Monday, September 2, 2013

YESU NI MUNGU


Adhama ambazo zina Yahweh pekee apatiwa Yesu Kristo:

1.   Yesu aliumba Ulimwengu:
Wakolosai 1: 16-17 Inasema: 16 Yeye ndiye aliyeumba vitu vyote mbinguni na duniani; vitu vinavyoonekana na visivyoonekana; kama ni viti vya enzi au nguvu, au watawala au milki na mamlaka: vyote viliumbwa na yeye kwa ajili yake. 17 Yeye alikuwapo kabla ya vitu vingine vyote na kwa uwezo wake vitu vyote vinahusiana kwa mpango.

Jambo hili lauumbaji lazima tuliwekee msisitizo kwasababu inafahamika kuwa ni Yahweh ndie aliye umba Ulimwengu, lakini katika kitabu hiki cha Wakolosai tunaona kuwa Yesu nayeye anapewa adhama hiyo ya uumbaji.

2.   Yesu anapewa adhama ya Umilele ambayo ni sifa pekee ya Mungu.
Yohana 8:58 Inasema:  58 Yesu akawa jibu, “Nawaambia wazi, kabla Abrahamu hajazaliwa, ‘Mimi nipo.’
Katika hiyo aya, Yesu anadai na kusema kuwa Kabla ya Ibrahimu kuwepo, yeye Yesu alikuwepo!!! Hii sifa ni ya Kimungu Pekee, kwani Mungu ndie pekee alikuwepo kabla ya uumbaji.
Na kwababu hiyo, Wayahudi wakashika Mawe ili wampige nayo Yesu.
Sasa tujiulize, je hawa Wayahudi wangetaka kumpiga Mawe Yesu kama haingekuwa ya kuwa alisikikika akikufuru kwa kusema yeye ni Mungu?

Ngoja tuongeze ushaidi zaidi wa Umilele kutoka Yohana 17: 5
Na sasa Baba nipe mbele yako ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe hata kabla dunia haijaumbwa.
Katika hii aya, Yesu anadai kwamba aliishi na Baba kabla ya dunia kuumbwa. Haya maneno ni ushaidi tosha kuwa kumbe Yesu aliishi kabla ya dunia kuumbwa na alikuwepo wakati wa uumbaji wa dunia.

3.   Yesu anapewa sifa ya kuwa kila mahali: (Omnipresent)
Mathay0 18:20, na Mathayo 28:20 Inasema:
20 Kwa maana wanapokutana watu wawili au watatu katika jina langu, hapo mimi nipo pamoja nao.”
Sifa ya kuwa kila mahali kwa wakati mmoja ni ya Mungu pekee, lakini Yesu anasema yeye hiyo sifa ni yake na anayo.

4.   Yesu ana adhama ya kufahamu yote:
Mathayo 16:21
Yesu Anazungumza Juu Ya Mateso Yake
21 Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi kutoka kwa wazee, makuhani wakuu na walimu wa sheria; na kwamba atauawa na siku ya tatu atafufuliwa.

5.   Yesu anapewa ADHAMA YA Mungu ya MUWEZA wa Yote:
Yohana 11: 38-44
Yesu Amfufua Lazaro

38 Yesu akafika penye kaburi akiwa amefadhaika sana. Kaburi lenyewe lilikuwa katika pango ambalo mlango wake ulikuwa umezibwa kwa jiwe.39 Akasema, “Ondoeni hilo jiwe.” Dada yake mare hemu, Martha, akasema, “Bwana, patakuwa na harufu kali kwani siku nne zimepita tangu azikwe.” 40 Yesu akamjibu, “Sikukuam bia kama ungeamini ungeuona utukufu wa Mungu?” 41 Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe. Yesu akaangalia mbinguni akasema, “Baba ninakushukuru kwa kunisikia.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW