Saturday, April 21, 2018

Roho Mtakatifu kwa Mujibu wa Biblia na Quran





JE ROHO MTAKATIFU NI NANI NDANI YA BIBLIA NA QURAN?
Vitabu vitakatifu vinatutaka kumpwekesha Mwenyezi Mungu, ya kwamba Yeye hana mshirika wala anayefanana naye. Tunasoma katika Quran;
“Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni mmoja tu, Mwenyezi Mungu tu ndiye anayestahiki kukusudiwa na viumbe Vyake (vyote kwa kumwabudu na kumwomba na kumtegemea), Hakuzaa wala hakuzaliwa, wala hana anayefanana naye hata mmoja” (Sura ya 112:1-3)
Mwenyezi Mungu naye anasema maneno hayo hayo ndani ya Biblia, kwamba.
“Sikia, Ee Israel; BWANA Mungu wetu, Bwana ndiye Mmoja” Torati 6:4
Dhana ya kuwa kuna Waungu watatu imepingwa kabisa kwa nguvu na vitabu vitakatifu, kama tunavyosoma katika Quran;
“Kwa hakika wamekufuru wale waliosema: Mwenyezi Mungu ni mmoja katika wale waungu watatu (yeye ndiye wa tatu wao), hali hakuna Mungu ila mwenyezi Mungu mmoja (tu peke yake). Na kama hawataacha yale wayasemayo, kwa yakini itawakamata—wale wanaoendelea na ukafiri miongoni mwao—adhabu iumizayo” (Sura ya 5:73)
“Enyi watu wa Kitabu! Msiruke mpiaka ya dini yenu, wala msiseme juu ya Mwenyezi Mungu ila kwa lililo kweli. Hakika Masihi Isa mwana wa Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, Na neno lake tu alilompelekea Maryamu, na ni roho iliyotoka kwake. Basi muaminini mwenyezi Mungu na Mitume yake, wala msiseme: Utatu. Wacheni (Itikadi hiyo) ni bora kwenu. Hakika mwenyezi Mungu ni mmoja tu. Amemeepukana na Kuwa na mtoto. Ni vyake Ni vyake vilivyomo Mbinguni na katika ardhi, na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi” (Sura ya 4:171)
Kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja na wapekee na kwamba hafananishwi na kitu chochote haina shaka kabisa ndani ya vitabu vitakatifu. Hoja ya msingi hapa itakuwa ni kuweza kuelewa huo upekee ni wa namna gani. Vitabu vyote vitakatIfu vinamaelezo mazuri kuhusu hali ya Mwenyezi Mungu. Kwa mfano tunaposoma katika 1Yohana 5:8 tunaona kuwa
“Kwa maana wako watuatu washuhudiao mbinguni, Baba na Neno, na Roho Mtakatifu na Watatu hawa ni Umoja”
Hapa tunaona kwamba kumbe Umoja katika habari ya Uungu hupatikana katika Watatu, yaani kwa maana nyingine, haupatikati umoja kwa Mungu mpaka paweta watatu.
Tunapochunguza vizuri maandiko matakatifu, tunaweza kugundua kwamba, dhana hii ya umoja katika utatu (wingi) inapatikana kwa wazi kabiza, kwa mfano. Wakati alipoumba mbingu na ardhi, tunaambiwa kwamba;
“Mungu (mmoja) akasema ‘Na tufanye (wingi) mtu kwa mfano wetu (wingi)” (Mwanzo 1:26)
Twaona kwa mujibu wa Aya hii kwamba Mungu anaongea katika hali ya umoja lakini kuna kiashiria kwamba yeye siyo mmoja kwa maana tunayojua sisi wanadamu, lakini ni mmoja katika hali yake yeye mwenyewe, yaani hali ya wingi. Na kwa mujibu ya 1Yohana 5:8, wingi huo ni wa Nafsi tatu.
Dhana hii iko wazi pia ndani ya Quran kuwa Mungu anaposema ni Mmoja, hana maana ya Umoja wa nafsi moja lakini ni zaidi ya nafsi moja, kwa mfano.
“Na hakika tulimuumba mtu, kutokana na udongo mkavu, kwa matope meusi yenye kufinyangwa” (Sura 15:26)
“Hatukuziumba mbingu na ardhi, na vilivyomo baina yake, ila kwa haki na kwa Muda uliowekwa…” (Sura ya 46:3)
Tamko hili ndani ya Quran linaonyesha wazi kwamba Mungu anazungumza katika hali ya wingi, nafsi zaidi ya moja. Wanazuoni wa Kiislamu wanatueleza kwamba, kauli hii ya Mwenyezi Mungu haina maana ya nafsi zaidi ya moja isipokuwa ni pale Mwenyezi Mungu anapozungumza kwa hali ya kujitukuza. Lakini uchunguzi zaidi ndani ya vitabu vitakatifu unaonyesha kuwa dhana hii haina msingi wowote, isipokuwa ni mafikara tu ya wanadamu.
Katiba Biblia takatifu tunaona kwamba, Wakati wa Uumbaji, neno linasema;
“Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa Maji…” Mwanzo 1:1
Kumbe kwa Mujibu wa Aya hii, Wakati wa Uumbaji, Mungu alikuwa pamoja na Roho yake. Je, huyu Roho wa Mungu ni nani?.
Tunaambiwa wakati wa Kuzaliwa kwa Nabii Isa (a.s) wakati Malaika Gabrieli (Jibril) alipokuwa kwa Maryamu, alisema.
“Roho Mtakatiafu atakujilia juu yako, na nguvu zake aliye juu zitakufunika kama kivuli…” (Luka 1:35)
Nabii Isa (Yesu) Mwenyewe alipoanza kazi yake alisema kuwa
“Roho wa Bwana yu Juu yangu…” (Luka 4:7)
Kwa Maandiko haya tunaona kwamba Kumbe, Mwenyezi Mungu, anaye Roho Mtakatifu wake, na Roho huyo, Mwenyezi Mungu humtuma kwa Manabii wake kama tunavyosoma;
“Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu, akapaza sauti kwa nguvu akasema…”
(Luka 1:41-42)
“Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii akisema:..” (Luka1:67)
“Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho Muda wa siku arobaini nyikani”(Luka 4:1)
“Naye Yesu alipokwisha kubatizwa, mara akapanda kutoka majini, na tazama, mbingu zikafunguka, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake” (Mathayo 3:16)
Roho Mtakatifu ni nafsi hai,  kwasababu, Mtu anaweza kufanya Ujeuri na Kushindana naye. Roho anatuombea, Roho mtakatifu anazungumza
“Bwana akasema Roho yangu haitashindana na Mwanadamu milele…” (Mwanzo 6:3)
“Lakini wakaasi, wakamhuzunisha Roho wake Mtakatifu…” (Isaya 63:10)
“Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye Mlitiwa Mhuri hata siku ya Mwisho” (Waefeso 4:30)
“Naye mtu yeyote atakayesema neno juu ya Mwana wa Adamu, atasamehewa, bali yeye atakaye neno neno juu ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa katika Ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao” (Mathayo 12:32)
Roho Mtakatifu wa Mungu anawaombea watu wa Mungu. Sifa ya kuomba siyo ya kitu kisichokuwa na uhai. Hii inamaana kwamba Roho Mtakatifu ni nafsi hai.
“Kadharika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo; lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamukwa” (Warumi 8:26)
Roho Mtakatifu huzungumza. Sifa hii ya kuzungumza ni sifa ya Nafsi hai, siyo kitu kisichokuea na uhai, au kama wengine wasemavyo kwamba ni nguvu tu.
“Roho akamwambia Filipo, sogea karibu na gari hili ukashikamane nalo” (Matendo 8:29)
“Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo” (Luka 2:25
“Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati uo huo mnachopaswa kusema” (Luka 12:12) (Msisitizo ni wangu katika aya hizi)
Wanazuoni wa Kiislamu wanapokutana na hoja ya Roho wa Mungu wanamnasibisha Roho wa Mungu na Mtume Muhammad, kwamfano wanaposoma katika Yohana 16:13
“Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa Kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote, kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na maneno yajayo atawapasha habari zake”
Aya hii Waislamu wanapoisoma, wanaona kuwa hapa katabiriwa Mtume Muhammad (s.a.w). Lakini, Tumekwisha kuona kuwa Roho Mtakatifu wa Mungu sifa zake ni kwamba.
Alikuwepo wakati wa Uumbaji (Mwanzo 1:1)
Alikuwepo toka wakati wa Nuhu (Mwanzo 6:3)
Alikuwepo wakati wa Musa Isaya (63:10)
Kazi yake ni Pamoja na kuwatia nguvu mitume na pia ni Mwombezi wetu.
Sifa hizi zinamtoa kabisa Muhammad kuwa Roho Mtakatifu, au Roho wa Mungu. Kamwe Muhammad hajaletwa ili awe mwombezi wetu, badalayake. Waumini ndio wanaamulishwa kumwombea Muhammad. Na kwa kweli Mwenyezi Mungu ndiye hasa mwombezi wa Muhammad.
“Hakika Mwenyezi Mungu na Malaika Wake humsalia Mtume; enyi mlioamini, msalieni (Mtume) na mwombeeni amani” (Sura 33:56)
Mwenyezi Mungu anamsalia mtume, na hivyo waumini nao wanaamrishwa wamsalie mtume. Siyo yeye awalalie au kuwaombea. Na ndiyo maana Mwislamu anapolitaja jina la Mtume lazima aishie na kuseama “Swala llhau aleyhi wa salaam”. Yaani Swala za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake pamoja na amani (Msisitizo ni wangu). Je Mwenyezi Mungu angewezaje kusali kwa Mtume, je asali kwa Mungu gani ikiwa yeye ni wa Pekee? Hivyo twaona kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja lakini siyo umoja huu tujuavyo sisi. Ni umoja wa Nafsi tatu, na ndiyo maana kwa habari ya kuwaombea watakatifu wa Mungu, nafsi moja yaweza kuomba kwa nafsi nyingine. (Tutaangalia kwa upana zaidi hoja hii ya kumnasibisha Muhammad na Roho mtakatifu mwishoni mwa somo hili)

Je Roho Mtakatifu ni nani ndani ya Quran?
Kama tulivyoona katika Biblia, Mwenyezi Mungu alimtia nguvu Nabii Isa kwa Roho Mtakatifu na alifanya miujiza mingi.
“Na hakika tulimpa Musa Kitabu, na tukawafuatisha mitume baada yake; na tukampa Isa mwana wa Maryam, hoja zilizo wazi wazi, na Tukamtia nguvu kwa Roho Takatifu. Kila alipowafikia mtume kwa yale yasiyopenda nafsi zenu, mlitakabari, kundi moja mkalikadhibisha, na kundi jingine mkaliua” (Sura ya 2:87)
“Atakaposema Mwenyezi Mungu: Ewe Isa Mwana wa Maryam! Kumbuka neema yangu juu yako na juu ya mama yako. Nilipokutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu utotoni na katika utu uzima, na nilivyokufundisha kitabu na hekima, na Taurati na Injil, na ulipotengeneza kwa udongo kama umbo la ndege kwa idhini yangu, kisha ukapulizia likawa ndege kwa idhini yangu, na ulipowaponyesha vipofu na wenye mbalanga kwa idhini yangu, na ulipowafufua wafu kwa idhini yangu, na nilipokukinga na wana wa Israeli ulipowafikia na hoja zilizo wazi…” (Sura ya 5:110)
Waislamu kwa kuepuka somo la utatu Mtakatifu katika Quran wanasema eti Roho Mtakatifu aliyekusudiwa katika aya hizi ni Malaika Jibril. Lakini wakiulizwa fundisho la kusema Roho Mtakatifu ni Jibril wanapata wapi ndani ya Quran, hawawezi kuwa na jibu. Ni dhana tu ya kumnasibisha Jibril na Roho Mtakatifu. Kuna aya mbili ndani ya Quran zinazotumiwa na Waalimu wa Kiislamu kudai kuwa Jibril ndiye Roho Mtakatifu. Na hapa tuzichunguze aya hizi.
“Sema: Anayemfanyia ushinde Jibril (kwa kuwa ndiye aliyemteremshia utume Nabii Muhammad asiwapelekee Mayahudi) (ni bure, hana kosa Jibril); hakika yeye ameiteremsha Quran Moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu (siyo kafanya kwa kupendelea kwake); (Quran inayosadikisha yale yaliyokuwa kabla yake, na ni uwongozi na khabari njema kwa wanao amini” (Sura ya 2:97)
“Sema: Roho takatifu (yaani Jibril) ameiteremsha kutoka kwa Mola wako kwa haki, ili kuwathibitisha wale walioamini, na kuwa uwongozi na khabari njema kwa walioamini” (Sura ya 16:102)
Hivyo Mwislamu kwa aya hizi mbili anajenga hoja kwamba, “kwakuwa 2.97 inasema Quran iliteremshwa na Jibril, na 16:102 inasema Qurani iliteremshwa na Roho Mtakatifu basi tunahitimisha kuwa Jibril ndiye Roho Mtakatifu”. Kwa kwei hii ni hoja dhaifu sana na isiyozingatia maana na Mantiki ya maandiko yote kwa ujumla. Hakuna mahali popote katika Quran, Jibril amtamkie Mtume kwamba, “mimi Jibril ndiye Roho Mtakatifu”, wala hakuna katika hadithi Mtume alipofunulliwa ya kwamba Jibril ni Roho Mtakatifu. Tuchunguze hoja hii kwa kina zaidi.
Je ufunuo (Wahyi) kwa mtume ulikuja katika njia (daraja) ngapi?.
Tunaambiwa katika kitabu kiitwacho Ar Raheeq al Makhtum ukrasa wa 109 juu ya mafungu ya Wahyi yalikuwa kama ifuatavyo;
1. Kudhihiri kwa ndoto za kweli, ilikuwa mwanzo wa Wahyi kwa mtume (s.a.w)
2. Kwa yale ambayo Malaika alikuwa akiyapenyeza kwenye fikra na Moyo wake
3. Kwa Malaika kujidhihirisha kwake katika Sura ya Mwanadamu
4. Mtume kujiwa na Wahyi kwa mfano wamlio wa Kengele uliokuwa na kishindo
4. Mtume alikuwa akimwona Malaika katika sura yake halisi
5. Maneno ya Mwenyezi Mungu moja kwa moja.
Hivyo kwa hili tu tunaona kwamba, haifai kabisa kuchukua aya moja ya namna alivyoshushiwa Wahyi Mtume (s.a.w) na kufananisha na aya nyingine inayoongelea kushushwa kwa Wahyi kwa mtume. Kufanya hivyo ni kuonyesha kwamba Mtume alishushiwa Wahyi kwa njia moja peke yake na hivyo kukana Historia ya Maisha yake na namna yeye mwenyewe alivyoeleza namna alivyokuwa akifunuliwa Wahyi.
Roho Mtakatatifu na Kuhusika kwake kuleta Wahyi kwa Mtume.
Unaporudia kusoma vizuri Sura ya 16:102 bila kuweka maneno ya Fikra za Wafasiri na Wasomi wa Kiislamu, udagunua inasema kwamba
“Sema: Ameiteremsha Roho takatifu kutoka kwa Mola wako, ili awathibitishe wale waliamini na kuwa ni uwongofu na bishara kwa Waislamu” (Sura 16:102)
Katika aya hakuna neno Jibril, lakini mtafsiri anatia mikono yake ili kuleta maana kwamba huyo Roho mtakatifu ni Jibril.
Tumekwisha kuona kuwa Mtume alipata ufunuo kwa nyanja au njia mbalimbali, ni wazi kuwa moja wapo ni kushukiwa na Roho Mtakatifu kama ambavyo tunaona kuwa, Mitume hupata ufunuo ama kwa Malaika kutumwa na kuwaletea ujumbe. Na wakati mwingine Roho Mtakatifu huwapatia uvuvio. Ni wazi kuwa Roho Mtakatifu ametofautishwa kabisha na Malaika kuonyesha yeye ni nafsi tofauti na Malaika pale tunaposoma katika Quran
“Hushuka Malaika na Roho, katika usiku huo, kwa idhini ya Mola wako kwa kila Jambo” (Sura ya 97:4)
Hapa tunaona Malaika hushuka na Wahyi na Roho Mtakatifu naye hushuka na Wahyi. Jibril ni Malaika ndiye aliyekusudiwa na kisha Roho Mtakatifu. Wote wawili wametajwa kwa pamoja wakihusika katika kuleta Wahyi.
Kwa Mujibu wa Quran, Roho Mtakatifu ndiye aliyemwezesha Maryam, Mama wa Isa kuwa na mtoto.
Kama ilivyo katika Biblia, kwamba Malaika Gabrieli alikuja kwa Mariamu na kumpasha habari njema za kuzaa mtoto kwa uwezo wa Roho Mtakatifu (Soma Luka 1:35 na Mathayo 1:20) ndivyo ilivyo katika Quran pia, tunasoma kwamba;
“Na Mariamu mtotto wa Imrani aliyejihifadhi nafsi yake, na tukampurizia humo roho yetu (inayotokana na sisi), na akayasadikisha maneno ya Mola wake, na vitabu vyake; na alikuwa miongoni mwa wanyenyekevu.” (Sura ya 66:12)
“Na (Mtaje yule mwanamke) aliyejilinda (aliyejihifadhi), nafsi yake, na tukampulizia roho yetu na tukamfanye yeye na mwanae kuwa miujiza ya kudra ( ya mwenyezi Mungu) kwa walimwengu” (Sura ya 21:91)
Katika aya hizi haiwezekani kusema kwamba Jibril ndiye roho iliyopulizwa kwa Mariamu. Neno linasema “ttukampurizia humo roho yetu”. Yaani Roho ya Mwenyezi Mungu. Na ndivyo kukawa kuzaliwa kwa Nabii Isa (a.s)
Malaika Gabriel katika Biblia alisema “mimba yake ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu” (Mathayo 1:21)
Haiwezekani wala haiingi akilini kwamba Malaika Jibril ndiye awe Roho Mtakatifu tena. Kwani aya za Quran zinasema, Mwenyezi Mungu alipuliza Roho yake ndani ya tumbo la Mariamu, na Roho huyo akafanyika Mwili.
Kwa Mujibu wa Quran, Roho Mtakatifu huwatia nguvu waumini ili wafanye vitendo vyema.
Tunafahamu kwamba, kwa mujibu wa Mafundisho ya Uislamu, Jibril hutumwa kwa mitume, na kazi yake ni kuletu ufunuo (Wahyi). Aya hii ifuatayo ndani ya Quran, inaondoa dhana ya kumdhania Jibril kuwa ni Roho Mtakatifu
“Huwapati (huwaoni) watu wanaomwamini mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, kuwa wanawapenda wale wanompinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake; hata wakiwa ni baba zao au watoto wao au ndugu zao au jamaa zao. Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu ameandika, ( amethibitisha kweli kweli) nyoyoni mwao imani na akawatia nguvu kwa Roho itokayo kwake, na atawaingiza katika mabustani yapitayo mito ndani yake, humo watakaa daima. Mwenyezi Mungu amekuwa radhi nao, na wao wamekuwa radhi naye. Hao ndio kundi la Mwenyezi Mungu. Sikilizeni! Hakika kundi la Mwenyezi Mungu ndilo linalofaulu.” (Sura ya 58:22)
Tunaambiwa kwamba Mwenyezi Mungu huwatia nguvu waumini “kwa Roho itokayo kwake”, hii kwa hakika siyo kazi ya Jibril. Ni wazi kwamba, waumini kwa mujibu wa aya hii, hufanya vitendo vyema kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Uelewa huu wa kwamba waumini hupewa uwezo kwa njia ya Roho Mtakatifu ndiyo fundisho kuu la Biblia. Yesu aliahidi kuwapatia Roho wake Mtakatifu wafuasi wake, ambaye angewasaidia katika kufanya kazi aliyo waachia;
“Lakini mtapokea nguvu, akisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu…” Matendo 1:8
“Basi ikiwa ninyi mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu wa mbinguni atawapa Roho Mtakatifu wale wamwombao”
(Luka 12:13)
Je Roho wa Kweli ni nani kwa mujibu wa vitabu vitakatifu?
Waislamu hudai kwamba Mtume Muhammad ametabiriwa ndani ya Biblia kuwa yeye ndiye Roho wa kweli. Wanasema kuna Roho Mtakatifu, na pia kuna Roho wa kweli. Wao kwao neno Roho Mtakatifu na Roho wa kweli ni vitu viwili tofauti. Chakushangaza katika dhana hii ni kwamba, Roho wa kweli siyo mtakatifu. Sasa jambo la kujiuliza je yeye Roho wa kweli ni Roho Mchafu? Maana kinyume cha utakatifu ni uchafu.
Kwa mujibu wa Vitabu vya Mungu, Roho atokaye kwa Mungu ni Roho Mtakatifu naye ni Roho wa kweli. Ameitwa Roho wa Kweli ili kumtofautisha na roho za mashetani ambazo Biblia inazielezea soma maandiko haya;
“Basi Roho anena wazi wazi ya kwamba, nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani” (1Timotheo 4:1)
“Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. Hizi ndizo roho za mashetani…” (Ufunuo 16:13-14)
Hivyo Yesu alimtaja Roho Mtakatifu kuwa Roho wa kweli ili kumtofautisha na hizi roho za uongo zinazodanganya ulimwengu wa imani katika zama zetu. Hata hivyo tuichunguzi aya hii ambayo Waislamu huitumia wakidai kuwa inamkusudia Muhammad.
“Lakini amin nawaambia, yafaa Mimi niondoke kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu. Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini Mimi, kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena, 11kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa. Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili Yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo. Atanitukuza Mimi, kwa maana atayachukua yaliyo Yangu na kuwajulisha ninyi. Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo Yangu na kuwajulisha ninyi.” (Yohana 16:7-15)
Kwa mujibu wa aya hii Waislamu wanasema, aliyekusudiwa hapo ni Muhammad kwa sababu
Roho wa kweli angeuthibitishia Ulimwengu kwa habari ya dhambi—Muhammad alianzisha dini ya Uislamu akionya watu juu ya maovu na dhambi
Roho wa kweli atauthibitishia Ulimwengu kwa sababu ya haki—Muhammad alifundisha dini ya haki
Roho wa kweli atauthibitishia Ulimwengu kwa sababu ya hukumu—Muhammad alifundisha Uislamu ambamo ndani yake zimu sharia na hukumu.
Hoja ya msingi tutaangalia iwapo sifa za huyo Roho wa kweli zinamfaa Muhammad, na kisha tuone habari ya dhambi, haki, na hukumu
Sifa za Roho wa kweli kwa mujibu wa maneno ya Yesu.
Yesu Mwenyewe amesema juu ya huyo Roho wa kweli kwamba
“Kama mnanipenda, mtazishika amri Zangu. Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine akae nanyi milele. Huyo ndiye Roho wa kweli ambaye ulimwengu
hauwezi kumpokea, kwa sababu haumwoni wala haumjui. Ninyi mnamjua kwa kuwa yuko pamoja nanyi naye anakaa ndani yenu” (Yohana 14:15)
Kwa Mujibu wa aya hii tunagundua mambo yafuatayo
Roho wa kweli anaitwa Msaidizi na analetwa kwa waumini pale wanapompenda Yesu na kushika amri zake. Swali la kujiuliza je Waislamu wanampenda Yesu na kuzishika amri zake
Roho wa kweli anakaa nasi milele. Swali la kujiuliza, je Muhammad anakaa na Waislamu milele? Hapana. Muhammad alikufa jumatatu mchana tarehe 8 mwezi wa 6 mwaka 632. Miaka zaidi ya 1400 iliyopita. (Abdala Farsy, Maisha ya Nabii Muhammad, uk. 81)
Roho wa kweli ulimwengu haumwoni anajulikana kwa waumini tu. Swali la kujiuliza, je Muhammad hakuonekana na makafiri? Hapana, Muhammad alionekana na wapinzani wa Uislamu, naye akapigana nao vita.
“Walipomwona haondoki, wale ‘Mashekhe’ waliamrisha watu wa mji wampige mawe kila wamwonapo, mpaka aende zake. Basi haikuwahi kutangaa habari hii ila kila mtu alitoka na akiba ya mawe mkononi mwake ili mpige mtume atakapomwona. Alipotokeza nje tu, mara walimtopoa kwa mawe, husemi watoto wanapopoa embe zilizoiva! Hakujamsaidia chochote hata kusema anakwenda zake; lakini waliendelea kumfuata njiani na kumpiga mawe, na huku wakimpigia sokole, muda wa maili 2. Aliloa damu tangu kichwani mpaka miguuni, hawajamwacha kupumzika hata chembe muda wa maili 2 zote hizo!” (Abdala Farsy, Maisha ya Nabii Muhammad, uk. 30)
Kisa hiki kinaonyesha ni wazi Muhammad alionekana na watu wa ulimwengu huu waliokuwa wapinzani. Roho wa kweli haonekani wala kufahamika na wale wasiomjua Mungu. Sana sana watapinga uwepo wake wakidai “Mungu hana mshirika”
Roho wa kweli hukaa ndani ya watu wa Mungu
“Lakini ninyi, hamtawaliwi na mwili, bali na Roho, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Mtu ye yote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo. Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, miili yenu imekufa kwa sababu ya dhambi, lakini roho zenu zi hai kwa sababu ya haki. Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, Yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho Wake akaaye ndani yenu.” (Warumi 8:9-11)
Muhammad hawezi kumwingia mtu akakaa ndani yake, kamwe ni jambo lisilowezekana. Ni dhahili kwamba Roho wa kweli siyo Muhammad.
Kwa mujibu wa Yohana 16:7 Roho Mtakatifu anatumwa ana Yesu. “lakini nikienda nitamtuma kwenu”. Swali la msingi, ikiwa Muhammad ni Nabii, na tunatambua kwamba Manabii hutumwa na Mwenyezi Mungu, Yesu anasema yeye ndiye atakayemtuma huyo Roho wa kweli, kwa kuwa Waislamu wanadai aliyekusudiwa hapa ni Muhammad, Je Yesu atakuwa nani kwa Muhammad? Bila shaka kwa kuwa ametumwa na Yesu, Basi Yesu ndiye Mungu wa Muhammad. Jambo ambalo kamwe Mwislamu hawezi kukubaliana nalo. Na kama hakubali hili, basi aachane na aya hii kabisha haimhusu Muhammad.
Je Roho Mtakatifu anauhakikishiaje Ulimwengu kwa habari ya dhambi, haki na hukumu?
Tumekwisha kuona kuwa Manabii wa Mwenyezi Mungu hunena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu
“Wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu” 2 Petro 1:21
“wakafunuliwa yakuwa si kwa ajili yao wenyewe, baali kwa ajili yenu walihudumu katika mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiri ninyi injili kwa Roho Mtakatifu…” 1 Petro 1:11
Hivyo watumishi wa Mungu wanapohubiri wakikemea dhambi na kuwaonya watu juu ya hukumu ijayo, kazi hiyo hufanywa na Roho Mtakatifu aliye ndani yao.
“Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote. 8Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo. Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya. Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbali mbali za lugha, kwa mwingine tafsiri za lugha. Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo mwenyewe.” (1Wakorintho 12:7-11)
Mungu ni Mmoja, lakini umoja huo wa Mwenyezi Mungu hauna maana ya umoja kama ambavyo akili ya mwanadamu inatambua. Mungu ni mmoja katika nafsi tatu zilizo hai. Na katika utatu huo ndio anasema hafanani na yeyote, kwa sababu hakuna mungu au miungu inayoweza kuwa na sifa ya Mungu mmoja na hapo hapo akawa na nafsi tatu zilizo hai. Quran inapokata utatu ni kwasababu Makuraishi wa maka walikuwa na waungu watatu walioabudiwa kwa mfano wa Masanamu. Muhammad akaipiga marufuku dini hiyo ya kipagani, na akawakataza watu wasimwabudu Mwenyezi Mungu kwa mifano ya waungu hao. Tunasoma katika Quran
“Je mmewaona Lata, na Uza na Manat mungu wenu mwingine wa tatu (kuwa ndio waungu hao badala ya Mwenyezi Mungu?). Je kwenu muwe na watoto wa kiume na Kwake waweko watoto wa kike? Huo ni mgawanyo wa dhuruma! (Mnamdhurumu basi Mungu!) (Sura ya 53:19-22)
Muhammad analalamika kwamba miungu hiyo inawatoto wa kike tuu! Na kwamba wale wanaoiabudu wanawatoto wa kiume. Kufanya hivyo—yaani kusema miungu yao makafiri ina watoto wa kike peke yake ni kufanya dhuruma kwa miungu hiyo, yaani hawaitendei haki.
Kisha anaendelea kusema
“Hayakuwa haya (majina ya Lata, mungu mwanamke na Al uzza, mungu mwanamke mwenye enzi na Manata, mungu mwanamke anayeneemesha) ila ni majina tu mliyowapa nyinyi na baba zenu (masanamu hayo; wala hawana lao jambo). Mwenyezi Mungu hakuteremsha dalili juu yao. Hawafuati ila dhana na zinayopenda nafsi (zao). Na kwa yakini uwongozi umewafikia kutoka kwa Mola wao…” (Sura ya 53:23
Hawa ndiyo waungu watatu ambayo Quran nzima inapinga itikadi ya makafiri wa Makka. Wayahudi na Wakristo hawakuwa wakiabudu miungu watatu wakati wa Muhammad, wala katika Biblia halipofundisho la waungu watatu, isipokuwa MUNGU NI MMOJA MWENYE NAFSI TATU ZILIZO HAI
Shalom,
Dr. Max Shimba

UTUME WA PAULO KWA MUJIBU WA QURAN NA HADITH

Image result for APOSTLE paul
Mwanzo wa Utume wa Paulo;
Katika Hesabu 12:6
Mwenyezi Mungu anaeleza namna mitume na Manabii wanavyopata Wahyi kutoka kwa Mungu:
Je sifa hii ya kuletewa Wahyi Paulo alikuwa nayo?
Tunasoma katika Matendo. 16:9
“Wakati wa usiku Paulo akaona maono…”
Je Mungu alieleza kuwa Paulo alitumwa kwa watu gani?
Matendo. 9:15
“Lakini Bwana akamwambia Anania…Mtu huyu ni chombo changu kiteule nilichokichagua apate kulichukua jina langu kwa watu Mataifa na wafalme wao na mbele ya watu wa Israeli.”
Matendo 13:2
“Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu akasema “Nitengeeni Sauli na Barnaba kwa kazi ile maalumu niliyowaitia”
Je Paulo Mwenyewe anajishuhudia vipi kuhusu utume wake?
Wagalatia 1:1
“Paulo, mtume, si mtume wa wanadamu aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu”
Wakolsosai 1:1
“Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.”
Hapa Paulo anatusaidia kujibu swali la Mada yetu, anasema ni “Mtume wa Mungu”
UTUME WA PAULO KWA MUJIBU WA QUR’AN NA HADITH ZA MTUME.
Kwanza Kabisa nikumbushe sifa za imani ya Mwislam. (Swifat ul I’iman mufaswalu)
Kwanza ni Kumwamini Mwenyezi Mungu
Pili ni Kuamini Malaika wa Mwenyezi Mungu
Tatu ni kuamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu
Nne ni Kuamini Mitume wake
Tano ni kuamini Kheri na Shari zake
Sita ni kuamini Siku ya Mwisho (Siku ya malipo)
Kwa mujibu wa Mada hii nitajikita katika sifa ya nne yaani Kuamini juu ya Mitume wa mwenyezi Mungu.
Katika imani ya Kiisalamu kuna jumla ya mitume wapatao 124,000 laki moja na Ishirinina tano, kati ya hao, ni mitume 25 tu, Mtume Muhammad (S.A. W) ndiyo aliweza kufunuliwa na kuelezewa habari zake. Kama inavyosema Qur’an katika Sura ya 4:164
“Na mitume tuliokwisha kukuhadithia kabla yake, na mitume wengine hatukukuhadithia. Na Mwenyezi Mungu alinana na Musa kwa Maneno”
“Semini nyinyi: Tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa sisi, na yaliyoteremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zake, na waliyopewa Musa na Isa, na pia waliyopewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatutofautishi baina ya yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake.”
Aya hii inawataka Waislamu kuwa amini mitume wote wa zamani, aya inasema wanatakiwa waamini walioteremshiwa wajukuu wa Yakobo, na Manabii wengine wote ambao hawakutajwa ndani ya Qurani.
Paulo Mwenyewe amesema kuwa ni Mjukuu wa Yakobo.
“…mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania..” (Wafilipi 3:5)
Benjamini alikuwa mtoto wa Yakobo. Hivyo twaona kuwa Qurani Sura ya 2:136 inakusudia kuaminiwa kwa mitume wote waliotangulia akiwemo na Paulo na manabii wote waliotajwa ndani ya Taurat, Zaburi na Injili.
Hivi yaonekana kuwa umati mkubwa wa mitume bwana Muhammad hakuweza kuelezwa habari zake. Sehemu kubwa ya Mitume na Manabii waliotajwa ndani ya Qur’an ni wale waliotajwa pia ndani ya Biblia. Hivyo basi Mwislam anapotaka kufahamu zaidi juu ya habari za Mitume na manabii yampasa kuzingatia agizo la Mwenyezi Mungu kwa Mtume katika Sura 10:94 kwamba;
“Na ukiwa na shaka juu haya tuliyokufunulia, basi waulize wasomao Kitabu kabla yako (Mayahudi na Wakristo)…”
Inashangaza kuona kuwa baadhi ya Waislam wameibuka siku hizi kupinga mitume waliofunuliwa katika Biblia hasa Mtume Paulo. Kwa sehemu kubwa upinzani huu unafanywa bila kuzingatia Qur’an Yenyewe pamoja na mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W). Yaonekana wale wanaopinga hawana elimu ya kutosha juu ya Qur’an na Imani yenyewe ya Uislam.
Hebu tuangalie mada hii kwa kutumia Qur’an na Hadith pamoja na Sherehe za Wanazuoni mbalimbali ndani ya Uislam.
Tunasoma Katika Qur’an 36:13-14 kwamaba
Mwenyezi Mungu hapa anamkumbusha mtume juu ya wakazi wa mji Fulani, ambapo yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu anasema—alituma “wajumbe wake”.
Wafasili wengi wa Qur’an wakiwemo Shekhe Balwani, pamoja na Yusufu Ali katika tafsiri zao wanautaja mji huo kuwa ni ANTIOKIA.
Ibn Kathir yeye anatueleza zaidi juu ya mitumehao kuwa majina yao yalikuwa, Yohana, Simoni pamoja na Paulo.
Ni dhahiri basi kwamba hoja hii ya upizani juu ya Paulo ndani ya Uislam ni ya hivi karibuni sana. Ushahidi wa hadithi za mtume Muhammad waonyesha kuwa Waislamu wa mwanzo hawakuwa na tatizo juu ya utume wa Paulo.
Katika kitabu kilichoandikwa na Ibn Hisham kiitwacho Sirat Nabawiyat, juzuu ya 4 uk. 140 (Tazama sehemu ya tatu ya somo hili) kuna section nzima Mtume Muhammad anawaelezea Masahaba wake orodha ya mitume wa Bwana Yesu na Sehemu walizotumwa, Miongoni mwa mitume hao, ametajwa pia Mtume Paulo, na kwamba Yeye Paulo alitumwa kwa watu wa Rumi.

Ndugu zangu Waislamu kama nilivyotangulia kusema, ikumbukwe kwamba kupinga utume wa Paulo ni kupinga Imani, kupinga Dini yenyewe na kupinga Qur’an, kuwapinga wanazuoni waliotutangulia, na mwisho wa yote, KUMPINGA MWENYEZI MUNGU. Hivyo basi twaona kuwa, kupinga utume wa Paulo ni Ukafiri uliokithiri ambao Mwenyezi Mungu hawezi kuuvumilia.
Shetani ni mjanja sana, anahila nyingi za kuwapotosha wanadamu, wengi wanadhani kuwa wanatetea dini wanapopinga utume wa Paulo kumbe kwa yakini wanapinga dini kwa kufanya hivyo. JIEPUSHE USINASWE KATIKA MTEGO HUU.
Bada ya kuangalia uthibitisho juu ya utume wa Paulo ndani ya Biblia Takatifu, hebu tuigeukie Quran tukufu ili kupata uthibitisho mwingine.
UTUME WA PAULO KWA MUJIBU WA QURANI TUKUFU
Kwa kuanza naomba niwakumbushe Waislam kwambu uislamu una sifa zifuatazo. (swifat ul I’iman mufaswalu)
1. Imani juu ya Mungu.
2. Imani Juu ya Malaika wa Mwenyezi Mungu.
3. Imani juu ya Vitabu vya Mwenyezi Mungu
4. Imani juu ya Mitume wa Mwenyezi Mungu
5. Imani juu ya Kheri na Shari za Mwenyezi Mungu.
6. Imani juu ya Siku ya Mwisho.
Kwa mujibu wa Mada ya leo. Nitajikita juu ya Imani juu ya Mitume.
Waislamu wanaamini kwamba, wapo Mitume wapatao 124,000. Kati ya hao. ni 25 tu ndiyo ambao mtume Muhammad (S. A. W) aliweza kupewa habari zake. kama tunavyosoma.
[ AN-NISAAI – 164 ]
Na Mitume tulio kwisha kukuhadithia kabla yake, na Mitume wengine hatukukuhadithia. Na Mwenyezi Mungu alinena na Musa kwa maneno.
Hii inamaana kwamba Muhamad alifahamu kidogo sana kuhusu habari za mitume. yaani kama ni asilimia ni 0.0002 ya uelewa wake juu ya mitume. na huo ndio uelewa wa waislamu wote linapokuja swala la mitume. Hata hivyo. Allah s.w alikwisha kumwelekeza mtume mahala pa kupata nuru zaidi aliposema.
(YUNUS – 94)
Na ikiwa unayo shaka katika tuliyo kuteremshia, basi waulize wasomao Kitabu kabla yako. Kwa yakini imekwisha kujia Haki kutoka kwa Mola wako Mlezi. Basi usiwe miongoni mwa wenye shaka.
Hivyo kwa habari za mitume, karibia mitume wote aliosimuliwa muhammad wamo kwenye Biblia. Basi kama tulivyoona sehemu ya kwanza ya mada yetu leo twawagabarisha waislamu juu ya utume wa Paulo.
Hata hivyo ukisoma Quran kwa uangalifu utagundua kuwa Habari za Paulo zimeelezwa vizuri humo.
Chunguza aya hii.
(YA-SIN – 13-14)
Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
Aya hii inaeleza kisa cha WAJUMBE WA MWENYEZI MUNGU.
Wafasiri na wanazuoni mfano Shekhe Balwani, Yusufu Ali wamefasiri aya hii na kusema mji huo walikotumwa wajumbe ni ANTIOKIA.
Ibin Kathir katika tafsir yake anasema wajumbe hao ni Yohana, Simoni na Paulo.
Na hapa namnukuru ibn Kathir.
Imesimuliwa na Ibn Jurayj kutoka kwa Wahb bin Sulayman, imepokelewa na Shu`ayb Al-Jaba’i, “Majina wajumbe wawili wa waliotumwa mwanzo ni Simoni na Yohana na jina la wa tatu ni Paulo. Na mji huo ulikuwa Antiokia” , and the city was Antioch. Na wakasema (kwa watu wa mji huo) “hakika sisi tumetumwa kwenu kama wajumbe”, hii ina maanisha “Wajumbe kutoka kwa Allah aliyewaumba nyinyi na anayewaamrisha mumwabudu yeye peke yake na msimfanyie washirika.” Qatada amesema walikuwa ni wajumbe wa Masihi Isa bin Maryam (a.s) waliotumwa kwa watu wa Antiokia. Wakasema “Ninyi ni wanadamu kama sisi…ni kwa vipi munaweza kupokea ufunuo wakati nyie ni wanadamu na sisi tu wanadamu kama nyie, kwanini sisi hatupokei ufunuo kama nyie?” hivi ndivyo ilivyokuwa kwa watu wa mataifa mengine walivyosema ‘hatuamini’, kama vile Allah anavyotuambia katika sura ya 64:6 , as Allah has told us in the Ayah: That was because there came to them their Messengers with clear proofs, but they said: “Shall mere men guide us!” (64: 6) “Hayo ni kwa kuwa walikuwa wakiwajia mitume wao kwa hoja zilizo wazi, nao wakasema: Hivyo binadamu ndiyo atuongoe? Basi wakakufuru na wakageuka upande. Mwenyezi Mungu akawa hana haja nao…”
Hivyo twaona kuwa hoja ya kumkataa Paulo ni uzushi wa hivi karibuni. Waislamu, wasomi na Maulamaa wa kale hawakuwa na hoja hii ya kumkataa Paulo.
UTUME WA PAULO KWA MUJIBU WA HADITHI ZA MTUME.
Baada ya Kuona Ushahidi wa vitabu vitakatifu juu ya utume wa mtume Paulo. Sasa tugeukie hadith za mtume Muhammad. na kwa nini tugeukie hadithi? Ni kwa ushauri unaotolewa na Allah s.w ndani ya Quran yenyewe.
[ AN-NISAAI – 59 ]
Enyi mlio amini! Mt’iini Mwenyezi Mungu, na mt’iini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema.
Katika kitabu kiitwacho SIRAT NABAWIYA. Kilichoandikwa na Ibn Hisham, aliyekuwa mwanafunzi wa ibn Ishak. Katika juzu ya 4 ya kitabu hicho uk 140 tunakuta Muhammad anaorodhesha majina ya Wanafunzi wa Yesu. na anawagawa katika mafungu 2. la kwanza ni wale waliomfuata wakati wa uhai wake na wale waliomfuata baada yakuwa amepaa juu. Muhammad anaeleza kila mmoja wa wanafunzi hao na mahala walikotumwa, kuhusu Paulo anaeleza kuwa Yeye alitumwa Rumi.
Na hapa namnukuru ibn Hisham.
*أسماء رسل عيسى عليه السلام*
أسماء رسل عيسى عليه السلام
قال ابن إسحاق ‏:‏ وكان من بعث عيسى بن مريم عليه السلام من الحواريين والأتباع ، الذين كانوا بعدهم في الأرض ‏:‏ بطرس الحواري ، ومعه بولس ، وكان بولس من الأتباع ، ولم يكن من الحواريين ، إلى رومية ، وأندرائس ومنتا إلى الأرض التي يأكل أهلها الناس ، وتوماس ، إلى أرض بايل من أرض المشرق ، وفيلبس إلى أرض قرطاجنة ، وهي أفريقية ؛ ويحنس إلى أفسوس ، قرية الفتية أصحاب الكهف ؛ ويعقوبس إلى أوراشلم ، وهي إيلياء قرية بيت المقدس ، وابن ثلماء إلى الأعرابية ، وهي أرض الحجاز ؛ وسيمن إلى أرض البربر ، ويهوذا ، ولم يكن من الحواريين ، جعل مكان يودس ‏.‏
Majina ya Mitume wa Yesu Masihi:
“Amesema ibh Is-hak: walikuwa mionguni mwa wanafunzi wa Yesu (amani iwe juu yake) wale waliomfuata wale waliokuwa baada yake duniani: Petro Mwanafunzi wa Yesu, na pamoja naye alikuwepo Paulo miongoni mwa wafuasi, Paulo hakuwa miongoni mwa wale wanafunzi wa Yesu. Naye (Paulo) alitumwa Rumi. Na Andrea naye alitumwa katika nchi ambayo wakazi wake wanakula watu. Na Tomaso alitumwa katika nchi ya Babeli katika nchi za mashariki. Na Philipo alitumwa katika nchi pande za Afrika, na Yohana alitumwa Efeso na Yakobo alitumwa Yerusalemu na Batholomeo alitumwa Uarabuni katika nchi ya Hijaz. Na Simoni alitumwa Baribari.”
Yashangaza kuona kuwa licha ya ushahidi mkubwa namna hii waislamu wa leo (hasa wanaharakati) wameamua kufumbia macho ukweli huu na kuanza kudanganya watu. ama kwa maksudi ama kwakutokujua. SWALI NI HILI. wanafanya hivyo kwa faida ya nani?
Rafiki yangu mwislamu, napenda kukutahadharisha kwamba, shetani ni mjanja, siku zote atakuja kwa hila akiwatukia waalimu wa uongo, wengine watakuja kana kwamba ni watetezi wa dini kumbe ndiyo waharibifu wakubwa wa dini.
Allah s.w anasema ndani ya Quran kuwaambia waislamu
[ AL – BAQARA – 136 ]
Semeni nyinyi: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyo teremshiwa sisi, na yaliyo teremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zake, na waliyo pewa Musa na Isa, na pia waliyo pewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatutafautishi baina ya yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake.
Unaona kwamba Allah s.w amewaagiza waislam siyo tu kuamini wale kitume 25 waliotajwa ndani ya Quran lakini pia wanapaswa kuamini w aliyoteremshiwa wajukuu wa Yakobo, PAULO PIA NI MJUKUU WA manabii YAKOBO. Lakini siyo hivyo tu, Allah s.w amewataka manabii waislamu kuamini walioteremshiwa “manabii wengine”. PAULO PIA NI MIONGONI MWA MANABII WENGINE.
Hivyo kumpinga Paulo ni kuipinga imani, kupinga Quran na Mwinsho kumpinga Allah mwenyewe. NA HUU NDIO UKAFIRI ULIOKITHIRI.
Je kuha hadithi yoyote ya Mtume mahali ambapo, Mtume aliwatahadharisha masahaba zake au Waislamu kwa ujumla juu ya Mafundisho ya Paulo?
Hapana, badala yake tunaona Muhammad yeye mwnyewe alinukuru mafundisho ya Paulo na akiuita ni ujembe kutoka kwa Mwenyezi Mungu‏

“Imesimuliwa na Abu Huraira, Mjumbe wa Allah (s.a.w) alisema; Mwenyezi Mungu kasema, ‘Nimewaandalia waja wangu ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio halijawahi kusikia wala moyo wa mwanadamu hauwezi kuyafikiri”
Hivyo twaona kuwa hoja ya kukataa utume wa Paulo hainamsingi wa mafundisho ya vitabu vitakatifu, ni upotoshaji wa waalimu wa dini wanaotafuta masilahi yao binafsi.

Sunday, April 15, 2018

MUNGU HANA UPENDELEO, LAKINI ALLAH YEYE AMEJAA UPENDELEO KWA WAARABU TU





Fikiria mara ya kwanza ulipojifunza kweli kumhusu Yehova Mungu wa kwenye Biblia na makusudi yake na kuanza kuwa na imani. Ulipata kuelewa kwamba ingawa ulizaliwa katika dhambi na kutenganishwa na Mungu, Mungu Baba kupitia Kristo Yesu alifungua njia ili ufikie ukamilifu ambao Adamu alipoteza na pia kukuwezesha kupata uzima wamilele.

Biblia iliyo kuwepo miaka 650 kabla ya kuzaliwa na kuanzishwa kwa Quran inasema hivi:

Warumi 2:11 kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu. https://www.wordproject.org/bibles/sw/45/2.htm#0

Matendo 10:34 Petro akafumbua kinywa chake, akasema, Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo; https://www.wordproject.org/bibles/sw/44/10.htm#0

Hii ndio maana ya Yehova, yaani Mungu wetu anatupenda wote sawasawa bila ya upendeleo.

LAKINI nilipo isoma Quran ya Allah nikagundua kuwa, yeye Allah amejaa upendeleo kwa watu fulani tu na kuwachukia wengine.

Nukuu: Quran Suratul Maidah aya ya 3 ambayo inasema.

( حُرِّمَتْ عَلَيْكُمُ الْمَيْتَةُ وَالدَّمُ وَلَحْمُ الْخِنزِيرِ وَمَا أُهِلَّ لِغَيْرِ اللَّهِ بِهِ وَالْمُنْخَنِقَةُ وَالْمَوْقُوذَةُ وَالْمُتَرَدِّيَةُ وَالنَّطِيحَةُ وَمَا أَكَلَ السَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيْتُمْ وَمَا ذُبِحَ عَلَى النُّصُبِ وَأَن تَسْتَقْسِمُوا بِالْأَزْلَامِ ۚ ذَٰلِكُمْ فِسْقٌ ۗ الْيَوْمَ يَئِسَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن دِينِكُمْ فَلَا تَخْشَوْهُمْ وَاخْشَوْنِ ۚ الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ فَمَنِ اضْطُرَّ فِي مَخْمَصَةٍ غَيْرَ مُتَجَانِفٍ لِّإِثْمٍ ۙ فَإِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ )

المائدة (3) Al-Maaida

Mmeharimishiwa nyamafu, na damu, na nyama ya nguruwe, na mnyama aliye chinjwa si kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na aliye kufa kwa kunyongeka koo, na aliye kufa kwa kupigwa, na aliye kufa kwa kuanguka, na aliye kufa kwa kupigwa pembe, aliye liwa na mnyama, ila mkimdiriki kumchinja. Na pia ni haramu kula nyama aliye chinjiwa masanamu. Na ni haramu kupiga ramli. Hayo yote ni upotovu. Leo walio kufuru wamekata tamaa na Dini yenu; basi msiwaogope, bali niogopeni Mimi. Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimeku-PENDELEENI UISLAMU uwe ndiyo Dini. Na mwenye kushurutishwa na njaa, bila ya kupendelea dhambi, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Msamehevu na Mwenye kurehemu.

Kumbe Uislam ni dini ya kupendelewa Waarabu tu na hakuwapendelea wengine wawe na dini hiyo. Hivi, tokea lini Mungu akajaa chuki kubwa kama za huyu Allah mwenye upendeleo?

Mungu wetu anasema hivi: "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye."
Yohana 3:16-17

Umesha soma kuwa, Yehova anatupenda sote wa duniani na sio kama Allah mwenye upendeleo kwa Waarabu tu.

Habari njema nilazima ihubiriwe kote kabla ya kurudi kwa Yesu. Imeandikwa Mathayo 24:14 "Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.

Twendeni na tufanye kazi ya Bwana katika Mataifa yote.

Yesu ni yule yule, Jana, Leo na Hata Milele.

Mungu awabariki sana,

Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Tito 2:13

For Max Shimba Ministries Org,

MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED

Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Saturday, April 14, 2018

Muslims in China fed pork sold as Halal beef

Muslims in China fed pork
By: World Bulletin
Police in Xi’an, the capital of China’s Shaanxi province, have seized more than 20 thousand kilograms of pork being sold off as halal beef products. The pork had been treated with chemicals such as paraffin wax and industrial salts to make it look like beef.
Taiwan’s Want China Times reported that the factory sold between up to 2,000 kg to local markets. A police statement revealed that the factory processed the pork at night and sold it as beef the next day.
This news has infuriated many Muslims in the region who bought the meat believing it was halal. Islam forbids Muslims from eating pork and other non-halal food.
Scandals like this are not at all uncommon in China. Earlier this year the Medical Daily said that 904 people were arrested for “meat-related offences”.
According to China‘s public security ministry. more than 22 meat products were found to have E. coli levels that “seriously exceeded standards”.

China Forces Muslims to Eat Pork…

Image result for pork in china

WASHINGTON, DC — The communist regime of Chinese President Xi Jinping has burned down Christian crosses at various churches and is forcing Muslim Uighurs to eat pork as part of its efforts to impose atheist values on everyone in the country, some U.S. government and independent analysts indicate.

During a discussion on religious persecution in China hosted by the Heritage Foundation on Friday, Bob Fu, the founder and president of the U.S.-based Christian human rights group China Aid, noted that Chinese Communist oppression is high in the Muslim-majority province of Xinjiang, home to the country’s Uighur (or Uyghur) minority.
He also pointed out that China’s religious freedom oppression is affecting Christians in the country, particularly those in the city of Wenzhou in Zhejiang province, known as the Jerusalem of China.
In Xinjiang province, communist party officials are “mandated to force themselves and stay in every household of Uighur families from two to five days every month” to monitor their activity and ensure they are loyal to the government, Fu noted.
China is sending Uighurs suspected of Islamic extremism and political dissent to “mind transformations centers,” Fu said.
“Many” of the Uighurs sent to the centers are “forced to even eat pork,” the China Aid president proclaimed, further adding that in the camp prisoners “are mandated to wear specially designed earphones and [listen] to 24 hours of propaganda from the communist party.”
“Many went into insanity,” Fu also said. “It’s happening right now.”
China is monitoring “every inch” of Xinjiang, pointed out Fu, a Christian refugee who fled China after Beijing imprisoned he and his wife for two months for “illegal evangelism” in 1996.
The human rights lawyer revealed that communist authorities in the city of Wenzhou “forcibly burned” and “demolished” “2,000 crosses,” adding the country’s judicial system sentenced some pastors affiliated with the affected churches “to 13, 10 years imprisonment.”
Echoing Fu, Kristina Arriaga, the vice chairwoman of the U.S. Commission on International Religious Freedom (USCIRF), confirmed that the Xi administration is taking down crosses from churches across China.
“Just earlier this year the Golden Lampstand Church was demolished and Chinese officials as was mentioned earlier have taken down crosses religions iconography from churches and from villages,” Arriaga declared.
“Incredibly, the Chinese government persecution goes beyond property damage,” she continued, noting that communist authorities routinely harass and imprison Christians.
In what appears to be an effort to expand its control of religion, the atheist Xi regime intends to make the country’s religious groups more “Chinese,” reported Newsweek in October 2017.
During the Communist Party conference, held every five years, President Xi reportedly indicated “that all religions must be ‘Chinese-oriented,’ as part of his effort to ‘Sinicize religion,’ or make it more Chinese, by instilling socialist core values.”

Cleric Helps Gang-Rape a 14-Year-Old Inside a Mosque…

14 Apr 2018: Uttar Pradesh: Cleric rapes 14-year-old girl inside mosque premises
Uttar Pradesh: Cleric rapes 14-year-old girl inside mosque premises
In a shocking incident, a 14-year-old girl was allegedly raped inside a mosque by a cleric and shopkeeper on Wednesday. A medical examination has confirmed rape.
The victim's father registered a complaint on Thursday evening in Bhagwatpur police station area in Moradabad.
The two accused- cleric Nazir and shopkeeper Mohsin, are absconding and the police are putting in efforts to arrest them.
Details: Cleric asks girl to clean his room, rapes her later
According to the girl's father, the cleric Nazir asked the girl to stay behind, after others left on Wednesday to clean his room in the mosque's premises.
When the girl went aside, Mohsin was present already. They overpowered the victim and raped her.
The two then fled from the scene, before the girl's father and others entered the mosque.
Fact: In UP, crimes against children hit record-high in 2016
According to data of National Crime Records Bureau, Uttar Pradesh is the worst state for children in terms of crime. The state recorded a record 2,115 incidents of rape (including under POSCO) in 2016, much higher than states like Maharashtra, Madhya Pradesh.

New Zealand Farmer Arrested For Selling Sheep as Sex Slaves for ISIS Islamic Terrorist Group

Allan Seymour sold thousands of sheep to Syria to “satisfy ISIS soldiers sexual appetite”
according to a joint CIA and MI6 report has admitted New Zealand’s Ministry of Defense
Bestiality and Islam

In a controversial interview last year, Dr. Zakir Naik – a noted Quranic scholar – explained why bestiality is permitted under certain conditions in Islam.
“A man is still considered pure when he releases his lust with a sheep or goat. If there is no woman, then there is no true lust or sexual sin. Then the animal becomes tainted and so must die. So says the Prophet Mohammed”.
According to New Zealand Customs services, over 20,000 sheep were shipped by Allan Seymour in the last year, but hundreds of thousands more could have been sent from other New Zealand farmers to ISIS forces which are presently unaccounted for.

UTABIRI KUHUSU SYRIA NDANI YA BIBLIA

Image may contain: outdoor
Macho ya ulimwengu hivi sasa yapo juu ya Syria. Maafa yanayojitokeza huko sasa hivi, na mbaya zaidi ni kwamba siku za mbeleni inaweza kuwa mbaya zaidi.
Manabii walishatabiri anguko la Dameski-Syria zaidi ya miaka 2500 iliyopita.
Dameski umedhoofika; Umejigeuza kukimbia; tetemko limeushika; Dhiki na huzuni zimeupata, Kama za mwanamke katika utungu wake... Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika njia kuu zake, na watu wote wa vita watanyamazishwa katika siku hiyo, asema BWANA wa majeshi. Yeremia 49:24,26
Katika kituo cha matukio, Syria na mji mkuu wake Damascus. Mji huu ni Mkongwe duniani kuendelea kukaliwa. Imetajwa tayari katika kitabu cha kwanza katika Biblia. Katika kutoka kwanza 14:15, 15: 2, unaweza kusoma kuhusu Damascus.
Mji Umetajwa mara 50 katika Biblia. Pia kuna unabii kuhusu Damascus katika Isaya 17: 1: Tazama, Dameski umeondolewa usiwe mji, nao utakuwa chungu ya magofu. "
Je, vita vinavyo endelea hivi sasa vya ISIS vinaweza timiza unabii huu wa Damascus kuwa mji wa gofu?
Urusi ni kama simba hasiye na meno anaunguruma lakini mawindo yake yanapokonywa. Taifa lolote linalotegemea Urusi litakuwa limeshika mwanzi unaomchoma mwenyewe. Sadam alitegemea Urusi mwisho wake Urusi ikaishia kumtazama kitanzini.
Watu wengi wanajua kuwa Urusi imefanikiwa kumsaidia Assad lakini hali ni tete uko Syria, maana Marekani ana mkono mrefu hapo, na Syria na Urusi wameshindwa kuhimili mkono wake. Urusi amechanganyikiwa na kuishia kushambulia wapinzani wa Assad ovyo ovyo kwa ndege, kiasi cha UN kumuonya hasitishe mashambulizi yanayoua raia wengi.
Syria itaanguka tu ingawa mpaka sasa imeshapoteza nguvu kwa asilimia kubwa imebakia kusaidiwa tu.
Shalom
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

TRENDING NOW