Saturday, November 25, 2017

THE CHURCH BURNT IN KAGERA TANZANIA




                                       The building  of T.M.R.C is down after set on fire

The building  of the Tanzania Missionary Revival Church (T.M.R.C) at Kyabitembe Parish, Bukoba Urban Distict, Kagera region in Tanzania, at dawn of 12/3/2015 was set on fire by petrol by un identified people.

Host Pastor Emmanuel John Mwesiga said when the incident occurred no one was in the church. He estimated the total damage to tsh.40M /- (U$ 23,000). The same was reported at the Regional Cenral Police at Bukoba and filed no BUK/RB/2600/2015 of 13/3/2015.

The Kagera Region Police Commander, Henry Mwaibambe said, the police have arrested some suspects, although, he was not ready to disclose neither their names nor their number, and insisted to carry on with more investigation.

So far more than 170 adherents of the Tanzania Missionary Revival Church, use temporary tents during conducting services.

Attacks against Christians are increasing in Tanzania including Kagera region, despite the efforts of the government to control them.  

On Thursday, Oct. 9,2014 unknown attackers killed a Christian man by machete the late Dioniz Ng'wandu, 31, a secondary school teacher and  injured anotherThemistores, 25,  in the same district of  Bukoba in northwest Tanzania.  The two men were at overnight prayer-meeting at the Busimbe Parish of the Pentecostal Assemblies of God-P.A.G. 

 Bukoba is reported to be a Muslim-dominated town of about 100,000 situated on the shore of Lake Victoria bordering Kigoma, which also has a local reputation as a Centre for Islamist extremism.
So far some religious leaders and lay Christians have been killed, while others have been attacked by extremist Muslims wielding acid. Some of the perpetrators have been arrested and charged, yet their cases continue in courts.

THREE MEN SENTENCED LIFE IMPRISONMENT FOR CHURCHES TORCHING IN BUKOBA TANZANIA


The Resident Magistrate of Bukoba Kagera region in Tanzania, Victor Biambo, has sentenced three men to life imprisonment for the offenses of conspiracy 

to burn various churches in the region.

 The Government Prosecutor, Emmanuel Manyere, said, despite the verdict, the three men still face with another accusation of cutting the throat with the killing of 16 people which continues in the Supreme Court in the Bukoba region.

Manyere said the three men, namely, Allyu Dauda,​​Rashid Mzee and Ngesela Keya appeared in Resident Magistrate's Court in front of Magistrate of Bukoba, Victor Biambo. He said the accused unanimously found guilty of conspiracy to burn 16 churches of various denominations in the region.

Magistrate Bigambo satisfied with the evidence from the complainants and to imprisonment for seven years in jail for all three of the offense of conspiracy and life imprisonment for the crime of burning churches.

Meanwhile, the Kagera Region PoliceCommander, Augustine Ollomi praised the court to exercise justice in this case as well as urging the country to continue to cooperate with the police to put an end to such practices.

Despite the judgment in this case the number 67,still three men are charged with the murder of 20people in various locations in the region going to the Supreme Court, Bukoba region.

Monday, September 18, 2017

Salafist cleric says fathers can marry off their newborn daughters



Last week, Egyptian Salafist preacher Muftah Mohammad Maarouf, also known as "Abu Yahya," stated that it's absolutely okay for a newborn girl to be married off by her father - even at such a young age. 
Yes, you heard that right. 
The statement was made during a live TV interview on a show that was discussing a controversial draft law aimed at lowering marital age in Egypt to 16. 
According to the preacher, if no harm will be done to a female, then nothing should prevent her from getting married, regardless of her age. 
"I am not the one saying this, in Islamic Sharia there is no set age for marriage when it comes to females," Maarouf said. 
When the show's presenter pressed on with: "If this is true, then any age would be fine for marriage, 2 months, 1 year," the preacher shockingly responded: 
"Even if she's just 1-day-old." 

People on social media were just not having it

A video of the interview that saw "Abu Yahya" drop his statement went viral on social media shortly after the show aired, sparking outrage. 
Here's a little of what people had to say: 

Many were understandably outraged

"Our religion is clear and straightforward... even a child would denounce such statements... these kinds of 'preachers' only represent themselves and have nothing to do with true Islam." 

"Regression, ignorance and stupidity"

Many raised this point

"He's a liar. Prophet Mohammad said that the consent of a female and her guardian are two conditions that any union must be based on. How will an infant or a young girl consent to a marriage when she doesn't even understand what it means?" 

Some were left speechless

"There are no more words to be said."  

"These fatwas from so called religious figures are defaming Islam"

Others felt that action must be taken against this type of "preaching"

"I am wondering, aren't there laws to punish such germs (preachers)? One that could prevent them from using media outlets to spread their agendas, one that would stop them from preaching in mosques?" 

Lowering marital age for females still up for debate in Egypt

While Abu Yahya's statements are shocking, they're not quite surprising given that the preacher previously voiced out his support for a draft law aimed at lowering marital age for females in Egypt from the current 18 to 16. 
Proposed by Egyptian Ahmed Samih, an independent MP representing the Giza district of Al-Talbiya, the controversial draft law has sparked controversy and debate across the country in recent months. 
Since it was proposed, Samih's legislation has faced intense backlash from fellow MPs, women's rights activists and several others who have labeled it 'regressive.' 
Egypt's government has yet to vote on the draft law, but with a number of MPs who have already taken a stand against it, it seems unlikely for it to pass. 

Sunday, September 10, 2017

JE, UNAYO NEEMA YA YESU KRISTO, MUNGU MKUU?

Image may contain: food
Nini basi maana ya neema? Watu wengi wamekuwa wakiimba ,”Neema, neema imefunuliwa” na kukariri na kuisema Neema ya Bwana (2 WAKORINTHO 13:14) kama Kasuku huku hawajui wayasemayo. Nini basi maana ya neema?
Neema, ni upendeleo wa kuchaguliwa, bila kustahili kutokana na matendo yoyote aliyoyafanya mtu au sifa aliyonayo mtu.
Neema pia, ni uwezo wa kushinda katika tabia na utumishi wa Mungu sawasawa na mapenzi yake, tunaopewa na Mungu bila gharama yoyote au nguvuzetu au kufanyia kazi yoyote.
1. Upendeleo wa kuchaguliwa bila kustahili- Kutokana na matendo yake, hakuna mwanadamu yeyote mwenye haki mbele za Mungu (WARUMI 3:20). Tangu kabisa amekuwa akimhuzunisha Mungu (MWANZO 6:5-7). Wakati wa Nuhu, watu waliangamizwa kwa Gharika. Wakati wa Musa, Mungu alitaka pia kufuta kabisa kizazi cha Wausraeli na kubaki na Musa tu kama siyo maombi ya Musa (HESABU 14:11-20). Wakati wote, wanadamu wote wamepotoka na kuoza (WARUMI 3:12). Ni Yesu peke yake tu ambaye siku zote alifanya yanayompendeza Mungu (YOHANA8:29).Alijaribiwa sawasawa na sisi lakini hakutenda dhambi (WAEBRANIA 4:14-15). Yesu huyu anayempendeza Mungu ndiye aliyekufa msalabani na Baraba aliyekuwa mhalifu mkubwa akafunguliwa. Kama Baraba alivyofunguliwa pamoja na ukosaji wake, kila mwanadamu amefunguliwa, akiamini tu. Mbele za Mungu kila mtu amepimwa na kuonekana amepungua (DANIELI 5:27). Sasa kwa kuamini tu kwamba Yesu alizichukua dhambi zetu pale msalabani, sisi tunaokolewa. Watu wengi hawaokolewi kwa sababu hawajui tunaokolewa kwa neema tu kwa njia ya imani peke yake (WAEFESO 2:5). Kazi aliyoifanya Yesu msalabani imetupa kuirithi mbingu aliyokwenda bila sisi kuifanya. Ni kama ambavyo bondia anavyopigana ulingoni kwa shida kubwa na kasha akishinda na kupewa mamilioni ya fedha, mke wake aliyebaki nyumbani bila kupigana naye atakuwa milionea. Hii ndiyo neema.
2. Uwezo wa kushinda bila kutumia nguvu zetu- Neema ni uwezo wa kushinda dhambi na kumtumikia Mungu apendavyo. Neema ndiyo inayotufundisha (inayotuwezesha) kukataa ubaya na tama za kidunia na kuishi kwa kiasi na haki na utakatifu (TITO 2:11-12; WAGALATIA 2:8). Maisha ya wokovu siyo ya kutumia nguvu zetu au kujitahidi. Uweza wa Mungu unatimilika kwetu katika udhaifu wetu yaani kutokuweza kwetu. Hatupaswi kujitumainia wenyewe katika kufanya lolote (2 WAKORINTHO 1:8-9).
Shalom,
Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

UNAYAJUA MADHARA YA KUANGALIA PICHA ZA UTUPU "PONOGRAFIA"? (SEHEMU YA SABA)


Madhara ya Kiroho unapo angalia ponografia:
Ponografia husababisha madhara mabaya ya kiroho. Inaweza kuwa kizuizi kikubwa kwa mtu anayetaka kuwa na uhusiano na Mungu.

Biblia huhusianisha hamu ya ngono na tamaa na ibada ya sanamu. (Wakolosai 3:5) Mtu anayetamani kitu huwa na hamu kubwa sana ya kukipata hivi kwamba kinakuwa jambo kuu maishani mwake kuliko vitu vingine vyote. Kwa kweli, wale ambao wamezoea ponografia hutanguliza tamaa zao za ngono badala ya Mungu. Kwa hiyo wanazifanya kuwa sanamu yao. Amri ya Mungu inasema: “Usiwe na miungu mingine ila mimi.”—Kutoka 20:3.
Ponografia huharibu mahusiano yenye upendo. Mtume Petro, ambaye alikuwa amefunga ndoa, aliwahimiza waume Wakristo wawaheshimu wake zao. Mungu hatasikiliza sala za mume anayekosa kufanya hivyo. (1 Petro 3:7) Je, mtu anayetazama picha chafu za wanawake faraghani anamheshimu mke wake? Mke angehisije akigundua? Na Mungu ambaye “ataleta hukumuni kila kazi” na ambaye “huzipima roho” angeonaje? (Mhubiri 12:14; Mithali 16:2) Je, mtu anayetazama ponografia anaweza kumtarajia Mungu asikilize sala zake?
Ponografia hukazia kutosheleza tamaa za mtu binafsi kwa vyovyote vile. Kwa hiyo, kutazama ponografia ni kukosa upendo. Hudhoofisha uwezo wa Mkristo wa kudumu akiwa safi kiadili na kuwa mwadilifu mbele za Mungu. “Haya ndiyo mapenzi ya Mungu,” akaandika mtume Paulo, “kwamba mjiepushe na uasherati; kwamba kila mmoja wenu apaswe kujua jinsi ya kupata umiliki wa chombo chake mwenyewe katika utakaso na heshima, si katika hamu yenye tamaa ya ngono . . . , kwamba yeyote asifikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake.”—1 Wathesalonike 4:3-7.
Ponografia huwatumia vibaya hasa wanawake na watoto. Huwavunjia heshima na pia huwashushia hadhi na kuwanyima haki zao. Yule anayetazama ponografia hushiriki na kuunga mkono matumizi hayo mabaya ya wanawake na watoto. ‘Hata mtu akijiona kuwa mwema kadiri gani,’ wasema watafiti Steven Hill na Nina Silver, ‘anapotazama au kukubali ponografia, anakuwa asiyejali au hata mwenye chuki kuelekea mtu anayedai eti anamjali.’
USIKOSE SEHEMU YA NANE
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi Wetu

NINI MAANA YA KUUMBWA KWA MFANO WA MUNGU?

Image may contain: cloud, sky, ocean, text, nature and outdoor
Mungu ni Roho. Je wewe ni nani?
Katika somo hili la uumbaji wa binadamu, nitajibu hoja na maswali mbali mbali ambayo yanaulizwa zaidi na waumini wa dini ya Kiislam katika Mihadhara mbalimbali ya kidini, kupitia wahadhiri wao wa Dini, Waislamu wamekuwa wakipinga kuwa Mungu hana Mfano kama ilivyo andikwa katika kitabu cha Mwanzo Sura ya Kwanza na aya ya 26.
Ndugu msomaji, nakusihi ufuatilie somo hili kwa makini ili ujue ukweli kuhusu kuumbwa kwa Binadamu kwa Mfano wa Mungu na nini maana yake:
Katika siku ya mwisho ya uumbaji, Mungu alisema, "Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu" (Mwanzo 1:26). Mungu alimuumba Mtu kutoka vumbi na akampa uhai kwa kumpulizia pumzi yake mwenyewe (Mwanzo 2:07). Binadamu ni kiumbe cha kipekee ambacho Mungu alikiumba na baada ya kukiumba, akatumia pumzi yake kukipa uhai, zaidi ya hapo, binadamu ni kiumbe pekee chenye Mwili, Roho na Nafsi.
Kuwa "mfano" wa Mungu maana yake, katika suala rahisi ni kwamba sisi hatufanani na Mungu katika maana ya mwili na sura na/au mwonekano wetu, bali sisi tunafanana na Mungu katika Roho. Maandiko yanasema kwamba "Mungu ni roho" (Yohana 4:24). Binadamu tuna Mwili, Roho, na Nafsi. Unaweza kuniuliza, ni kivipi ninaweza kuthibitisha hayo? Ngoja nikupe mfano mdogo. Mtu anapo kufa, huwa tunasema hivi: Huu ni Mwili wa Marehemu “Fulani”. Kwanini tunauita “MWILI WA MAREHEMU”…Fulani? Kwa kifupi ni kwamba, Yule ambaye alikuwa anaishi katika huo MWILI amesha ondoka na/au toka katika huo MWILI na kwenda sehemu nyingine. Kumbe basi Binadamu si Mwili, bali kuna zaidi ya MWILI.
Biblia inasema kuwa, Mungu alipo pulizia pumzi ya uhai ule udongo ambao aliuumba, huo udongo ukafanyika na ukawa kiumbe chenye uhai. Kumbe basi, kilicho fanya huo udongo kuwa kiumbe chenye uhai ni ile pumzi ambayo Mungu alipulizia ule udongo alio ufanya katika umbo la mtu. Hiyo pumzi ndio Roho ya Binadamu. Hiyo Roho ndio mfano halisi wa Mungu.
Sasa tuagalie zaidi maana ya Sura ya Mungu na inahusiana kivipi na sisi Wanadamu. Mtu ni tofauti na hafanani na Wanyama amboa hawana mamlaka juu ya vilivyo umbwa, nikimaanisha kuwa Binadamu alipewa Mamlaka katika kila kitu ambacho kipo hapa duniani (Mwanzo 1:28), na zaidi ya hapo, binadamu alikuwa na uwezo wa kuzungumza na Muumba wake, kitu ambacho Wanyama wote hawana.
Hebu, tumtazame Binadamu kiakili, kimaadili, na kijamii.
Kiakili, mtu ameumbwa kama wakala wa busara. Kwa maneno mengine, mtu anaweza kuchagua nini anataka kufanya kwa kutumia fikra yakinifu na/au pevu. Kwa kufanya hivyo, mtu ameonyesha uhuru wa akili ambayo Mungu anao. Mfano, mtu anapo tengeneza mashine, anapoandika kitabu, fanya mambo mbalimbali, huko ndiko kuna ashiria neno la kufanana na Mungu, maana Mungu aliumba vitu vyote na sasa binadamu anaonyesha ustadi wa akili pevu kwa kufanya mambo ya uvumbuzi katika sura ya Mungu.
Kimaadili, mtu aliumbwa kwa uadilifu na kutokuwa na hatia ya dhambi, huo ni mwaonekano wa utakatifu wa Mungu. Mungu akaona kila alichokifanya ( pamoja na uumbaji wa Mwanadamu) alikiita kuwa ni "kazi nzuri sana" (Mwanzo 1:31). Dhamiri zetu au "dira ya maadili yetu" ni alama ya awali ya hali tuliyo kuwa nayo. Binadamu tumetunga na kuandika sheria za kutuongoza na uovu, sifa na tabia nzuri , nk, hayo yote ni kuthibitisha ukweli kwamba sisi tulifanywa na/au umbwa katika mfano wa Mungu mwenyewe.
Kijamii, mtu aliumbwa kwa ajili ya ushirika na/au kushirikiana. Huu ni uthibitisho kuwa Mungu ni Utatu ambao ni asili ya upendo wake. Katika Bustani ya Edeni, Mtu alikuwa na uhusiano na Mungu (Mwanzo 3:08 ina maana ushirika na Mungu ), na Mungu alifanya mwanamke wa kwanza kwa sababu "si vema huyo mtu awe peke yake " (Mwanzo 2:18). Kila wakati mtu anapo oa, hufanya urafiki na huyo aliye muoa, huzaa watoto na kuwa na familia hayo yote ni kutuonyesha ukweli kwamba sisi ni tulifanywa katika mfano wa Mungu.
Sehemu ya kuumbwa kwa mfano wa Mungu ni kwamba Adam alikuwa na uwezo wa kufanya uchaguzi kwa huru. Adam alipewa haki ya kuchangua mema au mabaya, uhuru huo ni sehemu ya mfano wa Mungu.
Ndugu msomaji, nategemea leo umefahamu kidogo maana ya kuumbwa kwa mfano wa Mungu ni katika Roho na si Mwili au mwonekano wetu. Mungu ni Roho. Je wewe ni nani?
Katika Huduma yake
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

ROHO MTAKATIFU ROHO AWAFUFUAYE WATU WALIOKUFA KIROHO

Image may contain: cloud and text
Kurudi nyuma na kuacha wokovu kunaitwa pia kufa kiroho (Ufunuo 3:1;Waefeso 2:1). Kwa kila aliyerudi nyuma na kuacha wokovu, hii ni saa ya kuamka usingizini na kuanza upya (Warumi 13:11-12).
Lakini, je, inawezekana kuanza upya tena katika hali hii?
Ndiyo, kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Hii ni kazi yake nyingine. Roho Mtakatifu ndiye aliyemfufua Yesu, alipokufa
(Warumi 13:11).
Kwa jinsi hiyo hiyo, Roho Mtakatifu anaweza kutufufua kiroho na kutupa uhai tena wa kiroho (Waefeso 2:1,4-6). Mwambie Roho Mtakatifu kwamba unataka kufufuliwa kiroho, naye atafanya.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

JESUS IS GOD MALIK AL AMLAK

TRENDING NOW