Saturday, May 13, 2017

How many women in the Bible?

Image result for women of the bible
This Is How Many Words Are Spoken By Women In The Bible. There are 93 women who speak in the Bible, 49 of whom are named. These women speak a total of 14,056 words collectively — roughly 1.1 percent of the total words in the holy book

 Named Bible Women

NABII DEBORA SEHEMU YA KWANZA





JE, UNAMJUA NABII WA KIKE DEBORA WA KWENYE BIBLIA?
SEHEMU YA KWANZA
Biblia inapomtaja kwa mara ya kwanza Debora, inamrejelea kuwa “nabii wa kike.” Cheo hicho kinamfanya Debora awe wa pekee katika masimulizi ya Biblia ingawa haimaanishi kwamba ni yeye tu aliyekuwa na cheo kama hicho. * Debora alikuwa na daraka lingine pia. Inaonekana kwamba alitatua migogoro kwa kutoa majibu ya Mungu, matatizo yalipotokea.—Waamuzi 4:4, 5.
Debora aliishi katika eneo lenye milima la Efraimu, lililokuwa kati ya mji wa Betheli na Rama. Alikuwa na kawaida ya kukaa chini ya mtende na kutumikia watu kulingana na mwongozo wa Mungu. Ni wazi kwamba mgawo wake ulikuwa na changamoto, hata hivyo, Debora hakuruhusu hilo limvunje moyo. Kazi yake ilikuwa muhimu sana. Alishiriki kutunga wimbo ulioandikwa kwa mwongozo wa roho ya Mungu ambao ulitia ndani maneno haya kuhusu watu wake waliokosa kuwa waaminifu: “Wakaanza kuchagua miungu mipya. Ndipo kukawa na vita malangoni.” (Waamuzi 5:8) Kwa kuwa Waisraeli walimwacha Mungu na kutumikia miungu mingine, Mungu aliacha washambuliwe na adui zao. Mfalme wa Kanaani, Yabini, aliwatawala kupitia Sisera, mkuu wa majeshi mwenye nguvu.
Sisera! Jina hilo lilipotajwa katika Israeli lilifanya watu waogope na kushtuka. Dini na utamaduni wa Wakanaani ulikuwa wenye ukatili, kwa kuwa walitoa watoto wao kuwa dhabihu na walifanya ukahaba hekaluni. Hali ilikuwaje mkuu huyo wa jeshi la Kanaani na jeshi lake walipotawala nchi hiyo? Wimbo wa Debora unaonyesha kwamba ilikuwa vigumu kusafiri nchini na maisha katika maeneo ya vijijini yalikuwa magumu, hivyo watu walihama. (Waamuzi 5:6, 7) Tunaweza kuwazia jinsi ambavyo watu walikuwa wakiogopa na kujificha katika mapori na vilima, wakiogopa kulima au kuishi katika vijiji ambavyo havikuwa na ukuta na wakiogopa sana kushambuliwa kwa sababu ya kusafiri barabarani, watoto wao kutekwa, na wanawake wao kubakwa. *
Hofu ilitawala nchini kwa miaka 20 mpaka Yehova alipoona wazi kwamba watu wake wakaidi walikuwa tayari kubadilika au, kama wimbo ulioandikwa na Debora na Baraka kwa mwongozo wa roho ya Mungu unavyosema, “Mpaka mimi, Debora, niliposimama, mpaka niliposimama kama mama katika Israeli.” Hatujui ikiwa Debora, mke wa Lapidothi, alikuwa na watoto, lakini usemi huo ulikuwa lugha ya mfano. Ni kana kwamba Yehova alimpa Debora mgawo wa kulinda taifa hilo kama vile mama angefanya kwa watoto wake. Alimwagiza amwambie Mwamuzi Baraka, mwanamume mwenye imani yenye nguvu, aende kupigana na Sisera.—Waamuzi 4:3, 6, 7; 5:7.
Mungu alitoa agizo hili kupitia Nabii Debora: “Nenda, usambae katika Mlima Tabori.” Baraka alipaswa kukusanya wanaume 10,000 kutoka makabila mawili ya Israeli. Debora alitaja ahadi ya Mungu kwamba wanaume hao wangemshinda Sisera mwenye nguvu na magari yake 900 ya vita! Bila shaka ahadi hiyo ilimfanya Baraka astaajabu. Waisraeli hawakuwa na jeshi wala silaha. Licha ya hali hiyo, Baraka alikubali kwenda vitani ikiwa tu Debora angeenda pamoja naye katika Mlima Tabori.—Waamuzi 4:6-8; 5:6-8.
Kwa sababu ya ombi hilo, watu fulani hudai kwamba Baraka hakuwa na imani, lakini jambo hilo si kweli. Baraka hakumwomba Mungu ampe silaha zaidi. Akiwa mwanamume mwenye imani, Baraka aliona umuhimu wa kuandamana na mwakilishi wa Mungu ili kumwimarisha na kuimarisha watu wake. (Waebrania 11:32, 33) Mungu alikubali ombi lake. Alimruhusu Debora kwenda na Baraka kama alivyoomba. Hata hivyo, Mungu alimwezesha Debora kutabiri kwamba ushindi wa pigano hilo usingetokana na mwanamume. (Waamuzi 4:9) Mungu aliamua kwamba mwanamke ndiye atakayemuua Sisera aliyekuwa mwovu!
Katika ulimwengu wa leo, wanawake wanakabili matendo mengi ya ukosefu wa haki, jeuri, na kutendewa vibaya. Ni mara chache sana wanatendewa kwa heshima kama Mungu anavyotaka watendewe. Hata hivyo, machoni pa Mungu, wanawake na wanaume wana haki sawa na wanaweza kupata kibali chake. (Waroma 2:11; Wagalatia 3:28) Mfano wa Debora unatukumbusha kwamba Mungu huwabariki wanawake kwa kuwapa mapendeleo na hilo linaonyesha kwamba anawatumaini na kuwapa kibali chake. Ni muhimu kwamba tuepuke kuwa na maoni yasiyofaa kuelekea wanawake yaliyoenea ulimwenguni leo.
USIKOSE SEHEMU YA PILI YA NABII DEBORA: DUNIA ILITIKISIKA, MBINGU PIA ZIKATIRIRIKA MAJI...
Baraka alikusanya jeshi lake. Alikusanya wanaume 10,000 jasiri ili kupambana na jeshi la Sisera lenye kutisha...........
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

JE, TUNAWEZA AMINI UNABII NA MANABII WA SIKU ZA MWISHO? SOMO LA KWANZA

Image may contain: one or more people and text
Somo la Kwanza:
Karibu kila kitabu cha Bibilia kiko na unabii kuhusu nyakati za mwisho. Kuzungumzia huu unabii na kuupanga waweza kuwa kazi ngumu.
Miaka 2,000 hivi iliyopita, Biblia ilitabiri kwamba hali mbaya za ulimwengu zingefikia mwisho wakati wa “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3) Hatumaanishi “mwisho wa dunia” kama watu wengi wanavyofikiri utatukia. Badala yake, Biblia inaeleza kuhusu mfuatano wa matukio na mitazamo, au dalili, ambayo ingetokea katika kipindi cha wakati unaoitwa “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1) Yesu aliwaambia wafuasi wake kwamba wanapoona “mambo hayo yakitukia” wajue kwamba kitulizo kitafuata punde baadaye. (Luka 21:31) Fikiria baadhi ya unabii unaoonyesha kwamba wakati wetu ni wa pekee.
UNABII WA KWANZA:
“Taifa litasimama kupigana na taifa.”—Mathayo 24:7.
Utimizo: Katika miaka ya mapema ya karne ya 20, wengi walikuwa wakitazamia kwamba amani ingeendelea kuwapo. Ulimwengu ulishtuka Vita vya Kwanza vya Ulimwengu vilipozuka, na enzi ya vita visivyo na kifani ikaanza. Kama kitabu cha Ufunuo kilivyotabiri, amani iliondolewa “duniani ili [wanadamu] wauane.”—Ufunuo 6:4.
UTHIBITISHO UNAONYESHA NINI?
“Kutokea kwa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu katika mwaka wa 1914 kuliashiria mwisho wa enzi moja na kuanza kwa enzi nyingine.”—The Origins of the First World War, kilichochapishwa mnamo 1992.
Ingawa idadi ya watu waliokufa wakati wa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu haiwezi kujulikana kabisa, ensaiklopedia moja inakadiria kwamba idadi ya wanajeshi waliokufa ni 8,500,000.
Watu wengi zaidi walikufa wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu, kwani inasemekana kuwa kati ya wanajeshi na raia milioni 35 hadi milioni 60 waliuawa.
Kati ya mwisho wa vita vya pili vya ulimwengu na mwaka wa 2010, kumekuwa na vita 246 katika maeneo 151 ulimwenguni pote.
UNABII WA PILI:
“Kutakuwa na upungufu wa chakula.”— Mathayo 24:7.
Utimizo: Njaa ilisababisha zaidi ya vifo milioni 70 katika karne ya 20 na bado ni tatizo kubwa ulimwenguni pote.
UTHIBITISHO UNAONYESHA NINI?
Kulingana na Umoja wa Mataifa, njaa ndiyo tisho kubwa zaidi kwa afya ulimwenguni, na mtu 1 kati ya 7 ulimwenguni hana chakula cha kutosha.
“Leo upungufu wa chakula hausababishwi na kukosekana kwa mavuno ya kipindi fulani kwa sababu ya hali mbaya ya hewa ya muda, bali unasababishwa na mambo manne yanayoendelea kwa muda mrefu: kuongezeka ghafula kwa idadi ya watu, kupotea kwa udongo wa juu, kuenea kwa upungufu wa maji, na kuongezeka kwa kiwango cha joto.”—Scientific American.
UNABII WA TATU:
“Kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi.”— Luka 21:11.
Utimizo: Kwa sababu watu wengi zaidi wanaishi katika maeneo ambayo hupatwa na matetemeko ya nchi mara nyingi, idadi ya watu wanaokufa au wanaolazimika kuhama kwa sababu ya tetemeko la nchi imeongezeka haraka.
UTHIBITISHO UNAONYESHA NINI?
Ripoti inayoitwa World Disasters Report 2010 inasema hivi: “Kati ya misiba yote mikubwa, matetemeko ndiyo yamesababisha vifo vya watu wengi zaidi katika miaka ya karibuni.”
Kila mwaka, kuanzia 1970 hadi 2001, kulikuwa na wastani wa matetemeko ya nchi 19 yaliyosababisha misiba, * na wastani wa watu 19,547 walikufa kutokana nayo. Katika miaka kumi kabla ya 2012, wastani huo uliongezeka kufikia matetemeko ya nchi 28 kwa mwaka, kukiwa na wastani wa watu 67,954 waliokufa.
UNABII WA NNE:
“Mahali pamoja baada ya pengine kutakuwa na tauni.”—Luka 21:11.
Utimizo: Licha ya kwamba kuna maendeleo ya kitiba na sayansi, bado mamilioni ya watu hufa kila mwaka kwa sababu ya magonjwa ya kuambukiza. Usafiri wa kimataifa na kuongezeka kwa idadi ya watu katika majiji kumeongeza uwezekano wa kutokea na kuenea upesi kwa magonjwa.
UTHIBITISHO UNAONYESHA NINI?
Inakadiriwa kwamba ugonjwa wa ndui uliwaua watu milioni 300 hadi 500 hivi katika karne ya 20.
Taasisi ya Worldwatch inaripoti kwamba katika miaka 30 iliyopita, “zaidi ya magonjwa 30 ambayo hayakuwa yamejulikana hapo awali kama vile Ebola, virusi vya UKIMWI, virusi vya Hanta, na Mafua ya Ndege yametokeza hatari.”
Shirika la Afya Ulimwenguni limeonya kuhusu kuongezeka kwa virusi visivyoweza kutibiwa, likisema: “Tunaelekea wakati ambapo hatutatumia tena dawa za kuua viini, kwa kuwa maambukizo mengi ya kawaida hayataweza kutibiwa na yatawaua watu bila kuzuiwa.”
UNABII WA TANO:
Watu ‘watasalitiana na kuchukiana.
Upendo wa walio wengi zaidi utapoa.’—Mathayo 24:10, 12.
Utimizo: Mauaji ya jamii nzimanzima yanayochochewa na chuki yamesababisha vifo vya mamilioni ya watu. Mizozo na uhalifu katika nchi nyingi imechangia sana kuongezeka kwa woga na jeuri.
UTHIBITISHO UNAONYESHA NINI?
Serikali ya Nazi iliwaua Wayahudi milioni sita na mamilioni ya wengine. Mwandishi Zygmunt Bauman aliandika hivi akielezea jinsi raia walivyotenda: “Mauaji hayo ya halaiki hayakuwafanya watu wapandwe na ghadhabu, bali walinyamaza kimya kana kwamba hawakujali.”
Kulingana na Shirika la habari la BBC, inakadiriwa kwamba Watutsi na Wahutu ambao hawakuwa na msimamo mkali wapatao 800,000 waliuawa katika muda wa miezi michache. Mchunguzi mmoja anakadiria kwamba watu 200,000 hivi walihusika katika mauaji hayo ya halaiki.
Kila mwaka, zaidi ya watu 740,000 hufa kutokana na uhalifu na vita.
UNABII WA SITA:
“Watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, . . . wasio na upendo wa asili.”—2 Timotheo 3:2, 3.
Utimizo: Enzi yetu imejaa pupa na upotovu wa maadili. Mitazamo ya aina hiyo imetokeza matatizo mengi ya kijamii.
UTHIBITISHO UNAONYESHA NINI?
Ripoti moja ya UNICEF nchini Uingereza kuhusu hali njema ya watoto inasema kwamba wazazi na watoto nchini Uingereza “wanaonekana kuwa hawawezi kujizuia wasinunue vitu.” Watu katika familia hununua vitu vya kimwili ili “wajaribu kurekebisha mahusiano yao yaliyo na matatizo na pia ili wajihisi salama.”
Inakadiriwa kwamba watoto milioni 275 ulimwenguni pote hujionea jeuri inayotokea nyumbani.
“Nchini Marekani pekee, zaidi ya wazee 500,000 wanatendewa vibaya au kupuuzwa kila mwaka.”—Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa ya Kuambukiza.
UNABII WA SABA:
“Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa.” —Mathayo 24:14.
Utimizo: Biblia inafundisha kwamba Ufalme wa Mungu ni serikali halisi, inayotawala kutoka mbinguni na Yesu ndiye Mfalme. Ufalme huo wa kimbingu “utazivunja na kuzikomesha [serikali zote za wanadamu], nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.”—Danieli 2:44.
USIKOSE SOMO LA PILI: Unabii Mbalimbali Wenye Kustaajabisha.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds

  BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds. The targets included a Radwan Force training facility used for weapons drills ...

TRENDING NOW