Tafsiri
Imesimuliwa na Al – Mughira bin Shu’ba: nilimsaidia mtume katika kutawadha na ndipo akapitisha mikono yake iliyoloana juu ya viatu vyake na kusali.
Kwajumla haditi zote hizo zinazotambuliwa na kukubalika katika teolojia ya Uislam, zinaweka wazi juu ya hali halisi ya mfumo wa ibada wa mtume Muhammad kuwa desturi yake ilikuwa ni kusali akiwa na aina hiyo ya viatu vyake vinavyotambuliwa kama Khuffu’ hivyo hoja hiyo iko bayana kabisa.
Bwana Yesu / Manabii na Mitume katika farsafa ya ibada na kuvaa viatu.
Nikualike ndugu msomaji wangu tunapolekea ukingoni mwa achambuzi wa mada hii baada ya kujipatia majibu ya msingi juu ya hoja hii ya kusali au kutokusali na viatu.
Katika sehemu hii ya mwisho tutapitia kwa kifupi ili kuona jinsi mitume na manabii walivyotenda huko nyuma kwa habari ya matendo mbalimbali ya kidini na swala hili la uvaaji wa viatu, hii ikiwa ni pamoja na kujibu hoja ya msingi inayohusiana na dhana kwamba huenda panapokuwepo utakatifu basi viatu havipaswi kuwepo.
Hebu kabla hatujaenda mbali turejee kidogo kuangalia matukio machache ya manabii katika uhusiano na swala la uvaa wa viatu.
Ezekieli 24:17
Ugua lakini si kwa sauti ya kusikiwa, usifanye matanga kwaajili yake aliyekufa; jipige kilemba chako; ukavae viatu vyako.....
Katika andiko hilo nabii Ezekieli anaelekezwa na Mungu juu ya kanuni sahihi ya ibada na hapo hoja kuu ilikuwa ni juu ya ibada ya maombolezo, katika maelekezo yake kwa Ezekiel Mungu ana ainisha yaliyo sahihi kufanyika katika ibada hiyo ya maombolezo nay ale yasiyopaswa kufanyika..
Yaliyokatazwa:
- Ugua lakini si kwa sauti ya kusikiwa
- Usifanye matanga kwaajili ya aliyekufa
Yaliyoruhusiwa”
- Jipige kilemba chako ( hiyo ni kadri ya desturi ya Kiyahudi)
- Kavae viatu vyako..
Hivyo kadri ya andiko hilo Mungu mwenyewe ndiye anayetoa maelekezo kwa Ezekieli kumkumbusha kuvaa viatu vyake katika ibada hiyo ya maombolezo, na maelekezo hayo yalifuatia baada ya kumjulisha yasiyopaswa kufanywa katika ibada hiyo ya maombolezo, na hivyo basi tendo la kuvaa viatu linaangukia katika upande ule wa matendo yaliyoruhusiwa kufanywa wakati wa ibada hiyo ya maombolezo, hivyo hakukuwa na shida yeyote ya swala la uvaaji wa viatu mbali na tukio tu la Musa lililolenga kumtawadha kuwa kiongozi wa Israel
Kisa kingine katika Biblia ni kile kinachomhusu nabii Isaya ambaye aliagizwa kutembea akiwa hana viatu tena uchi, ikiwa ni tukio la kidini la kuonya juu ya uovu wa wanadamu na ugumu wao wa kuamini na kutubu, tendo hilo lililohusisha pamoja na kutembea uchi lakini Isaya kutotakiwa kuvaa viatu linatajwa na Biblia kuwa ni tendo la Ishara ya ajabu. ( rejea Isaya 20:3)
Je” eneo lenye utakatifu viatu haviruhusiwi?
Hii ni hoja ya msingi kuiangalia walau kwa kifupi, sababu ya kuangalia hoja hii pamoja na mambo mengine lakini ni tendo la kigezo hiki kuchukuliwa kama ndiyo sababu kuu ya kukaza madai ya kuvua viatu wakati wa ibada.
Lakini katika sehemu hii tutaona kisa kimoja tu kinachotoa jibu zima la hoja hii nacho ni kile kinachohusu tukio la Petro gerezani; hebu tuone kwa kifupi:-
Matendo 12:5-9
- Petro alikuwa amefungwa gerezani..
- Kanisa lilikuwa likomba kwaajili yake..
- Malaika alitumwa kumtoa Petro gerezani..
- Ndipo chumba cha Petro “kikajaa nuru kutoka mbunguni”....
- Akiwa katika nuru hiyo (takatifu) ya mbinguni, Malaika akamwamuru avae viatu vyake kisha amfuate....
Kisa hicho cha Petro kinajibu hoja hiyo bila ya kuacha swali lolote, kadri ya kisa hicho Biblia inaweka wazi kuwa mara Malaika alipoingia tu kwenye chumba cha gereza ndipo nuru ikafurika mle mchumbani, na jambo la kushangaza ni tendo la Malaika katikati ya nuru hiyo anamwagiza Petro kuvaa viatu vyake’ yaani maana yake ni kuwa Petro alivaa viatu hivyo huki akizungukwa na nuru hiyo takatifu aliyokuja nayo Malaika toka mbinguni.
Hivyo hiyo ni kumaanisha kuwa hapakuwa na tatizo lolote juu ya uwepo wa viatu katika nuru hiyo takatifu ya mbinguni iliyofurika katika chumba hicho cha gereza, na kubwa zaidi ni tamko la Malaika lililomtaka Petro kumfuata mara baada ya kumaliza zoezi la kuvaa viatu yaani kwa lugha nyingine ni kuwa Malaika bado aliendelea kumtaka Petro kudumu katika mafuriko ya nuru hiyo akiwa na viatu vyake kwa tendo hilo la kudumu kuambatana naye hadi nje ya gereza hilo.Wito wangu kwa watu wa Mungu bado ni kuwasisitiza kusoma maandiko kwa usahihi, ili kuepuka kuwaondoa wengine kwenye hali ya Mungu.
Kwa ushahidi huo ni wazi hakuna tatizo kuingia na viatu mahala penye utakatifu.
JE, YESU ALIVUA VIATU ALIPO INGIA KWENYE MAHEKALU?
Hakuna ushahidi wa Yesu kuvua viatu katika majengo ya ibada.
Biblia inaonyesha kuwa Yesu alikuwa akivaa viatu na hakuna mahali alipovua viatu hivyo ili kutekeleza kwanza matendo ya ibada, ni vyema ikiwa ni mkristo au hata kama ni Muislam kuzingatia kuwa hoja yoyote unayojenga ikiwa ina lengo la kutaka kuonyesha mapungufu ya Wakristo katika utekelezaji wa maamrisho ya kidini, lazima kwanza hoja hiyo iwe na vyanzo vya kimandiko ikihusisha maelekezo ya kiongozi mkuu wa Ukristo yaani Bwana Yesu mwenyewe.
Rejea; Qur an 5:47
Watu wa injili wahukumu kwa yale aliyotelemsha Mwenyezi Mungu ndani yake, na wasiohukumu kwa (kufuata) yale aliyotelemsha Mwenyezi Mungu basi hao ndio maasi.
Andiko hilo la Qur an linaweka bayana kuwa hukumu zozote dhini ya watu wa Injli zinapaswa kutokana na msingi wa Injili yenyewe, hivyo hii ni kumaanisha kuwa kama swala la kusali na viatu lingekuwa linapingana na msingi wowote wa mafundisho ya Injili ya Yesu basi hoja hiyo ya kusali na viatu ingekuwa sahihi na yenye nguvu.
Hivyo hii ni tofauti na wale wanaohoji leo kuonekana kutokuwa na kipengele chochote cha kusonda jamii ya Wakristo katika hoja hii kuwa kwa tendo la kusali na viatu wamekiuka kanuni Fulani zilizoamriwa na maandiko hayo.
Lakini badala yake tunaona Yesu mwenyewe akiwa na viatu ambavyo hakuna kifungu cha maandiko kinachoonyesha kuwa aliwahi kuvua viatu hivyo kwaajili ya kutekeleza ibada;
Matendo 13:25....Siwezi kulegeza viatu vya miguu yake...
Hitimisho:Nichukue fursa hii mpendwa msomaji wangu kukushukuru kwa kutumia muda wako kufuatilia uchambuzi huu, ni wito wangu endapo hapo nyuma uliyumbishwa kiufahamu juu ya hoja hii sasa usimame imara, na kama huenda hukuwahi kuwa Mkristo na huenda hoja hii ilichangia kusitisha maamuzi yako sasa fungua moyo wako umpokee Yesu.
Biblia inamaliza kwa kusema:
Yeremia 2:25: Zuia mguu wako usikose kiatu......
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 18, 2016

Thursday, March 17, 2016

MUHAMMAD AKIRI KUWA BABA YAKE YUPO MOTONI

Ndugu msomaji,
Huu ni MSIBA MKUBWA sana kwa Waislam. Muhammad ambaye baba yake anaitwa Abdullah ikimaanisha "mtumwa wa Allah" imethibitshwa kuwa yupo Jehanna/motoni akichomeka.
Haya si maneno yangu na wala mimi simsingizii baba ya Muhammad, bali haya ni maneno ya Muhammad.
Soma uthibitisho hapa.
Imeripotiwa na Anas: Hakika, mtu mmoja alisema: Mjumbe wa Allah, baba yangu yuko wapi? Akasema: Yuko motoni. Alipogeuka kuondoka, akamwita na kusema: Hakika baba yangu na baba yako wako Motoni. (Sahih Muslim, Kitabu 001, Namba 0398).
Na swali ambalo tungependa wajiulize Waislam ni kuwa, kwa nini baba yake Muhammad, ambaye alikuwa mpagani aliitwa ‘Abdullah’?
Na kwa kuwa ‘Abdullah’ maana yake ni ‘mtumwa wa Allah’, hii ni ishara ya wazi kwamba wapagani wa kipindi cha jahiliyah walikuwa wakimwabudu Allah hadi kufikia kuwapa watoto wao majina kwa heshima ya Allah – kama ambavyo Wayahudi nao walikuwa wakiwapa watoto wao majina kwa heshima ya Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.
Kwa mfano:
Yoshua – Yahwe ni wokovu;
Yothamu – Yahwe ni mkamilifu;
Yehoahazi – Yahwe ameshikilia;
Hezekia – Yahwe ametia nguvu;
Elisha – Mungu ni wokovu, n.k.
Jibu liko wazi. Allah alikuwa ni mungu wa kipagani aliyeabudiwa kabla ya Uislamu kuja. Na mungu huyu alikuwa ni ‘mungu mwezi’, yaani ‘al-ilah’. Jina lake jingine aliitwa ‘hubal.’ Mungu huyu wa kipagani aliabudiwa kote mashariki ya kati; wala si kwa Waarabu peke yake.
ZAIDI YA HAPO,
1. Kwanini Muhammad anakiri kuwa baba yake yupo Motoni?
2. Je, huyu Abdullah/abdallah alipata wapi hili jina lenye Allah ndani yake?
3. Je, inamaanisha kuwa Allah ambaye ni mungu wa kipagani alikuwepo kabla ya Muhammad?
Na ndiyo maana baba yake Muhammad, yaani Abdullah, alikoswakoswa kuchinjwa na babu wa Muhammad, yaani Abdul Muttalib. Abdul Muttalib alitaka kumchinja mwanawe huyo kama sadaka kwa Allah. Lakini mjomba wake Abdullah akamwokoa na hatimaye walichinjwa ngamia 100 badala yake. Na ifahamike kwamba machinjo hayo yalifanyikia kwenye kaaba (hili tutaliangalia huko mbeleni).
Tunaambiwa kwamba:
Mshale ulionyesha kwamba Abdullah ndiye aliyetakiwa kutolewa kafara. Kwa hiyo, Abdul Muttalib alimchukua yule kijana hadi kwenye Al-Kaaba pamoja na wembe kwa ajili ya kumchinja. Quraish, mjomba wake kutoka kabila la Makhzum na kaka yake Abu Talib, hata hivyo, walijaribu kugeuza mawazo yake. Walipendekeza kwamba amwite mwaguzi wa kike. Huyo aliagiza mishale ya uaguzi ichorwe baina ya Abdullah na ngamia kumi … hatimaye idadi ya ngamia ikafikia mia moja. (Ibn Hisham 1/151-155; Rahmat-ul-lil'alameen 2/89, 90).
Ndiyo maana Mungu wa Biblia alikuwa akiwaonya sana wana wa Israeli juu ya tabia za kipagani za jamii zilizowazunguka kuhusiana na masuala ya kuabudu familia ya nyota au jeshi la mbinguni. Kwa mfano, anasema:
….. tena usije ukainua macho yako hata mbinguni, na ulionapo jua, na mwezi, na nyota, jeshi la mbinguni lote pia, ukashawishiwa na kuviabudu, na kuvitumikia, ambavyo Bwana, Mungu wako amewagawanyia watu wote chini ya mbingu zote. (Kumbukumbu la Torati 4:19).
Ikiwa ameonekana katikati yako, ndani ya malango yako mojawapo, upewayo na Bwana, Mungu wako, mtu mume au mke afanyaye yaliyo maovu machoni pa Bwana, Mungu wako, kwa kuvunja maagano yake, ….. naye amekwenda kutumikia miungu mingine na kuiabudu, au jua, au mwezi, au vilivyo katika jeshi la mbinguni vyo vyote, nisivyoagiza mimi (Kumbukumbu la Torati 17:2-3).
Kwa maana akapajenga tena mahali pa juu alipopaharibu Hezekia baba yake; akamjengea Baali madhabahu, akafanya Ashera kama alivyofanya Ahabu mfalme wa Israeli. Akajiinama mbele ya jeshi lote la mbinguni na kulitumikia. (2 Wafalme 21:3).
Akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni katika behewa mbili za nyumba ya Bwana. (2 Wafalme 21:5).
Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni. (2 Wafalme 23:5).
… nao wataitawanya mbele ya jua, na mwezi, na jeshi lote la mbinguni, walivyovipenda, na kuvitumikia, na kuandamana navyo, na kuvitafuta, na kuviabudu haitakusanywa pamoja tena, wala kuzikwa; itakuwa ni samadi juu ya uso wa nchi. (Yeremia 8:2).
…. na nyumba za Yerusalemu, na nyumba za wafalme wa Yuda, zilizotiwa unajisi, zitakuwa kama mahali pa Tofethi; naam, nyumba zote ambazo juu ya dari zake wamelifukizia uvumba jeshi lote la mbinguni, na kuwamiminia miungu mingine sadaka za kunywewa. (Yeremia 19:13).
…. na wale walisujudiao jeshi la mbinguni juu ya dari za nyumba; na hao waabuduo, waapao kwa Bwana na kuapa pia kwa Malkamu (Zefania 1:5).
Katika mwaka 570 BK, mwaka uleule ambao Muhammad alizaliwa, alikuwapo mtawala mmoja wa dola ya Aksum ya Ethiopia ambaye alikaa Yemen. Huyu aliitwa Abrahah al- Ashram. Inaelezwa kwamba alikuwa na wivu na mji wa Makka kwa jinsi ambavyo watu wengi walikuwa wakienda kuhiji (yaani hija ya kipagani), hivyo na yeye naye akajenga kanisa kubwa kule Sanaa, Yemen akitarajia kuvuta watu wengi, jambo ambalo halikutokea.
Matokeo yake, aliamua kwenda kuvamia Makka kwa lengo la kuiharibu kaaba. Alisafiri na watu wake wengi juu ya kundi kubwa la tembo - ndiyo maana hata mwaka ule ukajulikana kama mwaka wa tembo.
Koo za Kiquresh ziliungana ili kujaribu kuikoa kaaba. Abdul Mutaleb (babu yake Muhammad) aliwaambia watu wakimbilie kujificha milimani wakati yeye na baadhi ya watu walibakia karibu na kaaba.
Lakini kwa sababu ya ukubwa na nguvu ya jeshi la yule Abrahah, Abdul Mutaleb alisema:
Mmiliki wa nyumba hii ndiye atakayekuwa Mlinzi wake, na nina uhakika ataiponya dhidi ya kushambuliwa na maadui na hawatawafedhehesha watumishi wa nyumba yake."
Mapokeo yanasema kwamba wakati Abrahah anasonga mbele kuiendea kaaba, lilitokea kundi kubwa la ndege ambao walianza kumdondoshea mawe kama mvua hadi wakamjeruhi. Hivyo, azma yake ya kuiharibu kaaba haikufanikiwa, badala yake akarudi kwake akiwa ameumizwa.
Sasa, swali ni kuwa, kama wakati ule Muhammad alikuwa bado kichanga, na hivyo Uislamu ulikuwa haujaanza; na pale kwenye kaaba inajulikana kwamba kulikuwa na mamia ya miungu ya kipagani; je, Mmiliki wa Nyumba anayetajwa na Abdul Mutaleb ni nani?
Ni wazi kwamba huyu ni mungu wa kipagani, yaani allah aliyekuwa akiabudiwa na kutumikiwa na Abdul Mutaleb, yaani mungu mwezi.
Na swali kubwa zaidi ni kuwa, Quran inasema katika sura Al-Fil (au Tembo) 105:1-5:
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
Swali ni kuwa:
Mambo haya yalitokea wakati Uislamu haupo, bali ulikuwa ni wakati wa upagani. Mtumishi wa mungu wa kipagani Abdul Mutaleb alisema kwamba Mmiliki wa Nyumba ile (kaaba) angeitetea.
Je, Mmiliki wa nyumba aliyetajwa na Abdul Mutaleb alikuwa yupi na Mola wako anayetajwa na Quran kwenye sura hii ni yupi? Au tuseme kulikuwa na miungu miwili iliyoshirikiana kumpiga mawe Abrahah na tembo wake?
Abdul Mutaleb hakumjua Allah wa Muhammad, kwa hiyo kwa namna yoyote ile hangeweza kumtaja huyo (kama kweli Allah wa Muhammad ni tofauti na wa Abdul Mutaleb).
Mazingira yote yanaonyesha kwamba mungu mwezi, aliyeabudiwa na Abdul Mutaleb ndiye aliyeilinda kaaba dhidi ya tembo wa Abrahah. Kwa hiyo, aya hii ya Quran haina uwezo wa kujinadi kwamba inamtaja mungu tofauti na huyo!!
Kumbe basi Kaaba ni nyumba ya kipagani.
Kumbe basi baba yake Muhammad yupo Motoni.
Kumbe basi Waislam wote wanao enda kuhiji wataingia motoni.
Kumbe basi Allah ni mungu wa kipagani.
Hakika Uislam ni dini ya wapagani ndio maana Muhamamd alikiri kuwa baba yake yupo motoni.
Nawakaribisha kwa Mungu Mkuu aliye hai, YESU MWOKOZI WETU.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 17, 2016

Saturday, March 12, 2016

KUMBE ADAM NA HAWA WALITUMIA LUGHA YA KIEBRANIA NA SIO KIARABU

Ndugu msomaji,
Katika somo letu hili, tutajifunza na kujibu swali kuhusu; ni lugha ipi Adam na Hawa walitumia wakati wakiwa katika Bustani ya Edeni?
Tunaweza kuthibitisha kuwa Adam na Hawa walitumia Kiebrania kwasababu ya majina mawili ambayo Adam alimpa Hawa ambayo yanaweza kuwa yakinifu pekee katika lugha ya Kiebrania. Adam alimuita Hawa jina la “ISHA” ikiwa na maana ya MWANAMKE kwasabau ya kuwa alitoka kwa “ISH” ikiwa na maana ya MWANAUME , zaidi ya hapo, Adam alimuita mkewe “CHAVA” [HAWA] ikiwa na maana ya mama wa watu wote “CHAI” [UHAI].
Zaidi ya hapo, jina la ADAM linatokana na neno la Kiebrania “ADAMAH” likimaanisha “udongo”, hili jina linathibitisha kuwa Mungu alimuumba Adam kutoka kwenye udongo, kama ambavyo Biblia inasema katika Kitabu cha Mwanzo Mlango 2 na aya ya 7. Hivyo basi, tokea wakati wa Adam na Hawa mpaka wakati wa Mnara wa Babeli, watu wote walitumia lugha ya Kiebrania. Bereshet 2:23, 3:20, Midrash Bereshet Rabbah 38
Wasomi wa Kiyahudi na wa Kikristo wanaendelea kuthibitsiha kuwa Lugha ya Kiebrania ndio ilikuwa lugha ya kwanza, na majadiliano makali yalifanywa zamani na watafiti kama Dante Alighierl (1265-3121), Guillaume Postel (1510-1581) Claude Duret (1570-1611), Etienne Guichard (wakati huo huo wa ATHANASIUS Kircher (1602-1680) na Franciscus Mercurius van Helmont (1614-1698) wana sema kuwa, lugha ya Kiebrania ndio ilitumika na Adam na Hawa. Kwa mfano Mtaalam Guichard alisema kuwa neno la Kilatini “divider” likimaanisha tenganisha au kutenganisha limetokana na neno la Kiebrania la “batar” likimaanisha kukata katika sehemu mbili, hili neno lilifanana na la “tarab” ambalo lilikuja neno la Kilatini la “tribus” likimaanisha “kabila “tribe”
Hebu tuangalie ushahid mchache kutoka Biblia:
Matendo ya Mitume 26:14 Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya KIEBRANIA, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo.
Yohana 19: 17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa KIEBRANIA, Golgotha.
Matendo ya Mitume 22: 2 Waliposikia kwamba anasema nao kwa lugha ya Kiebrania wakazidi kunyamaza; akasema,
Kutoka 2:6 Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, mtoto yule analia. Basi akamhurumia, akasema, Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.
Katika kitabu cha Kutoka hapo juu, tunajifunza kuwa MUSA ANAITWA MTOTO WA KIEBRANIA “Eevriym in Hebrew” na katika kipindi chote watoto wa Kiisraeli waliitwa kama WAEBRANIA ambao ni watoto au wajukuu wa Ibrahim na Musa. Soma Mwanzo 10:24. Zaidi ya hapo, katika kitabu cha Mwanzo 14:13 tunasoma kuwa Ibrahim anaitwa Muebrania (Eevriy in Hebrew).
Huu ni ushahid tosha kuwa Lugha ya Mungu kwa Adam na Hawa ilikuwa ni Kiebrania na sio Kiarabu au lugha nyengine.
Je, Kwanini Mungu alitumia Kiebrani alipo zungumza na Adm na Hawa?
Kwanini Adam na Hawa walitumia Kiebrania walipo kuwa katika Bustani ya Edeni?
Hapa pana hitaji ufunuo wa hali ya kuu kufahamu kwanini Mungu alitumia lugha ya Kiebrania ambayo ni tofauti kabisa na Allah anaye tumia Kiarabu tu.
Kumbe sababu za Allah kutumia Kiarabu ni kupinga Mungu wa Biblia ambaye alitumia Kiebrani na kuwapinga Waisraeli ambao waliitwa wana wa KIEBRANIA.
References:
1. Merrill F. Unger, "Tower of Babel," Unger's Bible Dictionary, 1977 ed.: 115. (BCE - Before the Common Era, equivalent to BC)
2. J.I. Packer, Merril C. Tenney, William White, Jr., Nelson's Illustrated Encyclopedia of Bible Facts (Nashville: Thomas Nelson, 1995) 337.
3. Madelene S. Miller and J. Lane Miller, "Sumer," Harper's Bible Dictionary, 1973 ed.: 710.
4. Unger, "Scythian," 987.
5. Unger, "Egypt," 288.
6. William Smith, "Hebrew Language," Smith's Bible Dictionary, 1948 ed.: 238.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 12, 2016

DINI NA MADHEHEBU NI MZIGO USIO WA LAZIMA


MAANA YA DINI
Kamusi ya Kiswahili Sanifu (Oxford: 2004) inaeleza neno ‘dini’ kama mfumo fulani wa imani inayohusiana na mambo ya kiroho na njia ya kuabudu, kusali au kuheshimu/kutii Muumba.

Kwa hiyo tunaweza kusema kwa kifupi kwamba, dini ni utaratibu anaotumia mwanadamu katika kumwabudu Mungu.

Zipo dini mbalimbali duniani. Japokuwa zote zinaweza kusema zinamwabudu Mungu aliyeumba vitu vyote, lakini kile kinachozitofautisha ni “utaratibu” zinazotumia katika huko kumwabudu Mungu – ndiyo sababu zikawa ni dini au madhehebu mbalimbali.

Utaratibu maana yake ni kanuni mahususi zinazotakiwa kufuatwa katika kufanya jambo fulani. Mathalani, unapotaka kujiunga na chuo, utatakiwa kulipa gharama za usajili, kujaza fomu, kufanya hivyo katika muda maalum, kuwasilisha maombi yako kwenye ofisi maalum, nk. Hali kadhalika kwa upande wa dini, ili muumini ahesabike kuwa ametekeleza ibada kwa Mungu, upo utaratibu au kanuni mbalimbali zinazotakiwa kufuatwa. Kanuni hizo ni pamoja na:
Kusema sala maalum;
Kusema sala mara idadi maalum;
Kusimama au kukaa kwa wakati maalum;
Kuvaa mavazi maalum;
Kutazama welekeo maalum; n.k.

YESU ALIANZISHA DINI GANI?
Ukisoma Biblia kwa makini, utagundua kwamba Yesu Kristo hakuanzisha Ukristo kama dini au madhehebu. Wakati Bwana Yesu alipokuja, kulikuwa na dini ya Kiyahudi (Judaism). Hii ni dini ambayo ilikuwa na utaratibu wake wa kumwabudu Mungu kama ilivyo kawaida ya dini yoyote kuwa na utaratibu.

Lakini ni wazi kwamba, Bwana Yesu hakukubalika kabisa ndani ya dini hii. Walikuwa ni wakuu wa dini hiyohiyo ndio waliomshitaki Bwana na kuwachochoea watu wa kawaida waanze kupiga kelele za kusema: asulubiwe, asulubiwe! Kati ya mashtaka yao, walisema: Sisi tulimsikia akisema, Mimi nitalivunja hekalu hili lililofanyika kwa mikono, na katika siku tatu nitajenga jingine lisilofanyika kwa mikono. (Mk. 14:58).

Lakini ni kwa nini walikuwa hawamtaki? Ni kwa sababu alikuwa anaonekana anavunja utaratibu wa dini. Pia ni kwa sababu alionekana kujizolea umaarufu mwingi kuliko wakuu wa dini. Kwa hiyo, waliona kwamba nafasi zao ziko hatarini. Kwa hiyo, walimchukia na kumtungia hila nyingi ili waweze kupata sababu ya kumwua.

Tunaona jambo hilohilo hata baadaye katika huduma ya mtume Paulo. Kabla ya kuokoka, Paulo alikuwa ni mshika dini ya Kiyahudi. Yeye mwenyewe anasema kwamba: Nami naliendelea katika dini ya Kiyahudi kuliko wengi walio hirimu zangu katika kabila yangu, nikajitahidi sana katika kuyashika mapokeo ya baba zangu. (Gal. 1:14).

Lakini pale alipoitwa na Bwana Yesu kwenye huduma, mambo yaligeuka kabisa. Wayahudi walitafuta kumwua Paulo kwa sababu waliona kwamba tayari yuko kinyume na dini yao. Mathalani, Paulo alipokuwa ameshikiliwa na utawala wa Kirumi, mjomba wa Paulo alienda kumwambia jemadari wa Kirumi kwamba: ...Wayahudi wamepatana kukuomba umlete Paulo chini kesho, ukamweke mbele ya baraza, kana kwamba wanataka kupata habari zake kwa usahihi zaidi. Basi wewe usikubali; kwa maana watu zaidi ya arobaini wanamwotea, wamejifunga kwa kiapo wasile wala wasinywe hata watakapomwua; nao sasa wako tayari wakitazamia ahadi kwako. (Mdo. 23:20-21).

Na ndiyo maana baadaye Paulo anasema: Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumwa wa Kristo. (Gal. 1:10).

Hapa Paulo anamaanisha kwamba, kabla ya kumjua Kristo alikuwa ni mshika dini tu ambapo wakati huo uhusiano wake na washika dini ulikuwa wa amani kabisa. Lakini baada ya kuachana na dini, ndio maana wakamchukia. Na anasema sasa, kama angekuwa bado anawapendeza wanadamu wale washika dini, basi asingekuwa anateseka hivyo kwa ajili ya Kristo.

Mtume Paulo anaonyesha kwamba kutoka kwenye dini kwa ajili ya Kristo kuna neema kubwa. Anasema: Lakini Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu, akaniita kwa neema yake, alipoona vema kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili niwahubiri mataifa habari zake. (Gal. 1:15-16).

Kumbe Mungu anaita dini kuwa ni mapokeo ya mababa (Gal. 1:14). Na kumbe, alipomwita Paulo katika huduma, hakutaka Paulo abakie tena humo ndani ya dini. Na kwa kuwa sasa Paulo alitoka nje ya dini, alijikuta akizalisha maadui wengi sana.

Watu waliokuwa wakimpinga Bwana Yesu na wale waliompinga Paulo hawakuwa wakitetea maslahi ya kisiasa, bali walikuwa wakitetea dini yao.

Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ

Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction ...

TRENDING NOW