Tuesday, May 7, 2013

Je, Nina wezaje kupokea msamaha wa dhambi toka kwa Mungu?


Matendo ya Mitume 13:38 yasema, “Basi naijulikane kwenu, ndugu zangu ya kuwa kwa huyo mnahubiriwa msamaha wa dhambi.”

Msamaha ni nini na kwanini ninauhitaji?

Neno “samehe” linamaanisha kusafisha nia au jambo nakulifanya kutokuwa na mawaa yoyote, ku achilia, kufutilia mbali deni. Tunapo kosea mtu, huuliza msamaha wao ili tukarudishe uhusiano. Msamaha haupeanwi kwa sababu mtu anastahili kusamehewa. Hakuna anaye stahili kusamehewa. Msamaha ni ishara ya upendo, huruma na neema. Msamaha ni uamuzi wa kutoshikilia jambo ndani yako kinyume cha mtu mwengine, haijalishi amekukosea kiasi gani.

Bibilia inatuambia yakwamba sote tunahitaji msamaha toka kwa Mungu. Sote tumefanya dhambi. Mhubiri 7:20 asema, “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.” 1Yohana 1:8 asema, “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.” Dhambi zote ni kitendo cha uasi kinyume chake Mungu (Zaburi 51:4). Basi kwa hivyo, tunahitaji kwa vyovyote msamaha wake Mungu. Kama dhambi zetu hazitasamehewa, tutakuwa katika adhabu ya milele tukiteseka kwa ajili ya madhara ya dhambi zetu (Mathayo 25:46;Yohana 3:36).

Msamaha-Je, ni upate vipi?

Kwa shukurani, Mungu ni mwenye upendo na huruma-mwenye ari ya kutusamehe dhambi zetu! 2Petro 3:9 asema, “Yeye hutuvumilia maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.” Mungu anatamani kutusamehe, kwa hivyo alitoa kwa ajili ya msamaha wetu.

Adhabu ya haki pekee inayostahili kwa ajili ya dhambi zetu ni mauti. Sehemu ya kwanza ya kitabu cha Warumi 6:23 yasema, “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti…..” Mauti ya milele ndiyo ndiyo tuliyopokea kama mshahara wa dhambi zetu. Mungu, kwa mpango wake mahususi, alifanyika kuwa mwanadamu - Yesu Kristo (Yohana 1:1, 14). Yesu alikufa juu ya msalaba kwa kuchukua adhabu tuliyo stahili-mauti. 2Wakorintho 5:21 inatufundisha, “Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika yeye. “Yesu alikufa msalabani, akichukua adhabu tuliyo stahili!Kama Mungu, kifo chake Yesu kilitoa msamaha wa dhambi kwa ulimwengu mzima. 1Yohana 2:2 asema, “Naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote. “Yesu alifufuka katika wafu, akishuhudia ushindi juu ya dhambi na mauti (1Wakorintho 15:1-28). Mungu apewe sifa kwa kupitia kifo na kufufuka kwake Yesu Kristo, Sehemu yote ya pili ya kitabu cha Warumi 6:23 ni kweli, “…bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.”

Je umeshapata Zawadi ya Uzima wa milele?


Bibilia inaonyesha njia ya wazi ya uzimani.Mwanzo ni sharti tutambue yakwamba tumetenda dhambi kinyume chake Mungu: “Kwasababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu” (Warumi 3:23). Sote tumefanya mambo ambayo hayampendezi Mungu,ambayo yanafanya tustahili adhabu.Kwa kuwa dhambi zetu ziko kinyume kabisa na Mungu aliye uzima wa milele,basi ni adhabu ya milele pekee itoshayo. “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti,bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu” (Warumi 6:23).

Hata hivyo Yesu Kristo asiyekuwa na dhambi (1 Petro 2:23), mwana wa Mungu alifanyika kuwa mwanadamu (Yohana 1:1,14) na akafa ili kutulipia adhabu. “Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi,kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu,tulipokuwa tungali wenye dhambi” (Warumi 5:8). Yesu Kristo alikufa msalabani (Yohana 19:31-42), kwa kuchukua adhabu ambayo sisi tulistahili (2Wakorintho 5:21). Siku tatu baadaye akafufuka katika wafu (1Wakorintho 15:1-4), kudhihirisha ushindi juu ya dhambi na mauti. “kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu” (1Petro 1:3).

Kwa imani ni sharti tuungame dhambi zetu na tumrejee Kristo kwa ajili ya wokovu (Matendo 3:19). Tukiweka imani yetu kwake, kwa kuamini kifo chake msalabani kama malipo ya dhambi zetu,tutasamehewa na kuahidiwa uzima wa milele mbinguni. “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele” (Yohana 3:16). “Kwa sababu,ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka” (Warumi 10:9). Imani pekee katika kazi aliyo ikamilisha Kristo pale msalabani ndiyo njia ya kweli ya pekee ya uzimani! “Kwa maana nimeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zetu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yoyote asije akajisifu” (Waefeso 2:8-9).

Monday, May 6, 2013

Ni kwa nini uzao wa ubikira ni wa maana?


 Funzo la uzao wa ubikira ni la maana sana (Isaya 7:14 Mathayo 1:23; Luka 1:27,34). Kwanza, hebu tuangazie vile bibilia inavyo lieleza swala la uzao wa ubikira. Kulingana na swali la Mariamu, “Litakuwaje neno hili?” (Luka 1:34), Gabrieli anasema, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu” (Luka 1:35). Malaika alimtia moyo Zekaria isiwe na hofu mchukue Mariamu kama mke wako kwa maneno haya: “mimba aliyoibeba ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu” (Mathayo 1:18). Wagalatia 4:4 pia yafunza juu ya uzao wa ubikira “Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke.”

Kutoka kwa ukurasa huu, ni kweli kwamba kuzaliwa kwa Yesu kulikuwa kwa Roho Mtakatifu uliofanya kazi ndani ya Mariamu. Roho usio na mwili na mwili (tumbo ya Mariamu) vyote viliusika. Mariamu hangeweza kujitia mimba, kwa hali hiyo alitumika kama “chombo” ni Mungu pekee angeweza kutenda muujiza wa mwili na kuchukua ule wa mwanadamu.

Kukataa upatanisho wa Mariamu na Yesu itamaanisha kwamba Yesu hakuwa binadamu kabisa. Maandiko yafunza kwamba Yesu alikuwa binadamu, mwili kama wetu. Huu aliupokea kutoka kwa Mariamu. Kwa wakati huo, kikamilifu Yesu alikua Mungu, akiwa na mwili wa milele usio na mawaa (Yohana 1:14; 1Timotheo 3:16; Waebrania 2:14-17.)

Yesu hakuzaliwa kwa dhambi; hiyo ni kusema hakuwa na hali ya dhambi (Waebrania 7:26). Itaonekana kuwa hali ya dhambi itapitishwa kutoka kizazi hadi kizazi kingine kupitia kwa baba (Warumi 5:12, 17, 19). Uzao wa ubikira wa Yesu haukufuata hali ile ya kupitisha dhambi kutoka kizazi hadi kizazi na kumruhusu Mungu aishiye milele kuwa mwanadamu kamili.

Je Yesu alienda kuzumuni kati ya kifo chake na kufufuka?


Kuna kuchanganyikiwa kwingi kuhusu swali hili. Mwelekeo watoka kwa mafunzo ya mitume kumi na wawili ambao wasema, “alishuka kuzumuni.” Kuna maandiko machache ambayo kulingana na vile yametafsiriwa yanaelezea juu ya Yesu kuenda kuzimuni. Kwa kulichanganua swala hili, ni muimu kwanza kuelewa chenye Bibilia inafunza kuusu ulumwengu wa wafu.


Katika bibilia ya Kiibrania neno ambalo limetumika kuelezea ulimwengu wa wafu ni sheol. Linamaanisha “mahali pa wafu” au “mahali pa roho/mioyo iliyotuacha” Neno la kigiriki katika Agano Jipiya limetumika kusimamia ni “kuzumuni” ambalo pia lamaanisha “mahali pa wafu” maandiko mengine katika Agano Jipiya yanaonyesha kuwa “kuzumu” ni mahali pa muda, ambapo roho zinawekwa zinapongoja ufufuo na hukumu ya mwisho. Ufunuo 20:11-15 unatupa tofauti halisi kati ya maneno hayo mawili kifungoni (sheol) na kuzumuni (hades). Jehanamu (ziwa la moto) ni mahali pa kudumu na hukumu ya mwisho kwa wanaoangamia. Kuzimuni ni mahali pa muda. Kwa hivyo, la! hasha Yesu hakuenda kuzumuni kwa sababu kuzumuni ni ulimwengu ujao ndio neno hilo litakapokuwa likitumika baada ya kiti cheupe cha hukumu (Ufunuo 20:11-15).

Kuzumu ni ulimwengu umegawa mara mbili (Mathayo 11:23, 16:18; Luka10:15, 16:23; Matendo ya Mitume 2:27-31), mahali pa watakaokolewa na wanao angamia. Mahali pa watakaokolewa paliitwa “paradiso” na ni “kifua cha Abrahamu”. Mahali pa watakaokolewa na watakaoangamia pametenganishwa na “shimo kubwa” (Luka 16:26). Wakati Yesu alipaa mbunguni, aliwachukua wa hudumu wa paradiso waliokuwa waumini pamoja naye kwenda mbunguni (Waefeso 4:8-10). Mahali pa kuzumuni hapakubadilishwa. Wafu wote wasioamini walienda huko wakingoja hukumu yao ya mwhisho ambayo inakuja. Je Yesu alienda kifungoni mahali roho zilikuwa zikingoja hukumu?. Ndio kulingana na (Waefeso 4:8-10 na 1Petero 3:18-20).

Yesu alikuwa wapi katika siku tatu toka siku ile ya kufa mpaka kufufuka?

Image may contain: outdoor and text
Kama Yesu alivyotabiri, alisalitiwa na mmoja wa wafuasi wake, Yuda Iscariot, na alikamatwa. Katika shitaka la kufedhehesha chini ya Gavana wa Kirumi, Pontio Pilato, alitiwa hatia ya uhaini na alilaaniwa kufa kwenye msalaba wa mbao. Kabla ya kupigiliwa misumari msalabani, Yesu alipigwa kwa ukatili kwa mjeledi wenye mifupa vyuma ambao ulinyofoa nyama. Alisukumwasukumwa, alipigwa mateke, na alitemewa mate.
Yesu akamwambia (mwizi aliyetubu) Amini nakwambia, leo utakuwa pamoja paradiso .
.
Luka 23:39 Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: "Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia." 40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: "Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo. 41 Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya." 42 Kisha akasema, "Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako." 43 Yesu akamwambia, "Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi."
Hii inathibitisha kuwa roho ya Yesu na yule Mwizi aliyetubu hazikukoma kuishi bali zilikwenda Paradiso . Je, huko ndipo alipo kuwa Yesu kwa siku tatu?
Petro wa kwanza 3:18-19 inaeleza, “kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi zetu, mwenye haki kwa ajili yao wasiohaki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake ukauawa, bali roho yake ikahuishwa, ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokuwa kifungoni akawahubiri.”
Siku tatu kuu za Pasaka ndizo kiini cha mwaka wa Kanisa.
Zinamuadhimisha Yesu mteswa, mzikwa na mfufuka, yaani siku ya kwanza (Alhamisi kuu jioni hadi Ijumaa kuu jioni) inaadhimisha mateso yake kuanzia karamu ya mwisho hadi kifo cha msalaba; siku ya pili (Ijumaa kuu jioni hadi Jumamosi kuu jioni) inaadhimisha maiti yake kubaki kaburini na roho yake kushukia kuzimu; siku ya tatu (kuanzia Jumamosi kuu jioni hadi Jumapili ya Pasaka jioni) inaadhimisha ufufuko wake mtukufu.
Petro wa Kwanza 3:18-22 inaeleza ushikamano wa kuteswa kwake Kristo (fungu la 18) na kutukuzwa kwake (fungu la 22). Petro ndiye anayefafanua yaliyotokea katikati ya matukio haya mawili. Neno “alihubiri’ katika fungu la 19 lina maana ya kuwa aliwasilisha ujumbe. Yesu aliteswa na kufa msalabani, mwili ukiuawa na roho yake pia kufa kwa kufanywa dhambi. Lakini roho yake ilifufuliwa naye akaikakabidhi Baba. Kulengana na Petro, muda huo baada ya kufa mpaka kufufuka Yesu aliwasilisha hali Fulani ya ujumbe kwa “roho waliokuwa kifungoni.”
Bwana wetu aliikabidhi roho yake kwa Baba, akafa na wakati Fulani toka kufa mpaka kufufuka, akatembelea kuzimu alikowasilisha ujumbe kwa viumbe vya kiroho 9 pengine ni malaika waasi tazama yuda 6) waliokuwa na uhusiano na nyakati za kabla gharika la wakati wa Nuhu. Kifungu cha 20 kinafafanua zaidi. Petro hakutuambia kilichoambiwa roho hawa waliokuwa kifungoni lakini haiwezi kuwa ilikuwa habari ya wokovu kwa kuwa malaika hawaokolewi (Waebrania 2:16). Pengine ilikuwa ni kutangazwa kwa kushindwa kwa shetani na milki yake (Petro wa kwanza 3:22; Wakolosai 2:15). Waefeso 4:8-10 pia inajaribu kueleza kuwa Kristo alienda “paradise” (Luka 16:20; 23:43) na akawachukua mpaka mbinguni wale waliokuwa wamemuamini kabla kufa kwake.
Biblia haifafanui wazi wazi kilichotendeka ndani ya muda wa siku tatu hizi toka kufa mpaka kufufuka. Haiwezi kueleweka ya kuwa alikuwa ameenda kuwapa watu nafasi ya pili ya kuokolewa kwa kuwa biblia inatuambia ya kuwa tunakutana na hukumu punde tu baada ya kufa (Waebrania 9:27).
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Friday, May 3, 2013

Where Do We Go When We Die?


Because he is the only one who died and came back to life on the third day, Jesus knows more about death than everyone who has speculated about what happens after we die. Even near-death experiences do not tell the whole story.

Believers

CrucifixionJesus told the dying thief on the cross next to him, "I tell you the truth, today you will be with me in paradise." (Luke 23:43) Jesus told his disciples, "I will come back and take you to be with me that you also may be where I am." (John 14:3). So, believers go to be with Jesus when they die.
Heaven

Non-believers

Lake of FireJesus told a parable about a rich man who was a non-believer. "The rich man also died and was buried. In hell, where he was in torment, he looked up and saw Abraham far away." (Luke 16:22-23) Jesus also said, "And if your eye causes you to sin, pluck it out. It is better for you to enter the kingdom of God with one eye than to have two eyes and be thrown into hell, where 'their worm does not die, and the fire is not quenched'." (Mark 9:47-48). Even though Jesus was exaggerating for emphasis when he said "Pluck it out," it is clear that non-believers go to a horrible place called hell.

Hell: Hades and Gehenna

Jesus used two different words for hell. The first is Hades which is a temporary place where the dead go until the final judgment. Sometimes Hades is translated as grave. "The sea gave up the dead that were in it, and death and Hades gave up the dead that were in them, and each person was judged according to what he had done." (Revelation 22:13)
The second word is Gehenna which literally referred to the Valley of Hinnom, which was Jerusalem's dump where the garbage was burned. Figuratively, Gehenna refers to the lake of fire. "Then death and Hades were thrown into the lake of fire. The lake of fire is the second death. If anyone's name was not found written in the book of life, he was thrown into the lake of fire." (Revelation 22:15-16)





Paradise, the Millennium and the New Jerusalem

New JerusalemParadise is also a temporary place for believers. When Jesus returns to the earth, he will bring with him all of the believers who have died. They and the believers who are still alive will reign with Jesus during the Millennium, the one thousand year period when Jesus is king over all the earth. See 1 Thessalonians 4:15-17, Revelation 20:4-6.
At the end of the Millennium comes the final judgment described above. "Then I saw a new heaven and a new earth, for the first heaven and the first earth had passed away, and there was no longer any sea. I saw the Holy City, the new Jerusalem, coming down out of heaven from God, prepared as a bride beautifully dressed for her husband. And I heard a loud voice from the throne saying, "Now the dwelling of God is with men, and he will live with them. They will be his people, and God himself will be with them and be their God. He will wipe every tear from their eyes. There will be no more death or mourning or crying or pain, for the old order of things has passed away." (Revelation 21:1-4)

Tuesday, April 30, 2013

Kujichua – je, ni dhambi kulengana na Biblia?


Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.

Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.

Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.

Biblia inasema je ju ya chale/ kujitoboa mwili?


Agano la kale liliwaamuru waIsraeli, “Msiikate miili yenu kwa ajili ya wafu wala kuchanja chale juu ya ngozi za miili yenu.Mimi ni Bwana” (mambo ya walawi 19:28). Hata hivyo ijapokuwa waumini kwa sasa hawako chini ya sheria ya agano la kale (warumi 10:4; wagalatia 3:23 – 25; waefeso 2:15), hoja ya kuwa kulikuwa na sheria juu ya chale lazima lituletee maswaliagano jipya haisemi lolote juu ya muumini achanjwe chale au asichanjwe.

Kulengana na swala la chale na kujikata alama mwilini, mtazamo wetu ni uwe; je, twaweza kumuomba Mungu atumie alama hizo kwa utukufu wake? “kwa hivyo mnapokula, mnapokunywa, chochote mfanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Biblia haituamuru kinyume cha chale na alama za mwili lakini pia haituonyeshi ya kuwa ana haja na alama hizo miilini mwetu.

Jambo lengine ni nidhamu. Biblia inatushauri kuvaa mavazi yetu kwa nidhamu (Timotheo wa kwanza 2:9). Kuvaa ki nidhamu ni kuziba sehemu zote zilizotarajiwa kuzibwa na mavazi. Lengo la nidhamu hii ya ki mavazi si juu ya wewe mwenyewe bali kwa ajili ya wengine wasije wakanaswa na hali yakuvutiwa nawe kiasi cha kukutamani. Chale pia zinaushawishi Fulani kwa hivyo zinakeuka mipaka ya nidhamu hii.

Kanuni muhimu ya kibiblia ni kutazama jambo kwa mfumo wa imani. Kama hulionei shaka moyoni juu yakuwa linampendeza Mungu basi lifanye. “kwa kuwa lolote ambalo, si la imani ni dhambi” (warumi 14:23). Tunapaswa kufahamu kuwa miili yetu na nafsi zetu pia zimekombolewa na ni mali ya Mungu. Ijapokuwa haelekei moja kwa moja juu ya chale na alama za miili, wakorintho wa kwanza 6:19 -20 inatupatia kanuni moja, “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, akaaye ndani yenu, ambaye mnaye kutoka kwa Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe. Mmenunuliwa kwa thamani kwa hivyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu na katika roho zenu ambvyo ni vya Mungu.” Miili yetu sharti iandamane na ukweli kokote tuendako. Kama miili yetu ni mali ya Mungu basi lazima tuwe na ruhusa yake kabla hatujajichanja chale hizo au alama hizo za mwili.

Mkristo ni mtu gani?


Kwa tafsiri kutoka kamusi ya Webster Mkristo ni “mtu mwenye kukiri imani ndani ya Yesu kama Kristo au Imani yenye msingi wa mafundisho na ufunuo wa Yesu.” Ijapokuwa huu ni mwanzo mwema wa kufahamu Mkristo ni mtu gani, kama maelezo mengi ya kidunia yalivyo, inapungukiwa na uhalisi wa kibiblia juu ya Maana kamili ya Ukristo au Mkristo. 


Neno Mkristo limetumika mara tatu katika agano jipya (Matendo 11:26; Matendo 26:28; Petero Wa Kwanza 4:16). Wafuasi wa Yesu Kristo waliitwa kwa mara ya kwanza “Wakristo” antiokia (Matendo 11:26) kwa sababu tabia zao, matendo yao na hotuba zao zilikuwa kama za Kristo. Ilitumika kiasili na watu wasiookoka wa Antiokia kama jina la kimajazi kuwadhihaki wakristo hao. Ina maana sawa na “Kuwa mmoja wa kundi la kristo” au “mfuasi wa Kristo,” ambayo imefanana na tafsiri ya Neno hili katika kamusi ya Webster.

Kwa bahati mbaya, neno Mkristo limepoteza kwa kiwango kikubwa usawa wa matumizi yake na Linatumika mara kwa mara kumaanisha tu mtu mwenye dini au pengine muadilifu kinyume cha Mfuasi halisi wa Yesu Kristo aliyezaliwa mara ya pili. Watu wengi wasioamini na kuwa na tumaini ndani ya Yesu Kristo hujichukulia tu kuwa ni wakristo kwa sababu wanahudhuria ibada za Kanisa ama wanaishi katika taifa la kikristo. Lakini, kuenda kanisani, kuwahudumia wale wasiobahatika maishani au kuwa mtu mzuri haviwezi kukufanya kuwa mkristo. Kama Muinjilisti mmoja alivyosema, “kuenda Kanisani hakufanyi mtu kuwa Mkristo sawa na mtu kuenda gereji hakumfanyi kuwa gari.” Kuwa mshirika wa kanisa anayehudhuria ibada kila mara na kutoa kwa ajili ya kazi za kanisa hakuwezi kukufanya wewe kuwa Mkristo.

Je ni nini kitawapata watu wale hawajawai pata nafasi ya kusikia kuhusu Yesu?


Je ni nini kitawapata watu wale hawajawai pata nafasi ya kusikia kuhusu Yesu? Je Mungu atawahukumu wale ambao hajawai sikia kuhusu Yesu?"

Jibu: Watu wote wamewajibika kwa Mungu hata kama wamesikia au hawaja “sikia kumhusu” Bibilia yatwambia wazi wazi kuwa Mungu anajidhihirisha mwenyewe kwa uungu (Warumi 1:20) na katika Roho za watu (Mhubiri 3:11). Shida ni kwamba ni uzao wa dhambi wa mwanadamu. Zote twakataa hii hekima ya Mungu na kuasi (Warumi 1:21-23). Kama isingekuwa ni neema ya Mungu, tungejitolea kwa mioyo ya dhambi, kujiruhusu kujigundulia vile maisha ni bure, yakustaajabisha ni sehemu kando naye Mungu. Anafanya haya kwa wale wanaoendelea kumkataa (Warumi 1:24-32).

Ukweli ni, si eti watu wengine hawajasikia juu ya Mungu. Badala, shida ni wamaekataa chenye wamesikia na chenye kinaonekana katika uumbaji. Kumbukumbu La Torati 4:29 yasema, “Lakini huko, kama mkimtatufa BWANA, Mungu wako, utampata, ukimtafuta kwa moyo wako wote, na roho yako yote.” Aya hii yatufunza nguzo muimu. Kila mmoja anayemtafuta Mungu atampta. Kama mtu amenuia kumjua Mungu, Mungu atajudhihirisha kwake.

Shida pekee, “Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu” (Warumi 3:11). Watu wanakataa hekima ya Mungu ambayo ipo katika uumbaji na katika mioyo yao, na badala wanaanza kuabudu “miungu” yao wenyewe wamejitengenezea. Ni ubumpavu kubishana juu ya haki/uungwana wa Mungu kumtuma mtu jahanamu mwenye hakuwa na nafasi ya kuisikia injili ya Kristo. Watu watawajibika kwa Mungu kwa yale yote Mungu ameyafunua kwao. Bibilia inasema watu wanakataa hekima na kwa hivyo Mungu ako haki anapowahukkumu kwenda jahanamu.

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW