Wednesday, February 6, 2019

CHAKULA CHA BWANA NI NINI?

Image may contain: one or more people and text
Chakula cha Bwana ni nini? Kwa nini kushiriki? Tushiriki mara ngapi? Haya ni maswali katika akili za wengi. Chakula cha Bwana kilianzishwa na Bwana mwenyewe kama kumbukumbu kwa ajili ya mateso yake kutokana na dhambi zetu (Mt. 26:26-29). Leo Wakristo wanaadhimisha jambo hili kukumbuka tukio kuu la vizazi vingi, kifo cha Kristo. Kushiriki katika hali ya kumpendeza Mungu, chakula hiki ni vema kiwe na vitu halali.
ASILI YA KIHISTORIA YA KARAMU YA BWANA
Injili ya Mathayo (26:26ff), Mariko (14:22ff) Na Luka (22:14ff) zinatoa habari kuhusu Karamu ya Mwisho ambayo Yesu alikula pamoja na wanafunzi wake usiku kabla ya kifo chake. Yote inaeleza Yesu kushukuru au kubariki mkate na kikombe, na kuwapa wanafunzi akisema kuwa mkate ni mwili na kikombe ni damu ya agano au agano jipya katika damu yake. Katika Luka 22:19 Yesu anasema, “fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” Injili ya Yohana haijatoa habari kuhusu kukula na kunywa bali mafundizo na matendo ambayo yalijawa kwenye jioni hiyo.
Yesu alisema: waliitekeleza karamu kama ukumbusho wa Yesu na kifo chake. Nyaraka za Paulo ndizo ushuhuda wa kwanza kabisa tulizo nazo na katika I Wakorintho 11:20 anamaanisha tukio katika uzima wa kanisa liitwalo “Karamu ya Bwana.” huitwa “Karamu ya Bwana.” kwa sababu ulianzishwa na kutawazwa na Bwana Yesu na aana yake halisi ni kusherehekea ukumbusho wa kifo cha Bwana. Paulo anasema kwenye I Wakorintho 11:23-24 “Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliowapa nanyi ya kuwa Bwana Yesu usiku ule aliyosalitiwa alitoa mkate, naye akisha kushukuru akaumega, akasema “Huu ndio mwili wangu uliyo kwa ajili yenu, fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu” “Mimi nalipokea kwa Bwana . . . ” Pengine inamaanisha kwamba Bwana mwenyewe alimdhibitishia Paulo (ambaye hakuwa mmoja wa wanafunzi siku hiyo ya Pasaka) kwamba kile wengine waliripoti kuhusu Pasaka hakika kilitendeka.
Hivyo asili ya historia ya Karamu ya Bwana ni hicho chakula cha mwisho ambayo Yesu na wanafunzi walikula usiku kabla ya kusulubishwa. Maana na kitendo hiki kina shina kwa kile Yesu alisema na kufanya katika usiku huo wa mwisho. Yesu mwenyewe ndiye chimbuko cha chakula cha Bwana. Aliamuru kwamba kiendelee na yeye ndiye tegemeo na muhusika ndani yake.
Vitu Halali
Mkate na uzao wa mzabibu ndivyo vitu vya msingi. Ingawa si mwili na damu halisi, mkate ni ushirika wa mwili wa Kristo na kikombe ushirika wa damu yake (Lk. 22:12-20). Wakristo wanapoizingira meza hii mioyo yao inachochewa kwa uaminifu kutambua maisha yake yenye utukufu yalivyotolewa kafara na kifo chake msalabani kwa ajili ya ulimwengu mwovu.
WASHIRIKI WANACHOKIAMINI CHAKULA CHA BWANA
Chakula cha Bwana ni kitendo cha mkusanyiko wa familia ya walioamini Yesu, yaani Kanisa. Si kitendo cha wasioamini. Wasioamini wanaweza kuwepo—kwa kweli, tunawakaribisha—hakika hakuna kilichositirika kuhusu chakula cha Bwana.
Yesu alisema angekunywa kwa kikombe hiki pamoja na wale waliomo katika Ufalme wa Baba (Mt. 26:29) waamini waliobatizwa waliendelea kwa juhudi katika kumega mkate, (Mdo. 2:42).
Wanafunzi walikuja pamoja kukutanika Siku ya Kwanza ya juma kumega mkate (Mdo. 20:7).
Wale waliomo katika Kanisa la Bwana ndio watu halali wa kushiriki Chakula cha Bwana.
Lakini hakuna aliye na haki ya kukataza au kufunga ushirika huo kwa sababu Paulo alisema “Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe,” (1 Kor. 11:28).
KUSHIRIKI KATIKA DAMU NA MWILI WA KRISTO KIROHO KWA IMANI
Mawazo haya ya “Kushiriki mwili wa Kristo na damu . . . kiroho . . . kwa imani” yametoka wapi? Kifungu cha karibu zaidi kuhimiza haya ni katika sura inayotangulia: I Wakorintho 10:16-18 Ninapokisoma jiulize “Ni nini maana ya ‘kushiriki’?” “Kikombe cha baraka tukibarikicho, Je! Si ushirika wa damu ya Kristo?
Naje ushirika huu una maana gani? Kushiriki, kugawana, na ushiririkiano yana maana gani? Nafikiri mstari wa 18 unatupa fikira kwa sababu unatumia neno sawa lakini analilenganisha na ninachotendeka katika dhabibu ya Wayahudi. “Waangalieni hao waisraeli: si wale wanaokula dhabibu Washirika ni kama kisawe kwenye madhabahu?” Nini maana ya washirika/washiriki, wanaoshiriki kwenye madhabahu? Ina maana kuwa wanashirikiana katika au wanafaidika kwa kile kinachoendelea katika madhabahuni. Wanafurahia, kwa mfano, msamaha na urejesho wa ushirika pamoja na Mungu.
Basi naichukua mstari wa 16 na 17 kumaanisha kwamba waumini wanapokula mkate na kunywea kikombe kimwili tunatenda aina nyingine ya kula na kunywa kiroho. Tunala na kunywa—yaani tunaingiza katika maisha yetu—Kilichotendeka kwa msalaba. Kwa Imani—kwa kutumaini ndani ya yote ambayo Mungu yu kwa ajili yetu ndani ya Yesu—tunajistawisha kwa fadhili ambazo Yesu aliyotupokeza kwetu alipotiririsha damu na kufa msalabani.
Hii ndiyo sababu tunawaongoza kwa mtazamo tofauti tofauti kwenye meza la Bwana kila mwezi (amani na Mungu, furaha kwa Yesu, tumaini la usoni, uhuru kutokana na uoga, usalama wakati wa mabaya, muelekeo wakati tumekwama, uponyaji wa magonjwa, ushindi wakati wa majiribio n. k). Kwa kuwa Yesu alipokufa damu yake iliyomwagika na mwili uliovunjika; uliotolewa kwenye kifo chake kwa niaba yetu, alizinunua kila ahadiza mungu.
Paulo anasema, “Maana ahadi zote za Mungu zilipo katika yeye ni ndiyo” (2 Wakorintho 1:20) kila kipawa cha Mungu na furaha ya ushirika wetu pamoja na Mungu, tuliupokea kwa damu ya Yesu. Paulo anaposema, “Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuuegemeao si ushirika wa mwili wa Kristo? Anaamanisha: Je, si tunashiriki kwenye meza ya Bwana kiroho kupitia imani kila Baraka ya kiroho uliogharamiwa kwa mwili na damu ya Yesu? Hakuna asiyeamini awezaye kufanya hivyo. Shetani hawezi. Ni karama kwa familia. Tunaposherehekea meza ya Bwana, tunasheherekea kiroho kwa imani katika kila ahadi za Mungu zilizonunuliwa kwa damu ya Yesu.
Roho Inayostahili
Isipokuwa katika jicho lenye akili, “Kuupambanua mwili, anakula na kunywa hukumu ya nafsi yake,” (1 Kor. 11:29). Kwa sababu baadhi ya Wakorintho walishiriki Chakula cha Bwana katika hali isiyostahili na wala taadhima katika Roho, wakawa dhaifu na wasiojiweza (1 Kor. 11:30).
Katika kushiriki, afanye hivyo kwa kumbukumbu....... “Fanyeni hivi…kwa ukumbusho wangu” na kwa kujihoji, “lakini mtu ajihoji mwenyewe” na kwa matazamio, “mwitangaze mauti ya Bwana hata ajapo,” (1 Kor. 11:25, 26, 28).
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW