Monday, May 6, 2013

Yesu alikuwa wapi katika siku tatu toka siku ile ya kufa mpaka kufufuka?

Image may contain: outdoor and text
Kama Yesu alivyotabiri, alisalitiwa na mmoja wa wafuasi wake, Yuda Iscariot, na alikamatwa. Katika shitaka la kufedhehesha chini ya Gavana wa Kirumi, Pontio Pilato, alitiwa hatia ya uhaini na alilaaniwa kufa kwenye msalaba wa mbao. Kabla ya kupigiliwa misumari msalabani, Yesu alipigwa kwa ukatili kwa mjeledi wenye mifupa vyuma ambao ulinyofoa nyama. Alisukumwasukumwa, alipigwa mateke, na alitemewa mate.
Yesu akamwambia (mwizi aliyetubu) Amini nakwambia, leo utakuwa pamoja paradiso .
.
Luka 23:39 Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: "Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia." 40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: "Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo. 41 Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya." 42 Kisha akasema, "Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako." 43 Yesu akamwambia, "Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi."
Hii inathibitisha kuwa roho ya Yesu na yule Mwizi aliyetubu hazikukoma kuishi bali zilikwenda Paradiso . Je, huko ndipo alipo kuwa Yesu kwa siku tatu?
Petro wa kwanza 3:18-19 inaeleza, “kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi zetu, mwenye haki kwa ajili yao wasiohaki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake ukauawa, bali roho yake ikahuishwa, ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokuwa kifungoni akawahubiri.”
Siku tatu kuu za Pasaka ndizo kiini cha mwaka wa Kanisa.
Zinamuadhimisha Yesu mteswa, mzikwa na mfufuka, yaani siku ya kwanza (Alhamisi kuu jioni hadi Ijumaa kuu jioni) inaadhimisha mateso yake kuanzia karamu ya mwisho hadi kifo cha msalaba; siku ya pili (Ijumaa kuu jioni hadi Jumamosi kuu jioni) inaadhimisha maiti yake kubaki kaburini na roho yake kushukia kuzimu; siku ya tatu (kuanzia Jumamosi kuu jioni hadi Jumapili ya Pasaka jioni) inaadhimisha ufufuko wake mtukufu.
Petro wa Kwanza 3:18-22 inaeleza ushikamano wa kuteswa kwake Kristo (fungu la 18) na kutukuzwa kwake (fungu la 22). Petro ndiye anayefafanua yaliyotokea katikati ya matukio haya mawili. Neno “alihubiri’ katika fungu la 19 lina maana ya kuwa aliwasilisha ujumbe. Yesu aliteswa na kufa msalabani, mwili ukiuawa na roho yake pia kufa kwa kufanywa dhambi. Lakini roho yake ilifufuliwa naye akaikakabidhi Baba. Kulengana na Petro, muda huo baada ya kufa mpaka kufufuka Yesu aliwasilisha hali Fulani ya ujumbe kwa “roho waliokuwa kifungoni.”
Bwana wetu aliikabidhi roho yake kwa Baba, akafa na wakati Fulani toka kufa mpaka kufufuka, akatembelea kuzimu alikowasilisha ujumbe kwa viumbe vya kiroho 9 pengine ni malaika waasi tazama yuda 6) waliokuwa na uhusiano na nyakati za kabla gharika la wakati wa Nuhu. Kifungu cha 20 kinafafanua zaidi. Petro hakutuambia kilichoambiwa roho hawa waliokuwa kifungoni lakini haiwezi kuwa ilikuwa habari ya wokovu kwa kuwa malaika hawaokolewi (Waebrania 2:16). Pengine ilikuwa ni kutangazwa kwa kushindwa kwa shetani na milki yake (Petro wa kwanza 3:22; Wakolosai 2:15). Waefeso 4:8-10 pia inajaribu kueleza kuwa Kristo alienda “paradise” (Luka 16:20; 23:43) na akawachukua mpaka mbinguni wale waliokuwa wamemuamini kabla kufa kwake.
Biblia haifafanui wazi wazi kilichotendeka ndani ya muda wa siku tatu hizi toka kufa mpaka kufufuka. Haiwezi kueleweka ya kuwa alikuwa ameenda kuwapa watu nafasi ya pili ya kuokolewa kwa kuwa biblia inatuambia ya kuwa tunakutana na hukumu punde tu baada ya kufa (Waebrania 9:27).
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Friday, May 3, 2013

Where Do We Go When We Die?


Because he is the only one who died and came back to life on the third day, Jesus knows more about death than everyone who has speculated about what happens after we die. Even near-death experiences do not tell the whole story.

Believers

CrucifixionJesus told the dying thief on the cross next to him, "I tell you the truth, today you will be with me in paradise." (Luke 23:43) Jesus told his disciples, "I will come back and take you to be with me that you also may be where I am." (John 14:3). So, believers go to be with Jesus when they die.
Heaven

Non-believers

Lake of FireJesus told a parable about a rich man who was a non-believer. "The rich man also died and was buried. In hell, where he was in torment, he looked up and saw Abraham far away." (Luke 16:22-23) Jesus also said, "And if your eye causes you to sin, pluck it out. It is better for you to enter the kingdom of God with one eye than to have two eyes and be thrown into hell, where 'their worm does not die, and the fire is not quenched'." (Mark 9:47-48). Even though Jesus was exaggerating for emphasis when he said "Pluck it out," it is clear that non-believers go to a horrible place called hell.

Hell: Hades and Gehenna

Jesus used two different words for hell. The first is Hades which is a temporary place where the dead go until the final judgment. Sometimes Hades is translated as grave. "The sea gave up the dead that were in it, and death and Hades gave up the dead that were in them, and each person was judged according to what he had done." (Revelation 22:13)
The second word is Gehenna which literally referred to the Valley of Hinnom, which was Jerusalem's dump where the garbage was burned. Figuratively, Gehenna refers to the lake of fire. "Then death and Hades were thrown into the lake of fire. The lake of fire is the second death. If anyone's name was not found written in the book of life, he was thrown into the lake of fire." (Revelation 22:15-16)





Paradise, the Millennium and the New Jerusalem

New JerusalemParadise is also a temporary place for believers. When Jesus returns to the earth, he will bring with him all of the believers who have died. They and the believers who are still alive will reign with Jesus during the Millennium, the one thousand year period when Jesus is king over all the earth. See 1 Thessalonians 4:15-17, Revelation 20:4-6.
At the end of the Millennium comes the final judgment described above. "Then I saw a new heaven and a new earth, for the first heaven and the first earth had passed away, and there was no longer any sea. I saw the Holy City, the new Jerusalem, coming down out of heaven from God, prepared as a bride beautifully dressed for her husband. And I heard a loud voice from the throne saying, "Now the dwelling of God is with men, and he will live with them. They will be his people, and God himself will be with them and be their God. He will wipe every tear from their eyes. There will be no more death or mourning or crying or pain, for the old order of things has passed away." (Revelation 21:1-4)

Tuesday, April 30, 2013

Kujichua – je, ni dhambi kulengana na Biblia?


Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.

Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.

Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.

Biblia inasema je ju ya chale/ kujitoboa mwili?


Agano la kale liliwaamuru waIsraeli, “Msiikate miili yenu kwa ajili ya wafu wala kuchanja chale juu ya ngozi za miili yenu.Mimi ni Bwana” (mambo ya walawi 19:28). Hata hivyo ijapokuwa waumini kwa sasa hawako chini ya sheria ya agano la kale (warumi 10:4; wagalatia 3:23 – 25; waefeso 2:15), hoja ya kuwa kulikuwa na sheria juu ya chale lazima lituletee maswaliagano jipya haisemi lolote juu ya muumini achanjwe chale au asichanjwe.

Kulengana na swala la chale na kujikata alama mwilini, mtazamo wetu ni uwe; je, twaweza kumuomba Mungu atumie alama hizo kwa utukufu wake? “kwa hivyo mnapokula, mnapokunywa, chochote mfanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Biblia haituamuru kinyume cha chale na alama za mwili lakini pia haituonyeshi ya kuwa ana haja na alama hizo miilini mwetu.

Jambo lengine ni nidhamu. Biblia inatushauri kuvaa mavazi yetu kwa nidhamu (Timotheo wa kwanza 2:9). Kuvaa ki nidhamu ni kuziba sehemu zote zilizotarajiwa kuzibwa na mavazi. Lengo la nidhamu hii ya ki mavazi si juu ya wewe mwenyewe bali kwa ajili ya wengine wasije wakanaswa na hali yakuvutiwa nawe kiasi cha kukutamani. Chale pia zinaushawishi Fulani kwa hivyo zinakeuka mipaka ya nidhamu hii.

Kanuni muhimu ya kibiblia ni kutazama jambo kwa mfumo wa imani. Kama hulionei shaka moyoni juu yakuwa linampendeza Mungu basi lifanye. “kwa kuwa lolote ambalo, si la imani ni dhambi” (warumi 14:23). Tunapaswa kufahamu kuwa miili yetu na nafsi zetu pia zimekombolewa na ni mali ya Mungu. Ijapokuwa haelekei moja kwa moja juu ya chale na alama za miili, wakorintho wa kwanza 6:19 -20 inatupatia kanuni moja, “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, akaaye ndani yenu, ambaye mnaye kutoka kwa Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe. Mmenunuliwa kwa thamani kwa hivyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu na katika roho zenu ambvyo ni vya Mungu.” Miili yetu sharti iandamane na ukweli kokote tuendako. Kama miili yetu ni mali ya Mungu basi lazima tuwe na ruhusa yake kabla hatujajichanja chale hizo au alama hizo za mwili.

Mkristo ni mtu gani?


Kwa tafsiri kutoka kamusi ya Webster Mkristo ni “mtu mwenye kukiri imani ndani ya Yesu kama Kristo au Imani yenye msingi wa mafundisho na ufunuo wa Yesu.” Ijapokuwa huu ni mwanzo mwema wa kufahamu Mkristo ni mtu gani, kama maelezo mengi ya kidunia yalivyo, inapungukiwa na uhalisi wa kibiblia juu ya Maana kamili ya Ukristo au Mkristo. 


Neno Mkristo limetumika mara tatu katika agano jipya (Matendo 11:26; Matendo 26:28; Petero Wa Kwanza 4:16). Wafuasi wa Yesu Kristo waliitwa kwa mara ya kwanza “Wakristo” antiokia (Matendo 11:26) kwa sababu tabia zao, matendo yao na hotuba zao zilikuwa kama za Kristo. Ilitumika kiasili na watu wasiookoka wa Antiokia kama jina la kimajazi kuwadhihaki wakristo hao. Ina maana sawa na “Kuwa mmoja wa kundi la kristo” au “mfuasi wa Kristo,” ambayo imefanana na tafsiri ya Neno hili katika kamusi ya Webster.

Kwa bahati mbaya, neno Mkristo limepoteza kwa kiwango kikubwa usawa wa matumizi yake na Linatumika mara kwa mara kumaanisha tu mtu mwenye dini au pengine muadilifu kinyume cha Mfuasi halisi wa Yesu Kristo aliyezaliwa mara ya pili. Watu wengi wasioamini na kuwa na tumaini ndani ya Yesu Kristo hujichukulia tu kuwa ni wakristo kwa sababu wanahudhuria ibada za Kanisa ama wanaishi katika taifa la kikristo. Lakini, kuenda kanisani, kuwahudumia wale wasiobahatika maishani au kuwa mtu mzuri haviwezi kukufanya kuwa mkristo. Kama Muinjilisti mmoja alivyosema, “kuenda Kanisani hakufanyi mtu kuwa Mkristo sawa na mtu kuenda gereji hakumfanyi kuwa gari.” Kuwa mshirika wa kanisa anayehudhuria ibada kila mara na kutoa kwa ajili ya kazi za kanisa hakuwezi kukufanya wewe kuwa Mkristo.

Je ni nini kitawapata watu wale hawajawai pata nafasi ya kusikia kuhusu Yesu?


Je ni nini kitawapata watu wale hawajawai pata nafasi ya kusikia kuhusu Yesu? Je Mungu atawahukumu wale ambao hajawai sikia kuhusu Yesu?"

Jibu: Watu wote wamewajibika kwa Mungu hata kama wamesikia au hawaja “sikia kumhusu” Bibilia yatwambia wazi wazi kuwa Mungu anajidhihirisha mwenyewe kwa uungu (Warumi 1:20) na katika Roho za watu (Mhubiri 3:11). Shida ni kwamba ni uzao wa dhambi wa mwanadamu. Zote twakataa hii hekima ya Mungu na kuasi (Warumi 1:21-23). Kama isingekuwa ni neema ya Mungu, tungejitolea kwa mioyo ya dhambi, kujiruhusu kujigundulia vile maisha ni bure, yakustaajabisha ni sehemu kando naye Mungu. Anafanya haya kwa wale wanaoendelea kumkataa (Warumi 1:24-32).

Ukweli ni, si eti watu wengine hawajasikia juu ya Mungu. Badala, shida ni wamaekataa chenye wamesikia na chenye kinaonekana katika uumbaji. Kumbukumbu La Torati 4:29 yasema, “Lakini huko, kama mkimtatufa BWANA, Mungu wako, utampata, ukimtafuta kwa moyo wako wote, na roho yako yote.” Aya hii yatufunza nguzo muimu. Kila mmoja anayemtafuta Mungu atampta. Kama mtu amenuia kumjua Mungu, Mungu atajudhihirisha kwake.

Shida pekee, “Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu” (Warumi 3:11). Watu wanakataa hekima ya Mungu ambayo ipo katika uumbaji na katika mioyo yao, na badala wanaanza kuabudu “miungu” yao wenyewe wamejitengenezea. Ni ubumpavu kubishana juu ya haki/uungwana wa Mungu kumtuma mtu jahanamu mwenye hakuwa na nafasi ya kuisikia injili ya Kristo. Watu watawajibika kwa Mungu kwa yale yote Mungu ameyafunua kwao. Bibilia inasema watu wanakataa hekima na kwa hivyo Mungu ako haki anapowahukkumu kwenda jahanamu.

Mpango Wa Wokovu ni nini?


Una njaa? Si njaa ya chakula, lakini je, una njaa ya kitu Fulani zaidi maishani? Je, kuna hali Fulani ya kutotosheka ndani yako? Ikiwa iko basi Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi mkate wa kweli. Kila ajaye kwangu hatahisi njaa na aniaminiye hataona kiu” (Yohana 6:35).

Je, umechanganyikiwa? Je, huoni mbele ya maishani mwako? Je, unajihisi kama umeachwa kwenye giza na huoni pa kutokea? Ikiwa hali yako ni kama hiyo basi Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi nuru ya ulimwengu. Anifuataye hatatembea gizani, bali atakuwa na nuru ya uzima” (Yohana 8:12).

Je, unajisikia kama umefungiwa nje ya maisha yako? Je, umejaribu njia nyingi na kutambua ya kwamba kile ulichokitarajia hakipo ndani yake? Je, unatafuta njia ya kufikia maisha makamilifu? Ikiwa haya ndiyo uyatafutayo, Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi mlango wa kondoo; aingiaye kupitia mimi ataokolewa. Ataingia na kutoka na kupata malisho” (Yohana 10:9).

Je, watu wengine husababisha kushindwa kwako? Je, uhusiano wako nao umekuwa si wa kina na bila muelekeo? Je, ni kama watu wanakutumia tu kwa manufaa yao? Ikiwa ndiyo hali unayopitia Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema hutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo……. Mimi ndimi mchungaji mwema; Ninajua kondoo wangu na kondoo wangu wananijua” (Yohana 10: 11,14).

Je, unashangazwa na kinachotendeka baada ya maisha haya? Je, umechoshwa na maisha ya kupigania tu vitu vinavyooza na kushika kutu? Je, wakati mwingine maana ya maisha yako huionea shaka? Je, unataka kuishi hata baadaya kufa? Ikiwa haya ndiyo uliyonayo basi Yesu ndiye njia! Yesu alisema, “Mimi ndimi huo ufufuo na uzima. Aniaminiye ataishi, hata ajapokufa; na aishiye na kuniamini hata kufa kamwe” (Yohana11:25-26).

Njia ni nini? Ukweli ni nini? Uzima ni nini? Yesu akajibu, “Mimi ndimi njia kweli na uzima.Hakuna afikaye kwa baba bila kupitia kwangu” (Yohana 14:6). 

Monday, April 29, 2013

Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga? Je, Ushoga ni dhambi?


Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.

Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.

Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).

Biblia inasema nini juu ya kushirikiana katika ngono kabla kuoana?


Pamoja na matendo mengine ya uchafu, kufanya kitendo cha mapenzi kabla kuoana kumekatazwa katika maandiko (matendo 15:20; warumi 1:29; wakorintho wa kwanza 5:1; 6:13, 7:2; 10;8; wakorintho wa pili 12:21; wagalatia 5:19; waefeso 5:3; wakolosai 3:5; wathesalonike 4:3; yuda7). Biblia inasisitiza kuepuka kitendo hicho kabla ya ndoa.hii ina maana ya kuwa ni dhambi kama ya uzinifu kwa kuwa hujaunganishwa na unayefanya naye kitendo hicho. Mapenzi baina ya mume na mke waliooana ndiyo mapenzi yanayokubalika mbele za Mungu (waebrania 13:4).

Kushirikiana katika ngono kabla ndoa kumeenea sana kwa sababu nyingi. Mapenzi yanastarehesha. Mungu aliyaumba hivyo. Anawataka wanaume na wanawake wafurahie kitendo cha ngono (ndani ya ndoa). Hata hivyo, lengo la msingi la ngono si starehe bali kuzaana tukaongezeke. Hivyo tunazuiwa kufanya kitendo cha ngono kabla ndoa ili tusijipatie watoto tusiowatarajia. Kama jambo hili lingezingatiwa, magonjwa ya zinaa na wamama wasioolewa na kuavya mimba na kadhalika kungepungua. Kujizuia kunaokoa maisha, kunalinda watoto wachanga na kuleta ladha halisi ya ngono pamoja na heshima kwa Mungu.

Biblia inasema nini juu ya kunywa kileo? Je, ni dhambi kwa mkristo kunywa kileo?


Maandiko yana ilani nyingi juu ya kunywa kileo (mambo ya walawi 10:9; hesabu6:3; kumbukumbu la torati 29:6; waamuzi 13:4,7,14; samueli wa kwanza 1:15; methali 20:1; 31:4,6; isaya 5:11;22; 24:9; 28:7; 29:9; 56:12; mika 2:11; luka 1:15). Maandiko hayakatazi mkristo kunywa pombe, divai wala kinywaji chochote chenye kileo ndani. Maana maandiko mengine huzungumzia kileo kwa kuhalalisha matumizi yake. Mhubiri 9:7 inaamuru, “ kunywa kileo na moyo mkunjufu.” Zaburi 104:14-15 inaeleza Mungu hutoa divai “ inayofurahisha mioyo ya wanadamu.” Amosi 9:14 inazungumzia juu ya kunywa divai kutoka kwa shamba lako kama alama ya baraka za Mungu. Isaya 55;11 inapongeza “ naam, njoo ununue divai na maziwa…”

Kile Mungu anachowaamuru wakristo juu ya kileo ni wajizuie na ulevi (waefeso 5:18). Biblia inakataza ulevi na athari zake (methali 23:29-35). Wakristo wanakatazwa kuachilia miili yao itawalwe na vitu vinginevyo. (wakorintho wa kwanza 6:12; petro wa pili 2:19). Kunywa kileo kingi kunaathiri mtu. Maandiko yanakataza chochote kile ambacho kwa kukifanya unasababisha wengine kujikwaa( wakorintho wa kwanza 8:9-13). Kwa mujibu wa haya ni vigumu mkristo kukiri kuwa anakunywa kileo kwa utukufu wa Mungu ( wakorintho wa kwanza 10;31). 

Yesu aligeuza maji kuwa Divai. Huenda ikawa Yesu alikuwa akinywa divai katika karamu Fulani Fulani (Yohana 2:1-11; Mathayo 26: 29). Katika nyakati za agano jipya, maji yalikuwa yakijawa na vidudu na uchafu kama hali ilivyo sasa katika mataifamengine ya ulimwengu wa tatu. Hii ndiyo sababu watu walipendelea kunywa divai kutoka kwa zabibu ili kuepukana na taka taka hizi. Katika timotheo wa kwanza 5:23, Paulo alimkataza timotheo kunywa maji yaliyokuwa yakimtatiza tumbo lake na mahali pake anywe divai. Divai ilikuwa na asili ya kileo ndani lakini haikuwa na kiwango cha kilevi sawa na cha leo. Haikuwa maji ya mzabibu moja kwa moja wala kileo sawa na cha leo. Maandiko hayakatazi mkristo kunywa kileo cha aina yoyote bali yanakataza ulevi na utumwa wa kileo (waefeso 5:18; wakorintho wa kwanza 6:12).

Kileo, kinapotumiwa kwa uchache hakina athari kwa mwenye kukitumia. Kutumia kiasi kichache cha kileo ni jambo linaloruhusiwa mkristo. Ulevi na utumwa wa kunywa kileo ni dhambi. Kwa sababu ya kushindwa kujizuia katika viwango vya matumizi ya kileo, kukwaza wengine na hata kupatikana na hatia mbali mbali, ni vizuri mkristo aepukane kabisa na matumizi ya kileo cha aina yoyote.

TRENDING NOW