Tuesday, January 10, 2017

ALLAH NA MUHAMMAD NI WAPINGA KRISTO

No automatic alt text available.
ALLAH ATEUA MTUME WA MAJINI NA MPINGA KRISTO 666
1. Allah ateua Mtume kwa Majini Quran 6: 130
2. Allah ateua Mtume wa Wanyama Surat An Naml 82
Ndugu zanguni,
Allah anasema katika Quran kuwa, ameteua Mtume kwa kila kiumbe mpaka Majini machafu. Hebu soma aya hapa chini
ALLAH ANASEMA KUWA MAJINI YANA MTUME WAO
Quran 6: 130. Enyi makundi ya majini na watu! Je, hawakukujieni Mitume kutokana na nyinyi wenyewe wakikubainishieni Aya zangu, na wakikuonyeni mkutano wa Siku yenu hii. Nao watasema: Tumeshuhudia juu ya nafsi zetu. Na yaliwadanganya maisha ya dunia. Nao watajishuhudia wenyewe ya kwamba walikuwa makafiri.
Swali lamsingi kwa Allah :
Jina la Mtume wa Majini ambaye ni Jini ni nani?
Kwasababu kila Umma ulipewa kitabu na mtume wake, Je, umma wa Majini walipewa kitabu gani?
Lakini nilipo soma Hadith nikagundua kuwa, Muhammad alikuwa anaongea na Majini na kuyafundisha Quran.
MTUME MUHAMMAD AKUTANA NA MAJINI USIKU
Allah S.W.T. ametuhakikishia wazi kuwa ujumbe aliopewa Mtume S.A.W. ulikuwa kwa Wanadamu na Majini na Mashetani pia. Na katika Qurani na Hadithi za Mtume S.A.W. kuna dalili zilizo wazi zinazoyakinisha kuwa Mtume S.A.W. alikuwa akikutana nao na kuwafundisha dini. Na hata wakati mwingine Majini walikuwa wakitoa majibu mazuri zaidi kuliko Binadamu kwenye masuala ya dini. Na mfano ni wakati waliposomewa Suratir Rahmaan. Hadithi iliyopokelewa na Jaabir bin Abdallah R.A.A. na iliyotolewa na Ttirmidhi kasema, “Wakati ambapo Mtume S.A.W. alipowasomea Majini Suratir Rahmaan, “
لَقَدْ قَرَأْتُهَا ‘‘يعني سُورَةَ الرَّحْمَنِ’’ عَلَى الْجِنِّ …، فَكَانُوا أَحْسَنَ مَرْدُودًا مِنْكُمْ ، كُنْتُ كُلَّمَا أَتَيْتُ عَلَى قَوْلِهِ ]فَبِأَيِّ آلاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ[ قَالُوا: لا بِشَيْءٍ مِنْ نِعَمِكَ رَبَّنَا نُكَذِّبُ ، فَلَكَ الحمد
Maana yake, “Hakika nimewasomea Majini (yaani Suratir Rahmaan)…wamejibu vizuri zaidi kuliko nyinyi. Kila nilipofikia kauli Yake (Mwenyezi Mungu S.W.T.) “Fabiayyi A-alaai Rabikumaa Tukadhibaan.) Maana yake, “Basi ipi katika neema za Mola wenu ambayo mnayoikanusha kuwa si kweli?” (Basi Majini) walijibu “Laa bishaay Min Niamika Rabbana Nukadhibu, Falakal Hamdu.” Maana yake, “Hakuna neema yoyote katika neema Zako Mola wetu tunayoikadhibisha, bali tunashukuru.” Na Mtume S.A.W. alipowasomea Wanadamu hawakujibu chochote, akawaambia, “Ndugu zenu wa Ki-Jini wamejibu jawabu nzuri waliposikia haya.” Na dalili nyingine kuwa Mtume S.AW. pia alikuwa ametumwa kwao ni kisa cha baadhi ya Majini ambao baada ya kuisikiliza Qurani waliiamini na wakarejea kwao na kuanza kuwaita wenzao kwenye dini ya Kiislamu.
ALLAH ANASEMA KUWA MAJINI YALITUMWA KWA MUHAMMAD ILI KUSIKILIZA QURAN
ALLAH HUYO HUYO ALISEMA KUWA KILA WATU/VIUMBE/WANYAMA WALIPEWA MTUME WAO. HAPO TEYARI KUNA SHAKA KWENYE QURAN YA MUHAMMAD AMBAYO SASA INAKABIDHIWA MAJINI MACHAFU.
Allah kasema katika Suratil Ahqaaf aya ya 29 mpaka 32, “
]وَإِذْ صَرَفْنَا إِلَيْكَ نَفَرًا مِنْ الْجِنِّ يَسْتَمِعُونَ الْقُرْآنَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوا أَنْصِتُوا فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوْا إِلَى قَوْمِهِمْ مُنْذِرِينَ * قَالُوا يَا قَوْمَنَا إِنَّا سَمِعْنَا كِتَابًا أُنْزِلَ مِنْ بَعْدِ مُوسَى مُصَدِّقًا لِمَا بَيْنَ يَدَيْهِ يَهْدِي إِلَى الْحَقِّ وَإِلَى طَرِيقٍ مُسْتَقِيمٍ * يَا قَوْمَنَا أَجِيبُوا دَاعِي اللَّهِ وَآمِنُوا بِهِ يَغْفِرْ لَكُمْ مِنْ ذُنُوبِكُمْ وَيُجِرْكُمْ مِنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ * وَمَنْ لا يُجِبْ دَاعِي اللَّهِ فَلَيْسَ بِمُعْجِزٍ فِي الأرْضِ وَلَيْسَ لَهُ مِنْ دُونِهِ أَولِيَاءُ أُوْلَئِكَ فِي ضَلالٍ مُبِينٍ[
Maana yake, “Na (wakumbushe) wakati tulipowaleta kundi la Majini kuja kwako kusikiliza Qurani. Basi walipoihudhuria walisema (kuambiana): “Nyamazeni! (Msikilize maneno ya Mwenyezi Mungu)” Na ilipokwisha somwa walirudi kwa jamaa zao kwenda kuwaonya. Wakasema “Enyi watu wetu! Sisi tumesikia Kitabu kilichoteremshwa baada ya (Nabii) Musa, kinachosadikisha yaliyokuwa kabla yake na kinachoongoza kwenye haki na kwenye njia iliyonyooka. Enyi kaumu yetu! Muitikieni Mlingani, (Muitaji) wa Mwenyezi Mungu na muaminini, atakusameheni (Mwenyezi Mungu) dhambi zenu na atakukingeni na adhabu iumizayo. Na wasiomuitikia Muitaji wa Mwenyezi Mungu, basi hao hawatamshinda (asiwapate) hapa katika ardhi, wala hawatakuwa na walinzi mbele Yake. Hao wamo katika upotofu ulio dhahiri.”
Na kisa kingine ni cha Majini waliosikia Qurani kutoka kwa Mtume S.A.W wakati alipokuwa akiwasalisha Masahaba wake Sala ya Alfajiri. Na hii ilikuwa bila ya yeye kuwa na habari mpaka Mwenyezi Mungu S.W.T. alipomjulisha. Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil Jin aya ya 1 na ya 2, “
]قُلْ أُوحِيَ إِلَيَّ أَنَّهُ اسْتَمَعَ نَفَرٌ مِنْ الْجِنِّ فَقَالُوا إِنَّا سَمِعْنَا قُرْآنًا عَجَبًا * يَهْدِي إِلَى الرُّشْدِ فَآمَنَّا بِهِ وَلَنْ نُشْرِكَ بِرَبِّنَا أَحَدًا[
Maana yake, “Sema: “Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la Majini lilisikiliza (Qurani) likasema: “Hakika sisi tumesikia Qurani ya ajabu. Inaongoza katika uwongofu; kwa hivyo tumeiamini, wala hatutamshirikisha yeyote tena na Mola wetu.”
Makala haya yametolewa katika kitabu changu kiitwacho, "Hakika ya Majini."
ALLAH SASA ATEUA MTUME KWA WANYAMA = 666. KUMBE BASI ALLAH NA MUHAMMAD NA DINI YAKE NDIO 666
Surat An Naml 82. Na itapo waangukia kauli juu yao, tutawatolea mnyama katika ardhi atakaye wasemeza, ya kuwa watu walikuwa hawana na yakini na Ishara zetu
Kifungu kuu katika Biblia ambacho kinataja "alama ya mnyama" ni Ufunuo 13:15-18. Marejeo mengine yanaweza kupatikana katika Ufunuo 14: 9, 11, 15:2, 16:2, 19:20, na 20:4. Alama hii hutumika kama muhuri kwa wafuasi wa Mpinga Kristo na nabii wa uongo (msemaji wa Mpinga Kristo). Nabii wa uongo (mnyama wa pili) ndiye ambaye husababisha watu kuchukua alama hii. Alama hasa huwekwa katika mkono au paji la uso na sio kadi mtu atabeba.
Je, jina la Mtume wa Wanyama ambaye ni Mnyama ni nani?
Je, wanyama walipewa kitabu gani?
SIRI IMESHA FUNGUKA, SASA TUNAFAHAMU KUWA, ALLAH NDIE ATAKAYE LETA MPINGA KRISTO 666, NA ALLAH AMEKIRI KATIKA SURAT AN NAML KUWA YEYE AMESHA TEUA MTUME AMBAYE NI MNYAMA NA HUYO MTUME ANASOMA QURAN YA MUHAMMAD.
KAMA kweli Quran ni maneno ya Allah, na aliiteremsha, basi, leo tunafahamu kuwa Allah sio tu ataleta Mpinga Kristo, bali Allah na Muhammad ndio Mpinga Kristo.
Ndugu msomaji utakaesoma mpambano huu sitanukuu moja kwa moja maandiko lakini nitakachokiandika, mashahidi mtakuwa wenyewe kuona kama ni kweli au uongo ya kuwa vitabu hivi vinapambana kiasi hicho..nami sitaandika uongo kamwe.
Hebu tuanze:
BIBLIA: ‘Yesu Kristo alisulubiwa. QURAN: hapana hapana walimsulubisha mwandaazimu mwingine wakizani ndiye!!.
BIBLIA: Yesu ni Mwana wa Mungu. QURAN: ni uongo kwa kuwa Mungu hana mwana wala hazai!!.
BIBLIA: ’tunapata msamaha wa dhambi kupitia damu ya Yesu. QURAN: sivyo kabisa…Mnyaai Mungu ndiye akusameheni madhambi yenu pale mtakapoenda Makka japo mara moja kuhiji. (kiswali chandu cha uzushi..wale masikini je?..Ndiyo kusema pepo ni ya matajiri tu?!!).
BIBLIA: Majini wana asili ya mashetani, ni kundi au jeshi la yule muovu, msishirikiane nayo katika ibada wala kuwatolea sadaka.QURAN: ALLAH asema:
nimekuumbeni na majini ili mpate kuniabudu!! (swali la uzushi:Shetani na majini yake yanaabudu na waisilamu ili yaende wapi wakati wao walisha laaniwa na wanachosubiri ni jehanam tu!!).
Huu ni Msiba Mwengine katika dini ya Allah ambayo sasa tumejifunza kuwa ni ya Mpinga Kristo.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

INA MAANA GANI YESU KUWA MWANA WA MUNGU?

Image may contain: text
1. Yesu ni Mwana wa Mungu
2. Yesu ni Mungu katika Mwili

Ndugu Msomaji,
Yesu si Mwana wa Mungu kulingana na ubaba wa kawaida wa binadamu. Mungu hakuoa na kupata mwana wa kiume. Mungu hakufanya tendo la ndoa na Mariamu, na pamoja naye kuzaa mtoto wa kiume. Yesu ni Mungu katika hali kwamba ni Mungu anajithirihisha kama mwili. (Yohana 1:1, 14) Yesu ni mwana wa Mungu kwa dhana kwamba Mariamu alipata mimba kupitia Roho Mtakatifu. Luka 1:35 yasema, “Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.”
YESU NI MUNGU KATIKA MWILI
Yohana 1:1 inasema “Neno alikuwa Mungu”. Yohana 1:14 inasema “Neno akafanyika mwili.” Hii inaonyesha wazi ya kwamba Yesu ni Mungu katika mwili. Matendo 20:28 inatuambia, “…Muwe wachungaji wa kanisa la Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe,” Ni nani aliyelinunua kanisa kwa damu yake mwenyewe? Yesu kristo. Matendo 20:28 inasema ya kwamba Mungu alilinunua kanisa kwa damu yake mwenyewe. Kwa hivyo Yesu ni Mungu!

YESU AKUBALI KUITWA MUNGU NA WANAFUNZI WAKE
Tomaso mwanafunzi wa Yesu alisema kuhusu Yesu, “Bwana na Mungu wangu” (Yohana 20:28). Yesu hamsahihishi kwa kuyasema haya. Tito 2:13 inatuhimiza kusuburi kurudi kwa Mungu wetu na mwokozi – Yesu kristo (Pia tazama petro wa pili 1:1). Waebrania 1:8, Baba asema juu ya Yesu, “Lakini juu ya mwana asema haya, “Na Kiti chako cha enzi, wewe Mungu, Kitadumu milele, na haki itakuwa fimbo ya ufalme wako.”

MALAIKA WANAMWABUDU YESU
Katika kitabu cha ufunuo wa Yohana, Malaika alimwamuru mtume Yohana kumuabudu Mungu tu(ufunuo wa Yohana 19: 10). Mra nyingi Yesu katika maandiko aabudiwa (Mathayo 2;11; 14:33; 28:9,17; Luka 24:52; Yohana 9:38). Hakemei watu kwa kumuabudu. Kama Yesu hakuwa Mungu, angewaambia watu wasimuabudu, kama vile malaika alivyofanya. Kuna aya nyingi za maandiko zinazoshuhudia ya kwamba Yesu ni Mungu.

Wakati wa kujaribiwa kwake mbele ya viongozi wa Kiyahudi, kuhani mkuu alimtaka Yesu, “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu” (Mathayo 26:63). “Yesu akamwambia wewe umesema,’ Yesu akamwambia, wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni” (Mathayo 26:64) viongozi wa Kiyahudi walimdhania kwa kukufuru (Mathayo 26:65-66). Baadaye mbele ya Pilato, “Wayahudi wakamjibu, Sisi tunayo sheria, na kwa sheria hiyo amestahili kufa, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu” Yohana 19:7) ni kwa nini makisio yake kuwa Mwana wa Mungu yachukuliwe kuwa kufuru na astahili hukumu ya kifo? Wayahudi wilielewa vizuri sana chenye Yesu alimaanisha kwa maneno haya “Mwana wa Mungu” kuwa Mwana wa Mungu ni kuwa hali moja na Mungu. Mwana wa Mungu “wa Mungu” kusema uko katika hali sawa na Mungu-hakika kuwa Mungu- kulikuwa sawa na kukufuru kwa viongozi wa Kiyahudi; kwa hivyo walimtaka Yesu auwawe, kulingana na Mambo ya Nyakati 24:15. Waebrania 1:3 inadhihirisha haya wazi, “Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu.”
Mfano mwingine unaweza patikana katika Yohana 17:12 mahali Yuda anaelezwa kama mwana wa “upotevu”? jina upotevu lamaanisha “uharibivu” Yuda hakuwa mwana wa uharibivu, lakini mambo hayo ndio ya kutambulisha maisha ya Yuda. Yuda anadhihirisha upotevu. Vile vile Yesu mwana wa Mungu. Ni Mungu anajidhihirisha (Yohana 1:1,14).
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015.
ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

MTUME PAULO ALIFUNDISHA KWENYE SINAGOGI KILA SABATO

Image may contain: text and outdoor
Matendo ya Mitume 18:
1 Baada ya mambo hayo, Paulo akatoka Athene akafika Korintho.
2 Akamwona Myahudi mmoja, jina lake Akila, mzalia wa Ponto; naye amekuja kutoka nchi ya Italia siku za karibu, pamoja na Prisila mkewe, kwa sababu Klaudio amewaamuru Wayahudi wote watoke Rumi, naye akafikilia kwao;
3 na kwa kuwa kazi yao ya ufundi ilikuwa moja, akakaa kwao, wakafanya kazi pamoja, kwa maana walikuwa mafundi wa kushona hema.
4 Akatoa hoja zake katika SINAGOGI kila Sabato, akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wayunani.
5 Hata Sila na Timotheo walipotelemka kutoka Makedonia, Paulo akasongwa sana na lile neno, akiwashuhudia Wayahudi ya kwamba Yesu ni Kristo.
HUWA KUNA HOJA YA WAISLAM KUWA, ETI YESU ALIKUWA MUISLAM KWASABABU ALIINGIA KWENYE SINAGOGI.
JE, TUKITUMIA UTAALAMU NA AU MBINU HIYO HIYO NA TUWAULIZE WAISLAM. JE, MTUME PAULO ALIKUWA MUISLAM MAANA ALIINGIA KWENYE SINAGOGI?
Cross reference:
Matendo 9 aya ya 20.
Matendo 17 aya ya 2.
Matendo 19 aya ya 8.
Basi tuendelee kujifunza neno lake bila kuchoka.
Barikiwa sana.
Shalom.

MTUME PAULO ANAVYO WANYIMA USINGIZI WAISLAM

Image may contain: 2 people, beard and text
Kati ya watu wanaowasumbua sana ndugu zetu Waislamu ni shujaa wa Bwana Yesu, Mtume Paulo. Na hii haikuanza kwa Waislamu pekee, bali kuanzia kwa washika torati waliokuwako wakati wake, yaani mafarisayo, wakuu wa makuhani, waandishi pamoja na Wayahudi wa kawaida waliofuata dini ya Kiyahudi.
Waislamu wanaendeleza tu ili roho ya upinzani dhidi ya Injili iokoayo ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Zifuatazo ni baadhi ya sababu ambazo Waislamu wanasema zinawafanya wamkatae Mtume Paulo, kama nilivyozitoa kwenye facebook kwenye post mojawapo ya ndugu mmoja wa Kiislamu.
Wanasema:
MOJA:
Eti aliweka amri ya watu wasitahiriwe, ndio maana Wakristo wengi leo wana magovi
JIBU:
Tohara ni suala la afya ya kawaida wala halina uhusiano na kwenda mbinguni. Yaani, ukitaka kufanyiwa tohara, ni faida kwa mwili wako tu na wala sio kwa roho yako. Kinachoenda mbinguni ni mwili na wala sio roho. Mwili uwe umetahiriwa au haujatahiriwa, ukifa ni kuozea tu ardhini. Kwa hiyo, Mungu alilitumia hilo suala la tohara kama ishara ya mambo halisi ya rohoni, na sio ya mwilini:
(Kumb 10:16) Basi, zitahirini govi za mioyo yenu, wala msiwe na shingo ngumu.
(Kumb 30:6) BWANA, Mungu wako, atautahiri moyo wako, na moyo wa uzao wako, ili umpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, upate kuwa hai.
(Yer 4:4) Jitahirini kwa BWANA, mkaziondoe govi za mioyo yenu, enyi watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu; ghadhabu yangu isije ikatoka kama moto, ikawaka hata mtu asiweze kuizima, kwa sababu ya uovu wa matendo yenu.
SWALI KWA WAISLAM: Wapi kwenye Koran panasema kuwa Muhammad alikatwa govi lake? Mtupe aya tuione.
MBILI:
Eti alikuwa gaidi wa kuwaua wanafunzi wa Yesu kisha akadai ni mtume wao ili azidi kuwaua kifkra
JIBU
Hii ni hoja kichekesho. Tangu lini mkawa na huruma na wanafunzi wa Yesu? Mnasemaje kuhusu makundi yenye itikadi kali ambayo yanaua Wakristo duniani hivi leo, yanavunja makanisa na kuwalazimisha kufuata miungu yao? Je, nayo mnayalaani?

UYAHUDI AU MYAHUDI MAANA YAKE NINI? (SEHEMU YA KWANZA)

Image may contain: text
Kama linavyotumiwa na watu wengi leo, neno hili linarejezea watu wenye asili ya Kiebrania na wengine ambao wamegeuzwa imani na kuwa wafuasi wa dini ya Kiyahudi. Pia Biblia inataja kwamba kuna Wakristo walio Wayahudi kiroho ambao wanafanyiza “Israeli wa Mungu.”
Je, Wayahudi wa asili leo ni watu wa Mungu waliochaguliwa?
Wayahudi wengi huamini hivyo. Encyclopaedia Judaica (Jerusalem, 1971, Buku la 5, safu ya 498) inasema hivi: “WATU WALIOCHAGULIWA, ni jina la kawaida la watu wa Israeli, linaloonyesha kwamba watu wa Israeli wana uhusiano wa pekee na usio na kifani pamoja na Mungu wa ulimwengu wote. Hilo ni wazo kuu katika historia ya Wayahudi.”—Ona Kumbukumbu la Torati 7:6-8; Kutoka 19:5.
Katika Torati-vitabu vitano vya kwanza vitano katika Biblia Mwanzo 14:13 inafundisha kuwa Abramu, kawaida anayetambuliwa kama Myahudi wa kwanza, alikuwa kama ilivyoelezwa "Kiebrania." Jina "Myahudi" linatokana na jina la Yuda, mmoja wa wana kumi na wawili wa Yakobo na mmoja wa makabila kumi na mawili ya Israeli. Inavyoonekana jina "Myahudi" awali lilijulikana tu kwa wale ambao walikuwa wanachama wa kabila la Yuda, lakini wakati ufalme uligawanyika baada ya utawala wa Sulemani (1 Wafalme 12), neno lilimaanisha mtu yeyote katika ufalme wa Yuda, ambayo ni pamoja na kabila la Yuda, Benjamin, na Lawi.
Leo hii, wengi wanaamini kwamba Myahudi ni mtu yeyote ambaye ana uzao wa kimwili na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, bila ya kujali makabila ya awali kumi na mbili anapotoka.
Kwa mujibu wa marabi Wayahudi, Myahudi ni yule ambaye ana mama Myahudi au mtu ambaye rasmi hubadilishwa kwa Uyahudi. Mambo ya Walawi 24:10 mara nyingi inachukuliwa kuupa uaminifu huu imani, ingawa Torati huifanyi madai maalum kwa msaada wa mila hii. Baadhi ya wanazuoni husema kwamba haina uhusiano wowote na kile mtu anaamini. Wanazuoni hawa hutuambia kwamba Myahudi hana haja ya kuwa mfuasi wa sheria na desturi ili achukuliwe kuwa Myahudi. Kwa kweli, Myahudi hawezi kuwa na imani katika Mungu wakati wote na bado kuwa Myahudi kwa misingi ya tafsiri ya marabi hapo juu.
Wanazuoni wengine hufanya wazi kwamba kama mtu afuatavyo maagizo ya Torati na anakubali "kanuni kumi na tatu za Imani" ya Maimondes (Mwalimu Moshe ben Maimon, mmoja wa Wayahudi wasomi wakubwa wa kipindi), hawezi kuwa Myahudi. Ingawa mtu huyu anaweza kuwa "kibiolojia" Myahudi, hana uhusiano halisi na Wayahudi.
Mt. 21:42, 43: “Yesu akawaambia [wakuu wa makuhani na wanaume wazee kati ya Wayahudi wa Yerusalemu]: ‘Je, hamkusoma kamwe katika Maandiko, “Jiwe ambalo wajenzi walilikataa ndilo limekuwa jiwe kuu la pembeni. Limetokana na Yehova, nalo ni la kustaajabisha machoni petu”? Ndiyo sababu ninawaambia ninyi, Ufalme wa Mungu utachukuliwa kutoka kwenu na kupewa taifa lenye kuzaa matunda yake.’”
Je, agano la Mungu pamoja na Abrahamu linatoa uhakikisho kwamba bado Wayahudi ni watu wa Mungu waliochaguliwa?
Je, Wayahudi wote watageuzwa wamwamini Kristo na kupata wokovu wa milele?
USIKOSE SEHEMU YA PILI
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

ALLAH KASEMA ADUI YAKE MKUBWA NI YESU KRISTO "MFALME WA WAFALME" WA KWENYE BIBLIA

Image may contain: people sitting and text
Ndugu msomaji,
Waislamu hudai kuwa Muhammad ametumwa na Mwenyezi Mungu wao, ambaye ni Mfalme wa Wafalme . Lakini tusomapo Biblia Takatifu katika kitabu cha Ufunuo 17:14 “ Hawa watafanya vita na Mwanakondoo, na Mwanakondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme; na hao walio pamoja naye ndiyo walioitwa na wateule, na waaminifu”

Katika Ufunuo 19:11-16 “ Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita. Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe. Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa Neno la Mungu. Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi. Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi. Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA “


Yesu Kristo ndiye Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana. Lakini tunaposoma Hadithi sahihi za Kiislamu zinaeleza kuwa adui mkubwa wa Allah (s.w) wanayemwabudu Waislamu, ni yule anayeitwa Mfalme wa Wafalme.

Sahih Al- Bukhari, Vol.8.Hadithi Na.225, Al-Lu’lu Wal-marjan,Juzuu ya 3, Hadithi Na.1385 “Hadithi ya Abu Huraira (r.a) amesema,Mtume wa Allah (s.a.w) amesema,” Majina yaliyo dhalili mno na mabaya mbele za Allah ni mtu kujiita,Malikil-Amlaak (Mfalme wa Wafalme).”

Hivyo, ufunuo aliopokea Muhammad, ambao anatutaka na sisi Wakristo tuuamini haujatoka kwa Mungu tunayemwamini sisi Wakristo, yaani, Yesu Kristo. Bali kama alivyonukuliwa katika vitabu vya Kiislamu, unatokana na kuchezewa na Shetani, na kwa sababu hiyo kwetu anakuwa nabii na mtume wa uongo’

Biblia Takatifu imetuonya kuwachunguza mitume na manabii. Katika kitabu cha Ufunuo 2:1-2 “ Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu. Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao siyo ukawaona kuwa waongo”

Kwa mujibu wa aya hizi Muhammad s.a.w hastahili kuitwa nabii na mtume wa Mungu wa Kweli, bali anaangukia katika kundi la manabii na mitume wa uongo. Hatufai.

Zaidi ya hapo, Allah ambaye ni adui mkubwa wa Yesu Kristo ambaye ni Mfalme wa Wafalme sio Mwenyezi Mungu.

Mungu awabariki sana


Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

ALLAH KATEREMSHA AYA NA KUSEMA KUWA MASINAGOGI SIO MISIKITI

Image may contain: sky, text and outdoor
Ndugu msomaji,
Leo nataka nimalize NGEBE ZOTE za Waislam ambazo zinalazimisha kuwa eti Masinagogi ni Misikiti kwa kutumia Quran yao.
Katika Suratul Hajj aya ya 40 iliyo teremshwa na Allah huko Madina na kutafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani ( alie fanya tarjuma).
Andiko hili linataja majina ya majengo mbalimbali ya ibada ikiwemo na Sinagogi kwenye tafsiri ya Qur-an ya Kiswahili ya Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani.
Suratul Hajj 40. Wale ambao wametolewa majumbani mwao pasipo haki, ila kwa kuwa wanasema: Mola wetu Mlezi ni Mwenyezi Mungu! Na lau kuwa Mwenyezi Mungu hawakingi watu kwa watu, basi hapana shaka zingeli vunjwa nyumba za wat'awa, na Makanisa, na MASINAGOGI, na misikiti, ambamo ndani yake jina la Mwenyezi Mungu linatajwa kwa wingi. Na bila ya shaka Mwenyezi Mungu humsaidia yule anaye msaidia Yeye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mtukufu. Maelezo
SASA MADA INAANZIA HAPA:
1. Kama kweli Masinagogi ni Misikiti ya Wayahahudi, kwanini Allah ameyatofautisha hayo majengo kimajina, "Masinagogi na Misikiti" kwenye hii aya?
2. Kama Masinagogi ni Misikiti ya Wayahudi, kwanini Allah asinge sema Nyumba za Watawala za Wayahudi ni Misikiti, LAKINI akaziita Masinagogi.
3. Je Sinagogi laweza kuwa ni Msikiti katika uasili wa lugha?
4. Ikiwa kuingia tu kwenye Sinagogi kulimaanisha Yesu ni Muislam, je Paulo naye kwa tendo hilo lakuingia humo alikuwa Muislam?
5. Je, Paulo kuingia kwenye Sinagogi alikuwa anaingia kwenye Misikiti?
6. Kama Masinagogi ni Misikiti, kwanini kwenye Masinagogi kuna viti na kwenye Misikiti hakuna viti?
7. Kama Masinagogi ni Misikiti, kwanini kwenye Masinagogi hakuna maji ya kutawadha kama kwenye Misikiti?
8. Kama Masinagogi ni Misikiti, kwanini Masinagogi hayaangalii Makka kama Misikiti?
9. Kumbe Misikiti ni Masinagogi ya Waislam.
10. Mwislam ni mtu wa ajabu sana, anakubali kuwa Masinagogi ni Misikiti ya Wayahudi lakini atakataa kuwa Misikiti ni Masinagogi ya Waislam.
Ndugu Waislam, tafadhali jibuni kwa aya. Hoja ujibiwa kwa hoja.
Max Shimba Ministries

WATOTO WA MUNGU NI NANI?

Image may contain: 12 people, people standing


Biblia ipo wazi kwamba watu wote ni viumbe wa Mungu (Wakolosai 1:16), na kwamba Mungu anaipenda dunia nzima (Yohana 3:16), lakini ni wale tu ambao wamezaliwa mara ya pili ndio watoto wa Mungu (Yohana 1:12; 11:52; Warumi 8:16, 1 Yohana 3:1-10).
Ninani mwana wa Mungu?
Kuzaliwa kwa kiroho hufanya mtu kuwa mwana wa Mungu. Imeandikwa Yohana 1:12-13 "bali waliompokea aliwapa uwezo wakufanyika watoto wa Mungu ndio wale waliaminio jina lake walio zaliwa sikwa damu wala si kwa mapenzi ya mwili wala sikwa mapenzi ya mtu bali kwa Mungu."
Mungu amefungua njia yakuwa watoto wake. Imeandikwa 1Yahana 3:1 "Tazameni ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu na ndivyo tulivyo kwa sababu hii ulimwengu haututambui kwa kuwa aukutambua yeye."
Wakristo wamefanywa kuwa jamaa ya Mungu imeandikwa Warumi 8:16 "Roho mwenywe hushuudia pamoja na roho zetu ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu."
Tazama watoto washanga. imeandikwa Luka 18:16-17 "Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema waasheni watoto wadogo waje kwangu wala msiwazuie kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao amininawaambia, mtu yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe."
Katika maandiko, waliopotea kamwe hawajulikani kuwa watoto wa Mungu. Waefeso 2:3 inatuambia kwamba kabla ya sisi kuokolewa sisi tulikuwa "kiasili wana wa hasira" (Waefeso 2:1-3). Warumi 9:8 inasema kwamba "si watoto wa kawaida ambao ni watoto wa Mungu, lakini ni watoto wa ahadi ambao ni kuonekana kama uzao wa Ibrahimu." Badala ya kuzaliwa kama watoto wa Mungu, sisi tumezaliwa katika dhambi, ambayo hutenganisha sisi kutoka kwa Mungu na kutuweka sisi pamoja na Shetani kama adui wa Mungu (Yakobo 4:4, 1 Yohana 3:8). Yesu alisema, "Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, kwa maana nalitoka kwa Mungu na mimi nimekuja; wal sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma" (Yohana 8:42). Kisha mistari michache baadaye Yohana 8:44, Yesu aliwaambia Mafarisayo kwamba "nanyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda." Ukweli kwamba wale ambao hawajaokoka si watoto wa Mungu pia huonekana katika 1 Yohana 3:10: "Katika hili watot w Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake."
Sisi huwa wana wa Mungu wakati tumeokolewa kwa sababu tumetwaliwa katika familia ya Mungu kwa njia ya uhusiano wetu na Yesu Kristo (Wagalatia 4:5-6, Waefeso 1:5).
Shalom.

KUZALIWA MARA YA PILI MAANA YAKE NINI?

Image may contain: text
Wakati Yesu akizungumza na Nikodemo, alisema, Amin, Amin, nakuambia, mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu. Nikodemo akamwambia, “Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee?” “Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?” Yesu akajibu, “Amin, Amin, nakuambia, mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni Roho. Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, hamna budi kuzaliwa mara ya pili…” (Yohana 3:3-7).
Msemo “kuzaliwa mara ya pili” unamaanisha “zaliwa toka juu” Nikodemo alikuwa na uhitaji wa kweli. Alihitaji mabadiliko ya moyo wake... Mabadiliko ya kirohoUzao mpya, kuzaliwa mara ya pili, ni kitendo au hatua ya Kiungu ambapo uzima wa milele hupewa mtu yule aaminiye (2Wakorintho 5:17; Tito 3:5; 1Petro 1:3; 1Yohana 2:29; 3:9; 4:7; 5:1-4, 18). Yohana1:12, 13 inasema ya kuwa”kuzaliwa mara ya pili” pia ina maana “kufanyika mtoto wa Mungu”kwa imani katika jina la Yesu Kristo.
Kuzaliwa mara ya pili ina maana kufa kwa matendo ya mwili ya kale. Imeandikwa, Warumi 7:4 "Kadhalika ndungu zangu ninyi pia mmeifia torati kwa njia ya mwili wa Kristo mpate kuwa mali ya mwingine yeye aliyefufuka katika wafu kusudi tuzalie Mungu matunda."
Swali hasa ni kuwa, “kwa nini mtu anahitaji kuzaliwa mara ya pili?” Mtume Paulo katika Waefeso 2:1 asema, “Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi …” Kwa Warumi katika Warumi3:23, Mtume aliandika, ”kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu. “Kwahivyo mtu anahitaji kuzaliwa mara ya pili ili asamehewe dhambi zake na awe na uhusiano na Mungu.
Je, hii hutokea vipi? Waefeso2:8, 9 yasema, kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yoyote asije akajisifu.” Mtu anapo “okolewa”, basi yeye amezaliwa mara ya pili, akijazwa upya kiroho, na sasa amefanyika kuwa mwana wa Mungu kwa haki ya uzao mpya. Kwa kumwamini Kristo Yesu, yeye aliye adhibiwa kwa ajili ya dhambi alipokufa msalabani, ndiyo maana ya “kuzaliwa mara ya pili” kiroho. “Hata imekuwa mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya…” (2Wakorintho 5:17 a).
Kama bado hujaweza kumwamini Bwana Yesu Kristo kama mwokozi wa maisha yako, je utakuwa na utayari wa kupokea Roho mtakatifu wakati akizungumza na moyo wako? Unahitaji kuzaliwa mara ya pili. Je, utaomba maombi ya kutubu na ufanyike kuwa kiumbe kipya ndani ya Kristo hivi leo? “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndiyo wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu” (Yohana 1:12-13).
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Friday, January 6, 2017

FRANCE: Muslim workers’ religious demands for prayer-breaks, halal food, days off for Islamic holidays, and resulting loss of productivity caused car plant closure


Excessive and relentless religious demands of Muslim workers at a car factory in Paris contributed, in large part, to the plant’s closure, Drancy deputy-mayor Jean-Christophe Lagarde has disclosed.

Breitbart  Lagarde made the revelation during an appearance on public service broadcaster France Info on Tuesday, in which he was asked about “communitarian trends” in Islam, where communities are becoming more religious and more insular.

“Religion has nothing to do with work” began his response, but the Union of Democrats and Independents (UDI) president went on to admit that Islam has caused a number of problems related to employment in the state he represents.

“There were difficulties, including in my area, for example in Aulnay-sous-Bois. It was never said, but part of the PSA closure was down to the ubiquity of religion and the fact that there were religious demands at work, work stoppage, [and] loss of productivity,” he said.

RATP has also experienced difficulties with Muslim employees Lagarde noted, referring to known cases of radicalization in the Paris transport company, which is said to employ a large number of Muslims who are watched by French intelligence as known extremists.

The PSA Group, a French car manufacturer who makes Peugeot and Citroën vehicles, shut its factory in Aulnay-sous-Bois in 2013. The plant was known for employing a large number of practicing Muslims as workers.

In addition to having installed a prayer room in the 1980s, the factory’s menus and schedule, with regards to Ramadan, prayer breaks, and religious holidays, were all adapted for the convenience of Muslim staff members.

Drancy, where Lagarde is mayor, neighbours Aulnay-sous-Bois and is a commune in Paris’s northeastern suburbs in Seine-Saint-Denis, the most violent area in France. The area, where 36 per cent of residents were born abroad, has long been known as a trouble spot in Paris, with police regularly attacked and buses torched.

But a recent report, which revealed the suburb to be a “no-go zone” for women in which they are invisible in the streets and unwelcome in bars and cafes, caused a stir across the media, with politicians voicing their disgust.

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW