Friday, July 14, 2017

WAISLAM ZAIDI YA MILIONI 1.4 WAMPOKEA YESU SAUDI ARABIA


Image may contain: 7 people

Ingawa hii ni asilimia ndogo ukilinganisha na watu wote wanao ishi Saudi Arabia, lakini asilimia hii ya 4.4 ni ongezeko kubwa kutoka ile ya 0.1 ya miaka mia iliyo pita.
Uislam ni dini ya nchi ya Saudi Arabia na Ukristo ni marufuku katika nchi hiyo. Adhabu ya kuwa Mkristo nchini humo ni kifo kwa kukatwa kichwa.
Adhabu hii ya kifo imeshindwa kumzuia Yesu kuto ingia nchini humo na kwasasa Ukristo unaongezeka kwa nguvu ya ajabu.
Kwa habari kamili ingia hapa: http://thesocialmag.net/muslims/

NANI KAMPA UTUME NA UNABII MTUME MUHAMMAD? SEHEMU YA KWANZA

Image may contain: 3 people, people on stage and text


Twakusalimu kwa mara ingine katika jina tukufu na takatifu la Yesu Kristo Bwana wetu.
Twazidi pia kukushukuru kwa ajili yakuyafuata mafundisho haya ya Biblia Takatifu.
Twaamini mada ile ile lakini ya tatu kuhusu imani ya kiislamu itakusaidia ukiwa mkristo wa kweli kutoishiriki mihadhara ya ubishi kati ya waislamu na wakristo.
Sababu ya pili, ni kwako ndugu na dada ambaye ungali bado katika upotevu wa uislamu bila yako kujuwa ukweli kwa wazi.
Katika zile sababu zaidi ya 25 zinazotudhihirishia uongo na upotevu wa dini ya uislamu tumetamani kuchimbua «Utume na unabii wa nabii Muhammad s.a.w»
Tunazo sababu zaidi ya mia (100) kuwauliza Waislamu na kitabu chao Qura'n swali tulilolitaja hapo juu na maswali mengine kuhusu UISLAMU na Qura'n! na moja ya hayo maswali ni sababu kitabu chao yaani Qur’ani kinatutaka sisi wakristo kusilimu, lakini kabla tusilimu nakuingia dini ya uislamu ni sherti tumjuwe vyema vilivyo huyu nabii sababu Yesu Kristo anatuonya kwamba manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi yamkini hata wachaguliwa wa Mungu. Mathayo 7 :15-20.
Kwa hivi ni sherti Muhammad atumbukizwe ndani ya Biblia iliyokitangulia kitabu alichopewa ijapokuwa baadaye tutajuwa alikipewa na nani ? na akizama ndani ya Biblia hatuna budi kumfwata na kumtumikia Allah subhanahu wa tahalah! Lakini ikimtema kando huyo si nabii na mtume wa Yehova Mungu.
Ukweli ambao hatuwezi kuupinga ni kwamba Biblia Takatifu ambayo waislamu pia huitumia kwakuichezea-chezea na isitoshe pia kwakuitumia kuwapiga wakristo waliopofushwa wakidhani kwamba waislamu wanaiamini, hiyo Biblia imekuwapo duniani zaidi ya miaka 2000 kabla ya Qur’ani tukufu kuwepo.
Biblia Takatifu inasema hivi:
Kutoaka 20:1-3
«Mungu akanena maneno haya yote akasema, Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi.»
Hapa Mungu alitutahazarisha mapema kumpitia mtumishi wake nabii Musa ya kwamba tuepuke kuwa na miungu mingine ila yeye pekee ambaye jina lake ni Yehova!
Haya maneno sawa na Mathayo 7:15-20 Mungu aliyasema kabla ya Muhammad kuwepo, kabla ya Qur’ani kuwepo na kabla kuwepo kwa wanaume 4 walioiandika Qur’ani tukufu ambao ni:Seidinah Umar, Osman, Abubakar na Ali.
Inamaanisha nini?
Ni kwamba kama Mungu mwenyezi anavyokuwa na watumishi kama vile mitume na manabii, vilevile miungu nayo yaweza kuwa namitume na manabii wake.
Kwa mujibu wa Mathayo 7:15-20, Yesu Kristo anatupatia alama yakuwatambuwa manabii wa uongo akisema katika mstari wa 16 hivi « Mtawatambua kwa matunda yao »
Basi natujaribu kuliangalia andiko lingine jinsi gani twaweza kuwatambua,
1Yohana 4:1-3, 15
«Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu.
Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.»
15 «Kila akiriye ya kuwa Yesu ni mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.»
Hiki ni kipimo tunachokitumia kuwapima mitume na manabii!
Mathayo 7:15-20
Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?
Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.»
Hebu niseme hivi kulingana na tahazari ambayo Mungu ametupatia katika maandiko hayo mawili hapo juu:
‘Muhammad namlinganisha na mti, sasa matunda yake yakiwa mazuri sina ubishi nitamfuata, lakini yakiwa ni matunda kinyume na hayo nitamhesabu kama nabi iwa uongo’.
Je, katika Qurani Allah wa waislamu na Muhammad anasemaje?
Qr. 112 au surat Al-Ikhlas’
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
Hakuzaa wala hakuzaliwa.
Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.
Qr. 19 au surat Maryam 35
Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwa na mwana, Subhanau, Yeye ametakasika! Anapolihukumia jambo basi huliambia tu: Kuwa! Likawa.
Huyu ni mungu tofauti na Mungu wa mbinguni ambaye jina lake ni Yehova! na tukilinganisha na yale maandiko ya Mathayo na waraka wa kwanza wa Yohana ukweli uko wazi kama huyu hatokani na Mungu na kwamba huyu ni Anti-Kristo! Kwani Biblia inasemaje ?
1Yohane 2:22-26,
Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana. Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia. Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba.
Na hii ndiyo ahadi aliyoyuahidia, yaani, uzima wa milele.
Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza.
Wakolosai 1:13-15,
Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi; Naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
Yohane 3:16-17,
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminie asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Kwa maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.
Kwahivi sisi wakristo tunazo sababu zaidi ya 100 kwanini hatumtambui mtume Muhammad, dini yake na mungu wake ambazo Mungu akituwezesha tutaziweka wazi moja kwa moja.
Ila hatuwezi kutosema hii moja ambayo ni hii:
Katika kitabu cha Qura’n tukufu kuanza na surat Al-Faatihah hadi surat Al-Nasmaandishi yake yanampinga Yehova Mungu wa israel.
CHIMBUKO NA UKOO WA UTUME NA UNABII WA MUHAMMAD
Kwanza kabisa, sote twajuwa kama kila mtoto huenda na kabila, lugha na mil aya babaake ila si ya mamaake. Hilo halina shaka hata kidogo!
Ibrahimu babaake Isaka na Ismail kabla aitwe na Mungu alikuwa ni mwarabu wa ki kurdi na baadaye Mungu aliyeviumba vyote akambadilisha na uzao wake wote baadaye ukawa ni waebrania.
Mwanzo 12:1-3
«Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.»
Lakini Muhammad, Qur’ani na wafuasi wake huzidi kuhakikisha kuwa Muhammad ni wa ukoo wa Ibrahimu wakati Ibrahimu si mwarabu tena!
Katika kitabu cha «maisha ya mtume Muhammad sw», twahakikishiwa kwamba Muhammad ni mwarabu wa kabila la Makureshi.
KUPEWA UTUME
Nilipokuwa nikichunguza kitabu cha historia ya Muhammad, kwa umri wake wa miaka 12 alikwenda na Abu Talib baba yake mdogo huko Shamu (Syria) kwa safari ya biashara, njiani wakakutana na mwanamume nabii wa kikristo ambaye jina lake alikuwa ni Bahirah naye akatowa unabii kuhusu Muhammad kwa maneno haya:
« Ewe Abu Talib;
Mtunze vema mtoto huyu kwa maana naona alama za umaarufu kwa mtoto huyu katika siku zake za usoni naye atapata kazi ya kumtumikia Mungu.»
Ni katika kitabu cha Maisha ya mtume Muhammad, ukurasa namba 4. Swali ni hili, lini nabii wa kikristo akatabiri uislam? Jibu ni hapana sababu neno la unabii kutoka kwa Mungu haliwezi kamwe kutabiri imani kinyume na Mungu na Kristo mwana wake wa pekee!
Mithali 8:7-9
«Maana kinywa changu kitasema kweli, Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu. Maneno yote ya kinywa changu yana haki; Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi. Yote humwelea Yule afahamuye, Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa.»
2Petro 1:20-21
« Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.»
Tito 1:2
« katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele; akalifunua neno lake kwa majira yake katika ule ujumbe niliowekewa amana mimi kwa amri ya Mwokozi wetu Mungu»
Kumbe ni wazi kwamba nabii huyu alikuwa na ujumbe muhimu kwamba siku moja Muhammad angalimtumikia Kristo Yesu na Ukristo lakini kwa bahati mbaya shetani akaubadilisha mwelekeo wa huyu maskini baadaye kama tutakavyoona katika wito wake.
Pangoni la Jabal Hira kaskazini mwa Mekka ndiko Muhammad alikuwa akienda kuabudu siku zote lakini alikuwa akimwabudu nani? Nakuomba tusome huu wito wake wa utume hapo chini.
USIKOSE SEHEMU YA PILI

MLEE MTOTO KATIKA NJIA IMPASAYO NAYE HATAIACHA HATA ATAKAPOKUA MZEE

Image may contain: one or more people, people standing and outdoor

"Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee." Mithali 22:6
Mwenendo wenu ni fundisho kubwa kabisa mbele ya mtoto wenu. Njia ipasayo kumlea mtoto ni kuketi na mtoto na kumshauri maadili mema ya maisha (Kumbukumbu la Torati 6:7). Ni kumwelekeza kwenye mambo matakatifu, kabla hajaharibiwa na walimwengu.
Bibilia iko na mengi ya kusema kuhusu njia tunayoweza kuwalea watoto wetu wawe wanaume na wanawake wa Mungu. Kitu cha kwanza tunastahili kufanya ni kuwafunza ukweli kuhusu neno la Mungu.
Pamoja na kumpenda Mungu na kuwa mfano mwema kwa kujitoa sisi wenyewe kwa amri zake, tunastahili kuzitii amri za Kumbukumbu 6:7-9 kuhusu kuwafunza watoto wetu kufanya hivyo. Ufahamu huu unasisitiza jambo linaloendelea wa maelekezo hayo.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

NANI KAMPA UTUME NA UNABII MTUME MUHAMMAD? SEHEMU YA PILI.

Image may contain: 1 person, smiling, text


Huu ni uhakikisho kwamba Muhammad hakupewa utume na Mungu wa israeli, sababu ukisoma pia kitabu chawakeze wakubwa na wanaweukurasa wa 12 kuna maneno yanayorudilia haya ambayo tumeyasoma hapo juu yakisema hivi:
Nanukuu,
Basi mtume akafanya hofu akarejea kwa mkewe, akamwadithia na palepale homa kubwa kabisa ikampanda, akataka afunikwe na maguo mara akawa anatetemeka kwa nderema na anaweweseka na kusema: «Najihofia nafsi yangu kuchezewa na mashetani na kuniharibu akili yangu na kunizuga!»
Hapo katika pango la Jabal Hira ndipo waislamu na qura’n hudai kwamba ndipo alipopokea Wahyi wa qura’n, utume na unabii.
Lakini twaona na kusikia maneno ya mtume mwenyewe yanashuhudia alichokutana nacho pangoni ambacho ni shetani sababu hata Biblia Takatifu hushuhudia hivi:
1Yohana 1:3
Hilo tuliloliona nakulisikia, twalihubiri na nyinyi: ili na nyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.»
Ukweli ni kwamba huyu shetani aliyekutana na maskini Muhammad pangoni hakumpa hata utume wala unabii isipokuwa mkewe Hadidja na Bwana Waraqa bin Naufal ndio waliomshauri Muhammad kujibashiria kuwa yeye ni mtume wa uma kama tulivyo soma katika kurasa ambazo tumekuwekea picha zake hapo juu.
Ikumbukwe vizuri kwamba haya yalitokea wakati ambao uislamu na qura’n havikuwepo kwanza na historia ya maisha ya mtume kinamtambuwa Waraqa bin Naufal kama mtu ambaye hakuwa naabudu sanamu za waarabu wenzake! Lakini yeye ni nani kutowa ruhusa kwa mtu kama Muhammad ili ajibashirie utume? Hapo kuna mashaka mengi.
Vipi kwa Hadidja?
Mjane aliyefiwa na waume wake 2 kisha akajichukulia Muhammad kama mume wake wa tatu, Huyu ndiye aliyeingia wa kwanza katika imani potofu ya uislamu. Lakini natujiulize hili swali: « je, inakuwaje mtu ambaye bado ni mkafiri kutowa utume kwa mwingine kabla yeye hajajuwa ujumbe wa mtume huyo nakuuamini?» Bila shaka jibu laweza kuwa ni upumbavu wakupindukia.
Hebu tuone qura’n inavyosema kuhusu kupewa utume, kupewa wahyi au ujumbe,
Qr.7:144 au surat Al-A’raaf 144
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Musa! Mimi nimekuteuwa wende kwa watu na ujumbe wangu na maneno yangu. Basi chukuwa niliyikupa na uwe katika wale wanaoshukuru.
Kwanini Allah Subhanau Watahallah hakufanya hivihivi kwa Muhammad s.a.w katika pango la Jabal Hira?
Swala la Muhammad kuwa ni mtume katika maandishi ya qura’n na hadithi zote siyo hoja lakini hoja tu ni «Kapewa na nani huo utume?»
Tuchunguze na kuchimbua tena hili andiko la Qura’n,
Qr. 13:43 au surat Ar-raa’d 43
Na waliokufuru wanasema kuwa wewe si mtume,
Sema, Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi, na pia yule mwenye ilimu ya kitabu.
Anayemwambia Muhammad kusema ni ALLAH wake na wa waislamu wote.
Anayedaiwa kuwa shahidi bain aya ALLAH na waislamu ni Mwenyezi Mungu.
Anayedaiwa kuwa ni mwenye ilimu ya kitabu ni Jibril.
Kwa wazi kabisa ni kwamba Allah wa awislamu ni tofauti na Mwenyezi Mungu sababu anamtowa kuwa shahidi kati yake na wafuasi wake yaani waislam. Je, Mwenyezi Mungu anasemaje kuhusu miungu mingine?
Isaya 42:8
«Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.»
Isaya 48:11
«Kwa ajili ya nafsi yangu, kwa ajili ya nafsi yangu, nitatenda haya; je! Litiwe unajisi jina langu? Wala sitampa mwingine utukufu wangu.»
Kumbukumbu 18:18
« Mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru. Hata itakuwa, mtu asiyesikiliza maneno yangu atakayosema yule kwa jina langu, nitalitaka kwake.
Lakini nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu, ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena katika jina la miungu mingine, nabii yule atakufa.»
Uislamu na qura’n wanadai aliyetabiriwa na nabii Musa kwamba ni Muhammad s.a.w lakini kama tulivyochunguza katika yale matoleo ya kwanza ni kwamba sio Muhammad bali alikuwa Yesu ambaye angekuwa masihi na Kristo wa dunia yote! Kwa sababu hizi chache tu:
ALLAH S.W NA MUHAMMAD S.A.W
YEHOVA MUNGU NA YESU KRISTO
mungu asye na jina kamili
Qr. 17 au surat Bani Israil 110 (Wana wa Israil)
Sema; muombeni (Mwenyenzi Mungu) kwa (jina la) Allah au muombeni (kwa jina la) Rahman. Kwa jina lolote mnalomwita (katika haya itafaa). Kwani ana majina mazuri mazuri………
Mungu anayejulikana
Kutoka 6:2-3,
Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, mimi ni YEHOVA;
Nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.
mungu wao ana maadui wake ambao ni wakristo na wayahudi
Qr. 4:51 na 57 (surat Al Maida)
Enyi mlioamini! Msiwafanye mayahudi na wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika hao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu.
Wafuasi wote wa Allah wanangojea moto wa jehanam kisha waokolewe waislam baadaye kutoka motoni
Qr. 19:70-72
Tena hakika sisi tunawajuwa vyema Zaidi wanaostahiki kuunguzwa humo
Wala hapana yeyote katika nyinyi ila ni mwenye kuifikia. Hiyo ni hukumu ya Mola wako mlezi ambayo lazima itimizwe. Kisha tutawaokoa wale waliomcha Mungu; na tutawaacha madhalimu humo hali wamepiga magoti motoni.
Mungu wetu ni mwenye rehema na wafuasi wake hatuna adui
Mathayo 5:43-44
Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
Kwetu wakristo sivyo ilivyo!
Zaburi 9:17
Wadhalimu watarejea kuzimu, Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.
Luka 16:23
Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.
Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
Allah wao ataionja jehanamu pia
Qr. 50 au Surat Qaf 30 (kuapa)
Siku tutakayoiambia Jahanamu, ‘Je! Umejaa?’ Nayo itasema ‘Je kuna ziada (zaidi? Naije tu!
Imesimuliwa na Anas kuwa: mtume alisema watu watatupwa jahanamu, Naye Allah ataiuliza jahanamu akisema je umejaa nayo jahanamu itasema kwani kuna nyingine zaidi na ije tu? Mpaka Allah atakapo ingiza mguu wake nayo jahanamu itasema inatosha! Inatosha
Dhawabu ya wakristo ni uzima wa milele
Yohana 14: 1-4
Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Nami niendako mwaijua njia.
Hizi ni sababu ndogo kutoka katika zile sababu zaidi ya 100 ambazo ziko wazi kabisa kama Muhammad kapewa utume na yeye mwenyewe kwa shauri la mkewe Hadidja na Bwana Waraqa bin Naufal.
Twataka tukupe baadhi ya mashaka katika qura’n
# Katika Qura’n sur aya 3, aya yake ya 7 (surat Al I’mran) panasema kwamba kuna aya nyingi katika Qura’n ambayo mwanadamu hana uwezo kuzisoma na kuzitafsiri isipokuwa Allah.
# Katika sura za 11:114, sur aya 17:78-79, sura ya 20:130, na sur aya 30:17-18 za qura’n Allah anasema kwamba kila mwislam analazimika kusali mara tatu kwa siku, lakini katika hadithi za mtume huyo huyo Allah anawalazimisha waislam kusali mara tano kwa siku. Je, Allah hana uamzi moja? Waislam kazi kwenu!
# Katika sur aya 18:86 ya qura’n, Allah hukiri kwa Muhammad kwamba jua hutua katika dimbwi la maji machafu duniani. Je, hiyo ni kweli? Kama Mwenyezi Mungu ni muumba jinsi gani anaweza kufanya makosa kama haya? Na je, Biblia inasemaje kuhusu uumbaji? Soma kitabu cha Mwanzo sura 1 na mbili.
# Katika sura 2:106 na sura 16:101 katika qura’n Allah anasema kama alirekebisha aya katika qura’n na kutangua au kubadilisha aya zingine ili kuweka zilizo bora zaidi. Je mungu ni mtu ili abadilishe neno lake?
Isaya 40:8, «Majani yakauka, ua lanyauka; Bali neno la Mungu wetu litasimama milele.»
Tunazo sababu zaidi tutakazoziweka hadharani katika sehemu zitakazofuata katika siku zinazokuja ili kukusaidia wewe muislam kuufikia wokovu kamili katika Kristo Yesu Bwana wetu na mwokozi wetu.
Twamalizia toleo hili tukikuomba katika upendo wa kristo kuikimbilia mbali sana ibada ya shetani katika dini ya uislamu na kukimbilia kwa Yesu Kristo ili upate uzima wa milele.
Matendo ya mitume 4:11,12
Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni. Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.
MBARIKIWE NYOTE
Ndugu yako katika Kristo

AISHA MKE WA MUHAMMAD MWENYE MIAKA SITA

Image may contain: 12 people, people standing, wedding and text

SEHEMU YA KWANZA
Watu wengi wamesema kuwa Muhammad alifanya tendo la ndoa na mke wake mwenye umri mdogo zaidi, A’isha, binti wa Abu Bakr, alipokuwa na miaka karibu 53 na [A’isha] alikuwa na miaka tisa. Baadhi ya Waislam wanakataa maneno haya. Kama mtu atadai kuwa Muhammad na A’isha walijamiiana wakati A’isha alipokuwa na umri wa miaka tisa, na walifanya makosa, jambo hili litakuwa ni kashfa kubwa sana kwa Muhammad. Kwa upande mwingine, kama ilikuwa kweli, jambo hili litaonyesha sura tofauti kabisa ya Muhammad itakayo washtua watu wengi. Kwa hiyo basi, madai haya dhidi ya Muhammad ni ya kweli au uongo?
Andiko hili litaanza kwa kutoa ushahidi wa A’isha kuwa na miaka tisa wakati ndoa yake ilipokamilishwa kwa tendo la unyumba, kisha litatoa vipingamizi 11 dhidi ya jambo hili, na mwishoni, litauliza itakuwa vipi endapo kila wazo lilikuwa sahihi.
Jambo hili ni la muhimu kwa desturi iliyotumika sehemu nyingi sana lakini ambayo imepuuzwa sana siku za leo: mabibi arusi watoto kwenye nchi za Kiislam waliotokana na mfano wa Muhammad.
Huko Iran, hadi kufikia Juni 2002 iliruhusiwa kisheria kwa msichana wa miaka 9 kuolewa kwa ruhusa ya wazazi. Voices Behind the Veil (Sauti Ttokea Nyuma ya Mtando) uk.136-137.
Huko Ivory Coast kitabu hiki pia kinatuambia kuhusu msichana wa miaka 12 ambaye alikuwa anaondoka nyumbani asubuhi kwa masaa mengi kabla ya kurudi nyumbani. Baada ya baba yake kumfunga, alimuunguza kwa kipande cha chuma, alimfungia kwa muda wa siku tatu bila chakula, hatimaye almwoza kwa mwanaume wa miaka 40. Hakuwahi kumpeleka shule kwa sababu alisema kuwa jambo hilo litawaondoa kwenye desturi zao, (mabinti) wataanza kuuliza maswali, na kutokupenda kuolewa mpaka wafikishe umri wa maka 19 au 20.
Wataliban walizishawishi familia zao kuoza mabinti wao wakiwa na umri mdogo hata miaka nane. Voices Behind the Veil uk.110.
Gazeti la Dallas Morning News 9/28/03 uk.1,10S lilikuwa na habari ya kusikitisha kuhusu tabu ya wasichana wa Kiislam wa Nigeria ambao waliolewa wakiwa na umri mdogo sana, walipata ujauzito na walipopata uchungu wa uzazi miili yao midogo ilikuwa bado haijawa tayari. Kwa kiasi kikubwa habari hii ilikuwa mbaya, kimsingi wengi wa wasichana hao walihitaji kuzaa kwa upasuaji (C-section) lakini hawakuweza kupata huduma hiyo. Wengi wao walinusurika, lakini hawakuweza kupata watoto tena kwa sababu ya kuharibiwa kwa miji ya mimba.
Ili kuelewa asili ya mamlaka ya mfano wa Muhammad, ni muhimu tufahamu jambo moja kuhusu Hadithi za Kiislam. Hadithi zina nafasi ya juu sana katika madhehebu ya Suni kuliko mapokeo yalivyo na nafasi kwenye makanisa ya Katoliki na Orthodox. Waislam wa madhehebu ya Suni wanaamini kuwa mikusanyiko sita ya Hadithi ndiyo yenye mamlaka kubwa zaidi kwenye Uislam baada ya Kurani. Sehemu iliyobaki ya andiko hili inaonyesha kuwa dai hili ni la kweli kabisa, kwa mujibu wa vyanzo vingi vya awali vya Kiislam vyenye kuunga mkono. Pamoja na nukuu hizi toka kwenye Hadithi sita zinazoaminika ni nukuu toka kwa wana historia wa zamani wa Kiislam wanaoheshimika sana ibn Ishaq na al-Tabari.
1. Sahih al-Bukhari 810-870 BK, 256 BH
1a. "Alisimulia baba wa Hisham: Khadija alkufa miaka mitatu kabla ya Nabii kuondoka Madina. Alikaa huko miaka miwili au zaidi kisha akamuoa ‘Aisha alipokuwa msichana mwenye umri wa miaka sita, na Muhammad aliikamilisha ndoa yao kwa tendo la unyumba wakati ‘Aisha alipokuwa na umri wa miaka tisa." Bukhari juzuu ya 5 kitabu cha 58 sura ya 43 na.236, uk.153.
1b. Habari hizo zipo pia kwenye Bukhari juzuu ya 5 kitabu cha 58 sura ya 43 na.234, uk.152.
1c. "Alisimulia ‘Urwa: Nabii aliandika (mkataba wa ndoa) na ‘Aisha wakati msichana alipokuwa na umri wa miaka sita na aliikamilisha ndoa yake nay eye kwa tendo la unyumba wakati akiwa na miaka tisa na ‘Aisha aliendelea kuwa naye kwa miaka tisa (yaani mpaka kifo cha Nabii). Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 62 sura ya 60 na.88, uk.65.
1d. Alisimulia ‘Aisha: Nabii alikuwa akinisitiri kwa Rida (vazi lenye kukinga sehemu ya juu ya mwili) yake nilipokuwa nawaangalia Waethiopia waliokuwa wanacheza kwenye ua wa nyuma wa msikiti. (Niliendelea kuangalia) hadi nilipotosheka. Hivyo unaweza kuelewa ni jinsi gani binti mdogo (ambaye hajafikia umri wa kuvunja ungo) ambaye ana hamu ya kufurahia burudani alivyofanyiwa mambo ya namna hii. Bukhari juzuu ya7 kitabu cha 62 sura ya 115 na.163, uk.119.
1e. "Alisimulia ‘Aisha: (mke wa Nabii) sikumbuki kama wazazi wangu waliamini dini yoyote ile isipokuwa dini ya kweli (yaani Uislam), na (sikumbuki) siku yoyote iliyopita bila sisi kutembelewa na Mtume wa Allah asubuhi na jioni." Bukharijuzuu ya 5 kitabu cha 58 sura ya 4 na.245, uk.158. Kwa hiyo, ‘Aisha ama hakuwa mkubwa ama hakuwa amezaliwa kabisa wakati wazazi wake walipo badili dini na kuwa Waislam. Jambo hili linaendana na yeye kuwa mtoto wakati ndoa yake na Muhammad ilipokamilishwa kwa tendo la unyumba.
2. Sahih Muslim 817-875 BK, 261 BH
Mkusanyiko huu unachukuliwa kuwa wa pili wenye kuaminika zaidi miongoni mwa Hadithi.
2a. "(3309) A’isha (Allah na apendezwe naye) aliripoti: Mjumbe wa Allah (amani na iwe juu yake) alinioa nilipokuwa na miaka sita, na niliingizwa nyumbani mwake nikiwa na miaka tisa. (A’isha) Aliendelea kusema: Tulikwenda Madina na nilishikwa na homa kwa muda wa mwezi mmoja, na nywele zangu zilianguka hadi kwenye ndewe (masikioni). Umm Ruman (mama yangu) alikuja kwangu na wakati huo nilikuwa kwenye bembea pamoja na wenzangu ninaocheza nao. Mama aliniita kwa sauti na nilikwenda kwake na sikujua kwa nini aliniita. Alinishika mkono na kunipeleka mlangoni, na nilikuwa ninasema: Ha, ha (kana kwamba nilikuwa natweta kwa mshangao), mpaka msukosuko wa moyo ulipomalizika. Alinipeleka kwenye nyumba ambako walikuwa wamekusanyika wanawake wa the Ansar. Walinibariki na kunitakia bahati njema na kusema: Uwe na sehemu katika mambo mazuri. Mama alinikabidhi kwao. Waliniosha kichwa changu na kuniremba na hapakuwa na kitu kilichonitisha. Mjumbe wa Allah (amani na iwe juu yake) alikuja pale asubuhi, na nilikabidhiwa kwake." Sahih Muslim juzuu ya 2 kitabu cha 8 sura ya 548 na.3309, uk.715-716.
2b. "(3310) A’isha (Allah na apendezwe naye) aliripoti: Mtume wa Allah (amani na iwe juu yake) alinioa nilipokuwa na miaka sita, na niliingizwa kwenye nyumba yake nilipokuwa na miaka tisa."
(3311) A’isha (Allah na apendezwe naye) aliripoti kuwa Mtume wa Allah (amani na iwe juu yake) alimuoa alipokuwa na miaka saba, na alipelekwa kwenye nyumba yake (Mtume) kama bibi arusi alipokuwa na miaka tisa, na hapa midoli (wanasesere) yalikuwa pamoja naye: na (Nabii Mtakatifu) alipokufa ‘Aisha alikuwa na miaka kumi na nane." Sahih Muslim juzuu ya 2 kitabu cha 8 sura ya 548 na.3310, 3311, uk.716.
2c. "(5981) A’isha aliripoti kuwa alizoea kuchezea midoli mbele ya Mjumbe wa Allah (amani na iwe juu yake) na wenzake aliokuwa akicheza nao walipokuja (nyumbani) kwake waliondoka kwa sababu walimwonea aibu Mjumbe wa Allah (amani na iwe juu yake), lakini Mjumbe wa Allah (amani na iwe juu yake) aliwatuma kwake (A’isha).
2d. (5982) Hadithi hii imesimuliwa kwa mamlaka ya Hisham ikiwa na mlolongo ule ule wa waenezaji huku ikiwa na utofauti kidogo wa maneno." Sahih Muslim juzuu ya 4 kitabu cha 29 sura ya 1005 na.5981-5982, uk.1299.
3. Sunan Abu Dawud 817-888/9 BK, 275 BH
3a. "(2116) A’isha alisema: Mtume wa Allah (amani na iwe juu yake) alinioa nilipokuwa na miaka saba. Msimuliaji Sulaiman alisema: Au miaks sita. Mtume alifanya nami tendo la unyumba nilipokuwa na miaka tisa." Sunan Abu Dawudjuzuu ya 2 kitabu cha 5 sura ya 700 na.2116, uk.569.
3b. "(4913) A’isha alisema: Nilizoea kuchzea midoli. Nyakati zingine Mtume wa Allah (amani na iwe juu yake) aliniingilia wakati wasichana walikuwa pamoja nami. Alipoingia (ndani ya nyumba) walitoka nje, na alipotoka nje waliingia ndani."Sunan Abu Dawud juzuu ya 3 kitabu cha 36 sura ya 1769 na.4913, uk.1373.
Angalia kwa ungalifu. Hii haimaanishi kuwa Muhammad alifanya tendo la ndoa na A’isha wakati wenzake aliokuwa akicheza nao wakiangalia. Badala yake inamaanisha kuwa wenzake walicheza naye, na walienda nje wakati Muhammad alipokuja, na walirudi baada ya Muhammad kuondoka.
3c. "(4915) A’isha alisema: Mtume wa Allah (amani na iwe juu yake) alinioa nilipokuwa na miaka saba au sita. Tulipokuja Madina, baadhi ya wanawake walikuja. Kwa mujibu wa maelezo ya Bishr: Umm Ruman alikuja kwangu nilipokuwa nabembea. Walinichukua, walinitayarisha na kunipamba. Baada ya hapo nilipelekwa kwa Mtume wa Allah (amani na iwe juu yake), na alinichukua na kuanza kuishi nami kinyumba nilipokuwa na miaka tisa. (Umm) alinivutia mlangoni na niliangua kicheko.
Abu Dawud alisema: Hii ndio kusema: Nilipata siku za mwezi, na nililetwa kwenye nyumba, na kulikuwa na wanawake kadhaa wa Ansari (Wasaidizi) ndani yake. Walisema: Kwa bahati nzuri na baraka. Masimulizi ya baadhi yao yamejumuishwa na mengine. Sunan Abu Dawud juzuu ya 3 kitabu cha 36 sura ya 1770 na.4915, uk.1374.
3d. (5916) [kosa la uchapaji, namba sahihi ni 4916]. Masimulizi yaliyotajwa hapo juu yalienezwa pia na Abu Usamah kwa namna kama hii hii kupitia mlolongo wa wasimulizi tofauti. Maelezo haya yanasema: ‘Kwa bahati nzuri.’ (Umm Ruman) alinikabidhi kwao. Waliniosha kichwa changu na kunivisha upya. Hakuna mtu aliyekuja kwangu mara moja isipokuwa Mtume wa Allah (amani na iwe juu yake) mchana wa kabla ya saa sita. Hivyo walinikabidhi kwake. Sunan Abu Dawudjuzuu ya 3 kitabu cha 36 sura ya 1770 na.4916, uk.1374.
3e. (4917) A’isha alisema: Tulipokuja Madina, wanawake walikuja kwangu wakati nilipokuwa nacheza kwenye bembea, na nywele zangu zilifika kwenye masikio. Waliniletea, wakaniandaa na kunipamba. Kisha wakanipeleka kwa Mtume wa Allah (amani na iwe juu yake) na alinichukua na kuishi nami kinyumba, nilipokuwa na umri wa miaka tisa. Sunan Abu Dawud juzuu ya 3 kitabu cha 36 sura ya 1770 na.4917, uk.1374.
3f. (4918) Masimulizi yaliyoelezwa hapo juu yalienezwa pia na Hisham b. ‘Urwah kupitia kwenye mlolongo wa asimlizi tofauti. Maelezo haya yanasema pia: Nilikuwa nabembea na nilikuwa na marafiki zangu. Walinichukua na kunipeleka kwenye nyumba; kulikuwa na wanawake kadhaa wa Ansar (Wasaidizi). Walisema: Kwa bahati njema na baraka. Sunan Abu Dawud juzuu ya 3 kitabu cha 36 sura ya 1770 na.4918, uk.1374.
3g. (4919) A’isha alisema: Tulifika Madina na kuishi na Banu al-Harith b. al-Khazraj. Alisema: Naapa kwa Allah, nilikuwa nabembea kati ya mitende miwili. Kisha mama yangu alikuja, na aliniambia nishuke chini; na nywele zangu zilifika kwenye masikio. Kisha muenezaji anasmulia masimulizi yaliyobaki." Sunan Abu Dawud juzuu ya 3 kitabu cha 36 sura ya 1770 na.4915-4919, uk.1374.
Hitimisho kuhusu Abu Dawud: nukuu na nukuu zinazopinga nukuu 7 zinathibitisha kuwa A’isha alikuwa na miaka tisa.
USIKOSE SEHEMU YA PILI

JE! WAJUA KWANINI NENO USIOGOPE LIMETAJWA MARA 365 KATIKA BIBLIA TAKATIFU?

Image may contain: 1 person, text and outdoor


Ipo sababu kubwa tunapo sema kuwa, Biblia ni Neno la Mungu, na huwa hatubahatishi. Biblia imekamilika na haina shaka ndani yake bali ni mwongozo thabiti kwa wanao taka kwenda kuishi na Mungu Mkuu, yaani Yesu Kristo.
Mwaka una siku 365 na katika kila siku, Yesu Mungu Mkuu (Tito 2:13) anakwambia usiogope, maana yupo pamoja nawe.
Isaya Mlango 43: 1 Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, USIOGOPE, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.
Yesu Mungu Mkuu yupo mahali pote na kwa wakati wote "omnipresent" na hii sifa ni ya Mungu pekee na si ya kibinadamu. ( Mathayo 18:20 ) “Kwa kuwa walipo wawili watatu, wamekusanyika kwa jina langu, mimi nipo papo hapo katikati yao”. Mwenye uwezo wa kukaa mahali pote ni Mungu.
Zaburi Mlango 23: 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
Mathayo : Mlango 10: 28 Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.
Leo nawakumbusha tu kuwa, "USIOGOPE YESU MUNGU MKUU YUPO PAMOJA NAWE"
Pokea ulinzi wa Yesu na USIOGOPE TENA MAANA YESU YUPO PAMOJA NAWE.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

SHETANI ANASEMA KWENYE QURAN

Image may contain: meme and text




Surah Al Hijr 39. Shetani akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
Kwenye Surat Al Hijr, tumesoma kuwa Shetani ndie anazungumza katika hiyo aya ya 39. Kumbe basi, Shetani ni msemaji ndani ya Qurani.
MSIBA MZITO HUU KWA MUHAMMADANS

NENO "MUNGU" KWA KIARABU NI "ILAHA"




USHAHIDI UPO NDANI YA QURAN NA AYA ALIITEREMSHA ALLAH MWEYEWE.
Shahada: LA ILAHA ILLALLAH Muhammadur Rasulullah, Quran 3:18 na soma hapa pia (Sahih Al-Bukhari, Volume 4, Book 56, Number 725)
Hakuna Mungu ila Allah na Muhammad ni Mtume wa Allah. Hii ni Shahada wanayo sema Waislam au mtu anaye taka kuwa Muislam.
Kwasababu Waislam ni wabishi, basi leo nawawekea maana ya hiyo SHAHADA neno kwa neno:
Maneno hayo manne "lâ ilâha illâ allâh" yana maanisha hivi:
:
lâ = HAKUNA, no, not, none, neither
ilâha = MUNGU, a god, deity, object of worship
illâ = ISIPOKUWA but, except (illâ is a contraction of in-lâ, literally if not)
allâh = ALLAH, allâh
Kama tulivyo soma hapo juu maana ya hayo maneno Manne. Utangundua kuwa Neno ILAHA maana yake ni MUNGU na Neno ALLAH halina Tafsir na kubakia ALLAH (Thibitisha kupitia Al Tafsir Kitengo cha Tafsir cha Serikali ya Saudi Arabia/ http://www.altafsir.com/).
Kumbuka Allah hana wa kufananishwa na au linganishwa. Hivyo Kumfananisha Allah na Mwenyezi Mungu wa Wakristo ambaye ni Yesu au mungu Buddah, au mungu wa Rasta Fari au na mungu wa Wabantu ni KUKUFUR. Allah yeye kasema hana wa kufananishwa wala linganishwa. Kumbe basi Allah sio Mwenyezi Mungu.
NARUDIA TENA, TAFSIR YA NENO:
ILAHA ==> MUNGU
ALLAH ==> ALLAH
Hakuma wa kubisah sasa kuwa Allah sio Mungu.
LEO KWA MARA NYINGINE TENA TUMEJIFUNZA KUWA
ALLAH SIO MUNGU.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo

ASILI MBILI YA YESU KRISTO “MUNGU NA BINADAMU”

Image may contain: one or more people and text


"DUAL NATURE OF JESUS CHRIST"
Tokea Dunia ianze, hapajawai toke Mtu yeyote alieishi kama Yesu Kristo. Yesu ni mtu wa maana sana ambaye ni Mwokozi, Mungu katika Mwili “Emanueli” (Isaya 9:6). Yesu sio Nusu Mungu na Nusu Binadamu kama watu na au imani nyingi zinavyo sema. Yesu yeye ni Mungu na ni Binadamu kwa wakati mmoja. Kwa maneno mengine, Yesu alikuwa na asili Mbili tofauti ambazo ni Mungu na Binadamu kwa wakati mmoja. "incarnation"
Biblia inasema kuwa, Yesu ni “Neno” ambaye ni Mungu na alikuwa kwa Mungu na akafanywa kuwa Mwili na kuishi nasi, soma Yohana 1:1 na 14. Hii inamaanisha kuwa, mtu huyu mmoja ambaye ni Yesu alikuwa ana asili mbili za Mungu na Binadamu.
Hii asili ya Mungu haikubadilika pale ambapo “NENO” lilipo kuwa Mwili (Yohana 1:1, 14). Badala yake, Neno liliunga ubinadamu (Wakolosai 2:9). Hivyo basi, Umungu wa Yesu Kristo haukuharibika na au badirika. Zaidi ya hapo, Yesu hakuwa mtu tu ambaye alikuwa na Mungu ndani yake au Mtu aliye fanya kazi ya Mungu pekee, la hasha, Yesu ni Mungu katika Mwili na ni sehemu ya Pili katika Utatu Mtakatifu. Biblia inatuambia katika Waebrania 1 aya ya 3 kuwa: Mwana ni mng’ao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi Yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno Lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko mbinguni. Hivyo basi, asilia hizi mbili za Yesu Kristo haziwezi kuchanganywa (Eutychianism), vile vile haziwezi kuwa pamoja na kuwa Mungu-Mtu (Monophysitism). Hizi asili mbili ni tofauti na zinajitemea na wakati huohuo ni moja katika Yesu (person of Jesus). Huu muungano unaitwa Hypostatic Union.
Jedwari lifuatalo litakusaidia uone hizi asili mbili za Yesu Kristo:
*******MUNGU-BINADAMU*******
1. Yesu anaabudiwa (Matayo. 2:2, 11; 14:33)
2. Yesu anamwabudu Mungu Baba (Yohana 17)
1. Yesu anaitwa Mungu (Yohana 20:28; Waebrania 1:8)
2. Yesu anaitwa Mtu/Binadamu (Marko 15:39; Yohana 19:5)
1. Yesu aliitwa Mwana wa Mungu (Marko 1:1)
2. Yesu aliitwa Mwana wa Adam (Yohana 9:35-37)
1. Anaombwa/prayed(Matendo ya Mitume7:59)
2. Anamwomba Mungu Baba (Yohona 17)
1. Yesu hana dhambi/sinless (1 Petro. 2:22; Waebrania 4:15)
2. Yesu alijaribiwa (Matayo. 4:1)
1. Yesu anafahamu kila kitu (Yohana 21:17)
2. Yesu alikuwa na Hekima (Luka 2:52)
1. Yesu anatoa uzima wa milele (Yohana 10:28)
2. Yesu Alikufa (Rom. 5:8)
1. Adhama zote za Mungu zipo ndani ya Yesu (Wakolosai 2:9)
2. Alikuwa na Mwili na Mifupa (Luka 24:39)
USHAHIDI ZAIDI WA ASILI MBILI YA YESU
Mafundisho ya muungano wa Hypostatic ni ya “communication idiomatum” (Ni maneno ya Kilatini “Communication of properties”). Haya ni mafundisho ya adhama mbili za Yesu Kristo za Mungu na Binadamu zote zipo ndani ya Yesu Mtu “person of Jesus”. Hii inamaanisha kuwa, binadamu Yesu alikuwa na haki ya kusema kuwa “Alikuwa na utukufu na Baba Mungu kabla ya dunia kuumbwa soma Yohana 17:5), vile ile kudai kuwa alitoka Mbinguni (Yohana 3:13), na kudai kuwa alikuwa kila mahalai “omnipresence (Matayo 28:20). Haya madai yote ya Yesu ni adhama za Mungu na kuwa yeye Yesu alikuwanayo.
Moja ya Makosa makubwa sana yanayo fanywa na wasio Wakristo ni kushindwa kwao kuelewa kuwa Yesu alikuwa na ASILIA MBILI. Kwa mfano, Mashahidi wa Yehova wao wanamwangali Yesu kama Binadamu na kupuuza adhama zake za Umungu. Mara zote wao hutumia zile aya ambazo zinakiri Ubinadamu wa Yesu na kuzipambanisha na aya ambazo zinasema kuwa Yesu ni Mungu. Kwa upande mwingine, Masayantisti wa Kikristo wao hufanya kinyume chake. Wao wana angalia zaidi upande wa Yesu ni Mungu na kusahau kuwa, Yesu alikuwa Binadamu vile vile.
Ili kumwelewa Yesu vyema, basi kila mafundisho ambayo yanamuhusisha Yesu, hayana budi kuzumgumzia Yesu kama Mungu na Yesu kama Binadamu. Hizo asilia Mbili ni zake. Kumbe ndio maana Yesu katika Luka 2:52 inasema: Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu. Na wakati huo huo alikuwa kila kitu “omniscient” Soma Yohana 21:17. Yesu ni Neno la Mungu aliye kuwa Mwili/Binadamu (Yohana 1:1, 14).
Zaidi ya hapo, Biblia inamhusu Yesu (Yohana 5:39. Mitume wote walimtabiri Yesu (Matendo ya Mitume 10:43). Mungu Baba anatoa ushahidi kuhusu Yesu, Soma Yohana 5:37; 8:18. Roho Mtakatifu naye anato Ushahidi kuhusu Yesu, Soma Yohana 15:26. Kazi zake Yesu nazo zinashuhudia kuhusu Yesu Soma Yohana 5:36; 10:25. Makundi ya watu nayo yanashuhudia kuhusu Yesu, Soma Yohana 12:17. NA YESU anajishuhudia mwenyewe Soma Yohana 14:6 ; 18:6.
Kuna aya nyingine nyingi ambazo zinamshuhudia Yesu kuwa ni Mungu nazo ni
Yohana 10:30-33; 20:28; Wakolosai. 2:9; Wafilipi. 2:5-8;
Waebrania 1:6-8; na 2 Petro. 1:1.
1 Timoteo 2:5 inasema , " Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani, mwanadamu Kristo Yesu, 6. aliyejitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wanadamu wote, jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake " Hivi sasa, kuna Mtu Mbinguni ambaye yupo katika kiti cha Enzi. Yeye ni Mpatanishi wetu kwa Mungu Baba (1 Yohana 2:1). Ni Mwokozi wetu (Tito 2:13). Ni Bwana wetu (Warumi 10:9-10) Huyo Mtu anaitwa YESU.
Hakika Yesu Ni Mungu.
Kwa Maswali zaidi wasiliana nasi katika
maxshimbaministries@gmail.com
Imeletwa kwenu na Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Kwa Max Shimba Ministries Org.
@2015, April.

YESU KWA KIARABU NI YASU NA SIO ISSA

Image may contain: text

Katika somo letu hili tutajifunza kuhusu jina sahihi la Yesu/Yashua na tafsiri yake katika Kiarabu. Je, Isa ni jina la Yesu wa Bibliaau tafsiri sahihi ya Yesu/Yashua?
Jibu sahihi la kihistoria na la wataalam wa kutafsiri litatupa ukweli halisi wa Jina la Yesu na kwanini alipewa Jina hilo katika " sherehe ya kumtaja " (Luka 2:21). Jina ambalo aliitwa na Mama yake, Baba yake wa Kambo, Ndugu zake na jamaa wengine, majirani zake , marafiki zake na wanafunzi wake wakati wa maisha yake duniani. Hakuna kutokuelewana kuhusu ukweli kwamba jina la Yeshua halikuwa la Kiarabu bali la Kiyahudi na Yesu/Yeshua mwenyewe aliishi katika Israeli, na alizaliwa katika familia ya Wayahudi wacha Mungu.
Jina la Yesu bila ya shaka yeyote ile ni la Kiyahudi. (Maana yake ni “kweli”). Tafsir ya jina la Yeshua Kiebrania katika Kiingereza itakuwa ni Jesus.
Jina la Yesu halikuchaguliwa kiholela na wazazi wake, lakini yeye alipata jina lake moja kwa moja kutoka kwa Mungu (Mathayo 1:21 , Luka 1:31) kwa sababu ya maana ya jina lake na nani alilileta, basi leo hii tunaelewa madhumuni ya Yesu kuzaliwa na kuja hapa duniani (Mathayo 1:21 ).
Katika utamaduni na jadi ya Kiarabu. Jina la Yesu ni Yasu na si Isa kama ilivyo andikwa kwenye Koran ya Kiislam. Na hata leo, jina la Yasu linatumiwa na zaidi ya 99.99% ya Wakristo wote wa Kiarabu. Tembea katika kanisa lolote la Kiarabu huto sikia wanatumia jina la Isa, Sikiliza matangazo ya Wakristo wa Kiarabu katika Radio na Televisheni (za Kiarabu) huto sikiwa Mkristo anatumia jina la Isa, bali wanatumia jina la Yasu. Matangazo yote ya Kikristo katika Uarabu wanatumia jina la Yasu. Kamwe huto ona jina la Isa kama lilivyo kwenye Koran ya Waislamu.
Katika jadi ya Kiarabu na utoaji wa tafsiri wa jina, jina sahihi la Kiebrania (Yeshua) ni Yasu katika Kiarabu. Kila uchaguzi wa tafsiri ya jina la kigeni katika lugha tofauti ni uvumbuzi wa binadamu.
Kiisimu ipo wazi jinsi jina la Yeshua Kiebrania lilivyo tafsiriwa na kuwa Yesu Kiswahili na Jesus Kiingereza:
Yeshua '(Kiebrania) -> Ιησους (Kiyunani) -> Yesu (Kilatini) -> Jesus (Kiingereza) -> Yesu (Kiswahili).
Mpito muhimu ni kutoka Kiyahudi kwenda Kigiriki. Hatua hii ilifanyika miaka 200 kabla ya Yesu kuzaliwa. Watafsiri wa Septuaginta (LXX), classical Kigiriki tafsiri ya maandiko ya Kiyahudi, kutokaa Yeshua Kiebrania jina kama Ιησους katika Kigiriki. Injili ziliandikwa katika lugha ya Kigiriki ilitumia utamaduni huu wa kutafsir kwa muda mrefu.
Kwasababu Kiyahudi na Kiarabu ni lugha mbili za Kisemiti, na zina uhusiano wa karibu, kuna baadhi ya sheria maalumu ambayo sauti/maneno/maandishi ya Kiebrania yanahusiana na ambayo sauti/maneno katika Kiarabu. Hasa, Neno la Kiebrania Shin mara kwa mara linatumika kama Dhambi katika Kiarabu, kwa mfano neno la Kiyahudi la amani, shalom ni sambamba na neno “salam” la Kiarabu. Kulingana na sheria za lugha na mahusiano kati ya Kiyahudi na Kiarabu, Yasu 'ni sahihi kwa Kiarabu na kwa Kiebrania ni Yeshua:
Yeshua '= Yod + + Shin Waw +' Ain
Yasu '= + Ya + Sin Waw +' Ain
Tena, katika lugha sahihi, jina la Yasu ni Kiarabu sawa na Yeshua Kiebrania. Hivyo, katika utamaduni na jadi ya Kiarabu jina la Yasu ndilo sahihi na pekee kutokana na kiisimu. Mpito kutoka Yeshua kwa Yasu inafuata sheria ya kawaida ya mabadiliko fonetiki kutoka Kiyahudi na Kiarabu. Yasu ni jina la Kiarabu la Yesu. Kinyume chake, Yasu ndio jina lenye asili ya Yeshua.
Early Hebrew (long form): Yehoshua' = Yod + He + Shin + Waw + 'Ain
Later Hebrew (short form): Yeshua' = Yod + Shin + Waw + 'Ain
Arabic (Christian): Yasu' = Ya + Sin + Waw + 'Ain
Arabic (Muslim): 'Isa = 'Ain + Ya + Sin + Ya
“Ya” na “Waw” ni maneno dhaifu, katika lugha ya Kiarabu, hufundisha kwamba mtu anaweza kurejea katika maneno mengine kama kuchukua juu ya aina mbalimbali (declension, inflection). Hivyo, mtu anaweza kuona kwamba fomula ya Kiislamu 'Isa kimsingi ni ya bandia/kutungwa na binadamu (inversion) (pamoja na mabadiliko ya Waw ili Ya) kwa Mkristo wa Kiarabu jina la Yesu ni Yasu na si Isa kama ilivyo andikwa kwenye Koran ya Kiislamu.
Nategemea leo umejifunza tofauti iliyopo kati ya Jina la Yesu-Kiswahili, Yasu-Kiarabu na Yeshua-Kiebrani.
Jina la Yesu Libarikiwe Sana
Katika Huduma yake
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW