Tuesday, April 11, 2017

VAENI SILAHA ZOTE ZA MUNGU

Image may contain: text
Je, umesha vaa silaha zote za Mungu?
Waefeso 6:10-12 yasema, “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” Ujumbe huu wafunza baadhi ya kweli muimu: tutaweza kuwa na uwezo kwa nguvu za Mungu, ni silaha ya Mungu ambayo yatulinda, na vita ni kupinga na nguvu za giza za ulimwengu huu.
Mfano wa nguvu sana juu ya ngunvu za Bwana ni ule wa malaika Mikaeli katika Yuda 9. Mikaeli ambaye ni mwenye nguvu zaidi ya malaika wote wa Mungu, hakumkemea Shetani kwa nguvu zake, bali alisema, “Mungu anakukemea!” Ufunuo 12:7-8 yanakiri kwamba katika nyakati za mwisho Mikaeli atamshinda Shetani. Bado, wakati inafikia mapigano yake na Shetani, Mikaeli alimkemea Shetani katika jina la Mungu na mamlaka yake, si kwa nguvu zake. Ni kupitia kwa uhusiano wetu na Yesu Kristo kuwa Wakristo wako na mamlaka yoyote juu ya Shetani na mapepo yake. Ni kupitia kwa jina lake kuwa kemeo letu liko na nguvu.
Waefeso 6:13-18 yatupa elezo la silaha za kiroho Mungu anapeana. Tunastahili kusimama dhabiti na kufunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kufuani, na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani, kuchukua ngao ya wokovu na kwa kuomba katika roho.
Kwa ufupi, njia za ufanisi wa vita vya kiroho ni zipi?
Shalom
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo.

Monday, April 10, 2017

UNAWAFAHAMU MALAIKA WAKUU SABA WA MUNGU "ARCHANGELS OF GOD? (SEHEMU YA SABA)


Kiumbe wa roho anayeitwa Mikaeli hatajwi mara nyingi katika Biblia. Hata hivyo, kila mara anatajwa akitenda jambo fulani. Katika kitabu cha Danieli, Mikaeli anapigana na malaika waovu; katika barua ya Yuda, anabishana na Shetani; na katika Ufunuo, anapigana na Ibilisi na malaika wake waovu. Anapoutetea utawala wa Mungu na kupigana na adui za Mungu, Mikaeli anatenda kupatana na maana ya jina lake—“Ni Nani Aliye Kama Mungu?” Lakini Mikaeli ni nani?

Malaika Mikaeli (kwa Kiebrania מִיכָאֵל, Micha'el au Mîkhā'ēl, maana yake Nani kama Mungu; kwa Kigiriki Μιχαήλ, Mikhaḗl; kwa Kiarabu ميخائيل, Mīkhā'īl) anaheshimiwa kama malaika mkuu katika imani ya dini za Uyahudi na Ukristo.

Mikaeli ni malaika mkuu, neno “malaika mkuu” la kigiriki ni ἀρχάγγελος (archaggelos) linalomaanisha “mtawala wa malaika” au “mkuu wa malaika”; kwa uhalisia “mkuu wa wajumbe”.
Katika Biblia ya Kiebrania anatajwa mara tatu katika Kitabu cha Danieli.

Katika Agano Jipya la Biblia ya Kikristo anatajwa katika Waraka wa Yuda na katika Kitabu cha Ufunuo.

Je Malaika wa Bwana anaweza kuwa ndiye malaika mkuu Mikaeli?

Zekaria 3:1-2 inasema, “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye. Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni?”

Hapa tunamwona malaika wa Bwana akimwambia shetani kwamba”Bwana na akukemee”, Ukisoma fungu la 3 utaona Yoshua alikuwa amevaa “mavazi machafu” hii inawakilisha dhambi. Halafu shetani akaja kwa Yoshua akidai kuwa yuko upande wake, na malaika wa Bwana hivyo hivyo, alikuja kumuondolea Yoshua uovu wake, hivyo akamwambia shetani kwamba Bwana na akukemee. Je ni wapi tena tunaona jambo kama hili hili?

Yuda 1:9 inasema, “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.”

Hapa tunaona kama hilo hilo lilitoke wakati wa Musa, na malaika aliyefanya hivyo ni Mikaeli malaika mkuu; kwa hakika “malaika wa Bwana” ndiye “Mikaeli”.

Danieli 12:1,2 inasema, “Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako;…na wakati huo watu wako wataokolewa; kila mmoja atakayeonekana ameandikwa katika kitabu kile. Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.”

Zingatia Danieli 12:1 inamwita Mikaeli kama “Jemedari Mkuu”, na katika Ufunuo 12:7 “Mikaeli na Malaika zake anapigana na shetani na malaika zake”. Shetani ni mkuu wa malaika zake na malaika zake humwabudu yeye na kutii amri zake; na malaika zake ni jeshi lake, vivyo hivyo Mikaeli ni mkuu wa malaika zake, na malaika zake ni jeshi lake, nao hutii amri zake (Ebrania 1:6-7

Yohana 5:28,29 “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.”

Ufunuo 12:7 Na vita vikatokea ghafula mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka mkubwa, naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana.

Sehemu zote tumeona Mikaeli ni malaika mkuu wa vita. Ukiona mambo hujayapata kama inavyotakiwa maana yake yupo azuiaye mahali amejificha hivyo fanya vita vya kiroho na utafanikiwa kwajina la Yesu.

Yupo saizi ya ibilisi ambaye anaitwa Malaika Mikaeli. Shetani alikuwa malaika lakini alimwasi Mungu na Mikaeli ndiye aliyemshughulikia.

Ukiona mambo kwenye maisha yako yameshindikana usifikiri Mungu hajakusikia maombi yako na amekuacha, kuna kizuizi cha mkuu wa anga mahali ambaye amekuzuia na huyo lazima ashughulikiwe na yale majibu yako yaje kwako kwa jina la Yesu.

Yupo malaika Mikaeli mkuu wa majeshi ya malaika ambaye tunamtumia ili tupigane na huyu mkuu wa anga na wakala zake waliozuia baraka zetu kwa jina la Yesu. Mashetani wote waliojificha kwenye ulimwengu wa rohoni lazima tuwafuate na kuwateketeza kwa jina la Yesu.

Malaika Mikaeli ni kiumbe wa Rohoni na wale waliokuzuia nao ni viumbe wa Rohoni na hakuna jambo gumu la kumshinda Mungu wetu. Mikaeli anajua mbinu za vita na leo tunaungana na majeshi ya malaika Mikaeli ili kupigana na mkuu wa anga la uajemi na mapepo yake.

USIKOSE SEHEMU YA NANE. MALAIKA URIEL NA KAZI ZAKE.......


Shalom,

Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

JE! KUANGALIA PICHA ZA NGONO NI DHAMBI? (SEHEMU YA PILI)

Image may contain: 1 person, sitting and text
Kuangalia picha za ngono "NI DHAMBI" kwa herufi kubwa. Katika Sheria ya Musa ilikuwa mtu anahesabika kuwa ametenda dhambi pale ambapo atakutwa akifanya kitendo hicho au kukiwa na mashahidi wawili au watatu atatakiwa kuhukumiwa sawasawa na Sheria husika.
Kwenye dhambi ya uzinzi mtu alitakiwa apigwe mawe hadi afe sivyo kwa Sheria ya Kristo yenyewe inazungumzia juu ya kitendo cha "kutamani" tu unahesabika kuwa umefanyika DHAMBI (Mathayo 6:27-29, Waebrania 10:28). Tamaa mbaya ni dhambi kama dhambi nyinginezo. Kwa kawaida tamaa huja na ile tamaa huchukua mimba na baadaye huzaa dhambi (Yakobo 1:13-16). Kitendo cha kuangalia picha za ngono hupofusha "FIKRA" nzuri za mtu alizonazo. Mawazo machafu uanza kutawala katika ubongo wako hadi "USHUSHE" huo mzigo ulioko kwenye viungo vyako vya uzazi. Ahaaa ni hatari aiseeee.
Wewe unayengalia picha za ngono Kama ndiyo starehe yako unaiharibi nafsi yako "unakuwa zezeta wa akili" Biblia inasema "taa ya Mwili jicho na jicho lako likiwa safi mwili wako wote utakuwa na nuru. Lakini jicho lako likiwa bovu mwili wako wote utakuwa na giza.."(Mathayo 6:22-23). Kwa wale wanandoa ni "MWIKO" kutumia picha za ngono ili kunogesha kufanya Tendo la Ndoa.
Wewe mume unaye hapo "chombo" unakiona "live" na kimethibitishwa na Mungu mwenyewe sasa hiyo mipicha ya nini? Kila kiungo Mungu alikiweka kwa ajili ya kusudi maalum kama ni mdomo kwa ajili ya kuongea na kupitisha chakula na si kunyonya sehemu za Siri za mwenzi wako. Mungu ameweka sehemu ya "haja kubwa" kwa ajili ya kutolea uchafu uliotengenezwa na tumbo na si kiungo kingine kiende kukoroga "zege" hilo huo ni uchafu(Ufunuo 22:10-15).
Warumi 1:26:27
“Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.”
USIKOSE SEHEMU YA TATU "JINSI YA KUSHINDA DHAMBI YA KUANGALIA PICHA ZA NGONO"
Shalom

KITABU CHA MWANZO (SEHEMU YA TATU)

Image may contain: cloud, text and nature
S: Kwenye Mwanzo 1:10, ilikuwaje Mungu aumbe dunia wakati dunia ilikuwa tayari imeishaumbwa kwenye Mwanzo 1:1?
J: Neno la Kiebrania (eres) ni hilo hilo linalotumika sehemu zote. Kama ilivyo kwenye kiingereza, eres inaweza kumaanisha ulimwengu chini ya anga, na inaweza kumaanisha ardhi au nchi kavu. Kwa hiyo Mungu aliiumba sayari kwenye Mwanzo 1:1, na nchi kavu kwenye Mwanzo 1:12. Tazama Encyclopedia of Bible Difficulties uk.65-66.
S: Kwenye Mwanzo 1 na 2, kwa nini inaonekana kana kwamba kuna matukio mawili ya uumbaji?
J: Mwanzo 1 ni uumbaji wa mbingu na nchi, na Mwanzo 2 ni uumbaji wa wanadamu kwenye bustani ya Edeni.
S: Kwenye Mwanzo 1 na sehemu nyingine, kwa nini Mungu anaitwa Elohim, wakati sehemu nyingine tena kama Mwanzo 2 Mungu anaitwa Yahweh?
J: Mungu ana idadi kubwa ya majina kwenye Biblia. Inaonekana kuwa jina Yahweh linaangalia zaidi uhusiano binafsi wa Mungu na sisi tofauti na Elohim, ambalo linaangalia zaidi haki na ukuu wake.
Lilikuwa jambo la kawaida katika jamii za zamani kuwa na majina zaidi ya moja kwa mungu huyohuyo. Hii hapa ni mifano:
Osiris - Wennefer, Khent-amentius, Neb-abdu
Bel - Enlil, Nunamnir
Sin - Nanna
El - Latpan
Baal - Larpan
Elohim is the general name for God and is used in the context of God as creator. It emphasizes that God is distant and powerful. It is used to describe God as the awesome and majestic creator. In our English Bibles, Elohim is translated as God.
Yahweh (the LORD) is God's personal name and is used in the context of God having a relationship with His people. When God goes about creating humanity, it is Yahweh who does this act. When the Lord is personally involved with His people, Yahweh is the proper way to designate Him. In our English Bibles Yahweh is translated as the LORD with all capital letters.
S: Kwenye Mwanzo 1, je Mungu aliweza kuumba dunia kwa siku sita halisi zenye masaa 24 kila moja?
J: Bila kujali kama wanadhani dunia iliumbwa miaka mingi iliyopita au michache, Wakristo wote wanapaswa kujibu swali hili "ndiyo."
Badala ya siku sita, Mwenye enzi angeweza kuiumba kwa muda wa sekunde sita kama angependa kufanya hivyo. Suala hapa si jinsi gani Mungu alipaswa kuumba bali ni jinsi gani Maandiko na ulimwengu vinaonyesha alichagua kuumba.
Kama nyongeza, Maandiko hayasemi siku ina urefu gani kwa Mungu kwenye Mwanzo 1. Kumbukumbu 7:1 inaonyesha kuwa "siku" inaweza kuwa ni kipindi cha muda kinachozidi masaa 24, kama ilivyoeleweka kuwa "siku" za Musa. Zaburi 90:4; 2 Peter 3:8 zinaonyesha kuwa siku za Mungu zinaweza kuwa ndefu sana.
S: Kwenye Mwanzo 1, je kufanana kwa maelezo haya ya uumbaji na yale ya Wababeli kunathibitisha kuwa yote haya yametoka kwenye chanzo kimoja kilichotungwa na watu?
J: Maelezo ya Wababeli yanafanana kwenye ufafanuzi wa kinaganaga lakini karibu ni kinyume kabisa kuhusiana na chanzo. Tofauti na Marduk aliyekuwa anashindana na vurugu za joka kubwa Tiamat, Mungu anaamuru nini kitokee. Kama kuna kitu cha kweli kwenye jamii zisizokuwa za kibiblia jambo hili halipaswi kutushangaza. Isitoshe mtindo wa Mwanzo 1 unaelekea kuwa ni utofauti uliokusudiwa dhidi ya nadharia za kipagani.
USIKOSE SEHEMU YA NNE: Kwenye Mwanzo 1:26 na 3:22, kwa nini neno "tumfanye" linatumiwa kwa Mungu Mmoja wa Kweli?
Shalom,

JE, MUNGU ALIMUUMBA SHETANI?

Image may contain: text

Mungu aliwaumba viumbe wote wakiwa Wakamilifu, lakini walikuwa na uhuru wa kuchagua Kumtii Mungu au Kutomtii Mungu. Tunajua ya kwamba wengine kati yao walitenda dhambi, na Biblia inawataja kama “Malaika walioanguka” (Mwanzo 6:2,4; Yuda. 1:6)
LUSIFA ALIKUWA NANI?
Lusifa alikuwa amejaa hekima na alikuwa Mkamilifu katika uzuri wote, lakini aliingia katika majivuno na kuwa asiyefaa kitu na kugeuka kuendelea katika njia ya dhambi, (Ezekieli 28:12-15). Alifikiri angeweza kujiinua juu ya Kiti cha Enzi cha Mungu (Isaya 14:12-14). Maasi yake yalishindwa na kutupwa chini, duniani katika nchi (Luka 10:18; pia katika Ufunuo 12:7,9).
MWANZO WA JINA LA SHETANI:
Lusifa alishawishi theluthi ya malaika kumfuata katika maasi yake. Ambao alifukuzwa nao na jina lake likabadilika na kuitwa shetani, yule joka mkubwa (Ibilisi) na malaika waliofuatana naye wanajulikana kama pepo wachafu (demons). Wote wanajulikana kama “Jeshi lililoanguka”
Biblia inamfafanua Shetani kuwa kiumbe halisi ambaye yuko katika makao ya roho. (Ayubu 1:6) Inatueleza kuhusu sifa zake za ukatili kutia ndani matendo yake ya uovu. (Ayubu 1:13-19; 2:7, 8; 2 Timotheo 2:26) Pia inasimulia mazungumzo kati ya Shetani na Mungu na pia kati yake na Yesu.—Ayubu 1:7-12; Mathayo 4:1-11.
MAANA YA JINA LA SHETANI:
Jina hilo ni la kumfafanua, na linamaanisha “Mpinzani; Adui; Mshtaki.” Alikuja kuitwa Shetani kwa sababu alichagua kumpinga Mungu.
Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata itakapokuja ile hukumu (1 Petro 3:18-20; 2 Petro 2:4-5; Yuda 1:6). Mapepo wengine wachafu, huzunguka zunguka katika dunia hii wakitafuta watu ili wawameze (Ayubu 1:6-12; Lk 8:30-32).
JE, UMEJIULIZA HIVI?
 Shetani alitoka wapi?—Ayubu 38:4-7; Yohana 8:44.
 Shetani huathiri ulimwengu kadiri gani?—Yohana 12:31; 1 Yohana 5:19; Ufunuo 12:9.
 Tunaweza kufanya nini ili kujilinda kutokana na mbinu za uovu za Shetani?—1 Petro 5:8-10.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

JE! KUANGALIA PICHA ZA NGONO NI DHAMBI? (SEHEMU YA TATU)

Image may contain: one or more people, people sitting, shoes, indoor and text
JINSI YA KUSHINDA DHAMBI YA KUANGALIA PICHA ZA NGONO
PICHA ZA NGONO zinavutia sana kuziangalia ila zina maangamizo makubwa sana katika maisha yako. Lazima ufikie mahali kukata shauri ndani ya Moyo wako kuambatana na Mungu. Kusudi kubwa la shetani kuachilia mambo yake ya NGONO kwenye mitandao ili apate wafuasi wengi zaidi. Hakuna kitu unachoweza kukifanya katika simu za Android wengine wasikitambue. Kila unalolipitia na kuliangalia kwa Siri siku ya siku litaletwa hukumuni na Mungu mwenyewe (Warumi 2:16, Mhubiri 12:14)
USHAURI WAKIVITENDO:
I) Yatie Nuru macho yako - Zaburi 13:3, 19:8 - Yaruhusu macho yako yaingiziwe nuru na Yesu. Chukua muda wa kutosha kuingiza PICHA zinazomhusu Mungu zaidi. Angalia wahubiri mbalimbali.
II) Tazama mambo ya Adili(mema) - Zaburi 17:2-3 - Kuna nguvu kubwa sana tunapokuwa tunaangalia mambo mema. Vipindi vizuri vya neno la Mungu. PICHA zinazojenga siyo zinazoharibu fikra zetu.
III) Kumuomba Mungu afumbue macho yako - Zaburi 119:18, 146:8- Maombi ni muhimu ili kufanya macho yako kuona kusudi la Mungu na Kutambua uwepo wa shetani katika PICHA ZA NGONO.
IV) Weka maneno ya Mungu Mbele za macho yako - Mithali 4:20-21
Wakati wote soma neno la Mungu kupitia kifaa chochote cha ki-electronic ili uweze kumjua Mungu zaidi.
V) Macho yako yatazame Mbele - Mithali 4:25-27
Kutazama Mbele maana yake uwe na maono. Maono ni PICHA au TASWIRA ya Mbele ya maisha yako. Yeremia aliulizwa unaona nini naye akasema "anaona ufito wa mlozi" anaona kitu kizuri (Yeremia 1:11-12).
VI) Pendezwa na njia za Mungu - Mithali 23:26
Kuanzia sasa anza kupendezwa na njia za Mungu katika maisha yako. Acha kuzifuata njia zako katika kuufurahisha mwili wako wa PICHA zisizofaa.
VII) Tafuta watumishi wa Mungu ili wakufundishe - Isaya 48:17, 30:20-21
Kuna mambo ambayo yanatupa shida katika maisha yetu ni vizuri kuwaona waalimu ili watusaidie jinsi ya kutoka katika mtego huo.
VIII) Omba rehema na neema ya Yesu - Waebrania 4:16
Tunahitaji neema ya Mungu ili kushinda Hali hiyo ya kupenda KUANGALIA PICHA ZA NGONO na pia kufunguliwa kutoka katika vifungo hivyo vya pepo wa tamaa na mahaba.
Mungu atakubariki ukipeleka ujumbe huu kwa wengine.
TUMEFIKIA MWISHO WA SOMO LETU KUHUSU DHAMBI YA PICHA ZA NGONO.
Barikiwa sana.
Shalom,

USIOGOPE KWA SABABU YESU YU PAMOJA NAWE

Image may contain: outdoor
Isaya 41:10-13
"usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia. "
Mpendwa USIOGOPE, YESU YU PAMOJA NAWE NA AMESHINDA VITA YOTE.
Barikiwa sana.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

NIFANYE NINI ILI NIWEZE KUSHINDA TAMAA NA FIKRA ZA NGONO KILA SAA?

Image may contain: one or more people and text
Je, Unatatizo la kupiga Punyeto?
Nifanye nini ili niweze kudhibiti fikira chafu za ngono?
Mpendwa:
Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke wakiwa na uvutano wenye nguvu kati yao, na hakuna ubaya wa kutosheleza tamaa za ngono katika mpango wa ndoa. Kabla ya kufunga ndoa, huenda ukawa na tamaa kali za ngono. Hilo likitokea, usidhani kwamba wewe ni mtu mwovu au kwamba huwezi kuishi maisha safi. Unaweza kudumisha usafi wa kiadili ukiamua kufanya hivyo! Lakini ili ufanikiwe, utahitaji kudhibiti mawazo yako kuhusu watu wa jinsi tofauti. Unaweza kufanya hivyo jinsi gani?
Epuka kujifurahisha kwa mambo machafu. Bila shaka, haimaanishi kwamba sinema zote, au miziki yote ni mibaya. Hata hivyo, katika ulimwengu wa leo burudani nyingi zimekusudiwa kuamsha tamaa zisizofaa za ngono. Biblia inatoa shauri gani? “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (2 Wakorintho 7:1) Epuka kabisa burudani zote zinazoweza kuchochea tamaa zisizofaa za ngono.
Je, unatatizo la kupiga Punyeto?
Vijana fulani hujaribu kupunguza tamaa ya ngono kwa kupiga punyeto. Lakini kufanya hivyo kunaweza kutokeza matatizo makubwa. Biblia inawahimiza Wakristo hivi: “Viueni viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye madhara, na kutamani.” (Wakolosai 3:5) Kupiga punyeto ni kinyume kabisa cha ‘kuua hamu ya ngono.’ Kwa kweli, kupiga punyeto huchochea na kukuza hamu hiyo!
Kupiga punyeto kwaweza kukufanya kuwa mtumwa wa tamaa zako. (Tito 3:3) Hatua moja unayoweza kuchukua ili kushinda zoea hilo ni kuzungumza na mtu unayemtumaini. Mkristo aliyekuwa na tatizo la kupiga punyeto kwa miaka mingi anasema hivi: “Laiti ningeweza kupata ujasiri wa kuzungumza na mtu fulani kuhusu tatizo hilo nilipokuwa kijana! Kwa miaka mingi nilisumbuliwa na hisia za hatia, nazo ziliathiri sana uhusiano wangu na wengine, na zaidi ya yote, uhusiano wangu na Yehova.”
Ni nani unayeweza kuongea naye? Mara nyingi ingefaa kuzungumza na mzazi. Au huenda Mkristo mkomavu kutanikoni anaweza kukusaidia. Unaweza kuanza kwa kusema, “Ningependa kuzungumza nawe kuhusu tatizo linalonisumbua sana.”
Nifanye nini ili niweke kudhibiti fikira chafu za ngono?
Mtume Paulo alisema: “Naupigapiga mwili wangu na kuuongoza kama mtumwa.” (1 Wakorintho 9:27) Vivyo hivyo, huenda wewe pia ukahitaji kujitia nidhamu wakati mawazo yasiyofaa kuhusu watu wa jinsia tofauti yanapoingia katika akili yako. Mawazo hayo yakiendelea, jaribu kufanya mazoezi ya kimwili. Biblia inasema: “Mazoezi ya kimwili ni yenye faida kidogo.” (1 Timotheo 4:8) Kutembea kasi kwa muda au kufanya mazoezi ya kimwili kwa dakika chache kwaweza kukusaidia kuondolea mbali mawazo hayo yasiyofaa.
Zaidi ya yote, usipuuze msaada kutoka kwa Baba yako wa mbinguni. Mkristo mmoja anasema hivi: “Tamaa za ngono zinapoanza kuamka najilazimisha kusali.” Si kwamba Mungu atakufanya uache kupendezwa na watu wa jinsia tofauti. Lakini anaweza kukusaidia kuona kwamba kuna mambo mengine mengi unayoweza kukazia fikira zako.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Saturday, April 8, 2017

Acid attacks, mainly on Muslim women

More than 1500 of them just since 2011. Shhh…don’t tell anyone.

In 2017, Muslims still believe that Allah turned Jews into pigs and apes as punishment for rejecting Islam


And how do they know this? Allah told them. That’s probably why in 2017, they still behave like barbarians and savages from the dark ages and should be banned from and driven out of the West.

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW