Baada ya kusoma katika Sehemu ya Kumi na Mbili kwanini Wakristo wanasali Jumapili, basi tuendelee kuona je, sheria inaweza batilishwa?
Maana ya Sheria:
Neno sheria lina maana nyingi.Lina maana kama kama;
.Desturi
.Kanuni,au
.Amri zilizo na lazima kufuatwa.
Vilevile neno sheria lina maana ya utaratibu wa maisha unaowekekewa kanuni zilizopitishwa na bunge; na pamoja na desturi zinazokabiliwa na Taifa zitumike kwa jamii (yaani sheria za mila). Ili kuakikisha kwamba sheria zinaheshimiwa na kufuatwa Taifa (Serikali) hutumia vyombo vya dola kama;
Polisi-kwa kuwakamata na kuwafikisha wahalifu mahakamani;
Mahakama-kwa kuwaadhibu wahalifu; na Magereza -kutekeleza adhabu ya mahakama kwa kuwafunga waalifu.
SASA TUJIFUNZE MAREKEBISHO YA SHERIA KATIKA AGANO JIPYA KUPITIA CHEKECHO LA MSALABA
Mungu habadiliki katika tabia na sifa zake, lakini Yeye mwenyewe amekuwa akiweka amri na kuzibadili kama apendavyo Yeye, katika vizazi mbalimbali. Na pia amekuwa akifanya maagano na vizazi mbalimbali kwa kadiri ya kusudi lake.
ADAM NA HAWA HAWAKUPEWA TORATI:
Adamu na Hawa hawakupewa torati, bali walipewa amri moja tu, yaani kutokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya kama Biblia inavyosema katika kitabu cha Mwanzo 2:16-17.
Mungu hakumpa Adamu amri ya ‘usizini’ kwa kuwa hakuwapo mwanamke mwingine ila mkewe Hawa. Vivyo hivyo hakumpa amri ya ‘usiibe’ kwa kuwa vitu vyote vilivyo kuwapo katika bustani ya edeni alipewa na Mungu kuwa vyake. Pia Mungu asingeweza kumwambia Adamu aheshimu wazazi wake kwa kuwa hawakuwapo. Katika maandiko hatuoni Mungu akimwagiza Adamu ashike sabato. Kwa hiyo zama za Adamu na Hawa walipewa amri moja tu.
AGANO LA MUNGU NA NUHU:
Tukija zama za Nuhu, tunaona Nuhu naye anafanya agano na Mungu na kupewa sheria zifuatazo katika Mwanzo 9:1-7; sheria ya kwanza Nuhu anaambiwa asile nyama pamoja na uhai wake yaani damu (Mwanzo 9:4-5), na sheria ya pili, Nuhu na kizazi chake wanakatazwa kuua (Mwanzo 9:6).
AGANO LA MUNGU NA IBRAHIMU:
Tukija kwa Ibrahimu tunaona Mungu anafanya agano na Ibrahimu na kumwambia awe mkamilifu (Mwanzo 17:1). Lakini pia anampa sheria mpya ya kutahiri nyama ya magovi yao, kitu ambacho Nuhu hakuamriwa kufanya.
SASA TUONE JINSI TORATI ILIVYO KUJA: