Saturday, January 19, 2019

HIVI UNAJUA MJI WA NINAWI UPO IRAKI?

Image may contain: people standing, sky, mountain, outdoor and nature
Ninawi (kwa Kiakadi: Ninwe; kwa Kiashuru: ܢܸܢܘܵܐ; kwa Kiebrania נינוה , Nīnewē; kwa Kigiriki Νινευη, Nineuē; kwa Kiarabu: نينوى, Naīnuwa) ulikuwa mji mkuu wa Waashuru upande wa mashariki wa mto Tigri.
Magofu yake yako ng'ambo wa mto huo ukitokea Mosul (Iraki).
Katika Biblia ni maarufu hasa kutokana na habari zinazopatikana katika kitabu cha Yona na zilizotumiwa na Yesu kuhimiza toba.
Mji huu ulikuwa mkubwa kuliko yote duniani kwa miaka hamsini hadi mwaka 612 KK uliposhindwa na Wababuloni.
Kitabu katika Agano la Kale ambacho kinaelezea juu ya tukio moja katika maisha ya Yona. Yona yawezekana hakuandika kitabu hiki yeye mwenyewe. Wazo kuu la kitabu cha Yona ni kwamba Yehova anatawala kila mahali na upande wake hauzuiliwi katika taifa moja au watu fulani tu.
Katika mlango wa 1, Bwana anamwita Yona kwenda kuhubiri Ninawi. Badala ya kufanya kama Bwana alivyomwamuru, Yona alitoroka kwa mashua na akamezwa na samaki mkubwa. Katika Mlango wa 2, Yona alisali kwa Bwana, na yule samaki akamtapika Yona nje kwenye ardhi kavu. Mlango wa 3 unaandikwa kuwa Yona alikwenda Ninawi na akatoa unabii wa kuanguka kwa mji huo. Hata hivyo, watu wale wakatubu. Katika Mlango wa 4, Bwana anamkanya Yona kwa kukasirika kwa vile Bwana aliwaokoa wale watu.
Katika Agano la Kale, ni mji mkuu wa Ashuru na kwa zaidi ya miaka mia mbili ulikuwa mji maarufu wa kibiashara katika kingo ya mashariki ya mto Tigri. Ulianguka wakati wa kushuka kwa ufalme wa Ashuru, 606 K.K.
Senakeribu, mfalme wa Ashuru, aliishi Ninawi, 2 Wafalme 19:36.
Yona alitumwa kuhubiri toba kwa mji ule, Yon. 1:1–2 (Yona 3:1–4).
Watu wa Ninawi walitubu, Yona 3:5–10.
Kristo aliitumia Ninawi kama mfano wa toba mbele ya Wayahudi, Mathayo 12:41.
Kwa jiji la Ninawi, lilitambuliwa tena katika karne ya 19 baada ya miaka zaidi ya 2,500 ya mashaka. Sasa inaaminika kuwa ndiyo jiji kubwa zaidi duniani lilikuwa wakati wa mauti yake (tazama Tertius Chandler ya Miaka Elfu Nne ya Ukuaji wa Mjini: Sensa ya kihistoria). Kulingana na Mheshimiwa Austen Henry Layard, ambaye aliandika juu ya utambuaji tena wa Ninawi katika fasihi yake Ugunduzi Huko Ninawi, mzingo wa Ninawi Kuu ilikuwa "safari ya siku tatu kamili", kama ilivyoandikwa katika Yona 3:3 (Austen Henry Layard. Akaunti Maarugu ya Ugunduzi Huko Ninawi, J.C. Derby: New York, 1854, uk. 314). Kabla ya ugunduzi wake, wenye kushuku walidharau kwa uwezekano kwamba jiji kubwa sana lingeweza kuwepo katika ulimwengu wa kale. Kwa kweli, wenye kushuku walikanusha uwepo wa Ninawi kabisa. Ugunduzi wake katikati ya miaka ya 1800 ulionyesha kuwa ni uthibitisho wa ajabu kwa Biblia, ambayo inataja Ninawi kwa jina mara 18 na kutoa vitabu vyote viwili (Yona na Nahumu) kwa hatima yake.
Shalom,


No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW