Wednesday, January 9, 2013

MBINU ZINAZOTUMIKA NA WAISLAMU ILI KUHARIBU IMANI YA KIKRISTO KATIKA KARNE YA 20-21 (21st CENTURY ISLAMIC STRATERGIES TO ELIMINATE/CORRUPT CHRISTIANITY IN AFRICA)


Utangulizi:

Leo hii, ukitembea sehemu mbalimbali hapa duniani utakutana na waislamu wengi. Waislamu wameenea kila Bara kama vile Ulaya, Afrika, Asia, na America. Inaaminika kuwa kwa kila watu watano hapa duniani, mmoja kati yao ni mwislamu. Tunashuhudia baadhi ya wakristo wakiacha imani yao na kukumbatia uislamu. Katika Bara la Afrika, uislamu umeenea kwa kasi ya ajabu. Je, ni nini kinachofanya uislamu uenee hivyo? Je, ni mbinu gani zinazotumika ili kueneza uislamu? Fuatilia somo hili ili uweze kujua hayo yote.

1. Maana ya neno "lslam"
Neno 'Islam' Asili yake ni lugha ya 'kiarabu' lenye maana ya 'utii' au 'amani'.

2. Mwanzo wa Dini ya Kiislamu
Neno "Islam" ni tofauti na "Dini ya Kiislamu". Hii ni kwa sababu neno "Islam" lilitumika na waarabu hata kabla ya kuanza kwa dini ya kiislamu. Kwa hivyo "Dini ya kiislamu", maana yake ni "kujisalimisha chini ya amri za Allah" au "Amani chini ya sheria za Allah".

i. Muhammad aliambiwa na Allah asema: -
Quran 39: 12 Suratul Zumar (Makundi / Vikosi)
"Na pia nimeamrishwa niwe wa kwanza wa (viumbe) wanaojisalimisha (kwa mwenyezi Mungu)"

Quran 6: 14 Suratul Al- An'am (Wanyama)
Sema "je nifanye mola (wangu) asiyekuwa Mwenyezi Mungu, (Ambaye ndiye) muumba wa mbingu na ardhi" naye hulisha wala halishwi" sema hakika mimi nimeamrishwa niwe wa kwanza katika wenye kusilimu na (nikaambiwa). usiwe miongoni mwa wanaomshirikisha (Mwenyezi Mungu).

Katika ufafanuzi wa aya ya 19-20, katika Suratul Yusuf 12:20 kuna maneno haya--
Unaona kuuzana kulikuwako zaidi ya miaka 4000 kabla ya kuja dini ya kiislamu aliyokuja nayo nabii Muhammad. Kisha wakausingizia uislamu kuwa ndio uliokuja na kuuza watu.

Kadiri ya aya hizi zote tunaona ya kuwa dini ya kiislamu ilianzishwa rasmi hapa duniani Ramadhan siku ya Jumatatu mwezi 17 sawasawa na Tarehe 27 December mwaka 610 Baada ya Kristo (B.K), na mtu aitwae Muhammad Bin Abdalah Bin Abd-Muttalib Bin Hashim Bin Abd Manafu Bin Kusay. Mama yake aliitwa Amina Bint Wahab.
Ama baada ya kuona mwanzo wa Dini ya uislamu sasa tuanze kuangalia mbinu za waislamu.

3. Mbinu Zinazotumika na Waislamu
Mwanzoni Muhammad, mtume wa waislamu, alitumia mbinu hata za kivita ili kueneza dini yake ya kiislamu. Hata wafuasi wake waliamrishwa kupigana kwa ajili ya dini yao. Qurani inasimulia hivi---

Qurani 5:35 Suratul Al -Maidah (Meza)
Enyi mlioamini mcheni mwenyezi Mungu na tafuteni njia ya kumfikilia (kufikilia pepo yake). Na piganeni kwa ajili ya Dini yake ili mpate kufaulu.
Katika Qurani, kitabu kinachowaongoza waislamu, zipo aya nyingi zinazowaamrisha waislamu
wapigane. Baadhi ya aya hizo ni Qurani 47:4 Suratul Muhammad na Qurani 9:123 Suratul At - Tawba. Muhammad mwenyewe alisema hivi katika kitabu cha hadithi zinazoaminiwa na waislamu wote:-

Sahih Al-Bukhari Vol. 4 Hadith na 196, Ukurasa wa 124:
Imesimuliwa na Abu- Huraira: Mtume wa Allah akasema, Nimeamrishwa kupigana na watu hadi watakaposema hakuna apasaye kuabudiwa ila Allah; Na yule atakayesema kwamba hakuna apasaye kuabudiwa ila Allah, maisha yake na mali yake yataokolewa nami…

Tafsiri ya Kiingereza:
Narreted Abu-Huraira Allah's Apostle said, I have been orderedt fight with the people till they say, none has the right to be worshipped but Allah ; his life and property will be saved by me…

Hivi ndivyo alivyosema mtume wa waislamu Muhammad,aliye mfano mwema wa waislamu wote (Qurani 33:21 Suratul Al-Ahzab). Muislamu ni lazima atekeleze kama alivyoamurishwa Muhammad na Allah. Tena tunajua kwamba, watu wote hawawezi kusema "hakuna apasaye kuubudiwa ila Allah". Hao wasiosema hivyo, kadiri ya Hadith hii, wanatakiwa kupingwa na kuawawa mara moja. Kadiri ya Qurani, miongoni mwa watu wanaotakiwa kuangamizwa ni "Wayahudi na Wakristo" (Qurani 9:30 sSuratul At-tawba). Katika kufanikisha uendelezaji wa uislamu hivi sasa, waislamu wamebuni na kutumia mbinu mbalimbali.

I. Kuunda Jumuiya na Taasisi Mbalimbali za Waislamu
Hatua ya kwanza iliyotumika na waislamu ni kuunda jumuiya. Waislamu wana jumuiya nyingi hivi sasa na taasisi nyingi Lakini nitazieleza baadhi yake.

i.Jumuiya ya Organization of Islamic Conference (O. I. C.)
Jumuiya hiyo ilianzishwa baada ya kumalizika vita kati ya Israeli na mataifa kumi na tatu (13) ya kiarabu. Vita hivyo vilipiganwa kwa siku sita na vikamalizika tarehe 5/6/1967. Katika vita hivyo waisraeli waliyashinda mataifa yote 13 ya kiarabu. Ina aminika kuwa wakati huo waisraeli walikuwa ni watu wachache wapata watu 400,000 tu. Baada ya kushindwa huko ndipo mataifa hayo 13 ya kiarabu yakafanya kikao cha kutathimini vita hivyo. Mkutano huo ulifanyika mjini Rabat nchini Morocco chini ya mfalme Hassani. Kikao hicho kilifanyika tarehe 25/9/1969 (kalenda ya kiislamu ni mwezi 12 Rajabu 1389), ndipo mataifa hayo yakaanzisha rasmi jumuiya hiyo ya Organization of Islamic Conference (O.I.C.). Hadi kufikia mwaka wa 2001, jumuiya hiyo imeweza kuwa na wanachama mataifa 56 duniani. Na juhudi zinafanyika ili kupata wanachama zaidi. Jumuiya hiyo ndiyo inayopanga na kutekeleza mbinu ya kuendeleza uislamu duniani.

ii.Kuanzisha kwa Jumuiya ya Islam in Africa Organization (I. A. O.)
Jumuiya hii ya 'Islam in Africa Organization' ilianzishwa chini ya O. I. C. na wawakilishi wa dini ya kiislamu kutoka mataifa 24 walikutana na kuunda jumuiya hiyo. Mkutano uliounda jumuiya hiyo ulifunguliwa na aliyekuwa Raisi wa Nigeria aliyeitwa Ibrahim Babangida.
Jumuiya hiyo ndiyo inayohusika kupanga na kutekeleza namna ya kuendeleza uislamu katika bara la Afrika. Jumuiya hiyo ilianzishwa tarehe 28/11/1989 kule Abuja Nigeria chini ya usimamizi wa O.I.C.

iii.Taasisi za Fedha (Tafakari kuhusu Sharia Banking System)
Ili kuendeleza dini ya kiislamu, mataifa ya kiarabu ambayo yana utajiri mkubwa unaotokana na mafuta yamezipatia nchi hizo mtaji usiotazamiwa kumalizika. Utajiri wao unatumika kueneza uislamu kwa kuishambulia imani yetu wakristo. Taasisi za fedha zilizoundwa chini ya jumuiya ya O.I.C. na I.A.O. ni hizi: -
Islamic Development Bank
Islamic Development Fund
Jukumu la taasisi hizo za fedha ni kuhakikisha kuwa wanatoa fedha za kuendeleza shughuli za kukuza na kusaidia nchi wanachama katika kuendeleza miradi ya uchumi, viwanda, biashara, hospitali, visima vya maji, barabara na mashule. Vile vile, taasisi hizo zinatoa fedha ili kuwashawishi hata viongozi wa mataifa mbalimbali ili wajiunge na jumuiya za O. I. C. na I. A. O. Kwa mfano, taifa ambalo lilipewa fedha nyingi mara baada ya kujiunga na jumuiya hizo za kiislamu ni Nigeria ambayo ilipewa dola za kimerikani US $ 21 BILLION. Kwa ajili ya maendeleo ya waislamu. Hata aliyekuwa Raisi wa nchi hiyo, Ibrahimu Babangida, alipokubali nchi yake iwe mwanachama wa O. I. C. na I. A. O., November 1989 kule Abuja Nigeria, Account yake iliyokuwa katika Bank inayoitwa Arab-African lnternational Bank, ilionyesha alikuwa na dola za kimarekani US $ 57.48 Billion. Aidha mawaziri wawili na mkuu wa jeshi, Account zao zilikuwa na fedha nyingi nazo zilionyesha fedha hizi:-
Mmoja alikuwa na US $ 15.2 Billion
Mwingine alikuwa na US $ 17.8 Billion
Mwingine account yake ilikuwa na US $ 24.9 Billion
Na hii ilikuwa ni motisha kwao. Jambo hili linatishia kuangamizwa kwa imani yetu sisi wakristo.



II. Uandishi wa Vitabu
Waislamu wa sehemu mbalimbali hapa duniani wameandika vitabu na bado wangali wanaendelea kuandika. Vitabu ambavyo vinaisema vibaya imani yetu wakristo. Vitabu hivyo vimeandikwa katika lugha mbalimbali Kama kiingereza, Kiswahili na lugha nyinginezo. Baadhi ya waandishi wanaojulikana sana ni hawa: -
Ahmed Deedat
Mtu huyo Deedat ndiye mwandishi maarufu wa vitabu. Ahmed Deedat anaishi kule Durban, Afrika Kusini. Shirika lao linaitwa 'The Islamic Propagation Centre'. Ukisoma vitabu vyake utaona jinsi anavyotumia hisia zake kutoa tafsiri potofu kupotosha maandiko matakatifu ya Biblia. Deedat ndiyo chanzo kikubwa cha mihadhara iliyoenea sana duniani na hasa katika nchi za Afrika Mashariki na Kati. Vitabu vyake pia vinatumika katika Makongamano, Semina, Mihadhara na kwenye Website mbalimbali. Waendesha mihadhara wamechukua hoja zipatazo 150 alizoziandika. Katika kitabu chake kinachoitwa "The God That Never Was" (Mungu Asiyekuwepo Kamwe), chenye kurasa 15 alichokiandika mwaka wa 1983, Deedat anasema hivi, "Kusema kwamba Yesu ni Mungu siyo tu kudhihaki Mungu, bali ni kukufuru kwa aina mbovu kabisa na ni kutukana hata akili ya mwanadamu". Anaendelea kusema "Yesu ni Mungu mlafi na mlevi" (Mathayo 11:19), "Mungu ambaye hakujua kusoma na kuandika" (Yohana 7:14-15), "Mungu aliyekuwa wa kabila la wayahudi" (Ufunuo 5:5), "Mungu aliyezidiwa na hisia zake" (Marko 14:33), na "Mungu bubu na asiyejikinga" (Matendo 8:32). Ukisoma kitabu hiki utasikitishwa sana na lugha mbaya za Deedat ambazo waislamu wanazishangilia na kuzitumia katika mihadhara yao. Isitoshe jumuiya kubwa za O.I.C., Islamic Development Bank na Mfalme Fahad wa Saudi Arabia ndio wafadhili wake wanaomsaidia kusambaza vitabu hivi duniani kote. Hii ni hatari kwa imani yetu sisi wakristo.



Sayyid Abul A’la Maududi
Mtu huyu alikuwa mwandishi maarufu wa kiislamu aliyekuwa anaishi bara Hindi kati ya mwaka 1903 na 1979. Aliandika kitabu kinachoitwa "Katika Kuufahamu Uislamu", mwaka 1932. Kinasambazwa na 'The Islamic Foundation', Nairobi, Kenya. Kitabu hiki kimechapishwa upya mwaka wa 1974, kina kurasa 136. Kupitia kitabu hicho, Maududi anasema katika ukurasa wa 84 kuwa "vitabu vitakatifu vya awali (Torati, Zaburi, Manabii na Injili) viliteremshwa katika lugha zilizokufa zamani". Anaendelea kusema kuwa "Hakuna nchi wala jamii inayozungumza lugha hizo sasa na ni watu wachache wanaodai kuwa wanazifahamu.

Prof, M. H. Maliki
Profesa Maliki ndiye mshauri wa wanafunzi waislamu katika chuo kikuu cha Nairobi. Ameandika kitabu kinachoitwa "The Mission of Jesus" (Ujumbe wa Yesu). Amekiandika mwaka wa 1993, kina kurasa 117 na kinaenezwa na "Islamic Foundation" Nairobi, Kenya. Katika kitabu chake anasema maneno mabaya ya kuvuruga wakristo. Naye anasema hivi: -
Yesu amemtabili Muhammad
Vitabu vya injili haviaminiki
Injili ya barnaba ni injili halisi
Paulo alibadili injili ya Yesu
Kumkubali Paulo ni kumkataa Yesu
Isitoshe profesa Maliki ameandika mara nyingi katika gazeti maarufu la kiislamu linaloitwa 'Al-Islam' kwa miaka mingi.

Ali Muhsin
Ali Muhsin ni mtu maarufu ambaye zamani alikuwa waziri katika nchi ya Zanzibar. Na alifungwa jela miaka kumi 10 Kitabu alichoandika kinaitwa "Let the Bible Speak" (Acha Biblia Ihukumu), chenye kurasa.169 Kimechapishwa na Ansaar Muslim Youth Organization, Mombasa, Kenya. Katika kitabu chake, Muhsin anasema hivi…
Yesu alikuwa Nabii mwema wa uislamu lakini alikufa kabla hajakamilisha utume wake, maisha yake mafupi yalimzuia kukamilisha utume ambao alitumwa aulete duniani.
Mwanzilishi wa ukristo ni Paulo
Paulo ni mtu mbaya aliyeingiza imani ya dhambi ya asili, wokovu kwa njia ya damu. Na fumbo lisilo eleweka kabisa la utatu.
Muhsin anaendelea kusema kuwa, mafundisho ya Paulo yamewachanganya wafuasi wa Yesu na kuwazuia wasimkubali Muhammad.

Sheikh Muzaffar Ahmad Durani
Vitabu alivyoandika ni vingi. Hapa ninavitaja viwili tu :-
Silaha za mahubiri
Zawadi kwa wakristo
Waenezaji wa vitabu hivyo ni jumuiya ya waislamu wa Ahmadiyya. Yaliyomo katika kitabu cha zawadi kwa wakristo ni haya:
Ukurasa wa 21 Yesu si Mungu kwa sababu alioa
" 22 Mke wa Yesu Mariam Magdalena
" 28 Yesu alitumwa kwa wana wa waisraeli tu (Mathayo 15:24)
" 31 Yesu aliteta upanga (Mathayo 10:34-35)
" 39 Paulo ni mhalifu wa Yesu( Matendo 26:9)
" 43 Bwana Yesu hakufia msalabani (Waebrania 5:7)
" 96 Nyimbo hazitakiwi (Amosi 5:23)
Nchini Kenya, jumuiya ya Ahamadiyya Muslim Mission imetafsiri Qurani katika Lugha za Kiswahili, na pia wametafsiri Qurani ya Kikuyu iliyotafsiriwa mwaka wa 1988, pia wana mpango wa kutafsiri Qurani kwa lugha za Kikamba na Kijaluo. Je mkristo, vitabu hivi vinaashiria nini kwako? Vinalenga kuharibu imani yetu au la? Tafakari.
Dar-es-Salaam, Tanzania Waislamu walikuwa na njama ya kuchapisha Biblia potofu, milioni 15, ambazo zingeonyesha utabili wa Muhammad. Angalizo kuna injili ya upotofu iitwayo "Injili ya Barnaba".

III. Vijarida (Tracts)
Waislamu wanachapisha vijarida na kugawa. Vingine vinawekwa hata mashuleni ili visomwe. Kijarida kimoja kilichoandikwa chasema "Yesu hakuzaliwa Tarehe 25 December".

IV Vikundi vya mihadhara.
Vikundi hivyo ni vingi na vimeenea sana katika za Afrika Mashariki na kati, na hadi kufikia mwaka 2001 kulikuwa na vikundi 15. Vikundi hivyo vinatumia Biblia Takatifu na wanatoa mafundisho potofu.

V. Magazeti (Newspaper)
Yapo magazeti mengi yanayoandika habari za kupotosha maandiko matakatifu ya kweli ya Biblia. Baadhi ya magazeti yameingizwa katika 'Internet' na 'Website' -
i. Magazeti yanayochapishwa nchini Tanzania:
Al – Nur.
Nasaha. .
Mapenzi ya Mungu.
ii. Magazeti yanayochapishwa nchini Kenya:
Al – Islam.
International Bulletin
Al-Madrasah
Sauti ya Umma
The Guide
Dunia-e-Farsi

VI. Internet na Website
Mafundisho ya kupotosha Biblia na hoja potofu zilizotengenezwa na waislamu dhidi ya wakristo siku hizi yanaonekana sana katika intenet na website nyingi Baadhi yake ni hizi: -
AI. Haramain Foundation (www. Alharamain .org )
Islam 101 (http://www.islam101.com/)
Al. Huda/the qur’an .com
The shia home page (http://www.shia.org/)
Jambo la kushangaza unaloweza kukutana nalo katika websites zao ni kuwa Qur’an iko sawa, haina makosa kwa asilimia 100. Lakini wanasema kuwa Biblia ina makosa 50,000.

VII. Kanda za Audio na Video (Cassettes)
Hizi ziko nyingi tu katika kanda mojawapo Ahmed Deedat anasema kwa kusisitiza kuwa katika Biblia hakuna injili wala Torati, bali iliyokuwepo ni injili kama, yaani "The Gospel according to Matthew, Mark, Luke and John".
Vile vile waendesha mihadhara wanarekodi kanda nyingi za video na audio na kuzisambaza sehemu mbalimbali duniani. Kwa mfano, nchini Kenya, kanda hizo zinasambazwa na Iranian Cultural Centre.

VIII. Ujenzi wa Misikiti (Building of Mosques)
Miongoni mwa mbinu zinazotumika kueneza uislamu ni ujenzi wa misikiti mizuri na mikubwa. Katika misikiti hiyo vimewekwa vipaza sauti (loud speaker) ambavyo vinatoa sauti kubwa sana. Wapiga adhana huanza kuwahamasisha watu waende kuswali (kusali) kuanzia saa kumi alfajiri (4:00 A.M.). Wapiga adhana hao wanatumia maneno makali ya kuwatisha watu wanaposema "hicho kitanda chako ni jeneza, chumba chako ni kaburi na shuka lako ni sanda".
Ujenzi wa misikiti hivi sasa unazidi kuenea kwa kasi ya ajabu baadhi ya nchi ni hizi --

Uingereza, Ujerumani na Ufaransa - kila baada ya wiki mbili msikiti mmoja mpya unafunguliwa.
Ethiopia – wakati wa utawala wa kikomusti nchini humo kwa miaka mitano (5) tu, misikiti 5002 ilijengwa
Malawi – kila umbali wa kilometa (15) msikiti mmoja umejengwa
Botswana – miaka kadhaa iliyopita walikuwepo waislamu wachache sana. Lakini hivi sasa, nchini humo imejengwa misikiti mingi.
Tanzania – nchini humo ukitembelea katika mji wa Dar-es-salaam utaona kuna misikiti mingi mikubwa na gharama kubwa ukienda katika barabara ya Iringa na Mbeya utaona kuwa kwa kila kilometa 10, msikiti mmoja umejengwa.
Siera leone - ijapokuwa nchi hiyo ndiyo ya kwanza kufikiwa na Injili kati ya mataifa ya Afrika magharibi yapata miaka 200 iliyopita. Lakini kwa sasa, idadi ya wakristo haipiti asilimia kumi. Nchi hiyo ina Misikiti ipasayo 3,812 na idadi ya waislamu kwa sasa ni asilimia 40. Watu wa makabila ya Yalunka, Temne, Mende, Koranko na Loko wanasilimu na kujiunga na uislamu kwa wingi sana.

IX. Ndoa (Marriage)
Hii ni mojawapo ya njia inayotumika katika kuendeleza uislamu kwani Qur’an inawaagiza waislamu waoe wake wengi, nayo inasimulia hivi--
Qurani 4:3 Suratul An Nisaa (wanawake)
Na kama mkiogopa kutowafanyia uadilifu mayatima (basi ogopeni vilevile kutowafanyia uadilifu wanawake). Basi oeni mnaowapenda katika wanawake, (maadamu mtawafanyia insafu) wawili au watatu au wanne (tu)…
Aidha Qur’an inatoa ruhusa ya kubadili mke kwa kumuacha mke wa zamani na kuoa mwingine (Surah 4:20) waislamu hufanya bidii ya kuwatafuta wasichana wakristo na kuwabadilisha dini na kuwaoa. Hivyo kusababisha kuongezeka haraka. Ili kuhakikisha idadi yao inaongezeka waislamu pia wameunda vikundi vya wanawake, kwa mfano Tanzania kuna vikundi viwili ambavyo wanasaidiwa kifedha ili kuwatafuta wasichana wakristo hata vijijini katika mikoa mbalimbali kwa kisingizio cha kuwapatia kazi za house girl kisha wanawasilimisha na kuwaozesha.
Vikundi hivyo ni hivi: -
Saraffiya women Development Islamic Group
Al-Mubaraghat Islamic Group
Nchini Kenya kuna kikundi cha wanawake kinachoitwa "Ahli- Sunat Women Group". Je wakristo, tunafanya juhudi gani kuwafikishia injili watu wasio wakristo?

X. Ajira (Employment)
Kupitia jumuiya ya kiislamu ya O.I.C. na I.A.O. pamoja na Taasi za fedha za Islamic Development Fund, Islamic Development Bank na African Muslim Agency, fedha nyingi zinatolewa kufungua miradi mbalimbali ya uchumi, biashara na viwanda. Kwani O.I.C. inatoa mikopo na kujenga viwanda katika nchi mbalimbali. Wafanya biashara wakubwa wa kiislamu hupewa fedha za kufungua viwanda ambapo wanawashawishi watu kwa vigezo vya kuajiriwa na hatimae wanawasilimisha.
Baadhi ya viwanda vinavyomilikiwa na waislamu nchini Tanzania wamejenga misikiti ndani yake, na hata katika vituo vya kuuza mafuta (Petrol Station) kuna misikiti. Je, ni wakristo wangapi wanajenga makanisa katika viwanda?. Maajenti wa O.I.C. ina aminika wapo hata katika kiwanda kimoja cha kutengeneza sukari, ambacho kinamiliki timu ya mpira. Kupitia maajenti hao hivi sasa tayari mchezaji mmoja, mlinda mlango(goal keeper) na kocha mmoja (asiye raia wa Tanzania) wamesilimishwa ili wawe na ajira bora. Nchini Uganda, Chuo Kikuu cha Kiislamu kinawavutia wasomi wengi, hata maprofesa wakristo, kwa sababu kinatoa mishahara minono.

XI. Elimu (Education)
Nchini Botswana ambapo miaka kadhaa iliyopita walikuwepo waislamu wachache hivi sasa shule nyingi zimejengwa zikiambatana na misikiti wanafunzi hupata elimu bure hadi kiwango cha shahada (Degree). Na wakati mwingine masomo katika nchi za ng’ambo katika vyuo vikuu vya kiislamu.
Nchini Uganda chuo kikuu cha kiislamu kinawavutia sana wanafunzi wakristo kwani waweza kupatiwa masomo bila malipo.
Nchini Tanzania pale Dar-es-salaam kuna shule moja inadhaminiwa na kuwett masomo kwa waislamu kuanzia primary hadi secondary ni bure. Isitoshe waislamu kabla ya uhuru na baada ya uhuru hadi kufikia mwaka wa1990 walikuwa chini kielimu kwa asilimia 10. Lakini kuanzia mwaka wa 1991-2001, waislamu wamepanda kielimu na kufikia asilimia 48. Hivi sasa wanaendelea kujenga shule zaidi.
Nchini Kenya, mashirika ya Iranian Cultural Centre, Al-Rasul Al-Akram Islamic Centre, Islamic Foundation na International Islamic Relief Organization of Saudi Arabia wanafadhili miradi ya shule na madrassa. Pia, mashirika hayo yanafadhili wale wanaotaka kujiendeleza zaidi kielimu.
Vilevile nchini Kenya shirika la African Muislim Agency wamejenga chuo kiuu cha kiislamu kipo huko Thika na kilifunguliwa mwaka wa 1978. kila mwanafuzi anapata elimu bure kwa miaka minne, na kinafadhiliwa na nchi za Kuwet na Saudi Arabia. Je, wakristo tunafanya nini?

XII. Afya (Health)
Shirika la maendeleo la waislamu liitwalo African Muslim Argency limefungua hospitali mbalimbali, na kupitia hospitali hizo utashangazwa kuona gharama ya matibabu inaweza kuwa kubwa kwa mkristo, na ikawa ni ndogo kwa mwislamu. Wahudumu wa hospitali hizo wanawashawishi wakristo ili wasilimu ili wawasaidie kwa matibabu mazuri. Nchini Kenya, shirika la International Islamic Relief Organization of Saudi Arabia limefadhili miradi ya ujenzi wa vituo vya matibabu (Dispensaries) katika miji ya Mombasa, Machakos, Wajir na Elwak. Hii ni hatari kwako mkristo kuacha imani yako.



XIII. Visima vya Maji
Visima hivi vimejengwa kwa wingi na African Muslim Agency katika mji wa Dar-es-salaam. Misikiti mingi ina visima vya maji ambavyo vinatumika. Pia vinawavutia baadhi ya wakristo kwa sababu ukitaka maji katika visima hivyo ni lazima usalimie "Asalam aleykum". Nchini Kenya, shirika la International Islamic Relief Organization of Saudi Arabia limefadhili miradi ya kuchimba visima vya maji sehemu kame. .Je, hilo linaashiria nini kwako mkristo?

XIV. Vituo vya Watoto Yatima (Centre for Orphans)
Nchini Kenya, mashirika ya Iranian Cultural Centre, Al-Rasul Al-Akram Islamic Centre, Islamic Foundation na International Islamic Relief Organization of Saudi Arabia yanafadhili vituo vya watoto yatima. Vituo hivyo vya kulelea watoto yatima vinawasilimisha wale ambao ni wakristo. Vile vile, wale wanaowalea wanasilimishwa ili wasaidiwe. Je, kumsaidia mtu ni lazima awe wa imani yako?

XV. Uchawi na Ushirikana (Witchcraft and Sorcery)
Waganga wakienyeji ambao wengi ni waislamu wanawashawishi wagonjwa wakristo wasilimu kwa madai kuwa ili matibabu yafanye kazi. Basi jina la kikristo libadilishwe na upewe jina la kiislamu, ndipo matibabu yatafanikiwa. Tahadhari kwa wakristo wenye tabia za kwenda kwa waganga wa kienyeji.

XVI. Vituo vya Radio na Televisheni (Radio Station and Television)
Njia nyingine inayotumika kueneza uislamu ni vituo vya radio na televisheni ambavyo waislamu wamevijenga. Kwa mfano, Televisheni ya Al-jazira mara kadhaa inatoa matangazo ya kuonyesha kuwa wakristo wa nchi za magharibi ni maadui wa uislamu. Nchini Kenya, ipo Radio Station itwayo IQRA F.M. 95.1. Wanaendesha kipindi kinachoitwa "Dini ya Haki". Wanatoa mafundisho potofu kwa kusema, "Yesu hakufa msalabani", "Paulo si mtume wa Mungu", "Ukristo siyo dini", na "Yesu sio Mungu". Pia huko Mashariki ya Kati imejengwa stesheni ya redio ambayo ina nguvu kubwa ya kupeleka matangazo. Redio hiyo ina 'transmitters' zenye nguvu za 2000 K.W., wakati stesheni ya redio kubwa ya wakristo ya kueneza injili ina 'transmitters' zenye nguvu ya 50 K.W. Wakristo tuwe makini na utangazaji wa injili tukikumbuka kuwa lnjili ndiyo uweza wa Mungu unaoleta wokovu (Warumi 1:16; na Marko 16:15-16). Isitoshe lnjili ndilo neno pekee la kweli ya Mungu (Wakolosai 1:15).

XVII. Misaada ya Vyakula
Shirika linaloitwa Ahmadiyya Muslim Mission linatoa misaada ya vyakula ili kuwavutia watu wasilimu na kuwa waislamu.

4. Idadi ya Waislamu
Ongezeko la waislamu duniani linatisha sana, kwani miaka mia moja 100 iliyopita, yaani 1900, waislamu dunia nzima walikuwa 14 Million. Lakini idadi ya waislamu imeongezeka kwa kasi ya ajabu, kwani hadi kufikia mwaka wa 2000, waislamu duniani kote wamefika 1.5 Billion. Ongezeko hilo la waislamu ni kubwa sana ukilinganisha na ongezeko letu wakristo. Kwani wakristo duniani kote miaka 100 iliyopita walikuwa 558 Million na hadi kufika mwaka wa 2000 wakristo duniani kote tumefikia 2.1 Billion tu. Katika Bara la Afrika peke yake, kuna idadi ya waislamu ni 324 Million. Yafuatayo ni baadhi ya mataifa yenye waislamu wengi:-


Bara la Afrika
Nchi Waislamu Asilimia(%) Wakristo Asilimia (%)
Tanzania 13 Million 40 17,234,449 51.42
Kenya 3.3 Million 10 23,655,205 78.64
Uganda 2.0 Million 7 19,306,596 88.65
Moroco 28,178,512 99.85 28,221 0.10
Libya 5,408,557 86.52 168,142 3.00
Misri 59,239,980 86.52 8,887,366 12.98
Nigeria 45,717,499 41.00 58,663,357 52.61

Bara la Asia
Nchi Waislamu Asilimia (%) Wakristo Asilimia (%)
Bangladesh 110,556,810 85.63 929,917 0.72
India 126,707,722 12.50 25 Million 2.40
Pakistan 150,349,015 96.08 3,614,761 2.31
Indonesia 171,032,517 80.30 34,078,708 16.00
Saudi Arabia 20,057,491 92.83 980,944 4.54

Bara la Ulaya
Nchi Waislamu Asilimia (%) Wakristo Asilimia (%)
U/ Kingdom 1,176,603 2.00 39,786,837 67.63
Ufaransa 5,907,971 10.00 40,008,779 67.72

Haya ni mambo ya kutafakari. Tukumbuke kuwa Bwana Yesu alianzisha kanisa miaka 577 kabla ya Muhammad hajaanzisha Dini ya Kiislamu. Yatufaa tujue kupigwa vita huku kwa ajili ya imani yetu. Lazima tuamke sasa. Wakati wa kulala umepita. Tutumie wakati wetu wote tukiongozwa na Roho Mtakatifu ili tuliokoe kanisa la kristo. Yatupasa kuanzia katika bara letu la Afrika na baadaye dunia nzima. Watu wa bara hili la Afrika wanatakiwa kujua habari njema na wakupeleka injili hiyo ni sisi sote. Yafaa kila mkristo kujiuliza swali hili akiongozwa na aya hii..
Warumi 8:35-36
Ni nani atakayetutenga na upendo wa kristo? Je! ni dhiki, au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, ua upanga?. Kama ilivyoandikwa ya kwamba, kwa ajili yako, tunauawa mchana kutwa, tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. Ndugu mpendwa, natumai kwamba umezijua mbinu zinazotumiwa kueneza uislamu. Utajitahidi kuwafahamisha wengine ili wasiongozwe na elimu za uongo na tamaa ya mali na kumwacha Bwana Yesu (Waefeso 4:15).
KWA UWEZO WA MWNYEZI MUNGU, MAJIBU YOTE BIBLIA INAYO.TUNATAMANI NA SISI KUCHAPA VITABU VINGI ILI KUJIBU MASWALI YOTE NA KUWAELEKEZA WAISLAMU KWENYE MSALABA WA KRISTO ILI WAPATE WOKOVU.KANISA KAA MACHO NA MBIZU HIZI NA NYINGINE NYINGI ZA AINA HIYO ZITAKAZOJITOKEZA. MILANGO YA KUZIMU HAITALISHINDA KANISA (MATH 16:18)

1 comment:

Anonymous said...

mbona mengi ni uongo

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW