Tuesday, January 10, 2017

KATIKA QURAN WAKRISTO HAWAITWI MAKAFIRI

Image may contain: text
Je, Makafiri ni akina nani?
Je, unawafahamu makafiri wa kwanza ni akina nani?
Neno kafiri ni neno ambalo lipondani ya Biblia takatifu, kabla hata ya Muhammad mtume wa waislamu kuzaliwa na wala uislamu haujakuwepo nawala Muhammad wala Quran haijaandikwa nawale Waarabu wa 4. Neno hilo kafiri lipo kwenye biblia kwa maana nyepesi neno hilo waislamu wamekuta likitumiwa na waliokuwa wanatumia biblia takatifu.
Katika Quran sijaona Wakristo wakiitwa MAKAFIRI, bali Quran nzima inawaita WAKRISTO wamchao mungu tena wasomi, SURATUL AL-MAIDAH 5:82.
Kwa kuthibitisha kuwa neno KAFIRI limo ndani ya BIBLIA hebu tuziangalie aya chache ndani ya Biblia.
EZEKIEL 34: 28-31
Mistari hiyo ni mungu mwenyewe anawahakikishia wana wa Israel kuwa hawatakuwa mateka wa MAKAFIRI, hivyo neno hilo hapo limetumika kabla hata uislamu haujakuwepo.
NEHEMIA 5: 8-9
NEHEMIA 5:17
NEHEMIA 6:16
MAOMBOLEZO 1:3
MAOMBOLEZO 1:10
MAOMBOLEZO 5:2
1TIMOTHEO 1:8-11
YUDA 1:4
1YOHANA 4:1-6
Maneno hayo yalisemwa kabla ya Muhammad hajazaliwa wa Quran haijaandikwa nawale waarabu wa4 yaani Saydina Abubakar, Omar, Athumani na Ali na uislamu ulikuwa haupo.
TUANGALIE NENO KAFIRI LINAVYOTUMIKA
_________________________
Neno KAFIRI ni neno la Kiarabu lenye maana ya Mpingaji kwa kiswahili.
Yaani anaepinga maneno ya Mwenyezi Mungu neno hili lilikuwepo kwenye Biblia kama tulivyoona kwenye baadhi ya mistari ya biblia hapo juu.
Ilikuwepo neno mpingaji KAFIRI nilazma kuwepo na kauli tangulizi iliyotangulia kusema kwahiyo kauli itakayofuata ya kupinga inaitwa kauli ya mpingaji kwa kiarabu KAFIRI.
Waislamu mara zote hukosi kuwasikia wakisema hawa MAKAFIRI wanatupa tabu au tuwakomeshe au wapigwe hawa MAKAFIRI kauli zao hizo zikitulenga sisi WAKRISTO.
SWALI LA UFAHAMU
Ni kati ya WAKRISTO au WAISLAMU nani MAKAFIRI?
2) Ni kati ya Imani ya KIKRISTO na dini ya KIISLAMU ni nani ilitangulia kuwepo duniani?
3) Ni kati ya YESU na Muhammad ni nani aliyepinga kauli ya mwenzake iliyotangulia?
HISTORIA FUPI KATI YA YESU NA MUHAMMAD.
Bwana Yesu ndiye mwanzilishi wa Imani ya Kikristo.
Waebrania 12:2
Huu ni mwaka 2015 tangu bwana Yesu alipopaa kurudi mbinguni na ni mwaka wa 1436 kwa mwaka wa kiislamu niandiko somo hili la KAFIRI kwani Muhammad alizaliwa mwaka wa 570 nandiye mwanzilishi wa dini ya kiislamu baada ya Yesu.
Hii inathibitisha kuwa Yesu alitangulia kuwepo duniani kabla ya Muhammad hakuna anaepinga hilo.
Kwamaana hiyo kauli za Yesu zitakuwa tangulizi na kauli za IMANI ya Kikristo zitakuwa kauli tangulizi.
Na kauli za Muhammad na Waislamu zitakuwa kauli za kupinga tangulizi.
Yohana 9:35-38
Kauli ya kusema yeye ni mwana wa mungu alijisema yeye mwenyewe Yesu aliitumia mwenyewe katika mistari ya sura ya hapo juu.
Hiyo ni kauli tangulizi ikipatikana kauli inasema Yesu sio mwana wa mungu hiyo ni kauli inayopinga maanayake ni KAFIRI?
JE NI NANI ALIEANZA KUSEMA YESU NI MWANA WA MUNGU?

KWANINI TUNAKULA NGURUWE? (SEHEMU YA KWANZA)

Image may contain: 4 people, people standing, shorts and outdoor
Kwa taarifa yako Allah ameruhusu kula Nguruwe.
* Mafundisho ya Quran Kuhusu Nyama ya nguruwe;
Pamoja na kuwa waislamu wanatushutumu sana wakristo kuwa tunakula Nguruwe Quran inajikanganya sana katika swala zima la kuliwa ama kutokuliwa kwa mnyama huyu ni muhimu kuangalia, kwa ufupi hakuna aya maalumu katika Quran inayoharimisha na kukataza kula nguruwe
Quran inasemaje kuhusu nyama ya nguruwe;-
Quran inaeleza wazi kuwa Mungu aliharimisha Vitu vizuri (akiwemo Nguruwe) kwa Wayahudi kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, yaani Mwenyezi Mungu aliwakataza kula nyama hii kama sehemu ya kuwahukumu wayahudi na si vinginevyo soma (Surat an-nisaa 4;160).
Quran inasema hivi katika aya hiyo “Basi kwa dhulma yao hao Mayahudi tuliwaharimisha vitu vizuri walivyohalalishiwa na vilevile kwa sababu ya kuzuiliwa kwao watu wengi na njia ya mwenyezi Mungu”
ni aya iliyo wazi kuwa wayahudi walizuiliwa vitu vizuri kwaajili ya dhuluma Mungu alitaka kuwahukumu kwa kuwanyima baadhi ya vitu vizuri Quran inakiri wazi kuwa Nguruwe ni kitu kizuri Umeona?
Quran inafundisha kuwa Yesu alikuja kuhalalisha yale yaliyo harimishwa (Surat al-Imran 3;50).
Quran inasema haya katika aya hii “ Na nitakuwa Msadikishaji way ale yaliyokuwa kabla yangu katika Taurati na nimekuja ili NIKUHALALISHIENI yale MLIYOHARIMISHWA na nimekujieni na hoja Kutoka kwa Mola wenu kwa hiyo mcheni mwenyezi Mungu na NITIINI”
Hayo ni meneno ya Yesu Ndani ya Quran ikionyesha wazi kuwa Yesu alikuja kuhalalisha yale yaliyoharimishwa katika Tourati na anatuamuru kumtii, ni wazi kuwa Yesu ameruhusu kula Nguruwe na Quran pia
Quran imehalalisha kula vilivyo vizuri walavyo waliopewa kitabu (Al-maida 5;3-5).
Sura hii almaida maana yake maswala ya meza inasema hivi “……..Leo mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri. Na chakula cha wale waliopewa Kitabu ni Halali kwenu na chakula chenu ni halali kwao…”
Hii ni aya iliyo wazi inayoruhusu kila muislamu kula vyakula vya wakristo na wayahudi na sisi kula vyao umeona!
Quran ina kigugumizi kwa vile hakuna katazo la moja kwa moja kuhusu kutokula Nguruwe yaani inakataza kula Nguruwe na wakati huohuo inaruhusu endapo utashurutishwa na njaa (Al-baqara 2;173) au kama una dharula waweza kula hapa ndipo quran inapojikanganya ni muhimu kujiuliza imekataza au imeruhusu? Na dharula hii ni ipi? Quran inajibu kuwa dharula hii ni njaa (Al-an nam 6;145)Quran inasema kula bila kupita kiasi hili ni jema kwani Biblia inafundisha kuwa hata kama una njaa kiasi gani kula kupita kiasi hata kama si nguruwe chakula chochote ni ulafi ni dhambi (Galatia5;21)
Quran inafundisha kuwa Mungu hakuharimisha chochote ila wazee wa kiyahudi waliharimisha kwa mapokeo yao tu (Al-an nam 146)
Quran inatahadharisha kuwa makini kumzulia Mungu uongo kuwa ameharimisha kitu kumbe hakuharimisha chochote (An Nahl 16;116)
Quran inaamuru uletwe Ushahidi kuwa ni wapi Mungu ameharimisha wanyama? Soma (Al an- am 6;150).
Hivyo ukisoma kwa makini Quran utaona hakuna kilicho haramu ndugu zangu waislamu kula nguruwe ni ruksa ila kiasi tu usizidishe ndivyo Quran inavyofundisha kama husadiki pale uwanja wa sabsaba Tanga kwa Minchi waislamu wenzenu hujumuika kula kiti moto kila iitwapo leo kwani wameelimika na wamegundua siri hii. Mimi sikushawishi ila nina kuweka huru kama mwalimu wa kweli ya Mungu “….. Mtaifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru
Mafundisho ya Agano jipya kuhusu vyakula (Nguruwe).
Biblia inasema mafundisho yoyote yanayokataza mtu kula vitu Fulani ni mafundisho ya Mashetani (1Timoth 4;1-5). Ndio maana waganga wa kienyeji mtu anapokwenda kuaguliwa hukatazwa kula baadhi ya vitu Mungu sio Mganga wa kienyeji. Na wanaomwamini hawana sheria ya kuwazuia nini cha kula au kutokula
Biblia inasema hakuna kitu najisi kwa mtu asiye najisi lakini kitu Fulani ni najisi kwake yeye aliye najisi (Rumi14;14)Biblia inafundisha kuwa kula au kutokula hakuongezi utakatifu wala hakuzuii tamaa za mwili (Kolosai 2;16-23) hivyo hatupaswi kujitia katika mambo ya kutunga tu ya mtu,au akilizake na maono ya wanao abudu malaika kumuabudu Mungu hakuji kwa kula au kutokula aina fulani ya vyakula bali katika moyo safi (Math 5;8)
Biblia inafundisha kuwa unajisi wa mtu hautoki nje bali ndani ya mtu pia Yesu alitakasa vyakula vyoote (Marko 7;14-16,17-19)
Paulo mtume alifundisha kuwa chakula ni kwa tumbo tu na si mambo ya rohoni
(1Koritho 6;13). Hoja ya Pepo waliotolewa na Yesu kuwaingia nguruwe je ina maana gani?
USIKOSE SEHEMU YA PILI........
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.

"MUISLAMU ZINDUKA KUTOKA USINGIZINI ILI UJUE KUWA MKRISTO SIYO KAFIRI"


Najua unaweza kustaajabu ni vipi muislamu wewe uzinduke ili hali unajiona kuwa u macho haupo kwenye Usingizi? ninaposema kuwa unajiona u macho ni katika imani uliyo nayo juu ya Mkristo kuwa ni kafiri, hivi ndivyo unavyoamini kwa sababu uliminishwa hivyo, ukaamini hivyo, kwa sababu tu Quran inasema! 👇
وَقَالَتِ الْيَهُودُ عُزَيْرٌ ابْنُ اللَّهِ وَقَالَتِ النَّصَارَى الْمَسِيحُ ابْنُ اللَّهِ ۖ ذَٰلِكَ قَوْلُهُم بِأَفْوَاهِهِمْ ۖ يُضَاهِئُونَ قَوْلَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن قَبْلُ ۚ قَاتَلَهُمُ اللَّهُ ۚ أَنَّىٰ يُؤْفَكُونَ
التوبة (30) At-Tawba
Na Mayahudi wanasema: Uzeir ni mwana wa Mungu. Na Wakristo wanasema: Masihi ni mwana wa Mungu. Hiyo ndiyo kauli yao kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya walio kufuru kabla yao. Mwenyezi Mungu awaangamize! Wanageuzwa namna gani hawa!
Muislamu ukisoma aya hii moja kwa moja unaamini kuwa Wakristo ni Makafiri kwa kusema kuwa Masihi Yesu ni Mwana wa Mungu! unaamini kabisa kuwa hayo maneno ya kusema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, tunayosema sisi kwa vinywa vyetu yaani sisi ndo tumebuni, hivyo unatuona sisi ni Makafiri! tena unafurahia ujio wa Quran kuwa umekuja kwa ajili ya 👇
وَيُنذِرَ الَّذِينَ قَالُوا اتَّخَذَ اللَّهُ وَلَدًا
الكهف (4) Al-Kahf
Na kiwaonye wanao nena: Mwenyewe Mungu ana mwana.
مَّا لَهُم بِهِ مِنْ عِلْمٍ وَلَا لِآبَائِهِمْ ۚ كَبُرَتْ كَلِمَةً تَخْرُجُ مِنْ أَفْوَاهِهِمْ ۚ إِن يَقُولُونَ إِلَّا كَذِبًا
الكهف (5) Al-Kahf
Wao hawana ujuzi wa jambo hili, wala baba zao. Ni neno kuu hilo litokalo vinywani mwao. Hawasemi ila uwongo tu.
Nawe unaamini fika kuwa Quran imekuja kwa ajili ya kuwaonya Wakristo kwa sababu wanasema kwa vinywa vyao kuwa Mwenyezi Mungu ana mwana, nawe bila kuzinduka uangalie kama kuna usahihi wa jambo hilo unakurupuka na kuanza kusema kuwa, Wakristo ni Makafiri, LEO naomba nikuzindue ili kama unapenda kwenda kwenye UFALME WA MUNGU, basi uungane nami leo.
JE! NI KWELI KWAMBA WAKRISTO WANASEMA KWA VINYWA VYAO KUWA YESU NI MWANA WA MUNGU?
Hili 👆ni Swali la msingi sana mtu kujiuliza, kabla ya kuamini kuwa Wakristo wanasema kwa vinywa vyao na kuwaona ni makafiri (wenye kwenda kinyume na Mungu) kabla Wakristo hawajapatikana, na Yesu ambaye ndiye chimbuko la Wakristo hajazaliwa, Malaika alisema. 👇
Luka 1:30 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

UPO WAPI UTHIBITISHO WA AYA KUWA MUHAMMAD ALITAIRIWA?

Image may contain: food
KUMBE MTUME MUHAMMAD HAKUTAIRIWA.
Ndugu msomaji,
KATIKA sehemu nyingi za ulimwengu, watoto wa kiume wanatahiriwa kwa sababu za kiafya. Watu fulani katika nyakati za zamani, kama vile Wamisri, walitahiriwa, yaani, walikatwa magovi ya kiungo chao cha kiume.
Yesu mwenye asili mbili ya Binadamu na Mungu, yeye alitairiwa kama BINADAMU. Kwa mujibu wa Agano la Kale, mapokeo haya yalianzia na Ibrahimu, Katika Mwanzo 17:10-13, imeandikwa, “Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa. Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na nyinyi. Mtoto wa siku nane atatahiriwa kwenu, kila mwanamume katika vizazi vyenu, mzaliwa nyumbani, na mnunuliwa kwa fedha, kila mgeni asiyekuwa wa uzao wako. Mzaliwa nyumbani mwako, na mnunuliwa na fedha yako, lazima atahiriwe; na agano langu litakuwa katika mwili wenu, kuwa agano la milele.
Katika Injili kwa mujibu wa Luka 2:21: “Hata zilipotimia siku nane za kumtahiri, aliitwa jina lake Yesu; kama alivyoitwa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.” Kwa hiyo, kutahiriwa ilikuwa ni sehemu ya njia ya Yesu.
LAKINI NILIPO ISOMA QURAN NA KUSOMA VITABU VINGINE VYA KIISLAM KAMA SAHIH AL BUKHARI, NIKAGUNDUA KUWA, NABII WA ALLAH AITWAYE MUHAMMAD YEYE HAKUTAIRIWA NA HAKUNA UTHIBITISHO WA KIMAANDIKO AU HISTORIA KUWA MUHAMMAD ALITAIRIWA.
Waislam bila ya jazba wala kutokwa mapovu. Naomba mnijibu swali langu:
Kwanini mnafuata Muhammad nabii wa Allah ambaye hakutairiwa?
Kumbuka kutuna hakufai na ni ishara kuwa wewe umejambiwa mdomoni na Shetani:
Abu Huraira (r.a) amesimulia kuwa: Mtume (s.a.w) amesema, "Ye yote mwenye kutukana, basi huyo amejambiwa na Shetani katika Mdomo wake." (Fat'hul Baary J. 10, Uk. 176)
NATANGULIZA POLE KWA WAISLAM KWA KUMFUATA MUHAMMAD AMBAYE HAKUTAIRIWA.
Shalom.

JE, BWANA YESU ANAPATAJE KUWA MUNGU?

Image may contain: text
Ni vyema sasa tukapiga hatua nyingine ya ufahamu kwa kuangalia swali hili makini ambalo kwa kiasi kikubwa pia huchanganya hisia za watu wengi katika ulimwengu wa imani, ambapo kile kinachoonekana kuwachanganya watu wengi hapa ni uelewa juu ya ukweli kuhusu chimbuko la Uungu wa Bwana Yesu na hivyo watu wengi kuhoji kuwa Yesu anapataje sasa kuwa Mungu?
Ni wazi kuwa swali hili hasa hulenga kutafuta kujua asili au chimbuko la mamlaka ya Kiuungu ya Yesu anayotajwa kuwa nayo hasa kutokana na kile kinachoonekana kuwa Bwana Yesu alikuwa na mwonekano unaoonyesha kuwa huenda naye alikuwa na asili au chimbuko la dunia hii.
Hivyo ili kupata majibu ya msingi ya hili ni vyema kwanza tuanze na hoja juu ya asili ya Yesu na ndipo tunaweza kufunguka zaidi kiufahamu na kuelewa mengi zaidi juu ukweli kuhusu Uungu wa Yesu.
Ufahamu juu ya asili ya Yesu:
Kile kilichoongeza upinzani mkubwa wa Mafarisayo na baadhi ya Wayahudi juu ya Uungu wa Yesu ni uelewa usiyo sahihi juu ya asili ya Yesu.
Ufahamu wa wengi kati ya Wayahudi uligotea katika dhana ya mwonekano wa ubinadamu wa Yesu na historia yake ya uzazi wa kidunia toka katika tumbo la Mariam, ambapo kama matokeo ya hili Wayahudi walisikika wakati fulani wakitamka:-
Yahana 6:42
Wakasema, Je! Huyu siye Yesu, mwana wa Yusufu, ambaye twamjua babaye na mamaye? Sasa asemaje huyu, Nimeshuka kutoka mbinguni?
Unaweza sasa kupata pichani juu ya mzizi wa hoja hii, na ni kama tunavyoona katika nukuu hiyo ya kitabu cha Yohana kuwa hoja kuu ya Wayahudi ilikuwa ni kile walichoona kuwa haikuwa sahihi kwa Yesu kusema ameshuka toka mbinguni maana kile wao wanachojua ni kuwa alizaliwa na bi’Mariam na baba yake ni Yusufu kwahivyo asili yake ni duniani tu.
Hivyo kwa hali hiyo iliwapa ugumu kukubali pale Yesu alipojitaja kuwa na asili ya mbinguni na kimsingi ndicho kilichokuwa chanzo kikubwa cha upinzani wao dhidi ya matamko ya Yesu.
Habu ona tena hoja ya Wayahudi pale Yesu alipoeleza uwepo wake wa milele’
Yohana 8: 56-58
Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi. 57 Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? 58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.

KAMA YESU NI MUNGU, KWANINI AZALIWE NA KUVAA MWILI WA KIBIDANAMU?

Image may contain: text
Ndugu msomaji,
Baada ya hoja na maswali mengi tuliyokwisha yapitia juu ya uhalali wa Uungu wa Yesu ndipo swali hili hufuatia ambapo hoja ya msingi hapa ni juu ya kile kinachoonekana kama kitu kisichowezekana kwa Yesu kuwa na asili ya Uungu na huku akiwa na umbile la kibinadamu umbile ambalo alilipata kwa njia ya kuzaliwa na Mariam, na kimsingi hapa ndipo mahali maswali mengi zaidi hujitokeza.
Kwanini kama ni Mungu avae ubinadamu?
Tendo la dhambi ya Adamu na Hawa lilimuingiza mwanadamu katika deni kubwa lisiloweza kulipwa na mwanadamu mwenyewe hebu tusome:-
Mwanzo 3:17
Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
Kwa kadri ya Andiko hilo tunasoma kuwa Mungu alipomuweka Adamu na Hawa katika bustani ya edeni aliwapa masharti yahusuyo ulaji ambapo wanadamu hao walikatazwa kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, lakini mbali na kukatazwa huko pia walionyeshwa hasara ambayo wangeipata kama matokeo ya kukaidi agizo hilo la kula matunda hayo ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
Kwa uwazi kabisa Mungu aliwaambia juu ya hatari hiyo ambayo wangejiingiza kwayo kuwa ilikuwa ni kifo’ (siku utakapokula utakufa hakika) kwahivyo kimsingi tendo la wazazi hao kujiingiza katika tendo hilo la dhambi ilikuwa ni sawa na kujiingiza katika deni la dhambi ambalo malipo yake ni mauti (kifo).
Na kwa hali hiyo basi mwanadamu huyu alihitaji msaada wa kunasuliwa toka katika deni hilo la dhambi, hivyo ilipasa upande wa pili unaoweza kukabili deni hilo kujitokeza ili kumsaidia mwanadamu kwakuwa kimsingi hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kukabili deni la kifo maana liko nje ya uwezo wa mwanadamu kama Daudi anavyoeleza:-

MUHAMMAD ALIKUWA AMEROGWA MPAKA AKAPOTEZA FAHAMU

No automatic alt text available.
Muhammad Aliwahi Kulogwa (Kwa Apizo, ‘Under a Spell’)
" ‘Aisha anasimulia: Nabii alifanyiwa uchawi hata akaanza kudhani kuwa anafanya kitu fulani wakati hakuwa anafanya. Siku moja alimwomba (Allah) kwa muda mrefu sana kisha akasema, ‘Naona kuwa Allah amenipa mwongozo wa namna ya kujitibu mwenyewe.’..." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 (Mwanzo wa Uumbaji) sura ya 10 na.490 uk.317.
Tazama pia juzuu ya 4 kitabu cha 53 (Wajibu wa Khumus) sura ya 34 na.400 uk.267, juzuu ya 8 kitabu cha 73 (Mienendo Myema) sura ya 56 na.89 uk.56-57, juzuu ya 8 kitabu cha 75 (Kitabu cha Maombi ‘Book of Invocations’) sura ya 59 na.400 uk.266-267. Juzuu ya 7 na.658-660 uk.441-443.
Pia tazama Muislam Sahihi juzuu ya 2 kitabu cha 4 (Kitabu cha Sala) sura ya 309 na.1888 uk.411
Muhammad alilogwa. Alisimulia ‘Aisha: Nabii aliendelea kwa kipindi fulani akidhania kuwa anafanya tendo la ndoa na mke wake, lakini haikuwa hivyo. Siku moja alisema kwangu, "O ‘Aisha! Mungu ameniagiza kuhusiana na suala nililomuuliza. Watu wawili walikuja, mmoja alikaa karibu na miguu yangu na mwingine karibu na kichwa changu. Yule aliyekuwa karibu na miguu yangu alimuuliza yule wa karibu na kichwa changu (akininyooshea kidole), ‘Mtu huyu ana shida gani? Yule mwingine akamjibu, ‘Ameathirika na uchawi. Yule wa kwanza akauliza, ‘Ni nani aliyemfanyia uchawi?’ Yule mwingine akajibu, ‘Lubaid bin A’sam." Yule wa kwanza akauliza, ‘(Alitumia) nyenzo gani?.’ Yule mwingine alijibu ‘Ngozi ya chavua ya mtende wa kiume na chanio lililowekwa nywele, na kuwekwa chini ya jiwe kwenye bwawa la Dharwan.’" Kisha Nabii alikwenda kwenye bwawa lile na kusema, "Hili ndilo bwawa lilelile nililoonyeshwa kwenye ndoto. Ncha za mitende yake inaonekana kama vichwa vya mashetani, na maji yake yanaonekana kama mchanganyiko wa hina."… ‘Aisha aliongeza, "(Mchawi) Lubaid bin A’sam alikuwa anatokea Bani Zuraiq, mshirika wa Wayahudi." Bukhari juzuu ya 8 kitabu cha 73 (Mienendo Myema) sura ya 56 na.89 uk.57. Tazama pia Bukhari juzuu ya 8 kitabu cha 75 (Kitabu cha Maombi ‘Book of Invocations’) sura ya 59 na.400 uk.266
1. Kwanini tumfuate Mtume aliyerogwa na kupoteza fahamu?
2. Hivi kuna Mtume au Nabii yeyote yule kwenye Biblia na yeye alirogwa?
3. Kwanini Allah alishindwa kumlinda Mtume wake kutoka nguvu za kurogwa?
4. Hivi wapi tunasoma kuwa Muhammad alifanyiwa maombi na urogi ukamtoka?
Hakuna ushahid wowote ule ambao unasema kuwa Muhammad aliombewa na kutokwa huo uchawi. Huu ni msiba kwa Nabii wa Allah kufa huku akiwa amefanyiwa urogi.
Ndugu msomaji,
Mtu yeyote yule akifa kwa kurogwa na huku akiwa amejaa Mashetani, basi huyo mtu yeye ataishia kwenye Jehannam ya moto.
Karibuni kwa Yesu aliye hai.
Max Shimba Ministries Org.

MUHAMMAD ALIKUWA NA UGONJWA WA KUSAHAU SAHAU

Image may contain: text
Katika Sahihi Al-Bukhar Vol vi hadithi nambari 556-558 zinamuelezea Muhammad naye Nabii wa Allah alivyokuwa ni mmoja kati ya watu waliosahau aya na sura za Qur’an. Tazama Qur’an 87:6-7. tena Sahihi al-Bukhari Vol vi hadithi nambari 530-557. sijawahi kusoma wala kusikia habari za Nabii yeyote wa Mungu wa kweli aliesahau ujumbe wake.
Maana sisi Wakristo tunasoma katika 2Petro 1:20-21 maneno haya.
“Mkijua neno hili kwanza ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu bali mwanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu”.
Kwa hiyo kwa maana ya maneno haya tunakuwa na shaka na imani ya Kiislamu kuwa Nabii anasahau aya na sura za ujumbe wa Mungu.
Sababu nyingine ambayo ni ya kushangaza ni kuondoshwa kwa baadhi ya aya kwa makusudi tu. Imeelezwa katika Sahihi al-Bukhari Vol vi hadithi nambaro 8 na 527 jinsi Sayyidina Umar alivyoziondoa sura za “ HAFD” na “KHAL’A”. Inasemekana sura hizo zilihifadhiwa na Ibn Ka’b. katika maelezo ya mwanazuoni mmoja Ibn majah yanasema katika heke heka ya mazishi ya Muhammad aya zingine ambazo zilihifadhiwa uchagani mwa kitanda cha bibi Aisha zilikuwa na mnyama wa kufugwa. Hii inashangaza sana, inanishangaza mimi hasa kutokana na yale wayasemayo kinyume na Ukristo. Maana ni wepesi wa kusema kudharau, kubeza na hata kutamka maneno yasiyofaa kwa Wakristo. Ukisema wewe utasikia tu huyo anamkashifu Mtume! Mara nyingi sana hujiuliza mbona Waislamu wengi katika mihadhara humkashifu Yesu tena hadharani? Isitoshe Mtume Paulo kwao amekuwa kama taka taka jinsi wanavyomtukana na kumdharau. Sijasikia watu wanapopiga kelele wakionya na kuwaambia waache kumkashifu Mtume.
Waislamu wengi na wanadamu mamia kwa maelfu kila siku wanamtukana Mungu kwa matendo yao, lakini sijawahi kusikia Waislamu wakiandamana na kuwaonya watu waache mara moja laa sivyo watasusia kila kitu kwa wale ambao wamehusika. Je, huyu Muhammad amekuwa bora kuliko Mungu? Nimechunguza kwa miaka mingi kwamba ukiongea lolote juu ya Allah hutasikia Waislamu duniani wakidai lolote, lakini ukiongea juu ya Muhammad tegemea nlipuko wa Waislamu wakikuzomea karibia dunia nzima. Wakianza mtu mashuhuri au kikundi cha watu mashuhuri hawa wengine watafanya bila kuuliza wala kufikiri. Jambo la kutisha lile ambalo mtu anafedha ambazo fedha hizo si zake bali ni za YEHOVA. Yeye atazitumia kwa kuweka dau eti yule atakaye muua mtu fulani kwa kumsema Muhammad nitampa kiasi fulani cha fedha. Na Waislamu wengine wakishangilia na pengine wakimuombea dua kwa Allah.
Kwa maana hiyo hiyo ukiwaambia ukweli kama haya niyasemayo utasikia wewe hujui, Qur’an siyo mchezo bwana!! Lakini ukiwauliza kwa nini aya za Qur’an zilikuwa katika mchago wa kitanda cha Aisha mke wa Muhammad? Hapo utakosa jibu la msingi. Na kwa wale ambao hawakusoma wataona haya niyasemayo hayakuandikwa katika vitabu vya Kiislamu.
Katika Qur’an Sura 5:48 Surat maida kuna maneno haya ya Allah.
Sisi ndiyo tulioshusha mawaidha haya na sisi ndio tutakao yalinda.
Je, maneno haya ambayo Allah ameyasema yana ukweli gani?
Maana tunajifunza katika mikasa mbali mbali za kupotea kabisa sura na aya za Qur’an kwamba mpaka sasa hazipo kabisa. Je, sisi tunajifunza nini? Je, kama kweli Qur’an ni maneno ya Mungu aliyehai zingewezaje sura na aya zake zipotezwe kabisa kwa mikono ya wanadamu na isiwepo kumbukumbu? Nitakupa mfano mmoja ili upate kuthibitisha kuwa maneno ya Mungu aliye hai hayawezi kupotea kwa mikono ya wanadamu na Mungu asiyalinde. Katika Yeremia 36:1-4 na 21-32 Hapo tunasoma kisa cha mfalme mmoja ambaye alichukizwa na maneno ya Mungu yenye kumuonya akaamuru liletwe na kulikata kwa kijembe hadi lote likamalizika. Lakini mfalme aligundua kuwa kama ataviacha vile vipande watu wangeviokota na kuviunganisha na neno hilo la Mungu aliye hai likaendelea. Mfalme akaamuru vile vipande vichomwe moto vyote.
Mfalme alijua kuwa kwa kufanya hivyo atayafuta kabisa maneno ya YEHOVA. Lakini tunaposoma katika mstari wa Sura hiyo hiyo tunasikia maneno haya:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia hapo mfalme hapo mfalne alipokuwa amekwisha kulliteketeza Gombo lile na maneno yote ya kwanza aliyoyaandika Baruku yaliyotoka katika kinywa cha Yeremia akasema: Haya twaa wewe Gombo lingine ukaandike ndani yake maneno yote ya kwanza yaliyokuwa katika Gombo la kwanza ambalo Yehoyakimu mfalme wa Yuda ameliteketeza.
Mungu hakuridhika kuona maneno yake yanapotezwa na mwanadamu. Akaamuru kuyarudisha maneno yale yale ambayo mfalme alichukizwa nayo.
Swali ambalo Waislamu wote wangejiuliza iweje maneno ya Allah yapotee tu hata yasiwe na kumbukumbu? Tunamuaminije yule yule aliyeshusha maneno ya Qur’an kuwa anauwezo wa Kimungu?
Katika hili mimi nimeona mambo mawilli muhimu.
1. Kutoaminika kwa madai ya sura 5:48, kupotea kwa sura na aya kadhaa ambazo Allah anadai alizishusha kuwaonesha sio kuaminika tu bali kukosa uwezo na mamlaka ya Kiungu (Divinity Authority) ya kutunza aya alizo ahidi kuzilinda.
2. Kuhusu madai ya Allah ya NASKH na MANSUWKH yaani aya moja inaweza kufutwa na nyingine hii ni ulaghai wa kibinadamu ili kutoa nafasi ya kubadilisha mambo kwa madai ya kwamba Mungu amesema.
Kwa mfano aya nyingi katika Qur’an inasemekana ni maneno ya watu mbalimbali. Nitakukumbusha tena jambo hili. Katika Sahihi al-Bukhar Vol vi musnad Harba Vol I Saifa ya 23-24 inamtaja sana Ibn Hanbal akimkaririAnnas akisema:
Umar bin Khatab baba mkwe wa Muhammad alisema nimekubaliwa mambo matatu. Nikasema ewe Mtumme wa Allah lau kama tungeweka kisimamo cha Ibrahimu ndipo ilipoteremka aya ya kuweka kisimamo cha Ibrahimu. Tazama Sura 2:125 Surat Bakara.
Neno la Kiarabu la WAAFAQTU (Yaani nimekubaliwa) katika hadithi hiyo lilionesha kuwa Umar bin Khatab alitoa pendekezo kuwa Qibla ya Waislamu kiwe Al-Kaaba na sio kwamba badiliko lile lilitoka kwa Allah Mungu wa Waislamu. Je, mashekhe hili mmnasemaje? Je, kisa cha aya hii ya 125 ya Surat Bakara ni Sahihi aliyosema Bukhari katika hadithi aliyoipokea? Kama sawa basi wapasheni Waislamu waiojua ukweli huu. Na kama siyo sawa toweni ukweli kinyume na yale ambayo Bukhari ameyapokea.
Ikumbukwe katika Sahihi Muslimu Vol:I hadithi 525 na 527 inaeleza kuwa miezi 17 tangu Muhammad ahamie Makka Waislamu walisali huku wameelekea Yerusalemu sawa na Wayahudi. Lakini ilipofika aya ya 125 ya Surat Bakara Qibla kilibadilika na kuwa Al-Kaaba.
Je inatupasa kusemama nini? Ya kusema ni haya: Ashukuriwe Umar bin Khatab kwa pendekezo lake lililomfanya Allah ahamishe Qibla kukipeleka AL-kaaba.
Si hilo tu Umar bin Khatib alilopendekeza bali anasema nikasema ewe Mtume wa Allah hakika wake zako wanaingia nyumbani hali vichwa vyao havijafunikwa? Ndipo alipoamrisha wavae Hijab. Hapo napo ndipo ilipoteremka aya ya kuvaa Hijab sura 33:59. Hili ni pendekezo la Umar na Allah akalikubali.
Haya ni baadhi tu ya mambo yanayoonesha kuwa madai ambayo wanadai Waislamu dhidi ya Wakristo hayana ukweli wowote.
Uislamu kamwe hata siku moja hauwezi kabisa kuufananisha au kuwa na nafasi ya kusema lolote juu yake. Uislamu na Ukristo ni sawa na watu wawili waliovaa nguo mmoja nguo nyeupe isiyo na doa na mwingine amevaa nguo nyeusi iliyo na uchafu wa grisi ya magari. Yohana aliwaona hao waliovaa nguo katika maoni anaandika katika Uf 7:13-18. katika mlango huo anajibiwa na wale wazee maalumu lile swali alilouliza. Akaambiwa hao waliovaa nguo nyeupe ni wale ambao wamepokea wokovu na nguo zao wamezifua kwa damu ya mwana kondoo. Nini maana yake? Ni kwamba hao ni Wakristo waliokubali kulitii neno la Mungu na kuamini kuwa Yesu ni mwana wa Mungu.
Bahati mbaya Wakristo tunapoongelea kuwa Yesu ni mwana wa Mungu Waislamu wasiosoma wale wanaofikiri mambo yaliyo nje ya mwilli wanauliza Mungu alioa lini?
Mke wake ni nani? Inashangaza kweli. Mungu kutamka yeye mwenyewe kuwaambia watu wale wa kwanza kwamba Yesu ni mwana wake aliyependezwa naye hana maana ya kuzaa. Nia ni kuwafundisha watu katika mazingira yao. Mtu anapokujulisha kwamba huyu ni mwanangu maana yake ujumbe wowote atakao muagiza huyo mtoto wake kwako lazima utauamini kwasababu umetoka kwa baba yake. Mungu alitufundisha katika mazingira yetu. Waislamu kwasababu wao huwaza sana mambo ya kimwili ya kidunia utasikia Yesu sio mwana wa Mungu. Mungu hakuzaa wala hakuzaliwa. Je, ni nani anayepinga hayo mambo ya kidunia. Wakristo wanaamini kuwa Mungu hakuzaa kidunia wala hakuzaliwa kidunia. Lakini kiroho akatamka kuwa Yesu ni mwana wake aliyependezwa naye tumsikie yeye.
Njoo kwa Yesu upate kupona.

MKRISTO MWENYE KUJITAMBUA HAWEZI KUMFUATA ALLAH ANAYE UGUA MACHO KAMA VIUMBE

Image may contain: one or more people


ALLAH ANA MACHO Na tunaamini kuwa Allah Anayo macho mawili kikweli, na hii inatokana na kauli Yake Subhaanahu wa Ta’ala Aliposema kumwambia Nuuh (‘Alayhis-Salaam):
وَاصْنَعِ الْفُلْكَ بِأَعْيُنِنَا وَوَحْيِنَا
"Na unda jahazi mbele ya macho yetu na kwa mujibu wa ufunuo wetu."
"Wakati mmoja macho ya Allah yalikuwa yanauma, na Malaika walikwenda kumuona, na kwamba Allah alitokwa na Machozi, kwa ajili ya Mafuriko ya Nabii Nuhu mpaka macho yake yakawa mekundu. (Al Milal Wannihal J. 1 uk. 141)
Hapa inaonekana Allah alijisahau na akajitupia ugonjwa wa Macho, RED EYES. Sasa Mungu gani huyu anaye Umwa kama Viumbe? Hakika Allah si Mungu bali ni kiumbe,

KWANINI TUNAKULA NGURUWE? (SEHEMU YA PILI)


Image may contain: 2 people, outdoor

Kiti moto mdudu mwenye mjadala mkali duniani.
Biblia inasema hivi katika Wakolosai 2 : 16 ‘Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;’ Kwa tafasiri nyepesi biblia inasema usimuache mtu yeyote akuhukumu ‘do not let anyone judge you’ kwa habari ya nunakula nini unakunywa nini, au kama huandami mwezi au kushika sabato mtu asikuhukumu, maana yake ni kuwa mafundisho yoyote duniani ya imani yoyote yanayokataza ule nini usile nini ni mafundisho ya Mashetani, sisi wakristo hatuna miiko, ukienda kwa wapunga pepo wanganga watakupangia ule nini usile nini haya ni mafundisho ya mashetani ona 1Timotheo 4 1-5 Biblia inasema :-
‘1. Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; 2. kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe; 3. wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli. 4. Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani; 5. kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.’
Ndugu zangu unaweza kuona maandiko haya yako wazi kabisa kwamba kumzuia mtu ajiepushe na chakula fulani ni mafundisho ya roho zidanganyazo yaani mapepo na mashetani biblia iko wazi kuwa kila kiumbe kilichoumbwa na Mungu ni kizuri kama ukikipkea kwa shukurani kwa vile vimeatakaswa na neno la Mungu !
Wakati najenga Msingi huu napenda pia nikufahamishe vema somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo :-
Ufahamu kuhusu Nyakati saba za Maongozi ya Mungu.
Mafundisho ya Quran kuhusu Nyama ya Nguruwe.
Mafundisho ya Agano jipya kuhusu kula Nguruwe.
Ufahamu kuhusu nyakati saba za maongozi ya Mungu.
Moja ya sababu zinazopelekeabaadhi ya watu kupinga aina Fulani ya vyakula ikiwemo nyama ya nguruwe ni kuto kuyajua maandiko na kutofahamu juu ya nyakati saba za Maongozi ya Mungu ambapo Mungu aliongoza kwa Sheria tofauti tofauti, ikumbukwe kuwa Mungu ndie mtunga sheria na huweza kupanga au kupangua sheria “Amendments” kulingana na nyakati Yeye mwenyewe, kama apendavyo, Kama bunge linavyoweza kupitisha sheria na hatimaye kuibadili wakati Fulani kama wapendavyo ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu, Mungu ameiongoza Dunia hii kwa nyakati tofauti tofauti zipatazo saba, maeneo sita kati yake yametimizwa na eneo la saba litakuwa ni wakati ujao
Nyakati za Maongozi ya Mungu kibiblia Zimegawanyika katika Maeneo makuu saba yafuatayo
Innocence Period-Hiki ni kipindi cha uumbaji mpaka anguko la Adamu(mwanadamu)
Concience Period-Hiki ni kipindi cha dhamiri mpaka gharika
Human Government Period-Hiki ni kipindi cha kujitawala mpaka wakati wa Ibrahimu
Promise au Patriach Period-Hiki ni kipindi cha mababa mpaka wakati wa Musa.
Dispensation of Law- hiki ni kipindi cha sheria ya Musa.
Dispensation of Grace-Hiki ni kipindi cha neema au wakati wa Mataifa.
Escatological times-Kipindi cha mambo yajayo (Dhiki kuu, hukumu ya mataifa, utawala wa miaka 1000,vita ya gogu na magogu, ziwa la moto, Mbingu mpya na nchi mpya.)
Katika vipindi hivi vyoote Mungu aliweka sheria mbalimbali za kuongoza vipindi hivyo,Mtu asipofahamu vizuri anaweza kuchanganya mambo katika vipindi hivyo Mungu aliweka au kubadili sheria zake kulingana na nyakati hizo na makusudi yake aliyoyakusudia kwa wakati huo.
Mfano sheria kuhusu Vyakula;-
Kipindi cha uumbaji mpaka anguko la Adamu (Innocence Period).
Sheria ilikuwa moja tu wasile tunda la ujuzi wa mema na mabaya tu wakati huu mwanadamu hakula nyama (Mwanzo 2;16-17,1;28-30) Mungu aliweka sheria hii moja kwa sababu Adamu na Eva walikuwa Peke yao na Mungu aliwapa vitu vyote hebu jaribu kuwaza kama Mungu angesema Usizini, usiibe hizo sheria pale Bustanini zingemuhusu nani wakati Adam yuko peke yake na mkewe
Kipindi cha dhamiri Anguko mpaka wakati wa gharika Gharika (Concience period.)
Wakati huu Mungu aliamuru wale vitu vyoote isipokuwa Damu tu (Mwanzo 9;1-4).Baada ya gharika Mungu alimruhusu Nabii Nuhu na wanawe kula kila kitu yaani vitu vyote isipokuwa Damu tu yaani lazima damu ya mnyama imwagike unapotaka kumla, soma biblia yako Mwanzo 9: 1-4 waliruhusiwa kula kila kitu yaani vyote akiwemo Yule mdudu Nguruwe!
Wakati wa sheria ya Musa (Mungu aliamuru wale baadhi ya vitu na baadhi vilikatazwa).
hii ilikuwa ni kwa sababu za kiafya na kutafuta utii wa Israel, baadhi ya vitu vilivyokatazwa ni pamoja na Ngamia, Sungura, Nguruwe, Kambale, Taa, Pweza, Ngisi, n.k. Mungu aliwakataza WAYAHUDI peke yao wasile baadhi ya wanyama na samaki wote wasio na Magamba na wanyama wasio na kwato zilizopasuliwa kati, au wenye kwato zilizopasuliwa kati lakini hawacheui soma (Walawi 11;1-47).
Wakati wa Neema,
Wakati huu Mungu aliamuru kuliwa kwa vitu vyoote isipokuwa damu ambayo kibiblia imekatazwa milele. ( Luka 17;10,1Koritho 10;25-27,Kolosai 2;16,1Timotheo 4;1-5). Wakati wa neema ndio wakati huu wa agano jipya wakati huu tunaruhusiwa kula kila kitu bila kujali wala kuulizauliza soma maandiko yale juu.
Tatizo kubwa la waislamu ni kutokujua nyakati hizi za maongozi ya Mungu na Sheria alizoweka, wanachanganya mambo. Aidha katika namna ya kushangaza waislamu wanaona Nguruwe tu kuwa ni haramu, huku wamesahau kuwa Mungu alikataza hata ngamia ambao mara nyingi huchinjwa na waislamu wakati wa iddi alhaji. wavuvi wengi wa pwani ni waislamu mara nyingi huvua taa, pweza na ngisi, Mtu anayeamua kuishika sheria na ashike yoote na asiyedumu katika yoote amelaaniwa (Galatia 3;10). Wanyama wengi miongoni mwa waliokatazwa wanahitilafu za kiafya kama wasipoandaliwa vema mfano Nguruwe ana tegu wengi katika nyama yake pia huharibika kwa Haraka nyama yake inapokaa zaidi ya wakati hivyo kutokana na mazingira ya jangwani walikokuwa wanasafiri Israel isingelikuwa vema kuruhusiwa kutumia aina hizi za nyama. Mungu aliwapa sheria hii Wayahudi peke yao wakiwa chini ya nabii Musa. Baada ya kuyaelewa haya sasa hebu tuangalie Mafundisho ya Quran kuhusu Nguruwe!
=====> USIKOSE SEHEMU YA TATU..........

BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds

  BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds. The targets included a Radwan Force training facility used for weapons drills ...

TRENDING NOW