Kama Paulo anavyoandika, Mungu hutuadhibu “ili isitupase adhabu pamoja na dunia” (11:32). Dunia itahukumiwa kupotea milele. Basi, Mungu huwaadhibu waamini watendao dhambi ili wasiende jehanamu.
Hili linaleta maswali kadhaa ya muhimu. La kwanza ni hili: Je, kweli ipo hatari ya mwamini wa kweli kufika jehanamu?
Jibu ni NDIYO. Kama mwamini wa kweli atarudia kutenda zile “dhambi zinazotenganisha” – yaani, zile ambazo Maandiko yanasema zikitendwa, mtu hataweza kuingia katika ufalme wa Mungu (ona 1Wakor. 5:11; 6:9-10; Wagalatia 5:19-21; Waefeso 5:5, 6). Anapoteza uzima wa milele. Mungu hajaondoa hiari yetu, wala uwezo wetu wa kufanya dhambi. Kinyume na jinsi waalimu wengi wa siku hizi wanavyofundisha, Biblia inafundisha kwamba mwamini yeyote atakayefuata asili yake ya kale ya dhambi – au mwili – yuko katika hatari ya kufa kiroho. Paulo anasema hivi, anapowaandikia Wakristo:
Basi kama ni hivyo ndugu, tu wadeni, si wa mwili tuishi kwa kufuata mambo ya mwili. Kwa maana, kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. Kwa kuwa wote wanao-ongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu (Warumi 8:12-14. Maneno mepesi kutilia mkazo).
Inatubidi tuseme kwamba Paulo alikuwa anasema na waamini Wakristo walio hai kiroho, kwa sababu mbili.
Kwanza: Ona kwamba anawaita ndugu.
Pili: Walikuwa na uwezo wa kuyafisha matendo ya mwili kwa njia ya Roho. Hiki ni kitu ambacho waamini tu wanaweza kukifanya, ambao Roho wa Mungu anakaa ndani yao.
Ona sasa kwamba Paulo aliwaonya Wakristo Warumi kwamba, kama wangeishi kulingana na mwili, ni lazima wafe. Je, alikuwa anazungumza juu ya kifo cha kimwili au cha kiroho? Ni sahihi tukisema kwamba alikuwa anazungumzia juu ya kifo cha kiroho kwa sababu, kila mmoja – hata wale wenye “kuyafisha matendo ya mwili” – watakufa kimwili siku moja. Je, si kweli kwamba wale “wanaoishi kwa kuufuata mwili” mara nyingi huendelea kuishi katika mwili kwa muda mrefu tu?
Uamuzi tunaoweza kufikia kutokana na kweli hizi ni kwamba waamini Wakristo wanaweza kufa kiroho kwa “kuishi kwa kuufuata mwili”. Basi, zile orodha za “dhambi” za Paulo katika 1Wakor. 6:9-10; Wagalatia 5:19-21 na Waefeso 5:5-6 hazipaswi kufikiriwa kwamba zinawahusu wale tu wasiokiri kumwamini Kristo. Zinawahusu hata wale ambao wamekiri kumwamini Kristo. Ukweli ni kwamba, katika mantiki yake, zile dhambi ziliandikwa ili kuwa maonyo kwa waamini. NI wale wanao-ongozwa na Roho badala ya mwili ndiyo walio wana wa kweli wa Mungu, kama Paulo alivyosema waziwazi kabisa (ona Warumi 8:14).
Uthibitisho Zaidi Kwamba Walio-Okoka Wanaweza Kufa Kiroho
Paulo aliandika maneno kama hayo kwa Wakristo Wagalatia. Baada ya kuwaonya kwamba wale wanaojihusisha na “matendo ya mwili” hawataurithi ufalme wa Mungu, alisema hivi: