Saturday, July 2, 2016

KWANINI ALLAH AMBAE SIO YEHOVA ALIOGOPA KUYAAMRISHA MAJINI YAISIKILIZE TAURAT, ZABUR NA INJILI?


ALLAH ANASEMA KUWA MAJINI MACHAFU YALITUMWA KWA MUHAMMAD ILI KUSIKILIZA QURAN
ALLAH HUYO HUYO ALISEMA KUWA KILA WATU WALIPEWA KITABU CHAO. HAPO TEYARI KUNA SHAKA KWENYE QURAN YA MUHAMMAD AMBAYO SASA INAKABIDHIWA MAJINI MACHAFU.
Allah kasema katika Suratil Ahqaaf aya ya 29 mpaka 32, “
]وَإِذْ صَرَفْنَا إِلَيْكَ نَفَرًا مِنْ الْجِنِّ يَسْتَمِعُونَ الْقُرْآنَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوا أَنْصِتُوا فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوْا إِلَى قَوْمِهِمْ مُنْذِرِينَ * قَالُوا يَا قَوْمَنَا إِنَّا سَمِعْنَا كِتَابًا أُنْزِلَ مِنْ بَعْدِ مُوسَى مُصَدِّقًا لِمَا بَيْنَ يَدَيْهِ يَهْدِي إِلَى الْحَقِّ وَإِلَى طَرِيقٍ مُسْتَقِيمٍ * يَا قَوْمَنَا أَجِيبُوا دَاعِي اللَّهِ وَآمِنُوا بِهِ يَغْفِرْ لَكُمْ مِنْ ذُنُوبِكُمْ وَيُجِرْكُمْ مِنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ * وَمَنْ لا يُجِبْ دَاعِي اللَّهِ فَلَيْسَ بِمُعْجِزٍ فِي الأرْضِ وَلَيْسَ لَهُ مِنْ دُونِهِ أَولِيَاءُ أُوْلَئِكَ فِي ضَلالٍ مُبِينٍ[
Maana yake, “Na (wakumbushe) wakati tulipowaleta kundi la Majini kuja kwako kusikiliza Qurani. Basi walipoihudhuria walisema (kuambiana): “Nyamazeni! (Msikilize maneno ya Mwenyezi Mungu)” Na ilipokwisha somwa walirudi kwa jamaa zao kwenda kuwaonya. Wakasema “Enyi watu wetu! Sisi tumesikia Kitabu kilichoteremshwa baada ya (Nabii) Musa, kinachosadikisha yaliyokuwa kabla yake na kinachoongoza kwenye haki na kwenye njia iliyonyooka. Enyi kaumu yetu! Muitikieni Mlingani, (Muitaji) wa Mwenyezi Mungu na muaminini, atakusameheni (Mwenyezi Mungu) dhambi zenu na atakukingeni na adhabu iumizayo. Na wasiomuitikia Muitaji wa Mwenyezi Mungu, basi hao hawatamshinda (asiwapate) hapa katika ardhi, wala hawatakuwa na walinzi mbele Yake. Hao wamo katika upotofu ulio dhahiri.”
Na kisa kingine ni cha Majini waliosikia Qurani kutoka kwa Mtume S.A.W wakati alipokuwa akiwasalisha Masahaba wake Sala ya Alfajiri. Na hii ilikuwa bila ya yeye kuwa na habari mpaka Mwenyezi Mungu S.W.T. alipomjulisha. Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil Jin aya ya 1 na ya 2, “
]قُلْ أُوحِيَ إِلَيَّ أَنَّهُ اسْتَمَعَ نَفَرٌ مِنْ الْجِنِّ فَقَالُوا إِنَّا سَمِعْنَا قُرْآنًا عَجَبًا * يَهْدِي إِلَى الرُّشْدِ فَآمَنَّا بِهِ وَلَنْ نُشْرِكَ بِرَبِّنَا أَحَدًا[
Maana yake, “Sema: “Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la Majini lilisikiliza (Qurani) likasema: “Hakika sisi tumesikia Qurani ya ajabu. Inaongoza katika uwongofu; kwa hivyo tumeiamini, wala hatutamshirikisha yeyote tena na Mola wetu.”
Makala haya yametolewa katika kitabu changu kiitwacho, "Hakika ya Majini."
MASWALI KUHUSU MAJINI:
1. Wapi katika Taurat tunajifunza kuwa Majini yaliumbwa ili kumwabudu Mungu?
2. Wapi katika Zaburi Tunafundishwa kuwa Majini yaliumbwa ili ya mwabudu Mungu?
3. Wapi katika Injil tunafundishwa kuwa Majini yaliumbwa ili kuwamudu Mungu?
JE, BIBLIA INASEMA NINI KUHUSU MAJINI?
Biblia Inasema nini kuhusu uhusiano na Mapepo au Majini
Mungu ametuonya kutokuwa na uhusiano na pepo. Imeandikwa, Mambo ya Walawi 19:31 "Msiwaendee wenye pepo wala wachawi, msiwatafute ili kutiwa unajisi na wao mimi ndimi BWANA Mungu wenu."
Ilikuwa kawaida ya watu wa zamani enzi za Biblia kusali pepo. Mungu aliwaonya wana wa Israeli kuhusu uombaji wa pepo na uchawi. Imeandikwa katika Kumbukumbu la torati 18:9-12 "utakapokwisha ingia katika nchi akupayo BWANA Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto wala asionekane mtu atazamaye mbao wala mtu atazamaye nyakati mbaya wala mwenye kubashiri wala msihiri wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo wala mtu apandishaye pepo wala mchawi wala mtu awaombaye wafu kwa maana mtu atandaye hayo ni chukizo kwa BWANA kisha ni kwa sababu ya hayo BWANA Mungu wako anawafukuza mbele yako."
Biblia yatupa mwanga kuhusu hali ya pepo. Imeandikwa, katika Matendo ya mitume 16:16-18 "Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua akamfuata Paulo na sisi akipiga kelele akisema watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye juu wenye kuwahubiria njia ya wokovu akafanya hayo siku nyingi lakini Paulo akasikitika akageuka akamwambia yule pepo nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo mtoke huyu akamtoka saa ili ile."
Pepo ni wale malaika waliomwasi Mungu kule mbinguni na kutupwa hapa duniani. Imeandikwa katika Ufunuo 12:7-9 "Kulikuwa na vita Mbinguni Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa yule mkubwa nyoka wa zamani aitwaye Ibilisi na Shetani adanganyaye ulimwengu wote akatupwa hata nchi na malaika zake wakatupwa pamoja naye."
Kwa sababu pepo za husiana na Shetani, mtu katika israeli angeonekana akifanya pepo ilibidi auawe. Imeandikwa, katika Mambo ya walawi 20:27 "Tena mtu mme au mke aliye na pepo au aliye mchawi hakika atauawa watawapiga kwa mawe damu ya itakuwa juu yao." Isaya 8:19 yasema "Na wakati watakapokuambia tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndeye na kunong'ona je haiwabasi watu kutafuta habari kutoka kwa Mungu waoje! waende kwa watu walio kufa kwa ajili ya watu walio hai?."
JILINDE DHIDI YA MAJINI NA SHETANI
Unaweza kujilinda jinsi gani dhidi ya roho waovu-Majini-Mapepo-Mashetani? Biblia inajibu hivi: “Jitiisheni kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.” (Yakobo 4:7) Tunatii agizo hilo tunapoishi kupatana na mafundisho yaliyo katika Biblia, kitabu pekee kitakatifu ambacho kinamfichua Shetani, roho waovu, na “hila” zao. (Waefeso 6:11; 2 Wakorintho 2:11) Pia, Biblia inatuambia kwamba roho waovu pamoja na wote wanaompinga Mungu, hawatakuwapo milele. (Waroma 16:20) “Wanyoofu ndio watakaokaa duniani, na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake,” inasema Methali 2:21.
JE, UMEJIULIZA HIVI?
● Je, Mungu ndiye aliyewaumba roho waovu?—2 Petro 2:4.
● Je, unaweza kuzungumza na wafu?—Mhubiri 9:5, 6.
● Unaweza kujilinda jinsi gani dhidi ya roho waovu?—Yakobo 4:7.
Katika Huduma yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

MUHAMMAD ASEMA: TUMIENI MAWE MATATU KUJISAFISHA BAADA YA HAJA KUBWA


Ndugu msomaji.
Waislam wanasema kuwa eti, Uislam ni muongozo kamili wa maisha. Hakika mimi siutaki huu muongozo wa utumiaji mawe.
Soma:
Baada ya kujisaidia haja kubwa, usitumie mifupa au kinyesi kujisafisha; Bali utumie mawe kujisafisha mwenyewe ... (Sahih Bukhari, 1.4.157)
Utakapo maliza kujisaidia, tumia mawe Matatu kujisafisha sehemu zako za siri ... (Sahih Bukhari, 1. 4.162)
Tumia mawe tatu kwa kujisafisha baada ya kujisaidia ... (Sunaan Abu Dawud, 1.0040)
Baada ya kutembelea choo, beba mawe matatu na uyatumie kujisafisha wewe mwenyewe ... (Sunaan Abu Dawud, 1.1.0040)
Baada ya kujisaidia haja kubwa, tumia udongo mara mbili kujisafisha; wala usitumie kinyesi kujisafisha... (Sunaan Nasai, 1.42)
Kama unajisaidia haja kubwa katika jangwa, basi tumia mawe matatu kujisafisha baada ya haja kubwa, hakuna haja ya kutumia maji ... (Sunaan Nasai, 1.44)
HUU NI MSIBA MKUBWA SANA KWA NDUGU ZETU WAISLAMU WANAO TUMIA MAWE.

MAISHA BAADA YA KIFO


1. WAISLAM KWENDA JEHANNAM
2. WAKRISTO KUINGIA MBINGUNI
3. WAPAGANI NA WASIO NA DINI KUINGIA JEHANNAM
4. MAJINI NA MASHETANI YOTE KUINGIA JEHANNAM
Je, unaamini kwamba kuna wakati wa hukumu baada ya binadamu kukutwa na mauti?
Ndugu Msomaji,
Nivyema ufahamu nini kitakutokea punde utakapo kata roho/kufa. Swali la muhimu la kujiuliza ni hili hapa: Je, unauhakika wa wapi utakuwa baada ya kifo?
Biblia inatuambia ya kuwa baada ya mtu kufa, hupelekwa mbinguni ya Muda “Peponi” (Sio Mbingu ambayo Mungu yupo sasa ila ni –Abraham’s bosom) au Jehanamu “kuzimuni ya muda-Akhera” kulingana na hoja ya kuwa alikuwa amemkubali ama kumkataa Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wake/wako. Kwa walioamini, kufa ni kuondoka katika mwili na kuenda kukaa na Bwana “to be absent from this body is to be present with the Lord” (Wakorintho wa pili 5:6-8; Wafilipi 1:23). Kwa wasioamini, kufa ina maana ya hukumu ya milele Jehanamu (Luka 16:22-23).
Hapa ndipo kwenye utata juu ya ni nini hufanyika baada ya kifo. Kitabu cha Ufunuo Sura 20:11-15 inaeleza juu ya wale walio kuzimu wakitupwa katika ziwa la moto. Ufunuo 21 na 22 inazungumzia juu ya mbingu mpya na dunia mpya. Kwa hivyo ina maana ya kuwa mpaka wakati wa ufufuo wa mwisho, baada ya kufa mtu hubaki katika mahali Fulani kwenye mfano wa mbinguni na kuzimu. Mahali pa mtu anapofaa kukaa milele hapatabadilika ila makazi ya muda yatabadilika “NI KAMA MAHABUSU, HALAFU MTU ANAPELEKWA JELA/ACHIWA”. Muda Fulani baada ya kufa, waumini watapelekwa katika mbingu mpya na nchi mpya (ufunuo wa Yohana 21:1) na wasioamini katika ziwa la moto (ufunuo 20:11-15). Haya ndiyo makao ya milele ya watu yanayotegemea kama mtu alimwamini Yesu Kristo pekee kwa wokovu kutokana na dhambi zake.
Wakati sisi hufa, sisi hupatana na hukumu ya Mungu (Waebrania 9:27). Kwa waumini, kuwa mbali na mwili ni kuwa pamoja na Bwana (2 Wakorintho 5:6-8; Wafilipi 1:23). Kwa makafiri kifo kinamaanisha adhabu ya milele katika jehanamu (Luka 16:22-23). “Makafiri ni wale walio kataa kuwa Yesu ni Mungu”
Mpaka kufufuka kwa mwisho, hata hivyo, kuna Mbinguni ya muda- Peponi (Luka 23:43, 2 Wakorintho 12:04) na kuzimuni ya muda-ahera (Ufunuo 1:18; 20:13-14). Kama inavyoweza kuonekana wazi katika Luka 16:19-31, katika Peponi wala katika Akhera watu hawalali. inanaweza semekana kuwa, mwili wa mtu "unalala" huku nafsi yake ikiwa peponi au kuzimuni. Wakati wa ufufuo, mwili huu "utaamshwa" na kubadilishwa hadi mwili wa milele mtu atamiliki milele, hata kama ni mbinguni au kuzimu. Wale ambao walikuwa katika peponi watapelekwa mbingu mpya na nchi mpya (Ufunuo 21:1). Wale ambao walikuwa katika kuzimu kutupwa katika ziwa la moto (Ufunuo 20:11-15). Hizi ndizo hatima za mwisho na milele ya watu wote ikitegemea ikiwa mtu aliamini katika Yesu Kristo kwa ajili ya wokovu au la.
Zaidi ya hapo, Bibilia inatuambia yakwamba sio maisha pekee tu baada ya kifo, bali kuna uzima wa milele wenye utukufu mwingi “Hakuna jicho limeshaona, wala sikio kuyasikia, wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao’’ (1Wakorintho 2:9) Yesu Kristo, Mungu katika mwili, alikuja duniani kutupa karama ya uzima wa milele. “Alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona’’ (Isaya 53:5).
YOHANA 14:1-3"Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo , ningaliwaambia ; maana naenda kuwaandalia mahali.Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali , nitakuja tena nitawakaribishe kwangu ; ili nilipo mimi, nanyi mwepo"
Je kuna haja ya kuogopa kifo??
“Yesu akamwambia, mimi ndiye huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi ajapokufa, atakuwa anaishi, naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je Unayasadiki hayo?” – John 11:25-26
Je, unaamini kwamba kuna maisha baada ya kifo?
Je, unaamini kwamba kuna wakati wa hukumu baada ya binadamu kukutwa na mauti?
Ikiwa ndivyo, hii ina maanisha kwamba binadamu anaishi baada ya kuondokana na mazingira ya duniani?
Je, anaishije huko?
Anakula, anakunywa, anatembea, anaongea au anasikia?
Vipi ana mwili wa nyama au roho?
Kama roho basi, ataunguaje motoni siku ya hukumu?
Maisha ya duniani ya sasa ni mtihani tu; ni matayarisho ya yale yajayo. Kwa waaminio, huu ni uzima wa milele kuweko mbele za uwepo wa Mungu. Basi ni kwa jinsi gani tunafanyinyika wenye haki na kustahili kupokea uzima huu wa milele?
YESU NDIO NJIA PEKEE YA UZIMA WA MILELE:
Kuna njia moja pekee – kupitia imani na tumaini ndani ya Mwana wa Mungu, Yesu kristo. Yesu alisema, “mimi ndimi huo ufufuo na uzima. Waniaminio mimi wajapokufa wataishi. Wanapawa uzima wa milele kwa kuniamini mimi na hawatapotea…” (Yohana 11:25-26).
Kipawa hiki cha uzima wa milele kinapatikana na ni bure kwa wote lakini kinagharimu kujikana wenyewe raha Fulani za dunia na kutoa sadaka kwa Mungu. “na wote wamwaminio mwana wa Mungu wana uzima wa milele. Wasiomtii Mwana hawatapata uzima wa milele bali ghadhabu ya Mungu inadumu juu yao” (Yohana 3:36).
BAADA YA KUFA HAKUNA NAFASI YA PILI YA KUTUBU:
Hatutapatiwa nafasi ya kutubu dhambi zetu baada ya kufa kwa kuwa tukimuona Mungu uso kwa uso hatutakuwa na lengine ila kumwamini. Anatutaka tumjilie sasa kwa imani na upendo. Tunapokubali kwamba kifo cha Yesu Msalabani ni malipo kamili ya dhambi zetu dhidi ya Mungu, tumeahidiwa si tu maisha mema duniani bali pia uzima wa milele mbele ya Kristo.
JEHANNAM:
Jehanamu, kama vile mbinguni, si mahali patajwapo kwa utisho tu bali ni mahali dhahiri. Hapa ni mahali ambapo wasiohaki watakutana na ghadhabu isiyokoma ya Mungu. Watavumilia mateso ya kihisia, kiakili, na kimwili wakiwa katika akili zao timamu huku wakijihisi kuaibika na kujuta kwa matendo yao maovu.
Jehanamu inaelezewa kama shimo la giza (Luka 8:31, Ufunuo wa Yohana 9:1), na Ziwa la Moto, liwakalo na kiberiti ambapo watakao kuwemo watateswa usiku na mchana milele na milele (Ufunuo 20:10). Huko kutakuwa na kulia na kusaga meno, ikiashiria machungu makali na hasira (Mathayo 13:42). Hapa ni mahali ambapo mdudu hatakufa wala makaa kuzimika (Marko 9:48). Mungu hafurahishwi na kufa kwa mtu muovu, lakini hutaka wazighairi njia zao mbaya ili waishi (Ezekiel 33:11). Lakini hatatulazimisha kumkubali; tukiamua kumkataa yeye. Hana budi kutupatia tulilolichagua – kuishi mbali naye.
Je unaamini kuwa kunayo maisha baada ya kifo?
Ni nini hufanyika baada ya kufa?
Je! Unaamini kuwa Jahannamu ni kitu cha kweli? Jehannamu ni ya milele?
Je, kuna ngazi mbalimbali za mbinguni?
Je, kuna viwango tofauti vya adhabu jehanamu?
Basi ungani nami katika kijarida kijacho kuhusu Maisha ya Milele.
Mungu awabariki sana,
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo
For Max Shimba Ministries Org.

MUHAMMAD AKIRI KUWA YEYE NI NABII WA UONGO NA BANDIA



Muhammad alikiri kuwa yeye hakuwa na uwezo wa kufanya Miujuza
Ndugu zanguni, leo ningependa tusome kidogo kuhusu huyu Muhammad aliye dai kuwa yeye katumwa na Mungu. Hebu soma kwanza:
17. SURA AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
90. Na walisema: Hatutakuamini mpaka ututimbulie chemchem katika ardhi hii.
91. Au uwe na kitalu cha mitende na mizabibu, na utupitishie mito kati yake ikimiminika.
92. Au utuangushie mbingu vipande vipande kama ulivyo dai; au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika uso kwa uso.
93. Au uwe na nyumba ya dhahabu, au upae mbinguni. Wala hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie kitabu tukisome. Sema: Subhana Rabbi, Ametakasika Mola wangu Mlezi! Kwani mimi ni nani isipo kuwa ni mwanaadamu na Mtume?
(Qur-Sura 17:90-93)
Baada ya kuombwa afanye angalau muujiza mmoja tu, Muhammad alishindwa vibaya sana na kuto fanya hata muujiza mmoja.
Swali:
1. Kwanini Muhammad alishindwa kufanya miujiza kama alivyo ombwa afanye?
2. Muhammad ni Nabii peke yake alieshindwa kufanya Miujiza tokea dunia iumbwe, Je, anafaa kufuatwa na kuaminiwa?
3. Kwanini Allah nayeye hakumsaidia Nabii wake kufanya muujiza?
HAKIKA MUHAMMAD ALIKUWA NABII WA UONGO

JE, YESU ALITUMWA KWA ISRAEL PEKE YAKE?


Waislamu “wanahubiri” kuwa Yesu hakuja kwa ajili ya ulimwengu wote bali alikuja kwa ajili ya Wayahudi peke yao. Kisha wanasema kuwa Muhammad ndiye mtume sahihi kwa sababu huyo alikuja kwa ajili ya ulimwengu wote. Andiko wanalotumia kupinga utume wa Yesu kwa ulimwengu ni lile alilolisema Yesu wakati akiongea na mwanamke Mkananayo (yaani asiye Myahudi), ambaye alikuwa anaomba Yesu amponye mwanawe.
Imeandikwa:
Akajibu akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. (Mathayo 15:26).
Mungu ni Mungu wa utaratibu na ratiba kamili. Ndiyo maana hakuumba kila mtu kwa mara moja. Alianza na mtu mmoja tu, kisha wengine wote tukatokea kwa huyo mtu. Vivyo hivyo, alianza kwa kujifunua kwa taifamoja tu duniani kote. Kisha kutokea hapo ndipo wokovu unasambaa kwenye mataifa yote. Ni ukweli ulio wazi kwamba, ukiacha Israeli, jamii zote zilizobakia duniani, kwa asili zilikuwa zikiabudu miungu (yaani mashetani). Ni Israeli peke yao ndio ambao kwa asili walianza na Mungu wa kweli.
Ndiyo maana Bwana Yesu alipoongea na mwanamke Msamaria pale kisimani alimwambia hivi:
Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi. (Yohana 2:22).
Wokovu unatoka kwa Wayahudi kwa sababu hakuna taifa jingine lolote duniani ambalo lilimjua Mungu wa kweli – yote yalikuwa na dini za kipagani – iwe ni wazungu, Waafrika, Wahindi, Waarabu, n.k. Huo ndio ukweli.
Kusema kwamba Yesu hakuja kwa ajili ya mataifa yote hakuna tofauti na kusema kuwa, kwa vile Mungu alimuumba Adamu na Hawa peke yake, basi Yeye si wa familia yangu maana hakuniumba na mimi kama alivyomuumba Adamu.
Yesu aliongea na wanafunzi wake siku moja na akawaambia kuwa:
Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanzia tangu Yerusalemu. (Luka 24:46-47).
Je, unaona kwamba Injili inatakiwa kuanzia Yerusalemu? Na je, unaona pia kwamba anasema kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake? Je, mataifa yote ni Israeli peke yake?
Mwanamke Mkananayo alikuja wakati usio wake. Huo ulikuwa ni wakati wa kuhubiri Injili kwa Israeli kwanza ndipo iende ulimwenguni kote.
Ufuatao ni ushahidi zaidi wa maneno ya Bwana Yesu mwenyewe kuthibitisha kwamba alitumwa kwa mataifa yote ulimwenguni na kwamba Yeye ndiye Masihi wa Mungu, yaani aliyepakwa mafuta kwa Roho Mtakatifu kwa ajili ya kuukomboa ulimwengu wote.
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katikaYerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi. (Matendo 1:8).
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu (Mathayo 28:19).
Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. (Yohana 3:17).
Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu. (Yohana 12:47).
Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo. na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja. (Yohana 10:15-16).
Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja. (Mat 24:14).
Nihitimishe kwa kurejea tena mambo machache niliyoyasema. Mungu amekuwa na kawaida ya kuanza jambo na mtu mmoja.
Aliumba mwanadamu mmoja, kisha tukatokea humo wote.
Alijifunua kwa taifa moja, kisha tukamjua wote.
Alianza na Mwana mmoja (Yesu), kisha tunazaliwa wote kwa imani katika huyo.
Vivyo hivyo, alileta wokovu kwa taifa moja la Israeli, kisha unasambaa kote – ndiyo maana anasema na mwanamke Msamaria pale kisimani – “Wokovu watoka kwa Wayahudi.” (Yohana 4:22).
Hali hii ya kuanza na mtu au sehemu moja, ni ushahidi kuwa wale wote wanaojifariji kwa maneno eti “dini mbalimbali ni njia tofauti ambazo zote zinaishia kwa Mungu”, wanajidanganya na kupoteza muda wao na uzima wao wa milele! “Wokovu watoka kwa Wayahudi” – yaani KWA YESU PEKEE!
Sasa, kwa kuwa muda wa kusambaa kwa wokovu huo ulikuwa haujatimia (maana Mungu anakwenda kwa ratiba ya majira na nyakati), ndiyo maana akamwambia yule mwanamke Mkananayo (yaani asiye Myahudi) kuwa hakutumwa ila kwa Israeli.
Lakini utimilifu wa majira ulipofika, yaani alipokufa na kufufuka, tunaona akiwaagiza sasa mitume wake waende ulimwenguni kote.
Na Biblia inasema wazi: Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwambazamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono; kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani. Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo. Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga. Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani. Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba. (Waefeso 2:11-16).
Tafakari
Hoji mambo
Jiulize
Chukua hatua

YESU NI MWANA WA MUNGU MAANA YAKE NINI?



Wanadhuoni wa Kiislam pamoja na waumini wa dini ya Kiislam huwa wanauliza na kusema kwa Wakristo yafuatayo:
1. Kivipi Yesu ni Mwana wa Mungu?
2. Mungu atakuwaje na Mwana bila ya Mke?
KIVIPI YESU NI MWANA WA MUNGU?
Yesu Kristo si Mwana wa Mungu kulingana na ubaba wa kawaida wa binadamu, nikimaanisha kuwa Mungu hakuoa na kupata mwana wa kiume. Nikiwa na maanisha kuwa, Mungu hakufanya tendo la ndoa na Mariamu, na pamoja naye kuzaa mtoto wa kiume ambaye anaitwa Yesu, la hasha.
1 YOHANA MLANGO 5 aya 1 Kila mtu aaminiye kwamba Yesu ni Kristo amezaliwa na Mungu. Na kila mtu ampendaye mwenye kuzaa, ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye.
MUNGU ATAKUWAJE NA MWANA BILA YA MKE?
Yesu ni Mungu katika hali kwamba ni Mungu anajithirihisha kama mwili. (Yohana 1:1, 14) Yesu ni mwana wa Mungu kwa dhana kwamba Mariamu alipata mimba kupitia Roho Mtakatifu ambaye ni Mungu. Luka 1:35 yasema, “Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, MWANA WA MUNGU.”
Mariamu aliambiwa na Malaika kuwa, Mtoto atakaye zaliwa atakuwa Matakatifu na ataitwa MWANA WA MUNGU. Huu ushahidi upo kwenye Luka 1:35.
YESU AKUBALI KUWA YEYE NI MWANA WA MUNGU MBELE YA KUHANI MKUU
Wakati wa kujaribiwa kwake mbele ya viongozi wa Kiyahudi, kuhani mkuu alimtaka Yesu, “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, MWANA WA MUNGU” (Mathayo 26:63). [NOTE: YESU HAKUKATAA ALIPO ITWA MWANA WA MUNGU NA KUHANI MKUU, SOMA JIBU LAKE] “Yesu akamwambia wewe umesema,’ Yesu akamwambia, wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni” (Mathayo 26:64) viongozi wa Kiyahudi walimdhania kwa kukufuru (Mathayo 26:65-66).
WAYAHUDI WANAKIRI KUWA YESU AMEKUBALI KUWA YEYE NI MWANA WA MUNGU
Baadaye mbele ya Pilato, “Wayahudi wakamjibu, Sisi tunayo sheria, na kwa sheria hiyo amestahili kufa, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu” Yohana 19:7) [KWENYE HIYO AYA YA YOHANA 19:7, WAYAHUDI WANAKIRI KUWA YESU AMEKUBALI KUWA YEYE NI MWANA WA MUNGU] ni kwa nini makisio yake kuwa Mwana wa Mungu yachukuliwe kuwa kufuru na astahili hukumu ya kifo?
Wayahudi wilielewa vizuri sana chenye Yesu alimaanisha kwa maneno haya “Mwana wa Mungu” kuwa Mwana wa Mungu ni kuwa hali moja na Mungu. Mwana wa Mungu “wa Mungu” kusema uko katika hali sawa na Mungu-hakika kuwa Mungu- kulikuwa sawa na kukufuru kwa viongozi wa Kiyahudi; kwa hivyo walimtaka Yesu auwawe, kulingana na Mambo ya Nyakati 24:15. Waebrania 1:3 inadhihirisha haya wazi, “Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu.”
Mfano mwingine unaweza patikana katika Yohana 17:12 mahali Yuda anaelezwa kama mwana wa “upotevu”? jina upotevu lamaanisha “uharibivu” Yuda hakuwa mwana wa uharibivu, lakini mambo hayo ndio ya kutambulisha maisha ya Yuda. Yuda anadhihirisha upotevu. Vile vile Yesu mwana wa Mungu. Ni Mungu anajidhihirisha (Yohana 1:1,14).
Hii mada iatufundisha maana ya Yesu ni Mwana wa Mungu, SWALI ambalo limekuwa likiulizwa na Waislam kila siku. Leo wamesha pata jibu thabiti tena lenye ushahidi wa aya za Biblia.
Hakika Yesu ni Mwana wa Mungu
Max Shimba Ministries

SHETANI ATEREMSHA AYA ZAKE KWENYE QURAN NA KUKIRI KUWA ALLAH NDIE MOLA WAKE MLEZI


1. Shetani akiri kuwa Allah ni Mola wake Mlezi.
2. Asema Allah ndie aliye mfundisha kutenda dhambi.
3. Asema na yeye atafanya maovu aliyofundishwa na Allah kwa Binadamu
4. Tabia za Shetani na Allah zafanana
SOMA:
Surah Al Hijr 39. Shetani akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
[Sûrah al-A`râf: 16-17], [Sûrah al-Isrâ’: 62] ,
Ndugu zanguni, huu ni MSIBA mwingine Mkubwa sana kwa Dini ya Jibril. Leo tunajifunza kutoka aya ambayo Jibril aliiteremsha kwa Muhammad. Aya hii katika Surat Al Hijir inakiri kuwa ALLAH NI MOLA MLEZI WA SHETANI.
Sasa Kama Allah ndie Mlezi wa Shetani, na sie wote tunafahamu kuwa Shetani kazi yake ni kufanya Maovu, Kuua watu, na kuendeleza ubaya hapa dunia, JE, inamaanisha hayo yote Shetani kajifunza kwa Allah?
Shetani anaendelea kusema kuwa, NI ALLAH ndie aliye mtia makosani, Je, inamaana kuwa MALEZI ya Allah ndio yaliyo mfunza ubaya na dhambi Shetani?
Shetani anaendelea kusema na kukiri kwa Allah kuwa, NUKUU "basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote" ATAWAPOTEZA WATU WOTE, Swali: Kwanini Allah alikaa kimya wakati Shetani anajitamba kufanya mabaya kwa viumbe visivyo na hatia? Au ni kwasababu yeye Allah ndie aliye mfuza ubaya Shetani, ndio maana alishindwa kumkanya au mwonya Shetani?
Ndugu zanguni, sidhani kuna Muislam atakaye weza bisha na au ipinga hii aya amabayo ipo wazi kabisa kuwa, ALLAH NI MOLA MLEZI WA SHETANI na ALLAH NDIE ALIYE MFUZA UBAYA SHETANI. Huu ni MSIBA MKUBWA SANA KWA WAISLAM.
Waislam, ningependa mtujibu sio kwa jazba bali kwa aya, KWANINI ALLAH HAKUKATAA KUITWA MOLA MLEZI WA SHETANI?
Max Shimba Ministries Org

MUHAMMAD ALIKUWA ANAVAA VIATU MSIKITINI



Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujikumbushe na kujifunza kuhusu kusali na viatu katika nyumba za ibada. Hususan Msikitini.
Waislam mara nyingi wamekuwa wakiwashutumu Wakristo na kuwakejeli kuwa, eti wanasali na viatu Kanisani.
Je, Mtume wa Allah aitwaye Muhammad alivaa viatu alipo kuwa anaswali Msikitini?
Hebu tuangalie ushahidi huu hapa:
Ukisoma kitabu cha Al-u-lu wal-marjan Uk. 179
14. Mlango:
Ruhusa ya kusali na Viatu.
325. Hadithi ya Anas Bin Malik (R.a) kutoka kwa Said Bin Yazid Al-Azid (r.a) amesema, Nilimuuliza Anas Bin Malik (r.a) “Hivi Mtume (s.a.w) alisali huku amevaa viatu vyake?” Akanijibu, “Ndiyo” (Bukhari, Hadithi N. 383, Juzuu ya 1)
Hapo tunamuona Muhammad akisali na Viatu, na mlango hapo umesema, Ruhusa ya kusali na Viatu, maana yake waislamu hapo wameruhusiwa kusali na Viatu, pia haikuishia hapo, Muhammad akasema tena kuwaambia Waislamu.
Ukisoma kitabu kinachoitwa “TAFSIRI YA BULUGH AL-MARAM MIN JAM’I ADILLATIL AHKAM
Ukurasa wa 101 Hadithi Na. 171
Abu Said (r.a) amesimulia: Mtume (S.a.w) amesema: “Ye yote miongoni mwenu atakapoenda msikitini kusali, basi atizame, akiona uchafu au najisi katika viatu vyake aondoe kisha aswali navyo”. Abu Dawud Ibnu Khuzaimah ameipa daraja ya Sahih.
*Murad wa kutwaharisha viatu:
Iwapo mtu amekanyaga najisi kwa kiatu, atakitwaharisha kwa kusugua chini mchangani*
Hapo kwa mtu mwenye akili zake timilifu, hawezi kukomaa na kuanza kuwalaumu Wakristo, eti kwa nini wana Sali na viatu? Wakati Muhammad mwenyewe, alisali huku amevaa viatu, na pia akawaambia waislamu wanapoenda kusali, basi watazame viatu vyao kama kuna najisi, basi wavisugue chini mchangani, labda waislamu watuambie wao kusali na viatu, ni Uviviu wa kusugua viatu mchangani? Au mazingira yao wanayoishi hayana mchanga?
Tena Muhammad akakazia zaidi kuhusu Viatu, aliponukuliwa katika Hadithi hii.
Kasema Mtume (S.a.w) “Atakaepata (ona) nge nae anasali, basi amuue kwa kiatu cha kushoto” (Mkweli Mwaminifu, Juzuu ya 1-2, Hadithi Na. 188, Uk, 88)
Muhammad anawataka Waislamu wakimuona Nge basi wamuue kwa kiatu cha kushoto, sasa jiulize, wewe umevua viatu, unaswali peku peku (kama bata) Halafu amekatiza nge, unaweza kweli kumkanyaga kwa mguu? Nachoweza kusema ni uvivu tu wa waislamu katika kusugua mchangani viatu vyao vilivyo na najisi, kwani wameshapewa ruhusa ya kusali navyo.
Kumbe Mtume Muhammad alikuwa anavaa viatu alipo kuwa ndani ya Msikiti.
Kumbe Mtume Muhammad alisali na viatu Msikitini.
Hakika Uislam ni dini bandia.
Max Shimba Ministries Org

IMAM KUTOKA YEMEN AKAMATWA NA NYAMA YA NGURUWE AIRPORT AKIWA AMEIFICHA KWENYE SEHEMU ZAKE ZA SIRI NCHINI QATAR



Maofisa wa Uhamiaji katika Uwanja wa Ndege wa Hamad International Airport, Nchini Qatari, wamemkamata raia wa Yemen aliye kuwa akijaribu kuiingiza nyama ya Nguruwe nchini humo.
Abd Al Rahman Smoun mwenye umri wa miaka 53 aliificha nyama hiyo kwenye sehemu zake za aja kubwa ikiwa ndani ya Kondom kubwa nne. Nyama hiyo yenye uzito wa Kilo 12 iligundulika baada ya Mbwa maalum ambao wamefungwa kuchunguza watu wenye Nyama ya Nguruwe na Madawa ya Kulevya.
SWALI LA KUJIULIZA:
KWANINI WAMEWEKA MBWA WA KUCHUNGUZA NYAMA YA NGURUWE UWANJA WA NDEGE?
HAKIKA HAWA NI WALAJI WAKUBWA WA HII NYAMA YA NGURUWE KIASI CHA KUWEKEWA MBWA WA KUWACHUNGUZA KILA WANAPO INGIA NCHINI QATAR.
NDIO MAANA NASEMA YANINI KUWA MUUMINI WA HII DINI YA KULAZIMISHANA HUKU NYOYONI MWAKO UNATAMANI KULA NYAMA YA NGURUWE?
Kwa habari zaidi soma hapa

UTHIBITISHO: ADAM NA HAWA WALITUMIA LUGHA YA KIEBRANIA NA SIO KIARABU


Ndugu msomaji,
Katika somo letu hili, tutajifunza na kujibu swali kuhusu; ni lugha ipi Adam na Hawa walitumia wakati wakiwa katika Bustani ya Edeni?
Tunaweza kuthibitisha kuwa Adam na Hawa walitumia Kiebrania kwasababu ya majina mawili ambayo Adam alimpa Hawa ambayo yanaweza kuwa yakinifu pekee katika lugha ya Kiebrania. Adam alimuita Hawa jina la “ISHA” ikiwa na maana ya MWANAMKE kwasabau ya kuwa alitoka kwa “ISH” ikiwa na maana ya MWANAUME , zaidi ya hapo, Adam alimuita mkewe “CHAVA” [HAWA] ikiwa na maana ya mama wa watu wote “CHAI” [UHAI].
Zaidi ya hapo, jina la ADAM linatokana na neno la Kiebrania “ADAMAH” likimaanisha “udongo”, hili jina linathibitisha kuwa Mungu alimuumba Adam kutoka kwenye udongo, kama ambavyo Biblia inasema katika Kitabu cha Mwanzo Mlango 2 na aya ya 7. Hivyo basi, tokea wakati wa Adam na Hawa mpaka wakati wa Mnara wa Babeli, watu wote walitumia lugha ya Kiebrania. Bereshet 2:23, 3:20, Midrash Bereshet Rabbah 38
Wasomi wa Kiyahudi na wa Kikristo wanaendelea kuthibitsiha kuwa Lugha ya Kiebrania ndio ilikuwa lugha ya kwanza, na majadiliano makali yalifanywa zamani na watafiti kama Dante Alighierl (1265-3121), Guillaume Postel (1510-1581) Claude Duret (1570-1611), Etienne Guichard (wakati huo huo wa ATHANASIUS Kircher (1602-1680) na Franciscus Mercurius van Helmont (1614-1698) wana sema kuwa, lugha ya Kiebrania ndio ilitumika na Adam na Hawa. Kwa mfano Mtaalam Guichard alisema kuwa neno la Kilatini “divider” likimaanisha tenganisha au kutenganisha limetokana na neno la Kiebrania la “batar” likimaanisha kukata katika sehemu mbili, hili neno lilifanana na la “tarab” ambalo lilikuja neno la Kilatini la “tribus” likimaanisha “kabila “tribe”
Hebu tuangalie ushahid mchache kutoka Biblia:
Matendo ya Mitume 26:14 Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya KIEBRANIA, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo.
Yohana 19: 17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa KIEBRANIA, Golgotha.
Matendo ya Mitume 22: 2 Waliposikia kwamba anasema nao kwa lugha ya Kiebrania wakazidi kunyamaza; akasema,
Kutoka 2:6 Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, mtoto yule analia. Basi akamhurumia, akasema, Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.
Katika kitabu cha Kutoka hapo juu, tunajifunza kuwa MUSA ANAITWA MTOTO WA KIEBRANIA “Eevriym in Hebrew” na katika kipindi chote watoto wa Kiisraeli waliitwa kama WAEBRANIA ambao ni watoto au wajukuu wa Ibrahim na Musa. Soma Mwanzo 10:24. Zaidi ya hapo, katika kitabu cha Mwanzo 14:13 tunasoma kuwa Ibrahim anaitwa Muebrania (Eevriy in Hebrew).
Huu ni ushahid tosha kuwa Lugha ya Mungu kwa Adam na Hawa ilikuwa ni Kiebrania na sio Kiarabu au lugha nyengine.
Je, Kwanini Mungu alitumia Kiebrani alipo zungumza na Adm na Hawa?
Kwanini Adam na Hawa walitumia Kiebrania walipo kuwa katika Bustani ya Edeni?
Hapa pana hitaji ufunuo wa hali ya kuu kufahamu kwanini Mungu alitumia lugha ya Kiebrania ambayo ni tofauti kabisa na Allah anaye tumia Kiarabu tu.
Kumbe sababu za Allah kutumia Kiarabu ni kupinga Mungu wa Biblia ambaye alitumia Kiebrani na kuwapinga Waisraeli ambao waliitwa wana wa KIEBRANIA.
References:
1. Merrill F. Unger, "Tower of Babel," Unger's Bible Dictionary, 1977 ed.: 115. (BCE - Before the Common Era, equivalent to BC)
2. J.I. Packer, Merril C. Tenney, William White, Jr., Nelson's Illustrated Encyclopedia of Bible Facts (Nashville: Thomas Nelson, 1995) 337.
3. Madelene S. Miller and J. Lane Miller, "Sumer," Harper's Bible Dictionary, 1973 ed.: 710.
4. Unger, "Scythian," 987.
5. Unger, "Egypt," 288.
6. William Smith, "Hebrew Language," Smith's Bible Dictionary, 1948 ed.: 238.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 12, 2016

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW