Saturday, January 12, 2019

UTAFUTENI UFALME WA MUNGU NA HAYO YOTE MTAONGEZEWA

Image may contain: 3 people, people sitting, hat, beard and outdoor
Ufalme wa Mungu (au Ufalme wa mbinguni unavyoitwa hasa katika Injili ya Mathayo) ni mojawapo kati ya mada kuu za ujumbe wa Yesu Kristo katika Injili . Neno "ufalme" (kwa Kigiriki βασιλεία, Basileia) linapatikana mara 162 katika Agano Jipya, kawaida kwa maana ya Basileia tou Theou (βασιλεία τοῦ θεοῦ), Ufalme wa Mungu, au Basileia tōn Ouranōn, (Βασιλεία τῶν Ουρανῶν), Ufalme wa Mbinguni.
Kwa uwazi, ufalme wa Mungu ni utawala wa Mungu wa milele, Mwenye nguvu juu ya ulimwengu wote. Vifungu vingi vya Maandiko vinaonyesha bila kupinga kuwa Mungu ndiye Mfalme wa viumbe vyote: "Bwana ameweka kiti chake cha enzi mbinguni, Na ufalme wake unavitawala vitu vyote" (Zaburi 103: 19). Na, kama Mfalme Nebukadineza alivyosema, "Ufalme wake ni ufalme wa milele" (Danieli 4: 3). Kila mamlaka iliyopo imeanzishwa na Mungu (Warumi 13: 1). Kwa hiyo, kwa maana moja, ufalme wa Mungu unahusisha kila kitu ambacho kilichoko.
"Bali utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake, na hayo yote mtazidishiwa" ( Mathayo 6:33)
Kutokana na maneno haya ya Yesu Kristo, tunapata msingi wa tatu ambao ukiuelewa na ukautumia, unaweza ukawa na uchumi mzuri sana! Msingi huo ni huu:
Tafuta kwanza ufalme wa Mbinguni na haki yake, na hayo yote unayoyatafuta katika uchumi utapewa na kuzidishiwa."
Ukisoma Mathayo 6:24-34 utaona ya kuwa Yesu alipokuwa anasema "na hayo yote mtazidishiwa" alikuwa na maana ya mavazi, vyakula na mahali pa kulala. Kwa tafsiri iliyo laini na nyepesi ya Mathayo 6:24-34,Yesu Kristo alitaka watu wake tujue ya kuwa. Mfumo wetu wa maisha na matokeo ya kuishi kwetu, kunaonyesha ya kuwa kuna kitu ambacho mioyo yetu inakitafuta.
Luka 12: 28 Basi, ikiwa Mungu huvika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatawatendea ninyi zaidi, enyi wa imani haba?
29 Ninyi msitafute mtakavyokula wala mtakavyokunywa; wala msifanye wasiwasi,
30 kwa maana, hayo yote ndiyo watafutayo mataifa ya duniani, lakini Baba yenu anajua ya kuwa mna haja na hayo.
31 Bali utafuteni ufalme wa Mungu, na hayo mtaongezewa.
32 Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.
33 Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, akiba isiyopungua katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu.
34 Kwa kuwa hazina yenu ilipo, ndipo itakapokuwapo na mioyo yenu.
= NA HAKI YAKE MAANA YAKE NINI? =
Haki ni tunda la utawala wa Mungu katika moyo. Zaburi 119:172, “Ulimi wangu na uiimbe ahadi yako, maana maagizo yako yote ni ya haki.”
Yesu hatuambii tu kutafuta haki, bali haki Yake. Haki yo yote tuliojitengenezea haina uthamani wowote.
• Isaya 64:6, “Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi, sisi sote twanyauka kama jani, na maovu yetu yatuondoa kama upepo uondoavyo.
• Rumi 10:3, “Kwa maana wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.”
Haki Yake ni ya nguo safi yote na haita haribika. Filipo 3:8-10, “Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi kwa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili
nipate Kristo; tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani; ili nimjue yeye na uweza, wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake.”
Paulo alisema kuwa haki ya Agano La Kale ili kuwa ni kuwekwa pembeni. Imani uja kwa kusikia neno la Mungu.
Je ulishawahi kujiuliza kwamba kwa nini Yesu alibatizwa?
Mathayo 3:13-17, “Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili ambatizwe. Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu? Yesu akajibu akamwambia, kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akakubali. Naye Yesu alipotokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini, na tazama mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake; na tazama sauti
kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninaye pendezwa naye.”
Hivyo, tunapaswa mkuruhusu Mungu awe na mamlaka juu yetu; atawale pasipopingamizi.
“UTAFUTENI KWANZA MAANA YAKE NINI?”
“Kwanza” inamaanisha kwamba kuna vitu vingine ambavyo tunavitafuta, lakini vinapaswa kutothaminishwa (shushwa kiwango).
“Kwanza” inamaanisha kwamba kuna mengine.
Hatupaswi kuutafuta ufalme wa Mungu kwa kukataa majukumu yetu ya dunia; hataivyo, hatuwezi kuruhusu majuku haya ya kidunia kuingilia majukumu ya mbinguni.
Bwana wetu haitaji kwamba tuwe bila mawazo kuhusu vitu vya maisha haya.
1 Timotheo 5:8, “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.”
Roho ambayo haijali na kuwajibika huondolewa katika roho wa kweli wa Ukristo. Rumi 12:11, “Kwa bidii si walegevu, mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;”
Mkristo wa kweli anachukia uchafu kama anavyochukia ulevi, na kukimbia mambo ya kipuuzi kama anavyo kimbia kutoka katika zinaa.
Bali tunapaswa kuweka vitu vya kwanza nambari moja , na
tusiruhusu kazi ya Mungu katika maisha yetu yatingwe na mambo ambayo hayana umuhimu.
Hatuwezi kuruhusu kazi zetu, masomo ya chuo, michezo, burudani, au kitu chochote kile kije kati yetu na huduma yetu kwa Mungu. Lazima tumuweke awe wa kwanza katika kila jambo tunalofanya.
Ujuzi wangu wa kuomba kazi katika shamba la Real Estate.
Niliombwa kufanya kazi siku ya juma pili. Niliambiwa, “Hufai katika kazi hii”. Nikajibu, “Hapana hii kazi sio ya kwangu.”
Ujuzi wangu wa kuomba kazi katika Kiwanda Cha Ndege.
Niliwaambia nilikuwa napenda kufanya kazi siku yo yote ya wiki na muda wo wote katika siku, isipokuwa niliitaji kuwa kanisani jumapili asubuhi. Tulikubaliana katika hili na barua ya makubaliano iliwekwa katika faili langu kwamba sitahitajika kazini siku za juma pili asubuhi.
Walijaribu hili mara moja tu. Nikawakumbusha makubaliano yetu, na wakanigeuka wakitaka nifanye kazi jumapili moja asubuhi. Nimefanya kazi masaa mengine yote ya siku isipokuwa siku ya jumapili asubuhi.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW