Friday, August 26, 2016

INJILI INATHIBITISHA KUWA YESU NI MUNGU

Utangulizi
Tafadhali angalia Biblia Takatifu au Fungua Bibilia Takatifu iliyo bure na tamatisho zifuatazo kutoka Taurah (Mwanzo), Zabur (Zaburi) na Ijil (Injili).
Injili inathibitisha ya kwamba Yesu alizaliwa kutoka kwa bikira, hakuwa na makosa, alipelekwa mbinguni na Mungu na atarudi tena. Kulingana na Injili Yesu ni zaidi ya nabii. Yeye ni zaidi ya mtu aliye heshimiwa zaidi, utakatifu na baraka. Umuhimu wake kwa mwanadamu ni zaidi ya mponyaji mkubwa wa wagonjwa.
Utetezi wa Yesu kuwa Mwana wa Mungu:
Ninyi mnachunguza Maandiko mkidhani ya kuwa ndani yake mna uzima wa milele, maandiko haya ndiyo yanayonishuhudia Mimi (Yohana 5:39).
Somo la kweli na Injili sio mafundisho au filosofia, ila ni mtu: Yesu Kristo. Yesu anatupa sisi msingi wa uhusiano wa dharura na uwiano kati yetu na Mungu. Huu uhusiano unafanya kazi kama chanzo cha uhakika na ujasiri.
Kwanini mwanishutumu kwa sababu nilisema ‘Mimi ni Mwana wa Mungu? (Yohana 10:36).
Wakati Injili inazungumza juu ya Yesu kuwa mwana wa Mungu, haisemi ya kwamba Mungu na Mariamu walipata mwana kwa njia ya kibaolojia. Hii ni dhihaka. Hii haiko katika Injili. Mariamu alikuwa bikira (Mathayo 1:18, Luka 1;34-35) Yesu ni mwana wa Mungu, aliyekuwepo toka mwanzo.
Vitu vyote vimekabidhiwa mikononi Mwangu na Baba. Wala hakuna amjuaye Mwana ila Baba, wala amjuaye Baba ila Mwana na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia (Luka 10:22).
Mungu Baba ni Bwana wa mbingu na dunia. Kwa hili dai kamili kama kwa ufahamu wa Baba, Yesu ana onyesha uungu wake. Mstari huu unaonyesha asili ya Yesu inayoweza kufikiwa na kwamba hatuwezi kuwa na ufahamu ulio sawa na Mungu ila ni kupitia ufunuo. Kwa hivyo tunaweza kuwa na ufahamu wa Yesu lakini hatuwezi kumjua kikamilifu
Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba (Yohana 16:28).

ATHARI NA LAANA UNAZOPATA KWA WAGANGA WA KIENYEJI


Naamini umeshasikia mara kadhaa watu wakitaja kile kinachoitwa “sayansi ya kiafrika”. Kwa kifupi maneno haya yanaongelea kazi za waganga wa kienyeji. Ni wazi kuwa yanamaanisha upigaji ramli, uaguzi, usafishaji nyota, na hata ulozi na mengine kama hayo.
Siku hizi watu wengi wanakimbilia kwa waganga wa kienyeji kwa lengo la kupata “mafanikio”, wakiwamo wanasiasa, wafanyabiashara, wafanyakazi, wake, waume, wapenzi, wachumba, wanamuziki, na hata wale wanaotaka kuwakomesha wabaya wao.
Ukipita sehemu nyingi, utakutana na matangazo ambayo, japo yanashangaza, lakini watu wanaenda kwa hao walioyaweka!
Kumfunga mpenzi mkorofi, kuzindika nyumba, kusafisha nyota, kupata kazi, n.k. ni baadhi ya maneno yaliyo kwenye mabango hayo. Kilichonishangaza mimi ni kuwa, kuna hata matangazo yanayosema wazi kabisa “Njoo tukusaidie kupata utajiri wa majini”!!
Sisemi kuwa hakuna dawa za kienyeji. La hasha! Zipo nyingi na nzuri kabisa. Lakini linapofikia suala la kuaguana na kuambiana kutumia dawa huku mtu yuko uchi, au aangalie mashariki, au akanywee makaburini, n.k., hapo liko jambo.
Kabla sijamjua Yesu, niliwahi kwenda kwa mganga mmoja. Alinipa dawa kwenye kichupa kidogo. Na akanipa sharti la kwenda kuinywa usiku wakati watu wote wamelala; na nihakikishe hanioni mtu yeyote.
Lakini kabla ya kuondoka kwake, alinichanja chale, ambapo aliniambia nifumbe macho na nisifungue kabisa wakati anaponichanja! Haya ni mambo ambayo yanafanyika kila siku sehemu mbalimbali.
Alikuwapo mfalme mmoja wa Israeli aliyeitwa Sauli, ambaye alimwasi BWANA. Baada ya kuona mambo hayamwendei vema, siku moja aliwaambia watumishi wake: Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, nipate kumwendea na kuuliza kwake. (1 Samweli 28:7).
Alipofika kwa huyo mwanamke, akamwambia: Tafadhali nibashirie kwa utambuzi, ukanipandishie yeye nitakayemtaja kwako.... Nipandishie Samweli. (1 Sam 28:8, 11).
Samweli alikuwa ni nabii mkubwa wa Mungu ambaye kwa wakati huo alishakufa. Kwa hiyo, kwa kutojua kwake, Sauli akataka eti apandishiwe huyo nabii kutoka huko aliko apate kuomba msaada kwake ili mambo yake ya kiutawala yamnyokee.

MUHAMMAD AMEKUFA LAKINI YESU ANAISHI

Yesu aliondoka kaburi!
Yesu yu hai leo, lakini Mtume Muhammad amekuwa maiti kwa muda mrefu!
Kuna tofauti kubwa kati ya Muhammad na Yesu. Muhammad amekufa, lakini Yesu anaishi leo! Yeye anaishi milele na milele.
Mtume Muhammad alizaliwa karibu 570 katika mji wa Makkah akafa saa kuhusu umri wa miaka 62 tarehe 8 Juni 632 mjini Madina kwa sasa Saudi Arabia. Pia ni kaburi lake.
Mtume Muhammad, basi alikufa na kuzikwa na mabaki yake bado katika kaburi leo.
Yesu alizaliwa miaka minne kabla ya enzi zetu, naye alikufa msalabani kuhusu miaka 30 katika Yerusalemu. Mwili wake uliwekwa kaburini, lakini haina kukumbuka ambapo sasa, kwa sababu Mungu akamfufua kutoka wafu baada ya siku tatu! Siku 40 Senar Mungu alimchukua juu mbinguni ambako ameketi mkono wa kulia wa Mungu juu ya kiti cha enzi.
Yesu yu hai leo na kamwe zaidi kufa! Ni tofauti kati ya Muhammad na Yesu. Muhammad amekufa, lakini Yesu anaishi leo! Yeye anaishi milele na milele.
Basi, nilipomwona tu (Yesu), mimi akaanguka kama maiti ya miguu yake, na yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema:.. "Msiogope Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na walio hai mimi alikuwa amekufa, kumbe Mimi ni hai milele na milele Ninazo funguo za kifo na kuzimu (Ufunuo 1: 17-18)..
Yesu anasema hapa kwamba yeye ni wa kwanza na wa mwisho. Hivyo kutakuwa na tena baada yake. Kwa basi kusema kwamba Uislamu kwamba Muhammad ni Mtume wa mwisho ni makosa, kwa sababu hakuna mtu atakuja baada ya Yesu. Yesu ndiye wa Mwanzo na Mwisho. Yeye ni ya kipekee kabisa!
Yesu / Ukristo
Muhammad / Uislamu

BIBLIA YATHIBITISHA KUWA YESU NI MUNGU

USHAIDI
Isaya 9: 6
Kwa maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume, nao utawala utakuwa mabegani mwake.
Naye ataitwa: Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
Huu ni ushaidi unatufahamisha kuwa Yesu atazaliwa na ataitwa Mungu mwenye Nguvu.
Katika Agano Jipya, kuna ushaidi ambao unakiri Umungu wa Yesu Kristo.
USHAIDI
Hebu tusome Wafilipi 2: 5-11
5
Tuweni na nia ile ile aliyokuwa nayo Kristo Yesu.
6
Yeye ingawa alikuwa sawa na Mungu, hakuona kule kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho,
7
bali alijifanya si kitu, akajifanya sawa na mtumwa, akazaliwa katika umbo la mwanadamu.
8
Naye akiwa na umbo la mwanadamu, alijinyenyekeza hata mauti, naam, mauti ya msalaba!
9
Kwa hiyo, Mungu alimtukuza sana na kumpa Jina lililo kuu kuliko kila jina, 10ili kwa Jina la Yesu, kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, vya duniani na vya chini ya nchi
11na kila ulimi ukiri ya kwamba YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu comment Baba.
NENO la "Kwas sawa na Mungu" kwa Kigiriki ni MORPHE-: Ikimanaisha Yesu alikuwa na adhama zote za Kimungu na Mungu. Hivyo basi katika ushaidi huu wa katika kitabu cha Wafilipi tunasoma kuwa Yesu hakuwa mtu wa kawaida bali alikuwa ni Mungu pamoja nasi yaani Imanueli.
USHAIDI
WAEBRANIA 1:
Mwana Ni Mkuu Kuliko Malaika

KWANINI WAISLAM WALITENGENEZA INJILI YA UWONGO YA BARNABAS? (SEHEMU YA NNE)



Mwalimu Chaka
Tunazidi Kuichambua Injili Hii ambayo inajaribu kuhusishwa na Mtume Barnaba.
Leo tuangazie Mwandishi.
MWANDISHI: Muislamu ambaye alikuwa na uelewa kiasi wa Biblia Kuna uhakika kabisa na wa kutosha kutibitisha kwamba mwandishi wa Injili hii bandia ni Muislamu. Mtu yeyote akisoma kwa makini kitabu hiki kinachojulikana kama Injili ya Barnaba atapata kina mguso wa Kiislamu ndani yake.
i) Kwanza, kitabu hiki kina maelezo ya kufanana na Kristo. Katika sura ya 112 inasema: "Jua, ewe Barnaba, ya kwamba mimi ninahofia. Mmoja wa wanafunzi wangu atanisaliti kwa vipande thelathini vya fedha. Zaidi ya hayo, nina uhakika kwamba yule atakayenisaliti atauawa kwa jina langu, kwa sababu Mungu ataniinua juu ya nchi na kubadilisha sura ya huyo atakayenisaliti ili kila mmoja
aweze kufikiri yeye kuwa ni mimi. Na wakati akifa kifo kibaya na cha kutisha, nitabaki na aibu hiyo kwa muda mrefu duniani. Lakini wakati Muhammad, mtume mtakatifu wa Mungu, akija, aibu hii itaondolewa kwangu” "(Surah 112:13-17).
Habari hizi ni sanjari na mafundisho ya Kiislamu ya Zama za miaka ya kati
ii) Kifo cha Yesu. Biblia inafundisha kuwa Yesu alisulubiwa na kufa. "Kisha (Pilato) akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Lakini alikuwa kuamuru Yesu apigwe mijeledi, akamtoa ili asulubiwe. ... Walipokuwa wakienda, walikutana na mtu mmoja wa Kirene aitwaye Simoni, wakamshurutisha auchukue msalaba. ... Walipikwisha kumsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kura ... ‘Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akaitoa roho yake". (Mathayo 27:26-50.)
Kinyume na Biblia, Qur'an inafundisha kuwa Isa ambaye anadaiwa kuwa ndiye Yesu hakusulubiwa na wala hakufa msalabani (Qur'an 4:156-157). Tunaona tena jaribio, katika Injili ya Barnaba la Mwandishi akijaribu kubadilisha tukio la kusulubiwa kwa Yesu ili kuendana sambamba na kile Qur'an inasema:
"Mungu alitenda ajabu hata, Yuda akabadilishwa kisura kuwa kama Yesu na hata katika usemi wake pia na askari walichukua Yuda wakamfunga ... Hivyo wale watu wakamwongoza mpaka mlima wa Kalvari, ambapo walitumia kutundika wahalifu,na ndipo wakamsulubisha Yuda "(Sura. 216-217).
Sasa hapa bila shaka ameowanisha usemi ya Qurani kuwa " Bali walibabaishiwa mtu mwingine wakamdhani kuwa Nabii Isa!!!

JE, BWANA YESU ANAPATAJE KUWA MUNGU?





Ni vyema sasa tukapiga hatua nyingine ya ufahamu kwa kuangalia swali hili makini ambalo kwa kiasi kikubwa pia huchanganya hisia za watu wengi katika ulimwengu wa imani, ambapo kile kinachoonekana kuwachanganya watu wengi hapa ni uelewa juu ya ukweli kuhusu chimbuko la Uungu wa Bwana Yesu na hivyo watu wengi kuhoji kuwa Yesu anapataje sasa kuwa Mungu?
Ni wazi kuwa swali hili hasa hulenga kutafut kujua asili au chimbuko la mamlaka ya Kiuungu ya Yesu anayotajwa kuwa nayo hasa kutokana na kile kinachoonekana kuwa Bwana Yesu alikuwa na mwonekano unaoonyesha kuwa huenda naye alikuwa na asili au chimbuko la dunia hii.
Hivyo ili kupata majibu ya msingi ya hili ni vyema kwanza tuanze na hoja juu ya asili ya Yesu na ndipo tunaweza kufunguka zaidi kiufahamu na kuelewa mengi zaidi juu ukweli kuhusu Uungu wa Yesu.
Ufahamu juu ya asili ya Yesu:
Kile kilichoongeza upinzani mkubwa wa Mafarisayo na baadhi ya Wayahudi juu ya Uungu wa Yesu ni uelewa usiyo sahihi juu ya asili ya Yesu.
Ufahamu wa wengi kati ya Wayahudi uligotea katika dhana ya mwonekano wa ubinadamu wa Yesu na historia yake ya uzazi wa kidunia toka katika tumbo la Mariam, ambapo kama matokeo ya hili Wayahudi walisikika wakati fulani wakitamka:-
Yahana 6:42
Wakasema, Je! Huyu siye Yesu, mwana wa Yusufu, ambaye twamjua babaye na mamaye? Sasa asemaje huyu, Nimeshuka kutoka mbinguni?
Unaweza sasa kupata pichani juu ya mzizi wa hoja hii, na ni kama tunavyoona katika nukuu hiyo ya kitabu cha Yohana kuwa hoja kuu ya Wayahudi ilikuwa ni kile walichoona kuwa haikuwa sahihi kwa Yesu kusema ameshuka toka mbinguni maana kile wao wanachojua ni kuwa alizaliwa na bi’Mariam na baba yake ni Yusufu kwahivyo asili yake ni duniani tu.
Hivyo kwa hali hiyo iliwapa ugumu kukubali pale Yesu alipojitaja kuwa na asili ya mbinguni na kimsingi ndicho kilichokuwa chanzo kikubwa cha upinzani wao dhidi ya matamko ya Yesu.
Habu ona tena hoja ya Wayahudi pale Yesu alipoeleza uwepo wake wa milele’
Yohana 8: 56-58
Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.57 Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? 58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Katika andiko hilo tena Wayahudi walipingana na Yesu kutokana na tamko lake lililoonyesha uhusiano wake na ukaribu na mzee Ibrahimu, kitendo ambacho kilifanya Wayahudi hao kumhoji kwa madai kuwa yeye ni kijana mdogo hasiyepata hata miaka hamsini anawezaje kuwa amemwona Ibrahimu?, na ndipo Yesu anajibu na kuwaambia bayana kuwa uwepo wake ni wa kabla ya Ibrahimu’ 58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Hivyo kwa mtazamo wangu binafsi ninaona kuwa tatizo la Wayahudi au wale wanaopinga Uungu wa Yesu kwasababu ya ubinadamu alokuwa nao au sababu ya kuzaliwa na Mariam tatizo lao kuu si hilo bali zaidi ni kutolewa kabisa msingi mzima wa asili ya Yesu kabla ya kuzaliwa kwake na Mariam.
Je’ Asili ya Yesu ni wapi?
Katika kujibu swali hili Bwana Yesu mwenyewe mara kadhaa aliwaelimisha Wayahudi juu ya ukweli kuhusu asili yake ili kuwasaidia kuondokana na dhana au mtazamo wa kumchukulia kama mtu mwenye asili ya kidunia na badala yake alitaka waone kuwa yeye alikuwako kabla ya kuja duniani kama mwanadamu kwa kusudi la ukombozi wa watu. Soma kwa makini maandiko haya:-
Yohana 8:23

JE, MUNGU ANAZALIWA IKIWA ALIKUJA KAMA BINADAMU?




Kimsingi Mungu yeye kama Mungu hazaliwi na hakuwahi kuzaliwa kamwe, ila kile kinachotajwa kuzaliwa na Mariam ni ubinadamu wa Yesu tu ambao ulizaliwa ili kufunika Uungu ambao kuwepo kwake ni tangu milele. Na kwa hivyo Mariam hakuzaa Uungu bali alizaa ubinadamu uliobeba Uungu, kwakuwa kusema kwamba Mariam alizaa Uungu wenyewe ni sawa na kusema kuwa Mungu ana mwanzo wa kuwepo kwake yaani alianza kuwako mara tu baada ya kuzaliwa na Mariam na kwa hali hiyo Mungu ana umri maalumu na mwanzo wa kuwepo kwake tendo ambalo linapingana na maelekezo tunayoyapata katika maandiko matakatifu:-
Zaburi 102:24-27
Nitasema, Ee Mungu wangu, usiniondoe katikati ya siku zangu; Miaka yako ni tangu kizazi hata kizazi.25 Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako.26 Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumu Naam, hizi zitachakaa kama nguo; Na kama mavazi utazibadilisha, Nazo zitabadilika.27 Lakini Wewe U Yeye yule; Na miaka yako haitakoma.
Na ili kukaza uelewa wa hili tunaweza kuona maelezo ya Yesu mwenyewe juu ya hili katika mjadala wake na Wayahudi pindi walipopingana na tamko la Yesu kujihusianisha na Ibrahimu ambapo Wayahudi walimkumbusha umri wake tangu alipozaliwa na Mariam na kutumia kigezo hicho kukosoa madai ya Yesu juu ya mahusiano yake na Ibrahimu hebu tusome majibu ya Yesu:-
Yohana 8:55
Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.57 Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Hilo ndilo tamko la Bwana Yesu akibainisha kuwa uwepo wake katika nyanja ya Kiuungu usingepaswa kuwekwa katika vipimo vya miaka ya kibinadamu maana kwa hali halisi yeye alikuwapo hata kabla ya Ibrahimu.

KAMA YESU NI MUNGU, KWANINI AZALIWE NA KUVAA MWILI WA KIBIDANAMU?

Ndugu msomaji,
Baada ya hoja na maswali mengi tuliyokwisha yapitia juu ya uhalali wa Uungu wa Yesu ndipo swali hili hufuatia ambapo hoja ya msingi hapa ni juu ya kile kinachoonekana kama kitu kisichowezekana kwa Yesu kuwa na asili ya Uungu na huku akiwa na umbile la kibinadamu umbile ambalo alilipata kwa njia ya kuzaliwa na Mariam, na kimsingi hapa ndipo mahali maswali mengi zaidi hujitokeza.
Kwanini kama ni Mungu avae ubinadamu?
Tendo la dhambi ya Adamu na Hawa lilimuingiza mwanadamu katika deni kubwa lisiloweza kulipwa na mwanadamu mwenyewe hebu tusome:-
Mwanzo 3:17
Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
Kwa kadri ya Andiko hilo tunasoma kuwa Mungu alipomuweka Adamu na Hawa katika bustani ya edeni aliwapa masharti yahusuyo ulaji ambapo wanadamu hao walikatazwa kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, lakini mbali na kukatazwa huko pia walionyeshwa hasara ambayo wangeipata kama matokeo ya kukaidi agizo hilo la kula matunda hayo ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
Kwa uwazi kabisa Mungu aliwaambia juu ya hatari hiyo ambayo wangejiingiza kwayo kuwa ilikuwa ni kifo’ (siku utakapokula utakufa hakika) kwahivyo kimsingi tendo la wazazi hao kujiingiza katika tendo hilo la dhambi ilikuwa ni sawa na kujiingiza katika deni la dhambi ambalo malipo yake ni mauti (kifo).
Na kwa hali hiyo basi mwanadamu huyu alihitaji msaada wa kunasuliwa toka katika deni hilo la dhambi, hivyo ilipasa upande wa pili unaoweza kukabili deni hilo kujitokeza ili kumsaidia mwanadamu kwakuwa kimsingi hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kukabili deni la kifo maana liko nje ya uwezo wa mwanadamu kama Daudi anavyoeleza:-
Zaburi 49:7-8
Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake,8 (Maana fidia ya nafsi zao ina gharama, Wala hana budi kuiacha hata milele;)
Hilo ni tamko la wazi la Biblia likibainisha kuwa kamwe mwanadamu hawezi kujiokoa au kumwokoa jirani yake kwakuwa nafsi ya mwanadamu inagharama ambayo haiwezi kulipwa na mwanadamu mwenyewe.

KAMA YESU NI MUNGU, MBONA ALILALA, JE MUNGU ANALALA?

Swali hili la msingi ndilo litakalotufikisha mwisho wa uchambuzi wa mada hii juu ya Maarifa kuhusu Utatu na Uungu wa Bwana Yesu. Na hapa hoja ya msingi inatokana na tukio la Yesu kusafiri na wanafunzi wake naye akiwa amelala katika Shetri hivyo wanafunzi wake baada ya kupata taharuki ya kubwa ya dhoruba wakaanza kumwamsha ili awape msaada katika kadhia hiyo kama tunavyosoma:-
Marko 4:37-38
Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.
38 Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?
Tendo hilo la kulala kwa Bwana Yesu linalosimuliwa hapo ndilo linalozalisha hoja hiyo ambapo waulizaji wa swali hilo hukaza hoja yao kwa kusoma pia andiko la kitabu cha Zaburi hii ifuatayo:-
Zaburi 121:4-5 Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
Andiko hilo la Zaburi linaeleza kuwa Mungu aliye mlinzi wa Israel hatosinzia wala kulala, hivyo wajengaji wa hoja hii hudai kuwa tendo la Yesu kulala kama yeye ni Mungu basi ni hatua ya kukana Uungu wake.
Jibu la msingi la swali hili’
kimsingi hili ni moja kati ya maswali rahisi sana katika hoja hii juu ya Utatu na Uungu wa Bwana Yesu, lakini kile kinachoonekana kuwa ni mapungufu kidogo kwa waulizaji wa swali hili ni kutochukua hatua ya usomaji linganishi wa maandiko na kupitia aya nyingi zaidi ili kutafuta mantiki ya kisa hiki cha Yesu kulala na maelezo ya Zaburi yanayotamka kuwa Mungu halali.
Lakini kwa kujibu swali hili niseme tu kuwa andiko la Zaburi ya Daudi liko sahihi tu kuwa Mungu yeye kimsingi halali usingizi, lakini bado Zaburi hiyo hiyo inaeleza kile anchoweza kufanya Mungu katika dhana hiyo hiyo ya kulala hebu tusome tena andiko jingine la Zaburi ili kuanza hatua hii muhimu ya kupata ufumbuzi juu ya swali hili lenye utata:-
Tusome pamoja katika andiko hilo la Zaburi:-

SABABU KUMI (10) KWANINI NAMPENDA YESU




1. YESU NI MCHUNGAJI MWEMA
Yohana 10: 10Mwivi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi imekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele. 11‘‘Mimi ndimi Mchungaji Mwema. Mchungaji Mwema huutoa uhai Wake kwa ajili ya kondoo.
Yesu ninae mpenda ni mwenye Mikono Wazi na yupo tayari kutupokea sote. Sote tumefanya makosa, lakini habari njema ya Ukombozi ni kuhusu Upendo wa Mungu kwetu sisi ambao tunaupata kutoka na kupitia Yesu Kristo ambaye ni Bwana na Mwokozi wa Maisha yangu. Karibu kwa Mchungaji Mwema ambaye ni Yesu Kristo aliye kufa Msalabani kwa ajili ya dhambi zako.
2. YESU ALIKUJA KUWASAIDIA WALIO LEMEWA NA MIZIGO AU MATATIZO YAO
Matayo 11: 28 “Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 29 Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. 30 Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.’’
Ukristo sio kuhusu kufanya sheria bali ni kupokea jibu ambalo Yesu alisha kujibu pale Msalabani. Hii ndio Raha ya kuwa na Yesu. Yesu alisha maliza matatizo yako yote pale Msalabani, alisha maliza au ponya Magonjwa yako yote. Ndio Maana Yesu anasema kwako kuwa, NJOONI NINYI NYOTE MLIO LEMEWA NA MIZIGO. Kitu ambacho unatakiwa kufanya ni kuja kwa Yesu, halafu yeye atakupa Majibu yako yote. Sasa njoo kwa Yesu na upokee majibu ya matatizo yako.
3. YESU AMEKUSAMEHE -UPENDO WA MUNGU
Zaburi 103: 2 Ee nafsi yangu, umhimidi BWANA, wala usisahau wema wake, 3 akusamehe dhambi zako zote na kuponya magonjwa yako yote, Kumfahamu Yesu ni kujua kuwa Yesu alisha maliza kazi zote pale Msalabani, ikiwa pamoja na kukusamehe dhambi zako zote. Sasa basi, najua unasema kuwa labda ulifanya vitu vibaya hapo nyuma na unashindwa elewa kivipi Yesu atakusamehe dhambi zako. Ndugu msomaji, Yesu hajali nini umefanya hapo nyuma, Yesu anacho taka kutoka kwako ni kuwa, umkabidhi matatizo yako yoke na yeye alisha maliza kazi pale Msalabani. Sasa basi, mwambie Yesu kuwa wewe ni mwenye dhambi na omba msamaha na amini kuwa amesha kusikia na kukujibu/samehe. Yesu ni Mungu na Mungu wetu ni Upendo.

Where are the names of the Apostles of Jesus (ʿĪsā ibn Maryam) in the Qu...

Where are the names of the Apostles of Jesus (ʿĪsā ibn Maryam) in the Qur’an? If ʿĪsā was truly a Muslim—a servant of Allah preaching Islam—...

TRENDING NOW