Monday, October 5, 2015

Freemasonry: The worship of Lucifer, SATAN

Freemasonry
The worship of Lucifer, SATAN
Part 1 of 5

33RD_Degree_2_Seattle.gif (6519 bytes)From the Analogy ("The Matrix") page you learned that certain Masonic authors praise Lucifer.  And it doesn't stop there.  It extends to their symbolism as well. It is important to STRESS that not all Masons worship Lucifer, only the top 5% do.
A majority of this page on Freemasonry was taken from Masonic books that were published by Masonic Publishing Companies.   Most of these writings were kept secret. Biblical admonition has been taken carefully, comparing Masonic teachings to the Holy Bible. In I John 4:1, we read: "Beloved, believe not every spirit, but try (test) the spirits whether they are of God: because many false prophets are gone out into the world." We see that any religious teaching that does not conform to Scripture is from a "false prophet."

Many people still do not understand the importance of studying this subject to its logical conclusion.  Their spiritual freedom is at stake.  Remember two things about Masonry: 1) Superior Masons deliberately lie to their fellow Masons, as those Masons "deserve to be mislead;" 2) Explanations given to 95% of all Masons are wrong.  This quote from Masonic author, Carl Claudy sums it all up: "Cut through the outer shell and find a meaning; cut through that meaning and find another; under it, if you dig deep enough, you may find a third, a fourth -- who shall say how many teachings?"  Many who are in Masonry are not aware that they are lied to.  Finally, remember Albert Pike's bold assertion in Morals & Dogma, that "Masonry is identical to the ancient Mysteries," which means that all their teachings in all their books are precisely the same as the Ancient, Pagan, Satanic Mysteries. [p. 624, teachings of the 28th Degree]

Of course these top 5% call Jesus Christ an "inferior god," they never, ever mention Him in their teachings or their rituals.  This shouldn't surprise you since the Pope carries a bent Satanic cross as seen on another page which shames Christ on the cross.
Freemasons used Luciferic symbols within the layout of government center Washington D.C.   Freemasons worship Lucifer, the Light-Bearer.  Lucifer and Satan are biblically the same individual, Freemasonry is really the worship of Satan. By quoting their own sources and depicting the symbols in which they use, this claim is proven.
Freemasonry gives itself away more through its symbols than it does in its writings.  You saw in the analogy page of "The Matrix" that high level Masons praise Lucifer.  It is within these writings the "smoking gun" will be found, proof that Masons worship Satan.  Once this is comprehended, you will understand why "they" have been trying to keep this all secret.  If people really understood that Masonry is the worship of Satan, no one in their right mind would join.  Not only that but people would demand that this organization be outlawed.   You have a continuous public relations campaign promoting the lie that Freemasonry is not a religion, and is just a "good works social organization."   As quoted above, you have secrets within secrets.

LUCIFER PRAISED AS THE LIGHT-BEARER OF FREEMASONRY

Thursday, September 24, 2015

OVER 700 PEOPLE DEAD IN MECCA: Graphic photos from Mecca stampede


Over 700 people died today in Hajj stampede in Mecca. Thousands were walking to the 'stoning of the devil' ritual when a sudden surge in the crowd caused many to fall. What caused the surge is not known. It's the worse since 1990. AFP just released some gruesome photos from the incident. 


Wednesday, September 23, 2015

Mabinti wa Allah

Mabinti wa Allah


Mara nyingi Waislam wamekuwa wepesi kuwaambia watu wengine kuwa Mungu ameruhusu Biblia kupotoshwa. Kitu wanachodokeza ni kuwa Kurani leo hii ni neno la Mungu lenye kuaminika wakati ambapo Biblia sivyo. Biblia ina maandiko yanayotofautiana mengi yenye tofauti ndogo, lakini ushahidi wa mabadiliko ya mafundisho hauna uzito. Kurani ina ushahidi mkubwa zaidi wa kupotoshwa kwa mujibu wa Ubai, aya zilizobatilishwa‘Uthman, na matatizo mengine ya Kurani. Hata hivyo, tofauti kubwa zaidi ya mafundisho ya Kurani, iliyoletwa na Waislam wenyewe, ni "mabinti wa Allah."

Muhtasari

Tovuti ya Kikristo http://answering-islam.org/Responses/Saifullah/sverses.htm inasema, "Moja ya matukio yenye kuaibisha zaidi kwenye maisha ya Muhammad lilitokea wakati Shetani alipoweka maneno yake kwenye mdomo wa Muhammad. Muhammad alisema maneno ya Shetani kama neno la Mungu. Tukio hili limethibitishwa kwa maandishi na waandishi kadhaa wa Kiislam wa kale na limeongelewa kwenye Hadithi na Kurani. Waislam wa miaka iliyofuata, kwa kujisikia aibu kuwa nabii wao aliyejitangaza mwenyewe amesema maneno ya Shetani, walikana kuwa tukio hili lilitokea. Visingizio na kukana kwingi vimekuwa vikitolewa na hawa Waislam wa miaka iliyofuata ili kulifunika kosa lenye kuhusisha dhambi la Muhammad.
Ni muhimu ikafahamika tena kuwa tukio la ‘Aya za Shetani’ si jambo ambalo limetungwa na watu wasiokuwa Waislam. Tukio hili limerekodiwa na vyazo vya kale zaidi vya Kiislam vilivyokuwepo wakati wa uhai wa Muhammad. Mtu yoyote asifikiri kuwa jambo hili ni hadithi iliyotungwa na watu wenye kuupinga Uislam. Ni kisa kinachopatikana moja kwa moja kwenye rekodi za kale za Kiislam.
Hili moja ya masomo yenye kubishaniwa zaidi kwenye Uislam. Shetani alimsababishia Muhammad kunena maneno yake (Shetani) kama maneno ya Mungu."

Je Kurani Ilisema Nini Mwanzoni?

Sura ya Nyota (Sura 53) mistari ya 19-20 inasema, "Je umemwona Lat, na ‘Uzza, Na mwingine, (mungu mke) wa tata, Manat?"

Allah alikuwa maarufu huko Arabia kabla ya kuja kwa uislam, kama mungu aliyekuwa na mabinti watatu: al-Lat, al-Uzza, na Manat. (Kumbuka kuwa al- inamaanisha ‘yule’, kwa Kiingereza "the".)

Waandishi wanne wa mwanzo wa maisha ya Muhammad waliandika kuwa awali aya hizi zilifuatwa na:

"Hawa ni mawinchi (wasuluhishi) ambao maombi yao yanapaswa kutumainiwa"

Tafsiri: Mabinti wa Allah walifikiriwa kuwa viumbe wa mbinguni wenye kuomba kwa ajili ya wengine. Mawinchi marefu ya Kinumidia ilikuwa ni sitiari yao. Maneno mbadala ya "inatakiwa kutumainiwa" (turtaja) ni "imekubaliwa kwa kuthibitishwa" (turtada). (Kutoka kwenye tafsiri ya Alfred Guillaume ya The Life of Mohammed, iliyoandikwa na Ibn Ishaq, uk.166.

Baadaye, kifungu hiki kiliondolewa na kifungu kifuatacho kiliwekwa badala yake:

"Nini! Kwako wewe mwenye jinsia ya kiume, Na kwake (mwanaume), mwanamke? Tazama, hakika mgawanyo huu hautakuwa wa haki kabisa." (aya za 53:21-22 leo)

Tafsiri: Wale wanaoamini kuwa Allah alikuwa na mabinti watatu hawakuntendea haki Allah, kwa sababu walipendelea watoto wa kiume ingawa walisema kuwa Allah alikuwa na wasichana tu.

Hizi ndizo ambazo zimeitwa "Aya za Shetani." Katika nyakati za sasa Salmon Rushdie alitumia msemo huu tu kwenye kichwa cha riwaya yake ya kubuniwa na isiyohusika na aya hizi, na andiko hili halikiongelei kisa hiki cha kisasa. Kwa upande wa Aya za Sheatani za asili, Muislam au mtu mwingine asiyekuwa Muislam mwenye kutazama jambo hil bila upendeleo anawezaje kujua aya ambazo zilikuwemo toka awali? Sehemu iliyobaki ya andiko hili inatoa ushahidi wa moja kwa moja na ule usio wa moja kwa moja kuwa Aya za Shetani zilikuwemo asilia, na mapingamizi tisa ya Kiislam.

Waandishi Wanne wa Maisha ya Muhammad: Ushahidi wa Moja kwa Moja

Ingawa si kila kitu Waislam wa kale walichosema kuhusu Muhammad kilikuwa kweli, wanazuoni wa kiislam wana uwezekano mkubwa zaidi wa kukubali mambo ambayo Muhammad aliyasema ambayo yameshuhudiwa na vyanzo vitatu au zaidi. Tunajua kuwa Aya za Shetani hazikutokana na vyanzo visivyokuwa vya kiislam, lakini kutoka wanazuoni wanne tofauti wa kale wa kiislam ambao walikuwa waandishi wa maisha ya Muhammad. Kumbuka kuwa watatu kati ya waandishi hawa walisimulia maisha ya Muhammad hata kabla ya mkusanyiko mashuhuri wa Hadithi ambao dhehebu la Kiisuni limejengeka juu yake.

Al-Wahidi/Wakidi (aliyekufa mwaka 207/823 BK) aliandika Asbab al-Nozul. "Kwenye siku fulani, wakuu wa Maka, walikusanyika kwenye kundi pembeni mwa Kaaba, walijadili kama ilivyo kawaida ya mambo ya mji wao; wakati Muhammad alipotokea na, kukaa karibu yao kwa namna ya kirafiki, alianza kusema sura 53 huku wakimsikia…. ‘Na usimwangalie Lat na Ozza, na Manat wa tatu zaidi?’ Alipofika kwenye aya hii, mwovu alipendekeza njia ya kujieleza mawazo yake ambayo iliitawala nafsi yake kwa siku nyingi; na aliweka mdomoni mwake maneno ya upatanisho na masikilizano, ufunuo aliokuwa anausubiri kwa hamu kubwa sana toka kwa Mungu, yaani; ‘Hawa ni wanawake waliotukuka, na hakika maombezi yao yanatakiwa kutumainiwa. ’ Wakoreish walishangazwa na kufurahishwa na kukubaliwa huku kwa miungu yao; na kama Mahomet alivyoimalizia Sura kwa maneno ya hitimisho ‘Kwa hiyo inama mbele ya Mungu, na mtumikie’ kusanyiko zima lilijiinamisha kwa moyo mmoja chini na kuabudu. … Jioni Gabriel alimtembelea; na nabii aliisema Sura hiyo kwake. Na Gabriel alisema, ‘Umefanya kitu gani? Umeyarudia mbele ya watu maneno ambayo sikuwahi kukupa’. Kwa hiyo Muhammad alisononeka zaidi …"

Ibn Sa’ad/Sa’d (aliyekufa mwaka 230/845 BK), aliifahamu kazi ya al-Wahidi lakini yeye mwenyewe alikuwa mwandishi wa habari za maisha ya watu aliyeandika kitabu chenye juzuu 15 kiitwacho Kitab al Tabaqat al Kabir.

Ibn Isaq/Ishaq (aliyekufa mwaka 145/767 au 151/773 BK) alikuwa Msuni wa mlengo wa Kishafi ambaye baadaye alianzisha shule yake mwenyewe iliyodumu kwa muda mfupi. Aliandika kitabu kiitwacho Sirat Rasullallah (Maisha ya Nabii wa Allah). "[Wahamiaji] walibakia sehemu ileile waliyokuwepo [Ethiopia] hadi waliposikia kuwa watu wa Maka wameukubali Uislam na wamejinyenyekeza. Hii ilikuwa ni kwa sababu sura ya Nyota [Sura 53] ilikuwa imetumwa kwa Muhammad na mtume aliinena. Mtu mmoja Muislam na mwenye kuamini miungu wengi alisikiliza kimya hadi alisema maneno haya ‘Je umemwona al-Lat na al-uzza?’ Walimsikiliza kwa uangalifu sana wakati waumini walimwamini [nabii wao]. Baadhi yao waliiasi imani yao walipoisikia ‘saj’ ya Shetani na kusema, ‘Kwa uwezo wa Allah tutawatumikia (mawinchi) ili kwamba watulete karibu na Allah.’ Shetani alifundisha aya hizi mbili kwa kila mtu aliyekuwa anaamini miungu wengi na ndimi zao zilizielewa kwa urahisi. Jambo hili lilimsunbua Mtume hadi Gabriel alipokuja kwake na kulalamika …." (Anaelezea mlolongo wa kuenea kuwa Yazid bin Ziyad-> Muhammad bin Ishaq -> Salama -> Ibn Hamid -> ibn Isaq

Ibn Jarir al-Tabari (aliyekufa mwaka 923 BK) alikuwa Msuni wa mlengo wa Kishati aliyeandika kitabu chenye juzuu 38 cha Kiislam cha Historia ya ulimwengu hadi mwaka 915 BK. Alipewa jina la "shehe wa wafafanuaji." Anaandika kwenye juzuu ya 6 uk.108-110, "Mjumbe wa Mungu alipoona jinsi kabila lake lilivyomkataa na kuhuzunishwa alipowaona wanauacha ujumbe aliowaletea toka kwa Mungu, alitamani moyoni mwake kuwa kitu chochote kimjie toka kwa Mungu ambacho kitampatanisha na kabila lake …. Na alipoyafikia maneno: ‘Je umewafikiria al-Lat na al-Uzza na Manat, wa tatu, Yule mwingine?’ Shetani alimlaumu, kwa sababu ya midahalo yake ya ndani na vitu alivyokusudia kupeleka kwa watu wake, maneno: ‘Haya ni mawinchi yanayopaa juu zaidi; hakika maombezi yao hupokelwa kwa kuthibitishwa [kwa mpokezano: kuhitajiwa au kutegemea].’ Waquraysh waliposikia hili, walifurahi sana na kupendezwa na namna alivyosema kuhusu muingu yao, na walimsikiliza, wakati Waislam, wakiwa wanamwamini kabisa nabii wao kuhusu ujumbe aliouleta kutoka kwa mungu, hawakumshuku kuwa amepotoka, anaota, au kafanya makosa. … Kisha [baadaye] Gabriel alikuja kwa Mjumbe wa Mungu na kusema, ‘Muhammad, umefanya nini? Umenena kwa watu kitu ambacho sikukuletea toka kwa Mungu …’"

Wanazuoni wa Kiislam wa miaka ya mbele waliosema jambo hili:
 Abu Ma’shar kutoka Chorassan (787-885 BH)
 Ibn Abi Hatim
 Ibn al-Mundhir
 Ibn Hajar from Asqalaan (773-852 BH)
 Ibn Mardauyah
 Musa ibn ‘Uqba
 Ufafanuzi mashuhuri sana wa Zamakhshari wa Sura 22:52. (1070-1143 BH)
Wanazuoni sita ni kwa mujibu wa kitabu kiitwacho The Book of the Major Classes, kilichotafsiriwa na S. Moinul ‘Haq.

Ushahidi usiokuwa wa moja kwa moja wa Aya za Shetani:
Kurani na Hadithi

Bukhari alikufa karibu na mwaka 870 BK (hata miaka mitatu baada ya vyanzo vitatu kati ya vinne vilivyoorodheshwa.) Wakati Muhammad alipoisema Sura ya Nyota, wapagani na Waislam walisujudu. (Bukhari juzuu ya 3 kitabu cha 19 na.173, uk.100 juzuu ya 3 kitabu cha 19, na.176, uk.101; juzuu ya 6 kitabu cha 60 na.385-386 uk.364-365; Abu Dawud juzuu ya 1 kitabu cha 2 sura ya 481 na.1401, uk.369). Wapagani hawasemekani kusujudu kwa ajili ya Muhammad kusema maneno mengine yoyote, ni kwa nini wakubaliane kiasi hiki na sura hii, hasa kwa vile Bukhari na Abu Dawud hawasemi kuwa hao wapagani waliwahi kuwa Waislam, na hii ilikuwa kabla ya vita na hawa wapagani wa Maka!

Pia, Sura 22:52 inasema, "Hatukuwahi kumtuma mtume au nabii Kabla yako, lakini, alipoumba nia, Shetani alimtupia (ubatili) kiasi kwenye nia yake: lakini Mungu atafuta kitu chochote (batili) ambacho Shetani anatupia ndani, na Mungu atafanya dhahiri (na kuthibitisha) Ishara Zake…"

Sura 17:73-75 inasema, "Na lengo lao lilikuwa kukujaribu na kukupeleka mbali na jambo tulilolifunua kwako, kuweka badala yake kitu tofauti kabisa kwa kutumia jina letu: (Kwa ajili hiyo), tazama! Watakuwa wamekufanya kuwa rafiki (yao)! Na je hatujakupa wewe, ungeweza kuelekea upande wao kiasi. Katika hali hiyo tulipaswa kukufanya uonje mara mbili (ya adhabu) kwenye maisha haya, na kiasi kama hichohicho mautini: na zaidi ya hapo usingepata mtu wa kukusaidia dhidi yetu!"

Tuesday, September 22, 2015

PICHA 10 TUKIO LA MAKANISA 3 KUCHOMWA MOTO BUKOBA

Makanisa yaliyochomwa moto ni Pentecostal Assemblies of God (PAG) kata bakoba eneo la buyekera,Living Water International na Evangelical Assemblies of God (EAGT) kata ya Kibeta yote ya mjini Bukoba. Chanzo chake hakijafahamika ambapo wachungaji na viongozi wa kiroho wanaomba vyombo vya dola kuwabaini wahusika.

kamanda wa polisi mkoani kagera Augstine Oromi amedhibtisha kutokea kwa tukio hilo na amemweleza mwandishi wa mtandao huu kuwa yupo katika ziara ya kazi wilayani ngara hivyo atatoa taarifa baadaye.

Matukio ya makanisa kuchomwa yameshamiri katika manispaa ya bukoba ambapo hili ni tukio la sita kwa kipindi cha mwaka mmoja










Saturday, September 12, 2015

UTATA: NUHU WA QURAN NI TOFAUTI NA NUHU WA BIBLIA

Ndugu Msomaji:
Siku zote Waislam huwa mnatutambia kuwa, Quran ni kitabu kilichoeleza kila kitu, ni kitabu ambacho kinajitosheleza, kitabu ambacho kimeshuka kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kuikandia BIBLIA, kuwa haitokanani na Mungu, sasa nitatoa aya mbili kutoka Katika BIBLIA, na kisha aya 2 kutoka ndani ya Quran, kisha nitawauliza swali,

GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA BIBLIA:Mwanzo 7:6 Naye Nuhu alikuwa mtu wa miaka mia sita hapo hiyo gharika ya maji ilipokuwa juu ya nchi.
BIBLIA ambayo mnasema haitokani na Mungu, imesema kuwa, Nuhu, alikuwa ni mwenye Umri wa miaka mia sita (600) GHARIKA lilipotokea, pia ikaeleza miaka ya NUHU baada ya Gharika.
Mwanzo 9:28 Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.

NUHU ALIKUFA NA MIAKA MINGAPI?29 Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
Tunaambiwa na BIBLIA kuwa, Nuhu aliishi miaka mia tatu na hamsini (350) baada ya gharika ya maji, akafa akiwa na miaka mia tisa na hamsini (950) HIYO NDIYO MIAKA ya maisha yote ya NUHU hakuishi zaidi ya miaka hiyo, sasa twende Quran kisha niulize swali.

GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA QURAN?Quran 29 وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَى قَوْمِهِ فَلَبِثَ فِيهِمْ أَلْفَ سَنَةٍ إِلَّا خَمْسِينَ عَامًا فَأَخَذَهُمُ الطُّوفَانُ وَهُمْ ظَالِمُون
َ14. Na bila shaka tulimpeleka Nuhu kwa watu wake na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka hamsini, basi mafuriko yakawaangamiza hali walikuwa madhalimu.

فَأَنجَيْنَاهُ وَأَصْحَابَ السَّفِينَةِ وَجَعَلْنَاهَا آيَةً لِّلْعَالَمِين
َ15. Na tukamuokoa yeye na watu wa (ndani ya ) safina, na tukaifanya (iwe mazingatio kwa walimwengu).

MADA KAMILI:BIBLIA imesema, Gharika limetokea Nuhu akiwa na miaka 600 Quran inasema, Gharika la Nuhu limetokea akiwa na miaka 950, sawa na miaka ya kufa kwa Nuhu, kwa mujibu wa BIBLIA, Biblia imesema, Nuhu akaishi miaka 350 baada ya Gharika, akafa na miaka 950 sawa na miaka ya gharika la Nuhu wa Ndani wa Quran.

MASWALI:-
1. Kwa kuwa ndani ya Quran, Nuhu alikuwa na miaka 950 Ndipo gharika likaja, na Biblia imesema ni miaka 600 gharika lilipokuja, na akafa akiwa na miaka 950 Sasa kwa mujibu wa Quran, Nuhu aliishi miaka mingapi kutoka katika Miaka hiyo 950 ya gharika?
2. au alikufa mwaka huo huo wa Gharika, akiwa na miaka hiyo 950 tuliyoambiwa alikuwa nayo wakati wa gharika ndani ya Quran?

NB. Majibu yatokane na Quran, tu kitabu ambacho mnatuambia ni cha Mungu, kama hakijitoshelezi, semeni, niwape ruhusa mtumie hata magazeti, na majarida.

Imeratibiwa na Abel Suleiman Shiliwa

For Max Shimba Ministres 

By Permission 2015

TAARIFA KUHUSU AJALI ILIYOTOKEA KWENYE MSIKITI MKUU WA MECCA SAUDI ARABIA

Hii taarifa imegusa Vichwa vya Habari vya Vyombo vingi vya habari Duniani, inahusu ajali ambayo imetokea wakati watu wakiwa ndani ya Msikiti Mtakatifu wa Mecca, Saudi Arabia ambako waumini wengi wa Dini ya Kiislamu huwa wanakwenda kwa ajili ya Hijjah.Ajali hiyo inahusisha winch kubwa ambalo lilikuwa likitumiwa kwenye ujenzi eneo la jirani na Msikiti huo kuangukia Msikiti huo, ambapo kwa wakati huo kulikuwa na watu zaidi ya 800 wakiendelea na sala ndani ya Msikiti.
Mecca II
Kumekuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa watu wanaoenda kwenye Msikiti huo kutokana na maeneo yanayozunguka Msikiti kuna majengo mengi yanayoendelea kujengwa na kukarabatiwa pamoja na Msikiti wenyewe kufanyiwa ukarabati wa upanuzi ili kuweza kungiza watu wengi zaidi.
Mecca
Mpaka sasahivi Ripoti zinaonesha zaidi ya watu 100 wamefariki, wengine zaidi ya 200 wamepata majeraha na Mamlaka za Mji huo wanasema sababu hasa za winch hilo kuanguka inatokana na upepo mkali pamoja na mvua kubwa.

Saturday, August 22, 2015

YESU NI UPENDO (SEHEMU YA KWANZA)

Shetani anataka tuamini nini kuhusu jinsi Yesu anavyotuona, lakini Yesu anatuhakikishia nini?
Hata hivyo, swali muhimu linazuka: Je, Mungu anampenda kila mmoja wetu?
Baadhi ya watu wanakubali kwamba Mungu anawapenda wanadamu kwa ujumla kama andiko la Yohana 3:16 linavyosema. Lakini wanahisi hivi: ‘Mungu hawezi kamwe kunipenda mimi.’ Shetani Ibilisi anataka sana tuamini kwamba Yesu hatupendi wala hatuthamini. Kwa upande mwingine, Yesu anatuhakikishia kuwa anamthamini kila mmoja wa watumishi wake waaminifu hata kama tunafikiri hatupendwi au hatuthaminiwi.

Kwa mfano, fikiria maneno ya Yesu kwenye Mathayo 10:29-31. Yesu alitoa mfano huu ili kuonyesha kwamba wanafunzi wake wana thamani: “Je, shore wawili hawauzwi kwa sarafu ya thamani ndogo? Na bado hakuna hata mmoja wao atakayeanguka kwenye ardhi bila Baba yenu kujua. Lakini nywele zenyewe za kichwa chenu zimehesabiwa zote. Kwa hiyo msiwe na hofu: nyinyi ni bora zaidi kuliko shore wengi.” Hebu fikiria jinsi wasikilizaji wa Yesu katika karne ya kwanza walivyoyaelewa maneno hayo.

Katika siku za Yesu, shore alikuwa ndege wa bei rahisi sana aliyenunuliwa ili kuliwa. Mtu aliyelipa sarafu moja ya thamani ndogo sana, alipewa shore wawili. Lakini kulingana na andiko la Luka 12:6, 7, baadaye Yesu alisema kwamba mtu aliyelipa sarafu mbili, alipewa shore watano badala ya shore wanne. Shore mmoja aliongezwa kana kwamba hakuwa na thamani yoyote. Huenda ndege hao hawakuwa na thamani machoni pa wanadamu, lakini Muumba aliwaonaje? Yesu alisema: “Hakuna hata mmoja wao [hata yule aliyeongezwa] hupata kusahaulika mbele ya Mungu.” Sasa huenda tumeanza kuelewa alilomaanisha Yesu. Ikiwa Mungu anamthamini sana shore mmoja, namna gani mwanadamu! Kama Yesu alivyosema, Mungu Baba anatujua vizuri sana. Kwani, hata nywele za kichwa chetu zimehesabiwa zote!

Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba Yesu hakutia chumvi aliposema kwamba nywele za kichwa chetu zimehesabiwa?
Huenda wengine wakafikiri kwamba Yesu alitia chumvi. Hata hivyo, hebu fikiria ufufuo. Ni lazima Mungu Baba awe anatujua vizuri sana ili aweze kutuumba upya! Anatuthamini sana hivi kwamba anakumbuka kila jambo, hata chembe zetu za urithi, kumbukumbu, na ujuzi wetu wote. Kichwa cha mtu huwa na nywele 100,000 hivi, kwa hiyo kuhesabu nywele za vichwa vyetu ni jambo rahisi sana ikilinganishwa na kukumbuka mambo hayo yote. Bila shaka, maneno hayo ya Yesu yanatuhakikishia kabisa kwamba Mungu Baba anamjali kila mmoja wetu.

Kisa cha Mfalme Yehoshafati kinaonyeshaje kwamba Mungu hutafuta mema ndani yetu ingawa sisi si wakamilifu?
Biblia hufunua jambo lingine linalotuhakikishia kwamba Mungu anatupenda. Yeye hutafuta na huthamini mema yaliyo ndani yetu. Kwa mfano, fikiria Mfalme Yehoshafati aliyekuwa mwema. Mfalme huyo alipotenda jambo la kipumbavu, nabii wa Mungu alimwambia hivi: “Kwa ajili ya hayo ghadhabu i juu yako itokayo kwa BWANA.” Ulikuwa ujumbe wenye kuogofya kama nini! Lakini ujumbe wa Mungu haukukomea hapo. Uliendelea kusema hivi: “Walakini yameonekana mema ndani yako.” (2 Mambo ya Nyakati 19:1-3) Kwa hiyo, hasira adilifu ya Mungu haikumzuia asione “mema” yaliyokuwa ndani ya Yehoshafati. Inatia moyo sana kujua kwamba Mungu wetu hutafuta mema ndani yetu hata ingawa sisi si wakamilifu.

Kumbuka kuwa Yesu anakupenda.

Max Shimba

Max Shimba Ministries @ 2015

YESU NI UPENDO (SEHEMU YA PILI)

Huruma ni sehemu nyingine ya upendo wa Yesu.

Huruma ni nini? Katika Biblia, huruma na rehema zinahusiana sana. Maneno kadhaa ya Kiebrania na Kigiriki yanadokeza sifa ya huruma yenye upendo. Kwa mfano, mara nyingi kitenzi cha Kiebrania ra·chamʹ hutafsiriwa “onyesha rehema” au “sikitikia.” Neno hilo la Kiebrania, ambalo Yesu anatumia kujihusu, linahusiana na neno linalomaanisha “tumbo la uzazi” linaloweza kufasiriwa kuwa “huruma ya mama.”

Biblia inatumia hisia ambazo mama huwa nazo kwa mtoto wake mchanga kutufundisha kuhusu huruma ya Yesu. Andiko la Isaya 49:15 linasema: “Je! mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie [ra·chamʹ] mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.” Ni vigumu kuwazia kwamba mama anaweza kusahau kumnyonyesha na kumtunza mtoto wake mchanga. Kwa kweli, mtoto mchanga ni dhaifu; anahitaji kupendwa na kutunzwa na mama yake usiku na mchana. Ingawa hivyo, inasikitisha kupata habari kuhusu akina mama wanaowatupa watoto wao, hasa katika ‘nyakati hizi za hatari.’ (2 Timotheo 3:1, 3) “Lakini mimi sitakusahau wewe,” atangaza Mungu. Huruma nyororo ya Yesu ni yenye nguvu zaidi ya hisia yenye nguvu tunayoweza kuwazia, yaani, huruma ambayo kwa kawaida mama humwonyesha mtoto wake mchanga.

Waisraeli walipatwa na nini katika nchi ya Misri ya kale, naye Mungu aliitikiaje kilio chao?
Mungu huonyeshaje sifa ya huruma akiwa kama mzazi mwenye upendo? Sifa hiyo ya huruma inaonekana wazi kutokana na jinsi alivyolitendea taifa la Israeli la kale. Kufikia mwisho wa karne ya 16 K.W.K., mamilioni ya Waisraeli waliteswa sana walipokuwa watumwa huko Misri. (Kutoka 1:11, 14) Waisraeli walimlilia Mungu awasaidie walipokuwa wakiteseka. Je, Mungu mwenye huruma nyororo aliitikiaje?

Mungu aliwahurumia. Akasema: “Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao . . . maana nayajua maumivu yao.” (Kutoka 3:7) Mungu hangeweza kuwatazama watu wake wakiteseka au kusikia vilio vyao na asiwahurumie. Yehova ni Mungu mwenye hisia-mwenzi. Nayo hisia-mwenzi, yaani, sifa ya kuguswa moyo na uchungu wa wengine, inahusiana sana na huruma. Lakini Mungu hakuwahurumia tu watu wake; alichochewa kuwasaidia. Andiko la Isaya 63:9 linasema: “Kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe.” Mungu wa Israel aliwaokoa Waisraeli kutoka Misri kwa “mkono hodari.” (Kumbukumbu la Torati 4:34) Baadaye, aliwalisha kimuujiza na kuwapa nchi yenye rutuba.

(a) Maneno ya mtunga-zaburi yanatuhakikishiaje kwamba Mungu anamjali sana kila mmoja wetu? 
(b) Mungu hutusaidia katika njia gani mbalimbali?
Mungu hawahurumii watumishi wake tu wakiwa kikundi. Mungu wetu mwenye upendo anamjali sana kila mmoja wetu. Anajua kabisa mateso yoyote yanayoweza kutupata. Mtunga-zaburi alisema: “Macho ya BWANA huwaelekea wenye haki, na masikio yake hukielekea kilio chao. BWANA yu karibu nao waliovunjika moyo, na waliopondeka roho huwaokoa.” (Zaburi 34:15, 18) Mungu anamsaidiaje kila mmoja wetu? Si lazima aondoe jambo linalofanya tuteseke. Lakini yeye amewapa maandalizi tele wale wanaomwomba msaada. Neno lake lina mashauri yanayofaa ambayo yanaweza kutusaidia sana. Katika kutaniko, Mungu ameweka waangalizi wanaostahili kiroho, ambao hujitahidi kuwa na huruma kama yeye wanapowasaidia waabudu wenzao. (Yakobo 5:14, 15) Akiwa “Msikiaji wa sala,” Mungu huwapa “Roho Mtakatifu wale wanaomwomba.” (Zaburi 65:2, NW; Luka 11:13) Maandalizi hayo yote ni uthibitisho wa “huruma nyororo ya Mungu wetu.”—Luka 1:78.

Utaitikiaje upendo wa Yesu?
Je, si jambo lenye kusisimua kutafakari juu ya upendo wa Baba yetu wa mbinguni? Katika makala iliyotangulia, tulikumbushwa kwamba Baba Mungu ameonyesha nguvu, haki, na hekima yake kwa njia ya upendo ili kutunufaisha. Na katika makala hii tumeona kwamba kwa njia ya pekee, Mungu ameonyesha upendo wake moja kwa moja kwa kila mmoja wetu na kwa wanadamu kwa ujumla. Sasa kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza, ‘Nitaitikiaje upendo wa Yesu?’ Na uitikie kwa kumpenda kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, kwa akili yako yote, na kwa nguvu zako zote. (Marko 12:29, 30) Maisha yako ya kila siku na yaonyeshe kwamba una tamaa ya kutoka moyoni ya kumkaribia Mungu hata zaidi. Na Yesu, Mungu ambaye ni upendo, na akukaribie hata zaidi—milele!—Yakobo 4:8.
Mungu awabariki sana.

Yesu anakupenda.

Max Shimba

Max Shimba Ministries @ 2015.

YESU NI UPENDO (SEHEMU YA TATU)

Yesu ni Mungu Aliye “Tayari Kukusamehe Dhambi”
Tunapofanya dhambi tunakuwa na hisia gani zenye kulemea, lakini tunaweza kunufaikaje na msamaha wa Yesu?

Tunapofanya dhambi, sisi huona aibu, hukata tamaa, na kuhisi hatia na huenda hali hiyo ikafanya tufikiri kwamba hatustahili kabisa kumtumikia Mungu. Hata hivyo, kumbuka kwamba Mungu ‘amekuwa tayari kusamehe.’ (Zaburi 86:5) Naam, Yesu anaweza kutusamehe dhambi zetu tunapotubu na kujitahidi kabisa kutozirudia. Ona jinsi Biblia inavyofafanua sehemu hiyo yenye kuvutia ya upendo wa Yehova.

Yesu Kristo anayo amri na mamlaka ya kusamehe dhambi

Kuna jambo lililowahi kutokea hadi likawashangaza watu; hebu fatilia kisa hiki. Biblia Takatifu inasema kwamba:

“Wakaja watu wakimleta mtu mwenye kupooza, anachukuliwa na watu wanne. Na walipokuwa hawawezi kumkaribia (Yesu) kwa sababu ya makutano, waliitoboa dari pale alipokuwapo; na wakiisha kuivunja wakalitelemsha godoro alilolilalia yule mwenye kupooza. Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako. Na baadhi ya waandishi waliokuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao, Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu?

Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu? Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?

Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi – Akamwambia yule mwenye kupooza,

Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako.
Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastajabu wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Namna hii hatujapata kuiona kamwe.” (Marko 2:3-12)

Kwa Wayahudi uponyaji haukuwa kitu kigeni kwao kwani hata manabii enzi za Agano la Kale nao walitumia nguvu za Mungu kuponya wagonjwa; lakini, jambo lililoonekana geni kwa Wayahudi ni kusikia Yesu amesema 
“...Umesamehewa dhambi zako...” (Marko 2:5) Kauli hiyo ya Yesu iliwafanya waone kwamba Yesu AMEKUFURU kwa maana mwenye mamlaka ya kusamehe dhambi ni Mungu pekee. Watu hao walidhani Yesu amekufuru kwa sababu hawakujua kuwa Yesu ni Mungu ingawa alikuwa ameuvaa mwili wa kibinadamu kama sisi.

Ukimpokea Yesu; anakusamehe dhambi zako zote. Haijalishi umetenda dhambi nyingi kiasi gani; haijalishi hali uliyonayo hivi sasa. Fahamu kwamba Yesu anakupenda. Neno la Mungu linasema kwamba:

“...asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji...” (Isaya 1:18)

Mungu huweka dhambi zetu mbali nasi kadiri gani?
Mtunga-Zaburi Daudi alitumia usemi mwingine ulio wazi zaidi kufafanua msamaha wa Mungu: “Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi.” (Zaburi 103:12, italiki ni zetu.) Mashariki ni mbali kadiri gani kutoka magharibi? Katika maana fulani, sikuzote mashariki huwa mbali kabisa na magharibi; pande hizo mbili haziwezi kamwe kukutana. Msomi mmoja anasema kwamba usemi huo unamaanisha “mbali iwezekanavyo; mbali kabisa.” Maneno ya Daudi yaliyoongozwa na Roho ya Mungu yanatuambia kwamba Mungu anapotusamehe, anaweka dhambi zetu mbali kabisa nasi.

Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba Mungu hutuona kuwa safi baada ya kutusamehe dhambi zetu?
Je, umewahi kujaribu kuondoa doa katika nguo nyeupe? Huenda hukufaulu kuondoa doa hilo ingawa ulijitahidi kadiri unavyoweza. Ona jinsi Mungu anavyoeleza msamaha wake: “Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.” (Isaya 1:18, italiki ni zetu.) Usemi “nyekundu sana” unaonyesha kwamba rangi hiyo ni nyangavu.* Rangi “nyekundu” ilikuwa mojawapo ya rangi zilizotiwa kwenye nguo. Hatuwezi kamwe kuondoa doa la dhambi kwa jitihada zetu. Lakini Yesu anaweza kuondoa dhambi ambazo ni nyekundu sana na kuzifanya kuwa nyeupe kama theluji au sufu isiyotiwa rangi. Kwa hiyo, Yesu anapotusamehe dhambi zetu, hatupaswi kuhisi kwamba tuna hatia ya dhambi hizo maisha yetu yote.

Ni katika maana gani Mungu hutupa dhambi zetu nyuma yake?
Hezekia alimwambia Mungu hivi katika wimbo wa shukrani wenye kugusa moyo ambao alitunga baada ya kuponywa ugonjwa wa kufisha: “Umezitupa dhambi zangu zote nyuma yako.” (Isaya 38:17, italiki ni zetu.) Ni kana kwamba Mungu anachukua dhambi za mtenda-dhambi mwenye kutubu na kuzitupa nyuma Yake ambako Hawezi tena kuziona wala kuzikazia fikira. Kichapo kimoja cha kitaalamu kinasema kwamba andiko hilo linaweza kuelezwa hivi: ‘Umefanya iwe ni kana kwamba sikufanya dhambi.’ Je, hilo si jambo lenye kufariji?

Nabii Mika anaonyeshaje kwamba Mungu anapotusamehe Anafutilia mbali dhambi zetu daima dawamu?
Katika ahadi ya urudisho, nabii Mika alieleza usadikisho wake kwamba Mungu Yehova angewasamehe watu wake wenye kutubu: “Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye . . . kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? . . . Nawe utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari.” (Mika 7:18, 19, italiki ni zetu.) Hebu fikiria maana ya maneno hayo kwa watu walioishi nyakati za Biblia. Haingewezekana kupata tena kitu kilichotupwa “katika vilindi vya bahari.” Kwa hiyo maneno ya Mika yanamaanisha kwamba Yesu anapotusamehe, anafutilia mbali dhambi zetu daima dawamu.

Yesu ni Mungu, endapo ukimpokea atakusamehe dhambi zote ulizozitenda. Yesu anakupenda sana. Hebu leo mpe Yesu maisha yako ayatawale; Yesu ataiondoa kiu hiyo ya kutenda dhambi ikufanyayo ushindwe kujizuia kuwaka tamaa mbaya za mwili wako; Yesu atakupatia ulinzi ambao utazuia pepo wachafu wasiingilie maisha yako; Yesu atakubariki na kufungua tumbo lako lililokosa mtoto kwa muda mrefu wote huo unaotaabika hata sasa; Yesu atawarejesha kwako watoto wako ambao wamekataa kukutii hata wametoweka kwako; Yesu atakupatia uzima na kuyaondoa magonjwa yote hayo yanayokutesa hata sasa; Yesu atakubariki na kukupatia uzima wa milele.

Kwa kweli nashindwa kuuelezea kwa ufasaha zaidi upendo wa Yesu juu yako kwa maana wewe ni wathamani kubwa sana mbele za Mungu. Mimi nachoweza kukwambia ni kwamba: Yesu anakupenda tena hataki upotee. Mpe Yesu maisha yako sasa ili ufurahie uzuri wa pendo Lake.

Damu ya Yesu inamamlaka ya kusafisha dhambi zako zote.

Mpokee Yesu sasa na upate msamaha wa dhambi.

Yesu anakupenda.

Max Shimba

Max Shimba Ministries @2015.

YESU NI UPENDO (SEHEMU YA NNE)


Ndugu yangu, wajua yakwamba Yesu Kristo anakupenda ? Wajuwa yakwamba alisulubiwa kwa ajili ya watu wote: Wanaume na Wanawake, Watoto, Vijana na Wazee?  Yesu Kristo alikufa kwa ajili yako.

Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

TAFAKARI: “Yesu anakupenda upeo, amepoteza kila kitu, na kufa kifo cha aibu ili asikupoteze.”


JE, WEWE UPO KATIKA KUNDI HILI?
…Wewe ni mnyanganyi, mwizi, mwongo, muuaji, usiye kuwa na ukweli? Yesu anakupenda na anataka kukuponya.


JE, WEWE UPO KATIKA KUNDI HILI?
…Wewe ni mlozi mkubwa mwenye kutumikia Shetani, tangu ujana wako unazuru wanadamu wengine, unaua watoto, wanawake hata wanaume, unaharibu mavuno, unatawanya magonjwa toka jamaa kwa ingine, unaua hapa na pale.Unapopita ni woga mtupu na kukimbia mbali sababu ya mapepo mabaya yako. Mara na mara unajiuliza nini ulikuja kufanya hapa duniani, ukitafuta kujua sababu ya mabaya yote unayoyatenda. Unajiuliza namna gani uliweza kufikia hapo. Fahamu neno moja tu, hata unaishi mabaya haya yote : Yesu anakupenda na anataka kukuponya.


JE, WEWE UPO KATIKA KUNDI HILI?
…Wewe ni mkoma,tangu miguu hadi kichwani. Ulipoteza vidole, sikio, pua, ukageuka kilema kwa namna fulani; fahamu jambo hili: Yesu anakupenda na anataka kukuponya.


JE, WEWE UPO KATIKA KUNDI HILI?
… Wewe ni msichana, waonekana kuwa ni mrembo sana na wakati wako wote unavunja jamaa za wengine. Unapotosha rafiki zako za darasa, za shule lako, za ofisi ao za mtaa wako. Mara nyingine ulitoa mimba, ulitafuta kupatia wengine sumu, ao uligonganisha wapenzi wako: wamoja wafariki ao wangali wagonjwa sana sababu yako, sababu ya unyofu wako, na sura yako nzuri sana. Sasa wajiuliza mengi kuhusu maisha yako: uliweza kutambua mabaya yote uliyotenda na unajiuliza nini Mungu atakayokutendea.

 Unapatwa na woga wakati unawaza haya yote sababu unaambiwa yakuwa siku moja Mungu atahukumu matendo ya watu.Unaishi katika uasi, unajua ya kwamba JEHENAMU ndiyo inakungojea na unajifariji ukisema kwamba ni maneno yasiyokuwa na msingi hata unasema : Mungu hayuko!



…Wewe ni kijana uliyetenda mambo sawasawa na yale na mwisho ukafikia kusema hivyo. Unajitia kwa mstari ya wale wasiosadiki kuwa Mungu yuko, ili ujitulize.

Ndugu yangu, rafiki yangu, Shetani anakupoteza. Unajuwa ni nini inayokungojea. Hata ikiwa hivyo, ninataka kukujulisha ya kwamba wakati ungali wa kugeuza yale yote, kwani katika upendo wake Mungu alituma Mwana wake wa pekee ili akuondoshe katika maisha yale. Yesu anakupenda, anataka akuokowe kwa damu yake na uwe safi mbele ya Mungu.

…Wewe ni mwanaume, mwanamke, mtoto unayelala kitandani katika hospitali sababu ya ugonjwa, ya msiba wa barabarani, ya ulozi; ili ujue neno hili: Yesu ni karibu yako na anakupenda na anataka akuponye.

… Ulifanya kosa fulani na kwa sasa unapatikana katika mateso ya gereza: Yesu anapatikana hapo kwa kukuponya.
…Wewe ni mtumishi, kiongozi, uliyepata cheo kikubwa kwa njia ya madawa na ulozi, kuua na kusengenya, uongo na vibaruwa vya uongo: ulipita juu ya wengine ili ufikiye pahali ulipo, sasa maneno haya ni mkononi mwako: usifikiliye ni kwa bahati tu. Yesu anakuambia ya kwamba anakupenda hata ulipitia kwa njia hizo. Ulisoma mistari hii na unashangaa ukigundua kwamba hata ukiwa mwenye kutenda mabaya kama hayo, Yesu anakupenda pia.
Sikiliza anayosema Mwokozi wako:


“Watu wenye afia njema hawahitaji muganga, ila wenye ugonjwa tu.. Sikuja kuita wenye haki bali wenye zambi”( Marko 2.17) .
Unasikia hayo? Yesu anasema ya kwamba alikuja kwa ajili ya watu kama wewe.Unaona mlango wa kutoka mahali ulipo sasa, ni Yesu Kristo mwenyewe.


…Mara nyingine wasema: mimi si Muisraeli anayeambiwa maneno hayo ya Yesu ! Mimi ni Muafrika, Muasia,Muamerika…jua ya kwamba maneno hayo ni kwako pia na usikilize asemayo:
“Muniangalie, na muokolewe, miisho yote ya dunia;kwani mimi ni Mungu,na hapana mwengine.” ( Isaya 45:22).


Wasikia zaidi ya hayo? Ulizani kwamba ulifikia mwisho, ukitesa wanadamu wengine, unajisikia hakuna tena kukaribia Mungu. Ulisema haya na yale kuhusu zambi zako. Na Yesu anakuambia:
“Leo kama mtasikia sauti yangu, msifanye migumu mioyo yenu.”( Waebrania 4.7).


Una maneno haya mkononi mwako, jua ya kwamba ndiyo “leo” yako hii na Mungu anasema: Usifanye moyo wako kuwa mgumu.
Kwa kumaliza, Roho Mtakatifu anakupa ujumbe huu:


“Basisisi,! Tutapona namna gani, tusipochunga wokovu mkubwa namna huu?” (Waebrania 2.3).


Ndugu, rafiki, wajua sasa ya kwamba Mungu anakupenda, wajuwa kuwa Mwana wake Yesu ni tayari kukuponya. Haupatikane tena katika kutokujua. Mungu anataka kukufungua macho kwa maneno haya na anasema:


“Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mtu akimwamini asipotee, bali apate uzima wa milele” (Yoane 3.16).


Chaguo ni lako: amini na uokolewe ao kutoamini na kuhukumiwa. Ndiyo, katika neema yake kubwa, Mungu anakuonyesha wazi njia ya kupitia. Anasema:


“Nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; kwa hivi chagua uzima ili uwe hai.” (Kumbukumbu la torati 30.19).
Unapenda kumusikia Mungu? Ama kama asemavyo mtume Paulo:
“Ao unazarau utajiri wa wema wake na saburi na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu unakupeleka kwa toba? Lakini kwa ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya asira kwa siku ile ya asira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu” (Warumi 2.4-5), na inaandikiwa tena “Basi, zamani wakati huu wa ujinga, Mungu hakuangalia ; lakini sasa anaamuru watu wote wa kila mahali watubu. Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki,kwa mtu yule aliyemuweka kwa kazi hii; naye amewapa watu wote hakika ya mambo haya kwa kumfufua toka wafu” (Matendo ya mitume 17.30-31).


Pamoja na mtume Paulo:
“Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kama kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo mpatanishwe na Mungu” (2 Wakorintho 5.20) kabla wakati haujapita.


Pokea upatanishi unaopewa na Mungu. Kwa hivyo unaombwa kukiri makosa yako, ukitambua ya kwamba wewe ni mwenye zambi.

Kumbuka kuwa Yesu anakupenda,

Max Shimba 

Max Shimba Ministries 2015

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW