Saturday, October 29, 2016

MUHAMMAD ALIPEWA UTUME NA MKEWE KHADIJA


Alipokuwa pangoni alichezewa na Shetani: Katika kitabu kiitwacho “ Wakeze Mtume Wakubwa Na Wanawe” kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al Farsy uk.12 tunasoma maneno haya
“Basi Mtume akafanya hofu akarejea kwa mkewe akamhadithia; na pale pale homa kubwa kabisa ikampanda akataka afunikwe maguo. Mara akawa anatetemeka kwa nderema na anaweweseka na kusema “Najikhofia nafsi yangu kuchezewa na shetani na kuniharibu akili yangu na kunizuga”. Bibi Khadija palepale alimdakiza akamwambia; “ Wacha hayo; Siyo yatakayokuwa hayo. Wewe huwezi kuchezewa na mashetani. Shetani hawezi kumchezea mtu mwenye sifa zako. Wewe unatazama vyema jamaa zako, unachukuwa mizigo ya hata watu wasiokuwa wako, unawadhihirishia watu sifa zako nzuri ambazo hakuna mwenye nazo. Unafanya hivi na unafanya hivi. Furahi ndugu yangu. Tua moyo wako, Wallahi! Mimi naona umekwishakuwa mtume”.
Katika tukio hili lililompata Muhammad akiwa pangoni , ndipo Waislamu wote ulimwenguni wanapolieleza kuwa hapo ndipo Muhammad s.a.w alipoletewa wahyi (ufunuo) na kupewa unabii na utume. Lakini unapotafakari juu ya ujumbe huo utaona kuwa hata yeye mwenyewe hajui nini kilichokuwa kimemtokea kule pangoni. Ndiyo maana tunasoma kuwa alipofika nyumbani kwake mkewe Bi. Khadija alimfunika nguo mumewe akidhani ana homa. Muhammad alimweleza mkewe kilichomtokea kuwa ni “Shetani” hakumsema malaika yeyote kama Waislamu wanavyotaka kutuaminisha leo. Kwa sababu kama angekuwa ni malaika kama tunavyosoma ndani ya Biblia ,asingesita kujitambulisha kwa Muhammad kuwa yeye ni nani. Hii ni hoja ya kwanza.
Mwisho wake Bi Khadija akamsimika UTUME Mume wake Muhammad.
Leo umejifunza kuwa Muhammad alipewa utume na Mkewe.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
www.maxshimbaministries Org

BALAA: KUMBE WANAUME WA KIISLAM WAMERUHUSIWA KUINGILIANA KIMWILI.


Surah An Nisaai 21. Na mtachukuaje na ilhali mmekwisha ingiliana nyinyi kwa nyinyi, na wao wanawake wamechukua kwenu ahadi iliyo madhubuti?
Allah amewaruhusu Waislam waingliane wenyewe kwa wenyewe. Huu ni Msiba mkubwa sana.
Mungu haumbi Mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (Warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
SASA TUMSOME MUHAMMAD, JE NA YEYE ALIKUWA NA HII TAMAA MBAYA?
Hadith Idadi 16,245: "maneno ya Washami," Hadith ya Mu'awiya Ibn Abu Sufyan": "Nilimwona Nabii wa Allah(saw) - akimnyonya ulimi na kulamba mdomo wa Al-Hassan Mwana wa Ali, Mwenyezi Mungu amrehemu, maana hakuna mtu atakaye teswa kwa Moto wa Jehannam baada ya kunyonywa ulimi na kulambwa midomo na Nabii wa Allah.
Mnaona tabia chafu ya Nabii wa Allah? Eti akikunyonya na kukulamba midomo basi wewe huto kwenda Jehannam. Hivi lini hawa ndugu zetu watafunguka macho?
Pia alisema, "Siku baadaye tuliomba muuguzi kwa ajili yake (Ali) lakini alikataa, basi tukamwita Nabii Muhammad - SAW -.ambaye alimnyonya ulimi "Ali" kwa kinywa chake mpaka akalala. Hivi ndivyo Allah alivyo taka Ali afanyiwe na Nabii wake
Astaghafurillah, huyo ndio Muhammad nabii wa Allah na ndio mwenye dini ya Uislam. Umeisoma mwenye tabia yako, lakini Waislam hawasei kitu hapo.
Nakushauri ndugu ambaye hujaokoka uachane na huyo Muhamamd aiye nyinya mdomo wa Ali na umpokee Yesu amabye ni Mungu Mkuu.
Yesu anakupenda sana.
Katika huduma yake,
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu.

NENO LA MUNGU LINASEMA NINI KUHUSU SABATO? (SEHEMU YA TISA)


Kwenye somo letu lililo pita “Sehemu ya Nane” tulijifunza sababu zilizo mfanya Bwana Yesu kuingia Sinagogi. Sasa tutajifunza kama kusali na au kuabudu siku ya Jumapili ni makosa.
Wasabato wanasema kuwa, Mungu aliweka agano lake na kamwe haliwezi kubadilika. Hivyo basi, kwenda Kanisani siku ya Jumapili ni kinyume na sharia ya Nne kati ya zile kumi, na ni makossa. Je, kusali jumapili ni makossa? Zifuatazo ni baadhi tu ya hoja hizo na majibu yake;
Neno la Mungu linasema wazi kuwa kuitunza Sabato ilikua ishara maalumu kati ya Mungu na Waisraeli: “Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli watishika sabato, kuiangalia sana hiyo sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele. Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita BWANA alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika” (Kutoka 31: 16-16).
1. WASABATO WANASEMA KUSALI JUMAPILI NI MAKOSA: Wasabato hudai kwamba, Wakristo wanaofanya ibada zao siku ya jumapili, ni makosa mbele za Mungu, maana siyo agizo la Mungu bali ni agizo la mwanadamu.
Hoja hii ya Wasabato si ya msingi na haina ukweli ndani yake na ni dhaifu katika maantiki ya kuwa Mungu alivunja sabato kupitia Yesu ambaye ni Bwana wa Sabato.
HOJA FUPI: WAKRISTO NI WANAFUNZI WA YESU NA SIO MUSAKwanza kabisa ningependa watu waelewe kwamba, Wakristo wanaofanya ibada zao siku ya jumapili na siku nyingine, hao si wanafunzi wa Musa, bali ni wanafunzi wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye ndiye mdhamini wa agano lililo bora zaidi, yaani agano jipya, kama Biblia inavyosema katika Waebrania 7:22, “Basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.”
Lakini pia, msingi wao, wa kufanya ibada siku ya Jumapili na siku nyingine, hautokani na torati ya Musa, bali ni msingi unaotoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo (nitaeleza kwa upana katika sura inayosema ‘Kwa nini Wakristo wanafanya ibada zao siku ya Jumapili’).
Hata hivyo, bado katika agano la kale Mungu aliagiza watu wakusanyike Jumapili ingawa wasabato wengi hawalioni andiko hilo.
UTHIBITISHO:Tukiangalia katika Kutoka 12:16 Biblia inasema, “SIKU YA KWANZA kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na SIKU YA SABA kutakuwa na kusanyiko takatifu, haitafanywa kazi yoyote katika SIKU HIZO, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula, hiyo tu ifanyike kwenu.” Siku ya kwanza ya juma ni Jumapili, na siku ya saba ni Jumamosi kwa kalenda yetu. Kwa hiyo mtoto wa Mungu, mwanafunzi yeyote wa Musa wa nyakati za leo anapokuja na kukusumbua juu ya siku ya Jumamosi, mwambie mbona siku ya kwanza ya juma yeye hafanyi ibada na ni agizo la Mungu kama tulivyokwisha kuona katika Kutoka 12:16.
2. WASABATO WANADAI KUWA, KUABUDU JUMAPILI “SUNDAY” NI IBADA YA MUNGU JUA:
Wasabato wanadai kwamba, Wakristo wanafanya kusanyiko siku ya Jumapili, wana abudu mungu Jua, kwa sababu siku ya Jumapili kwa Kiingereza huitwa ‘Sunday’ ikimaanisha siku ya Jua.
Hoja hii si ya msingi na haina ukweli ndani yake zaidi ya kusema kinyume na maandiko. Ili tupate kuelewa ukweli wenyewe, kwanza ni vema tukaziorodhesha siku zote saba kwa kiingereza alafu tuangalie maana ya siku zote saba, hapo ndipo tutabaini ukweli. Lakini ni vema tukafahamu kuwa, siku hizi saba, zilipewa majina na wapagani wa Kirumi kulingana na mungu wa kila siku hiyo, ingawa Mungu alipoumba siku, hakuzipa majina, bali alitumia siku ya kwanza hadi siku ya saba. Hivyo kuzipa kwao majina ya miungu yao ya kipagani, haizuii Wakristo wa kweli kumuabudu Mungu wao aliyeumba siku hizo, maana Yeye ndiye Mzee wa siku. Kwa mfano, siku inapoitwa, siku ya Mwenge (Mwenge day) ikiangukia Jumamosi, je tutasema wasabato wanamwabudu mungu Mwenge, na hivyo kuwafanya wasifanye ibada siku hiyo? Kwa sababu serikali imetangaza siku hiyo ni siku ya Mwenge (Mwenge day). Au siku ya ukimwi duniani, ikiangukia Jumamosi, je itawazuia wasabato wasifanye ibada siku hiyo, kwani ni siku ya ukimwi, hivyo wakifanya ibada zao watakuwa wanamwabudu mungu ukimwi? Ebu sasa turudi kwenye kuangalia majina ya siku zote saba kwa Kiingereza na maana yake;
MAANA YA MAJINA YA SIKU KWA KIINGEREZA:>Jumatatu (Monday) - inatokana na moon day, kwa wapagani wa nyakati zile ilimaanisha siku ya kumwabudu mungu moon (mwezi).
>Jumanne (Tuesday) –inatokana na tiw’s day, kwa wapagani wa nyakati zile ilimaanisha ni siku ya mungu Tiw.
>Jumatano (Wednesday) –inatokana na wedn day au woden day, kwa wapagani ilimaanisha siku ya mungu wedn au woden.
>Alhamisi (Thursday) –inatokana na thor day, kwa wapagani ilikuwa ni siku ya kumwabudu mungu thor.
>Ijumaa (Friday) - inatokana na frig day au freia day, kwa wapagani ilikuwa ni siku ya mungu frig au freia.
>Jumamosi (Saturday) –inatokana na Saturn day (siku ya sayari zohari), kwa wapagani ilikuwa ni siku ya kumwabudu mungu wa Kirumi aitwaye Saturnyaani kwa Kiswahili sayari ya zohari.
>Jumapili (Sunday) –ilitokana na sun day (siku ya jua), kwa wapagani waKirumi ilikuwa ni siku ya kumwabudu mungu sun (jua).
Hivyo basi, Siku zote za juma, Warumi walizipa majina ya miungu yao, kwa sababu hao kwa kipindi hicho ndiyo walikuwa watawala. Swali linakuja, kwa vile zimepewa majina ya miungu ya kipagani, hivyo siku zote hazifai kufanya ibada?
Siku ya Jumamosi, Warumi walikuwa wakimwabudu mungu Saturn kwa Kiswahili zohari, swali ni kwamba, kwa kufanya ibada zao Jumamosi, wasabato wote wanamwabudu mungu zohari yaani sayari ya zohari (Saturn)?

YESU ALIKUWEPO KABLA YA KUZALIWA


Ufuatao ni ushahidi wa kibiblia kwamba YESU KRISTO ni Mungu.

Yohana 8:58
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.

NIKO ni jina la Mungu peke yake. Tunakutana na jina hilo pale Musa alipoongea na Mungu na kutumwa kuwakomboa wana wa Israeli kutoka Misri. Imeandikwa:

Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO (Kutoka 3:13-14).

Mwanadamu yuko kwa sababu Mungu alisababisha awepo. Gari liko kwa sababu injinia au mbunifu alisababisha liwepo. Nyumba ipo kwa sababu fundi alisababisha iwepo. Lakini Mungu YEYE YUKO TU!! Hayupo kwa kusababishwa na yeyote! Ndiyo maana akasema MIMI NIKO AMBAYE NIKO! Yesu ni NIKO. Kwa hiyo, Yeye ni Mungu.

DAMU YA YESU INAMAMLAKA

Matendo 20:28
Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake MUNGU, ALILOLINUNUA KWA DAMU YAKE MWENYEWE.
Ni Mungu gani mwenye damu huyu? Jibu liko wazi. Huyu ni Yesu Kristo. Huyu ndiye aliyetoa uhai wake na kumwaga damu yake msalabani; na hapo ndipo alipoanzisha Kanisa.
YESU NI MUNG

YESU ANAWEZA YOTE

OMBENI NANYI MTAPEWA
“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa” Mathayo7:7
“Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” Waebrani 4:12
YESU NI MUNGU

Thursday, October 27, 2016

ALLAH HAJUI HISABATI NA AU HESABU


Jambo ambalo linathibitisha kuwa Allah sio Mwenyezi Mungu, ni makosa makubwa ya kimahesabu katika Quran yake anayo dai kuiteremsha kwa Muhammad kwa usaidizi wa Jibril.
Sheria zake za mirathi zimegawanywa katika sura kadhaa kama Al Bagarah, Al Maidah, na Al Anfah. Lakina kwa undani zaidi zimewekwa katia Surat Al Nisaai.
Surat An Nisaai 11. Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Fungu la mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili. Na ikiwa wanawake zaidi ya wawili, basi watapata thuluthi mbili za alicho kiacha maiti. Lakini akiwa mtoto mwanamke ni mmoja, basi fungu lake ni nusu. Na wazazi wake wawili, kila mmoja wao apate sudusi ya alicho kiacha, ikiwa anaye mtoto. Akiwa hana mtoto, na wazazi wake wawili wamekuwa ndio warithi wake, basi mama yake atapata thuluthi moja. Na akiwa anao ndugu, basi mama yake atapata sudusi. Haya ni baada ya kutolewa alicho usia au kulipa deni. Baba zenu na watoto wenu, nyinyi hamjui ni nani baina yao aliye karibia zaidi kwenu kwa manufaa. Hiyo ni Sharia iliyo toka kwa Mwenyezi Mungu. Bila ya shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na Mwenye hikima.
Surat An Nisaai 12. Na fungu lenu ni nusu walicho acha wake zenu ikiwa hawana mtoto. Wakiwa na mtoto basi fungu lenu ni robo ya walicho acha, baada ya wasia waliyo usia au kulipa deni. Na wake zenu watapata robo mlicho kiacha, ikiwa hamna mtoto. Mkiwa mna mtoto basi sehemu yao ni thumni ya mlicho kiacha, baada ya wasia mlio usia au kulipa deni. Na ikiwa mwanamume au mwanamke anaye rithiwa hana mtoto wala wazazi, lakini anaye ndugu mume au ndugu mke, basi kila mmoja katika hawa atapata sudusi. Na wakiwa zaidi kuliko hivyo basi watashirikiana katika thuluthi, baada ya wasia ulio usiwa au kulipa deni, pasio kuleta dhara. Huu ndio wasia ulio toka kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na Mpole.
Surat An Nisaai 176. Wanakuomba uhukumu, sema: Mwenyezi Mungu anakupeni hukumu juu ya mkiwa. Ikiwa mtu amekufa, naye hana mtoto, lakini anaye ndugu wa kike, basi huyo atapata nusu alicho acha maiti. Na mwanamume atamrithi ndugu wa kike ikiwa hana mwana. Na ikiwa wao ni ndugu wa kike wawili, basi watapata thuluthi mbili za alicho acha maiti. Na wakiwa ndugu wanaume na wanawake, basi mwanamume atapata sehemu iliyo sawa na ya wanawake wawili. Mwenyezi Mungu anakubainishieni ili msipotee; na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
Ingawa Allah anasema kuwa, ameziweza hizo sheria kiuuwazi na bila ya shaka, lakini unapo zisoma hizo aya, zote zimejaa shaka na kuchakuana.
Quran 4:11 inasema kuwa akiwa mtoto mwanamke ni mmoja, basi fungu lake ni nusu. Lakini aya hiyo hiyo inadai kuwa Kaka mtu atapata mara mbili ya mwanake, kimahesabu, Kaka mtu atachukua kila kitu. Huu ni msiba wa kimahesabu kwa Allah.
Zaidi ya hapo, unapowahusisha Wazazi wa kike katika hiyo mirathi, Allah anawaacha solemba, maana mahesabu yanakuwa magumu kwake.
Ndio maana nauliza, hivi, ni nani alimfundisha hesabu na au hisabati Allah?
HUU NI MSIBA MKUBWA SANA KWA WAISLAM.

UISLAM NI DINI YA VITA NA KULAZIMISHANA




Uislam unafundisha nini kuhusu kulazimishana katika dini?
Ndugu msomaji,
Waislam wameembiwa wapigane na Makafiri au wawauwe au wakubali kujiunga na dini ya Muhammad. Uislam hauruhusu waumini wa imani zingine au dini zingine waabudu kwa uhuru. Ndio maana kwenye nchi za Kirabu kama Uarabuni kwenye Makkah, huko hakuna kanisa hata moja. Allah hapendi uhuru wa kuabudu.
Surat Tawba 29. Piganeni na wasio muamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho, wala hawaharimishi alivyo harimisha Mwenyezi Mungu na Mtume, wala hawashiki Dini ya Haki, miongoni mwa walio pewa Kitabu, mpaka watoe kodi kwa khiari yao, hali wamet'ii
Surat Al Anfaal 38. Waambie wale walio kufuru: Wakikoma watasamehewa yaliyo kwisha pita. Na wakiyarudia basi imekwisha pita mifano ya wa zamani.
39. Na piganeni nao mpaka isiwepo fitna na mateso, na Dini yote iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Lakini wakiacha, basi hakika Mwenyezi Mungu anayaona wanayo yatenda.
Surat Tawba 5. Na ikisha miezi mitukufu basi wauweni washirikina popote mwakutapo, na washikeni na wazungukeni, na wavizieni katika kila njia. Lakini wakitubu, wakashika Sala, na wakatoa Zaka, basi waachilieni. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
Surat Al Baqaara 193. Na piganeni nao mpaka pasiwepo fitina, na Dini iwe ya Mwenyezi Mungu tu. Na kama wakiacha basi usiweko uadui ila kwa wenye kudhulumu
Surat Al Imran 84. Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyo teremshiwa sisi, na aliyo teremshiwa Ibrahim, na Ismail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo pewa Musa na Isa na Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi. Hatubagui baina yao hata mmoja, na sisi ni wenye kusilimu kwake.
Juhudi za Muhammad za kuutanganza Uislam bila ya chuki ziligonga mwamba. Kwa miaka 13 Muhamamd alikuwa na watu 100 tu ambao wengi wao walikuwa ni ndugu zake na jamaa zake. Baada ya kushindwa vibaya sana kuutangaza Uislam kwa kutumia amani, Muhammad akabadilisha mbinu ya kuutangaza Uislam na kuteremsha hizi aya hapo juu za kulazimisha watu wajiunge na dini yake, au lasivyo watakiona cha mtema kuni, kama sio kuuliwa kabisa. Aliwaambia wafuasi wake kuwa Allah amemuamrisha kuwalazima watu wajiunge katika dini yake ya Uislam.
Katika miaka yake ya mwishoni. kabla ya kifo chake, Muhammad hakujali tena kwamba watu wanajiunga au, la, bali alikuwa analazimisha kila mtu ajiunge na Uislam kwa kutishia kifo. Hii ni pamoja na adui yake mkubwa Abu Sufyan na mke wake Hind. Kutokana na wana historia wa Kiislam, Abu Sufyan alikwenda kwa Muhammad kutaka wawe na amani baada ya chuki kubwa ya Muhammad, lakini Muhammad alimlazimisha kujiunga na Uislam, la sivyo alimwambia atamuua. Maneno halisi ambayo Muhammad alimwambia ni haya "Nyenyekea na shahadia kuwa hakuna Mungu ila Allah na Muhammad ni Mtume wake au ukikataa utakatwa kichwa chako" Soma Ushahdi katika Ibn Ishaq/Hisham 814. Hivyo basi Abu Sufyan akakubali.
Mji mzima wa Mekkah ulisaliti amri, pale Muhammad alipo uvamia akiwa na kundi lake. Wengi walikataa lakini walilazimishwa kuingia Uislam na walio kataa walikatwa kichwa na Muhammad mwenyewe.
Wengine walifukuzwa kutoka Mekka baada ya hija ya mwisho Soma Quran 9:5. Wakristo na Wayahudi walio kuwa Urabuni wakati huo, nao walipatwa na hii shida/balaa ya Muhammad kulazimisha kujiunga na Uislam au unauwawa. Wengi walipewa chaguo moja wajiunge na Uislam au wafukuzwe kutoka kwenye ardhi zao. SOMA Sahihi Muslim 19:4366.
Kabla hajafa, Muhammad alituma majeshi yake kwenda kuwalazima Wapagani wa Kiarabu kujiunga nae, kabila la al Harith. Aliwaambia wamepewa chaguo moja tu kujiunga nae au atawauwa wote kwa upanga. Lakini hilo kabila la kipagani liliogopa na kiunga nae. Baadae Muhammad akawalaani Wakristo wote na Wayahudi. SOMA Sahihi Bukhari 8:427.

YESU NI MUNGU






“Wahubiri wa injili” wa Kiislamu huwa wanapinga kuwa Yesu ni Mungu na unapowakatalia wanakwambia, “Lete andiko.”
Maandiko yapo mengi sana ndani ya Biblia juu ya ukweli kwamba Yesu ni Mungu. Ni mengi mno!
Ukishawapa andiko, wanabadilika na kusema, “Nataka maneno aliyoongea Yesu mwenyewe.” Kwa madai haya hata kwenye Qurana hawawezi thibitisha kuwa Allah Allah ni mungu, zaidi ya hapo, hata Utume wa Muhammad unakuwa kwenye njia panda, maana hakuna aya kwenye Quran Muhammad anasema mimi Muhammad ni mtume wa Mungu.
Hiki ni kigezo POTOFU na si cha kibiblia hata kidogo. Ukweli ni kwamba, Biblia YOTE ni Neno la Mungu. Haijalishi amezungumza Musa, Isaya, Yohana, Petro au Yesu mwenyewe. Imeandikwa:
Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. (2Petro 1:21).
Hivyo, kudai kwao eti, “Nataka maneno aliyosema Yesu mwenyewe,” ni kigezo batili na kisicho na mantiki hata kidogo.
1. YESU ALIKUWEPO KABLA YA KUZALIWA
Ufuatao ni ushahidi wa kibiblia kwamba YESU KRISTO ni Mungu.
Yohana 8:58
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.
NIKO ni jina la Mungu peke yake. Tunakutana na jina hilo pale Musa alipoongea na Mungu na kutumwa kuwakomboa wana wa Israeli kutoka Misri. Imeandikwa:
Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO (Kutoka 3:13-14).
Mwanadamu yuko kwa sababu Mungu alisababisha awepo. Gari liko kwa sababu injinia au mbunifu alisababisha liwepo. Nyumba ipo kwa sababu fundi alisababisha iwepo. Lakini Mungu YEYE YUKO TU!! Hayupo kwa kusababishwa na yeyote! Ndiyo maana akasema MIMI NIKO AMBAYE NIKO! Yesu ni NIKO. Kwa hiyo, Yeye ni Mungu.
2. YESU NA BABA NI WAMOJA
Yohana 10:30
Mimi na Baba tu umoja.
Waislamu wana msemo wao kwamba eti, Yesu na Mungu ni wamoja katika malengo, si katika asili yao. Basi huwa nawauliza swali kuhusu aya ifuatayo ya Isaya, nao wanazimika na kukosa jibu:
Isaya 9:6
Maana kwa ajili yetu MTOTO amezaliwa, Tumepewa MTOTO MWANAMUME; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE, Mfalme wa amani.
Aya hii iko wazi kabisa. anayetajwa ni Yesu kwamba Yeye ni Mungu mwenye nguvu.
Yohana 14:9
Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?
Maneno haya Yesu aliyasema baada ya kuulizwa swali lililo wazi kabisa, ambalo lilikuwa na lengo la kumjua MUNGU BABA! Imeandikwa: Filipo akamwambia, Bwana, UTUONYESHE BABA, yatutosha. Ndipo Yesu akajibu waziwazi: ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA. Maana yake ni kuwa, “Mimi ndio Baba mwenyewe.”
3. YESU NI MWANZO NA MWISHO
Ufunuo 1:17 na Ufunuo 22:13
Mimi ni wa kwanza na wa mwisho
Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
Ni Mungu TU ndiye mwenye uwezo wa kuwa wa kwanza na wa mwisho; Yesu ni Alfa na Omega. Kwa hiyo Yeye ni Mungu.
4. YESU NI NENO
Yohana 1:1
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye NENO ALIKUWA MUNGU.
Andiko hili Waislamu hawalipendi kabisa. ni kwa sababu liko wazi mno. Yesu ni Neno; na Neno ni Mungu; hivyo, Yesu ni Mungu!
5. THOMASO AKIRI KUWA YESU NI MUNGU, NA YESU HAKUKATAA KUITWA MUNGUYohana 20:28
Tomaso akajibu, akamwambia, BWANA WANGU NA MUNGU WANGU!
Tomaso aliposema hivi, Bwana Yesu hakukanusha na kusema, “Mimi sio Mungu.” Badala yake: Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. (Yoh 20:29).
Kama Thomaso alikuwa muongo, kwanini Yesu hakukataa kuitwa Mungu. Imani zote zinakiri kuwa Yesu hakufanya dhambi na hakuwa na dhambi.
6. DAMU YA YESU INAMAMLAKA
Matendo 20:28
Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake MUNGU, ALILOLINUNUA KWA DAMU YAKE MWENYEWE.
Ni Mungu gani mwenye damu huyu? Jibu liko wazi. Huyu ni Yesu Kristo. Huyu ndiye aliyetoa uhai wake na kumwaga damu yake msalabani; na hapo ndipo alipoanzisha Kanisa.
7. KATIKA YESU, KILA KITU KILIUMBWA
Wakolosai 1:16
Kwa kuwa KATIKA YEYE VITU VYOTE VILIUMBWA, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
Katika Yeye Yesu vitu vyote viliumbwa. Ina maana kuwa vitu vyote vilitokana na Yesu; maana Yesu ni Neno la Mungu. Na tunajua kuwa Muumba wa vitu vyote ni Mungu; hivyo, Yesu ni Muumba – Yeye ni Mungu!!
8. KATIKA YESU, UNAKAA UTIMILIFU WA MUNGU
Wakolosai 2:9
Maana KATIKA YEYE UNAKAA UTIMILIFU WOTE WA MUNGU, kwa jinsi ya kimwili.
Sisi sote ni watu wasio wakamilifu. Tunaanguka tena na tena kwenye dhambi. Kwa hiyo, hakuna mwanadamu wa kawaida ambaye anaweza kujigamba kwamba yeye ametimia kama alivyo Mungu. Lakini katika Yesu “utimilifu WOTE wa Mungu unakaa.” Kwa nini? Kwa sababu Yeye ndiye Mungu huyohuyo.
9. YESU NI MUNGU PAMOJA NASI "EMMANUEL
"1Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.
Ni Mungu gani aliyedhihirishwa katika mwili? Jibu liko wazi. Ni Yesu Kristo peke yake.
10. YESU NI MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Tito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Waislamu ni hii: Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yer 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Lakini utakuta Waislamu wanauliza maswali ya ajabu sana. Eti, kama Yesu ni Mungu, wakati amekufa, nani alikuwa anaangalia dunia?
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO!
YESU NI MUNGU MILELE NA MILELE!!
HALELUYA!!
Tafakari
Hoji mambo
Chukua hatua!
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo

NENO LA MUNGU LINASEMA NINI KUHUSU SABATO? (SEHEMU YA NANE)



JE, UNAZIFAHAMU SABABU ZILIZOMFANYA BWANA YESU KUINGIA HEKALUNI SIKU YA SABATO?
Wasabato wa karne hii, wanadai kuwa, kitendo cha Yesu kuingia Hekaluni/Sinagogi ni ushahidi tosha kuwa Yesu alikuwa Msabato na au alikuwa anatunza Sabato. Lakini wanashindwa kuelewa kuwa, Yesu aliingia Hekaluni siku ya Jumamosi KUHUBIRI HABARI NJEMA [kuvua Samaki] na sio kutunza siku, maana Yesu yeye ndie Bwana wa Sabato.
USHAHIDI KUHUSU SIKU YA SABATO:
Biblia inasema, Matendo 13:13-15 “Kisha Paulo na wenziwe wakang’oa nanga wakasafiri kutoka pafo, wakafika Perge katika Pamfilia. Yohana akawaacha akarejea Yerusalemu. Lakini wao wakatoka Perge, wakapita kati ya nchi, wakafika Antiokia mji wa Pisidia, wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Kisha baada ya kusomwa torati na chuo cha manabii, wakuu wa sinagogi wakatuma mtu kwao, na kuwaambia, NDUGU, KAMA MKIWA NA NENO LA KUWAFAA WATU HAWA, LISEMENI.”
SABABU YA YESU KUINGIA HEKALUNI:
Katika karne ya kwanza, kwenye Mahekalu/Masinagogi KULIKUWA NA UTARATIBU kwamba, baada ya kusoma torati na chuo cha manabii, wakuu wa Masinagogi, walikuwa wakikaribisha watu, waliokuwa na jambo jema la kuwaambia watu kwenye kusanyiko.
Ndio maana wahubiri kama Bwana Yesu na Paulo, hii kwao ilikuwa ni fursa na au nafasi ya pekee sana ya kuwahubiria Wayahudi habari njema za ufalme wa Mungu, kwani walikuwa wamepotea kwa kuendelea kushika sheria ya sabato na mapokeo mengine. Kwa hiyo, Bwana Yesu na Mhubiri kama Paulo walitumia nafasi hii, kuwafikishia Mafarisayo na Wayahudi wengine habari njema, kwa kuwa siku ya sabato, watu wengi walifika hekaluni.
Hivyo basi, Bwana Yesu na mitume kama Paulo, hawakwenda hekaluni kukusanyika kwa kusudi la kushika au kutunza sabato au kushiriki kusanyiko la Wasabato, bali waliwafuata Wayahudi waliokuwa bado wamefungwa na mzigo wa sabato “sheria” na mapokeo mengine. Na kwa kulithibitisha hilo, Bwana Yesu, alikuwa akienda hekaluni kila siku kufundisha, na siyo siku ya sabato tu.
YESU ANAFUNDISHA HABARI NJEMA KILA SIKU KWENYE HEKALU/SINAGOGI NA SIO JUMAMOSI PEKE YAKE KAMA WANAVYO DAI WASABATO
UTHIBITISHO:
Luka 19:47 tunasoma, “Naye akawa akifundisha kila siku hekaluni. Lakini wakuu wa makuhani, na waandishi, na wakuu wa watu walikuwa wakitafuta njia ya kumwangamiza.”
Luka 21:37 tunasoma, “Basi kila mchana, alikuwa akifundisha hekaluni, na usiku huenda kulala katika mlima uitwao wa Mizeituni.”
Zaidi ya hapo, katika Yohana 18:20 tunasoma, “Yesu akamjibu, Mimi nimesema na ulimwengu wazi wazi; siku zote nalifundisha katika sinagogi na katika hekalu, wakusanyikapo wayahudi wote; wala kwa siri mimi sikusema neno lolote.”
Kwenye aya za hapo juu, tumemsoma Bwana Yesu na anathibitisha kuwa alikuwa akienda kwenye sinagogi na hekalu kila siku ili kufundisha watu, kwani ilikuwa ni sehemu ambayo angeweza kuwapata Wayahudi, hivyo kumpa nafasi ya kufundisha kweli ya neno la Mungu. Kwa lugha nyingine, Yesu alikuwa anavua Samaki.
WASABATO WANADAI KUWA SABATO NI YA MILELE, JE HAYA MADAI NI KWELI?
Wasabato hudai kwamba, sheria ya kushika sabato haijakomeshwa na inaendelea hata sasa kwani imeamriwa kuwa ni agano la milele kama Biblia inavyosema katika Kutoka 31:16, “Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika sabato, kuiangalia sana hiyo sabato, katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele.”
NINI MAANA YA NENO MILELE KAMA LILIVYO TUMIWA KWENYE “KUTOKA 31:16”?
Kabla hatujaingia kwa undani zaidi katika kutafuta ukweli wa hoja hii, ni vizuri, watu wakielewa maana ya neno MILELE kwa msingi wa maisha ya duniani. Neno MILELE, likitumika kwa matumizi ya kidunia haimaanishi isiyo na mwisho, kwa kuwa hakuna umilele kwenye maisha ya hapa duniani, bali humaanisha muda mrefu. Lakini neno MILELE, likitumika nje ya matumizi ya kidunia, mfano maisha baada ya kufa, hapo ndipo milele humaanisha “isiyo na mwisho”. Kwa ujumla, siyo kila palipoandikwa kwenye Biblia MILELE, inamaanisha isiyo na mwisho.
UTHIBITISHO:
Kwa mfano, katika kitabu cha 1 Samweli 27:12 tunasoma, “Hivyo akishi akamsadiki Daudi, akasema, amewachukiza kabisa hao watu wake Israeli; kwa hiyo atakuwa mtumishi wangu hata MILELE”
Daudi anatangazwa kuwa ni mtumishi Akishi hata milele, lakini, ebu tujiulize, kama kila litumikapo neno milele, lina maana isiyo na mwisho, je Daudi aliendelea kuwa mtumishi wa Akishi? Je baadaye hakuwa Mfalme? Akishi hapa, alimaanisha kwamba, Daudi kuwa mtumishi wake kwa muda mrefu.

UTHIBITISHO:

TRENDING NOW