Thursday, November 17, 2016

JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?


Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.

KITABU CHA DANIEL (SEHEMU YA KWANZA)


Kwenye hili somo tutajifunza kuhusu Kitabu cha Daniel kwa kutumia maswali na majibu. Tutazipitia aya zote na sura zote katika Daniel. Sasa tulia na tuanze kujifunza Neno la Mungu.
SWALI:
Kwenye Danieli, kitabu hiki kiliandikwa nini?
Kitabu cha Danieli kinaelekea kuandikwa muda mfupi baada ya matukio kutokea, kwenye karne ya 6KK, kwa mujibu wa The Bible Knowledge Commentary: Old Testament, uk.1324. Vijana wengi wa Kiyahudi walipelekwa uhamishoni Babeli mwaka 605 KK, na wafafanuzi wengine wa vitabu vya Biblia wanakadiria kuwa Danieli alikuwa na miaka kama 16 hivi. Makadirio haya yanamfanya Danieli awe na umri wa miaka 85 wakati Waajemi walipoiteka Babeli.
Kitabu chenye kutia shaka kiitwacho Asimov’s Guide to the Bible, uk.596 kinadai kuwa Danieli inaweza kuwa iliandikwa mwishoni mwa mwaka 165 KK. Hata hivyo, mwana historia wa Kiyahudi Josephus kwenye Antiquities of the Jews 11.8.5 (karibu mwaka 93-94 BK) anarekodi kuwa wakati Alexanda Mkuu alipoikaribia Yerusalemu (karibu mwaka 333 KK), Kuhani Mkuu Jaddua alikutana naye na alimwonyesha sehemu ya kitabu cha Danieli isemayo kuwa Wagiriki watawashinda Waajemi. Alexanda anaelekea kuwa alipendezwa na maneno haya, na aliachana na Wayahudi.
Origen (mwaka 225-254 BK) alisema kuwa wakati Alexanda wa Macedon alipokwenda Yerusalemu, kuhani mkuu wa Kiyahudi, alikutana naye akiwa amevaa joho lake takatifu. Alexanda aliinama mbele zake, akisema kuwa alimwona mtu mwenye joho kama hilo kwenye ndoto aliyoota, akimfahamisha kuwa anapaswa kuishinda Asia yote. Origen Against Celsus, kitabu cha 4, sura ya 50, uk.565.
SWALI:
Je Kitabu cha Danieli kiliandikwa kwenye karne ya pili (baada ya ushindi wa Alexanda), kwa sababu ya maneno ya Kigiriki yaliyopo kwenye Danieli?
Hapana. Ingawa kitabu cha mwenye kushuku kiitwacho Asimov’s Guide to the Bible, uk.597 kinadai, "sehemu nyingine za lugha zisizoeleweka kwa urahisi zilizotumiwa zinaonyesha kipindi cha Kigiriki tofauti na kile cha uhamisho wa Babeli", kuna maneno matatu tu ya Kigiriki kwenye Kitabu cha Daniel, ambayo ni kidogo kuliko maneno saba ya Kiajemi yaliyomo. Yafuatazo ni maelezo zaidi ya mambo haya mawili.
Maneno matatu tu ya Kigiriki yapo kwenye Kitabu cha Danieli (Dan 3:5, 10, 15), na yote hayo matatu ni majina ya vifaa vya muziki. Hata hivyo, jambo hili halionyeshi kuwa kitabu hiki kiliandikwa kwenye karne ya pili (2 KK), kama maandishi ya Kiashuri yanavyosema kuwa mateka wa Kigiriki walikuwa Mesopotamia kwenye karne ya 8 KK. Isitoshe, kwenye karne ya 7 KK, mshairi wa Kigiriki, Alcaeus wa Lebos, anasema kuwa kaka yake alikuwa kwenye jeshi la Babeli. Vivyo hivyo, The Expositor’s Bible Commentary, juzuu ya 1, uk.247 pia inasema, "Hakuna shaka kuwa majina ya vifaa (vya muziki) kwenye Kitabu cha Danieli yalikuwa na sifa za Kiajemi, na yalifanya na Wagiriki kuwa sehemu ya utamaduni wao na kufanyiwa mabadiliko machache ya kitahajia (herufi). Kwa hiyo, hoja hii ni ya muhimu tena katika kutathmini uandishi wa Danieli."
Maneno sita na nusu ya Kiajemi yaliyomo kwenye Kitabu cha Danieli yanaongelea utawala (Dan 6:1-4, 6-7), na yaliacha kutumika karne moja baada ya Himaya ya Kiajemi kuchukuliwa na Alexanda Mkuu. Kama 735 Baffling Bible Questions Answered, uk.193 inavyosema, ". . . Utumiaji sahihi wa Danieli wa maneno haya hauwezi kuelezwa endapo mwandishi alikuwa hafahamiki kwenye karne ya pili na hakufahamu undani wa serikali ya Kiajemi miaka mia tatu kabla ya muda alioishi." (Neno satrap [maliwali] linahesabiwa kuwa nusu, kwa sababu lilikuwa neno la Kimidiani, ambalo baadaye lilichukuliwa na Waajemi pia.
SWALI:
Je Kitabu cha Danieli kiliandikwa baada ya Kitabu cha Sirach, kwani Sirach 47-49 ina orodha ndefu kiasi ya Agano la Kale, isipokuwa Danieli, kama Asimov’s Guide to the Bible, uk.623 inavyosema?
Utawala wa Wamakabia haukuanza hadi mwaka 165 KK. Hata hivyo, kuna mambo manne yenye kutoa ushahidi unaotofautiana na nadharia hii ya karne ya pili.
1. Kwenye Apokrifa (vitabu vya kubuniwa vya dini ya Kiyahudi), 1 Maccabees 2:49-60 inawataja Danieli na vijana wengine watatu kwa namna ambayo inaashiria kuwa Kitabu cha Danieli kilikuwa tayari kimeishaandikwa. Vinginevyo, wasomaji wa 1 Maccabees wangewezaje kumwelewa Danieli na vijana wengine watatu?
2. Wataalamu wa elimukale wamekadiria muda hati ya kale yenye maandiko ya Kitabu cha Danieli ilipoandikwa kuwa ni mwaka 120 KK. Wycliffe Bible Dictionary, uk.436-438 inalitaja jambo hili, ikisema kuwa "linaibua swali kuhusu muda unaodaiwa kitabu cha Maccabean kuandikwa."
3. Uchimbuaji ulifanyika Babeli unaonyesha kuwa maelezo ya Danieli ni sahihi. M. Lenormant anasema, "Kwa kadri maandishi ya kikabari yanavyozidi kufahamika ndivyo haja ya kurekebisha shutuma zilizofanywa kwa haraka na shule ya ufafanuzi wa maandiko ya Ujerumani dhidi ya Kitabu cha Danieli inavyoongezeka" (La Magie, uk.14; nukuu ya 1001 Bible Questions Answered, uk.367).
4. Pia marejeo ya Josephus yaliyokwishatolewa kwenye swali lililotangulia.
USIKOSE SEHEMU YA PILI "Kwenye Kitabu cha Danieli, kuna vitu gani vinavyofanana na sehemu nyingine za Biblia?"
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Shalom

MAANA YA KANISA


Kwanza kabisa neno Kanisa linamaanisha "mkusanyiko wa waamini" kama ule wa Waisraeli chini ya Musa kwenye mlima Sinai walipopewa Amri za Mungu.
Neno hilohilo lilitumiwa na Wakristo wa kwanza kwa ajili yao wenyewe kusema wameshika nafasi ya Israeli kama taifa la Mungu hata wasipokuwa Wayahudi bali watu wa mataifa mengine.
Watu wengi siku hizi wanaelewa kanisa kumaanisha jengo. Huku si kuelewa kibibilia maan ya kanisa.
Neno “kanisa” maana ya asili yatoka kwa neno la Kiyunani ekklesia lili lo na maana ya “kusanyiko” au “walioitwa.” Maana ya asili ya “kanisa” sio ile ya jingo, bali ni watu. Ni kinaya kwamba unapowauliza watu ni kanisa gani wanashiriki, mara nyingi huwa wanajihushisha na jingo. Warumi 6:5, yasema, “…salimia kanisa linalokutana kwa nyumba.” Paulo anaashiria kanisa lilo katika nyumba yao- si jengo la kanisa bali mwili wa washiriki.
Wakristo walipoanza kujenga mahali pa ibada, pakaja kuitwa vilevile "kanisa" kwa sababu ndani yake lilikusanyika Kanisa hai.
Hivyo mara nyingi neno hilo linatumika kwa maana ya jengo, ambalo ni mfano mwingine uliotumiwa na Paulo kuhusu umoja wa Wakristo, ukiwa na Yesu kama jiwe kuu la msingi.
Majengo hayo ya ibada yanaweza kuwa na ubora tofauti hata upande wa sanaa; baadhi yake yanatembelewa na watalii na kuhifadhiwa kwa bidii kwa sababu hiyo.
Kwa namna ya pekee ni muhimu Kanisa kuu la kila jimbo (dayosisi), halafu Basilika na Patakatifu.
Jina hilo lilitumika kwa jumuia mama ya Yerusalemu, kwa kila mojawapo ya jumuia za Kikristo zilizotokana na umisionari wa wafuasi wa Yesu Kristo, na kwa umoja wao wa kimataifa uliotazamwa na Mtume Paulo kuwa Mwili wa Kristo, ukiwa na Yesu kama kichwa chake.
Kanisa ni mwili wa Kristo, ambapo ye ndie kichwa. Waefeso 1:22-23 yasema, “Akivitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.” Mwili wa Kristo umejengwa na wanaoamini katika Yesu Kristo toka siku ya Pentekosti (Matendo Ya Mitume 2) hadi Kristo arudi. Mwili wa Kristo uko na sehemu mbili:
1) Kanisa lote kwa ujumula ambalo ni wale wote wako na uhusiano na Kristo. “Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni Upendo” (1 Wakorintho 12:13). Aya hii inasema yeyote atakaye amini in sehemu ya mwili wa Kristo na ameupokea Roho wa Kristo ni ushaidi. Kanisa la jumla la Mungu ni wale wote ambao wamepokea wokovu kwa imani katika Yesu

WAISLAM WENYE KUIMBA/KUSIKILIZA MUZIKI WATAGEUZWA KUWA NYANI NA NGURUWE.


HUU NI MSIBA MKUBWA SANA KWA WAISLAM WOTE DUNIANI WANAO SIKILIZA MUZIKI AU IMBA MUZIKI.
Muziki ni haraam kutokana na dalili dhahiri tulizopewa katika Qur-aan na Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
وقال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((ليكونن من أمتي أقوام يستحلون الحر و الحرير و الخمر و المعازف، و لينزلن أقوام إلى جنب علم، يروح عليهم بسارحة لهم، يأتيهم لحاجة، فيقولون: ارجع إلينا غدا، فيبيتهم الله، ويضع العلم، ويمسخ آخرين قردة وخنازير إلى يوم القيامة ((رواه البخاري
Na akasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Watakuweko watu katika Ummah wangu watakaojaribu kuhalilisha zinaa, uvaaji wa hariri, pombe na MUZIKI. Baadhi ya watu watakuwa pembeni mwa mlima na mchungaji wao atawajia jioni na kuwaomba haja [fulani]. Watasema: “Rudi kesho”. Allaah Atawaangamiza usiku, Atawaangushia milima kisha Atawabadilisha waliobakia wawe nyani na nguruwe na watabakia hivyo hadi siku ya Qiyaamah))[Al-Bukhaariy]
Imaam Abu Haniyfah amesema: “Kuimba (nyimbo, ngoma) ni katika madhambi makubwa ambayo inatakiwa Muislamu kujiepusha nayo haraka”
Khofu zaidi imuingie Muislamu kuwa anaweza kupata adhabu ya kugeuzwa nyani au nguruwe kwa maasi haya kama tulivyoonywa katika Hadiyth ifuatayo:
Na kasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Watu katika Ummah wangu watakunywa pombe wakiipa jina jengine lisilokuwa hilo, MIZIKI itapigwa kwa ajili yao na watakuweko waimbaji wanawake. Allaah Atawadidimiza ardhini na Atawageuza wawe nyani na nguruwe)) [Ibn Maajah na Shaykh Al-Albaaniy ameipa daraja ya Sahiyh]
GHADHABU ZA ALLAH KUWAANGAMIZA WAFANYAO MAASI HAYA
Vile vile ghadhabu za Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) ni kali mno za kuangamizwa pindi maasi haya yatakapodhihirika.
عن عمر بن حصيل عن رسول الله صلى الله عليه وسلم انه قال: ((يكون فى امتى قذف ومسخ وخسف)): قيل يارسول الله ومتى ذلك قال: ((اذا ظهرت المعازف… )) اخرجه الترمذى وصححه العلامه الالبانى
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Kutatokea katika Ummah huu maafa ya kuteremshiwa mawe kutoka mbinguni, kugeuzwa maumbile ya binaadamu [kugeuzwa kufanywa nyani na nguruwe] na mididimizo [ya ardhi]. Ikaulizwa: Ewe Mjumbe wa Allaah, lini yatatokea hayo? Akasema: ((Itakapodhihirika muziki … )) [At-Trimidhy na ameipa daraja ya Sahiyh Shaykh Al-Albaaniy]
SAUTI ZA NYIMBO ZIMELAANIWA DUNIANI NA AKHERA
قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((صوتان ملعونان فى الدنيا والاخره مزمار عند نعمه ورنه عند مصيبه ((البزار و صححه العلامه الالبانى
Na kasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Sauti mbili maluuni [zilizolaaniwa] duniani na Akhera; mizumari katika furaha na kuombeleza katika misiba)) [Al-Baazaar – na Shaykh Al-Albaaniy kaipa daraja ya Sahiyh]
Hivyo tumeona kuna umuhimu mkubwa wa kuwakumbusha ndugu zetu waepukane na haramu hii ili wajiokoe na ghadabu za Mola Mtukufu, ghadhabu kali ambazo zinafika kumgeuza mtu awe nyani au nguruwe kama tutakavyosoma katika hizi dalili za wazi wazi zenye uhakika.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
((وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا أُولَئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ))
((Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno ya upuuzi, ili wawapoteze watu na njia ya Mwenyezi Mungu pasipo kujua, na wanaichukulia ni maskhara. Hao watapata adhabu ya kuwafedhehesha)) [Luqmaan: 6]
Ibn Mas’uud (Radhiya Allaahu ‘anhu) amesema kuhusu Aayah hii “Naapa kwa Allaah hii inamaanisha ni kuimba” [At-Twabariy 20:127]
وعن ابن عباس قال عن آية: ((ومن الناس من يشتري لهو الحديث))، قال :الغناء وأشباهه إسناده صحيح – المحدث: الألباني
Na Ibn ‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhuma) pia amesema kuhusu Aayah: ((Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno ya upuuzi)) “Ni nyimbo na maneno ya yanayofanana (ya upuuzi)” [Isnaad Sahiyh kutoka kwa Shaykh Al-Albaaniy]
Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anamwambia Ibliys:
((وَاسْتَفْزِزْ مَنِ اسْتَطَعْتَ مِنْهُمْ بِصَوْتِكَ وَأَجْلِبْ عَلَيْهِم بِخَيْلِكَ وَرَجِلِكَ وَشَارِكْهُمْ فِي الأَمْوَالِ وَالأَوْلادِ وَعِدْهُمْ وَمَا يَعِدُهُمُ الشَّيْطَانُ إِلاَّ غُرُورًا))
((Na wachochee uwawezao katika wao kwa sauti yako, na wakusanyie jeshi lako la wapandao farasi na waendao kwa miguu. Na shirikiana nao katika mali na wana, na waahidi. Na shaytwaan hawapi ahadi ila ya udanganyifu)) [Al-Israa: 64]
Hii inamaanisha ni nyimbo kama ilivyo rai ya Mujaahid katika Tafsiyr ya Ibn Kathiyr]
Vile vile Hadiyth zifuatazo zimedhihirisha uharamu wa nyimbo, ngoma na kila aina ya muziki:
عبدالله بن عمرو بن العاص عن رسول الله صلى الله عليه وسلم انه قال: ((إن الله حرم الخمر والميسر والكوبه وكل مسكر حرام ((إسناده صحيح
و في رواية أحمد قال سفيان: قلت لعلي بن بذيمة: “ما الكوبة؟” قال: “الطبل”
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amru ibnul ‘Aasw kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Ameharamisha pombe na kamari na kuubah na kila kilinacholewesha ni haram)) [Isnaad yake ni Sahiyh]

Wednesday, November 16, 2016

MUHAMMAD AWARUHUSU WAISLAM KULA NYAMA ZA FISI NA MIJUSI KAFIRI

Waislam wapo mstari wa mbele na wanasema kuwa eti Nguruwe ni Haran, lakini wamesahau kuwa Torati inakataza kula Ngamia, Fisi, nk.
MUHAMMAD AWARUHUSU WAISLAM KULA NYAMA YA FISI:
Sayyidina Ibn Ammar (RA) alisema kuwa, siku moja alimuuliza Jabir Jbn Abdullah (RA) kuhusu uwindaji wa FISI. Alinijibu na kusema, inaruhusiwa kuwinda Fisi. Nilimuuliza, Je, tunaruhusiwa kula, na akanijibu kuwa Kula Fisi ni Halal (Inaruhusiwa kula Fisi).
Nikamuuliza tena, Je, Nabii wa Allah(SAW) aliruhusu kula Fisi? Jabir r alinijibu na kusema. NDIO, Nabii wa Allah aliruhusu kula Fisi.
[Abu Dawud 3801, T 1798, Ibn e Majah 3085, Ahmedl4456]
9- Kitabu cha HAJJ.
MTUME MUHAMMAD ASEMA KULA NYAMA YA MIJUSI/KENGE NI HALAL.
Sahih Muslim Kitabu 21, 4788 Idadi :
Ibn 'Umar taarifa kwamba kulikuwa na baadhi ya watu na Mtume wa Allah (amani iwe juu yake) miongoni mwa maswahaba wake alikuwepo Sad. Basi ililetwa nyama ya Mjusi na mwanamke miongoni mwa wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (amani iwe juu yake) alisema: Ni nyama ya mjusi. Hapo Nabii Muhammad alisema: Kuleni hiyo nyama ya Mjusi kwa kuwa ni halali…
Eti kula Nguruwe ni haram lakini wanakula Fisi na Mijusi
Karibu kwa Yesu aliye hai na Mungu Mkuu,
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

ALLAH AMETEREMSHA AYA NA KUSEMA MUHAMMAD NI NABII WA UONGO


WAISLAM BADO WAMENG'ANG'ANIA ETI MUHAMMAD NI MTUME WA MUNGU, LAHA HASHA.
USHAHIDI HUU HAPA!!!!
ALLAH ANASEMA ATAUKATA MSHIPA MKUBWA WA MOYO WA NABII WA UONGO:
Quran 69;44_46 Allah ataukata mshipa mkubwa wa Moyo wa Nabii wa uongo.
MUHAMMAD ANAKIRI KUWA MSHIPA WAKE MKUBWA MOYO UMEKATWA NA ALLAH:
USHAHIDI WA KWANZA:
Sahih Bukhari 5;59;713 Muhamadi amekiri wakati anakufa: Ninahisi kama mshipa mkubwa wa Moyo wangu unakatwa .
USHAHID WA PILI:
Abu Dawud 34;4498 huu ndio wakati ambapo mshipa mkubwa wa Moyo wangu unakatwa
Swali moja tu kwa Waislam: ..Allah kamwita Muhammad nabii wa uongo, Je kwa nini nyinyi Waislamu mnamfuata nabii wa Uongo?
Tafadhali toeni majibu yenye aya za Allah.

YESU YUPO KILA MAHALI, KOTEKOTE DUNIANI.


MATHAYO 18:20 “Kwa kuwa walipo wawili watatu,wamekusanyika kwa jina langu, mimi nipo papo hapo katikati yao”.
Mwenye uwezo wa kukaa mahali pote ni Mungu.
"JESUS IS OMNIPRESENT"

KWA NINI YESU ALIVUNJA SABATO?


Ndugu msomaji,
Hebu tuangalie mifano kadhaa hapa:
MFANO WA KWANZA
Yesu alipomponya mtu ambaye alikuwa hawezi kwa muda wa miaka 38, alimwambia ‘jitwike godoro lako, uende.’ (Yohana 58). Hii ilikuwa ni siku ya sabato.
Lakini tunaona kwamba Wayahudi walipomwona mtu huyo walimwambia, Leo ni sabato, wala si halali kwako kujitwika godoro. (Yohana 5:10). Bila shaka walisema hivi kwa kuwa walifahamu fika jinsi sabato inavyotakiwa kutunzwa.
Hii ni kusema kwamba, kwa kadiri ya kanuni za utekelezaji wa sabato, hili lilikuwa ni kosa. Sasa, swali ni kwamba, kwa nini Yesu alivunja sabato kwa kumruhusu yule mtu abebe godoro?
MFANO WA PILI
Wayahudi walipomkasirikia Yesu kwa sababu ya kumruhusu yule mtu kubeba godoro siku ya sabato, Bwana Yesu aliwajibu kwamba: Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. (Yohana 5:17). Haya ni maneno ya ajabu sana. Wewe uliye Mungu ulituambia kwamba siku ya sabato tusifanye kazi bali tupumzike; tumemwona mtu anafanya kazi ya kubeba godoro, tumekuja kwako, lakini wewe si tu kwamba hukumkemea, bali unasema tena kwamba na wewe unafanya kazi hata sasa (siku ya sabato)!
Kama sabato hasa ni kuacha kufanya kazi, iweje tena Yesu atamke jambo ambalo ni wazi kabisa linavunja sheria aliyoiweka mwenyewe ya kutofanya kazi; yaani aseme kuwa hata sasa yeye anafanya kazi?
MFANO WA TATU
Siku moja Yesu aliingia kwenye sinagogi ambamo mlikuwamo mwanamke mwenye pepo wa udhaifu. Yesu alimponya mama yule.
Hata hivyo, Biblia inasema: Basi mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu amemponya mtu siku ya sabato, akajibu, akawaambia mkutano, Kuna siku sita zifaazo kufanya kazi, basi njoni mponywe katika siku hizo, wala si katika siku ya sabato. (Luka. 13:14).
Maneno haya ya mkuu wa sinagogi yanatuonyesha kwamba, jambo alilofanya Yesu lilikuwa ni kuvunja sabato. Swali ni lilelile, kwa nini Yesu alivunja sabato?
Tunafahamu kuwa maandiko yanasema kwamba kuvunja sabato ni dhambi, tena ambayo iliadhibiwa vikali sana. Na katika mifano hiyo hapo juu, tunaona kwamba Yesu alivunja sabato kwa kufanya mambo ambayo jamii nzima ilikuwa haiyafanyi siku ya sabato. Kwa harakaharaka, mtu anaweza kusema kwamba, Yesu alitenda dhambi.
Lakini wakati huohuo, maandiko yanasema kwamba, katika kuishi kwake kote hapa duniani, Bwana Yesu hakuwahi kutenda dhambi. (Waebrania 4:15).
Swali la kujiuliza hapa ni kwamba, iweje uvunje sabato, jambo ambalo ni dhambi, halafu uhesabiwe kuwa hujatenda dhambi? Pili, iweje wewe ambaye ndiye ulisema watu wapumzike siku ya sabato, ndio uwe wa kufanya kinyume na agizo lako mwenyewe? (Maana Yesu ndiye Mungu aliyeagiza sheria ya sabato ifuatwe). Iweje hapa yeye ndiye awe wa kuivunja?

ADHABU YA KUVUNJA SABATO


Utunzaji wa sabato uliandamana na utoaji adhabu kwa yeyote ambaye alivunja sheria hiyo. Mtu ambaye aliasi sheria ya sabato, adhabu yake ilikuwa ni kuuawa. Maandiko yanasema: Kila mtu atakayefanya kazi yoyote siku ya sabato, hakika yake atauawa. Sasa tukija kwenye agizo la kushika sabato halikuwa ni siku ya kukusanayika, bali ni pumziko la kazi tu na kustarehe kama tunavyoweza kuona katika kitabu cha KUTOKA 31:14-15, “Basi mtaishika hiyo sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake. Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa Bwana, kila mtu atakayefanya kazi yoyote katika siku ya sabato, HAKIKA YAKE ATAUAWA.”
Pia KUTOKA 35:2 Biblia inasema, “Fanyeni kazi siku sita, lakini siku ya saba itakuwa siku takatifu kwenu; ni sabato ya kustarehe kabisa kwa Bwana; mtu awaye yote atakayefanya kazi yoyote katika siku hiyo ATAUAWA”.
Maswali kwa watunza Sabato:
1. Je umesha wai vunja Sabato?
2. Je, umesha wai uwa mtu kwa sababu alivunja Sabato?
3. Kwanini hamfuati hii amri ya kuuwa watu wanao vunja Sabato?
Ndio maana ninasema kuwa Yesu ndio Mwishop wa Sabato na aliitengua.
Ni mimi Max Shimba Mtumwa Yes Kristo

UCHAWI WASHAMIRI ZANZIBAR


WAZIKA VIPANDE VYA MITI WAKIFIKIRIA MTU
MAREHEMU AONEKANA AKITEMBE MITAANI
Mtu mmoja aliyezikwa wiki mbili zilizopita huko Zanzibar, akutwa akiwa hai anatembea mitaani bila wasiwasi.
Wananchi walipokwenda kukagua kaburi wakakuta kaburi likiwa tupu ila wamekuta vitambaa vya sanda na miti kama inavyo onekana.
Nini maoni yako ?.....akikisha una like na kushea ili marafiki zako nao waone kabla ya kutoa jibu

Jesus is good because He is God

 

TRENDING NOW